Sunday, November 5

Walivyokuwa awali, si walivyo sasa


Walivyokuwa sivyo walivyo! Ndivyo unavyoweza kuwaelezea baadhi ya wanasiasa katika vipindi viwili tofauti vyenye misimamo miwili tofauti.
Haieleweki kama tofauti hiyo ya misimamo yao ina uhusiano na nafasi walizokuwa nazo na baadaye kutokuwa nazo, lakini kwa kuwaangalia na kuwasikiliza kwa makini wana misimamo tofauti katika vipindi tofauti.
Mitazamo hiyo imekuwa ikitolewa na makada wa CCM kama katibu wa itikadi na uenezi, Humphrey Polepole na wabunge wake akiwemo Nape Nnauye (Mtama).
Wengine ni waliowahi kuwa mawaziri katika utawala uliopita, Khamis Kagasheki na Profesa Mark Mwandosya.
Polepole, aliyekuwa mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, amekuwa akizua mijadala kutokana na mitazamo yake ya hivi sasa kuhusu suala la Katiba, tofauti na alivyokuwa wakati Bunge la Katiba likiendelea na vikao vyake.
Akiwa nje ya Bunge la Katiba lililokuwa likiendelea na vikao vyake mjini Dodoma, Polepole alipata umaarufu kutokana na kupingana na jinsi lilivyokuwa likiendeshwa, hasa kutokana na kuachana na Rasimu ya Katiba iliyoandaliwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyoongozwa na Jaji Joseph Warioba.
Kasoro hiyo ilionekana hasa katika suala la muundo wa Muungano na tunu za Taifa. Tume ya Warioba, ambayo Polepole alikuwa mjumbe wake, ilipendekeza Muungano wa serikali tatu, lakini Bunge hilo, likiwa na wajumbe wengi kutoka CCM, lilibadilisha na kurejesha serikali mbili.
Polepole aliitwa na vituo vingi vya televisheni kujadili suala hilo, na akapinga kwa nguvu, akisema Rasimu ya Katiba ilibeba maoni ya wananchi.
Lakini sasa amebadilika. Sasa anazungumzia kitu kinaitwa “ukatiba”.
Mara baada ya kuteuliwa kuwa katibu wa uenezi, amekuwa na mawazo mbadala, akisema kwa sasa Tanzania haihitaji Katiba mpya, bali “ukatiba”.
Hoja hii aliibua Oktoba 19, wakati wa uwasilishaji wa maoni ya wananchi waliohojiwa na taasisi ya Twaweza kuhusu mchakato wa Katiba.
Polepole alisema CCM inaamini dhana na uhalisia ambapo kuna ukatiba na katiba na Watanzania kwa mujibu wa Twaweza wana vitu wanapenda kuviona navyo ni ukatiba.
“Ukatiba ni mambo ya jumla, utamaduni, mila, mienendo yetu na mambo fulani fulani tuliyokubaliana. Viongozi wetu wawe wanajua dhamana waliyopewa, wananchi wajue viongozi jukumu lao ni kuwahudumia, kiongozi kuwa na cheo kimoja ili aweze kukimudu,” alisema Polepole.
Mwandishi wa Mwananchi aliyekuwapo eneo hilo, alitaka kufahamu kwa nini hakueleza falsafa hiyo wakati akiwa ndani ya Tume ya Warioba, lakini Polepole hakujibu swali hilo.
Nape
Mtangulizi wake, Nape pia amekuwa akiibua mijadala kutokana na kauli zake za hivi karibuni baada ya kuachwa katika mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri mapema mwaka huu.
Tangu Machi 23 alipovuliwa uwaziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, amekuwa akitumia mitandao ya kijamii kutoa mitazamo yake kwa tungo tata na wakati mwingine kuonekana kama anaunanga uongozi wa CCM.
“Wapinzani si maadui, tushindane kwa hoja,” aliwahi kusema Nape. Kauli hiyo ameitoa wakati wanasiasa wa upinzani wakikamatwa kila mara, wengine kufunguliwa kesi na hata kushambuliwa kwa risasi.
Ndani ya Bunge wamejikuta wakiadhibiwa kwa kuzuiwa kuhudhuria vikao na wakati mwingine kulalamikia kiti kutowatendea haki.
Pia amewahi kusema “uonevu husababisha maumivu ya moyo, maumivu ya moyo hutunga mimba ya chuki, chuki huzaa kisasi na matokeo yake ni mauti” bila ya kufafanua. Ni dhahiri kuwa kwa mazingira hayo ya kisiasa, kauli hiyo haiwezi kuchukuliwa kuwa ya kawaida.
Alimpinga Polepole aliyesema kuwa mwaka 2020, wabunge watakaopewa fursa ya kugombea ni wale wanaoishi kwenye eneo wanalotaka kuwakilisha.
Nape pia alisema: “Huhitaji kuwa mkamilifu kuwavutia wengine. Watavutiwa na wewe kwa jinsi unavyoshughulikia mapungufu yako! Mungu kagawanya kazi, wengine kusifu, wengine kukosoa, wengine yote pamoja! kwanini unakerwa na kuhangaika na mgawanyo wa kazi? acha ushamba.”
Hakufafanua alikuwa akimtumia ujumbe nani, lakini Nape alikuwa mtu anayesema wazi anachokiamini bila ya kutumia kauli tata au mafumbo.
Kagasheki
Mwingine anayeonekana kuwa tofauti ni Kagasheki, ambaye amekuwa nje ya siasa tangu mwaka 2015 baada ya kushindwa ubunge wa Bukoba Mjini.
Mitazamo yake imekuwa ikifikirisha, ikiibua gumzo na hasa alipounga mkono kauli ya Rais mstaafu, Jakaya Kikwete ya Agosti, 2017 kwamba wapinzani wasichukuliwe kama maadui.
“Nimetafakari kauli ya JK kuhusu vyama Afrika, nakiri kiongozi aliobobea katika uongozi, hukabiliana na muziki hata kama hapendi mdundo wake,” aliandika katika akaunti yake mtandaoni akiweka fumbo pia kuhusu hali ya kisiasa nchini.
Pia, Kagasheki aliweka nukuu ya Ibrahim Bin Adham inayosema: ‘’Kama huwezi kuwasaidia watu katika utatuzi wa matatizo yao basi wafariji kwa maneno mazuri na hata kwa tabasamu.”
Profesa Mkumbo, Anna Mghwira
Wengine katika kundi hili ni katibu mkuu wa Wizara ya Maji, Profesa Kitila Mkumbo na mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira ambao wote wameteuliwa na Rais Magufuli wakitoka Chama cha ACT- Wazalendo.
Wawili hao walikuwa miongoni mwa wakosoaji, lakini sasa hawataweza na Profesa Kitila ameamua hadi kujivua uanachama wa ACT Wazalendo.
Akizungumzia hali hiyo, mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine, Dk Charles Kitima alisema chama na Serikali vinapaswa kuwa tayari kupokea mawazo mbadala na kuyafanyia kazi bila ya kuyabeza.
“Watu wawe huru kutoa mawazo yao na mitazamo wanayoona inafaa, lakini tunaweza kujiuliza hayo mawazo yao ni ujenzi wa taifa au maslahi yao binafasi?” alihoji.
“Na je, chama kiko tayari kuyapokea na kuyafanyia kazi?
“Chama kinapaswa kujinoa na kuona dhana ya upinzani si uadui na demokrasia nzuri ni ile inayoruhusu mawazo mbadala.”

Visa, mikasa inayowakuta wakazi wanaopakana na makaburi


Dar es Salaam. Maeneo ya makaburi yanatisha, hasa nyakati za usiku na kuibua imani kuwa huenda mizuka huibuka usiku na kufanya mambo yao.
Hali hiyo ya utulivu na kutokuwa na harakati nyakati hizo, inatumiwa kama fursa na watu wengine; waganga, watambikaji na wengine watafuta bahati-bila kusahau wahalifu.
Wakazi wanaoishi pembeni mwa maeneo hayo ya kuzikia wafu wanaona mengi, kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na gazeti hili katika maeneo mbalimbali.
Lakini ukosefu wa maeneo ya makaburi pia unasababisha adha kwa majirani wa maeneo hayo kwa kuwa nyumba hizo za wafu ‘zinawafuata’ wasipokuwa makini na wachimbaji.
Katika makaburi ya Mbuyuni, Tandika wilayani Temeke, ambako mwandishi alikuta familia ikilinda eneo lao lisigeuzwe kaburi.
“Tunakaa hapa kuwadhibiti hawa wachimba makaburi, bila hivyo unakuta kaburi jipya limechimbwa nje ya nyumba,” anasema Zuhura Hussein ambaye ni mama wa makamu.
Lakini, Hussein, ambaye ameishi eneo hilo tangu mwaka 1985, ameona mengi zaidi ya hayo ya wachimbaji kuvamia maeneo.
“Watu huwa wanakuja wakati mwingine mchana. Wanaoga na wanaacha hapohapo nguo walizoogea, wakati mwingine kaniki, shuka nyekundu na nyeupe,” anasema.
Anasema awali walitishika, lakini sasa wamezoea kwa sababu hilo eneo limekuwa njia na watu wengi wanapita. Pia, anasema wapo wanaokwenda na vichwa vya mbuzi na kondoo na kuvifukia makaburini.
Zuhura anasema wiki iliyopita alikwenda mtu aliyelowa damu akiwa na kichwa cha kondoo mkononi na kila anapokanyaga aliacha matone ya damu na kukifukia makaburini.
“Alivyomaliza kukifukia akaja kuomba maji ya kunawa,” anasema na kwamba walipoumuuliza sababu za kufanya hayo, alisema wanajaribu kuua kesi iliyopo mahakamani.
Zuhura haamini kama wanafanikiwa, lakini anasema “kila mmoja na imani yake. Kwa jinsi watu wanavyomiminika inawezekana wanapata matokeo halisi.”
Mkazi mwingine anayeishi jirani na makaburi ya watoto Temeke, Mohammed Hassan anasema kukithiri kwa vitendo vya ushirikina katika eneo hilo kulisababisha wananchi kukata mti uliokuwepo eneo hilo.
Anasema kulikuwa kukining’inizwa matambara ya rangi nyeupe, nyeusi na nyekundu na kukiwa na karatasi vyeupe zenye maandishi.
“Siogopi labda usiku mara mojamoja kwa sababu nimezaliwa hapa na makaburi nimeyakuta,” anasema.
Hussein anasema mara nyingi usiku wa manane huwa wanahisi mtu akitembea nyuma ya nyumba yao kuelekea makaburini.
Naye Mariamu Ulugulu anayeishi jirani na Zuhura, anasema wamekuwa wakivuta harufu ya ubani na udi uliochomwa.
Naye amekumbana na tishio la eneo lao kuchimbwa kwa ajili ya kuzikia.
“Unaona kaburi hili (anaonyesha kaburi lililopo karibu na nyumba yao). Lilichimbwa tulivyokwenda kumzika baba,” anasema.
“Haya mengi yaliyo jirani yote yalichimbwa tulipoondoka kidogo, hivyo tunalazimika kila tukitoka nyumbani abaki mtu kwa sababu wanaweza kuchimba hata hapa uani.”
Mkazi mwingine, Rapahel Mkotya anayeishi jirani na makaburi ya Mbagala Misheni anasema licha ya uangalizi ulipo bado kuna watu huenda kufanya kafara.
“Utaona wanaoga hapa, wanalala juu ya kaburi wengine wanaelekezwa walale chali, wengine kifudifudi wake kwa waume, ilimradi kila mmoja na lake,” anasema Mkotya.
Utapeli wa kiganga
Lakini pia maeneo ya makaburini hutumiwa kwa utapeli, kwa mujibu wa Mariamu Ulugulu, ambaye anasema wajanja hao hujidai waganga wa dawa za asili.
Huku akicheka anasema: “Mara kadhaa anapita kijana au mtu mzima anakwenda nyuma ya mbuyu, anajivisha nguo nyingi na anavaa kofia kubwa.
“Baada ya muda anapita mtu, mara nyingi ni wanawake. Akikaribia mwanzo wa makaburi eneo hili tulilokaa, anaambiwa kwa sauti ya kukwaruza na kutisha, ‘njoo kinyume nyume. Ndiyo tumesikia shida zako, weka hela hapo chini usigeuke kutazama mizimu. Tutakusaidia, una mitihani mingi umeibeba. Ondoka kwa usawa ulioelekea.”
Mariamu anasema baada ya mteja kuondoka anayesadikiwa kuwa mganga huvaa nguo za kawaida na kuondoka na anapopita nyumbani kwao huwaaga.
Anasema wapo ambao hufika maeneo hayo wakiwa na matenga yenye kuku na huzungumza lugha ambazo anasema hawazielewi na baadaye huyaacha makaburini.
Mariamu anasema wanapoamka asubuhi hukuta matenga matupu na kuku wakiwa wameshachukuliwa.
“Wakati mwingine wanafunga kuku kwenye miti hapa makaburini na baadaye kuku hukata kamba na kukimbilia mtaani,” anasema.
Anasema baadhi ya wanaochimba makaburi huokota kaniki na mashuka mekundu yanayoachwa makaburini, pia wapo ambao huchukua kuku wanaowakuta maeneo hayo.
Makaburi kujaa
Wakazi hao pia wamesema wamekuwa wakishuhudia wachimba makaburi wakivunja mabaki ya miili na kuhamisha ili kuwezesha kuzika maiti nyingine.
“Mara nyingi wanapochimba kaburi hupasua lile la awali, hivyo kwa bahati mbaya siku nyingine wanakuta nywele na mifupa, au wakati mwingine miili inatoa harufu,” anasema Mariamu.
“Hutuonyesha nywele, au huambiana wenyewe kwa wenyewe duh... nywele zinachelewa kuoza na wakati mwingine hutoa mifupa na kuiweka pembeni. Wakimaliza kuchimba kaburi jipya, huichimbia pembeni na kuifukia upya.
“Kuna kijana alikuwa anapita njia aliwahi kuokota mfupa wa mguu kuanzia gotini hadi kwenye nyayo na kusema anakwenda kuupamba ndani kwake kama fenicha.”
Makaburi kugezwa dampo
Jirani mwingine wa maeneo ya makaburi ya Kwa Kindale, Mtoni Mtongani anayeitwa Monica Lazaro anasema makaburi hayo yanawapa tabu ya kuzoa taka kila siku kutokana na kugeuzwa jalala.
Anasema wauza samaki na mizoga ya aina mbalimbali huitupa eneo hilo, hivyo kuwalazimu kuifukia ili kuepuka harufu.
Monica anasema pia wanaotumia dawa za kulevya hutumia makaburi hayo kujificha.
“Mara nyingi wanakuwa kule mwisho wa makaburi wakijichoma sindano na kusinzia kutwa nzima,” anasema Monica.
Anasema kulikuwa na mchimba kaburi aliyeitwa Kimwaki ambaye kila alipochimba na kukuta mifupa ya binadamu alituita kutuonyesha.
“Tulikuwa tunamkimbia. Mnaweza kwenda hadi mtaa wa pili kukaa kwa woga,” alisema.
“Akishatutisha ndiyo anaitenganisha na kuiweka pembeni kabla ya kuchimba shimo dogo pembeni ya hilo kaburi la awali na kuizika. Tulikuwa tunaogopa hadi tukazoea. Akianza kuchimba kaburi juu ya la zamani kila mtu anaingia ndani.”
Makaburi kuwa gesti
Mkazi aliyejitambulisha kwa jina la Nasra, ambaye madirisha ya nyumba yake yanapakana na makaburi ya Kinondoni, anasema eneo hilo limegeuzwa kuwa nyumba ya wageni, maarufu kama Guest Bubu.
“Huwa natamani nimwage upupu eneo lote hilo kwa sababu imekuwa kero. Watu hufika hapo jioni hadi asubuhi,” alisema.
Anasema angekuwa amepanga angehama kutokana na yanayoendelea eneo hilo.
“Unaona dirisha la chumbani nililiziba na nikatoboa huku mbele. Napata joto kwa sababu huku kumezibwa, lakini afadhali natulia kidogo,” alisema.
Sultani Athumani, mmoja wa vijana wanaolima mboga katika eneo la makaburi ya Chang’ombe ameshuhudia wengi wakifika eneo hilo kufanya kafara.
Anasema kwa hali ilivyo sasa katika makaburi hayo, kuna siku mafuvu yataelea na hasa kipindi cha mvua kwa sababu makaburi hufukuliwa, kuchimbwa na mabaki kuzikwa upya. “Wanafukua makaburi ili wachimbe mengine, kuna siku waliisahau mifupa bila kuifukia ikiwa na sanda yake tukaifukia,” anasema.

Uwanja wa Ndege Chato kugharimu Sh39 bilioni


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa ameweka jiwe la msingi katika Uwanja wa Ndege wa Chato wenye kiwango cha daraja la 4C ambao ujenzi wake utagharimu Sh39.15 bilioni.
Akizungumza katika hafla ya uwekaji wa jiwe hilo jana, alisema kiwanja hicho kinajengwa na mkandarasi Mtanzania kwa kiwango cha kimataifa.
Profesa Mbarawa alisema: “Tunahitaji maendeleo na Serikali hii imefufua shirika la ndege na tayari imenunua ndege sita ambazo zitafanya kazi ndani na nje ya nchi. Kila mkoa utakuwa na kiwanja cha ndege cha kisasa kitakachohudumia wananchi wasiopungua 100.”
Alisema uwapo wa viwanja vya ndege nchini kutakuza na kuchochea uzalishaji kwenye sekta ya viwanda, madini uvuvi na ufugaji.
Waziri Mbarawa alisema katika awamu hii ya tano, wizara imeboresha na kuimarisha ujenzi katika viwanja vya ndege vya Lindi, Iringa, Moshi na Simiyu.
Pia, alisema katika bajeti ya mwaka 2017/18 Serikali imepanga kufanya upembuzi katika viwanja vya Iringa, Musoma na Songea na sasa wanatafuta makandarasi.
Awali, mtendaji mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), Patrick Mfugale alisema kiwanja hicho kina ukubwa wa kilometa tatu.
Ujenzi huo ulioanza Septemba 2016 umeshajengwa kwa asilimia 52 na unategemewa kuchochea shughuli za maendeleo wilayani Chato na Mkoa wa Geita kwa jumla.
Mbunge wa Geita, Dotto Biteko aliishukuru Serikali kwa ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Chato akisema kitachochea maendeleo ya mkoa huku akimwomba Profesa Mbarawa kusaidia ujenzi wa barabara inayounganisha Wilaya ya Bukombe na Geita yenye urefu wa kilometa 60.

Wajawazito wasafiri umbali mrefu kufuata upasuaji


Madaba. Wakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba, Mkoa wa Ruvuma wamesema wajawazito wamekuwa wakisafiri umbali wa kilometa 127 kutoka eneo hilo kwenda Songea Mjini kufuata huduma ya upasuaji.
Kutokana na changamoto hiyo, wameiomba Serikali kuwasaidia kujenga chumba cha upasuaji katika Kituo cha Afya cha Madaba ili kuepuke kero ya kufuata huduma hiyo Songea Mjini.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya wanawake wanaoishi Madaba walisema ujenzi wa chumba hicho ulioanza muda mrefu lakini haujakamilika.
Mmoja wa wanawake hao, Esta Mlelwa mkazi wa Kijiji cha Mtepa alisema wajawazito wamekuwa wakikabiliwa na kero hiyo hali inayowalazimu kutumia pesa nyingi kusafiri kwenda kujifungulia mjini.
Alisema iwapo Serikali itaharakisha ujenzi wa chumba cha upasuaji, itasaidia kuokoa maisha ya wajawazito kwa kuwa baadhi wamefariki dunia kwa kukosa huduma hiyo kutokana na kushindwa kumudu gharama.
Mkazi wa Madaba, Agnes Myoka alimshukuru mbunge jimbo la Madaba, Joseph Mhagama kwa jitihada zake za kusaidia wajawazito kupata huduma bora za afya kwa kupeleka vitanda vya kujifungulia katika kituo hicho, magodoro, viti vya kubebea wagonjwa na gari la wagonjwa ili kupunguza changamoto zinazoikabili halmashauri hiyo.
Katibu wa afya wa kituo hicho, Yasinta Peter alizitaja changamoto zinazowakabili kuwa ni ukosefu wa chumba cha upasuaji, wodi ya watoto, chumba cha kupumzika wajawazito na upungufu wa wahudumu wa afya.
Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, Shafii Mpenda alimshukuru mbunge wa Madaba kwa kutoa ushirikiano kusaidia kutatua kero mbalimbali za wananchi.
Mbunge wa Madaba, Joseph Mhagama alisema amechaguliwa na wananchi ili awasaidie kutatua kero zao ikiwa ni pamoja na kuwapelekea huduma za kijamii karibu.
Alisema licha ya kuwa na mfuko wa jimbo, lakini ameamua kutumia nguvu zake kwa lengo la kuleta maendeleo jimboni humo.

Marekani yaishambulia ISIS Somalia

African Command katika Pembe ya Afrika
Marekani imefanya shambulizi la anga kwa kutumia ndege zisizokuwa na rubani dhidi ya wapiganaji wa Kikundi cha Islamic State nchini Somalia Ijumaa na kusema imepiga hatua ya kipekee katika vita hii.
Katika miezi ya karibuni, Marekani imeendelea kushambulia wapiganaji jihadi kutoka katika kikundi cha waasi cha al-Shabaab ambacho kinamafungamano na al-Qaeda, lakini yaliyotokea Ijumaa ni hatua kubwa iliyofikiwa kutokana na kuendelea kwa vita hii dhidi ya IS.
“Majeshi ya Marekani yataendelea kutumia njia zote zinazokubalika na muwafaka kulinda Wamarekani na kuvidhoofisha vikundi vya kigaidi,” AFRICOM imesema.
Hii ni mara ya kwanza kwa Marekani kushambulia kikundi hicho katika nchi ya Pembe ya Afrika, Maafisa wamesema.
Shambulizi hilo limefanywa katika eneo la kaskazinimashariki mwa Somalia na kuuwa “magaidi kadhaa,” Kikosi cha jeshi la Marekani cha Africa Command kimeleza katika tamko lake.
Kwa mujibu wa VOA, ambayo imemtaja mwenyekiti wa mji wa Qandala katika eneo ambalo linajitawala lenyewe huko Puntland, makombora sita yalipiga kambi ya IS katika Kijiji cha Buqa, kilomita 60 upande huo.
“Wakazi wa eneo hilo na wafugaji walishtushwa na shambulizi hilo na kutoweka kutoka sehemu hiyo,” Jama Mohamed Qurshe ameiambia VOA.
Mashambulizi ya angani
Msemaji wa kikosi cha AFRICOM Luteni Kamanda Anthony Falvo amesema hakuna raia waliokuwa karibu na eneo hilo lililokuwa limeshambuliwa.
“Walipiga maeneo waliokusudia kuyashambulia,” alisema, na kueleza kuwa haya yalikuwa ni mashambulizi ya awali dhidi ya IS nchini Somalia.
Shambulizi la kwanza lilifanyika katikati ya usiku kwa saa za Somalia na shambulizi la pili kufuatia saa tano mchana.
IS imedai kufanya shambulizi la kujitoa muhanga ndani ya nchi ya Somalia mwezi Mei, na kuuwa watu wasiopungua watano na kuendeleza harakati zake katika eneo linalotawaliwa na al-Shabaab.
Wapiganaji hao wanaongozwa na Mhubiri wa zamani wa al-Shabaab Abdiqadir Mumin, ambaye alihama kutoka Al-Qaeda kwenda kujiunga na IS Octoba 2015 na kuitwa ni “gaidi la kimataifa” na Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani mwezi Agosti.
Mumin alizaliwa Puntland na kuishi Sweden kabla ya kurudi Uingereza miaka ya 2000, ambapo alipewa uraia wa Uingereza.

Marekani yawaondosha wafanyakazi wake Somalia

Wanajeshi wa Marekani wanaolinda ofisi za ubalozi nchini Somalia chini ya uongozi wa kikosi cha African Command.
Serikali ya Marekani imewataka wafanyakazi wake wote ambao hawahitajiki kuwepo ubalozini nchini Somalia, kwa wakati huu kuondoka katika mji mkuu, Mogadishu, ikieleza inatokana na vitisho maalum vilivyo elekezwa dhidi yao.
Taarifa iliyotolewa Jumamosi na Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani inahusisha tishio hilo na kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Mogadishu, ambacho kinalindwa na Vikosi vya Umoja wa Afrika (AU) na uwanja huo unaendeshwa na kampuni ya Uturuki.
“Kutokana na taarifa ya vitisho hivyo dhidi ya wafanyakazi wa Marekani katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mogadishu, Ubalozi wa Marekani nchini Somalia umewaagiza wafanyakazi hao kuondoka Mogadishu mpaka pale taarifa zaidi itakapotolewa,” limesema tamko hilo.
Pia imewataka raia wa Marekani walioamua kubakia Somalia kuwa macho.
“Wizara ya Mambo ya Nje inawataka raia wote wa Marekani walioamua kubakia Somalia kuangalia upya mpango mzima wa usalama wenu, kuchukua hatua zinazofaa kuhakikisha usalama wenu, kuwa macho na mazingira yenu, kufuatilia vituo vya habari nchini Somalia juu ya taarifa mpya, na kuendelea kuwa waangalifu kwa kiwango cha hali ya juu,” taarifa hiyo imesema.
Wakiongea na VOA kwa sharti la kuwa wasitajwe majina, vyombo vya usalama katika uwanja wa ndege wa Somalia vimesema tishio hilo limewasilishwa kwa vyombo vya usalama na hawajui hasa tishio hilo linahusu nini hasa.
Brigedia Jenerali Abdi Ashkir Jama, ambaye ni meneja mkuu wa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Aden Adde, Mogadishu – ambao umepewa jina hilo la aliyekuwa rais wa kwanza Somalia, Aden Abdullah Osman—VOA iliwasiliana naye, lakini amekataa kuzungumza kuhusu suala hilo na kutaka iwasiliane na wizara ya usalama ya Somalia.

Wana wa ufalme wakamatwa Saudi Arabia

Saudi Crown Prince Mohammed bin Salman attends a conference in Riyadh, on October 24, 2017Haki miliki ya pichaAFP
Image captionPrince Mohammed bin Salman
Mawaziri 11 miongoni mwao wakikwa wana wa ufalme wameachichwa kazi na hata kuzuiliwa katika Mabadiliko makubwa yaliyotangazwa kwenye serikali ya Saudia.
Wengine wanaozuiliwa ni mawaziri wa zamani ambao wamehusishwa na kashfa za rushwa.
Katika hatua hiyo ambayo si ya kawaida inaelekea mwana mrithi wa mfalme Mohammed Bin Salman ambaye ndiye anaesimamia kitengo cha kupambana na ufisadi, anapania kujitenga na kuwadhibiti wapinzani wake wenye mamlaka makubwa nchini humo.
Miongoni mwa wanazuiliwa ni wana wa wafalme mmojawao ni mtoto wa marehemu mfalme Abdullah Prince Miteb aliyekuwa mkuu wa kitengo cha kikosi cha kiusalama National guard ambapo sasa amepokonywa wadhfa huo.
Saudi Arabian Prince Miteb bin Abdullah at the Elysee Palace in Paris, 18 June 2014Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionPrince Miteb bin Abdullah ameondolewa kutoka kijiji chenye nguvu cha ulinzi
Mwengine ni billionaire Prince Al-Waleed bin Talal.
Inaripotiwa kwamba hisa katika kampuni aliyoekeza huko uingereza iitwayo Kingdom Holding, zimeporomoka kutokana na hisia hizo.
Mwandishi wa BBC anaefuatilia kwa karibu swala hilo anasema mabadiliko hayo bila shaka yatawabugudhi wale wanaopendelea mambo yabaki yalivyo Saudia ambako wenye mamlaka ya juu ya kiukoo na kikabila hawapendelei hatua kama hizo za kubadili mambo gafla.

Kombora larushwa karibu na uwanja wa ndege Saudi Arabia

Riyadh skylineHaki miliki ya pichaAFP
Image captionUwanja huo hupatikana kaskazini mwa Riyadh
Saudi Arabia imetungua kombora ambalo lilikuwa limerushwa karibu na uwanja mkuu wa ndege mjini Riyadh, taarifa zimesema.
Mlipuko mkubwa ulisikika karibu na uwanja huo wa ndege.
Duru kutoka jeshi la wanahewa la Saudia zimenukuliwa na shirika la utangazaji la serikali ya Al-Arabiya zikisema kombora hilo lilitunguliwa kaskazini mashariki mwa mji huo mkuu.
Runinga yenye uhusiano wa waasi wa Houthi kutoka yemen limesema kombora hilo lilikuwa limerushwa kulenga uwanja huo wa ndege.
Shirika la habari la serikali la Al-Ekhbariya limesema kombora hilo lilikuwa "ndogo kiasi" na kwamba hakuna uharibifu uliotokea.
Kombora hilo la masafa marefu lilikuwa limerushwa kulenga uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mfalme Khalid, kwa mujibu wa televisheni ya wapiganaji wa Houthi ya Al-Masirah.
Yemen imesambaratishwa na vita kati ya wanajeshi watiifu kwa serikali inayotambuliwa kimataifa ya Rais Abdrabbuh Mansour Hadi na wapiganaji wa kundi la waasi wa Houthi.
Saudi Arabia inaongoza kampeni ya kuwashinda wapiganaji hao wa Houthi.

Wanaharakati wa kulinda mazingira waandamana Bonn

 Maelfu ya waandamaanji walikusanyika mjini Bonn Jumamosi kabla ya kuanza kwa mkutano wa kimataifa unaoandaliwa na Umoja wa Mataifa wa kujadili mabadiliko ya tabia nchi mjini humo.

Klimakonferenz Bonn Demonstrationen gegen Kohle (Getty Images/S. Gallup)
Mkutano huo wa mazingira unaanza Jumatatu Novemba 6, na utadumu kwa wiki mbili zijazo hadi Novemba 17. Kiasi ya watu 25,000 wanatarajiwa kuhudhuria mkutano huo wa kimataifa.
Suala la kuachana na uzalishaji wa makaa ya mawe Ujerumani ni moja wapo ya vipengele muhimu vinavyojadiliwa katika mazungumzo ya kuunda serikali ya muungano kati ya Kansela wa Ujerumani Angela Merkel na vyama vengine vya kisiasa , Chama cha walinda mazingira cha  Kijani na chama kinachoelemea upande wa biashara cha Free Democrats.
Waaandaji wa maandamano hayo wapatao 20,000 wameitolea wito serikali ya Ujerumani kutekeleza makubaliano ya mwaka 2015 yaliyofikiwa mjini Paris yenye lengo la kuhakikisha katika karne hii, uchumi wa dunia hautegemei mafuta na inachukua hatua kupunguza ongezeko la viwango vya joto duniani.
Ujerumani huenda isifikie malengo
Data za hivi karibuni zinaonesha kuwa Ujerumani itashindwa kufikia lengo lake la kupunguza kwa asilimia 40 kiwango cha gesi chafu ya Carbon Monoxide ifikapo mwaka 2020. Miongoni mwa waliondamana ni wanachama wa mrengo wa kushoto, vyama vya kisiasa vinavyolinda mazingira, vyama vya wafanyakazi na makundi yanayoipinga utandawazi.
Klimakonferenz Bonn Demonstrationen gegen Kohle (Getty Images/AFP/S. Gallup)
Utekelezaji wa mkataba huo utajadiliwa katika mkutano huo wa Umoja wa Mataifa unaofanyika mjini Bonn, utakaowaleta pamoja wajumbe wa nchi 196 wanachama wa umoja huo. Makubaliano ya Paris yaliyofikiwa 2016 yanalenga kupunguza viwango vya joto duniani hadi chini ya nyuzi mbili.
Taarifa kutoka makundi 100 ya kiraia imesema maisha ya mamilioni ya watu duniani yako hatarini kutokana na athari za mabadiliko ya hali ya hewa na kuwa kuna baadhi ya visiwa huenda vikapotea kabisa kutokana na kuongezeka kwa viwango vya maji ya bahari.
Mkataba wa Paris utafikiwa?
Mashirika hayo yanataka hatua za dharura kuchukuliwa kuepusha hatari hizo ikiwemo kuanza kupunguzwa kwa kiwango cha nishati itokanayo na mafuta na pamoja na makaa ya mawe. Makaa hayo ya mawe yanachangia kwa karibu thuluthi moja ya matumuzi ya nishati duniani na inachangia asilimia 40 ya umeme unaozalishwa, hiyo ikiwa mara mbili ya ile ya gesi asilia.
Ikilinganishwa na gesi na mafuta, makaa ya mawe yanachafua mazingira zaidi. Nchini Marekani utumiaji ya makaa hayo umepungua ambako sasa matumizi ya gesi ya asilia yanashika kasi, japo sio kwa kiwango cha kuridhisha.
Mkutano huo muhimu wa kujadili mabadiliko ya tabia nchi unafanyika wakati ambapo Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza nchi yake inajiondoa kutoka mkataba uliofikiwa mwaka jana mjini Paris, Ufaransa, wa makubaliano ya kihistoria ya tabia nchi na hivyo kuibua mashaka na wasiwasi kuwa huenda hatua hiyo iliyochukuliwa na Marekani, taifa lenye nguvu duniani ikahujumu kufikiwa kwa malengo ya makubaliano hayo.

Merkel asema muungano wa pande tatu unaweza kufanikiwa

Kansela wa Ujerumani Angela Merkel amesema anaamini vyama vya siasa vinavyojaribu kuunda serikali mpya vinakabiliwa na mazungumzo magumu, lakini vinaweza kupunguza tofauti zao.

Fortsetzung der Sondierungsverhandlungen (picture alliance/dpa/M. Kappeler)
Wakati ambapo washirika wake katika muungano uliopita, chama cha Social Democratic SPD, kimeazimia kwenda katika kambi ya upinzani, Merkel anashinikiza kuunda muungano na watetezi wa mazingira - chama cha Kijani pamoja na kile kinachoelemea upande wa biashara cha Free Democrats FDP, baada a muungano wake wa vyama vya kihafidhina kupoteza kura nyingi kwa chama cha siasa kali za mrengo wa kulia cha Alternative für Deutschland AfD katika uchaguzi wa mwezi Septemba.

"Nadhani kwamba tunakabiliwa na mazungumzo magumu katika siku zijazo lakini pia nadhani bado tunaweza kufikia muafaka ikiwa tutafanya juhudi katika namna ambayo kila mshirika anaweza kuleta utambulisho wake ili kuunda kitu kizuri kwaajili ya taifa zima," alisema Merkel katika mkutano na waandishi habari mjini Berlin.
Alisema chama cheka cha CDU kwa namna yoyote iko tayari kufanya hilo katika moyo huu," kabla ya kuingia katika awamu nyingine ya mazugumzo.
Balkon-Galerie Jamaika-Sondierungsgepräche (picture-alliance/dpa/B. von Jutrczenka)
Merkel na wenzake wakiwa katika picha ya pamoja na viogozi wa chama cha Kijani - Die Grüne mjini Berlin.
Hatari ya uchaguzi mpya
Merkel anahitaji kuunda muungano ambao haujawahi kujaribiwa kwa ngazi ya taifa, ili aweze kuanza tena kazi, vinginevyo anaweza kushuhudia uongozi wake ukifikia tamati baada ya miaka 12. Kushindwa kwa mazungumzo hayo kunaweza kupelekea kuitishwa uchaguzi mpya, ambao yumkini ukakipa mafanikio zaidi chama cha AfD, kilichoingia bungeni kwa mara ya kwanza katika uchaguzi wa Septemba.
Lakini baada ya wiki mbili za mazungumzo, washirika wenye mitazamo tofauti wanaedelea kusigana, hususani kuhusu masuala ya uhamiaji, mazingira, usafiri na sera ya kigeni. "Tumekaa pamoja kwa siku 10, mada 12. Matokeo ni nyaraka nane zenye orodha ndefu ya upinzani," alisema Juergen Trittin, mwakilishi wa chama cha Kijani katika mazungumzo na shirika la utangazaji la umma ARD, na kuongeza kuwa katika maeneo manne, hawajaweza kukubaliana hata juu ya nini wanachotofautiana.
Merkel alisema usiku wa siku ya uchaguzi wa Spetemba 24, kwamba ana imani kutakuwa na serikali imara kabla ya siku ya X-mas. Maafisa wa juu katika muungano wake wa kihafidhina, sasa wanasema huenda ikachukuwa hadi mwakani kwa serikali mpya kuweza kuundwa.
Uwezekano wa mazungumzo kufanikiwa
Fortsetzung der Sondierungsgespräche (picture alliance/dpa/M. Kappeler)
Mwenyekiti wa FDP Christina Lindner.
Kiongozi wa chama cha FDP Christian Lindner, anaweka uwezekano wa kufanikiwa kwa mazugumzo hayo kwa asilimia 50-50. Baada ya chama chake kushindwa kupata kiti chochote katika bunge lililopita, ana wasiwasi kuhusu kuridhia mambo ambayo yanaweza kukirejesha tena chama chake katika mashaka kisiasa.
Mtaalamu wa sera ya kigeni wa chama cha Kijani Omid Nouripour, alisema mazugumzo ya kuunda serikali yanaweza kushindwa kiujumla. Chama cha Kijani kipanga kuwasilisha matokeo ya mazungumzo ya awali kwa wanachama wake Novemba 25, ambapo baada ya hapo makundi hayo matatu yanalenga kuhamia kwenye mazungumzo ya kina zaidi.
Merkel amesema wiki mbili za mazungumzo ya kutafuta muafaka zimewaruhusu kujenga misimamo na kuanza kufanyakazi kuelekea makubaliano ya mwisho.

Waziri Mkuu Lebabon ajiuzulu, asema anahofia maisha yake

Waziri Mkuu wa Lebanon Saad Hariri amejiuzulu wadhifa wake, na kuilaumu Iran kwa kuingilia masuala ya ndani ya mataifa ya Kiarabu. Alisema pia anahofia maisha yake katika mazingira ya sasa ya kisiasa nchini mwake.

Saad Hariri Libanon (picture-alliance/dpa/W.Hamzeh)
Akitangaza kujiuzulu kwake ambako kumekuja kwa kushitukiza siku ya Jumamosi, Hariri alisema katika hotuba iliyotangazwa moja kwa moja kupitia televisheni, kwamba alihisi "njama dhidi ya maisha yake" katika mazingira yanayofanana na yaliokuwepo kabla ya baba yake, waziri mkuu wa zamani wa Lebanon Rafik Hariri.
Rafiki Hariri aliuawa katika mripuko wa bomu pamoja na watu wengine 21 katika mji mkuu, Beirut, Februari 2005 katika mazingira ambayo mpaka leo hii hayajatolewa ufafanuzi. Saad Hariri pia ameilaumu Iran, akisema ilikuwa inaingilia masuala ya ndani ya mataifa ya Kiarabu na kuchochea machafuko.
Mwanasiasa huyo wa Kisunni mwenye umri wa miaka 47, amejiuzulu chini ya mwaka mmoja baada ya kuundwa kwa serikali yake, ambayo tawi la kisiasa la Hezbolla ni sehemu yake. "Iran inataka kuwa mwamuzi wa hatma ya mataifa ya kanda Mashariki ya Kati. Hezbolla ndiyo tawi la Iran siyo tu nchini Lebanon, lakini pai katika mataifa mengine ya Kiarabu," alisema Hariri.
Libanon Saad Hariri, ehemaliger Ministerpräsident (picture-alliance/AP Photo/H. Ammar)
Waziri Mkuu wa Lebanon aliejiuzulu Saad Hariri.
"Katika miaka ya karibuni, Hezbollah imetumia nguvu ya zana zake za kivita kulaazimisha mambo," alisema akisoma hotuba ilioandaliwa. Hariri ameituhumu Iran kwa kuchochea uhasama miongoni mwa watoto wa taifa moja na kuunda taifa ndani ya taifa -- kiasi kwamba yenyewe ndiyo inao usemi wa mwisho kuhusu uendeshaji wa mambo nchini Lebabon.
Nguvu kuliko jeshi la taifa
Kundi la Hezbolla ni mshirika muhimu wa rais wa Syria Bashar al-Assad katika vita vya utawala wake dhidi ya Kundi linalojiita Dola la Kiislamu na makundi mengine ya upinzani. Linaungwa mkono na Iran na ndiyo kundi pekee la nchini Lebabon lililobakiza silaha zake baada ya vita vya wenyewe kwa wenyewe vya 1975-1990. Nguvu yake ya kijeshi imeongezeka tangu wakati huo na sasa inazidi hata ile ya vikosi vya kijeshi vya taifa.
Kundi hilo linadai ndiyo ngome pekee ya kuaminika dhidi ya nchi jirani ya Israel, na kukataa kwake kusalimisha silaha ndiyo kiini cha mgogoro wa kisiasa nchini Lebanon. Wanachama wa Hezbollah wametuhumiwa kuhusika na mauaji ya Rafiki Hariri, mtu aliekuwa na ushawishi mkubwa katika siasa za Lebanon baada ya vita.
Hariri alipata utajiri wake nchini Saudi Arabia, ambako mwanae Saad Hariri alizaliwa. Riyadhi ndiyo hasimu mkuu wa kikanda wa Iran, na ushindani wa ushawishi katika kanda umejitokeka katika migogoro inayoendelea nchini Iraq, Syria na Yemen.
Ofisi ya rais wa Lebanon Michel Aoun, kiongozi mkongwe wa Kikristu anaeshirikiana na Hezbollah, ilitoa taarifa ikithibitisha kwamba Hariri amekabidhi barua yake ya kujiuzulu.
Michel Aoun (Picture-Alliance/AP Photo/H. Malla)
Rais wa Labenon Michel Aoun anamsubiri Hariri arudi nyumbani kuzungumzia mazingira ya kujiuzulu kwake.
"Rais Aoun anasubiri Hariri arudi Beirut ili kumuuliza kuhusu mazingira yaliopelekea uamuzi wake na baadae kuamua kuhusu hatua zinazofuata," ilisema taarifa kutoka ofisi hiyo. Hariri alisema katika hotuba kwamba mazingira ya kisiasa nchini Lebanon yanafanana kabisaa na yaliokuwepo kabla ya kuuawa kwa baba yake.
Mauaji hayo ya Februari 2005 yalisababisha mabadiliko makubwa ya ghafla ya kisiasa yaliopelekea kujiondoa kwa jeshi la Syria kutoka Lebanon.
Atahri za kisiasa kwa Lebanon
Walid Jumblatt, mmoja wa wanasiasa wakubwa nchini Lebanon, na kiongozi maarufu zaidi wa Druze, alisema kujiuzulu kwa Hariri kunaweza kuiathiri vibaya nchi hiyo ambayo tayari inakabiliwa na hali ngumu.
Alihoji kwamba kujiuzulu huko ndiyo idhara ya karibuni zaidi ya mvutano kati ya Saudi Arabia na Iran, na kutoa wito wa kuzidisha juhudila kidiplomasia kutatua mgogoro huo. "Lebabnon ni nchi ndogo sana ilioko katika mazingira hatarishi kuweza kuhimili mzigo wa kisiasa unaoambatana na kujiuzulu kwa Hariri. "Nitaendelea kutoa wito wa kuwepo na mazungumzo kati ya Saudi Arabia na Iran."

Trump awaonya madikteta, serikali dhalimu

Rais Trump na mkewe Melania alipowasili katika kituo cha kijeshi Yokota, mji wa Fussa , Tokyo, Novemba. 5, 2017.
Rais wa Marekani Donald Trump Jumapili amewaambia wanajeshi wa Marekani walioko katika kituo cha jeshi la anga cha Yokota, Japan kwamba “hakuna mtu yeyote, siyo dikteta, siyo serikali … asijaribu kudharau azimio la Marekani.”
Matamko yake yamekuja wakati akianza ziara yake itakayo mchukua takriban wiki mbili katika Bara la Asia ambayo itaangaza suala la Korea Kaskazini.
Baadhi ya ahadi zake, zikiwa zimeelekezwa kwa vikosi vya Marekani, zinaweza kutafsiriwa kama ni onyo lisilo la moja kwa moja kwa taifa ambalo limetengwa:
“Nyinyi ni tishio kubwa kwa madikteta na wakandamizaji ambao wanataka kuwaangamiza watu wasiokuwa na hatia.”
Ujumbe kwa Korea Kaskazini
Wakati akiwa njiani kuelekea Japan, rais amezungumza na waandishi wa habari akiwa katika ndege ya Air Force One, ambapo mwandishi wa VOA alimuuliza iwapo ana ujumbe kwa watu wa Korea Kaskazini.
“Nafikiri ni watu wazuri sana,” rais alisema. “Niwachapa kazi. Ni watu wakarimu, ni wakarimu kuliko vile dunia inavyowafahamu na kujua, ni watu wazuri sana. Na natumai kila kitu kitaenda sawa na kila mtu. Itakuwa ni jambo la kupendeza iwapo tutaweza kutatua hili kwa ajili ya watu hawa wema na kwa kila mtu.”
Trump pia amegusia kuwa anatarajia kukutana na Rais wa Russia Vladimir Putin pembeni ya mkutano wa viongozi wa APEC utakaofanyika baadae Ufilipino wakati wa ziara yake hii.

Wanasiasa Marekani wahoji usiri wa operesheni za jeshi lao Afrika

Wanasiasa nchini Marekani wameelezea wasiwasi juu ya kuongezeka kwa uwepo wa kijeshi wa Marekani barani Afrika, ambako wanahofu wizara ya ulinzi inazidi kujiingiza katika kampeni za siri dhidi ya adui anaebadilika.

Senegal US Soldaten (Getty Images/AFP/Seyllou)
Kuuawa mwezi uliyopita kwa wanajeshi wanne wa Marekani katika shambulizi la kuvizia nchini Niger kumemulika suala hilo, ambapo wabunge sasa wanatoa wito wa kuwepo na uwazi zaidi juu ya kinachoendelea barani Afrika.
Seneta wa chama cha Democratic Tim Kaine, alisema wiki hii kuwa uwepo wa kijeshi wa Marekani barani Afrika ni mkubwa kuliko umma unavyojua.
Shambulio la Niger limeasha pia mjadala juu ya mamlaka ya kisheria inayoitumia wizara ya ulinzi kupambana dhidi ya makundi ya itikadi kali nje ya taifa hilo, hususani barani Afrika ambako wanajeshi karibu 6,000 wamewekwa. Waziri wa ulinzi Jim Mattis alikumbana na maswali ya wabunge wiki hii kuhusu sheria hizo za kupigana vita.
Mattis, Tillerson: Sheria bado zinahitajika
Sheria hizo zilipitishwa awali siku tatu baada ya shambulizi la Septemba11, 2001 mjini New York na Washington, kwa lengo la kupambana na kundi la Al-Qaeda lakini tangu wakati huozimekuwa zikitumiwa kuwasaka wapiganaji wa Kiislamu kutoka makundi mengine tofauti.
USA Ankunft der toten US-Soldaten aus dem Niger (picture alliance/AP Photo/L. Hiser/U.S. Army)
Kuuawa kwa wanajeshi wa Marekani katika operesheni ya siri nchini Niger kumeibua mjadala kuhusu kiasi gani jeshi la Marekani limejishirikisha barani Afrika.
Wabunge wa Marekani wanazingatia kuzirekebisha sheria hizo au kuzifuta, lakini Mattis na waziri wa mambo ya nje Rex Tillerson hawadhani iwapo zinapaswa kubadilishwa au kufutwa bila kuwepo na sheria mbadala.
Mattis alisema kundi la Al-Qaeda hivi sasa limegawika katika makundu mengine, likiwemo kundi la Dola la Kiislamu, na kwa sababu hiyo sheria hizo bado zinatumika. Aliwambia wabunge kuwa makundi hayo yanatengana, na kisha kurudi pamoja, yanaweza kubadili majina yao mara kadhaa kama zifanyavyo bendi za muziki.
Seneta wa Democratic Chris Coons, alisema janga lililotokea nchini Niger, la kupotolewa na wanajeshi wao wanne, lilisaidia kuwavutia nadhari juu ya ukweli kwamba wanao raia, na wanao maseneta wasio wakweli kuhusu hasa wapi duniani wanashiriki dhidi ya adui huyo anaebadilika katika zama mpya za mapigano.
Askari 6,000 katika mataifa 11
Marekani wiki hii iliahidi kiasi cha dola milioni 60 kusaidia kikosi cha kupambana na ugaidi katika kanda ya Sahel maarufu G5. Wanachama wa G5, Burkina Faso, Chad, Mali, Mauritania na Niger, wanaangaliwa na Marekani kama washirika wa kikanda.
Rasmi, ujumbe wa Marekani katika eneo la Afrika una jukumu la kutoa mafunzo, ushauri na msaada kwa majeshi ya Kiafrika ili kusaidia mataifa kusimama dhidi ya makundi ya itikadi kali. Lakini kiuhalisia, kama ilivyoonyeshwa nchini Niger, jukumu la Marekani linakwenda mbali ya hilo.
Kulingana na taarifa kutoka Ikulu ya Marekani kwenda Congress mwezi Juni, wanajeshi walio tayari kwa mapambano wameplekwa katika mataifa 19 -- na 11 kati yake ni katika bara la Afrika - ambayo ni Somalia, Libya, Kenya, Niger, Cameroon, Uganda, Sudan Kusini, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Djibouti na Misri.
Rex Tillerson und James Mattis (picture alliance/ZUMAPRESS/Planet Pix/G. Johnson)
Waziri wa Ulinzi Jim Mattis (kushoto) na waziri wa mambo ya nje Rex Tillerson (kulia) wanasema sheria zinazotumiwa katika kujihusisha na mapambano dhidi ya makundi ya itikadi kali bado zinahitajika.
Kufichuka kwa mauaji ya wanajeshi
Kwa seneta Mrepublican Rand Pual, ujumbe rasmi wa mafunzo ni kisingizio tu cha kuficha ukweli hasa kile kinachoendelea. Inaonekama kama vile una mgogoro unaoendelea nchini Niger. Tuna wanajeshi 6,000 katika mataifa 54 barani Afrika," Paul alimuambia Mattis.
Kulingana na Pentagon, tukio la Niger lilitokea mapema mwezi Oktoba, wakati timu ya Marekani na Niger ikifanya doria ya kawaida katika kijiji cha Tongo Tongo karibu na mpaka wa Mali. Walishambuliwa na wapiganaji karibu 50 wa ndani wanaohusishwa na kundi la Dola la Kiislamu.
Kituo cha ABC News kiliripoti siku ya Alamisi kuwa ujumbe huoulibadilika na kimsingi walikuwa wakijaribu kumteka au kumuua kiongozi wa wapiganaji mwenye mafungamano na Dola la Kiislamu na Al-Qaeda.

Saturday, November 4

Kiongozi wa genge auawa Mexico akibadili sura

Jesus Martin au El Kalimba amekuwa akisakwa na polisi kwa kuendesha biashara ya kuiba mafuta kwa kukata mabomba ya usafirishaji wa bidhaa hiyo muhimu.Haki miliki ya pichaEPA
Image captionJesus Martin au El Kalimba amekuwa akisakwa na polisi kwa kuendesha biashara ya kuiba mafuta kwa kukata mabomba ya usafirishaji wa bidhaa hiyo muhimu.
Kiongozi mmoja wa genge nchini Mexico ameuawa kwa kupigwa risasi wakati alipokuwa katika kliniki akifanyiwa upasuaji wa kubadili sura yake mbali na kuondosha alama zake za vidole.
Maafisa wanasema kwamba watu walio na silaha walivamia kliniki hiyo ya mjini Puebla na kumfyatulia risasi kiongozi huyo wa genge Jesus Martin, anayejulikana pia kwa jina la mtaani El Kalimba.
Maafisa hao wanaendelea kueleza tathmini yao kwamba tukio hilo ni baada ya ugomvi baina ya magenge hasimu ambapo pia watu wengine watatu wamefariki .
Jesus Martin au El Kalimba amekuwa akisakwa na polisi kwa kuendesha biashara ya kuiba mafuta kwa kukata mabomba ya usafirishaji wa bidhaa hiyo muhimu.
Ukubwa wa biashara hiyo umefananishwa na ile ya ulanguzi wa mihadarati nchini Mexico.