Thursday, December 20

Washikiliwa Kwa Wizi Wa Kwenye Mitandao

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA POLISI TANZANIA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI TAREHE 20/12/2012

Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma linawashikilia watu watatu kwa tuhuma za kujihusisha na shughuli za wizi wa mtandao hususani katika maduka yanayotoa huduma za M-PESA,Tigo Pesa na Airtel Money katika maeneo mbalimbali ya Manispaa ya Dodoma.
Watu hao ambao wanadaiwa kujipatia zaidi ya shilingi 1,730,000 /= kwa Mawakala wanne tofauti wanaotoa huduma hizo walikamatwa jana tarehe 19/12/2012 majira ya saa 12:00 hrs mchana.
Watuhumiwa hao ambao wanatokea Jijini Dar es Salaam majina yao ni Mohamed s/o Dotto @ Sefu, mwenye umri wa miaka (30) Mnyamwezi mkazi wa Kigogo, Mohamed s/o Pazi, Mzaramo Miaka (28) na Ally s/o Mohamed miaka (25) ambao ni wakazi wa Ilala.

Wamekuwa wakitumia mbinu mbalimbali kufanikisha wizi huo, moja ya mbinu ni kwenda kwenye maduka yanayotoa huduma hizo na kumwambia wakala kuwa wanaharaka na kutaka kuweka Pesa kiasi fulani ambacho wanakuwa nazo mkononi na kuanza kuzihesabu.
Mara meseji ya pesa toka kwa wakala zinapoingia katika simu zao, simu zao huita wakati huo huo na kujifanya wanapokea simu huku wakisogea pembeni wakiongea na simu na kuondoka julma kwenda kuzitoa mahala pengine kwa haraka.

Wakala walioathirika na Wezi hao mpaka sasa ni Consolata d/o Martini ambaye duka lake liko eneo la Kuu Streetu shilingi 300,000/=, Perndo d/o Martin qambaye Duka lake liko eneo la CBE Tsh. 860,000/= Mlay s/o Felix eneo la Makole Tsh. 300,000/=, Masala s/o Mabula wa eneo la Changombe Tsh. 70,000/= na Duka la Lazia Shop ambalo liko Mtendeni Street Tshs 200,000/=.
Natoa wito kwa wamiliki na wakala wote wanatoa huduma hizo kuwa makini wanapoendesha shuguli zao, kwa kutoa taarifa za watu wanaowatilia shaka wanaofika kutaka huduma katika maduka yao mara moja ili wakamatwe na kufikishwa katika vyombo vya sheria.

[D. A. MISIME – ACP]
KAMANDA WA POLISI [M] DODOMA

CONTACT:
POLISI MKOA WA DODOMA
DAWATI LA HABARI, ELIMU NA MAHUSIANO,
Phone: 0715 006523 – Luppy Kung’alo – Mrakibu msaidizi wa Polisi (ASP)
Phone: 0712 360203 – Silyvester Onesmo – Police Konstebo (PC)

No comments:

Post a Comment