Wednesday, December 21

Nyumba zachomwa moto kwa imani za kishirikina. Na Fredy Bakalemwa, Mbeya.

Wakazi wa mtaa wa Igoma A kata ya Isanga jijini Mbeya wamezizoma moto nyumba mbili, moja ikiwa ya mwenyekiti wa mtaa huo Bwana Juma Kahawa.

Nyumba nyingine iliyoteketezwa kwa moto na watu walioamua kujichukuliwa sheria mkononi ni ya Bwana Herman Tonji naye ni mkazi wa mtaa huo.

Imedaiwa na baadhi ya wakazi wa mtaa huo kuwa hatua hiyo imefikiwa kutokana na kuwatuhumu watu hao kuwa ni washirikiana kwa madai kuwa baadhi ya watoto katika mtaa huo wamepotea na kukutwa wakiwa wamekufa katika mazingira tatanishi.

Tukio la Jumatano jioni katika mtaa wa Igoma kata ya Isanga lilinaswa na kamera ya Star Tv ambapo umati wa watu walitoka mkutanoni baada ya kushindwa kupata mwafaka hasira zikawaelekeza kujichukulia sheria mkononi.

Wakati tukio likiendelea kikosi cha zima moto kilifika eneo la tukio ili kuokoamalizilizokuwa zimesalia lakini hata hivyo sehemu kubwa yamalizilikuwa zimeteketea.

Kwa kuwa watekelezaji wa hatua hiyo walitambua kuwa wanavunja sharia, baada ya kuona askari polisi wakiwa na silaha hakuna aliyesalia bali walihamia katika nyumba nyingine ya Bwana Herman Tonji.

Polisi walipofika wakachukua hatua za kuokoa baadhi yamalikabla ya kuteketea, lakini siyo kila kitu kiliguswa.

Kamanda wa polisi mkoani Mbeya ACP Advocate Nyombi alitoa tamko, kuthibitisha tukiohilokwa kuwataka wananchi kutojichukulia sheria mkononi.

Mwisho.

No comments:

Post a Comment