Friday, April 20

TB Joshua again: Delivers man from shocking addiction!

This post and link to the video below were shared to us by Ihechukwu Njoku -- Controversial Nigerian Prophet T.B. Joshua can’t seem to stay out of the news. However, this time it’s not concerning a prophetic utterance or political visitor.

On Sunday 15th April 2012, Joshua’s popular church in Lagos was witness to a disgusting yet dramatic case of a man with a truly repulsive addiction. Mr Mukaila Malomo, a Nigerian who lived in Germany for 16 years, confessed to being addicted to regularly taking a sickening concoction of faeces, semen and urine.

According to Malomo, a graduate from the London School of Journalism, it all started one night in a prison cell in Germany. "I woke up in the middle of the night and a very wicked demon instructed me to get up from my bed,” he told the bewildered SCOAN congregation. “This strange voice said that I should go to the toilet, defecate and mix it with my sperm and urine. I mixed my urine, sperm and faeces and swallowed everything.”

Malomo, who worked in a reputable organic salad company in Munich before a drunken brawl landed him in prison, explained that an unusual anger and desire to fight immediately followed. “After I swallowed it, a very strange power came over me. I felt as if I was a small god. It overcame me and I became very strong and angry - as if there's an extra power from another world entering my body. I was ready for war. Ever since then, for over 15 years, I have been addicted to eating my faeces, urine and sperm. I can’t stop it.”

He continued his sordid tale, explaining how each indulgence in the addiction would result in further violence. “After my release from prison, I was always fighting in Germany. Sometimes, the police would have to cover the whole street to try and stop me - and I was using only a bottle. I kept on stabbing without getting tired – because of this power that entered me.”

People present in the church could scarcely contain their shock as Malomo’s revelations continued. “It is not only my own faeces; on many occasions, I visited public toilets here in Nigeria and Germany and ate from there.” He described the mixture as food to him. “I enjoy it. I don't even perceive any smell. I eat it as if I eat eba (Nigerian cuisine) or something like that.”

Malomo, married to a German Hungarian lady who gave birth to his only son while in prison, described how he had kept this addiction a total secret from the world around him. “As I am eating it, that evil spirit will be telling me that this thing is only for me, that nobody should know, otherwise the power will go.”

Joshua proceeded to tell his congregation and the viewers worldwide watching the live broadcast via Christian television station Emmanuel TV that a video clip would be shown to verify Malomo’s confession. Stating that it was too graphic for him to witness, he covered his face and advised viewers without strong stomachs to do likewise. The clip showed Malomo mixing his own urine and faeces together and then drinking the revolting contents with apparent ease and delight. People within the auditorium vomited at the sight, distressed at the level of degradation the addiction had rendered on Malomo.

Joshua then called on the congregants to join together in supplication and proceeded to pray for the ‘demon’ within Malomo to come out! Falling to the floor, Malomo’s body began vibrating uncontrollably and uncannily. Asked to explain what was happening, Malomo said he felt as if something was leaving his body.

Joshua then instructed Malomo to go to the church’s public toilet to see how his reaction towards human waste had changed following the prayer. Merely perceiving the odour of other’s defecation caused Malomo himself to vomit. He returned to the church, testifying that all desire for his former addiction had vanished as the realization of his earlier actions dawned upon him.“Apart from being irritated by the odour, I feel ashamed, in the sense that – how can a human being be eating faeces,” he told the congregation, as he joined Joshua in a joyful dance.

SCOAN has now controversially released the video on popular video-sharing site YouTube and via their Facebook account which has garnered well over 100,000 fans in just four months. Although Malomo’s case appears to be the most extreme, many with strange addictions claim to have been delivered at Joshua’s ministry over the last few months, including those addicted to drinking kerosene, eating ice cubes, sand, charcoal, mothballs and soil.

T.B. Joshua has set social networks and local media ablaze in recent months, especially with his prediction concerning the death of the late Malawian president Bingu wa Mutharika and revelations of his relationships with African leaders such as Ghana’s John Atta Mills, Zimbabwe’s Morgan Tsvangarai and Malawi’s new head Joyce Banda. His television station Emmanuel TV continues to increase in popularity, especially across Africa where he is becoming a household name.

Tafrisi ya Mjengwa kuhusu Zitto Kabwe na saini za Wabunge 70 kumg'oa Pinda


Ndugu zangu,

Leo asubuhi wakati nikifanya ' jogging' kwenye mitaa ya Dar es Salaam niliwasikia watu wa kawaida kabisa wakijiuliza na kujadili; " inakuwaje Serikali iwalipe marehemu mishahara huku sisi tulio hai hatuna hata uhakika wa milo miwili ya siku?" Wanauliza watu wa mitaani.

Naam, nchi yetu imekumbwa na mafuriko ya habari. Kule bungeni Dodoma kuna moto unawaka. Zimeitishwa sanini 70 ili Jumatatu ipigwe kura ya kukosa imani na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. Ndio, kuna wanaotaka Pinda ang'oke, na labda kutolewa kafara, maana, siamini kama tatizo la msingi ni Pinda, bali ni la kimfumo zaidi. Na jana kuna mbunge wa CCM kayasema makali yafuatayo;

“Mheshimiwa Naibu Spika, inashangaza na kusikitisha kuwa nchi inatafunwa. Wanaofanya haya ni mawaziri wetu. Nchi inakufa na tuelewe kuwa Tanzania sio mali ya CCM, ni ya Watanzania wote.“Mawaziri wetu wamekuwa mchwa, wanaangamiza nchi na leo nitamtaja waziri anayeongoza kwa kutafuta fedha za Watanzania. Ni Waziri wetu wa Fedha, Mustafa Mkulo. Ameuza viwanja, amelidanganya Bunge baada ya kuivunja CHC,”- Deo Filikunjombe ( CCM) Bungeni jana.

Lakini ya jana yalitanguliwa na ya juzi; Mbunge mwanadamizi wa CCM Godfrey Zambi aliyasema makali haya;

" CCM inaweza kung'olewa madarakani katika uchaguzi wa mwaka 2015 endapo kasi ya ufisadi na ubadhirifu wa fedha za umma itaendelea kama ilivyo sasa"- Godfrey Zambi ( CCM, Mbozi Mashariki).

Kauli za wabunge hao wawili wa CCM zinatoa tafsiri ya kilio cha wabunge wa CCM kuomba msaada kwa anayeweza kuwasaidia. Inatoa tafsiri pia kuwa hicho ni kilio cha wabunge wengi wa CCM. Kwamba hayo ndiyo wanayaongea hata chini chini.

Ndio, wananung'unika na wameanza kuiona adhabu wanayokwenda kuipata kutoka kwa wananchi ifikapo 2015. Wanaona pia, kuwa ' kisungura' hiki kidogo kinachopatikana kila mwaka kinavyoliwa na wajanja na wengine kuachiwa mifupa.

Wabunge wa CCM na wengine wanaona jinsi baadhi ya mawaziri wa kutoka chama chao wanavyojiangalia wenyewe kwa kujikatia zaidi kasungura hako kadogo na hata minofu mingine kuikimbizia kwenye majimbo yao badala ya kuangalia majimbo mengine pia. Hakika, Wabunge wa CCM sasa wanatoa kilio cha kuomba msaada na kilichochanganyika na hasira na hofu ya kupoteza mamlaka ya kuongoza dola ifikapo mwaka 2015. Ndio, kuna wanaokiona chama chao kikielekea kwenye kuzama 2015. Kelele wanazopiga bungeni zimegeuka kama kelele za nyikani, hazisikiki. Wameanza sasa kuwa na ujasiri wa kuzomeana wazi wazi kwenye vikao vyao badala ya kusubiri kuzomewa na wananchi hadharani. Naam, CCM ya sasa inapata tabu hata kwenye kujua namna ya kuitumia misamiati mipya ya kisiasa, maana, kuna wanaojivua gamba, wanaovuliwa magamba na sasa kuna ' wanaojinyambua' magamba wakiwa ndani ya chama- 'Political evolution' ya namna fulani.

Na Mtego wa Zitto Kabwe kwa CCM?

Jana Mbunge Zitto Kabwe ameitega CCM. Ni mtego wa hatari. Saini zile 70 zina maana hii;
- Kama wabunge wa CCM hawatachangamkia kutia sahihi zao zikavuka hata mia na hamsini, basi, kuna ujumbe unaopelekwa kwa umma. Kuwa wabunge wa CCM ni maneno tu, hawana dhamira ya kweli ya kupambana na ufisadi. Wabunge wengi wa CCM hawataiepuka adhabu ya umma inaweza kuwa inawasubiri 2015.
- Kwa wabunge wa CCM kutia sahihi zao na hata Pinda kupigiwa kura ya wabunge kukosa imani nae ina maana pia kuwa wabunge hawana imani na bwana mkubwa aliyemteua Pinda. Busara haiwataki wabunge wa CCM kufikia hapo. Hilo halina maslahi kwa taifa.

Nini kitakachotokea?

Kuna matatu;
Mosi, Mawaziri wale watano wanaotuhumiwa kwa ufisadi na ubadhirifu wa mali ya umma wanaweza kuepusha aibu kwa Serikali kwa wao wenyewe kutangaza kujiuzulu. Ingawa hili ni gumu kufanyika katika nchi hii, lakini, wakati mwingine kuna lazima ya kufanyika- maana, hapo watakuwa wamemnusuru Waziri Mkuu na aliyemteua.

Pili- Likishindikana la kwanza, basi, kabla ya Jumatatu, Waziri Mkuu Pinda awe ameshajiandaa kufanya maamuzi magumu. Kujiuzulu na kulinda heshima yake na ya aliyemteua. Au kutolewe ' Tamko la Serikali' litakalobadili upepo unaovuma sasa bungeni.

Tatu: La kwanza na la pili yaweza yasifanyike, na badala yake. Rais anaweza kuyaona yanayotokea sasa bungeni kama fursa ya kufanya mabadiliko makubwa Serikalini mara akitua Dar kutoka ziara ya Brazil.

Naam, yumkini pale Diamond Jubilee, kabla ya Jumatatu, kuna watakaopewa kazi ya kusafisha ukumbi na kupanga viti tayari kwa Mkuu wa Nchi kusema jambo kubwa kwa taifa kupitia kwa ' Wazee wa Darisalama'.

Tuhuma za Ray kuhusika na kifo cha Kanumba

Baada ya taarifa kuenea kwamba mwigizaji Ray anahusika moja kwa moja na kifo cha mwigizaji marehemu Steven Kanumba, mwigizaji huyo amezungumza kwenye AMPLIFAYA ya CLOUDS FM na Millard Ayo na kusema yafuatayo:

“...nimekuqa nikizisikia sana hizi tuhuma, sio kweli kwa sababu Kanumba ni mdogo wangu wa karibu sana tumetoka mbali sana kimaisha mimi na yeye, nimekua na mazoea ya kuona vitu kila siku vinaandikwa ambapo juzi nilipigiwa simu na kuambiwa nitazame kwenye blog ya U-Turn ambayo anaimiliki huyu dada ambaye simfahamu anaitwa Mange Kimambi”

“...alikuwa ameandika kwamba amepata taarifa kutoka kwa polisi mmoja wa Oysterbay kwamba Ray ndio aliyepiga simu kwa Lulu siku ya kifo cha Kanumba kwa hiyo Lulu ametumika kufanya mauaji bila kujijua, na pia kukawa kuna swali kwamba kwa nini Ray alikua wa kwanza kufika kwa marehemu Kanumba. Mungu ndie anaejua...”

“...kwa hiyo anataka kuwadhihirishia Watanzania kwamba Ray ndiyo anahusika na hicho kifo, baada ya hilo nimeshirikiana na polisi na kushitaki na kufungua kesi ambapo hivi sasa ninapozungumza yupo polisi Oysterbay akihojiwa kwa sababu ameandika kitu ambacho bado kipo ndani ya uchunguzi, hana uhakika nacho sijui Lulu amekamatwa Coco Beach which is not true, sijui hizi habari kaipata wapi...”

“...sasa hii ni kutaka kunivunjia heshima, mimi nafanya kazi ya kuigiza ndio maisha yangu unapoandika kitu kama hicho kwenye internet inafika sehumu kubwa dunia nzima, sasa unategemea watu wanichukuliaje kama sio kunivunjia heshima, kunipotezea mashabiki wangu… nasema hili sitoweza kuliacha, nitalifanyia kazi na nitalifikisha mahakamani ili iwe fundisho, sitolichekea...”

Kwenye sentensi nyingine Ray amesema baadhi ya maoni yaliyotolewa na watu mbalimbali kwenye hiyo habari iliyoandikwa kwenye blogu hiyo, “maoni niliyoyasoma mengine yanamwambia yule dada kwamba anachokiandika kinaweza kum-cost kwenye maisha yake, na nyingine zinasema kwamba tuko tayari kumvamia Ray na kumuua, sasa hichi kitu ni hatari sana kwenye maisha yangu kwa hiyo nimemshitaki polisi na kuandika kwa kusema chochote kitakachonikuta hata nikipigwa jiwe na kuanguka mimi na-deal na huyo mwanamke kwa sababu yeye ndio mtu aliye-publish hivyo vitu watu wanichukulie mimi vinginevyo kabisa tofauti jinsi nilivyo na sihusiki kabisa na hicho kifo, kimsingi maisha yangu yapo hatarini lakini nasema haya ni maisha nitaendelea kuvumilia...”

Thursday, April 19

Ufisadi wa mabilioni kila kona

NI KWENYE MAGARI YA SERIKALI,TANESCO,MALIASILI,MABILIONI YA JK,AFYA NA MISHAHARA HEWA
Daniel Mjema Dodoma na Fidelis Butahe
WABUNGE jana waliijia juu Serikali kwa matumizi mabaya ya fedha za umma na ufisadi ulijitokeza kwenye taasisi zake mbalimbali katika mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, mwaka jana.

Hasira za wabunge hao zilitokana na ripoti tatu za Kamati za Bunge; Mashirika ya Umma (POAC), Serikali za Mitaa (LAAC) na Hesabu za Serikali Kuu (PAC) kuonyesha upotevu wa mabilioni ya shilingi yaliyotumika katika nyanja mbalimbali ikiwemo mishahara hewa na mikataba mibovu.

Mbunge wa Longido (CCM), Michael Laizer alisema ni aibu kila mwaka kuwa na ripoti za wizi wa mali za umma lakini Serikali inakaa kimya.

Alisema katika Halmashauri ya Wilaya ya Longido, mmoja wa maofisa wake aliidhinisha Sh11 milioni kwa ajili ya matengenezo ya gari. “Labda Serikali imechoka sasa inafanya makusudi fedha za wananchi zinaliwa lakini yenyewe inakaa kimya. Serikali itujibu hizi fedha zinazopitishwa kila mwaka zinakwenda wapi?” alihoji Laizer

Mbunge wa Viti Maalumu (CUF), Magdalena Sakaya alisema Serikali inapaswa kuona aibu kwa kutekeleza pendekezo moja tu kati ya 12 yaliyotolewa na Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita.

Alihoji suala la mishahara hewa kuendelea kujitokeza huku Serikali ikikaa kimya na kila mwaka CAG anatoa ripoti yake… “Kuna vitabu vya halmashauri za wilaya ambavyo CAG hakuvikagua kwa kuwa havikuonekana vilipo, sasa hapo tunakwenda wapi? Kuna Sh8 bilioni hazikufika katika halmashauri husika zimekwenda wapi? Wabunge tunatakiwa kuhoji na kupewa majibu sahihi.”

Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari alisema sasa Tanzania imekuwa kama Saccos kwa kuwa fedha za umma zinatafunwa bila utaratibu huku vielelezo vikitoweka kusikojulikana.

“Wakati wa uchaguzi wa wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki, mawaziri walijaa bungeni ila sasa tunajadili hatima ya Watanzania hawaonekani. Wabunge tuwe kitu kimoja tuibane Serikali itueleze hizi fedha zimekwenda wapi?” alisema Nassari.

Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Ester Bulaya alisema chama tawala kisipokuwa makini katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 kitahukumiwa na vijana.

“Serikali ndiyo chanzo cha fedha kutafunwa… inakuwaje Naibu Waziri wa Maji anasimama na kuahidi mambo mengi wakati anajua wazi kuwa fedha za kutekeleza miradi hazipo?” alihoji.

Alisema mwaka 2015, utakuwa mgumu kwa CCM kwa kuwa wakati huo vijana watakuwa asilimia 85 na wanaweza kukinyima kura kutokana na Serikali yake kushindwa kusimamia masuala ya msingi ya maendeleo.

Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee aliwataka wabunge kuacha kulalamika kwa kuwa wao ndiyo wenye rungu la kuishikisha adabu Serikali: “Tukilalamika wananchi waliotuchagua nao watatushangaa kwa kuwa wametutuma kuwawakilisha na si kulalamika.”

Alisema umefikia wakati wa wabunge kuweka itikadi za vyama vyao pembeni na kuwashughulikia mawaziri wa wizara husika ambazo zinaonekana kuwa tatizo.

Mbunge wa Mwibara (CCM), Alphaxard Lugola alimlipua Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo akisema alihusika katika uuzaji wa mali ya Serikali katika Kiwanja namba 10 Barabara ya Nyerere na kwamba anaingilia utendaji wa mashirika ya Serikali.

Alisema kuwa kiwanja hicho awali, ilikuwa kiuzwe kwa Shirika la Tanzania Motors chini ya Kampuni ya Mashirika Hodhi ya Umma (CHC) kwa Sh1.3 bilioni lakini baadaye Mkurugenzi Mkuu wa CHC alipewa barua kusitisha uuzwaji wa jengo hilo na kumtaka kuitisha mazungumzo upya na Morad Sadik, ambaye alikuwa akitaka kununua eneo hilo awali.

“Inakuwaje wizara inaingia utendaji wa taasisi au kampuni zilizopo chini yake?” alihoji.

Awali, baada ya Kipindi cha Maswali na Majibu, Wenyeviti wa Kamati hizo za Bunge; Zitto Kabwe (POAC), John Cheyo (PAC) na Augustine Mrema (LAAC), waliwasilisha ripoti za kamati zao zinazoonyesha kukithiri kwa vitendo vya ufisadi serikalini na matumizi mabaya ya fedha za umma.

Kamati ya PAC
Cheyo alisema kamati yake imebaini kuwapo kwa matumizi ambayo hayakupitishwa na Bunge na kutaja Maonyesho ya Sabasaba, Nanenane na Utumishi kama sehemu ambako fedha hizo zilitumika.

Alisema mwaka 2009/2010 Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, ilitumia fedha za matumizi ya jumla ya Sh1.10 bilioni kwa ajili ya Maonyesho ya Nanenane ambazo hazikuwamo kwenye bajeti iliyopitishwa na Bunge.

Alisema hata matumizi ya Sh21.63 bilioni zilizotumika kuendesha Mfuko wa Kukwamua Wananchi kiuchumi maarufu kama ‘mabilioni ya JK’ hazikuwapo katika bajeti iliyopitishwa na Bunge. Alipendekeza kuwa ili kuondoa hali hiyo, mfuko huo unatakiwa kuwa na mtu au taasisi ya kuusimamia badala ya kuachwa bila usimamizi.

Alisema kuwepo kwa udanganyifu na ukwepaji kodi kumeisababishia Serikali hasara ya Sh15.4 bilioni na Dola 2.6 milioni za Marekani.

Alisema Wizara ya Maliasili na Utalii na ilipoteza Sh874,853,564 baada ya kufanya uamuzi wa upendeleo wa kutoa kiwango cha chini cha mrabaha kwa mazao ya misitu.

Kuhusu magari ya Serikali, Cheyo alisema kumekuwa na matumizi yasiyo ya lazima katika uendeshaji na ukarabati wa magari hayo. Hadi Juni 30, 2010 Serikali ilikuwa inamiliki magari yenye thamani ya Sh5 trilioni.

Alisema mwendelezo wa ununuzi wa magari unaofanywa na Serikali unaongeza gharama za uendeshaji na kusisitiza kwamba matumizi hayo si ya lazima kwa Serikali yenye uchumi mdogo uliozidiwa na madeni.

Kuhusu ukaguzi wa magari uliofanywa na wakala chini ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS), PAC imependekeza kuwajibishwa kwa ofisa masuuli wa Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kuisababishia Serikali hasara ya Dola 18,343,540 za Marekani ambazo ni karibu Sh30 bilioni na kusisitiza: “Sh30 bilioni zilitumika kufanyia ukaguzi wa magari ambao haukuwepo.”

Alisema pia wamegundua kuwa Serikali inatumia fedha nyingi kwa ajili ya kukodi majengo ya wizara na kusisitiza kuwa moja inaweza kulipa kodi ya Sh485 milioni.

Alisema kuna watumishi hewa takriban 3,000 na kwamba Serikali haifahamu lolote kuhusu hali hiyo… “Kuna Sh1.8 bilioni ambazo hutumiwa na Serikali kwa ajili ya kulipa watumishi hewa. Pia imebainika kuwa Serikali haijui thamani ya majengo yake yaliyopo ndani na nje ya nchi.”

POAC

Zitto kwa upande wake, alielezea maeneo yenye matatizo sugu ya matumizi ya fedha ambayo yanahusisha ukiukwaji mkubwa wa Sheria ya Ununuzi wa Umma na kanuni zake.

Alitola mfano wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), ambalo kwa mwaka mmoja wa fedha linafanya ununuzi wenye thamani ya kati ya Sh300 bilioni hadi Sh600 bilioni.

Alisema kwa mwaka wa fedha 2009/2010, Tanesco ililitumia Sh1.8 bilioni ukilinganisha na Sh65 milioni zilizokuwa zimepangwa katika bajeti ya ukarabati wa gati mojawapo katika Kituo cha Bwawa la Mtera.

“Ongezeko hilo la gharama za ununuzi kwa ajili ya ukarabati, ni kiasi kikubwa na Kamati haikuridhika na majibu ya menejimenti hivyo kuagiza uchunguzi wa ndani ili kubaini uhalisia wa ununuzi huo,”alisema na kuongeza:

“Tumependekeza Tanesco ianze kutumia vyanzo vyake vya umeme na iache kununua umeme hasa wa kampuni ya IPTL kwani inatumia Sh62.4 kununua umeme katika kampuni hii kwa mwaka.”

Alisema Chuo Kikuu Kishiriki cha Mkwawa (MUCE) kilishindwa kuthibitisha kwa wakaguzi wa hesabu uwepo wa vifaa vya maabara vilivyonunuliwa ambavyo vina thamani ya Sh267 millioni.

Katika ripoti hiyo, Zitto alisema imebainika pia mkataba kati ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), na Kampuni ya Startimes unatakiwa kupitiwa upya ili uinufaishe TBC.

Pia aliugusia matumizi mabaya ya fedha katika Bodi ya Pamba ambako alisema kuwa kiasi cha Sh2 bilioni zilizotolewa na Serikali hazijulikani zilipo na wala hazikuwafikia wakulima wa zao hilo.

LAAC

Kwa upande wake, Mrema aliitaka Serikali ivunje mtandao wa wezi wa mali za umma na kuhoji inakuwaje inawakumbatia mafisadi?
Alihoji majalada ya watuhumiwa wa ufisadi kukaa zaidi ya miaka 10 katika Ofisi za Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Mkurugenzi Mkuu wa Mashtaka (DPP) na ile ya Makosa ya Jinai (DCI) wakati kesi za uchaguzi zimewekewa kikomo.

Alisema ripoti ya CAG kwa mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, 2010, inaonyesha kuwa Sh583.2 milioni zililipwa kama mishahara hewa kiasi ambacho alisema kingetosha kujenga madarasa 194.

Mrema alisema katika ripoti hiyo, imebainika kwamba Sh8 bilioni zilitumika katika ununuzi usiokuwa na nyaraka na ama wenye nyaraka pungufu hali inayoashiria kuwapo kwa wizi.

Aliwataja watumishi wa Halmashauri ya Kishapu akisema ni vinara wa ubadhirifu wa Sh6 bilioni na kudai kuwa walishirikiana na baadhi ya watumishi wa Benki ya NMB Tawi la Manonga, Shinyanga kuiba fedha hizo za umma.

Aliwataja watumishi hao kuwa ni Mweka Hazina, Muhdin Mohamed, Mtunza Fedha wa Halmashauri hiyo, Walugu Mussa, Boniface Nkumiming na Mhandisi wa Halmashauri, Leonard Mashamba.

Alisema fedha hizo zilitafunwa kwa kutumia nyaraka feki, uhamisho wa fedha bila idhini na kuzitumia kinyume cha malengo, uhamisho wa fedha ambao haukufika kwenye akaunti husika na malipo kwa walipaji wasiofahamika.

Mrema aliilaumu Serikali kwa kuwahamisha kutoka halmashauri moja kwenda nyingine na Serikali Kuu, watumishi wanaotuhumiwa kwa ufisadi badala ya kuwachukulia hatua za kisheria.

Kamati hiyo imependekeza Bunge likubali kuitaka Serikali kutoa maelezo ya kuridhisha ni kwa nini ubadhirifu huo umeachwa ukishamiri kwa miaka mitatu mfululizo bila wahusika waliotajwa na CAG kuchukuliwa hatua.

“Shida iliyopo hapa ni Serikali kuonekana inawakumbatia wahusika kwa kisingizio cha uchunguzi unaendelea… nini kinachochunguzwa badala ya kupeleka watu mahakamani na kumuita CAG kama shahidi?”

Thursday, April 12

Lazima tulinde haki za wasanii. Hotuba yangu Bungeni #kazizawasanii #hakizawasanii na zitto kabwe

MHE. KABWE Z. ZITTO:

Mheshimiwa Naibu Spika, nami nikushukuru kwa kunipa fursa ya kuchangia katika Muswada huu ambao unabadilisha Sheria Mbalimbali za Biashara. Kumekuwa kuna malalamiko mengi sana kwamba nchi yetu iko nyuma sana katika kuweka mazingira mazuri ya watu kuweza kusajili Makampuni, kupata leseni na kufanya biashara. Nakumbuka kwamba kwa miaka mitatu sasa mfululizo nchi yetu imekuwa ikipata alama ambazo si nzuri katika ripoti ya Benki ya Dunia inayoangalia mazingira ya biashara (Doing Business Report) ambapo ripoti ya mwaka 2012 inayoonyesha kwamba tumeshuka zaidi kutoka nafasi ya 125 duniani katika nchi 180 na zilizofanyiwa kazi mpaka nafasi ya 127. Kwa hiyo naamini kabisa kwamba mabadiliko haya ambayo tunayafanya yataweza kusaidia kupunguza muda ambao mtu anaweza akasajili biashara au kusajili Kampuni na kadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, ningependa kuanzia pale ambapo mzungumzaji aliyepita alianza kuzungumza na suala ambalo napenda leo nichukue muda mrefu na wa kutosha kabisa ni suala la biashara ya sanaa. Biashara ya sanaa kwa sababu ni biashara ambayo imekuwa haiangaliwi nami niseme kabisa kwamba tulichokishuhudia jana heroic funeral ambayo alifanyiwa marehemu Kanumba inadhihirisha kabisa kwamba Watanzania ni wapenzi sana wa sanaa. Kwa hiyo ni jukumu letu sisi kama wawakilishi wa wananchi, kama watunga sheria, kama watunga sera kupata ujumbe kutokana na umati wa Watanzania wa mkoa wa Dar es Salaam na waliotoka mikoa ya jirani na waliotoka mikoa ya mbali ambao walienda kumzika na kumpunzisha ndugu Kanumba jana. Kwa hiyo ule ni ujumbe ambao tunaupata na leo tunapoandika sheria hii tuwe na kumbukumbu tuangalie wananchi waliojitokeza kwenye mazishi yale na kuweza kuona tuweke sheria maalum ambazo zitaweza kuwasaidia na kuwalinda wasanii wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunafanya marekebisho kwenye merchandise marked act ambapo tunaangalia pamoja na mambo mengine copy right neighbouring right act, paterns act, trade and services marked acts na hizo zingine mbili ambazo kwa leo sitaweza kuzichangia. Nataka nichangie hasa copy right and neighbouring act. Katika hotuba yetu ya Kambi ya Upinzani Bungeni mwaka jana tulitoa mapendekezo maalum ya kuweza kuangalia namna ya kuweza kulinda kazi za wasanii waweze kufaidika na kazi zao tuzuie wizi wa kazi za wasanii ambao Watanzania wanashiriki kwa sababu tunapoenda kununua kazi ya msanii ambao una uhakika kazi hii sio original, una uhakika kazi hii ni ya kutengenezwa na wewe ukatoa fedha yako ukanunua maana yake ni kwamba unamwua msanii ambao ungepaswa kuweza kumsaidia. Sasa njia pekee ya kuweza kuzuia hali hiyo ni kuweka sheria jinsi ambavyo inavyopaswa kuwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nimegawa sekta hii katika maeneo matatu ambayo ni ya kawaida unayakuta sana katika sekta ya mafuta au madini. Kwamba kuna up stream, mid stream na down stream. Kwenye up stream ni pale ambapo msanii anatengeneza kazi yake, pale sioni shida kwa sababu msanii atakaa nyumbani kwake, atakaa wapi ataandaa kazi yake. Lakini kwenye mid stream kwenye studios ambapo wasanii wanaenda kurekodi na baada ya hapo kazi zao zinaenda kusambazwa hapa kuna shida kubwa sana na ni eneo ambalo ni lazima tuliwekee regulations. Lazima tuliwekee kazi maalum na ningependa katika hili eneo la part four bahati mbaya sheria niliyonayo ni ile ambayo ilichapishwa tarehe 29 Julai, 2011. Kwa hiyo mtaweza kuangalia, muangalie namna ambavyo tutaweka leo katika sheria jinsi ambavyo tutalinda mid stream part katikati hapa ya kazi ya msanii pale anapoenda kurekodi na kuhakikisha kwamba kinachozalishwa pale kinafahamika, msanii anakifahamu na lile pendekezo ambalo lilitolewa na Waziri wetu kivuli wa masuala ya Habari, Utamaduni na Michezo la stickers lianzie pale ili kuweza kujua ni kiwango gani ambacho kimezalishwa katika studio na kiwango gani ambacho kinaingia kwenye soko.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pili eneo ambalo ningependa Mheshimiwa Waziri liongezwe pia katika part four hii ni down stream part kwenye retail kwamba kazi ambayo inauzwa ya msanii biashara ile ya rejareja ya msanii iwe ni kazi ile ambayo ilizalishwa, kwa hili eneo pia tuweze kuliona namna ambavyo tutakavyoweza kulitilia nguvu katika sheria hii. Kwa maana hiyo ni kwamba nilikuwa napendekeza kwamba yale maeneo ambayo yameachwa ya Sheria ya Hatimiliki cap. 218 yachukuliwe na kuingizwa ndani ya mabadiliko haya ambayo tunayafanya ili kuweza kuhakikisha kwamba kazi za wasanii zinalindwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pili hivi sasa tumepata taarifa kwamba TRA wanaandaa regulations kwa ajili ya stickers. Lakini nimeongea na mmoja wa wasanii wa muda mrefu Ndugu John Kitime anasema tayari regulations zipo wanaita epigram zipo lakini bado hazijaanza kutekelezwa. Kwa hiyo nilikuwa nadhani kwamba Mheshimiwa Waziri kwa sababu yeye ndio Waziri wa Wizara ambayo yuko responsible kwa hili ukishirikiana na Waziri wa Fedha kuhakikisha kwamba zoezi hili la TRA la kuandaa regulations nyingine za stickers liunganishwe na regulations ambazo tayari zimeshatengenezwa na ziko tayari toka mwaka 2006 ili ndani ya mwaka wa fedha unaoanza tarehe 1 Julai, 2012 stickers ziwe tayari na kazi za wasanii ziweze kutambulika pale ambapo zinakuwa zimetengenezwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pili nadhani hili litamhusu sana Mheshimiwa Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwamba tayari kuna regulations kuhusiana na royalties ambazo broadcasters wanapokuwa wanacheza miziki hii zile regulations kwa ajili ya royalties hazijawa enforced na hasa haya Makampuni makubwa, televesheni kubwa, redio kubwa hazi-enforce hili. Kwa hiyo miziki na filamu na kadhalika za wasanii wetu zinapokuwa zinachezwa hawapati zile royalties ambazo zinatakiwa na kama tulivyosema kwamba hii ni biashara na ni biashara ambayo inaweza ikawafaidisha sana wasanii wetu. Nilikuwa naomba tu Waziri tena narejea kwamba natumia iliyokuwa published tarehe 29 Julai 2011 kwa mtu anaweza kuangalia namna ambavyo inakwenda.

Mheshimiwa Naibu Spika, kifungu cha 36 Prohibition to deal in counterfeit goods. Nimeangalia hapa orodha ya offence ambazo mtu atafanya kutokana na counterfeit sioni moja kwa moja mtu ambaye atahusika na wizi wa kazi za sanaa. Kwa hiyo nilikuwa naomba ile “a” mpaka “i” tutafute mahali ambazo tutaweka tuta-include copy right issues katika counterfeit act ili kuweza kuhakikisha kwamba tunaposema counterfeit hatutakuwa na maana tu ya bidhaa kama maji, bidhaa zingine hapana, lakini pili kazi ya msanii iweze kuwa included katika jambo hilo. Kwa hiyo tu-include katika ile “a” mpaka “i” masuala ya piracy, book leading na kadhalika yawe ndani ya sheria. Lakini lingine ambalo nimeliona hapa ni adhabu, sasa sijui itakuwepo kwenye amendment maana yake amendments nimezipata sasa hivi sioni adhabu kwa mtu ambaye hatakutwa anafanya biashara ya kazi ambazo zimeibwa za wasanii, sioni katika kifungu hiki cha prohibition to deal in counterfeit.

Kwa hiyo nilikuwa napendekeza sio tu adhabu ya kawaida iwe ni adhabu kali, adhabu ambayo ita-discourage kabisa watu kuiba kazi za wasanii wetu na kuweza kuziuza. Kwa hiyo nilikuwa nashauri kwamba nimeona kuna maeneo kuna faini za shilingi milioni 20, kuna miaka mitano jela sasa sina uhakika maana yake leo nimeiona sasa hivi kama hizi zinahusiana na hii yaku-deal na counterfeit. Kwa sababu hii section yote ya counterfeit imetajwa offences lakini haitaji adhabu. Kwa hiyo nilikuwa naomba Mheshimiwa Waziri na watu wa Idara ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali iongeze kipengele cha adhabu mara baada ya zile offences na iseme kabisa kwamba mtu yoyote at a written level atakayekutwa anauza ama ni CD au ni DVD ambayo ni Pirated ambayo ni counterfeit adhabu yake isiwe chini ya shilingi milioni 50. Hiyo ita-discourage kabisa kabisa kazi ambazo zinafanywa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini sio hivyo tu sio mtu tu atakayekutwa anauza lakini pia mtu yoyote atakayekutwa in possession kwa hiyo hata kama wewe umepita pale Ubungo vijana wamekuuzia lakini ni kazi ya wizi umekaa labda umempa lifti Polisi akaona akagundua kwamba hii ni kazi ulionunua ni ya wizi wewe ambao umekutwa in possession uadhibiwe ili kujenga mentality ya Watanzania kuacha kununua kazi ambazo ni za wizi dhidi ya wasanii wetu. Kwa hiyo haya ndiyo mapendekezo ambayo nilikuwa nayaomba tuyaweke kwa sababu kuna fedha nyingi sana kwenye sanaa.

Commitment ya Serikali kulinda wasanii wetu(hansard) by zittokabwe

WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA:

Napenda kutoa kauli ya Serikali, kwamba kutokana vikao vyote hivyo ambavyo nimesema kumi na sita vya Mawaziri lakini leo tena tumekutana mara ya kumi na saba, tumeazimia kwamba hotuba ya bajeti ya mwezi wa sita Mheshimiwa Waziri wa Fedha atalizungumzia jambo hilo na utekelezaji wa mambo yote pamoja na utengenezaji wa sticker, na jinsi ambavyo TRA watafanya jambo hilo yatawekwa bayana na mara baada ya bajeti speech kuanzia tarehe 1 Julai, kutakuwa na mabadiliko kubwa katika kazi za wasanii wa nchi yetu ya Tanzania.

Kwa hiyo nataka niwashukuru Waheshimiwa Wabunge, nataka tu watambue kwamba Serikali inaliona hilo Serikali iko pamoja na wao na ndiyo maana tumekutana namna hiyo na kwa hakika katika hili tuko pamoja kabisa na mtaona utekelezaji wake.

KAMATI YA BUNGE ZIMA

MHE. KABWE Z. ZITTO:

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeleta mapendekezo, Jedwali la Marekebisho kipengele hicho cha 38. Wakati Mheshimiwa Waziri anafanya winding up alitoa commitment ya Serikali kuhusiana na mabadiliko makubwa ya eneo la copyrights kwa ajili ya kulinda kazi za wasanii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba Mheshimiwa Waziri arejee ile commitment kabla sijaweza ku-move hii amendment. Tafadhali. Airejee kwa faida ya Taifa na kwa faida ya Bunge.

MWENYEKITI:

Mheshimiwa Waziri, Mheshimiwa Zitto pamoja na amendment aliyoleta, amezingatia sana kauli yako wakati unajibu hoja za Waheshimiwa Wabunge. Anaomba ile commitment ya Serikali ya kufanya marekebisho kwenye sheria ya copyright. Sasa hiyo commitment ya Serikali ndiyo itakayomsababisha yeye kuondoa jedwali lake la marekebisho ili sasa tuhoji kifungu hiki.

WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA:

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati ninafanya majumuisho nilisema kwamba mimi na Mheshimiwa Mkulo – Waziri wa Fedha na Mheshimiwa Nchimbi tumekutana mara nyingi sana kwa ajili ya suala hilo la kuangalia haki za wasanii Watanzania kwamba hazipotei. Lakini vile vile tumeagiza mamlaka zilizoko chini ya Wizara zetu; COSOTA kwa Viwanda na Biashara, TRA kwa upande wa Wizara ya Fedha na BASATA kwa upande wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wakae. Wamefanya vikao mara tatu. Kutokana na yaliyokubaliwa katika vikao vyote vya Waheshimiwa Mawaziri na wajumbe wa zile Kamati, Mheshimiwa Mwenyekiti, narudia commitment ya Serikali kwamba kwenye Bajeti ijayo, Serikali italeta mapendekezo makubwa ambayo yatakuwa yamezingatia maoni yote ambayo yametolewa na BASATA, COSOTA na TRA kuhusu namna bora ya kulinda haki za wasanii wa aina zote katika nchi yetu ya Tanzania.

MHE. KABWE Z. ZITTO:

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nataka hiyo commitment ili itakapofika siku ya bajeti tutumie Hansard hii kuhakikisha kwamba commitment hiyo imetekelezwa. Kwa maana hiyo nikwamba naondoa amendment yangu ambayo nimeileta.

MWENYEKITI:

Nakushukuru. Na nafikiri kwamba Serikali iko makini, inavyofanya commitment hapa inaelewa nini inachokifanya.

Tuesday, April 10

How to Stop Teeth Grinding

7 tips to overcome bruxism and save your teeth
Teeth grinding: Causes and consequences
My friend’s teeth grinding had started during a period of higher than normal stress in his life. But as he told me: “My life is good at the moment, so I don’t understand why it’s still happening!” Actually, a problem habit formed during stressful times often hangs around once the stress has lessened simply because it has become just that: a habit. Bad news if something isn’t done about it.
Teeth grinding and jaw clenching can unfortunately cause many different problems. When you grind your teeth, you wear away the tooth enamel. Too much wear and tear can lead to sensitive teeth, decay, and also damaged dental work. Continued and prolonged teeth grinding can damage the muscles and joints of the jaw, which could even cause osteoarthritis.
Of course the sooner you stop grinding your teeth, the less damage you do.
So what can be done to stop the rot? Well, here are some ideas I’ve used with teeth grinding clients over the years and, of course, my good friend. : )

Tip 1: Raise your awareness to stop teeth grinding
Take a couple of moments each day just to be aware of what your jaw is doing. Set your watch to check, say, once at 9am, once at 11am, then again at 3pm, 6pm, and just before you go to sleep. Your lips should be sealed but your teeth should not be touching. Consciously drop your jaw and let your whole lower face relax. Imagine that you are ‘re-setting’ your jaw and teeth to ‘behave’ for the next few hours - like programming your body. This will help change the teeth grinding pattern so that soon you’ll notice it’s been better without you having to think about it.

Tip 2: Get a night guard
No, not a security night watchman (unless you live in a really rough neighbourhood).
If teeth grinding has got to such a stage that you fear you might be doing damage, then consider asking your dentist to make a ‘night guard’ for you. This will be a plastic device to help redistribute the force from grinding, protecting your teeth from damage. And relax; you won’t look like Hannibal Lector. : )

Tip 3: Try a bit of mouth massage

Massage relaxes the body directly. In a sense, we can look upon massage as a communication to your body. Massage ‘says’: “Let go of tension and start to relax!” Massage works for stressed backs and necks and can also help calm your jaw muscles, easing away tensions. Before you retire for the night, take five minutes to gently massage your own face and jaw. Use gentle small circular rubbing motions with your hands to loosen everything up before you head off for Slumberland.

Tip 4: Stay away from alcohol
Teeth grinding tends to worsen after excessive alcohol consumption, so drink wisely. This may be partly because the quality of sleep is affected by heavy boozing sessions. More disturbed sleep means less rest and more nocturnal activity, which might include more teeth grinding.

Tip 5: Quit chewing gum and delicious pen lids
If you chew gum, then don’t - or at least, not very often. Constant chewing of gum (or pens, pen lids, or table legs…just kidding) just gets your jaws used to clamping. Remember, you want to re-condition them to be more relaxed and less active more of the time.

Tip 6: Stop teeth grinding by melting stress away
Because so much bruxism is caused by stress, it makes sense to relax deeply. Think of stress as like water in a bucket which you carry around with you. If you don’t empty it now and then, it can overflow from the slightest knock or nudge. It’s the same with stress: if you don’t ‘empty the stress’ by regular relaxation, then any small life knock can leave you feeling flooded with tension.
Mind and body relaxation will help calm the muscles of your whole body, including your jaw. Take time out once a day to listen to a relaxation CD. Or just close your eyes and focus on your breathing, then take your mind to each part of your body, imagining the different parts relaxing in turn.
If you know how to use self-hypnosis, then use this time to make suggestions to your own unconscious mind to stop teeth grinding.
Or let me help you relax quickly by clicking the free audio link below.

Tip 7: Really get what you need
We all have basic emotional and physical needs. If we consistently fail to meet these needs, we feel stressed. And, as you know, the more stressed you are, the more likely you are to grind your teeth. Being clear about what these needs are means you can work towards meeting them effectively.

You have a need:
For adequate and healthy nutrition, exercise, sleep, and water.
To feel safe and secure in life.
To regularly give and receive quality attention.
To feel a sense of influence and control over your life.
To feel part of a wider community.
To enjoy friendship, fun, love, and intimacy with significant people.
To feel a sense of status; basically, to feel you have a recognizable role in life. This also connects to a sense of competence and achievement.
To feel stretched but not stressed so you can avoid boredom and stagnation. This also enhances your self-esteem.
So if you do feel particularly stressed at present, think about how well the above needs are being met in your life. Meeting them better may help you quickly stop teeth grinding.
Follow these tips and teeth grinding will be a past irritation, not a current ‘nightmare’.

Share this article

Thursday, April 5

Maana ya matokeo Arumeru Mashariki by zittokabwe Matokeo ya Arumeru na kata za Mwanza, Songea na Mbeya ni mwanzo wa safari ya mwisho ya CCM na kwamba wanaondolewa madarakani kwa sababu wananchi wamekasirishwa, hasira ambazo fedha haiwezi kununua. Hasira ambayo matusi hayawezi kuifuta. Hasira ambayo vitisho havifui dafu. Hasira ya kutaka huduma bora. Hasira ya kuchoka na umasikini na kufukarishwa. Hasira ya kuchoshwa na ufisadi. Mhe Mwenyekiti Freeman Mbowe na Mhe Joshua Nassari Mnamo tarehe 11 Machi mwaka huu 2012 nikiwa ndani ya ndege natokea Arumeru kuzindua kampeni za uchaguzi mdogo wa jimbo la Arumeru Mashariki kwenda Kirumba Mwanza kuzindua kampeni za Udiwani katika kata ya Kirumba, niliandika makala kuhusu nini kitaamua mshindi katika uchaguzi ule. Nilianza makala yangu ile kwa kusema haya "Uchaguzi wa Ubunge Arumeru Mashariki ni kipimo cha namna wananchi mnavyoridhika na watawala, namna mnavyoridhika na mgawo wa Ardhi na namna mnavyoridhika na mgawanyo wa Maji katika Wilaya yenu". Haya maneno ilikuwa ni nukuu ya sehemu ya hotuba niliyotoa wakati namkaribisha Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA ndugu Freeman Mbowe kuzindua rasmi kampeni zetu. Ardhi ilikuwa ajenda kubwa sana. Washindani wetu wa CCM wakaona hatari ya hoja ya Ardhi na kuanza kutoa ahadi mbalimbali za kumaliza kero ya Ardhi. Hawakuaminika. Wananchi walisema, hawa wamemaliza miaka 50 bila kutatua kero hii, watawezaje kupata suluhisho sasa. Wakakataa. Hawakuichagua CCM na badala yake wakamchagua kwa kura nyingi sana ndugu Joshua Nassari, kijana wa miaka 26 tu kuwa Mbunge wa Jimbo Lao. Katika makala ile nilieleza wazi kwamba "Uchaguzi wa Arumeru ni uchaguzi kati ya kuwa na Ardhi au kuendelea kutokuwa nayo. Ni uchaguzi muhimu kwa watu wa Meru. Wasio na Ardhi watamchagua mgombea atakayesimamia mgawo wa Ardhi unaozingatia haki. Mgombea huyo ni mgombea wa CHADEMA ndugu Joshua Nassari. Sasa Nassari lazima aibebe ajenda Ardhi. Hana namna ni lazima awe sauti ya wananchi masikini waliofukarishwa na mfumo mbovu wa kugawa Ardhi ulioanzishwa wakati wa ukoloni na kuendelezwa chini ya Uongozi wa CCM. Ushindi wa CHADEMA katika uchaguzi wa Arumeru ni ishara ya dhahiri kabisa kwamba siku za CCM kuongoza Taifa letu zinahesabika. Ukilinganisha nguvu ya rasilimali watu na fedha ambayo CCM waliiweka huko Meru kulinganisha na CHADEMA unaona dhahiri kabisa kuwa fedha sio kigezo cha kushinda uchaguzi. Wananchi sasa wanataka masuala Yao yashughulikiwe. Hii pia imejionyesha katika chaguzi za Madiwani. CCM imepoteza nusu ya viti vya Udiwani vilivyokuwa vinagombewa. Katanza Lizaboni Songea, Kiwira Mbeya na Kirumba Mwanza zote zimeenda CHADEMA. Kata ya Msambweni Tanga imeenda CUF. CCM walipata kata katika Wilaya ya Bagamoyo, Bariadi na Temeke. Pia walipata kata katika manispaa ya Dodoma. Huu ni uchaguzi wa kwanza wa Madiwani ambao CCM imepoteza nusu ya viti vilivyokuwa vinagombewa toka mfumo wa vyama vingine uanze. Arumeru imekuwa jimbo la kwanza CCM kulipoteza kwa chama cha upinzani Tangu mwaka 1997 ambapo CCM walipoteza jimbo la Magu kwa chama cha UDP. Kwa CHADEMA hili ni jimbo la kwanza kulichukua kutoka CCM katika uchaguzi mdogo toka ianzishwe mwaka 1992. Itakumbukwa kwamba mwaka 2008 CHADEMA ilishinda jimbo la Tarime kwa kulirejesha maana kilikuwa linashikiliwa nacho. People's power Hivyo ni dhahiri kabisa kwamba siku za CCM kuwa madarakani zinahesabika. Ushindi wa Arumeru na Udiwani katika kata mbalimbali umeleta mageuzi makubwa ya kisaikolojia kwa wananchi kuliko hata ushindi wa Tarime. Ni wazi kabisa kuwa ushindi huu utafutiwa na mikutano wa kunadi chama katika mikoa mbalimbali nchini ikiwemo mikoa ya Kusini na ile ya Magharibi ambapo CHADEMA haijafanya operesheni. Kushindwa kwa CCM Arumeru pia kutal eta mpasuko zaidi ndani ya CCM na kuunganisha nguvu za wanasiasa ndani ya CHADEMA. Wakati CCM itakuwa inanyoosheana vidole kutafuta mchawi na hata wengine kufurahia kushindwa kwao (wakiamini ni kushindwa mmoja wa mahasimu wao), CHADEMA itakuwa inashikana mikono na kuimarisha mshikamano ili hatimaye kuchukua Dola ifikapo mwaka 2015. Jambo moja la dhahiri unaliona Baada ya uchaguzi wa Arumeru. Sasa ukipanda Basi kutoka Moshi kwenda Arusha, utopita ngome ya Chadema tu. Moshi mjini, Hai, Arumeru Mashariki na Arusha Mjini. Kwa waliomsoma Rais Museveni katika kitabu chake cha Sowing the Mustered seed, akitumia njia za Frelimo katika ukombozi, eneo hili sasa ni Liberated Zone. Ukanda uliokombolewa. Lengo langu ni kuonyesha kuwa hii ndio safari ya mwisho ya CCM na kwamba wanaondolewa madarakani kwa sababu wananchi wamekasirishwa, hasira ambazo fedha haiwezi kununua. Hasira ambayo matusi hayawezi kuifuta. Hasira ambayo vitisho havifui dafu. Hasira ya kutaka huduma bora. Hasira ya kuchoka na umasikini na kufukarishwa. Hasira ya kuchoshwa na ufisadi.

Matokeo ya Arumeru na kata za Mwanza, Songea na Mbeya ni mwanzo wa safari ya mwisho ya CCM na kwamba wanaondolewa madarakani kwa sababu wananchi wamekasirishwa, hasira ambazo fedha haiwezi kununua. Hasira ambayo matusi hayawezi kuifuta. Hasira ambayo vitisho havifui dafu. Hasira ya kutaka huduma bora. Hasira ya kuchoka na umasikini na kufukarishwa. Hasira ya kuchoshwa na ufisadi.

Mnamo tarehe 11 Machi mwaka huu 2012 nikiwa ndani ya ndege natokea Arumeru kuzindua kampeni za uchaguzi mdogo wa jimbo la Arumeru Mashariki kwenda Kirumba Mwanza kuzindua kampeni za Udiwani katika kata ya Kirumba, niliandika makala kuhusu nini kitaamua mshindi katika uchaguzi ule. Nilianza makala yangu ile kwa kusema haya
"Uchaguzi wa Ubunge Arumeru Mashariki ni kipimo cha namna wananchi mnavyoridhika na watawala, namna mnavyoridhika na mgawo wa Ardhi na namna mnavyoridhika na mgawanyo wa Maji katika Wilaya yenu".

Haya maneno ilikuwa ni nukuu ya sehemu ya hotuba niliyotoa wakati namkaribisha Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA ndugu Freeman Mbowe kuzindua rasmi kampeni zetu.
Ardhi ilikuwa ajenda kubwa sana. Washindani wetu wa CCM wakaona hatari ya hoja ya Ardhi na kuanza kutoa ahadi mbalimbali za kumaliza kero ya Ardhi. Hawakuaminika. Wananchi walisema, hawa wamemaliza miaka 50 bila kutatua kero hii, watawezaje kupata suluhisho sasa. Wakakataa. Hawakuichagua CCM na badala yake wakamchagua kwa kura nyingi sana ndugu Joshua Nassari, kijana wa miaka 26 tu kuwa Mbunge wa Jimbo Lao. Katika makala ile nilieleza wazi kwamba
"Uchaguzi wa Arumeru ni uchaguzi kati ya kuwa na Ardhi au kuendelea kutokuwa nayo. Ni uchaguzi muhimu kwa watu wa Meru. Wasio na Ardhi watamchagua mgombea atakayesimamia mgawo wa Ardhi unaozingatia haki. Mgombea huyo ni mgombea wa CHADEMA ndugu Joshua Nassari. Sasa Nassari lazima aibebe ajenda Ardhi. Hana namna ni lazima awe sauti ya wananchi masikini waliofukarishwa na mfumo mbovu wa kugawa Ardhi ulioanzishwa wakati wa ukoloni na kuendelezwa chini ya Uongozi wa CCM.
Ushindi wa CHADEMA katika uchaguzi wa Arumeru ni ishara ya dhahiri kabisa kwamba siku za CCM kuongoza Taifa letu zinahesabika. Ukilinganisha nguvu ya rasilimali watu na fedha ambayo CCM waliiweka huko Meru kulinganisha na CHADEMA unaona dhahiri kabisa kuwa fedha sio kigezo cha kushinda uchaguzi. Wananchi sasa wanataka masuala Yao yashughulikiwe. Hii pia imejionyesha katika chaguzi za Madiwani.

CCM imepoteza nusu ya viti vya Udiwani vilivyokuwa vinagombewa. Katanza Lizaboni Songea, Kiwira Mbeya na Kirumba Mwanza zote zimeenda CHADEMA. Kata ya Msambweni Tanga imeenda CUF. CCM walipata kata katika Wilaya ya Bagamoyo, Bariadi na Temeke. Pia walipata kata katika manispaa ya Dodoma.

Huu ni uchaguzi wa kwanza wa Madiwani ambao CCM imepoteza nusu ya viti vilivyokuwa vinagombewa toka mfumo wa vyama vingine uanze. Arumeru imekuwa jimbo la kwanza CCM kulipoteza kwa chama cha upinzani Tangu mwaka 1997 ambapo CCM walipoteza jimbo la Magu kwa chama cha UDP. Kwa CHADEMA hili ni jimbo la kwanza kulichukua kutoka CCM katika uchaguzi mdogo toka ianzishwe mwaka 1992. Itakumbukwa kwamba mwaka 2008 CHADEMA ilishinda jimbo la Tarime kwa kulirejesha maana kilikuwa linashikiliwa nacho.

People's power

Hivyo ni dhahiri kabisa kwamba siku za CCM kuwa madarakani zinahesabika. Ushindi wa Arumeru na Udiwani katika kata mbalimbali umeleta mageuzi makubwa ya kisaikolojia kwa wananchi kuliko hata ushindi wa Tarime. Ni wazi kabisa kuwa ushindi huu utafutiwa na mikutano wa kunadi chama katika mikoa mbalimbali nchini ikiwemo mikoa ya Kusini na ile ya Magharibi ambapo CHADEMA haijafanya operesheni.

Kushindwa kwa CCM Arumeru pia kutal eta mpasuko zaidi ndani ya CCM na kuunganisha nguvu za wanasiasa ndani ya CHADEMA. Wakati CCM itakuwa inanyoosheana vidole kutafuta mchawi na hata wengine kufurahia kushindwa kwao (wakiamini ni kushindwa mmoja wa mahasimu wao), CHADEMA itakuwa inashikana mikono na kuimarisha mshikamano ili hatimaye kuchukua Dola ifikapo mwaka 2015.

Jambo moja la dhahiri unaliona Baada ya uchaguzi wa Arumeru. Sasa ukipanda Basi kutoka Moshi kwenda Arusha, utopita ngome ya Chadema tu. Moshi mjini, Hai, Arumeru Mashariki na Arusha Mjini. Kwa waliomsoma Rais Museveni katika kitabu chake cha Sowing the Mustered seed, akitumia njia za Frelimo katika ukombozi, eneo hili sasa ni Liberated Zone. Ukanda uliokombolewa.

Lengo langu ni kuonyesha kuwa hii ndio safari ya mwisho ya CCM na kwamba wanaondolewa madarakani kwa sababu wananchi wamekasirishwa, hasira ambazo fedha haiwezi kununua. Hasira ambayo matusi hayawezi kuifuta. Hasira ambayo vitisho havifui dafu. Hasira ya kutaka huduma bora. Hasira ya kuchoka na umasikini na kufukarishwa. Hasira ya kuchoshwa na ufisadi.

Monday, April 2

CCM hali mbaya Arumeru

CHADEMA YAFANYA VIZURI KATA 11KATI YA 17, YASHINDA PIA UDIWANI MWANZA. SONGEA,MBEYA,CUF YAPETA TANGA

CHAMA Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeongoza kwenye kura za awali kwa mgombea wake, Joshua Nassari kupata kura nyingi katika kata 11 kati ya Kata 17 za Jimbo la Arumeru Mashariki.

Dakika chache kabla ya kutangaza matokeo hayo, baadhi ya wafuasi wa CCM waliokuwa wamefurika katika Ofisi za Mji Mdogo wa Usa River na baadhi ya polisi, walikuwa wameondoka eneo hilo, wakiwaacha wapambe wachache wa mgombea wao, Sioi akiwamo, Beno Malisa.

Huu ni uchaguzi wa kwanza mdogo kwa Chadema kushinda katika jimbo lililokuwa likishikiliwa na CCM na uchaguzi wa pili kwa chama hicho cha upinzani, kushinda katika uchaguzi mdogo baada ya ule uliofanyika katika Jimbo la Tarime, kuziba nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Chacha Wangwe.

Katika matokeo hayo yanayokusanywa na kujumlishwa katika ofisi za mji mdogo wa USA River, CCM, imefanya vema katika kata tatu ambako mgombea wake, Sioi Sumari amepata kura nyingi ikilinganishwa na Nassari.

Takwimu zinaonyesha kuwa Chadema wanaongoza katika kata za Akheri ambako ni nyumbani Kwa Sioi, Poli, USA-River, Mbuguni, Seela, Sing'isi, Nkoarua, Maji ya Chai, Kikwe, Maroroni, Nkoaranga, King'ori na Songoro ambako ni nyumbani Kwa Nassari. Jimbo la Arumeru Mashariki lina kata 17.

Mgombea wa CCM Sioi ameongoza katika kata za Makiba, Leguruki na Mkoandrua hadi saa 7:15 usiku jana ambapo msimamizi wa uchaguzi, Trasias Kagenzi alikuwa akisubiri masanduku ya kura kutoka kata mbili.

Kata ambazo masanduku na matokeo yake yalichelewa kutokana na umbali wa maeneo hayo ni Kikatiti na Ngarenanyuki.

Mbali na Chadema kuongoza Arumeru chama hicho pia kimeibuka kidedea katika uchaguzi mdogo wa udiwani katika mikoa ya Mbeya, Ruvuma na Mwanza.

CUF imeambulia kiti kimoja cha udiwani Tanga na CCM Dar es Salaam.

Katika tukio lingine, wakala wa Chadema katika chumba Cha kujumlisha kura, Godbless Lema, jana alilazimika kutumia nguvu dhidi ya msimamizi msaidizi wa kata ya Maroroni ambaye jina lake halikupatikana mara moja baada ya kumtuhumu kutaka kubadili tarakimu za matokeo kwenye fomu rasmi zilizowasilishwa.

"Yule msimamizi alikuwa akitaka kuchezea tarakimu katika fomu za matokeo kutoka kwenye kata yake bila kujua kama nilikuwa namfuatilia," alisema Lema.