Tuesday, September 12

Mtoto wa msichana wa miaka 13 afariki dunia India

Watu wataka haki itekelezwe kwa watoto wabaonajisiwaHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionWatu wataka haki itekelezwe kwa watoto wabaonajisiwa
Mtoto wa msichana wa miaka 13 raia wa India ambaye alinajisiwa na kushika mimba lakini baadaye akaruhusiwa kuitoa mimba hiyo, amefariki siku mbili baada ya kutolewa kwenye mji wa uzazi wa msichana huyo.
Mtoto huyo, aliyetolewa kwa njia ya upasuaji, amekuwa katika chumba cha kuwatunza watoto wachanga walio katika hali mahututi huko Mumbai na alifariki siku ya Jumapili.
Msichana huyo ambaye alikuwa mimba ya wiki 32, alijifungua mtoto mwanamume kupitia njia ya upasuaji siku ya Ijumaa, hospitali hiyo imesema.
Mwanamume anayefanya kazi na babake, amekatwa kwa kutekeleza ubakaji huo.
India kwa kawaida inaruhusu utoaji wa mimba baada ya wiki 20 na iwapo tu maisha ya mama yamo hatarini.
Kesi hiyo iligonga vichwa vya habari baada ya mimba yake kugundulika mwezi Agosti 9 pale wazazi wake walipompeleka kwa daktari kupokea matibabu kutokana na ongezeko la uzani kupita kiasi.
Wakili ambaye makao yake ni mjini Delhi alifika mbele ya mahakama kuu kumuwakilisha, akitaka msichana huyo aruhusiwe kumtoa mtoto huyo.
Katika uamuzi wa mahakama ambao hautasahaulika, korti hiyo ilimpatia ruhusa siku ya Jumatano kupata usaidizi wa madaktari kutoa mimba hiyo.
Madaktari hao walikuwa wamesema asubiri kwa wiki mbili zaidi ili kupatia kijusi muda kukua zaidi lakini majaji waliamrisha utoaji wa mimba hiyo ufanyike kwa haraka ili kumsaidia msichana huyo kuepukana na mshtuko.
Kikosi cha madaktari watano, wakiongozwa na daktari wa watoto Dkt Ashok Anand , walifanya upasuaji huo katika hospitali ya JJ huko Mumbai.
Kwa kuwa mimba yake ilikuwa katika kiwango cha juu, utoaji wa mimba hiyo ulisababisha kuzaliwa kwa mtoto huyo wa kiume, Dkt Anand aliambia BBC siku ya Jumatatu.
''Msichana huyo anaendelea kupata afueni na atatolewa hospitalini katika siku zijazo.''
Daktari huyo alisema mtoto huyo mvulana alizaliwa na uzani mdogo wa kilo 1.8(41b).
Haijabainika kilichosababisha kifo cha mtoto huyo, lakini ripoti kutoka gazeti la Times of India limewanukuu madaktari waliosema mtoto huyo alikuwa na matatizo ya mapafu na shida kubwa ya uvutaji wa pumzi.
Watoto wa India wanaonajisiwa wanaomba haki yao.Haki miliki ya pichaAFP
Image captionWatoto wa India wanaonajisiwa wanaomba haki yao.
Katika ripoti nyengine, gazeti hilo limesema ''familia ya msichana huyo ilionyesha mabadiliko ya kutaka kumlea mtoto huyo.''
Wafanyikazi wa hospitali hiyo waliambia BBC, msichana huyo mwenye umri wa miaka 13 alikuwa amearifiwa kuhusiana na kifo cha mtoto wake na kwa hivi sasa ameonekana kupata afueni.
Mwanahabari wa BBC, Geeta Pandey huko Delhi amesema hiyo ni kesi ya tatu kwa miezi michache iliyopita inayohusiana na ubakaji miongoni mwa watoto wa India ambao walipata uja uzito na kufika mbele ya mahakama kupata ruhusa ya kutoa mimba .
Mwezi uliopita mtoto wa miaka 10 aliyekuwa ambebakwa alijifungua mtoto msichana kaskazini mwa mji wa Chandigarh. Alikuwa na uja uzito wa wiki 32 lakini alinyimwa ruhusa ya kutoa mimba hiyo baada ya kundi la madaktari kusema utoaji wa mimba utakuwa na ''harati kubwa sana.''
Mwezi Mei, kesi sawia na hiyo iliripotiwa kutoka jimbo lililoko kaskazini mwa Haryana ambapo msichana wa miaka 10, anadaiwa kubakwa na babake wa kambo, aliruhusiwa kutoa mimba hiyo na alikuwa na uza uzito wa wiki 20, daktari alisema.
Hatuwezi kutaja majina ya wasichana hao kwa sababu za kisheria.
Kesi hizi zilianza kuangaziwa kuchelewa , kwa sababu watoto wenyewe hawakutambua hali zao wenyewe na wazazi pia hawakutambua dalili za kawaida za mimba kwani hawakuamini kwamba watoto wao wangeweza kupata mimba katika umri mdogo, mwandishi wa BBC mjini Delhi amesema.

Kenyatta: Tutatumia Bunge kumuondoa Odinga madarakani akishinda

Uhuru Kenyatta, 10 March 2013Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionUhuru Kenyatta aliingia madarakani mara ya kwanza 2013,
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amesema mpinzani wake katika uchaguzi mkuu mpya utakaofanyika mwezi ujao akifanikiwa kushinda chama chake kitamuondoa madarakani muda mfupi baadaye kupitia bunge.
Uchaguzi mpya utafanyika tarehe 17 Oktoba baada ya matokeo ya uchaguzi uliofanyika tarehe 8 Agosti kufutiliwa mbali na Mahakama ya Juu.
Rais Kenyatta alikuwa ametangazwa mshindi akiwa na zaidi ya kura 1.4 milioni kumzidi Bw Odinga lakini kiongozi huyo wa muungano wa National Super Alliance (Nasa) alipinga ushindi wake mahakamani.
Kampeni zimekuwa zikishika kasi nchini humo viongozi wa chama cha Jubilee chake Bw Kenyatta na muungano wa Nasa wakijibizana hasa kuhusu Tume ya Uchaguzi (IEBC) ambapo Nasa wanataka tume hiyo ifanyiwe mabadiliko kwanza kabla ya uchaguzi kufanyika.
"Hakuna cha kuogopa kama anavyosema William (Ruto). Hata Raila akichaguliwa, niambie atatawala nchi ya kenya kwa njia gani. Vipi, Jubilee tulivyo sasa. Katika seneti muhula uliopita tulitatizika kwa sababu ya idadi ya wabunge, leo hii tukiwa na maseneta 41, tunaweza kuendesha shughuli seneti bila kuwa na mwanachama hata mmoja wa Nasa. Hatuwahitaji," amesema.
"Leo hii katika Bunge, tukiwa na wabunge zaidi ya mia mbili na ishirini na kitu, tumepungukiwa na wabunge 13 pekee tuwe na wingi wa theluthi mbili, hii ina maana kwamba tunaweza hata kubadilisha katiba bila kuwa na mbunge wa Nasa."
"Atafanya nini, hata mkimpatia kura zote, atafanya nini? Anaweza kufanya nini? Hata akichaguliwa, tuna fursa Bunge, katika kipindi cha miezi miwili mitatu hivi, tumemtoa."
Kwa mujibu wa katiba nchini Kenya, Rais anaweza kuondolewa madarakani iwapo atabainika kutokuwa na uwezo kimwili na kiakili kuongoza.
Anaweza pia kuondolewa madarakani iwapo atakiuka sana katiba au atekeleze makosa ya jinai chini ya sheria za kitaifa au kimataifa.
Muungano wa upinzani Nasa umeshutumu vikali tamko la Bw Kenyatta na kusema halina busara.
"Bwana Uhuru Kenyata/ Jubilee, usijidanganye wewe na Wakenya, hauna idadi ya kutosha ya kumuondoa Raila madarakani au rais yeyote yule. Soma kifungu 145 cha katiba," aliandika Seneta wa Bungoma Moses Wetangula, mmoja wa viongozi wakuu wa Nasa.
Kiongozi mwingine wa muungano huo Musalia Mudavadi ambaye ni makamu wa rais wa zamani pia ameshutumu tamko la Bw Kenyatta.
Bw Odinga baada ya ushindi kortiniHaki miliki ya pichaAFP/GETTY
Image captionBw Odinga
Kando na kutishia kumuondoa madarakani Bw Odinga iwapo atashinda, Rais Kenyatta alipokuwa anahutubu ikulu ameushutumu upinzani kwa kutishia kususia kikao cha kufunguliwa rasmi kwa mabunge yote mawili.
Bw Kenyatta amesema mabunge yote mawili yanaweza kuendelea na shughuli zake bila kutegemea wabunge wa Nasa.

Huduma za jamii zitachukua muda kurejea Florida

MarekaniHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMifumo ya nishati imeharibiwa vibaya
Gavana wa Florida amekuwa akitoa maelezo ya operesheni ya kazi ya misaada inavyofanyika kutokana na hali inayoikabili Marekani baada ya kukumbwa na kimbuga na dhoruba maruufu Irma.
Rick Scott , asema kwamba vipaumbele vya haraka vimeelekezwa katika kusaidia hospitali na kuokoa maisha. Zaidi ya theluthi mbili ya taifa hilo haina nishati ya umeme na bwana Scott amearifu kuwa itachukua wiki kadhaa kurejeshwa kwa ukamilifu wake nishati hiyo.
Moja ya maeneo yaliyoathiriwa vibaya na kimbunga hicho ni maeneo ya pwani ya mji wa Florida yajulikanayo kama vitovu vya Florida na imearifiwa kuwa itachukua muda kwa wakaazi wa maeneo hayo kurejea katika makaazi yao.
Scott anasema Kuna uharibifu mkubwa , nina matumaini kila mtu alinusurika, ni mambo ya kutisha tuliyoyaona.
Ninajua hali ya taifa letu lakini hasa vitovu vya Florida itachukua muda kurejea katika hali yake ya kawaida, kwakweli kuna uharibifu mkubwa .
''Naelewa kuwa watu walio wengi wanataka kurejea katika maisha yao ya kawaida, najua kila mmoja anataka kuanza upya, nawasihi kuwa na subra, mnapaswa kupata msaada wa haraka katika maeneo yenu, tunapaswa kupata maji tena, tunahitaji huduma zote za kijamii zirejee kama kawaida lakini nasema, itachukua muda nrefu!''

Kampuni ya madini ya Petra Diamonds yasitisha uchimbaji mgodini Tanzania

Magufuli amekuwa akisema taifa hilo linafaa kufaidi zaidi kutokana na madiniHaki miliki ya pichaAFP
Image captionMagufuli amekuwa akisema taifa hilo linafaa kufaidi zaidi kutokana na madini
Kampuni ya uchimbaji almasi ya Petra Diamonds imesimamisha shughuli zake za uchimbaji katika mgodi wake uliopo Mwadui Shinyanga, Kaskazini Magharibi mwa Tanzania.
Hii imekuja siku chache tu baada ya kamati za bunge kuwasilisha ripoti zao kwa Rais John Magufuli kufuatia uchunguzi walioufanya katika sekta ya uchimbaji madini ya almasi na tanzanite.
Petra, ambao ndio wachimbaji wakubwa wa almasi nchini Tanzania, wamekuwa wamejikuta kuwa kampuni nyingine ya kigeni kuingia katika mgogoro serikali ya Tanzania katika harakati za kufanya mageuzi katika sekta ya uchimbaji madini nchini humo.
Wiki mbili zilizopita, mamlaka nchini Tanzania ziliripoti kukamatwa kwa vifurushi vya almasi katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere ambavyo vilikuwa ni mali ya Petra na vilikuwa mbioni kusafirishwa kwenda Ubelgiji kuuzwa.
Maafisa wa serikali walisema Petra ilidanganya juu ya kiasi na thamani ya almasi hizo ambapo, wakati kampuni ya Petra ikisema almasi hiyo ilikuwa na thamani ya dola za kimarekani milioni 14.8, uchunguzi wa serikali ulibaini almasi hiyo ilikuwa na thamani ya dola milioni 29.5.
Hata hivyo, Petra imekanusha tuhuma hizo na kusema kwanza wao ni wawazi katika kuripoti thamani ya almasi yake lakini pia ni wakala wa serikali ndio unaokisia na kutoa thamani ya almasi inayochimbwa na kampuni hiyo.
Mwandishi wetu Sammy Awami akiwa Dar es Salaam anasema katika waraka wake leo hii, Petra imesema pia kwamba baadhi ya maafisa wake wa ngazi za juu wanahojiwa na mamlaka nchini Tanzania kuhusiana na sakata hiyo.
Kuhusu kufungwa kwa mgodi wake wa Williamson uliopo Mwadui, Shinyanga, Petra imesema uamuzi huo wameufikia kutokana na sababu za "kiafya na kiusalama" na kwamba wanaendelea kutoa ushirikiano wao kwa serikali ya Tanzania katika uchunguzi wa mkasa unaoendelea hivi sasa.
Serikali ya Tanzania imeendelea na harakati zake za kimapinduzi katika sekta ya madini ikiwa ni sehemu ya mkakati wa Rais Magufuli kuona sekta hiyo inachangia zaidi katika pato la taifa.
Tayari kuna sheria kali ambazo zimewekwa kuhakikisha kwamba sekta ya madini nchini Tanzania inabanwa katika kuchangia zaidi mapato kwa serikali.

Huduma za jamii zitachukua muda kurejea Florida

MarekaniHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMifumo ya nishati imeharibiwa vibaya
Gavana wa Florida amekuwa akitoa maelezo ya operesheni ya kazi ya misaada inavyofanyika kutokana na hali inayoikabili Marekani baada ya kukumbwa na kimbuga na dhoruba maruufu Irma.
Rick Scott , asema kwamba vipaumbele vya haraka vimeelekezwa katika kusaidia hospitali na kuokoa maisha. Zaidi ya theluthi mbili ya taifa hilo haina nishati ya umeme na bwana Scott amearifu kuwa itachukua wiki kadhaa kurejeshwa kwa ukamilifu wake nishati hiyo.
Moja ya maeneo yaliyoathiriwa vibaya na kimbunga hicho ni maeneo ya pwani ya mji wa Florida yajulikanayo kama vitovu vya Florida na imearifiwa kuwa itachukua muda kwa wakaazi wa maeneo hayo kurejea katika makaazi yao.
Scott anasema Kuna uharibifu mkubwa , nina matumaini kila mtu alinusurika, ni mambo ya kutisha tuliyoyaona.
Ninajua hali ya taifa letu lakini hasa vitovu vya Florida itachukua muda kurejea katika hali yake ya kawaida, kwakweli kuna uharibifu mkubwa .
''Naelewa kuwa watu walio wengi wanataka kurejea katika maisha yao ya kawaida, najua kila mmoja anataka kuanza upya, nawasihi kuwa na subra, mnapaswa kupata msaada wa haraka katika maeneo yenu, tunapaswa kupata maji tena, tunahitaji huduma zote za kijamii zirejee kama kawaida lakini nasema, itachukua muda nrefu!''

Uchaguzi Norway unanukia

Norway
Image captionKiongozi mkuu wa upinzani nchini Norway Bi Erna Solberg kutoka katika chama cha Conservatives
Utabiri rasmi kuhusiana na uchaguzi wa bunge la Norway unaonyesha kuwa zinaelekea ukingoni huku vyama viwili vikichuana vikali , kati ya chama kikuu chenye mrengo wa kati kulia na kile cha mrengo wa kushoto.
Muungano wa kihafidhina wa Bi Erna Solberg unawania nafasi ya kurejea madarakani kwa kipindi cha pili.Endapo atafanikiwa atakuwa ni mwanamke wa kwanza kutoka chama cha mrengo wa kulia katika kipindi cha miongo mitatu iliyopita kuchaguliwa katika nafasi ya waziri mkuu.
Chama cha upinzani cha Labour kinaonekana kutetea nafasi yake ipasavyo kama chama kikuu katika bunge la nchi hiyo.
Kampeni za uchuzi huo mkuu zimelenga na kuzungumzia vilivyo suala la kodi, pamoja na kupunguzwa kwa ushuru kwa watunga sera ili kuongeza ukuaji wa uchumi, wakati chama cha Labour chenyewe kimejikita katika ahadi ya kuboresha huduma za umma.
Bi Solberg ametawala katika ushirika na chama cha kupambana na wahamiaji .

Vilipuzi viliyovtegwa Myanmar vyawajeruhi wati wa Rohingya

Azizu Haque in Bangladesh hospital
Image captionMtoto wa kiume wa miaka 15 anayetibiwa huko Bangladesh alipoteza miguu yote miwili
BBC imefanya mazungua na waislamu wa Rohingya waliojeruhiwa baada ya kukanyaga milipuko walipokuwa wakiikimbia Myanmar.
Mtoto wa kiume wa miaka 15 anayetibiwa huko Bangladesh alipoteza miguu yote miwili huku mwanamke mwingine kwenye hospitali hiyo hiyo akisema kuwa alikanyaga kilipuzi baada ya kufyatuliwa risasi.
Eneo hilo liliondolewea vilipuzi miaka ya 1990 lakini taarifa zinasema kuwa Myanmar iliweka vilipuzi vipya, madai yanayokatailiwa na Mynmar.
Zaidi ya watu 300,000 wa jamii ya Rohingya wamekimbia oparesheni mbaya ya kijeshi nchini Myanmar.
Siku ya Jumatau mkuu wa haki za binadamu katika Umoja wa Mataifa Zeid Raad al-Hussein, alisema kuwa oparesheni mbaya ya kijeshi inafanyika akiitaja kuwa mauaji ya kikabila.
Sabequr Nahar
Image captionSabequr Nahar alipoteza miguu yote miwili
Rohingya ambayo ni jamii isiyo na utaifa wowote, wakiwa ni waislamu wachache, wamekumbwa na mateso ya miaka mingi nchini mynmar, ambayo inasema kuwa wao ni wahamiaju haramu.
Waziri mkuu wa Bangladesh Sheik Hasina, anatarajiwa kuzuru moja wa kambi za wakimbizi nchini humo walio Rohingya.
A Rohingya refugee man pulls a child as they walk to the shore after crossing the Bangladesh-Myanmar border by boat through the Bay of Bengal in Shah Porir Dwip, Bangladesh, 10 September 2017Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionZaidi ya watu 300,000 wa jamii ya Rohingya wamekimbia oparesheni mbaya ya kijeshi nchini Myanmar
Alisema kuwa Myanhama ni lazima itatue shida ambazo imejiletea yenyewe.
Ikulu ya White Hosue nchini Marekani imeitaka Myanmar kuheshimu sheria na kuacha kuwahamisha raia.

Mpigapicha ashinda kesi kuhusu 'selfie ya tumbili'

Monkey selfieHaki miliki ya pichaWILDLIFE PERSONALITIES/DAVID J SLATER
Image captionPeta walidai huo alikuwa tumbili jike kwa jina Naruto lakini Bw Slater alidai alikuwa tumbili tofauti
Mpigapicha mmoja ameshinda kesi iliyodumu kwa miaka miwili dhidi ya kundi la kutetea haki za wanyama kuhusu haki za kumiliki picha ambayo ilipigwa na tumbili.
Tumbili kwa jina Naruto alidaiwa kujipiga picha hiyo katika msimu mmoja Indonesia mwaka 2011 alipoichukua kamera iliyokuwa inamilikiwa na David Slater kutoka Monmouthshire.
Majaji nchini Marekani wamesema tumbili huyo hangekabidhiwa haki miliki ya picha hiyo.
Watetezi wa haki za wanyama kutoka kwa kundi la People for the Ethical Treatment of Animals (Peta), ambao walikuwa wamewasilisha kesi hiyo kwa niaba ya tumbili huyo, walisema mnyama huyo anafaa kufaidi kwa njia fulani.
Kesi hiyo ya Peta "kwa niaba ya tumbili" imetupiliwa mbali lakini Bw Slater amekubali kutoa asilimia 25 ya mapato yatakayotokana na picha hiyo siku zijazo.
Kwenye taarifa ya pamoja, Peta na Bw Slater, wamesema mpiga picha huyo atatoa robo ya pesa atakazopata kupitia uuzaji wa selfie za tumbili huyo kwa mashirika ya hisani yaliyosajiliwa "ambayo yamejitolea kulinda maslahi au makazi ya Naruto".
"Kesi hiyo ya Peta ilikuwa imezua mjadala mkubwa kimataifa kuhusu haki za kimsingi za wanyama kwa jumla, na si zaidi kwa jinsi wanavyotumiwa na binadamu kujifaidi," wakili wa Peta, Jeff Kerr amesema.
Bw Slater, kutoka Chepstow, alikuwa amejitetea kwamba anafaa kuimiliki picha hiyo akisema alifanya juhudi sana kabla ya kuipata picha hiyo.
Alisema juhudi zake hazingeweza kulipwa hata kwa kudai hakimiliki pekee.
David Slater na tumbili IndonesiaHaki miliki ya picha©DAVID J SLATER
Image captionDavid Slater amesema ilimchukua siku tatu za 'kazi ngumu' kupata picha hiyo
Bw Slater akijitetea alisema ilimchukua siku tatu za 'kazi ngumu' kupata picha hiyo. Alisema pesa zinazotokana na kutumiwa kwa picha hiyo, aliyoipiga katika kisiwa cha Sulawesi nchini Indonesia mwaka 2011, ni zake.
"Ilinichukua siku tatu za kutoa jasho kupata selfie hii kuhakikisha ninakubalika na kundi la kima kabla yao kunikubali kiwakaribie vya kutosha na kuwaonyesha kamera yangu," Bw Slater aliambia BBC mwaka 2015.
"Tatizo ni kwamba, watu wengine wanajaribu kuiba haki zangu za umiliki na nitapinga hilo."
David Slater
Image captionSlater alikuwa amesema angekuwa taabani kifedha akishindwa kwenye kesi hiyo au aamrishwe kulipa gharama ya kesi
Selfi hiyo ilisambazwa sana kote duniani na mtandaoni.
Waliompinga Slater wanasema hawezi kuwa na hakimiliki ya picha hiyo kwa sababu ilipigwa na mnyama.
Bw Slater amesema yeye ni mhifadhi wa wanyama na mazingira na kwamba kuvuma kwa picha hiyo kumewasaidia sana wanyama Indonesia.
Kesi hiyo ilikuwa imeorodheshwa kama "Naruto v David Slater" lakini kulikuwa pia na mzozo kuhusu utambulisho wa tumbili aliyehusika.
Peta walidai alikuwa tumbili jike kwa jina Naruto lakini naye Bw Slater akadai alikuwa tumbili tofauti wa kiume.
Lakini majaji wa mahakama ya rufaa mjini San Francisco wamekubali hoja za Bw Slater baada ya vuta nikuvute ya miaka miwili mahakamani.
Taarifa ya pamoja ya Peta na Bw Slater imesema kesi hiyo "iliibua masuala muhimu kuhusu kupanuliwa kwa haki za kisheria kwa wanyama, ambao si binadamu".

Monday, September 11

Kikosi maalum chatua Mwadui kuchunguza almasi


Kikosi Maalumu cha upelelezi kinachoundwa na maofisa wa vyombo vya ulinzi na usalama kutoka makao makuu jijini Dar es Salaam tayari kimeanza kazi ya kuchunguza shughuli za uzalishaji na biashara ya madini ya almasi katika mgodi wa Mwadui unaomilikiwa na kampuni ya Williamson Diamonds Limited.
Kutokana na mahojiano yanayoendelea, shughuli za mgodi huo ulioko Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga zimesimama kuanzia juzi kutoa fursa kwa viongozi na watumishi wa vitengo nyeti vinavyosimamia uchimbaji, uthamini na usafirishaji kuhojiwa.
Akizungumza kwa njia ya simu leo Jumatatu asubuhi Agosti 11, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainabu Tellack amethibitisha uwepo wa kikosi kazi hicho mkoani humo na kufafanua kuwa shughuli za mgodi huo zitarejea kama kawaida baada ya mahojiano kukamilika.
“Hawajafunga mgodi; kinachofanyika ni mahojiano na uchunguzi unaofanywa na maofisa wa ngazi za juu kutoka kwenye vyombo vya ulinzi na usalama. Yakikamilika shughuli zitarejea kama kawaida,” amesema Tellack
Licha ya kuthibitisha uwepo wa kikosi kazi hicho mkoani mwake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Simon Haule amesema hawezi kuzungumzia utendaji wake kwa sababu linahusisha na kusimamiwa na maofisa kutoka makao makuu ya jeshi hilo jijini Dar es Salaam.
Bila kutaka kuingia kwa undani kuhusu suala hilo, ofisa uhusiano wa mgodi huo, Joseph Kaasa ameliambia Mwananchi kwa njia ya simu kuwa yuko kituo cha polisi na kuahidi kutoa taarifa atakapokamilisha kulichompeleka kituoni hapo.
Kampuni ya WDL juzi imesitisha kwa muda baadhi ya shughuli za uzalishaji mgodini.
Uongozi wa kampuni hiyo katika taarifa kwa wafanyakazi iliyotolewa juzi Jumamosi kwa tangazo namba 3311 imesema kwa mtazamo wa uchunguzi ulioanzishwa na Serikali na kwa sababu za kiusalama, umeamua kusitisha kwa muda baadhi ya shughuli za uzalishaji katika mgodi.
Taarifa hiyo imesema shughuli ambazo zitaendelea ni za huduma maalumu za ulinzi, tiba, umeme, maji, zimamoto na usafiri unaohitajika katika huduma hizo.
“Huduma za kiutawala zitaendelea kufanya kazi. Tutawajulisha wakati uzalishaji utakaporejea,” imesema .
WDL imesema inasubiri kuachiwa kifurushi namba WI-FY18 cha almasi iliyokuwa ikisafirishwa nje kutoka mgodini.
Hata hivyo, serikali imezuia kusafirishwa kifurushi hicho kwa misingi ambayo haijawasilishwa rasmi kwa uongozi wa kampuni ya WDL isipokuwa kwa taarifa zilizotangazwa na vyombo vya habari vya redio na runinga.
Hatuwezi kutoa maoni yoyote kutokana na matokeo ya uchunguzi huo. Vifurushi vyote vinavyosafirishwa kwa biashara nje hukadiriwa thamani yake hapa mgodini na watumishi wa Tansort (Hiki ni kitengo cha kukadiria thamani ya almasi na vito) ambao wanawakilisha Wizara ya Nishati na Madini. Kifurushi kinaposafirishwa kinapigwa mihuri miliwiili ya vyombo viwili vya serikali.
Sisi kama uongozi hatuna ujuzi wanaotumia tansort wa kukadiria na kuthamini au kukokotoa thamani ya alimasi. Huwa tunapokea hati ya ukadiriaji kutoka tansort ambayo hutumika kukadiria kwa muda malipo ya mrabaha wa serikali. Malipo ya mrabaha yanakamilishwa baada ya kupatiwa matokeo halisi ya zabuni ya wazi ya almasi za WDL (uaminifuunaothibitishwa na tansort) kutoka Wizara ya Nishati ana Madini.
kama mnavyotambua, serikali ni mbia asilimia 25 katika WDL. Tupo kwenye mazungumzo na serikali ili kuafikiana njia ya kufuata.
Tunawashukuru kwa kuendelea kutoa ushirikiano na kuelewa.

Wabunge wa CUF wavurugana bungeni


Wabunge wa CUF wameonekana kuvurugana bungeni kutokana na mgogoro unaoendelea katika chama hicho.
Mvurugano huo umeonekana leo Jumatatu mjini Dodoma baada ya wabunge wanaomuunga mkono Profesa Ibrahim Lipumba ambaye ni Mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kufanya uchaguzi na kumchagua Mbunge wa Mtwara Mjini, Maftaha Nachuma kuwa mwenyekiti wao bungeni.
Naibu Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson ametangaza kuwa Spika wa Bunge, Job Ndugai amepokea barua kutoka kwa Katibu wa CUF, Magdalena Sakaya kuhusu safu hiyo ya uongozi.
Baada ya tangazo hilo, Mbunge wa Malindi, Ally Salehe aliomba mwongozo wa Spika akitaka  kujua ni nani anaamua kuhusu uongozi wa wabunge bungeni kwa sababu wao wameshafanya uchaguzi na kumchagua Mbunge wa Temeke, Abdallah Mtolea kuwa mwenyekiti wao baada ya kufukuzwa kwa wabunge wanane.                       
Pia, amehoji inawezekanaje kuwa na viongozi wawili bila wa kwanza kufutwa.
Akijibu mwongozo huo, Dk Tulia amesema Spika amepokea taarifa ya viongozi hao lakini hajapokea taarifa ya uchaguzi wa upande wa akina Ally Salehe ambao unamuunga mkono Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad.
Amesema watakapopeleka taarifa yao ndipo Spika ataamua.

Waziri Kairuki aagiza watumishi 10 kusimamishwa kazi


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angellah Kairuki ameagiza kusimamishwa kazi watumishi zaidi ya kumi wa halmashauri za wilaya za Gairo na Kilosa.
Uamuzi huo unatokana na kulipwa mshahara hewa kwa aliyekuwa mwalimu wa Shule ya Sekondari Dumila ambaye hayupo kazini tangu mwaka 2009.
Kairuki ametoa agizo hilo alipozungumza na wakuu wa idara katika halmashauri hizo. Amesema ni kosa lisilovumilika mtumishi hayupo kazini tangu 2009 lakini ameendelea kulipwa hadi Agosti.
"Kuanzia leo naagiza waliokua maofisa utumishi, waweka hazina na maofisa elimu sekondari wa halmashauri hizi tangu 2009 watafutwe popote walipo na wasimamishwe kazi kupisha uchunguzi dhidi yao," amesema.
Waziri Kairuki ameagiza vyombo vya usalama kumtafuta mwalimu huyo popote alipo ili kurejesha fedha na afikishwe kwenye vyombo vya sheria.
Awali, ilidaiwa mwalimu huyo aliaga kwenda masomoni katika Chuo cha St. John lakini hakuripoti chuoni.