Thursday, April 12

Commitment ya Serikali kulinda wasanii wetu(hansard) by zittokabwe

WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA:

Napenda kutoa kauli ya Serikali, kwamba kutokana vikao vyote hivyo ambavyo nimesema kumi na sita vya Mawaziri lakini leo tena tumekutana mara ya kumi na saba, tumeazimia kwamba hotuba ya bajeti ya mwezi wa sita Mheshimiwa Waziri wa Fedha atalizungumzia jambo hilo na utekelezaji wa mambo yote pamoja na utengenezaji wa sticker, na jinsi ambavyo TRA watafanya jambo hilo yatawekwa bayana na mara baada ya bajeti speech kuanzia tarehe 1 Julai, kutakuwa na mabadiliko kubwa katika kazi za wasanii wa nchi yetu ya Tanzania.

Kwa hiyo nataka niwashukuru Waheshimiwa Wabunge, nataka tu watambue kwamba Serikali inaliona hilo Serikali iko pamoja na wao na ndiyo maana tumekutana namna hiyo na kwa hakika katika hili tuko pamoja kabisa na mtaona utekelezaji wake.

KAMATI YA BUNGE ZIMA

MHE. KABWE Z. ZITTO:

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeleta mapendekezo, Jedwali la Marekebisho kipengele hicho cha 38. Wakati Mheshimiwa Waziri anafanya winding up alitoa commitment ya Serikali kuhusiana na mabadiliko makubwa ya eneo la copyrights kwa ajili ya kulinda kazi za wasanii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba Mheshimiwa Waziri arejee ile commitment kabla sijaweza ku-move hii amendment. Tafadhali. Airejee kwa faida ya Taifa na kwa faida ya Bunge.

MWENYEKITI:

Mheshimiwa Waziri, Mheshimiwa Zitto pamoja na amendment aliyoleta, amezingatia sana kauli yako wakati unajibu hoja za Waheshimiwa Wabunge. Anaomba ile commitment ya Serikali ya kufanya marekebisho kwenye sheria ya copyright. Sasa hiyo commitment ya Serikali ndiyo itakayomsababisha yeye kuondoa jedwali lake la marekebisho ili sasa tuhoji kifungu hiki.

WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA:

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati ninafanya majumuisho nilisema kwamba mimi na Mheshimiwa Mkulo – Waziri wa Fedha na Mheshimiwa Nchimbi tumekutana mara nyingi sana kwa ajili ya suala hilo la kuangalia haki za wasanii Watanzania kwamba hazipotei. Lakini vile vile tumeagiza mamlaka zilizoko chini ya Wizara zetu; COSOTA kwa Viwanda na Biashara, TRA kwa upande wa Wizara ya Fedha na BASATA kwa upande wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wakae. Wamefanya vikao mara tatu. Kutokana na yaliyokubaliwa katika vikao vyote vya Waheshimiwa Mawaziri na wajumbe wa zile Kamati, Mheshimiwa Mwenyekiti, narudia commitment ya Serikali kwamba kwenye Bajeti ijayo, Serikali italeta mapendekezo makubwa ambayo yatakuwa yamezingatia maoni yote ambayo yametolewa na BASATA, COSOTA na TRA kuhusu namna bora ya kulinda haki za wasanii wa aina zote katika nchi yetu ya Tanzania.

MHE. KABWE Z. ZITTO:

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nataka hiyo commitment ili itakapofika siku ya bajeti tutumie Hansard hii kuhakikisha kwamba commitment hiyo imetekelezwa. Kwa maana hiyo nikwamba naondoa amendment yangu ambayo nimeileta.

MWENYEKITI:

Nakushukuru. Na nafikiri kwamba Serikali iko makini, inavyofanya commitment hapa inaelewa nini inachokifanya.

No comments:

Post a Comment