Friday, June 9

BARAZA LA TAIFA LA USALAMA BARABARANI LATOA TATHIMINI


 Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani ambaye ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Massauni, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani), kuhusu utekelezaji wa mpango mkakati wa kupunguza ajali za barabarani nchini katika kipindi cha miezi sita, mjini Dodoma leo, kulia ni Makamu Mwenyekiti wa baraza hilo ambaye ni Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Edwin Ngonyani.
 Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani ambaye ni Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Edwin Ngonyani (kulia), akifafanua jambo katika mkutano na Waandishi wa Habari kuhusu hatua za utekelezaji wa mpango mkakati wa kupunguza ajali za barabarani nchini katika kipindi cha miezi sita, mjini Dodoma leo, kushoto ni Mwenyekiti wa Baraza hilo Mhandisi  Hamad Massauni.
 Mjumbe wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, Mhandisi Julius Chambo (Kushoto), akisikiliza kwa makini taarifa ya utekelezaji wa mpango mkakati wa kupunguza ajali za barabarani nchini katika kipindi cha miezi sita, iliyotolewa na Mwenyekiti wa Baraza hilo Mhandisi Hamad Massauni (hayupo pichani), mjini Dodoma leo.
Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani ambaye ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Massauni, akitoa taarifa ya utekelezaji wa mpango mkakati wa kupunguza ajali za barabarani nchini katika kipindi cha miezi sita kwa wajumbe na waandishi wa habari, mjini Dodoma leo. 

Imetolea na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

No comments:

Post a Comment