Thursday, September 19

bunduki: 10 Things You Probably Didn’t Know About Nelson Ma...

bunduki: 10 Things You Probably Didn’t Know About Nelson Ma...: Most people know Nelson Mandela as the first black president of South Africa, a man who became a symbol of the anti-apartheid movement,...

10 Things You Probably Didn’t Know About Nelson Mandela


Most people know Nelson Mandela as the first black president of South Africa, a man who became a symbol of the anti-apartheid movement, and one who gave up nearly 30 years of his life in prison. He remains a hero to South Africans as well as to the international community, and will continually represent the struggle for freedom. But it’s easy to forget that even legends are human. Here are 10 things you probably didn’t know about Nelson Mandela.

*For the conspiracy theorists out there, I regret to inform you that Mandela is not in fact a part of the Illuminati, does not lead a Satanist cult, and did not die in Robben Island 30 years ago, only to be replaced by an impersonator.


1. Mandela’s tribal nickname is “Rolihlahla,” meaning “Troublemaker.”
Other accounts translate Rolihlalhla to mean “to pull a branch from a tree,” which, of course, is something only a troublemaker would do. It was his teacher, Miss Mdingane, who gave him the English name “Nelson,” much to the relief of journalists everywhere when he became famous.


2. Mandela was expelled from university after less than a year.
After finishing boarding school, Mandela headed to Fort Hare Missionary College. Less than 12 months later, he was expelled from college for helping to organize a strike against the white colonial rule of the institution. One might call this foreshadowing.


3. The United Nations decreed his birthday as Mandela Day.
In 2009, the U.N. declared Mandela’s birthday, July 18, as Mandela Day to mark his contribution to world freedom. The holiday calls on individuals to donate 67 minutes to doing something for others, reflecting the 67 years that Mandela had been a part of the anti-apartheid movement


4.  Mandela is often referred to as Madiba, his Xhosa clan name
Mandela is a member of the Thembu, a Xhosa clan, and is often referred to by his clan name, Madiba. It is a sign of the incredible diversity of people and languages in South Africa. The country has 11 different official languages.


5. Mandela’s father had four wives, and Nelson is one of 13 children.
Mandela’s father, a local chief and councellor to the Thembu king, died from tuberculosis when his son was 9. Before that, he fathered 13 children by four wives, four boys and nine  girls. After his father’s death, Mandela was put under the guardianship of Jongintaba, the Thembu regent


 6. Mandela has received more than 250 awards for his accomplishments.
Among these awards is the shared 1993 Nobel Peace Prize with F.W. de Klerk, the last president of the apartheid government of South Africa (he too is widely credited as an instrumental force in ending apartheid). Additionally, Mandela has received more than 50 honorary degrees from international universities worldwide, became the first honorary Canadian citizen in 2001, and received the last Lenin Peace Prize from the Soviet Union.


7. Stevie Wonder dedicated his 1985 Oscar for “I Just Called to Say I Love You” to Mandela.
After Stevie accepted his award in honor of Nelson Mandela, the government-owned South African Broadcasting Corporation banned Stevie’s music from the airways. It wasn’t until Mandela was elected in 1994 that Stevie was finally allowed back in South Africa.


 8. Mandela outlived his two oldest sons.
Mandela had six children, but tragically lost his two oldest sons. Thembi died in a car crash at age 25. Mandela was in prison at the time of the death and was unable to attend the funeral. Another son died of AIDS in 2005 at age 54. While Mandela’s administration was criticized for not doing enough to fight the AIDS epidemic in South Africa, he established the Nelson Mandela Foundation in 1999 following his retirement to help fight the spread of AIDS.

9. Mandela ran away from home at age of 19.
When his guardian tried to arrange a marriage, Mandela ran away from home in 1941 and headed to Johannesburg. He began to work as a night watchman at Crown Mines, but was fired after it was discovered that he was the Thembu regent’s runaway.


10. Mandela spent his first night after being freed from prison in Archbishop Emeritus Desmond Tutu’s home.
Tutu had his helpers prepare his own favorite meal of chicken curry, rice and green salad, followed by rum raisin ice cream and custard.

Wednesday, September 11

Alex Massawe afikishwa mahakamani huko Dubai

Mfanyabiashara maarufu nchini, Alex Massawe amefikishwa mahakamani Dubai, Falme za Kiarabu (UAE), kwa tuhuma za mauaji baada ya Serikali ya Tanzania kupitia Shirika la Polisi la Kimataifa (Interpol), kuiomba Serikali ya nchi hiyo kumkamata. 

Massawe anayetarajiwa kuletwa nchini wakati wowote kuanzia sasa, alikuwa anatafutwa na Polisi wa Tanzania kwa muda mrefu na alikamatwa Dubai, mapema Julai na maofisa wa usalama wa UAE baada ya alama zake za vidole kuonyesha kuwa alikuwamo kwenye orodha ya watu waliokuwa wanasakwa na Interpol.
 
 
Baada ya kukamatwa, Mkuu wa Interpol, Tawi la Tanzania, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Gustav Babile alisema Massawe alikamatwa kati ya Juni 20 na 25, mwaka huu kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dubai akitokea Afrika Kusini.
 
 
Massawe ambaye anafanya biashara zake katika Miji ya Arusha, Dar es Salaam na Moshi, inadaiwa kwamba akiwa Dubai, alikutwa na pasi tatu bandia za kusafiria zilizokuwa na majina tofauti wakati alama zake za vidole zilionyesha anaitwa Alex Massawe. “Ombi la kuleta mhalifu nchini kutoka nje ya nchi (extradition request), lina hatua ndefu. 

Unajua kuna mlolongo wa taratibu za kutekeleza. Kwanza lazima Polisi wa Tanzania watoe tangazo kwa Interpol kuhusu kumsaka mtu huyo ili aletwe,” alisema Babile.
 
 
Hivi karibuni, Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu Dar es Salaam ilitoa hati ya kukamatwa na kurejeshwa nchini kwa Massawe ili kukabiliana na kesi mbili ikiwamo ya madai ya kughushi nyaraka mbalimbali.
 
 
Hati hiyo ilitolewa baada ya Wakili Mwandamizi wa Serikali, Tumaini Kweka kuwasilisha ombi la kutaka mfanyabiashara huyo arejeshwe nchini kwa kuwa tayari amefunguliwa kesi namba 150/2013.
 
 
Akizungumza Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI), Kamishna wa Polisi, Robert Manumba alisema kwa agizo hilo, polisi kupitia kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali waliandika barua kwa Mwanasheria Mkuu wa Dubai kuangalia taratibu za kisheria za kumrudisha baada ya kumfikisha mahakamani mtuhumiwa huyo.
 
 
“Massawe alifikishwa mahakamani Dubai kwa makosa ya kukutwa na hati bandia za kusafiria, lakini vilevile kugundulika kuwa ni kati ya watu wanaotafutwa na Polisi wa Interpol kwa tuhuma za mauaji,” alisema Manumba.
 
 
“Sheria inasema mtu akikamatwa nchi nyingine, anashtakiwa nchini humo, huku taratibu za kisheria za kumrejesha zikiendelea kwa nchi ambazo zina utaratibu wa kubadilishana wafungwa kama ilivyo Tanzania na UAE,” alisema Manumba.
 

Alisema ushahidi dhidi ya mtuhumiwa huyo umekamilika na tayari umewasilishwa Dubai ili kuendelea na taratibu nyingine za kisheria za kumrejesha Tanzania haraka kujibu tuhuma zinazomkabili.
 
 
Kutajwa mahakamani
 
Aprili 4, mwaka huu, Massawe alitajwa mahakamani katika kesi ya mauaji ya mfanyabiashara Onesphory Kituly ambaye aliuawa katika mazingira ya kutatanisha Novemba 6, 2011 akiwa nyumbani kwake Magomeni, Dar es Salaam.

Katika kesi hiyo ambayo mshtakiwa wa kwanza ni mfanyabiashara maarufu, Abubakar Marijani ‘Papaa Msofe’, mshtakiwa mwingine, Makongoro Joseph Nyerere alitoa malalamiko, mbele ya Hakimu Mkazi, Agnes Mchome mara baada ya Wakili wa Serikali, Mwanaisha Kombo kudai upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na kuomba tarehe mpya ya kuitaja.
 
Mshtakiwa huyo, aliomba jalada la kesi yao lipelekwe mahakamani hapo kwa ajili ya kulifanyia kazi na kutuhumu kuwa ndugu wa marehemu Kituly hawataki maendeleo ya kesi yao hadi Massawe akamatwe.

-Mwananchi

Haya ndo mashitaka matatu aliyosomewa makamu wa Rais wa Kenya mbele ya mahakama ya ICC

William Ruto amekana mashtaka yote yanayomkabili kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC). 
  
Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Mahakama hiyo, Fatou Bensouda anayesimamia kesi hiyo, alisema watuhumiwa wawili waliofikishwa mahakamani hapo jana, Ruto na mtangazaji wa Redio, Joshua arap Sang wanakabiliwa na mashtaka matatu kila mmoja, ambayo ni kuwalazimisha watu kukimbia makazi yao, mauaji na kuchochea ghasia.
 
 
Kesi hiyo imeanza kusikilizwa siku chache baada ya Bunge la Kenya kupiga kura kutaka nchi hiyo ijitoe uanachama wa ICC, wakieleza kwamba imekuwa haina tija na inatumiwa kuwakandamiza Waafrika.
 
 
Ruto ambaye alionekana kujiamini alifika kwenye jengo la Mahakama akiwa ameambatana na baadhi ya wabunge waliosafiri kutoka Kenya hadi The Hague kwa ajili ya kumuunga mkono.
 
 
Mwendesha Mashtaka wa ICC, Fatou Bensouda alianza kwa kusoma mashtaka matatu yanayomkabili kiongozi huyo wa Kenya na akaiomba Mahakama hiyo kumtia hatiani kutokana na vurugu zilizojitokeza baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007.
 
 
Akiwasilisha hoja ya mashtaka, Bensouda alisema kuwa Ruto ni mwanasiasa aliyejawa na kiu ya madaraka na wakati fulani aliitii kiu yake kwa gharama ya maisha ya wengine. 

Alieleza kuwa Ruto alianzisha machafuko alipoona shabaha yake kutwaa madaraka kwa njia ya kura kushindwa.
 
 
“Ruto alikuwa mwanasiasa mwenye nguvu sana ambaye alikuwa tayari kuratibu uhalifu dhidi ya binadamu ili kukidhi matakwa yake ya kutwaa madaraka.
 
 
"Ni vigumu sana kutathmini maumivu na mateso waliyoyapata wanaume, wanawake na watoto ambao baadhi yao walichomwa moto huku macho yao yakishuhudia kile kilichotendeka. 


"Wengi waliteswa hadi kufa huku wengine wakitimuliwa kutoka kwenye nyumba zao na kwenda kuishi uhamishoni,” alisema Bensouda katika sehemu ya hoja zilizowasilishwa na upande wa walalamikaji.
 
 
Akieleza zaidi mahakamani hapo, Bensouda alisema kuwa Ruto na wenzake waliapa kutwaa madaraka kwa njia yoyote na walipoona jaribio lao kwa kuingia Ikulu kwa njia ya kura limeshindikana walianzisha hila kwa kuchochea machafuko ya kikabila.
 
 
Alisema upande wa walalamikaji uko tayari kuthibitisha madai kwamba Ruto alihusika kuandaa mashambulizi dhidi ya wananchi wa kabila la Kikuyu.
 
 
“Tupo tayari kudhibitisha madai yetu pasipo na shaka yoyote kwamba mashambulizi ya Wakikuyu yaliratibiwa na kutekelezwa na wahusika hawa,” alisema Bensouda.
 
 
Wakati Bensouda akiendelea kuwasilisha ushahidi upande wa pili, Ruto alionekana kuwa mtulivu na wakati fulani alitikisa kichwa na kisha akanyanyua glasi ya maji na kunywa. Kuna wakati pia alitabasamu na kuendelea kufuatilia kwa makini ushahidi wa upande wa walalamika.

Ruto akana mashtaka
“ Sasa Ruto ni fursa yako kusimama na kujitetea kuhusiana na mashtaka yaliyopo mbele yako,” alisema mmoja wa majaji kwenye kesi hiyo. Wakati aliposimama Ruto hakuwa na maneno mengi mbali ya kurudia maneno yake mara tatu “Sina hatia, sina hatia, sina hatia”.
 
Ilipowadia zamu ya utetezi wa upande wa washtakiwa, Mwanasheria wa Ruto, Karim Khan alikosoa vikali maelezo ya walalamikaji aliyoyaita kuwa ni “uzushi” na baadhi ya washahidi walirubuniwa kwa fedha ili kutoa ushahidi wa uwongo.
 
“ Waheshimiwa majaji, najua haki ni muhimu itendeke, lakini katika hili hakuna ukweli wowote. Sehemu kubwa ya ushahidi uliotolewa na walalamikaji na hapa singependa nimlalamikie Bensouda kwani ushahidi huu ulikusanywa na mtangulizi wake Ocampo…hakuna ukweli wowote.
 
“ Ushahidi huu umekusanywa bila ya kuwepo mwongozo wa Mahakama hii waheshimiwa majaji… tena napenda nithibitishe hapa, Ruto ni mwanasiasa mwadilifu tena mtu safi aliyeletwa kwenye Mahakama hii kwa makosa,” alisisitiza Khan katika sehemu ya ushahidi wake.
 
Ili kuonyesha msisitizo wa hoja zake, Mwanasheria Khan alilazimika kutumia sehemu ya mahojiano yaliyofanywa baina ya Ruto na Mtangazaji wa K24 Jeff Koinange.
 
Inakariwa kuwa zaidi ya watu 1,200 walipoteza maisha wakati wa machafuko hayo ya baada ya uchaguzi na wengine 600,000 walifurumishwa toka sehemu zao na kwenda kuishi maeneo ya mbali kwa kuhofia usalama wa maisha.
Taarifa za hivi karibuni zinasema kuwa zaidi ya watu 40,000 bado wanaendelea kuishi kwenye makambi kutokana na makazi yao kuharibiwa.
 
Hata hivyo serikali ya Rais Uhuru Kenyatta wiki iliyopita ilisema kuwa hadi ifikapo Septemba 20 mwaka huu kambi hizo zitakuwa zimefungwa na wahusika wake watapatiwa msaada wa fedha ili kujenga nyuma mpya.
 
Baadhi ya mlolongo wa matukio muhimu kabla ya machafuko na baada ya machafuko hayo
 
• Rais Mwai Kibaki alitangazwa mshindi wa uchaguzi wa mwezi Desemba 2007 huku mpinzani wake Raila Odinga aliyalalamikia matokeo hayo

• Vuguvugu la upinzani lilianza rasmi na kufuatiwa na machafuko yaliyosambaa nchi nzima. Vikosi vya polisi vilikabiliana vikali na makundi ya waandamanaji.
 
• Kiasi cha watu 1,200 waliuawa na wengine 600,000 walikimbia nyuma zao
 
• Uhuru Kenyatta aliyekuwa kwenye kambi ya Kibaki alishutumiwa kwa kuchochea mapigano dhidi ya wafuasi wa Odinga.
 
• William Ruto aliyekuwa kwenye kambi ya Odinga alilalamikiwa kwa kuchochea mapigano dhidi ya wafuasi wa Kibaki
 
• Kilianzishwa majadiliano ya kusaka amani na baadaye April 2008 mkataba kugawana madaraka ulisainiwa kutokana na majadiliano yaliyoendeshwa na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa cKofi Annan
 
• Machi 23, 2013 Kenyatta na Ruto waliungana na kufanikiwa kushinda uchaguzi mkuu
 
• Septemba 10, kesi dhidi ya Ruto ilianza rasmi wakati kesi dhidi ya Kenyatta akitazamiwa kuanza Novemba
 
Macho yake yanapepesa kwa umbali mfupi na kisha anaelekea moja kwa moja katika chumba maalumu ambacho kimefurika wataalamu wa sheria.

-Mwananchi

Ndugai na Mbowe walivunja kanuni za Bunge MAKUSUDI kwa maslahi ya vyama vyao.....

Kumekuwa na mjadala mkali kuhusu iwapo Naibu Spika, Job Ndugai alikiuka Kanuni za Bunge katika kushughulikia vurugu zilizotokea Bungeni Alhamisi iliyopita kwa kuamuru kutolewa nje kwa Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe. 


Ndugai ambaye alikuwa kiongozi wa shughuli za Bunge siku hiyo, aliwaamuru askari kumtoa nje Mbowe baada ya kukaidi amri yake ya kutaka kuketi chini aliposimama kutaka kupewa nafasi ya kuzungumza, hali iliyozua tafrani bungeni.
 
 
Pamoja na mambo mengine Ndugai amekuwa akituhumiwa kwamba anaminya uhuru wa wabunge wa upinzani kutokana na mapenzi aliyonayo kwa chama chake, CCM.
 
 
Kwa upande mwingine, kumekuwa na lawama kwamba Mbowe alikosea kukaidi amri ya Naibu Spika kwa kuwa kanuni zinamtaka mbunge yeyote (hata akiwa waziri), kuketi pale kiongozi wa Bunge (Spika, Naibu au Mwenyekiti) anaposimama, hivyo kusababisha mtafaruku.
 
 
Mwenyekiti wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar, Profesa Chris Peter Maina alisema tatizo lililojitokeza bungeni linaweza kumalizwa na kuwapo kwa sheria inayokataza Spika wa Bunge kuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa.
 
 
“Unajua kwa Katiba ya sasa Spika wa Bunge anaweza kuwa mwadilifu lakini akapata shinikizo kutoka upande wa chama chake, Ibara ya 128 ya Rasimu ya Katiba Mpya inaeleza kiundani kuhusu spika kutokutoka miongoni mwa wabunge jambo ambalo ni zuri,” alisema Profesa Maina na kuongeza:
 
 
“Mwenendo wa Bunge siyo mzuri. Wabunge hawaheshimiani hata kidogo, nadhani wanahitaji kukubaliana kwa hoja, wao ndiyo wanatunga sheria, hivyo wanatakiwa kulumbana kwa kufuata utaratibu uliowekwa.”
 
 
Spika wa zamani, Pius Msekwa alisema wakati akiongoza Bunge hakuwahi kuona vurugu, fujo na malumbano ya wabunge kama ilivyotokea Alhamisi iliyopita.
 
 
“Wakati nikiwa Spika sikumbuki kama kuna siku ziliwahi kutokea vurugu za aina hii, kilichotokea ni sawa na uhalifu kwa sababu taratibu hazikufuatwa,” alisema Msekwa.
 

Matakwa ya Kanuni
 
Ibara ya 76 (1) na (2) ya Kanuni za Bunge Toleo la Aprili 2013, zinaeleza jinsi ya kudhibiti fujo bungeni, lakini Ndugai anakosolewa kwamba hakuzingatia taratibu hizo kushughulikia vurugu za Alhamisi.
 
 
Kanuni ya 76 (1) inasema: “Kwa madhumuni ya kudhibiti fujo endapo itatokea ndani ya Ukumbi wa Bunge na Spika ataona kuwa kuna haja ya kutumia nguvu, basi anaweza kuahirisha shughuli za Bunge bila ya hoja yoyote kutolewa au kusitisha kikao kwa muda atakaoutaja ili fujo hiyo iweze kudhibitiwa na Mpambe wa Bunge”.

Kadhalika, fasili ya pili ya Kanuni hiyo inasema: “Baada ya utulivu kurudia, Spika atalipeleka kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge suala ambalo lilisababisha kutokea kwa fujo ikiwa ni pamoja na jina la mbunge au majina ya wabunge waliohusika na fujo hiyo ili kamati hiyo iweze kulishauri Bunge kuhusu adhabu inayostahili kutolewa”.
 
Wakati vurugu zilipozuka bungeni, Ndugai aliwaita askari badala ya mpambe, kumtoa nje Mbowe na hakuwa amesitisha wala kuahirisha shughuli za Bunge kama kanuni zinavyotaka.
 
Pia Naibu Spika alitangaza kumsamehe Mbowe na Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ kwa maana ya kuwaruhusu kuendelea na vikao vya Bunge siku hiyo jioni, badala ya suala hilo kupelekwa kwenye kamati husika kama kanuni ya 76 (2) inavyoelekeza.
 
Utetezi wa Ndugai
Ndugai alisema hakuzingatia kanuni hizo kwani mazingira ya vurugu hizo hayaendani na kanuni husika, hivyo alitumia nafasi yake ambayo pia inatambuliwa na kanuni za Bunge.
 
“Vurugu zilikuwa zimepangwa na zilifanywa kwa makusudi ili kuhakikisha kwamba shughuli za Bunge zinakwama maana hiyo kanuni wanafahamu kwamba ipo, sasa hatuwezi kuwa na Bunge ambalo mtu akiamua tu anafanya fujo ili liahirishwe,” alisema Ndugai na kuongeza:
 
“Mimi kama kiongozi wa shughuli za siku hiyo, kazi yangu ni kuhakikisha kwamba shughuli zilizopangwa zinafanyika, kwa hiyo nisingeweza kuruhusu watu wachache watukwamishe kutokana na masilahi yao.”
 
Alipoulizwa kwamba alifahamu vipi kuwapo kwa njama hizo, alisema kauli na matendo ya wabunge wa upinzani vilionekana tangu mwanzo wa mjadala kutaka kukwamisha shughuli za Bunge siku hiyo.
 
Kuhusu kuwatangazia wabunge hao msamaha badala ya kupeleka suala hilo kwenye kamati husika, Ndugai alisema: “Hakukuwa na adhabu kubwa ya kuwapa zaidi ya kuwatangazia msamaha.”
 
“Niliwasamehe kwa mujibu wa kanuni maana zinaruhusu kuzingatia uamuzi ambao uliwahi kutolewa na maspika waliopita, kwa hiyo kama unakumbuka kesi ya Mengi (Regnald) na Malima (Adam), Spika Samuel Sitta baada ya kumwita Malima akakataa kwenda alisema anamsamehe,” alisema na kuongeza:

“Yeye (Sitta) alitumia neno kwamba nimeamua kumpuuza lakini mimi sikusema hivyo, nilisema kwamba namsamehe kwa sababu tu namheshimu na ni kiongozi mkubwa tu katika jamii”.
 
Lissu amtetea Mbowe
Mbowe hakupatikana juzi na jana kuzungumzia suala hilo, lakini Mnadhimu Mkuu wa Upinzani Bungeni, Tundu Lissu alisema kiongozi wake huyo hakufanya makosa kwani alisimama wakati Mbunge wa Vunjo (TLP), Augustine Mrema alipokuwa akizungumza na kwamba hilo siyo kosa kikanuni.
 
Alisema Ndugai alipaswa kumheshimu Mbowe kwa kuzingatia wadhifa wake bungeni na kwamba kitendo cha kumwambia “kaa chini” hakikubaliki.
 
“Hatuwezi kuruhusu na hatutaruhusu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kudhalilishwa, ikiwa tutaruhusu hilo litokee, basi miongoni mwetu sisi wapinzani hakuna atakayepona,” alisema Lissu na kuongeza:
 
“Naibu Spika amelidhalilisha Bunge kwa sababu kwa kumdharau Mbowe ni kwamba amemdharau mmoja wa viongozi wakuu wa Bunge”.

-Mwananchi

"CHADEMA wamepewa mamilioni ya fedha na wazungu ili wakwamishe mchakato wa katiba mpya"..Nape Nnauye

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimeibua madai mazito dhidi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kuwa kimepewa mamilioni ya fedha kutoka nje ya nchi, kwa nia ya kukwamisha mchakato wa Katiba Mpya.

 CCM kimeibua tuhuma hizo, ikiwa ni siku chache baada ya wabunge wa upinzani kupigana ngumi na askari wa Bunge muda mfupi baada ya kupitisha hoja ya kujadili Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba.

Wabunge wa upinzani wanapinga sheria hiyo, kwa madai kuwa Zanzibar haikushirikishwa.

Akihutubia mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika jana wilayani Kahama, Katibu wa Halmashauri Kuu, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, alisema kinachowasumbua Chadema hadi kufikia hatua hiyo ni mamilioni ya fedha waliyopewa kutoka nje ya nchi.

“Wenzetu hawa nasikia wamepewa mamilioni toka nje, kwa kisingizio cha kushiriki mchakato wa Katiba na kama ilivyo kwa vibaraka wengine katika bara la Afrika, lengo la fedha hizo si kuwawezesha kushiriki bali kuanzisha fujo na vurugu ili mchakato usimalizike salama kupata ajenda mwaka 2015, kwani kimsingi hawana mpya.

Nape alidai kuwa mara baada ya rasimu ya kwanza kutoka, Katibu Mkuu wao alikwenda nje ya nchi na kukaa kwa muda na kabla ya kurejea ndipo Chadema wakapanga kuanza kuzunguka na helikopta na hivyo kutaka waseme fedha hizo walikozipata.

“Walichokifanya Chadema bungeni walipanga katika mkakati wao wa 'civil disobedience' ...machafuko ya umma dhidi ya dola, mkakati ambao unaratibiwa kutoka nje na baadhi ya wale waliokuwa wakoloni katika nchi zetu za Afrika,” alisema Nape.

Naye, Katibu Mkuu wa (CCM), Abdulrahman Kinana, alisema chama hicho kimekuwa kikitumia njia ya mkato ili kutafuta madaraka ya lazima kwa Watanzania pamoja na kushindwa kuonyesha lengo katika mchakato wa uundwaji wa Katiba Mpya.

Kutokana na tuhuma hizo, gazeti hili lilimtafuta Msemaji wa Chadema, Tumaini Makene ambaye alisema imekuwa ni desturi ya CCM hasa Nape, kukituhumu chama hicho pamoja na kudai kuwa ana ushahidi wa mamilioni ya shilingi ambayo anashindwa kuthibitisha.

“Tuhuma kama hizo aliwahi kuzitoa awali, watoe ushahidi wa fedha zilikotolewa mbona anatuhumu tu? Serikali kama kiasi kikubwa cha fedha kinapitishwa na inashindwa kuchukua hatua za kudhibiti, basi ni mfu,” alisema Makene.


-Mtanzania 

Tuesday, September 10

Taharuki kubwa yaibuka katika mpaka wa Rwanda na Tanzania.


Taharuki imeibuka katika mpaka wa Tanzania na Rwanda wakati madereva wa malori kutoka nchini wakihaha kuvuka kuingia Rwanda kabla ya kuanza kutumika kwa ushuru mpya wa barabara ambao unaanza kutumika tena leo kwa upande wa Rwanda ukilenga magari kutoka Tanzania tu.  

Rwanda iliongeza ushuru kwa zaidi asilimia 229 dhidi ya magari ya mizigo ya Tanzania tu kutoka viwango vya zamani vya Dola za Marekani 152 hadi Dola 500 kwa madai ya kutaka usawa na Tanzania. 
Ushuru huo ambao ulianza kutumika rasmi Septemba mosi mwaka huu kisha kusitishwa kwa muda, unatarajiwa kurejeshwa tena leo kulingana na tangazo la Rwanda mpakani Rusumo. 


Kadhia hiyo imesababisha msururu mrefu wa malori yanayoingia Rwanda kutoka Tanzania kuanzia jana ambayo ilikuwa siku ya mwisho kabla ushuri huo wa kutoka Dola za Marekani 152 hadi 500 kuanza kutozwa tena kuanzia leo. 


Kaimu Ofisa Mwandamizi wa Forodha wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) katika kituo cha Rusumo, Sure Mohamed, jana alilithibitisha NIPASHE kwamba wiki moja iliyopita serikali ya Rwanda iliweka ongezeko la ghafla la ushuru wa barabara kutoka Dola 152 hadi Dola 500 za Marekani. 
  
Alisema hali hiyo ilisababisha msururu mrefu wa magari umbali wa zaidi ya kilometa 20 kwa kuwa madereva wengi hawakuwa na taarifa za ongezeko hilo, hali iliyowalazimu kuwasiliana na waajiri wao ili wawatumie fedha za ziada. 

Hata hivyo, alisema ongezeko hilo la ushuru lililodumu kwa takribani wiki moja inakadiriwa magari zaidi ya 200 yalitozwa ushuru mpya wa Dola 500 kabla serikali ya Tanzania kufanya mazungumzo na serikali ya Rwanda na kufikia mwafaka wa kurejesha ushuru wa zamani wa Dola 152. 
 
Alisema ingawa serikali ya Rwanda ilikubali kurejesha ushuru wa zamani, lakini baadaye iliweka bango mpakani upande wake lililosema tozo hiyo ya zamani ingedumu hadi jana na baada ya hapo malori yatatakiwa kulipa Dola 500.“Ni kweli kulitokea ongezeko la ghafla la road toll (ushuru wa barabara) kwa upande wa wenzetu kutoka Dola 152 hadi Dola 500. 
 
Tulipouliza kwa nini wamefanya hivyo tena ghafla, walidai wanataka kuwa na kiwango sawa na cha kwetu,” alisema. 
Aliongeza kwamba kimsingi, madai hayo ya Rwanda kwamba wanataka kuwa na kiwango cha tozo sawa na cha Tanzania hayana ukweli wowote kwa sababu hapa nchini ushuru wa barabara unatozwa kulingana na umbali ambao gari linasafiri. 
 
“Sisi hapa nchini tunatoza ushuru wa barabara kwa kuangalia kilometa, hiyo Dola 500 wanayodai tunatoza ni umbali wa kutoka hapa Rusumo hadi Dar es Salaam ambao ni zaidi ya kilometa 1,800,” alisema Mohamed. 


Aliongeza kwamba kwa magari yanayoishia Isaka wilayani Kahama yanayotozwa Dola 110 tu, tofauti na Rwanda ambao wao kiwango chao ni kimoja hata kama gari litasafiri umbali wa nusu kilometa. 


DC NGARA ANENA
  Mkuu wa Wilaya ya Ngara, Constantine Kanyasu, alithibitisha serikali ya Rwanda kuongeza ushuru wa barabara kutoka Dola 152 hadi Dola 500 na kwamba baada ya mazungumzo na serikali ya Tanzania walikubali kurejesha kiwango cha zamani, lakini kwa muda tu. 
 
“Baada ya kufanya nao mazungumzo kuhusu uamuzi wao wa kupandisha ushuru wa barabara, walikubali kurejesha kiwango cha zamani, lakini wakasema wanafanya hivyo kwa muda tu ili kuruhusu magari yaliyokuwa tayari yamepakia mizigo Dar es Salaam hadi Septemba 9, hivyo tunasubiri kuona hiyo kesho (leo) kama watarejesha tozo mpya au wataendelea na tozo ya zamani,” alisema. 

Hata hivyo, Kanyasu alisema Tanzania ina mtandao mrefu wa barabara wa karibu kilometa 2,000 na ndiyo sababu tozo inafikia hadi Dola 500, lakini Rwanda ina mtandao wa barabara usiozidi kilometa 300, hivyo madai yao ya kupandisha ushuru wa barabara hauna maelezo ya kuridhisha. 
  
KAULI ZA MADEREVA  
Baadhi ya madereva wa malori ya mizigo waliozungumza na NIPASHE wakati wakisubiri kuvuka kuingia Rwanda walisema ingawa hawana uwezo wa kuzuia ongezeko la ushuru, lakini pia hawaoni kama lina tija hususani kwa wananchi wa Rwanda. 
  
Kassim Salum anayeendesha lori la mizigo la kampuni ya Bhanji Logistics ya jijini Dar es Salaam, alisema ameshangazwa na ongezeko hilo kwa upande wa Rwanda kwa sababu kwa upande wa Burundi kiwango ni kile kile cha Dola 152. 
 
“Kimsingi, hakuna tofauti kubwa ya kijiografia kati ya Rwanda na Burundi, lakini tumeshangaa kusikia kwamba Rwanda wanakusudia kupandisha ushuru kutoka Dola 152 hadi Dola 500 wakati wenzao wa Burundi kiwango ni kile kile na hakuna usumbufu wowote,” alisema. 
 
Aliongeza kwamba kama Rwanda wataendelea na msimamo wao ni wazi watakaoathirika ni wananchi wake kwa sababu wenye magari wataongeza gharama za usafirishaji na wafanyabiashara wataongeza bei ya bidhaa, hivyo atakayeathirika ni mlaji wa mwisho ambaye ni mwananchi wa Rwanda. 
  
John Nzigila, anayeendesha lori la Kampuni ya Mafuta ya Eafco, alisema alifika katika mpaka wa Rusumo juzi na kukuta foleni kubwa. 
  
Alisema pengine foleni hiyo ilitokana na malori mengi kutaka kuwahi kuvuka kuingia Rwanda kabla ya jana ambayo ilikuwa siku ya mwisho ya kutozwa kiwango cha zamani cha ushuru. 
  
“Mimi nimeingia hapa jana (juzi) na nililazimika kulipia hiyo hiyo jana (juzi) ili kuepuka kulipa tozo mpya ambayo tuliambiwa inaanza kesho,” alisema Nzigila. 
 
Naye Zuberi Denya anayeendesha lori la mizigo la Kampuni ya Kleb ya jijini Dar es Salaam, alisema serikali ya Rwanda ina uhuru wa kuongeza ushuru kadri itakavyoona inafaa, lakini haoni kama kulikuwa na sababu yoyote ya msingi ya kufanya hivyo hivi sasa. 
 
“Unajua katika siku za karibuni kumekuwapo na mgongano wa kisiasa kati ya Tanzania na Rwanda, hivyo hatuwezi kuhusisha moja kwa moja ongezeko la ushuru na mgongano huo, lakini tunajiuliza kwa nini wafanye hivyo sasa hivi baada ya Tanzania kuwataka wahamiaji haramu kurejea kwao?” 
 
NIPASHE ambalo limefika eneo la Rusumo kwenye mpaka wa Tanzania na Rwanda jana lilishuhudia msururu mrefu wa malori yakisubiri kuvuka mpaka huku baadhi ya madereva wakijaribu kuvunja utaratibu na kuchepuka foleni kwa lengo la kutaka kuwahi. 
  
KAULI YA WAZIRI MGIMWA  
Waziri wa Fedha, Dk. William Mgimwa, jana aliliambia NIPASHE kuwa amesikia habari hizo, lakini alisema mazungumzo kuhusiana na suala hilo kati ya Tanzania na Rwanda yanaendelea. 
 
Dk. Mgimwa alisema kesho atakutana na waziri mwenzake wa Fedha wa Rwanda jijini Kampala, Uganda kuzungumzia suala hilo. 
  
Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, hakupatikana jana kuzungumzia suala hilo kwani simu zake zilikuwa zimefungwa. 

  
Hata hivyo, Naibu wake, Dk. Charles Tizeba, alipoulizwa jana, alisema asingeweza kulizungumzia suala hilo kwa kuwa alikuwa katika ziara ya Rais Jakaya Kikwete mkoani Mwanza na kushauri aulizwe Waziri Mwakyembe. 
  
TATOA YATANGAZA MSIMAMO  
Naye Msemaji wa Chama cha Wamiliki wa Malori Tanzania (Tatoa), Elias Lukumay, alisema msimamo wao uko pale pale kwamba hawatakuwa tayari kulipa nyongeza ya ushuru. 

Lukumay alisema wataendelea kusimamisha magari mpakani mpaka pale mawaziri wawili wa fedha watakapokutana na kufikia mwafaka. 
  
Septemba 3, mwaka huu, Serikali ya Tanzania ilisema mgogoro wa ushuru mpakani kati ya wafanyabiashara wa Tanzania na Rwanda kwa sasa umemalizika. 


Hayo yalisemwa na Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk. Charles Tzeba, na kusema kuwa wafanyabiashara wa Kitanzania walisumbuliwa baada ya kulazimika kulipa Dola 500 za Marekani ili kuingiza mizigo yao Rwanda. 
  
Alisema baada ya kutokea tatizo hilo, alimpigia simu Waziri wa Uchukuzi wa Rwanda, Profesa Silas Lwakabamba, ambaye alisema hana taarifa juu ya taarifa hizo na kuwasiliana na Waziri wa Fedha wa Rwanda ambaye alimpa taarifa kuhusiana na suala hilo. 
  
Hata hivyo, Tzeba alikanusha madai ya kupandishwa ushuru huo kutokana na mgogoro wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Rwanda. 


Alisema walipata taarifa zisizo rasmi kuwa Rwanda ingepandisha gharama za ushuru kuanzia mwanzoni mwa mwezi huu na kwamba walikuwa wakisubiri taarifa rasmi. 

Hata hivyo, alisema taarifa hizo zilikuwa na ukweli kwani Septemba Mosi, mwaka huu alipigiwa simu kutoka mpakani kuwa magari ya Tanzania yamezuiwa eneo la Rusumo na wanatakiwa walipe Dola 500. 
 
Tzeba alisema baada ya kuwasiliana na Profesa Lwakatamba walikubaliana kuwa suala hilo litafanyiwa kazi na mawaziri wa fedha wa nchi hizo mbili.

- Nipashe.