Tuesday, November 7

ZITTO ATAKA ASHITAKIWE



KIONGOZI wa Chama cha ACT- Wazalendo , Zitto Kabwe amelitaka Jeshi la Polisi limshtaki mahakamani ili madai yake dhidi ya sheria ya takwimu yapate tafasiri ya kisheria.
Akizungumza na waandishi wa habari jana katika Kituo cha Polisi cha kushughulikia makosa ya uhalifu wa kimtandao eneo la Kamata jijini Dar es Salaam, alisema anataka kesi hiyo ipelekwe mahakamani ili tafasiri sahihi ya kisheria kuhusu masuala ya takwimu itolewe.
“Sheria ya takwimu ni miongoni mwa sheria zilizokuwa zinapigiwa kelele na wabunge kabla ya kupitishwa lakini Serikali ilifanya haraka kuipitisha huku ikiwa na upungufu katika baadhi ya vipengele. Upungufu huo unanyima uhuru wa kutoa taarifa,” alisema Zitto.
Alisema ni wakati mwafaka kwa Polisi kuifikisha kesi yake hiyo mahakamani ili mgongano uliopo uweze kupatiwa majibu ya kisheria na chombo hicho.
“Itakuwa ni kesi ya kwanza ya takwimu kufikishwa mahakamani tangu sheria hii ilipopitishwa na Bunge na hicho ndicho ninachokitaka kwa sababu kesi za takwimu haziwezi kumalizika kinyemela kwani zinaweza kuleta utatanishi,” alisema Zitto.
Awali kabla ya kuhojiwa kuhusu takwimu alizozitoa zikipingana na za serikali kuhusu ukuaji wa uchumi, Zitto alisema ACT  kilipanga kufungua kesi ya kuondoa vipengele vinavyokandamiza uhuru wa kutoa taarifa na maoni katika sheria ya takwimu.
Alisema hilo likifanakiwa litatoa tafasiri ya kisheria na kuondoa vipengele vinavyokandamiza utoaji wa taarifa.
Kabla ya kufika Kituo cha Polisi Kamata, Zitto alikwenda Kituo cha Polisi Chang’ombe kusikiliza tuhuma anazoelekezewa kuwa alitoa maneno ya uchochezi katika baadhi ya mikutano yake ya kisiasa.
Zitto aliwasili katika kituo hicho saa 10:37  na kutoka saa 4:47 baada ya kutakiwa aripoti tena Novemba 17, 2017.
Alisema polisi walimweleza faili lake bado lipo kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) hivyo arudi Novemba 17.
“Nimefika kituoni kuitikia wito wa polisi kama nilivyoambiwa wiki iliyopita lakini wamesema faili langu lipo kwa DPP ambaye analipitia kabla hajaamua kama napelekwa mahakamani au la,” alisema Zitto.
Jana viongozi wa ngazi za juu wa ACT- Wazalendo, walihojiwa na Polisi wa Kitengo cha Makosa ya Uhalifu wa Kimtandao na Takwimu kuhusu takwimu za uchumi zilizotolewa na Zitto.
Waliohojiwa ni Kaimu Mwenyekiti, Yeremiah Maganja, Katibu Mkuu, Doroth Semu na Mkurugenzi wa Ulinzi, Mohamed Babu.
Viongozi hao walifika kituoni hapo saa 3:00 na kutoka saa 9:00 alasiri.
Mwenyekiti Maganja, aliwaambia waandishi wa habari baada ya kuhojiwa kuwa lengo la mahojino hayo ni kupata ukweli wa taarifa za takwimu zilizotolewa kwenye kikao cha kamati kuu ya chama hicho.
“Kamati kuu ya chama chetu imeitwa kuhojiwa lakini unajiuliza kuwa polisi wanaweza kuiita Kamati Kuu ya CCM kuwahoji? ili ni jambo la kushangaza sana ndani ya nchi yetu,” alisema Maganja.
Alisema wakiwa katika mahojiano hayo walitakiwa kutoa majina ya wajumbe wengine wa kamati hiyo pamoja na namba zao za simu ili waweze kuitwa kuhojiwa, jambo ambalo wamelitekeleza.
“Tumewapa namba za simu pamoja na kuwaandikia majina ya wajumbe wengine wa kamati kuu ili waweze kuwaita na kuwahoji kwa sababu wanatoka mikoa tofauti,” alisema.

JPM AWANG’OA WAKURUGENZI WALIOSHINDWA KUJIBU SWALI LAKE

RAIS Dk. John Magufuli, ametengua uteuzi wa wakurugenzi wa Halmashauri za Manispaa ya Bukoba, Erasto Mfugale na Hamashauri ya Wilaya ya Bukoba Vijijini, Mwantumu Dau, kwa kushindwa kueleza kuhusu fedha za Mfuko wa Barabara (Road Fund) zilizotumwa katika halmashauri zao.
Alitengua uteuzi huo jana muda mfupi baada ya kumaliza kuhutubia wananchi katika hafla ya uzinduzi wa Uwanja wa Ndege wa Bukoba.
Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Ikulu jana, ilisema wakurugenzi hao watapangiwa kazi nyingine.

ILIVYOKUWA
Rais Magufuli akiwa uwanjani hapo, aliwaita wakurugenzi hao na kuwataka waeleze kiasi cha fedha za Mfuko wa Barabara kilichotumwa kwa bajeti ya mwaka 2017/18 katika halmashauri zao.
Aliyeanza kuulizwa ni Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Bukoba, Mfugale ambaye alishindwa kujibu.
“Bajeti ya Manispaa ni Sh milioni 33, na kuna mapato ya ndani na ya Serikali Kuu ambayo ni pamoja na fedha za elimu bure na mishahara ambayo ni Sh bilioni 19 kwa mwaka. Fedha hizi zinakuja kwa wakati unaotakiwa,” alisema Mfugale.
Rais Magufuli aliendelea kumuuliza tena fedha za Mfuko wa Barabara ni kiasi gani, lakini mkurugenzi huyo alishindwa kujibu.
“Nani anakumbuka fedha za barabara ni kiasi gani, naweza kuteua mkurugenzi mpya leo,” alisema Rais Magufuli.
Baada ya hapo, alifuatia Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba Vijijini, Mwantumu, ambaye pia alijibu kwa kusema hakumbuki kiasi cha fedha kilichotolewa.
Alisema anapokea fedha nyingi za miradi mbalimbali, si rahisi kukumbuka fedha zilizotumwa na Serikali za bajeti ya mwaka huu.
“Ndiyo mimi ni mkurugenzi, nina idara nyingi sana mheshimiwa Rais, naona mweka hazina anisaidie… naogopa kusema uongo,” alisema.
Kauli hiyo, ilionekana kumkera Rais Magufuli, ambaye alisema: “Huwezi kunijibu hivyo mimi.”
Baada ya hapo, aliitwa Meya wa Manispaa ya Bukoba, Chief Karumna, aliyeokoa jahazi baada ya kueleza mchanganuo wa fedha za bajeti, ikiwamo ukarabati wa barabara na stendi kuu ya Bukoba.
“Angalau wewe umejieleza vizuri, leo nimewasamehe, siku nyingine mtaondoka. Kwenye fedha za Serikali sitanii mimi, nataka fedha hizi zitumike vizuri,” alisema Rais Magufuli.

MASILAHI YA WATUMISHI
Rais Magufuli alisema Serikali imetenga zaidi ya Sh bilioni 156 kwa watumishi wa Serikali na kuanzia mwishoni mwa mwezi huu, itaanza kulipa promosheni zote zilizokuwa zimesimama.
Pia aliagiza watumishi wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora waliohusika kuidhinisha madeni yasiyo halali kuchunguzwa na vyombo vya dola.
Alisema Serikali imeanza kupitia madai ya baadhi ya wafanyakazi na kati yake majina 110 yamekwishapitiwa ambayo wanadai zaidi ya Sh bilioni 115.2.
Rais Magufuli alisema wakati anayapitia baadhi ya majina hayo, alibaini kuwapo madai hewa ya baadhi ya watumishi, ambayo yalikwishaidhinishwa malipo yake na maofisa wa Wizara ya Utumishi na kuwasilishwa Wizara ya Fedha kwa mchakato wa malipo.
“Kuna baadhi ya majina mengine nitayataja hapa. Kuna mtu anaitwa Jackson Kaswahili Robert wa Ukerewe, yeye anadai Sh bilioni 7.626,  tulipoyapitia na kuyakagua tumebaini hadai chochote.
“Mwingine ni Mwachano Ramadhan Msingwa, huyu anatoka Bagamoyo, yeye anadai Sh bilioni 1.754, lakini kwenye ukaguzi tumekuta anadai Sh milioni 2 tu.
“Yuko pia Gideon Zakayo wa Mafia, yeye alikuwa anakaimu nafasi, anadai Sh milioni 104 za kukaimu nafasi hiyo.
“Mnaweza mkaona ni kwa jinsi gani tumekuwa na watu ambao hawana uchungu kwa nchi yao na kama tusingefanya ukaguzi hizo fedha tungewalipa.
“Watumishi waliopitisha madai haya na hawa niliowataja hapa, naagiza vyombo vya dola vianze kuwachunguza, walizoea vya bure sasa havipo na mimi nitawanyoosha mpaka wanyooke,” alisema.
Pia alisema Serikali inakusudia kupeleka bungeni muswada wa mabadiliko ya sheria ya mifuko ya hifadhi ya jamii ili kubaki na mifuko miwili ambayo mmoja utawahusu watumishi wa serikali na mwingine wale wa sekta binafsi.
“Sh tirioni 1.2 zimelipwa katika mifuko ya hifadhi ya jamii kwa ajili ya kuwalipa wastaafu, tunakusudia kupeleka muswada wa mabadiliko ya sheria ya mifuko ya hifadhi ya jamii ili badala ya kuwa na utitiri wa mifuko inayoshindania wanachama, ibaki miwili tu, tunataka wakati neema inapatikana wafanyakazi halali wanufaike na haya matunda na kupata wanachostahili,” alisema.

UWANJA WA BUKOBA
Rais Magufuli, aliagiza zaidi ya Sh bilioni 9 zilizokuwa zimetengwa kulipa fidia kwa wakazi 295 wa eneo la Kajunguti ili kupisha ujenzi wa uwanja mpya wa ndege, kutumika kupanua uwanja wa Bukoba ili ndege kubwa za mizigo na abiria ziweze kutua.
“Wataalamu wa wizara tumieni mahesabu yenu uwanja upanuliwe na kufikia kilometa mbili, fedha zilizotengwa na nyingine zitakazopungua,” alisema.
Rais Magufuli, aliishukuru Benki ya Dunia (WB) kwa kutoa Dola za Marekani bilioni 57 kwa ujenzi na upanuzi wa viwanja vya ndege vya Tabora, Kigoma na Bukoba na Sh bilioni 925 kwa upanuzi wa Bandari ya Dar es Salaam na barabara.

UCHUMI
Alisema uchumi wa Tanzania unakua kwa kasi na ndiyo maana WB imeamua kuikopesha Serikali mikopo yenye riba nafuu.
“Nitashangaa kama atatokea mtu mwingine aje kupingana na takwimu hizi, pakitokea mtu wa namna hiyo atakuwa kachanganyikiwa,” alisema.

MALISHO YA MIFUGO
Rais Magufuli alisema Tanzania si machungio ya mifugo kutoka nje ndiyo maana wameamua kukamata mifugo inayotoka nchi jirani na kuchukua hatua za kisheria.
Alisema hata ikitokea nchi jirani wakishika mifugo kutoka Tanzania, wachukue hatua za kisheria za nchi hizo.
Pia aliwataka wananchi wa Mkoa wa Kagera kuacha tabia ya kuvamia maeneo ya hifadhi, ikiwamo Hifadhi ya Pori la Burigi.
“Kuna walanguzi walipewa ranchi 54 wamekaa nazo na wanakodisha kwa wengine tu, hawajaziendeleza, nitawafukuza na kuwapatia watu wengine wanaoweza kuziendeleza,” alisema.

ATAMSHANGAA MWIJAGE
Alisema hadi sasa viwanda vipya 3,306 vimeanzishwa nchini na kusisitiza kuwa dhana ya Tanzania ya viwanda maana yake anamaanisha vijengwe nchi nzima.
“Kuna viwanda vipya 3,306, sina uhakika Kagera mna viwanda vingapi. Nitashangaa sana niwe na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji halafu kwenye mkoa anaotoka hakuna hata kiwanda.
“Leta viwanda huku nako ni Tanzania mimi sitasema umejipendelea… weka hata kiwanda cha Lubisi,” alisema.

WAZIRI WA UJENZI
Awali Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, alisema ujenzi wa uwanja huo umegharimu Sh bilioni 31.95 na kati ya fedha hizo, zilizotolewa na Serikali ni Sh bilioni 6.35 na nyingine Sh bilioni 25 zimetolewa na Benki ya Dunia.
Alisema Serikali ilikopa WB Dola za Marekani milioni 57.5 ambazo zimefanikisha ukarabati na ujenzi wa viwanja vya Bukoba, Tabora, Kigoma na kuhamisha Shule ya Msingi Tumaini iliyokuwa jirani na uwanja wa Bukoba.
“Katika miradi yote hii, fedha za Serikali ni Dola za Marekani milioni 11.7 na fedha zingine zimetumika kufanya upembuzi yakinifu katika viwanja 11 nchini. Uwanja wa Bukoba utatumika mwaka mzima katika majira yote,” alisema Profesa Mbarawa.
Alisema pia katika bajeti ya mwaka 2017/18, wametenga fedha kufanya upembuzi yakinifu na ukarabati wa viwanja vya Iringa, Musoma na Songea na kwamba zabuni zimeshatangazwa.

Trump ziarani Korea kusini

Kiongozi wa Korea kusiniHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionKiongozi wa Korea kusini
Rais wa Marekani Donald Trump amewasili Korea ya kusini ikiwa ni sehemu ya ziara yake mashariki mwa Asia.
Katika mtandao wake wa Twitter, Rais Trump amemuelezea Rais wa Korea kusini Moon Jae-in kama mtu mwema na kusema kuwa watafanya kazi pamoja kuweza kushughulikia kitisho cha nyuklia kutoka Korea kaskazini.
Awali Rais Trump alielezea mbinu ya Rais Huyo wa Korea Kusini ambayo ni mbinu shirikishi dhidi ya Korea ya Kaskazini kama ya makubaliano na kwamba raia wa Korea Kusini walikuwa na wasiwasi na kauli za mabavu za Rais Trump kwamba zinaweza kuifanya Korea ya Kaskazini kuchukua hatua za kijeshi katika eneo hilo ya rasi.

Kipimo cha pumzi kugundua Malaria chaonyesha matumaini

Kipimo cha pumzi kugundua Malaria chatoa matumainiHaki miliki ya pichaWASHINGTON UNIVERSITY
Image captionKipimo cha pumzi kugundua Malaria chatoa matumaini
Watu wanaougua ugonjwa wa malaria sasa watalazimika kupimwa kwa kutumia pumzi zao kulingana na wanasayansi wa Marekani.
Tayari walikuwa wametumia mfano wa kifaa cha kutumia pumzi barani Afrika, mkutano wa dawa za kitropiki ulielezewa.
Kifaa hicho kilionekana kuwa imara katika kuwapima watoto lakini kitahitaji kuimarishwa zaidi ili kutumiwa mara kwa mara.
Miongoni mwa harufu inazotoa ni sawa na ile inayowavutia wadudu wanaosambaza ugonjwa wa malaria.
Miti aina ya Pine na ile ya Conifers hutoa harufu hiyo ili kuwavutia mbu pamoja na wadudu wengine kulingana na watafiti kutoka chuo kikuu cha Washington mjini St. Louis .
Wanaamini kwamba watu wanaougua ugonjwa wa malaria ambao hutoa harufu hiyo wakati wanapopumua pia wao huvutia mbu na kuwaambukiza wadudu hao wanapowauma, hatua ambayo hupelekea kusambazwa kwa ugonjwa huo na mbu.
Ijapokuwa kipimo hicho kinahitaji kuimarishwa, kinaweza kutoa mwelekeo mpya na rahisi wa kuugundua ugonjwa huo, profesa Audry Odom John na wenzake wanasema.
Kipimo hicho cha kutumia hewa ya mtu anapopumua kinaweza kugundua harufu sita tofauti ili kubaini visa vya malaria.Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionKipimo hicho cha kutumia hewa ya mtu anapopumua kinaweza kugundua harufu sita tofauti ili kubaini visa vya malaria.
Kipimo hicho cha kutumia hewa ya mtu anapopumua kinaweza kugundua harufu sita tofauti ili kubaini visa vya malaria.
Watafiti hao walijaribu sampuli kadhaa za vipimo hivyo kutoka kwa watoto 35 wenye homa nchini Malawi wengine wakiwa na malaria wengine wakiwa bila ugonjwa huo.
Kilitoa vipimo sawa miongoni mwa watoto 29, ikimaanisha kiliweza kufanikiwa kwa asilimia 83.
Hatahivyo Matokeo hayo ni ya chini sana kwa kifaa hicho kutumika mara kwa mara , lakini watafiti wana imani kwamba wanaweza kukiimarisha na kuanza kuuzwa madukani.

Saudia yadai Iran ilihusika katika shambulio la kombora

Hatua hiyo inaimarisha hatua ya mwanamfalme Mohammed bin SalmanHaki miliki ya pichaEPA
Image captionHatua hiyo inaimarisha hatua ya mwanamfalme Mohammed bin Salman
Saudia imeongeza mashambulizi yake ya maneneo shidi ya Iran na washirika wake.
Imelishutumu kundi la wapiganaji wa Lebanon Hezbollah kwa vitendo vya uchokozi ambavyo imevitaja kuwa tangazo la vita.
Riyadh pia imeilaumu Tehran kwa shambulio la kombora siku ya Jumamosi lililolenga mji mkuu wa Saudia ambalo lilitekelezwa na waasi wa Houthi mjini Yemen.
Iran imekana madai hayo ikisema kuwa ni uchokozi wa kivita wa Saudia ambao unatishia amani katika eneo la mashariki ya kati.
Marekani imesema kuwa inaunga mkono msimamo wa Saudia dhidi ya Iran.
Rais Trump ambaye yuko mashariki mwa bara Asia pia alichapisha ujumbe wa Twitter akisema kuwa ana matumaini na hatua zinazochukuliwa na mfalme Salman na mwanamfalme Mohammed kukabiliana na ufisadi katika ufalme huo.
Siku ya Jumatatu mwanasheria mkuu wa Saudia alisema kuwa kukamatwa kwa wafanyikazi wakuu wa ufalme huu wiki hii ikiwemo mawaziri na wafanyibiashara ulikuwa mwanzo tu wa vita dhidi ya ufisadi.

Mpiga picha akamatwa Kenya akipiga picha shamba la Rais Kenyatta

Uhuru KenyattaHaki miliki ya pichaAFP
Image captionUhuru Kenyatta
Mpiga picha mmoja wa shirika la kimataifa amekamatwa na kushtakiwa mahakamani Jijini Nairobi, baada ya 'kuzuru shamba la Kenyatta' bila idhini.
Shirika la habari la AFP, limesema kwamba, mpiga picha wake mkuu wa Afrika Mashariki, amefikishwa Jumatatu mahakamani nchini Kenya na kushtakiwa kwa kosa la kuingia kwenye shamba linalomilikiwa na familia ya Rais Uhuru Kenyatta.
Mpiga picha huyo raia wa Japan Yasuyoshi Chiba, mwenye umri wa miaka 46, alikamatwa siku ya Ijumaa kwenye shamba la kampuni ya maziwa ya Brookside dairy, inayomilikiwa na familia ya Rais wa kwanza wa Kenya na wa sasa Bw. Uhuru Kenyatta.
Alikuwa amekwenda huko kupiga picha ya nembo ya kampuni hiyo ya maziwa, baada ya muungano wa upinzani nchini humo-NASA, kutoa wito wa kususiwa kwa bidhaa zote za vigogogo wakuu wa chama tawala cha Jubilee zikiwemo bidhaa za Brookside, kufuatia kumalizika kwa uchaguzi mkuu enye utata wa Urais.

Magufuli: Tanzania sio shamba la kuchungia mifugo wa taifa jirani

Rais Magufuli amesema kuwa Tanzania sio shamba la kuchungia mifugo ya taifa jirani
Image captionRais Magufuli amesema kuwa Tanzania sio shamba la kuchungia mifugo ya taifa jirani
Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli amesisitiza kuwa serikali yake itaendelea kuwakamata mifugo watakaoingia nchini humo kutoka taifa jirani.
Akizungumza katika mkoa wa Kagera ambako ameanza ziara yake ya kikazi Magufuli amesema kwamba Tanzani sio shamba la kuchungia mifugo ya nchi jirani na kwamba ataichukulia mifugo hatua kali za kisheria mifugo yoyote.
Vilevile ameitaka nchi Jirani kuchukua hatua kama hiyo iwapo mifugo ya Tanzania itaingia nchini humo kinyume na sheria.
Tanzania kuwapiga mnada zaidi ya ng'ombe 1000 kutoka Kenya
"Tanzania sio shamba la kuchungia mifugo ya nchi jirani, ndio maana tumeamua kukamata mifugo na kuchukua hatua kwa mujibu wa kisheria, na hata huko kwenye nchi jirani wakishika mifugo ya kutoka Tanzania wachukue hatua za kisheria za nchi hizo" alisisitiza rais Magufuli.
Matamshi hayo ya Magufuli yanajiri wakati ambapo kumekuwa na mgogoro wa mpakani mwa Kenya na Tanzania kuhusu mifugo katika siku za hivi karibuni.
Wafugaji wa Kenya wapata hasara kwa kuingiza ngombe zao Tanzania
Wiki tatu zilizopita serikali ya Tanzania ilizikamata zaidi ya ng'ombe 1000 kutoka Kenya na baadaye mahakama moja nchini humo ikaamuru mifugo hao kupigwa mnada na fedha hizo kutumiwa na serikali iwapo wamiliki wa ng'ombe hizo watashindwa kulipa faini ya shilingi milioni 500 za Tanzania.
Mifugo ya jamii ya Maasai nchini Kenya
Image captionMifugo ya jamii ya Maasai nchini Kenya
Na wiki moja iliopita takriban ng'ombe 4000 kutoka Tanzania zilidaiwa kupatikana katika jamii moja ya Maasai mjini kajiado.
Hivi majuzi hatua ya taifa la Tanzania kuwachoma kuku 6,400 kutoka Kenya wenye thamani ya shilini milioni 12 za Tanzania kwa madai kwamba wangesambaza ugonjwa wa homa ya ndege ilizua hizo tofauti kutoka kwa watetezi wa wanyama .
Afisa mkuu wa maswala ya mifugo nchini Tanzania Obedi Nyasembwa alisema kuwa kuku hao waliingizwa nchini humo kinyume na sheria na kwamba uwpo wao nchini humo ulikuwa hatari kwa ndege wengine.
Vifaranga wa kuku 6,400 wenye thamani ya zaidi ya dola 5,000 wamechomwa moto Tanzania
Kuku hao wa siku moja walikamatwa katika eneo la Namanga huku mfanyibishara wa Tanzania akikamatwa.
Baadaye mamlaka ya Tanzania iliwamwagia mafuta na kuwachoma kulingana na gazeti la mwananchi.
Aidha rais Magufuli amewaagiza viongozi wa Kagera kuhakikisha kuwa mifugo yao inawekwa alama kwa mujibu wa sheria, ili kurahisisha utambuzi wa mifugo inayoingizwa nchini kutoka nchi jirani na pia kudhibiti ruzuku inayotolewa na Serikali kwa dawa za mifugo za hapa nchini.
Kuku hao wa siku moja walikamatwa katika eneo la Namanga huku mfanyibishara wa Tanzania akikamatwa.
Image captionKuku hao wa siku moja walikamatwa katika eneo la Namanga huku mfanyibishara wa Tanzania akikamatwa.
Hata hivyo amewataka wananchi wa Kagera kuacha kuvamia maeneo ya hifadhi ikiwemo hifadhi ya Burigi na ameagiza viongozi wa Wilaya ya Muleba kufuatilia madai ya wananchi juu ya kuuzwa kwa ardhi ya kijiji hatu iliosababisha wananchi kukosa maeneo ya kulima na kulisha mifugo yao.
"Na kuna watu waliouziwa ranchi na Serikali, watu hao hawajaziendeleza ranchi hizo na badala yake wanawakodisha wananchi, wafuatilieni na mkiona hawajaziendeleza nyang'anyeni muwape wananchi wazitumie kwa ufugaji, lakini pia hakikisheni wananchi hawavamii maeneo ya hifadhi yaliyotengwa" aliongeza Magufuli

Mwanamke afutwa kazi kwa kuuonyesha msafara wa Trump kidole cha kati

Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 50 anasema kuwa hajuti kufutwa kaziHaki miliki ya pichaAFP/GETTY
Image captionMwanamke huyo mwenye umri wa miaka 50 anasema kuwa hajuti kufutwa kazi
Mwanamke aliyepigwa picha akiuonyesha msafara wa rais Donald Trump ishara ya kidole cha kati ameripotiwa kufutwa kazi na kampuni iliomuajiri kufutia picha hiyo.
Picha hiyo ilisambazwa baada ya kupigwa mnamo terehe 28 mwezi Oktoba mjini Virginia karibu na uwanja wa kucheza Gofu wa Trump.
Juli Briskman ambaye alitambulika kama mwendesha baiskeli anadai kwamba alifutwa kazi na mwajiri wake Akima LLC baada ya kuichapisha katika mtandao wake.
Kampuni hiyo hatahivyo haikutoa tamko lolote ilipotakiwa kufanya hivyo na BBC.
Bi Briskman aliambia vyombo vya habari kwamba kampuni hiyo ilimuita katika mkutano siku moja baada ya kumwambia afisa mkuu wa ajira kwamba ni yeye ndiye aliyepiga picha hiyo.
Trump alivyomkaribisha mfuasi jukwaani Florida
Alilimbia gazeti la Huffington Post kwamba maafisa wakuu wa kampuni hiyo walimwambia kwamba picha hiyo imeorodheshwa kama chafu na kwamba ilikiuka viwango vya sera za mitandao baada ya kuichapisha katika akaunti zake za Twitter na facebook.
Hatahivyo bi Briskman alisema kuwa aliusisitizia usimamizi wa kampuni hiyo kwamba hakuwa akifanya kazi wakati picha hiyo ilipopigwa na kwmaba hakuwataja waajiri wake katika mtandao huo wa kijamii.
Bi Briskman anasema kuwa mwenzake wa kiume hakufutwa kazi baada ya kufuta picha iliodaiwa kuwa chafu katika kisa chengine.
Pingamizi dhidi ya misafara sio jambo lisilo la kawaida, kwnai picha hii iliopigwa na Mike Smialowsk ilipigwa siku hiyohiyoHaki miliki ya pichaAFP/GETTY
Image captionPingamizi dhidi ya misafara sio jambo lisilo la kawaida, kwnai picha hii iliopigwa na Mike Smialowsk ilipigwa siku hiyohiyo
Hivyobasi amekuwa akihoji ni kwa nini alifutwa kazi mara moja.
Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 50 ambaye ana watoto wawili ameripotiwa kufanya kazi katika kampuni hiyo ya serikali kwa miezi sita akifanya kazi ya mawasiliano.