Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Fortonatus Musilimu (kulia) na askari wa kikosi chake kikagua moja ya mabasi ya abiria jana alfajiri katika Kituo Kikuu cha Mabasi jijini Mbeya katika ukaguzi wa kushitukiza, ambapo mabasi kadhaa yalikuwa na ubovu katika mfumo wake wa usukani, tairi vipara na matatizo mengineyo na kuyazuia. Picha na Godfrey Kahango
Kamanda Musilimu alimuagiza Mkuu wa Usalama Barabarani Mkoa wa Mbeya (RTO) Butusyo Mwambelo kutekeleza amri hiyo jana baada ya kufanya ukaguzi wa kushtukiza katika mabasi na madereva eneo hilo.
“Hawafanyi kazi ipasavyo na hii inatokana na kukaa kituo kimoja zaidi ya miaka mitano,” alisema Kamanda Musilimu.
Pia, alisitisha mabasi matano kutoendelea na safari baada ya kubaini hitilafu kwenye mfumo wa usukani na magurudumu.
Ofisa Mfawidhi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) Mkoa wa Mbeya, Denis Daud alisema chombo cha moto lazima kifanyiwe ukaguzi na maofisa wa polisi kama kina sifa ya kuingia barabarani.
Mdau wa usafiri, Mohamed Abdalah alisema ukaguzi uliofanywa na kamanda unaisadia kubaini mabasi ambayo hayaruhusiwi kuwapo barabarani.
No comments:
Post a Comment