Tuesday, December 20

Trump aadhinishwa rasmi Rais wa Marekani


Washington, Marekani. Wajumbe wa Jopo la Kuamua Mshindi wa Urais nchini Marekani wamemuidhinisha Donald Trump kuwa mshindi wa uchaguzi wa urais uliofanyika Novemba. Wajumbe hao walikutana katika majimbo yao kupiga kura.
Awali, kulikuwa na juhudi za kutaka kumzuia bilionea huyo kuingia ikulu kwa madai amekuwa akiendesha siasa za kibaguzi.
Hata hivyo, Trump amesema atakuwa rais wa Marekani wote na atafanya kila liwezekanalo kuwaunganisha wananchi.
Wajumbe walikuwa wametumiwa ujumbe kupitia baruapepe na pia kupigiwa simu wakihimizwa kutomuunga mkono bilionea huyo kabla yao kukutana kupiga kura.
Shughuli yao ya kupiga kura kwa kawaida huwa kama shughuli ya kutimiza wajibu kwani mara zote  huwa wanamuidhinisha mshindi.
Kumekuwa na lawama kuwa uchaguzi wa mwaka huu ulitawaliwa na hila ikiwamo vitendo vya udukuzi kutoka Urusi. Madai hayo yamepuuzwa na Urusi iliyosema hayana msingi wowote.
Jimbo la Texas hatimaye lilimuwezesha kufikisha idadi ya kura 270 za wajumbe alizohitaji,, licha ya wajumbe wawili wake kugeuka na kupiga kura kumpinga.
Matokeo ya kura hiyo yatatangazwa rasmi 6 Januari 6 kwenye kikao maalum cha pamoja cha Bunge la Congress.
"Nawashukuru Wamarekani kwa kunipigia kura kwa wingi kuwa rais wa Marekani," alisema Trump kupitia taarifa baada ya matokeo kutangazwa.
"Kwa hatua hii ya kihistoria tunaweza sasa kutazama mbele na kutarajia maisha ya kufana siku za usoni. Nitafanya kazi kwa bidii kuunganisha nchi yetu na kuwa rais wa Wamarekani wote," alisema.

No comments:

Post a Comment