Thursday, October 16

ANGALIA PICHA MELI KUBWA KULIKO ZOTE DUNIANI YATIA NANGA UINGEREZA (The world's largest cruise ship arrived in the UK)


Longer than The Shard and wider than a Boeing 747 wingspan:




The world's largest cruise ship arrived in the UK today for the first time.
The £800m Oasis Of The Seas sailed into Southampton at 10am on Wednesday in dense fog, welcomed by a crowd of hundreds and helicopters circling overhead.


Weighing 225,282 tonnes, the 1,187ft ship is longer than London's The Shard is tall, and at 208ft wide, larger than the wingspan of a Boeing 747.
















Tight squeeze: On its maiden voyage, the ship is pictured lowering its smokestacks to squeeze under the Great Belt Bridge

Dominic Paul, senior vice president of Royal Caribbean International, said: 

'Today is an important milestone in the global expansion of the Royal 

Caribbean International business.

'We are marking a significant step change in our investment into growth markets around the world.


'The welcome of Oasis of the Seas to Southampton is followed next year by 

sistership Allure of the Seas sailing outside the Caribbean for the 

first time during a summer 2015 season based in Barcelona.



'These investments highlight our commitment to deliver the most innovative and architecturally advanced ships to Europe and are part of our ongoing  


effort to redefine the cruise sector.


'Our extensive investments into new ships, new technology and new ideas are 

increasing the appeal of the cruise sector around the world.'




















Monday, September 8

Kigwangala ajitosa rasmi urais 2015

  • Awaponda wanaosubiri kuoteshwa .Mtoto wa Malecela amuunga mkono

MBUNGE wa Nzega, Dk. Hamisi Kigwangala, amejitosa rasmi katika mbio za kuwania urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), mwaka 2015.
Tangazo hilo la Kigwangala, linaongeza idadi ya wanaowania kiti hicho baada ya January Makamba, Bernard Membe, Edward Lowassa,William Ngeleja, Frederick Sumaye na Waziri Mkuu Mizengo Pinda kutangaza nia na baadhi yao kutajwa kuwa na nia ya kufanya hivyo mwakani.
Akizungumza na waandishi wa habari, wazazi wake, familia yake na makada wa CCM, akiwemo William Malecela (Mtoto wa Waziri Mkuu wa zamani John Malecela), Dk. Kigwangala alitumia muda mrefu kufafanua hotuba yake iliyokuwa na kurasa sita akielekeza kuwa, watanzania wanapaswa kubadili mipangilio ya kipaumbele na kusimiamia mambo wanayoyasema ili kujikwamua kiuchumi.
Kigwangala aliwaambia waandishi kuwa, anatangaza rasmi sasa, kuwa anatia nia ya kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka 2015.
Alisema amefikia uamuzi huo bila kuelekezwa, kusukumwa, kushawishiwa, kupangiwa ama kupanga na mtu ama na kikundi cha watu, isipokuwa utashi utayari wake.
Bila kuwataja majina, Kigwangala aliponda njia wanazotumia wengine akisema kuwa yeye hasubiri kuoteshwa, kushauriwa au kuombwa kama wanavyofanya wagombea wengine kupitia CCM. Alisema baadhi ya wanasiasa wa CCM, wamekuwa waoga kujitosa au kutangaza nia zao bali husema kuwa wanasubiri kuoteshwa, au wengine wameombwa na watu wengine.
Alibainisha kuwa, anatangaza nia ya kugombea urais mapema ili kuwapa fursa watanzania wampime na kumtazama mwenendo na uwezo wake, akiamini kuwa ataungwa mkono si kwa rangi ya ngozi yake, si kwa jinsi yake, si kwa umri wake au kwa daraja lake kijamii, dini, ama kabila lake, bali kwa sifa na uwezo wake kama mtanzania.
Kigwangala alitumia msemo wa kilatini kusema kuwa yeye ni  baina ya wengi, mmoja! (E Pluribus unum), hivyo hawezi kuwa salama ikiwa wengine wanateseka.
Bila kutaja wazi kuwa anakosoa utendaji wa serikali ya Kikwete, Kigawangala alitoa mifano mbalimbali ikiwemo kitisho cha njaa, kucheleweshwa hukumu za mahakamani, shida za mzee mmoja wa Pemba aliyefiwa na mtoto wake, au kasoro za operesheni za wamachinga na mamantilie jijini Dar es Salaam.
“Kitisho cha njaa ya familia fulani maskini kule Sakasaka, wilayani Meatu, ni kitisho changu na familia yangu, hata kama siyo familia yangu. Kucheleweshewa haki ya kuhukumiwa kwa mtuhumiwa wa mauaji ya kule Sombetini, ni kitisho kwangu pia, hata kama kesi siyo yangu,” alisema.
Aliongeza kuwa Mama Ntilie wa Sokoni Kariakoo, akifukuzwa, akapigwa virungu, akanyang’anywa pesa zake, akadhalilishwa na kumwagiwa chakula chake na mgambo wa Jiji la Dar es Salaam inaniumiza na kunigusa moyoni, hata kama yeye si mama yangu,” alisema.

Sarafu ya Sh. 500 kuanza kutumika mwezi ujao

Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imetangaza kutoa toleo jipya la sarafu ya Sh. 500, inayotarajiwa kuingizwa kwenye mzunguko na kutumika rasmi kama fedha halali nchini, kuanzia mwezi ujao.

Hatua hiyo imechukuliwa na BoT kwa kuzingatia sababu mbalimbali, ikiwamo noti ya Sh. 500 iliyopo sasa kwenye mzunguko kupita kwenye mikono ya watu wengi katika kipindi cha muda mfupi na hivyo, kuchakaa haraka.

Mkurugenzi wa Huduma za Kibenki wa BoT, Emmanuel Boaz, aliwaambia waandishi wa habari, jijini Dar es Salaam jana kuwa sarafu hiyo itakuwa ikitumika sambamba na noti zilizopo za Sh. 500 mpaka hapo noti hizo zitakapokwisha katika mzunguko.

“Hatua hii imezingatia kwamba, noti ya Sh. 500 ndiyo inayotumika zaidi kwenye manunuzi ya kawaida ya kila siku ya wananchi wengi kuliko noti nyingine yoyote. Hivyo, noti hiyo hupita kwenye mikono ya watu wengi katika kipindi cha muda mfupi sana na kuchakaa haraka,” alisema Boaz.

Alitaja sababu nyingine iliyozingatiwa katika kutoa sarafu hiyo kuwa ni noti hizo (za Sh. 500) kukaa katika mzunguko kwa muda mrefu bila kurejeshwa kwenye mabenki kwa wakati muafaka ili zibadilishwe zinapokuwa zimefikia ukomo wake.

Sababu nyingine ni sarafu kuwa na uwezo wa kukaa kwenye mzunguko kwa miaka mingi (zaidi ya miaka 20) zaidi kuliko noti.

Alisema sarafu hiyo ina umbo la duara lenye michirizi pembezoni, kipenyo cha milimita 27.5 na uzito wa gramu 9.5, ina rangi ya fedha na imetengezwa kwa madini aina ya chuma na “Nickel”.

Pia upande wake wa mbele ina sura ya Rais wa Kwanza wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Sheikh Abeid Aman Karume, na kwa nyuma ina taswira ya mnyama nyati akiwa mbugani.

Vilevile, ina alama maalumu ya usalama iitwayo “latent image”, iliyopo upande wa nyuma, ambayo ni kivuli kilichojificha, ambacho huonesha thamani ya sarafu “500” au neno BoT inapogeuzwageuzwa.

Zitto: Wapambe wametufitini na Mbowe

Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe akifafanua jambo. Picha na Edwin Mjwahuzi 


Dar es Salaam. Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe ameeleza tofauti yake na mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, akisema imesababishwa na watu aliowaita wapambe.
Zitto (37), ambaye alikuwa naibu katibu mkuu wa Chadema, alisema kuwa hata kuvuliwa nyadhifa zake ndani ya chama kulisababishwa na wapambe hao, lakini akasisitiza kuwa hana kinyongo tena kwa kuwa alishamwomba Mungu na sasa amesamehe kabisa.
Tofauti za wawili hao hazijawahi kutolewa hadharani licha ya mitandao mbalimbali kuzungumzia kuharibika kwa uhusiano wao ikinukuu habari kutoka vikao vya ndani vya Chadema.
Hata hivyo, mapema mwaka huu, Zitto alirushiwa tuhuma nzito na Chadema kutokana na uhusiano wake na baadhi ya makada wa CCM, lakini mbunge huyo aliyahusisha maneno hayo na mwenyekiti wake na aliandika maneno makali dhidi ya Mbowe kwenye ukurasa wake wa facebook.
Lakini katika mahojiano na Mwananchi yaliyofanyika wiki iliyopita nyumbani kwake Masaki jijini Dar es Salaam, Zitto alionekana kujutia kuharibika huko kwa uhusiano wao na kusema “wapambe ndiyo wanatugombanisha”.
“Sina shida yoyote na Mbowe, naamini ipo siku tutagundua wapambe walituathiri na ndiyo waliotufikisha hapa,” alisisitiza Zitto bila kutaja ni kina nani hasa.
Zitto alisema yeye na Mbowe wametoka mbali tangu akiwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na hafurahii uhusiano wao ukiishia katika hali hiyo.
“Naumia sana, lakini naamini ipo siku ama nikiwa hai au nimekufa watu wataujua ukweli,” alisema mwanasiasa huyo kijana aliyepata umaarufu kutokana na uwezo wake wa kujenga hoja.
Alisema, akiwa mwenyekiti wa Serikali ya wanafunzi wa Chuo Kikuu (Daruso) yeye na mwenyekiti wake ndiyo waliokijenga chama wakati huo Mbowe akiwa mbunge wa Hai.
Alisema wakati huo Mbowe alikuwa akienda chumbani kwake kusuka mikakati ya kuiinua Chadema na kwamba walikuwa wakila chips pamoja na wakati mwingine kwenye klabu ya usiku ya Bilicanas inayomilikiwa na Mbowe.
“Wakati mwingine naangalia, naumia sana. Wakati tunafanya hayo yote wengine walikuwa CCM, wengine walikuwa wafanyabiashara, lakini sasa ndiyo wana sauti katika chama,” alisema Zitto.
Zitto alisema kuwa wakati huo walikuwa na kampeni yao waliyoiita ‘Real Madrid’ ambayo ilikuwa na lengo la kuingiza kila mwanasiasa bora katika chama chao.
Real Madrid ni klabu ya soka ya Hispania yenye mafanikio makubwa duniani na sera yake ni kusajili wachezaji nyota duniani kwa gharama zozote.
“Na kweli tulifanikiwa na kuongeza wabunge kutoka watano hadi 48 wa sasa,” alisema.
“I real miss that (nakumbuka sana). Naumia sana, mimi leo sina maelewano na watu ambao tulikuwa nao katika mapambano. Lakini nasononeshwa zaidi na kitu kinachoendelea ndani ya Chadema.
“Nini kimetokea Chadema? Kwa nini tumejikuta tumeondoka katika mstari? Tupo wabunge 48 bungeni sasa, lakini hatusogezi mbele nchi, tumerudi nyuma wakati huo tulikuwa watano lakini tulikuwa tunaenda vizuri sana.”
Akizungumzia jinsi wapambe walivyoharibu uhusiano wao, Zitto alisema kuna siku Mbowe alimtuhumu kuwa ameanzisha chama cha umma, pia akasema ana majina mawili tofauti katika mtandao wa Jamii forums ambayo anayatumia kuwasema viongozi wa Chadema.
“Kukatokea vurugu, baadaye nikasema naondoka. Ile nataka kutoka wabunge wakanizuia mlangoni nisipite, waliponizuia nilikuwa na hasira sana, nikawaambia lazima nitoke. Waliponizuia hasira zikanipanda nikaanguka chini nikalia sana, yaani sana” alisema akionekana mwenye hisia huku machozi yakimlengalenga.
Kwa mujibu wa Zitto, jioni ya siku hiyo walijikuta wamekaa meza moja na Mbowe na baada ya kuzungumza waligundua kuwa walikuwa wamelishwa maneno.
“Tulizungumza na wote tulilia sana. Wakati kama huu nikikumbuka nasikia uchungu kwa sababu ni wapambe wametufikisha hapa,” alisema.
Hata hivyo, Zitto alisema kuwa migogoro ni sehemu ya maisha na kwamba yeye anachukulia kama changamoto kwa kuwa hakuna njia inayonyooka moja kwa moja na hiyo ni sehemu ya kuendelea kumkomaza.
“Mmoja wa viongozi ambao ni role model wangu ni aliyekuwa Waziri Mkuu wa Malaysia, Mahathir Mohamad ambaye kila mwezi Oktoba huwa nakwenda Malaysia kuonana naye.
Mwaka jana wakati vurugu hizi zimeanza kushika kasi, watu wakaniambia unaweza vipi kukabili mambo kama haya, ila Mahathir ambaye alifukuzwa kwenye chama chake akiwa mbunge na baadaye akaja kuwa Waziri Mkuu, aliniambia hizi ni changamoto ambazo lazima upite,” alisisitiza Zitto.
Aliongeza kuwa hata Makamu wa Rais wa Kenya, Raila Odinga, alionana naye mwanzoni mwa mwaka na akamshauri asikate tamaa na kumweleza kuwa yeye hajafikia hata robo ya changamoto ambazo amepitia.
“Kwangu mimi changamoto hizi ni kukomazwa na sizungumzii kuonewa au kutoonewa, what I know (ninachojua) ni kwamba sijafanya kosa lolote na kwangu mimi nimesamehe na sina kinyongo na mtu yoyote.”
Mwaka huu baada ya msiba wa mama nimekwenda Umra Maka nimemuomba Mwenyezi Mungu na nimetoa vinyongo vyangu vyote na nimesema I have to move on (sina budi kusonga mbele) katika maisha yangu, sina chuki na tatizo na mtu.
“Huwezi kujua huko mbele mtakutanaje, just few months ago (miezi michache iliyopita) wabunge wa Chadema waliwaambia wabunge wa CUF kuwa ni mashoga, lakini leo ni marafiki.
Alikuwa akirejea kauli ya Chadema kuwa CUF ni mwanachama wa taasisi ya kimataifa ya kiliberali ambayo moja ya misingi yake ni kutetea usagaji, ushoga na ndoa za jinsia moja.
“Hivyo ndivyo ninavyoiona na huko mbele usishangae kuona tunafanya kazi pamoja. Kwangu mimi nimeshasahau kila kitu nimelia Umra na kila kitu nimesamehe,” alisema.
Alipoulizwa sababu za kutomfuata Mbowe ili wayazungumze na kuondoa tofauti zao, Zitto alisema sasa hivi siyo muda wa kumbugudhi kwa sababu yuko bize na Ukawa na uchaguzi, lakini anachoamini kuwa hata kama yeye Mbowe hatutakuwa hai, ipo siku itagundulika kuwa huu mgogoro ulipikwa na wapambe tu.
Akizungumzia uhusiano wake na katibu mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa, mbunge huyo alisema kuwa alikuwa na ukaribu wa kikazi tu na katibu huyo kutokana na kuwa kiongozi wake bungeni.
Kutelekeza ofisi
Akijibu tuhuma za kutelekeza ofisi ya naibu katibu mkuu, mbunge huyo alisema kuwa hizo ni tuhuma kama tuhuma nyingine na kwamba alikuwa anafanya kazi zake kama kawaida na kuhudhuria vikao, lakini kuna taratibu za kikatiba za kushughulika na jambo kama hilo.
“Hamuwezi mkakaa miaka miwili siji ofisini halafu mnakurupuka na kusema tumemfukuza kwa sababu alikuwa haendi ofisini. Kuna taratibu za kikatiba kwa mtu ambaye hashughuliki na kazi za chama au vikao mfululizo.
Kwa nini taratibu hizo hazikutumika wakati hiyo ni justification (uthibitisho) za mambo ambayo yalitokea, ambayo nisingependa kuyarejea kama vilivyosema hapo mwanzo.” aliongeza.
“Kazi za siasa siyo za ofisini ni kazi za field na kazi za field nimezifanya kwa kuendesha Operesheni Sangara na matunda yake ni kupata wabunge wengi Kanda ya Ziwa.
“Ni justification (uhalalishaji) tu kwamba kuna kitu kimetokea unatafuta sababu tu na kwangu mimi ni jambo dogo sana. Muhimu zaidi ni wapi tumekitoa chama na kukifikisha na wengine wakifikishe mbele zaidi,” alisema na kuongeza:
“Mimi nilikuwa nafanya kazi zangu kama kawaida na nilikuwa na ushirikiano mzuri na katibu mkuu kama inavyotakiwa,” alisisitiza.
Kuhusu madai kuwa CCM ilimuomba kujiunga na chama chao baada ya mgogoro huo kutokea, Zitto alisema hawajawahi kumtaka kabisa.
“Moja ya vitu ambavyo nashutumiwa na wenzangu ni kwamba mimi natumiwa na CCM lakini haijawahi kutokea kiongozi yeyote wa chama hicho, licha ya kuwa na uhusiano nao mzuri, kunitaka nijiunge nacho.
“January Makamba, Deo Filikunjombe, Kangi Lugola ni baadhi ya marafiki zangu walioko CCM lakini si vibaya kwa sababu hata watu wa Chadema wana marafiki ambao wapo CCM na wapo ambao wanaishi pamoja,” alisema Zitto.
Alisema mke wa Dk Slaa alikuwa diwani wa CCM lakini halikuwa tatizo, ila kwa Zitto kuwa na marafiki CCM lilikuwa tatizo.
Kujiunga chama kingine
Kuhusu kujiunga na chama kingine cha upinzani, Zitto alisema kuna vitu ambavyo unapokuwa kiongozi huwezi kuviweka wazi kwani kuna mazungumzo na watu ambayo ameyafanya lakini hawezi kuyatoa.
“Niishie kusema kwamba viongozi wengi sana nimezungumza nao. Wapo walionipa pole kwa yaliyonikuta na wengine kuniomba niungane nao, lakini sikuona sababu ya kutoka chama hiki kwenda chama kingine. Utapata faida ya siku mbili tatu katika kurasa za mbele za magazeti kuwa Zitto kaingia chama fulani lakini hutapata sustainable benefit (manufaa ya kudumu)” alisema.
“(Wilfred) Lwakatale alitoka CUF na kwenda Chadema, lakini hivi sasa wanafanya kazi pamoja. Kafulila katoka Chadema kaingia NCCR, Chadema wakamshambulia kuwa ni sisimizi lakini leo Kafulila ni shadow minister (waziri kivuli) chini ya Mbowe.”
Aliongeza kuwa hizo yeye anaona ni siasa nyepesi, kwa kuwa ana ndoto ya kuona nchi inabadilika na inabadilika kwa watu wanyonge na watu ambao leo hii hawana matumaini. Alisema kwa muda mrefu wananchi wanavumilia kuwa Watanzania, lakini hawajivunii kuwa Watanzania. Ndiyo maana katika ubunge wake ana kazi ya kuibua mambo mazito ili yafanyiwe kazi.
Akizungumzia mambo ambayo anaamini alifanikiwa katika maisha yake, Zitto alisema kuwa ni Bunge la 2005 hadi 2010 ambalo alizungumzia suala la madini kuhusu Buzwagi mpaka sheria mpya ya madini ikapatikana mwaka 2010.
“Leo hii katika tanzanite, Serikali inamiliki asilimia 50 kwa sababu ya sheria mpya. Pia Stamico ina hisa katika migodi na hii ilitokana na hoja za Buzwagi,” alisema Zitto ambaye ana shahada ya uchumi.
“Nilisimama bungeni kuzungumzia madini na siyo kuwa kulikuwa hakuna wabunge, lakini walikaa miaka mingi bungeni na hawakuona kuwa madini ni tatizo.
Nilichekwa na kuonekana sina maana lakini Rais aliunda Tume ya Bomani na watu wakaniambia nisiingie katika hiyo Tume lakini kwa mara ya kwanza ripoti ya Bomani ndiyo ripoti pekee iliyojadiliwa bungeni kati ya ripoti zote zilizoundwa kwenye sekta ya madini.”
Alisema kuwa katika Bunge la 2010 na 2015 alianza vibaya na hoja yake ya kuinua zao la mkonge ilikataliwa. Lakini hakuchoka na Aprili 2012 ripoti ya CAG ikatoka na akiwa mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) alitaka waliohusika kuwajibika na ndiyo akaibua hoja ya kutokuwa na imani na waziri mkuu na mawaziri wanane wakafukuzwa.
Kujiunga ACT
Alipoulizwa kuhusu mipango ya kujiunga chama kipya cha ACT, Zitto alisema pamoja na kwamba kauli yake kwamba atakuwa wa mwisho kuihama Chadema iko palepale na ndiyo maana ameenda mahakamani kutetea uanachama wake, kuna mambo matatu ya kuzingatia:
Moja, “viongozi wa ACT ni marafiki zangu na ni washirika wangu na falsafa (ideology) ya ACT ndiyo aidiolojia ninayoiamini ambayo ni ujamaa na tatu mimi ni mwanasiasa na hapa Tanzania mpaka sasa ili ufanye siasa lazima uwe kwenye chama cha siasa.”
Kutokana na matokeo ya mahakamani yatakavyokuwa kwa vyovyote vile Watanzania watarajie kuniona katika siasa na katika chama cha siasa ila hawataniona CCM.
“Siwezi kung’ang’ania kama wenzangu wa Chadema hawataki kuwa na mimi.
Lakini nafuatilia kwa karibu shughuli zinazofanywa na ACT na mimi siasa zangu ni hoja, ndiyo maana hamnioni nagombana wala natukana mtu na mkisikia Zitto mtasikia katika hoja na ACT wanajenga siasa za hoja.
“Wanaoongoza ACT ni watu ambao ninawaamini na haitakuwa jambo la ajabu itakapobidi kuwa nao, lakini cha msingi sasa hivi ni kwamba tuna kesi na leo mwanasheria wangu alitakiwa kuwasilisha majibu na tunasubiri hatima ya kesi ambayo ufafanuzi mkubwa ni kupata jibu la, hivi mtu anaweza kukurupuka tu na kumfukuza uanachama mtu bila kufuata taratibu zinazotakiwa?
Nikiiacha kesi bila kupata uamuzi, kuna watu wengi zaidi watakuja kuumia kwenye uamuzi wa aina hii.”
Alisema lazima mahakama itoe uamuzi kwamba taratibu za chama chenu ni hizi, zifuateni mzimalize, hamna sababu za haraka za kumnyonga mtu. Jaji mmoja alisema huwezi kumnyonga mtu halafu baadaye ndiyo unataka ajibu mashtaka.
Mabilioni ya Uswisi
Kuhusu mabilioni ya Uswisi, Zitto alisema kwa mara ya kwanza kwa nchi za kusini mwa Jangwa la Sahara, Bunge la Tanzania lilikuwa la kwanza kupitisha azimio la kutaka masuala ya utoroshaji fedha yachunguzwe, likitokana na hoja yake.
Alisema uchunguzi wa mabilioni ya Uswisi bado unaendelea ingawa watu wanataka majina ila kwake majina si tatizo kwa sababu yataandikwa tu katika magazeti kwa siku mbili kama ambavyo ilitokea yalipotajwa majina ya mafisadi, lakini waliotajwa mpaka leo bado ni mawaziri.
“Mwaka jana nilikwenda kwenye mkutano Uingereza kumweleza Waziri Mkuu wa Uingereza kabla ya mkutano wa G8 nikiwa na Rakesh Rajan na leo hii kuna uchunguzi unaendelea.

Friday, April 25

Rais anakemea “wanasiasa wanaomtukana Nyerere na Karume” amekaa kimya matusi kwa Jaji Warioba na kauli za Lukuvi

NI dhahiri sasa kuwa mjadala wa Katiba mpya, hususan kipengele cha muundo wa Muungano, unaelekea kulipeleka taifa mahali pabaya. Japokuwa dalili za Bunge Maalumu la Katiba linaweza kuishia kuwa jukumu ghali kwa walipakodi masikini, hasa baada ya kusikika madai ya baadhi ya wajumbe wa Bunge hilo kuwa posho ya shilingi 300,000 kwa siku haitoshi, lakini Watanzania wengi walikuwa na imani kwamba ‘upepo huo mbaya’ ungepita na hali ingekuwa shwari.

Hata hivyo, kadiri siku zinavyozidi kwenda ndivyo hali inavyozidi kuwa mbaya. Kinacholeta wasiwasi zaidi 
kwa sasa ni kuibuka kwa dalili za ubaguzi wa waziwazi, sambamba na jitihada hatari za kumwaga petroli kwenye moto kwa kuingiza udini kwa nguvu kwenye siasa.

Lakini pasi ‘kuuma maneno’ naomba nielekeze lawama zangu kwa Rais Jakaya Kikwete na chama chake - CCM. Pamoja na wasiwasi uliokuwepo awali, kwamba huenda Rais Kikwete angeendeleza desturi iliyoota mizizi ndani ya CCM kwamba kila wazo lililoanzia vyama vya upinzani (kama hilo la umuhimu wa kuwa na Katiba mpya) ni baya, na hivyo angekwamisha uwezekano wa kupata Katiba mpya, alitushtua wengi alipoonyesha dalili za kuwa amepania kwa dhati kuweka historia kwa kufanikisha suala hilo muhimu.

Mambo yalionekana kwenda vizuri licha ya jitihada za hapa na pale ndani ya CCM kulifanya suala la Katiba mpya kuwa la kiitikadi zaidi kuliko la kitaifa. Wengi mtakumbuka vijembe walivyopigwa baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani walipotaka kukutana na Rais Kikwete. Badala ya kupongeza kile kilichoonekana kama mwanzo mpya wa siasa za maridhiano, baadhi ya wanasiasa huko CCM waliwakebehi wapinzani kuwa wanataka kwenda Ikulu kunywa chai tu!

Dalili za mwanzo kuwa hatma ya suala la Katiba mpya ipo shakani zilianza kujichomoza zaidi baada ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba, chini ya Jaji Joseph Warioba kuweka hadharani Rasimu ya Kwanza ya Katiba mpya, ambapo pendekezo la muundo wa Muungano wa Serikali tatu liliwekwa bayana. Taratibu, CCM, chini ya uongozi wa Kikwete, ilianza harakati za chini chini kujaribu kuingilia mchakato wa Katiba mpya, ikiwa ni pamoja na jitihada za kubinafsisha mchakato huo.

Lakini Mungu si Athumani au John, pamoja na vizingiti vya hapa na pale, hatimaye Rais Kikwete alitangaza majina ya wajumbe 201 kutoka makundi mbalimbali ya jamii, kuingia katika Bunge la Katiba. Lakini kabla ya hapo, tayari Rais Kikwete alishatangaza mkoani Mbeya wakati wa maadhimisho ya kuzaliwa kwa CCM kwamba msimamo wa chama hicho ni Serikali mbili. Japo alitangaza msimamo huo kama Mwenyekiti wa taifa wa CCM, katika mazingira ya kawaida tu, isingewezekana kuwapo kwa mitizamo tofauti kati ya Kikwete wa CCM na Kikwete Rais.

Kuanzia hapo ikawa kama ‘jini lililopo kwenye chupa’ (a genie in the bottle) limefunguliwa. Zikaanza harakati za waziwazi ‘kulazimisha’ matakwa ya chama tawala kwamba muundo wa Muungano lazima ubaki kuwa wa Serikali mbili. Mara zikapatikana taarifa kuwa CCM imetengeneza rasimu yake ya siri.
Mara tu baada ya kikao cha Bunge Maalum la Katiba kuanza, ishara kuwa hali huko mbele inaweza kuwa si shwari zikawa zinajitokeza kila kukicha. Baada ya mshikemshike wa madai ya posho, likaibuka suala la utaratibu wa kupiga kura (yaani kura zipigwe kwa usiri au uwazi.)

Lakini kwa vile tangu awali CCM walionyesha kuwekeza nguvu zao kubwa katika suala la muundo wa Muungano wakitaka Serikali mbili, suala hilo limeteka takriban kila kipengele cha Katiba mpya, na kwa bahati mbaya au makusudi, mjadala wa muundo wa Muungano unazidi kutishia umoja na mshikamano wa taifa letu.

Japo lugha za matusi na kashfa si jambo geni kwenye vikao vya Bunge la Jamhuri, hali imezidi kuwa mbaya kwenye kikao cha Bunge Maalumu la Katiba, tunasikia baadhi ya wajumbe wakiwatuhumu wenzao kuwa mashoga, huko wengine wakienda mbali na kuhoji Uafrika wa wenzao. Lakini kama nilivyobainisha hapo juu kuwa tumeshazoea matusi na lugha chafu bungeni, kuna waliokuwa na imani kuwa “wakimaliza kutukanana, watarejea kwenye suala lililowakutanisha huko Dodoma.”

Mara vikaanza kuibuka vitisho kuwa iwapo Katiba mpya itaridhia Serikali mbili, jeshi litatwaa madaraka. Na aliyeanzisha vitisho hivi si mwingine bali Rais Kikwete katika hotuba yake ya ufunguzi wa Bunge hilo la Katiba, wiki chache zilizopita.

Lakini wakati Rais Kikwete aliliongelea suala hilo katika jukwaa la kisiasa (bungeni), mmoja wa wasaidizi wake akaamua kulitoa suala hilo katika anga za siasa na kulipeleka kwenye nyumba za ibada. Hapa ninamzungumzia William Lukuvi.

Inaniwia vigumu kupata maneno stahili ya kumwelezea mwanasiasa huyo ambaye ghafla ametokea kuwa mtu mwenye kauli chafu, hatari na za kiharamia.

Huyu mtu bila aibu wala uoga amediriki kwenda kanisani na kutangaza waziwazi kuwa jeshi litaasi pindi uamuzi wa kuwa na Serikali tatu utakapopitishwa. Naomba nitamke bayana kwamba nahisi Lukuvi ana matatizo kutokana na hatua yake ya kwenda kanisani kufanya mahubiri ya kushawishi jeshi kuasi.

Lakini anayempa jeuri Lukuvi ni Rais Kikwete, kwani naye aligusia suala hilo kwenye hotuba yake ya ufunguzi wa Bunge la Katiba. Kwa hiyo anachofanya Lukuvi ni kusambaza tu ujumbe ulioanzishwa na Rais Kikwete.

Na wakati Rais Kikwete akiwakemea “wanasiasa wanaomtukana Nyerere na Karume” amekalia kimya matusi ya Lukuvi kwa Mwenyezi Mungu (naam, kutumia nyumba ya ibada kujenga chuki na kuhamasisha uasi wa jeshi ni matusi kwa Mungu.)

Ni watu wenye upeo mdogo tu watakaochukia kusikia kwamba Nyerere na Karume wana mchango katika matatizo tuliyonayo kuhusu Muungano, hasa kwa uamuzi wao wa kulifanya suala hilo kama lao binafsi bila kuangalia madhara yake miaka kadhaa ijayo.

Mara kadhaa Rais Kikwete amekuwa akiasa kuhusu athari za kuchanganya siasa na dini. Amewahi kudai kuwa kuna maadui wa nje wanaotumia suala la dini kwa minajili ya kututenganisha.

Lakini kipi cha kushangaza ilhali kwenye chaguzi kadhaa wamekuwa wakitumia nyumba za ibada kupandikiza chuki dhidi ya wapinzani wao?

Japo hainisumbui sana iwapo Katiba mpya haitopatikana, napata wasiwasi kuona uhuni wa kisiasa (political thuggery) ukihalalishwa kwa kisingizio cha ‘kuhubiri athari za Serikali tatu.’
Lakini nani wa ‘kuokoa jahazi’? Rais Kikwete anakemea wanaowatukana Nyerere na Karume, lakini anapuuza matusi ya wasaidizi wake kwa Jaji Warioba.

Nimalizie makala hii kwa kumkumbusha Rais Kikwete kwamba mwakani ataondoka madarakani na kurejea uraiani. Asipotengeneza mazingira mazuri kwake na kwa Watanzania, janga hili linalopikwa na akina Lukuvi litamwathiri naye pia.

Ni muhimu kwa Rais kuweka kando ushabiki wa kisiasa na kuchukua hatua za makusudi kuepusha nchi kutumbukia kwenye machafuko yanayochochewa na mahubiri ya ubaguzi na kuitumia dini kwa minajili ya kisiasa.

Siku 67 za mipasho, matusi bungeni

Wajumbe wa Bunge Maalum la katiba wakipinga jambo ndani ya bunge juzi  wakati Kamati namba tatu  na nne za kijadili vifungu vya rasimu ya Katiba walipokuwa wakiwasilisha ripoti zao Bungeni Dodoma juzi. Picha na Salim Shao 


Dodoma. Bunge Maalumu la Katiba linaahirishwa leo baada ya kukutana kwa siku 67 bila kupitisha hata ibara moja kati ya 240 zilizomo katika Rasimu ya Katiba.
Badala yake Bunge hilo likiongozwa na Samuel Sitta “Mzee wa Kasi na Viwango” linaahirishwa hadi Agosti, mwaka huu likiendelea kujadili Sura ya Kwanza na ya Sita zenye jumla ya Ibara 19, zinazohusu masuala yanayojenga msingi wa aina ya Muungano unaopendekezwa.
Tume ya Mabadiliko ya Katiba katika rasimu iliyowasilishwa bungeni na aliyekuwa Mwenyekiti wake, Jaji Joseph Warioba ilipendekeza muundo wa shirikisho lenye serikali tatu, pendekezo ambalo limeligawa Bunge hilo vipande viwili.
Kutokana na mgawanyiko huo, kauli zenye utata, kejeli, matusi, dhihaka na ubaguzi ni mambo yaliyoshika hatamu katika mjadala wa sura hizo mbili, huku viongozi wa Bunge; Sitta na Makamu wake, Samia Suluhu Hassan wakilaumiwa kwa kushindwa kudhibiti hali hiyo.
Mwanzoni mwa wiki hii, Mjumbe wa Bunge hilo, Ezekiah Oluoch alimshutumu Sitta kwamba ameshindwa kudhibiti nidhamu katika Bunge na kwamba ndiye chanzo cha kuondoka kwa wajumbe wapatao 200 ambao ni wanachama wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).
“Mwenendo wa Bunge Maalumu ulikuwa na dalili zote za kuonyesha kungetokea matatizo ndani yake kutokana na mipasho ambayo ilikuwa ikitokea kwa wajumbe pamoja na lugha ambazo siyo za staha wakati wa kutengeneza kanuni,” alisema Oluoch na kuongeza:
“Kwanza matumizi ya lugha zisizo na staha, mwenyekiti anaruhusu wajumbe kuchangia hoja kwa kupeana mipasho bila kujali hoja iliyopo mezani kinyume na kanuni,” alisema Olouch.
Hata hivyo, Suluhu alisema amekuwa akiendesha Bunge hilo kwa umakini mkubwa na kwamba kila anaposikia lugha chafu amekuwa akiwabana wajumbe kwa kuwaamuru kufuta kauli au kuomba radhi kwa matamshi. “Sipendezwi na lugha chafu, kwa hiyo mojawapo ya mambo ambayo huwa najitahidi kusikiliza kwa makini kila michango inapotolewa na wajumbe bungeni ni kubaini kama wametumia lugha zisizostahili, kisha kuchukua hatua kwa mujibu wa kanuni zetu,” alisema Suluhu.
Alikiri kwamba wapo baadhi ya wajumbe ambao wamekuwa wakigoma au kukataa kuomba radhi na kwamba masuala yao hupelekwa kwenye Kamati ya Maadili ambayo ina mamlaka ya kuchukua hatua zaidi kwa mujibu wa kanuni za Bunge hilo.
Matakwa ya Kanuni
Sehemu ya Tano ya Kanuni za Bunge Maalumu inatoa mwongozo wa mambo yanayokatazwa na yale yanayopaswa kufuatwa wakati wa mjadala.
Kanuni ya 46 imeorodhesha mambo yasiyoruhusiwa ambayo ni pamoja na kusema uongo, kutoa taarifa zisizokuwa za kweli, kuzungumza jambo lolote ambalo halipo kwenye mjadala na kutumia majina ya marais na waasisi wa Taifa kwa dhihaka.
Pia inazuia matumizi ya lugha ya kuudhi, kubagua, kunyanyapaa au inayodhalilisha watu wengine, kuzomea, kupiga kelele za aina yoyote zinazoweza kuvuruga mjadala au mwenendo bora wa shughuli za Bunge hilo.
Licha ya makatazo hayo, wajumbe wamekuwa wakikiuka kanuni bila kuchukuliwa hatua na hali hiyo imekuwa chanzo cha mivutano, zomeazomea, kelele na mambo mengine hadi kundi la Ukawa kususia kikao wakieleza kutokuridhishwa na mwenendo wa Bunge.
Kuufyata na kuufyatua
Baadhi ya kauli tata zilizojitokeza ni pamoja na ile iliyotolewa na Asha Bakari Makame kwa mjumbe mwenzake, Ismail Jussa kuwa anafanana na watu wenye mabusha nyuma ambao ndiyo huufyata.
Makame ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT), alikwenda mbali zaidi na kumwambia Jussa kuwa ana matatizo ya kiafya na si mwanamume kamili, kwani ameshindwa kuoa na hana watoto wakati ana umri mkubwa.
“Huyu Jussa anasema kwamba tumeufyata, hapa tuwekane sawa, maana ya kuufyata ni mtu kuwa na mabusha pale yanapokuwa nyuma ndiyo kuufyata kwa hiyo yeye ndiyo ameufyata, ana busha huyu,” alisema Bakari.
Naye Profesa Ibrahim Lipumba alichafua hali ya hewa pale alipowafananisha wajumbe wa Bunge Maalumu na kundi la mauaji nchini Rwanda, Intarahamwe.
“Tumechoka kusikiliza matusi. “Tumechoka kudharau mawazo ya wananchi, tumechoka ubaguzi hatuwezi kuwa sehemu ya kundi la Intarahamwe linalohamasisha ubaguzi ndani ya Tanzania hili hatulikubali. Tunawaachia, watu wote tunaotaka Katiba ya wananchi tunawaachia Intarahamwe mwendelee na Bunge lenu.”
Mjumbe mwingine ni Mwanakhamis Kassim Said aliyesema: “Mimi nilikuwa namwomba baba yangu mdogo Seif (Maalim Seif Sharif Hamad) awarejeshe watu wake humu (bungeni) kwa sababu mpira unachezwa huku ndani. Hatutakii mema humu, tena ana choyo na husuda. Namwomba baba mdogo atuache, alichokitaka amekipata, king’ora anazunguka saa 24 Dar es Salaam, Unguja. Mheshimiwa Mwenyekiti Baba mdogo kila mara yuko kwenye pipa (ndege) mara Uingereza, mara Canada mara wapi? Hicho ndicho anachokitaka amekipata.”
Mjumbe mwingine, Mohamed Seif Khatibu alisema: “Nimejifunza kuwa baadhi ya wanasiasa wa upinzani ni vinyonga. Lakini Maalim Seif ni kinyonga, wakipita kwenye mvua wanakuwa na rangi ya mvua, kwenye jua wanakuwa na rangi ya jua, baharini wanakuwa na rangi ya bahari.”
Tuhuma za rushwa
Mjumbe Ezekiah Wenje alisema baadhi ya mawaziri wamewahonga wajumbe wa kundi la 201 ili waunge mkono msimamo wao, lakini alipotakiwa kufuta kauli hiyo alikataa na suala lake kufikishwa kwenye kamati ya kanuni.
“Kuna wajumbe wengine walikwenda hadi kwa waziri mkuu ambako walikula, walikunywa hadi saa 7:00 usiku, wengine walikwenda kwa Gaudensia Kabaka (Waziri wa Kazi na Ajira) na walikula na kunywa na kupewa bahasha.”
Kuingia msituni
Kapteni John Komba alitangaza kuingia msituni iwapo Bunge Maalumu la Katiba litapitisha muundo wa serikali tatu, huku akimshutumu Mwenyekiti wa Tume ya Marekebisho ya Katiba, Jaji Joseph Warioba na timu yake ni waasi kama Adamu na Eva waliomuasi Mungu kutokana na kile walichokifanya cha kupendekeza serikali tatu. Mwingine katika orodha ni Bernard Membe aliyesema, Tume ya Mzee Warioba itakuja kukumbukwa kwa kuratibu mauaji ya Muungano na Bunge nalo litakuja kulaaniwa kwa kubariki mauaji hayo.
Watoto wa shetani
Mjumbe Paul Makonda alisema: “Shetani alikuja duniani kuiharibu dunia, kuiangamiza na kuteketeza kila kilichostahili kuungana… watoto wake ni Mheshimiwa Jussa, watoto wake ni Mheshimiwa Mbowe, watoto wake ni Mheshimiwa Lipumba… Hawa ni watoto wa shetani”.
Mwingine: Waride Bakari Jabu alisema: “Chiku Abwao mimi namshangaa sana anayesema bora Muungano uvunjike lakini Tanganyika iwepo. Tunafahamu asili yake mwenyewe ni Mkongo mumewe ndiye Mtanganyika, namwambia Muungano huu utakuwepo na utaendelea kuwapo.”
Mjumbe Tundu Lissu alisema: “Tanganyika haikuuawa na makubaliano ya Muungano, bali iliuawa kwa amri za Nyerere…. Mwalimu Nyerere hakuwa na mamlaka yoyote ya kikatiba ya kutunga amri na kuua Tanganyika.”

Imeandikwa na Neville Meena, Daniel Mjema, Sharon Sauwa na Beatrice Moses.

Friday, March 7

DAR ES SALAAM HAINA MASTER PLAN!!??


Kumbe jiji la Dar-es-salaam halina mpango unaoeleweka wa ujenzi, 
hali inayopelekea jiji kuendelea kukua bila mpangilio maalum, ambao unaendena
na mahitaji ya watu kwa maana ya Idadi pamoja na uwezo wa Miundombinu yake..


Na kweli mitaa yetu angalia hapa parking barabarani watu wanapita humo humo yaani kila kitu kipo kipo tuu


Kariakoo nako hakufai vurugu mechi hujui wapi pa kupita waendao kwa miguu wapi pa magari wapi pa biashara wote wamo humo humo 


Na hii ndio upanga 


Hapa sijui huu ni mtaa wa biashara au ila wamo humo humo


Sehemu zenye nafasi mimi nadhani ni kama hizi tuu keepleft au sijui round about ila majina hayo kwa kiswahili usiniulize 


Cheki jinsi majengo yalivyoumana 




Na umeme umo humo humo well usifikirie hizi nyaya zikianguka juu ya umati huo w watu itakuwaje


Vichochoroni nako tumo tumo tuu biashara madampo kama kawa


Ila ukichoka sehemu za kupumzika ndio kama hizi humo humo zipo


Foleni unatamani gari lingekuwa na mabawa upae humo barabarani ni cheni mtindo mmoja


Wale wa kigamboni wao hubanana humo humo kwenye pantoni




Sijui hata hewa ya oxigen inapita ila tumo humo humo wengi ila hatuna jinsi


Mtaa wa kisutu napo wanajenga humo humo na fikiria sasa zamani zileeee kulikuwa na stendi ya mabasi ya mikoani hapo hapo


Biashara hapo hapo kwa kitaa


Ndio masoko yetu tena humo humo


Wateja hawaji kiivyo ila ndio kutafuta tena masoko


Ila wakija wanatukuta humo humo tunawauzia tuu


Hata Obama alipopitia alitukuta humo humo twajeuka kumpungia halafu tunaendelea na yetu


Mungu awalaze mahala pema wale wote waliotutoka maana na lile lililoanguka lilikuwa humo humo kwa kitaa

Hii ndi Dar Es Salaam