Friday, May 18

'Amali Za Kutenda Na Ya Kujiepusha Nayo Katika Mwezi Mtukufu Wa Rajab

Nasiha Za Minasaba Mbalimbali AlhamduliLLaah. Inapasa tumshukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Kutupa umri hadi kutufikisha mwezi mtukufu wa Rajab ambao ni fursa kwetu kutenda mema yatakayotuchumia thawabu nyingi kuliko miezi mingine. Mema ambayo hatuna budi kuyatenda kwa ajili ya kujenga Aakhirah yetu kabla ya siku hii kufika. Siku ambayo hakuna mmoja wetu yeyote atakayeweza kuikwepa. Basi hebu kila mmoja wetu ajiulize: "Nimetanguliza nini kwa ajili ya siku hiyo?" Siku ambayo safari yake ni ndefu mno. Vyovyote tutakavyobeba kama ni zawadi huko Aakhirah, hazitoshi wala hatuna hakika nazo kama zitapendekezeka au zitakuwa na thamani huko tuendako ambako kuna makazi ya milele tusiyokuwa na hakika nayo; ima moto au Pepo. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala): (( يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّهَ وَلْتَنظُرْ نَفْسٌ مَّا قَدَّمَتْ لِغَدٍ وَاتَّقُوا اللَّهَ إِنَّ اللَّهَ خَبِيرٌ بِمَا تَعْمَلُونَ)) ((Enyi mlioamini! Mcheni Allaah, na kila nafsi iangalie inayoyatanguliza kwa ajili ya Kesho. Na mcheni Allaah, Hakika Allaah, Anazo khabari ya mnayoyatenda)) [Al-Hashr: 18]. Vile vile ni miezi miwili tu imebakia kutufikia mgeni wetu tunayemsubiri kwa hamu kila mwaka, mwezi mtukufu wa Ramadhaan. Kwa hiyo ni fursa nyingine pia kujitayarisha kuupokea mwezi huo kwa kujizoesha ibada mbali mbali kama Swawm, tahajjud, na pia kutenda mema mengi ili tutakapofikia mwezi wa Ramadhaan tuwe na nguvu za kufanya zaidi ya tuliyoyazoea kutenda katika miezi hii iliyobakia miwili ijayo. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala): (( إِنَّ عِدَّةَ الشُّهُورِ عِندَ اللّهِ اثْنَا عَشَرَ شَهْرًا فِي كِتَابِ اللّهِ يَوْمَ خَلَقَ السَّمَاوَات وَالأَرْضَ مِنْهَا أَرْبَعَةٌ حُرُمٌ ذَلِكَ الدِّينُ الْقَيِّمُ فَلاَ تَظْلِمُواْ فِيهِنَّ أَنفُسَكُم )) ((Hakika idadi ya miezi kwa Allaah ni miezi kumi na mbili katika hukumu ya Allaah, tangu Alipoumba mbingu na ardhi. Katika hiyo iko mine mitakatifu. Hiyo ndiyo Dini iliyo sawa. Basi msidhulumu nafsi zenu humo)) [At-Tawbah: 36] Miezi minne hiyo imetajwa katika Hadiyth ifuatayo: عَنْ أَبَى بَكْرَة أَنَّ رَسُول اللَّه - صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ - قَالَ فِي حَجَّة الْوَدَاع : (( إِنَّ الزَّمَان قَدْ اِسْتَدَارَ كَهَيْئَتِهِ يَوْم خَلَقَ اللَّه السَّمَوَات وَالْأَرْض السَّنَة اِثْنَا عَشَر شَهْرًا مِنْهَا أَرْبَعَة حُرُم : ثَلَاث مُتَوَالِيَات ذُو الْقَعْدَة وَذُو الْحِجَّة وَالْمُحَرَّم وَرَجَب مُضَر الَّذِي بَيْن جُمَادَى وَشَعْبَان)) صَحِيح الْبُخَارِيّ Kutoka kwa Abu Bakrah ambaye amesema: "Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa wa sallam) amesema alipokuwa katika Hijjah ya kuaga (Hijjah wa mwisho): ((Mgawanyo wa nyakati umerudi kama ulivyo (wakati) Allaah Alipoumba mbingu na ardhi. Mwaka una miezi kumi na mbili, minne ambayo ni mitukufu; mitatu inafuatana pamoja (nayo ni) Dhul-Qa'adah, Dhul-Hijjah na Muharram, na (wa nne ni) Rajab wa (kabila la) Mudhwar ambao upo baina ya Jumaada na Sha'abaan)) [Al-Bukhaariy] Katika miezi yote kumi na mbili Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Ameichagua hii minne na Ameifanya kuwa ni mitukufu na kusisitiza kuitakasa, na kwamba dhambi zitakazofanyika humo ni zaidi na hali kadhalika thawabu za vitendo vyema zinakuwa maradufu na zaidi. [Atw-Twabariy 14: 238] Ni sawa kama Anavyoonya Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) kufanya maasi katika sehemu tukufu Alipotaja Masjidul-Haraam (Msikiti Mtukufu Makkah): ((إِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا وَيَصُدُّونَ عَن سَبِيلِ اللَّهِ وَالْمَسْجِدِ الْحَرَامِ الَّذِي جَعَلْنَاهُ لِلنَّاسِ سَوَاء الْعَاكِفُ فِيهِ وَالْبَادِ وَمَن يُرِدْ فِيهِ بِإِلْحَادٍ بِظُلْمٍ نُذِقْهُ مِنْ عَذَابٍ أَلِيمٍ)) ((Hakika wale waliokufuru na wakazuilia Njia ya Allaah na Msikiti Mtakatifu, ambao tumeufanya kwa ajili ya watu wote sawasawa, kwa wakaao humo na wageni. Na kila atakayetaka kufanya upotofu humo kwa dhulma, basi Tutamwonjesha adhabu iumizayo)) [Al-Hajj: 25] Qataadah amesema kuhusu kauli ya Allaah: (( فَلاَ تَظْلِمُواْ فِيهِنَّ أَنفُسَكُم)) ((Basi msidhulumu nafsi zenu humo)) "Dhulma itakayotendeka katika miezi mitukufu ni mbaya na kubwa (au hatari) kuliko dhulma itakayotendeka katika miezi mingine. Hakika dhulma daima ni makosa, lakini Allaah Hufanya baadhi ya vitu kuwa ni vizito kuliko vingine kama Anavyopenda". Akaendelea kusema: "Allaah Amechagua baadhi ya viumbe Vyake na baadhi ya vitu kuwa bora zaidi kuliko vingine. Amechagua Wajumbe kutoka Malaika na kutoka binaadamu. Vile vile Amechagua baadhi ya kauli Zake kuwa ni bora kuliko nyingine, Misikiti kuwa bora kuliko sehemu nyingine za ardhi, Ramadhaan na miezi mitukufu kuwa bora kuliko miezi mingine, siku ya Ijumaa kuwa ni bora kuliko siku nyingine, na usiku wa Laylatul-Qadr kuwa ni bora kuliko masiku mengine. Kwa hiyo takasa vile Alivyovitakasa Allaah, kwani kufanya hivyo ni vitendo vya watu wenye akili na wenye kufahamu" [Tafsiyr ya Ibn Kathiyr] Miongoni mwa yaliyokatazwa katika miezi hii mitukufu ni kama Anavyosema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala): (( يَسْأَلُونَكَ عَنِ الشَّهْرِ الْحَرَامِ قِتَالٍ فِيهِ قُلْ قِتَالٌ فِيهِ كَبِيرٌ وَصَدٌّ عَن سَبِيلِ اللّهِ وَكُفْرٌ بِهِ وَالْمَسْجِدِ الْحَرَامِ وَإِخْرَاجُ أَهْلِهِ مِنْهُ أَكْبَرُ عِندَ اللّهِ وَالْفِتْنَةُ أَكْبَرُ مِنَ الْقَتْلِ )) ((Wanakuuliza juu ya kupigana vita katika mwezi mtakatifu. Sema: Kupigana vita wakati huo ni dhambi kubwa Lakini kuzuilia watu wasiende katika Njia ya Allaah na kumkanusha Yeye, na kuzuilia watu wasiende kwenye Msikiti Mtakatifu na kuwatoa watu wake humo, ni makubwa zaidi mbele ya Allaah. Na fitina ni mbaya zaidi kuliko kuua..))[Al-Baqarah: 217] Hivyo basi katika mwezi mtukufu wa Rajab, maasi na mema yafuatayo yanatupasa kuzingatia: Maasi Mengine Ambayo Tunatakiwa Tujikumbushe Kuyaacha: - Kuiba; - Kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) kama kwenda kwa wachawi na waganga na kuwaamini wanayoyatabiri kwa watu; - Kuzini; - Kulewa; - Kumdhulumu mtu haki yake; - Kugombana, kutukanana, kuvunjiana heshima, kudharauliana n.k.; - Kusengenya (Ghiybah); - Kusema uongo, na kila aina ya uovu mwengine. Mambo Mema Ya Kukumbushana Kufanya Katika Mwezi Huu Mtukufu - Kuongeza Sunnah za Swalah; *(tazama maelezo chini) - Kufunga Swawm za Sunnah kama Jumatatu na Alkhamiys, Masiku meupe (Ayyaamul-biydhw) (tarehe 13, 14 na 15) na Swawm ya Nabii Daawuud (kufunga kila baada ya siku moja); - Kujielimisha mambo ya Dini kwa kusoma vitabu na kusikiliza mawaidha; - Kuomba Maghfirah na Tawbah; - Kufanya kila aina ya dhikr (kumkumbuka na kumtaja Allaah), kwa kusoma Qur-aan kwa wingi, kumshukuru, kumtukuza, kuomba du'aa n.k.; - Kuwasiliana au kutembeleana na ndugu na jamaa; - Kutenda wema kwa jirani, marafiki na watu wote kwa ujumla; - Kutoa sadaka; - Kulisha masikini; - Kupatanisha waliogombana; - Kuamrishana mema na kukatazana maovu, na mengi mengineyo katika vitendo vyema. * Swalah za Sunnah Ratiba Ya Swalah Za Sunnah Zilizosisitizwa Na Zisizosisitizwa ALFAJIRI Kabliya Rakaa 2 ADHUHURI Kabliya Rakaa 4 Baadiya Rakaa2 ALASIRI Kabliya Rakaa 4 MAGHARIBI Kabliya Rakaa 2 Baadiya Rakaa 2 'ISHAA Kabliya Rakaa 2 Baadiya Rakaa 2 Fadhila Zake: (( مَا مِنْ عبْدٍ مُسْلِم يُصَلِّي للَّهِ تَعَالى كُلَّ يَوْمٍ ثِنْتَيْ عشْرةَ رَكْعَةً تَطوعاً غَيْرَ الفرِيضَةِ ، إِلاَّ بَنَى اللَّه لهُ بَيْتاً في الجَنَّةِ ، أَوْ : إِلاَّ بُنِي لَهُ بيتٌ في الجنَّةِ )) رواه مسلم * ((Hatoswali mja Rakaa 12 zisizo za fardhi kwa siku, ila atajengewa [na Allaah] nyumba peponi)) [Muslim] Nazo ni hizo Muakkadah (Zilosisitizwa) jumla yake ni 12 (( ركْعتا الفجْرِ خيْرٌ مِنَ الدُّنيا ومَا فِيها )) رواه مسلم ** ((Rakaa mbili (za Sunnah) kabla ya Alfajiri ni kheri kuliko duniya na yaliyomo ndani yake) [Muslim] ‏‏((ما من عبد يسجد لله سجدة إلا كتب الله له بها حسنة ومحا عنه بها سيئة ورفع له بها درجة فاستكثروا من السجود)) رواه ابن ماجه ((Mja yeyote atakayesujudu sijda moja ataandikiwa wema mmoja, na atafutiwa baya moja, na atapandishwa daraja yake, kwa hiyo zidisheni kusujudu)) [Ibn Maajah] Swalah ya Tahajjud (( أفضل الصلاة بعد الفريضة صلاة الليل)) رواه مسلم ((Swalah iliyo bora kabisa baada ya Fardh ni Swalah ya usiku)) [Muslim] Swalah Ya Dhuhaa na Swalah Ya Witr عـَن أبي هـُريْرَة رضيَ الله عنه قال : أوصـَانـِي خـَليلي صـَلـَّى الله عليه وسلم بـِصـِيامِ ثـَلاثـَة ِ أيـَّام ٍ مـِنْ كـُل شـَهر ٍ، وَ ركـْعـَتي الضـُّحى ، وأنْ أوتـِرَ قبلَ أنْ أرقـُـد " ـ متفق عليه ـ Kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ‘anhu) kwamba “Ameniusia rafiki yangu Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam [mambo matatu]; kufunga siku tatu katika kila mwezi, Rakaa mbili Dhuhaa na niswali Witr kabla ya kulala” [Al-Bukhaariy na Muslim] Tunamuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Atuwezeshe kujitenga na maasi na kuzidisha mema katika mwezi huu mtukufu na Atufikishe Ramaadhaan. Aamiyn

Wednesday, May 16

Mzee Makamba awarushia kombora Nape, Pinda

Midraji Ibrahim, Dodoma BAADA ya ukimya wa muda mrefu, Katibu Mkuu mstaafu wa CCM, Yusuf Makamba ameibuka katika kikao cha Halmashauri Kuu ya chama hicho (Nec) na kumtuhumu Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye kwamba amekigeuza chama kuwa mali yake binafsi. Taarifa kutoka ndani ya kikao hicho, zimesema kwamba Makamba alisema hatua ya Nape kugeuza chama hicho kama taasisi yake binafsi ndiyo ambayo imesababisha kikose mwelekeo. Makamba licha ya kuelekeza mashambulizi yake kwa Nape, alimrushia pia kombora Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kuwa ana uhusiano mdogo na wananchi. “Mzee (Makamba) amesema hivi sasa CCM imekuwa kama jogoo anayepelekwa kwa mganga, kila anakoelekezwa ndo huko, hali hiyo ndiyo inakikumba CCM hivi sasa. Amemweleza Nape kuwa amegeuza chama kama mali yake binafsi, anafanya mambo nje ya utaratibu na anaangaliwa tu.” Makamba alidai kuwa badala ya sekretarieti kushughulikia matatizo ya chama, imekuwa ikihangaika na watu kwa sababu ya kutofautiana nao misimamo na wakati huo wakijidai kuzika tofauti ili kukiimarisha. Nape alipoulizwa kuhusu suala hilo alipuuza na kusema: “Si kweli, lakini ninyi andikeni tu maana tumewazoea.” Alipotakiwa kueleza kama Kingunge na Makamba walisema nini dhidi yake katika kikao cha Nec alijibu: “Walikuwapo, lakini hakuna kati yao aliyenitaja hata kwa jina.” Nape alitumia muda mwingi kulalamika kuwa taarifa nyingi ambazo zimekuwa zikitolewa kutoka ndani ya mkutano huo uliomalizika jana zimetoka kwa watu aliowataja kuwa wana maslahi nazo binafsi na kuhoji,” Kwa nini msiwe mnasubiri taarifa rasmi (za chama) ili habari iwe ya ukweli zaidi?” Mkongwe mwingine wa chama hicho, Kingunge Ngombale-Mwiru, ambaye anadaiwa kusikitishwa na vitendo vya rushwa na ugomvi vinavyoendelea ndani ya chama huku vikiangaliwa na viongozi kama vile vinakistawisha wakati vinakiporomosha. Kingunge alidai kuwa hivi sasa chama hicho kimetawaliwa na matajiri ambao ndiyo wanaopata nafasi za uongozi na maskini wanawekwa kando. Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Hamis Mgeja aliunga mkono suala la Pinda kuwa na uhusiano mdogo na wananchi na kwamba, amekuwa mkimya zaidi na hamsaidii Rais Jakaya Kikwete. “Yule Mwenyekiti wa Shinyanga, amemweleza Pinda kuwa ng’ombe wakila mazao mtu wa kwanza kuchapwa viboko ni mchungaji, halafu mmiliki anatozwa faini baadaye. Hivyo, alitakiwa kuwajibika kwanza kabla ya mawaziri walioondolewa,” kilidokeza chanzo chetu. Mgeja alidai kuwa uwajibishwaji wa mawaziri, haukuzingatia haki kwa sababu George Mkuchika, Profesa Jumanne Maghembe na Hawa Ghasia walilalamikiwa, lakini kilichofanywa ni kutoa kafara wengine na hao kubadilishiwa wizara. Pia, inadaiwa kuwa Mwenyekiti Kikwete aliwataka wajumbe kuzika tofauti zao ili kuweka msimamo wa pamoja kwa ajili ya ushindi kwenye Uchaguzi Mkuu ujao wa 2015 na kwamba adui namba moja wa CCM hivi sasa ni Chadema. Rushwa yakishtua chama Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye alisema Nec imejadili changamoto zinazokikabili chama kwenye uchaguzi unaoendelea na kubaini kuwa rushwa imekithiri. Nape alisema tishio la rushwa ni kubwa na mgombea atayakayethibitika kujihusisha na vitendo hivyo rushwa ataondolewa mara moja, huku viongozi na watendaji wakitahadharishwa kuchukuliwa hatua za nidhamu. “Kwa kisingizio cha kuwasalimia wajumbe, kuwapa nauli au kujitambulisha. Mgombea atakayethibitika anazunguka au amezunguka ataondolewa bila kuchelewa katika orodha ya wagombea,” alisema na kuongeza: “Kwa watendaji na viongozi wa chama ngazi zote kuanzia sasa ni marufuku kuwatembeza ndani ya maeneo yao, kwa nia ya kuwatambulisha kwa wapiga kura. Mtendaji au kiongozi atakayebainika anakiuka agizo hili, atachukuliwa hatua za nidhamu mara moja.” Pia, Nape alisema kuanzia sasa ni marufuku kwa watendaji na viongozi wa chama ngazi zote kuwaitia wagombea, wajumbe wa mikutano ya uchaguzi kwa lengo lolote, kwani vikao vya aina hiyo havimo katika katiba. Alisema vikao vya aina hiyo ni haramu na vinapalilia rushwa na kuongeza kwamba wanachama wa CCM wanatakiwa kupiga vita rushwa na kutoa taarifa ya vitendo hivyo katika ofisi za chama na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru). Aliitaka Takukuru kutomuonea aibu au kumuogopa mtu anayejihusisha na vitendo vya rushwa badala yake wamchukulie hatua. Mishahara na chakula Kuhusu mishahara ya watumishi wa umma na mfumuko wa bei ya chakula, Nape alisema Nec imeagiza Serikali kuhimiza waajiri kupandisha mishahara na malipo mengine kwa wafanyakazi wao ili waweze kumudu gharama za maisha. Alisema gharama za maisha zimepanda na mishahara inayolipwa haiendani na hali halisi. Alisema nayo Serikali inatakiwa nayo kupandisha mishahara kwa watumishi wake. “Serikali idhibiti malipo ya huduma ya ndani kwa kutumia fedha za kigeni, hasa Dola ya Marekani. Pia, iongeze udhibiti wa maduka na hoteli zinazofanya biashara ya fedha za kigeni ili kuondoa hujuma kwa uchumi wa nchi inayofanywa kutokana na uhuru uliokithiri katika biashara hii,” alisema. Nape alisema Serikali inatakiwa kuweka jitihada zaidi za kudhibiti ulanguzi wa bidhaa muhimu na upandishaji holela wa bei za vyakula, kodi za nyumba na usafiri. Alisema Nec imeagiza Serikali kuendelea kuchukua hatua za muda mrefu na kati za kukabiliana na tatizo la mfumuko wa bei. “CCM inaiagiza Serikali kuchukua hatua za haraka na muda mfupi ikiwamo kuangalia upya baadhi ya kodi katika vyakula pamoja na Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) katika sukari,” alisema Nape. Pia, Nape alisema wameagiza Serikali kupitia upya utaratibu wa ruzuku ya mbegu na mbolea ili upanuliwe kunufaisha wakulima wengi. Alisema Nec imeitaka Serikali iongeze kasi ya utekelezaji wa mpango wake wa kuongeza uwezo wa kuhifadhi chakula nchini, hasa kupitia Mamlaka ya Hifadhi ya Nafaka ya Taifa (NFRA), ikiwamo kujenga maghala zaidi ya mazao ya chakula maeneo ya uzalishaji na kutenga fedha nyingi zaidi kwa ununuzi wa mazao hayo. “Wakati wa uhaba wa vyakula maeneo ya mijini, kasi ya kupeleka chakula maeneo hayo iongezwe na utaratibu mzuri zaidi wa usambazaji chakula utumike ili walaji na siyo wasafirishaji na wasindikaji, wanufaike,” alisema.

Monday, May 14

Losing Jerusalem

Visiting Jerusalem is up for debate now, and it's good that it is being taken up and understood now. The question is not whether to visit Jerusalem or not, rather it is visiting it under Israeli's occupation. Islamic scholars have different opinions on this, all of which are respected. Let's look at it from the religious perspective first. Jerusalem has always been a sacred place as mentioned in the Holy Quran "... to Masjid Al-Aqsa, whose surroundings we have blessed..." (17:1). It is the land of prophets all of whom are revered and respected. This mosque is the place where all the prophets (May Allah be pleased with them all) met on the night of Isra. When the Holy prophet (PBUH) migrated to Madinah, the Muslims prayed in its direction for more than one and a half year. Being host to the third holiest place of Islam, Jerusalem is equally dear to Muslims, as it is for Jews and Christians. The holy Prophet (PBUH) has specifically mentioned Al-Aqsa Mosque to be visited along with the ones in Makkah and Madinah. So it's more important for Muslims to try and visit there if conditions allow. Though under Israeli occupation, we can still go there via Jordan. According to some scholars, it's like recognizing Israel, and they have a valid point too - in accepting the norms and procedures formed by the occupying Israeli government. But let's look at the other side as well. All these decades we have been "not recognizing Israel", but have also been losing an opportunity to visit Al-Quds. So just by going there, do we "recognize Israel"? No, as long as you are just going to fulfill your religious duty. We have the treaty of Hudaibiyah as an example, where the holy Kaabah was still in control of the Quraysh, but the Prophet (PBUH) and his companions made a pact with them, stayed in Makkah for three days and performed their pilgrimage. Did they recognize the Quraysh's ownership of the Kaabah? Definitely not.
Babri Masjid as it stood once in India Now coming to the political and strategic aspect - Israel has long been trying to drive out all the Palestinians from the remaining lands they hold. And it has been blocking all attempts to even talk of return of refugees to their own country. The only aim is to declare and let the whole world accept Israel as a Jewish state. More importantly there have been concerted efforts to Judaize the surroundings of the Al-Aqsa Mosque. Now if Muslims continue to isolate Jerusalem and Al-Quds, just because its under Israel, will it not boost their efforts to Judaize the whole of Jerusalem? The more number of Muslims visiting Al-Aqsa, the more Islamic right it retains. Of course, the struggle against the Israeli occupation can continue, but the more we shun Jerusalem the stronger will be the Judaization of Jerusalem. If we are honest with ourselves and with the Palestinians, we really don't see even a rare chance of Israel returning back the occupied territories in decades to come. So how long will we be leaving Jerusalem alone? And what do we say about the Muslim countries who already have either full diplomatic ties with Israel or have some tacit (hand in glove) understanding with Israel? Refrain from them as well? An interesting example should be of significance here: The destruction of historic Babri Masjid in India at the hands of right wing Hindu fanatics. The controversy and court cases over this issue were in existence ever since the British rule in India. At one time a court declared the complex locked for both Hindus and Muslims. And after decades the locks were opened and Hindus given access to perform their worship, thereby reducing the Muslims' chances of winning back the right to offer prayers in the Masjid. One of the significant stands taken by right wing propaganda in the run up to opening the locks for Hindus was - "No Muslim prayers were offered there for so many decades, No Muslim ever entered there so it cannot be a Masjid".

Saturday, May 12

ELIMU YA MADRASA TANZANIA:

BISMILLAHIR RAHMANIR RAHIIM
Historia, Matatizo na Taaluma za Walimu
MUHTASARI:
- Madrasa na Kazi zinazonasibishwa nazo.
- Historia ya Elimu ya Madrasa Tanzania.
- Sahihisho kwa madrasah zetu.
- Taaluma muhimu kwa walimu na madrasah.
· Njia na mbinu zakufundishia.
· Uendeshaji wa Madrasah kwa ujumla.
· Saikolojia ya watoto na malezi.
· Maarifa katika fani wanazofundisha.

1.0 UTANGULIZI

1.1 Neno la Awali
Kwa muda mrefu sasa taasisi muhimu ya kiislam, taasisi ya “madrasa” imeachwa na kupoteza hadhi yake. Pamoja na hilo, taasisi hii imeacha pengo kubwa ambalo halizibiki kwa urahisi ila kwa kuinua hadhi ya Madrasa zetu.
Umma wa Waislam unazidi kupata kizazi kinachokosa haki za kimsingi za kuandaliwa kama madhalifa. Mwenyezi Mungu katika Qurani 51:56 ametwueleza “SIKU WAUMBA MAJINI NA WATU ILA WANIABUDU” ili kutekeleza lengo hilo, waislamu lazima waipe hadhi Madrasa. Kadhalika ili kufikia hadhi yetu wanaadam kama inavyoelezwa katika Quran 2:30 waislam lazima tuipe madrasah, hadhi yake sahihi. Kwa sababu hizo, kuna haja ya kufanya fikra juu ya kuinua hadhi ya madrasa zetu kwa ajili ya kuuendeleza umma wa kiislam utapotea na kuacha wanaoitwa Waislam lakini ummah wa kiislam haupo.

1.2 Maana ya Madrasa
Ilivyozoeleka, madrasa ni kituo cha kiislam ambapo watu hupata elimu juu ya mambo ya msingi katika uislam. Wengine wameita Shulel za Quran, wengine wamesema, vyuo vya Quran, na wengine wanaelewa kuwa madrasa ni vituo vya watoto ambapo masomo ya Quran, kusoma na kukandika hufundishwa.

1.3 Kazi zinazonasibishwa na Taasisi ya Madrasa
Madrasa zetu Tanzania, kwa muda mrefu tangu Historia ya kuingia kwa uislam nchini zimenasibishwa na kazi zinazofanywa na taasisi hii. Kwa ujumla madrasa zetu zimejikita katika taaluma zifuatazo:-
(i) Kuandika herfu za kiarabu.
(ii) Kuzisoma herfu za kiarabu.
(iii) Kutafsiri llugha ya kiarabu.
(iv) Kusoma Quran kwa ghaibu au kwa kutazamia.
(v) Jinsi ya kufanya ibada maalum na kanuni zake. Mfano, ibada, swala, swaum, hija na utoaji zakat na sadakat.

1.4 Athari za Madrasa kujikita katika shughuli hizo
Kwa kuwa Madrasa ni vituo vya elimu ya kiislam, na kwa vile madrasa zinaoa elimu hizo tu, basi elimu ya kiislam inafahamika kuwa ni ile tu inayohusiana na:
- Kusoma na kuandika Quran.
- Kukariri sura za Quran na tafsiri zake.
- Kanuni za utekelezaji wa nguzo tano.
- Kukariri hadithi kadhaa za Mtume (s.a.w).
- Kukariri visa vilivyo katikak lugha ya kiarabu.
Matokeo ya hilo, Uislam nao umeeleweka kukwa ni mambo ya kimaisha yanayohusiana na shughuli hizo tu. Nje ya shughuli hizo si vitu vya lazima katika uislam. Mfano kuksimamisha dola ya kiislam.

2.0 HISTORIA YA ELIMU YA MADRASA TANZANIA KWA UFUPI
Ø Historia ya Elimu ya Madrasa Tanzania inanasibiana na Historia ya kuenea kwa uislam katika Afrika Mashariki kuanzia Pwani hadi bara.
Ø Elimu itolewayo na Madrasa zetu ilichipuka tangu wakati walivyoanza kuja Waarabu kutoka Saudia, Oman, Uajemi, Hadhramaut na Yemen.
Ø Karne ya 9 na 10 wahamiaji kutoka Saudia walianza kusihi BENADIR (Pwani ya Somalia).
Ø Karne ya 12 Waarabu wageni (Afro-arabs) walianza kufika hadi mji wa Kilwa.
Ø Karne ya 12 wageni kutoka Hadhramawt na Yemen waliingia Afrika Mashariki. Wageni hawa nao pia walitoa elimu inayohusu uislam. Lakini kufahamu uzito wa elimu waliyoitoa kunategemea ufahamu wa sababu zilizowaleta Afrika Mashariki. Hawakuja kueneza uislam na kuufundisha uislam. Bali wali kuja kutokana na:
(i) Njaa iliiyokuwapo Arabuni wakati huo.
(ii) Ukame huko Arabuni.
(iii) Ukandamizaji wa Kisiasa uliotawala huko.

2.1 Kustawi kwa Elimu ya Madrasa Afrika Mashariki
Ø Mwaka 1332, Mwarabu aitwaye IBN BATUTA alipotembelea Kilwa alikuta mji umekaliwa waliokuwa wakitumia lugha ya Kiswahili.
Ø Baadaye miji ya Tanga, Dar-es-Salaam, Mombasa, Lamu, Malindi, na Mikindani vikawa vituo vya kueneza uislam na elimu ya kiislam katika miji ya Tanzania, Kenya, Uganda, Rwandda, Zaire, Msumbiji, Malawi na Burundi.

2.2 Maarifa yaliyotolewa na njia za kufundishia
Ø Maarifa yaliyotolewa na kuonekana hayo ndiyo maarifa ya uislam ni pamoja na:
(i) Zipi ni nguzo za imani na maana yake.
(ii) Zipi nguzo za Swala na maana yake.
(iii) Namna ya kusoma Quran, lugha ya kiarabu na vira kadhaa.
(iv) Sirah ya Mtume (s.a.w)
(v) Kanuni zinazotawalal utendaji wa Ibada Maalumu.
Ø Maarifa haya yalifundishwa kwa njia kuu ya Kipurure. Mwanafunzi hakusoma kwa kuwa mdadisi sana. Wanafunzi walikasirishwa waliyofundishwa.
Ø Walimu wa kufundisha hayo, ni wale tu, walioonekana wanaweza kuyasoma hayo. Hakukuwa na mazingatio kuhusu uwezo na ujuzi wa mfundishaji kufikisha maarifa anayoyatoa.
Ø Kwa sababu hizo, pia njia kuu ya kudhibiti nidhamu, ilibaki kuwa ni viboko tu.
Ø Kwa ujumla taaluma kuu za elimu ya Madrasa zilizotawala ni KUSOMA, KUANDIKA, KUIFADHI na KUIGA ambazo zilitolewa na walioweza kuzipata taaluma hizo.

2.3 Dosari za Elimu ya Madrasa iliyotolewa wakati wa Waarabu
Utangulizi
Ø Dosari hizo zimetokana na asili ya kuenea kwa dini na elimu ya Kiislam Afrika Mashariki, hususan Tanzania.
Ø Tatizo linakuja kwa vile Uislam na elimuk ya Kiisam:-
(i) Vilenea katika taratyibu za walioeneza kkujitafutia maisha yao wala si kwa madhumini ya kufanya umisionari.
(ii) Vilienezwa na wailam ambapo hawakuwa na maandilizi ya kufanya hivyo hivyo hakukuwa na matayarisho yoyote ya malengo ya kieleimu.
Ø Matokeo yake uislam ulifundishwa ili kupata wenzi na washirika katika mas[ala ya kijamii kama vile:
o Misiba
o Harusi n.k..
· Utangulizi

(i) Zilifundishwa Taaluma chache tu.
Mfano: Kusoma, Kuandika, Kukariri Quran.
Taaluma hizo si pana kiasi cha kuwawezesha wanafunzi kuuhani uislam kifikra, au vyovyote Taaluma hizo hazimwezeshi mwanafunzi kumudu changamoto zinazoibuka kila kukicha; Japo uislam haushindwi na changamoto yoyote ile.
(ii) Njia za kuendeleza nidhamu, na maadili zilikuwa viboko tu, ukali tu, pasi na kuchunguza tatizo kwa lengo la kkuondoa tatizo hilo na kusaidia.
(iii) Njia za kkufundishia hazikuzingatia umuhimu wa kuendeleza na kuhusisha nyanja tatu za kujifunza.
(a) Nyanja ya ung’amuzi (Cognitive domain).
(b) Nyanja ya matendo (Psychomotoar domain)
(c) Nyanja ya kuhusisha (Affective domain)
Kila nyanza hapo inaumuhimu katikak uislam wa mtu mmoja mmoja au jamii na hatimaye Ummah.
(iv) Hakukuwapo chombo maalum cha kijamii, kinachosimamia swala zima la utoaji wa Elimu hii. Matokeo yake kila mmoja alifundisha kadiri na namna alivyodhani ni sawa.

2.4 Athari za dosari hizo
(i) Kukosekana kwa taaluma muhimu za kifiqih
Mfano:
- Taaluma inayowezesha kkuhusianisha mazingira na fatwa kadhaa za kifiqih.
- Taaluma inayofafanua hukumu kadhaa za kifiqih na yanayotokea katika maisha. Katika hili, kumekosekana taaluma ya kubainisha tofauti ya RIRA na HIBA.
(ii) Watu wachache sana ndio waliweza kwendelea na elimu ya Madrasa kwa
kiwango cha juu kwa kulinganisha na waislam wengine.
Mfano:
Ni Masheikh wachache waliweza kkufikia kiwango Fulani. Matokeo hata vitu vidogo vidogo kuweza kufahamika kwa waislam wote, vinafahamika na masheikh tu.

(iii) Kuibuka kwa Matabaka miongoni mwa waislam kutokana na dosari hizo,
kumeibuka matabaka kadhaa mingoni mwa waislam.

Mfano:
o Tabaka la wasomi wa elimu katika mfumo huu wa madrasa tu.
o Tbaka la waliosoma elimu ya madrasa kidogi na elimu ya kisekula kidogo.
o Tabaka la waliosoma kiasi elimu ya kisekula na kukosa elimu ya madrasa lakini badaye (ukubwani) wakajifunza elimu ya uislam kwa mfumo mwingine.
Mahusiano ya matabaka haya hayasaidii kuendeleza uislam na waislam wa kiislam, ni sumu kwa maendeleo ya jamii ya kiislam.

3.0 MATATIZO YANAYOIKABILI ELIMU YA MADRASA TANZANIA
i) Utangulizi
Taasisi ya Madrasah inazidi kukpoteza hata hadhi yake ndogo iliyokuwa nayo.
Mfano:
Jamii haiipi hadi na thamani stahiki licha ya kuwa madrasa ni taasisi muhimu katika kurithisha mila, na mfumo mzima wa uislam toka kizazi hadi kingine. Wazazi wa watoto wa kiislam leo hii hawana hari ya kupeleka watoto wao kwenye vituo vya madrasa. Wala wazazi hao hawana hata haja ya kujua mikati ya madrasa zinazowazunguka.

(ii) Matatizo

Matatizo yanayoikabili elimu ya madrasa ni:

3.1
Matatizo ya Kitaasisi (Institutional Problems)

(a) Hakuna mfumo wa uendeshaji elimu ya madrasa. Mfumo huo
Mfumo huo hautoi picha halisi juu ya nani hasa ndiye mratibu au msimamizi wa elimu ya Madrasa. Kwa sababu hiyo hakuna upimaji wala tathimini yoyote ili kuelewa mustak bal wa elimu hii muhimu
(b) Kukosekana kwa “usare” (uniformity) katika ufundisjaji.
Matokeo yake anapohama motto kwenda madrasa nyingine anaathirika kitaaluma.
(c) Hakuna utaratibu fasaha/muafaka wa kuwahusisha wazazi wa Kiislam katika kujadili maendeleo na kutathimini uendeshaji wa madrasa. Athari yake ni wazazi kutojihusisha na uendelezaji wa madrasa zetu na ufuatiliaji wa taaluma muhimu zipatikanazo.
(d) Kukosekana kwa utaratibu wa kubadilishana mawazo baina ya walimu tofauti tofauti, juu ya uboreshaji wa njia za ufundishaji na mafanikio katika uendeshaji madrasa.
(e) Kukosekana kwa mipango inayohusiana na madrasa, wanafunzi na walimu. Athari yake ni kupungua kwa idadi ya wanafunzi na walimu wa madrasa.
(f) Kukosekana kwa utaratibu maalumu juu ya vigezo vinavyomuwezesha mtu kuwa mwalimu. Kwa kawaida yeyote anayejua kusoma na kuandika herufi za kiarabu, kusoma Quran na mambo kadhaa katika Ibada maalumu za kifiqih, aweza kuwa mwalimu hata kama sifa za kitabia, na uwezo wa kkurithisha elimu kwake ni vikwazo.

TANBIH:
Aina za walimu zaweza kkuwa kama ifuatavyo:-
(i) Mwenye sifa (Qualified) – Anazo sifa kitabia, anaweza na ujuzi wa kkufundisha na ana elimu.
(ii) Mwenye sifa (Underqualified) – Anayo elimu ila hana mbunu bora za ufundishaji.
(iii) Asiye na sifa (Unqualified) – Hana sifa hata kidogo. Huyu ni hatari sana.

Matatizo ya Kijamii
(a) Fikra za watu juu ya elimu ya madrasa na thamani yake
- Jamii na mtu mmoja mmoja wanachukulia elimu ya msingi ya madrasa ni kusoma Quran na kujua kanuni muhimu za utekelezaji wa Ibada maalumu kama vile Swala, hija, swala ya maiti, kushona sanda na kadhalika.
- Athari yake ni kuwa, mara baada ya watoto kufikia ngazi hiyo huonekana imetosha na kwamba, wana elimu ya kutosha juu ya uislam. Elimu kuhusu uislam inapungua miongoni mwa waislam.
(b) Uchumi duni kwa wazazi na walimu
- Umaskini na kipato kidogo kwa walimu wa madrasa inakuwa tatizo kubwa kwa uendeshaji wa madrasa zetu. Hali hii husababisha walimu wa madrasa kutenga muda kidogo sana kwa ajili ya kazi ya madrasa. Kadhalika kujituma juu ya kuboresha madrasa hupungua.
- Vile vile pato la wazazi kuwa dogo huchangia tatizo. Mara nyingi watu wenyekipato cha chini ndio wanaopeleka watoto wetu madrasa na wenye uwezo na wito wa kiislam wao huwaajiri walimu wa kuwafundisha watoto nyumbani. Kwa sababu hiyo, wazazi wengi hawana uwezo wa kkuchangia fedha muhimu kwa ajili ya madrasa. Wakati mwingine mchango wao huwa kidogo na mgumu kupatikana.
- Athari ya hayo, ni kudorora kwa madrasa zetu na kupatikana kwa watoto, mabarabara, vijana wasio na elimu sahihi ya msingi kuhusu uislam na hatimaye kuporomoka kwa maadili.
(c) Mfumo wa elimu ya nchi na utaratibu wa kisekula
Mfumo wa elimu ya kisekula umembana kiasi motto anayesoma madrasa kutokana na utaratibu ulivyo. Uendeshaji wa elimu ya kisekula umezaa desturi ya “Tuition” (masomo ya ziada), desturi amabyao sit u inamfanya motto achoke bali pia inamkosesha muda wa kuhudhuria katika madrasa zetu.

Mfano:
Mtoto wa darasa la kwanza na pili wanaingia shule kwa zamu, mara asubuhi, mara saa tano, mara mchana. Hii inaleta ugumu kwa madrasa kuratibu jinsi ya kuwasaidia watoto.
Mtoto wa darasa la kwanza atokapo shule, anapumzika kidogi, kasha anaenda “Tuition” masomo ya zaida.
Mtoto wa darasa la tano hadi saba, anakosa muda kabisa. Muda wote, kutwa mzima anashughulishwa na elimu ya kisekula na usiku anajisomea nyumbani.
Athari ya tatizo hili ni kushuka kwa mahudhurio ya watoto katika madrasa zetu, na mara nyingine kuwapo kwa mahudhuria yasiyotabirika na kuelezeka. Mara kuna mahudhurio ya kuridhisha mara mabaya.
(d) Shughuli za Kijamii miongoni mwa Waislam
- Ndani ya jamii ya Kiislam, inapotokea shughuli kama vile harusi na kadhalika, madrasah nyingi kuhusishwa. Mfano kuandaa kaswida kwa ajili ya maulidi harusini. Hili hupunguza za muda wa ufundishaji na kujifunza katika madrasa zetu.
- Athari yake ni kuongezeka kwa tatizo katika madrasa zetu. Wazizi wengine huona kua hakuna haja ya watoto kusoma madrasa hizo.

4.0 SOLUHISHO KWA MADRASA ZETU

4.1 Utangulizi
- Ni vigumu kuliondoa tatizo hili kwa kulifanya jukumu hilo kuwa la watu Fulani tu. Mfano, kulifanya liwe jukumu la masheikh tu, au jukumu la walimu tu, au la wazazi tu. Inapaswa kuwa ni tatizo linalomgusa kihisia kila muislam.
- Kwa hakika elimu hii ni muhimu sana kwa maendeleo ya uislam na waislam kiitikadi, kitaaluma, kielimu n.k.

4.2 Mfumo
- Kunahaja ya kuudhurusi mfumo wa elimu ya madrasa na kuangalia namna ya kuuendeleza na kuuboreha kwa manufaaa ya kikazi cha kiislam.
- Mfumo wa madrasa zetu uendane kabisa na haja iliyopo katika jamii kwa lengo la kuwaendeleza watoto kitaaluma.

4.3 Walimu
- Kuwepo na mpango maalumu wa kuwaendeleza walimu kielimu, kitaaluma na kiuchumi ili kuwaongezea hari ya kujituma na kukfikiri kwa ajili ya maendeleo ya taasisi hii muhimu, “madrasati”.
Mfano:
Kuwepo kwa warsha, makongamano na semina ili kuwawezesha walimu kushirikiana ujuzi na mbinu za kufundishia na kuendeshea madrasa zetu.
- Walimu wawe wabunifu kiuchumi ili waweze kujikwamua kiuchumi na kuendeleza madrasa zetu.
- Walimu wasijione kuwa wao ni waislam au watu wa daraja la chini sana kimaisha. Bali wajione wao ni watu muhimu na kazi yao ni jukumu lao si jukumu la mtu Fulani na wala hawafanyi kazi hiyo ili tu kuwaridhisha watu Fulani bali ili kumridhisha allah (s.w).

4.4 Jamii ya Kiislam
- Ifanye fikra juu ya jinsi ya kuboresha na kuendeleza madrasa zetu na watoto wetu katika taaluma muhimu za kiislam.
- Jamii nzima ieleweshwe juu ya nafasi sahihi ya Madrasa na Elimu ya Madrasa kwa maisha yua Waislam nchini.

4.5 Taasisi za Kiislam
Zishirikiane kuona jinsi ya kutatua matatizo hayo.

5.0
TAALUMA MUHIMU KWA WALIMU WA MADRASA

5.1 Utangulizi
Kila nyanja inahitaji taaluma Fulani ili kuifanya nyanja hiyo iwe makini na yenye manufaa kwamaisha na ummah kwa ujumla. Hata mitume (radhi za Allah ziwafikie) walipewa taaluma maalumu kwa kazi zao. Katika maisha yetu tunahitaji taaluma zinazowezesha watu kutekeleza majukumu yao katika mazingira wanayoishi.
Mfano:
Mwalimu wa madrasa anahitaji taaluma juu ya;
(i) Uendeshaji wa madrasa.
(ii) Ufundishaji.
(iii) Saikolojia ya watoto na malezi.
(iv) Taaluma inazofundisha kama vile Fiqih, Tareikh, Qurani, Kiarabu, Tawhiid, Sirah, Akhlaq n.k.

5.2 Njia za kkufundishia (Muhtasari)
Zipo njia kadhaa Bwana Mtume (s.a.w) amekuwa akizitumia katika kufundishia watu. Pia Quran imeeleza njia kadhaa kwa ajili ya ufundishaji na uchamasishaji. Kwa muhtasari njia hzo ni pamoja na zifuatazo.

(a) Simulizi (Narration)
- Hii ni njia ambayo mwalimu anafundisha kwa kutumia visa vya kubuni au visa halisi. Njia hii inafaa sana kutumika hususan kwa watoto wadogo.
- Katika Quran njia hii imetumika kutafundisha mara kadhaa. Kanuni na njia yenyewe katika Quran zimeelezwa katika “NJIA ZA KUFUNDISHIA KATIKA MADRASA ZETU”. Hapa ni muhtasari tu.
- Njia hii yaweza kutumika katika kufundisha Sira ya Mtume, Akhlaq, Tareikh, Fiqih hata tawhiid. Alimradi mwalimu afahamu jinsi ya kuitumia njia hiyo kwa ufanisi.
(b) Uelezeaji (Description)
- Njia hii hutumika kuelezea dhana au wazo Fulani katika uislam. Muhimu kwa mwalimu ni kuifahamu misingi ya njia hii pamoja na kuelewa mazingira yanayofaa kwa njia hii.
Mfano:
(i) Ili kutoa maf’hum nzuri kuhusu “UISLAM” kama dini njia hii yafaa kutumika.
(ii) Ili kufunldisha vizuri, mazingira ya vita vya Badr, Uhud, Khandaq n.k. kwa lengo la kkufundisha mazingatio yanayopatikana, mwalimu aweza kutumia njia ya UELEZEAJI (Description)
- Kadhalika, cha muhimu ni maarifa kuhusu njia hii.
(c) Njia ya Uoneshaji (Demonstration)
- Ni njia inayotumika kufundishia mada zinazolenga kutoa ujuzi kwa wanafunzi kutenda matendo maalum:
Mfano:
(i) Swala la mait.
(ii) Swala la Faradh na Sunnah.
(iii) Kushona Sanda.
(iv) Kuosha Maiti.
(v) Kuchukua Udhu n.k.
- Mada kama hizi zikifundishwa pasipokutumia njia hizi, ueleo wa wanafunzi unaathirika.
- Mwalimu anatakiwa kuifahamu njia hii kwa madhumuni ya kuitumia kwa ufanisi.
(d) Njia ya ugunduzi na udadisi
- Njia hii inamtaka mwalimu aoneshe tatizo kasha aongeze wanafunzi katika kugundua suluhisho. Kwa kufanya hivi, milki ya ung’amuzi (Cognitive Facult) itakuwa imeendelezwa. Quran inasisitiza matumizi ya milki ya ung’amuzi (Cognition domain).
Mfano:
(i) Baada ya kufundisha “Tawhid” – Mwalimu anaweza kutoa habari ya kweli kuhusiana na tawhiid kasha wanafunzi wakajadili kwa mnasaba wa tawhid.
(ii) Mwalimu aweza kufundisha “Tareikh” – Hijar kutoka Makka kwenda Madina, alafu wanafunzi watatakiwa kugundua wanachojifunza.
(iii) Mwalimu awezatoa tatizo liliopo katika jamii kwa mnasaba wa uislam, kasha akawataka wanafunzi waonyeshe sabbu na suluhisho.
(e) Njia ya Kuhidadhi
- Hii ni muhimu sna katika elimu na maarifa ya kiislam. Mwalimu anatakiwa kuwawezesha wanafunzi kuhifadhi katika mada kadhaa.
Mfano:
(i) Ktika Swala, mwalimu atumie njia rahisi kwa wanafunzi kuhifadhi.
(ii) Katika Wudhuu, mwalimu atumie njia hii pia ili wnafunzi waweze kuhifadhi maneno muhimu.
(iii) Katika Dua, wanafunzi wahifadhishwe dua.
(iv) Katika Tarekh, wanafunzi wahifadhishwe aya na hadithi mbalimbali zinazonasibiana na matukio katika mada. Mathalani, kufundisha Mkataba wa hudaybiya, Quran 48:1. 48:18 ni vema zikahifhadhiwa. Pia katika kufundisha AKHLAQ mwalimu awahifadhishe watoto, Sura ya 64.4 ikiwekana, kulingana na umri wa watoto, Pia wahifadhi Quran 33:21.
(f) Njia za Kufundisha Quran
Njia na mbinu pamoja na mikakati ni muhimu sana katika ufundishaji wa usomaji Quran, vinginevyo motto atosoma muda mrefu sana ili kuelewa. Baadhi ya mbinu za kufundishia ni pamoja na kusoma herufi bila irobu kwa njia ya ubao, kadi, daftari n.k.

MUHIMU:
- Mwalimu afundishe kwanza herfu bila irabu. Yaani: ALIF, BE …….
- Kisha afundishe Irabu. Yaani: FAT’HA, KISRA, ……
- Afundishe kuchanganya herufi hizo na rabu;
Mfano: BE FAT’HABA, TE FAT’HATA …….
- Mwalimu atumie michezo kadhaa kwa watoto kuzitambua herufi.
Mfano: NGAZINGAZI, KIKAPU, UPANGAJI, GURUDUMU ZA GARI, NYUMBA …. n.k.
- Mwalimu afundishe kuchanganya SILABI ili kupata neno. Ni vizuri Mwalimu akaanza na kinachoeleweka kwenda kisichoeleweka.
Mfano: Kumwezesha motto kuandika BABA kwa herufi za Kiarabu, kasha aandike neno la kiarabu kwa herfu hizo.

6.0 HITIMISHO
Mwalimu anapaswa sit u kujua anachokifundisha, bali pia kufahamu na kuweza kutumia njia na mbinu muafaka. Kwa kawaida hatupaswi kulenga kusema sana, au kueleza mengi, bali tulenge kuwezesha mengi kufahamika kwa urahisi zaidi.

7.0 MWISHO
Kwa muda mrefu MADRASA zimesahaulika na kusababisha athari mbaya. Ili kuzikuisha tunapaswa kuzingatia kazi zinazotakiwa kukfanywa na madrasa na zipi zinafanywa. Kuelewa tatizo kwa undani. Historia ya Madrasa Tanzania ni muhimu kufahamika ili kurudisha mzizi wa tatizo. Kadhalika, Matatizo yanayoikabili taasisi ya Madrasa na ufumbuzi wake ni muhimu vikajadiliwa. Aidha , kuna haja ya kukumbuka taluma muhimu kwa walimu wa Madrasah na kuona kama wengi wanazo. Kama si hivyo, basi mikakati iwepo kuwawezesha walimu wa Madrasa kuendesha madrasa zetu (Uendeshaji Madrasa) pamoja na kuwa na mbinu bora za kufundishia katika madrasah zetu.
Mbinu zilizomo humu ni muhtasari tu, hazijaelezwa zote. Na wala hazijafafanuliwa hasa.
ALLAH NDIYE MJUZI WA YOTE

Saturday, May 5

Mawaziri, hakuna sherehe, nendeni mkawajibike! by zittokabwe

Juhudi za kurejesha misingi ya uwajibikaji katika utumishi wa umma zimeanza kuzaa matunda Baada ya Rais kutekeleza shinikizo la Bunge la kuwafukuza kazi baadhi ya Mawaziri ambao Wizara zao zimetuhumiwa kwa ubadhirifu wa fedha za umma, rushwa na utendaji mbovu. Mawaziri 6 wamefukuzwa kazi baada ya kugoma kujiuzulu wao wenyewe, manaibu Waziri 2 wamefukuzwa pia.

Ndugu George Mkuchika alitakiwa kujiuzulu, akajiuzulu lakini Rais amemrudisha kwenye Baraza kama Waziri wa Utawala Bora. Yeye nampongeza kwani hakuwa na makuu ya kuanza kujitetea kama wengine. Atakuwa ametoa funzo kwa wenzake.

Kwa kawaida wateule hufanya sherehe kwa kuteuliwa kwao. Nitawashangaa watakaofanya sherehe safari hii kwani hakuna cha kufurahia. Nitawashangaa Watakaokwenda kuapa na Maua kwa furaha kwani furaha itakuwa ya muda mfupi tu. Mkutano wa Bunge wa Bajeti ni mwezi ujao tu na Wateule wote watakuwa kikaangoni. Too short honeymoon.

Hakuna cha kusherehekea kwa sababu nchi in a changamoto nyingi sana. Changamoto ya kuzalisha umeme wa kutosha na kuusambaza kwa wananchi wengi, changamoto ya kukuza uchumi wa vijijini na kukuza uzalishaji viwandani ili kutengeneza ajira kwa vijana, changamoto ya kuongeza mapato ya Utalii kutoka katika hifadhi zetu na kuvutia watalii zaidi katika nchi yetu.

Nimewapigia simu wateule wengi na kuwaambia, siwapi pongezi Bali nawatakia kazi njema. Nawatakia uwajibikaji mwema. Uwajibikaji ndio msingi wa kupambana na rushwa, uvivu na uzembe.

Kwa Waziri wa Fedha, ambaye mimi ni Waziri Kivuli wake (Kama Kiongozi wa Upinzani Bungeni hataniwajibisha pia), namwambia uteuzi wake ni changamoto kubwa sana katika maisha yake.

Hivi sasa eneo lenye Bajeti kubwa kuliko zote nchini ni huduma kwa Deni la Taifa (services to national debt). Lazima kuangalia upya Deni la Taifa. Hivi sasa Deni la Taifa ukijumlisha na Dhamana za Serikali (government guarantees) limefikia tshs 22trn mpaka Desemba 2011. Nimewahi kutaka ukaguzi Maalumu katika 'account' ya Deni la Taifa. Linarejea wigo huu. Tunalipa takribani 1.9trn tshs kwa mwaka kuhudumia Deni la Taifa. Zaidi ya Bajeti ya miumbombinu, Afya, Maji, Umeme nk.

Mfumuko wa Bei, misamaha ya kodi na kodi zinazozuia watanzania kujiajiri ni changamoto kubwa sana Wizara ya Fedha lazima ihangaike nayo.

Usimamizi wa Mashirika ya Umma kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina na hasa usimamizi wa Hisa za Serikali katika kampuni binafsi ni masuala yanayohitaji masuluhisho sasa na sio baadaye.

Kwa Mwalimu wangu Dkt. Mwakyembe, utakumbukwa kwa Jambo moja tu. RELI. 'make our Railway system work'. Hutakuwa na 'legacy' nyingine isipokuwa Reli maaana Bandari bila Reli ni sawa na Bure.

Tunatumia zaidi ya tshs 300bn kwa mwaka kukarabati barabara wakati tunahitaji tshs 200bn kukarabati Reli iweze kusafirisha mzigo kwenda Bandarini na kukupa Bandarini.

Ndio maana nasema hakuna Jambo la kusherehekea maana wajibu mliopewa na Rais ni mtihani mkubwa kwenu katika kukitumikia Taifa letu. Msipowajibika, mtakumbwa na fagio la chuma!

Mkisha kula kiapo, kimbieni kazini. Nothing to celebrate. Hit the ground running.

ZZK

Dar-es-Salaam

Jumamosi, Mei 5 2012

Friday, April 20

TB Joshua again: Delivers man from shocking addiction!

This post and link to the video below were shared to us by Ihechukwu Njoku -- Controversial Nigerian Prophet T.B. Joshua can’t seem to stay out of the news. However, this time it’s not concerning a prophetic utterance or political visitor.

On Sunday 15th April 2012, Joshua’s popular church in Lagos was witness to a disgusting yet dramatic case of a man with a truly repulsive addiction. Mr Mukaila Malomo, a Nigerian who lived in Germany for 16 years, confessed to being addicted to regularly taking a sickening concoction of faeces, semen and urine.

According to Malomo, a graduate from the London School of Journalism, it all started one night in a prison cell in Germany. "I woke up in the middle of the night and a very wicked demon instructed me to get up from my bed,” he told the bewildered SCOAN congregation. “This strange voice said that I should go to the toilet, defecate and mix it with my sperm and urine. I mixed my urine, sperm and faeces and swallowed everything.”

Malomo, who worked in a reputable organic salad company in Munich before a drunken brawl landed him in prison, explained that an unusual anger and desire to fight immediately followed. “After I swallowed it, a very strange power came over me. I felt as if I was a small god. It overcame me and I became very strong and angry - as if there's an extra power from another world entering my body. I was ready for war. Ever since then, for over 15 years, I have been addicted to eating my faeces, urine and sperm. I can’t stop it.”

He continued his sordid tale, explaining how each indulgence in the addiction would result in further violence. “After my release from prison, I was always fighting in Germany. Sometimes, the police would have to cover the whole street to try and stop me - and I was using only a bottle. I kept on stabbing without getting tired – because of this power that entered me.”

People present in the church could scarcely contain their shock as Malomo’s revelations continued. “It is not only my own faeces; on many occasions, I visited public toilets here in Nigeria and Germany and ate from there.” He described the mixture as food to him. “I enjoy it. I don't even perceive any smell. I eat it as if I eat eba (Nigerian cuisine) or something like that.”

Malomo, married to a German Hungarian lady who gave birth to his only son while in prison, described how he had kept this addiction a total secret from the world around him. “As I am eating it, that evil spirit will be telling me that this thing is only for me, that nobody should know, otherwise the power will go.”

Joshua proceeded to tell his congregation and the viewers worldwide watching the live broadcast via Christian television station Emmanuel TV that a video clip would be shown to verify Malomo’s confession. Stating that it was too graphic for him to witness, he covered his face and advised viewers without strong stomachs to do likewise. The clip showed Malomo mixing his own urine and faeces together and then drinking the revolting contents with apparent ease and delight. People within the auditorium vomited at the sight, distressed at the level of degradation the addiction had rendered on Malomo.

Joshua then called on the congregants to join together in supplication and proceeded to pray for the ‘demon’ within Malomo to come out! Falling to the floor, Malomo’s body began vibrating uncontrollably and uncannily. Asked to explain what was happening, Malomo said he felt as if something was leaving his body.

Joshua then instructed Malomo to go to the church’s public toilet to see how his reaction towards human waste had changed following the prayer. Merely perceiving the odour of other’s defecation caused Malomo himself to vomit. He returned to the church, testifying that all desire for his former addiction had vanished as the realization of his earlier actions dawned upon him.“Apart from being irritated by the odour, I feel ashamed, in the sense that – how can a human being be eating faeces,” he told the congregation, as he joined Joshua in a joyful dance.

SCOAN has now controversially released the video on popular video-sharing site YouTube and via their Facebook account which has garnered well over 100,000 fans in just four months. Although Malomo’s case appears to be the most extreme, many with strange addictions claim to have been delivered at Joshua’s ministry over the last few months, including those addicted to drinking kerosene, eating ice cubes, sand, charcoal, mothballs and soil.

T.B. Joshua has set social networks and local media ablaze in recent months, especially with his prediction concerning the death of the late Malawian president Bingu wa Mutharika and revelations of his relationships with African leaders such as Ghana’s John Atta Mills, Zimbabwe’s Morgan Tsvangarai and Malawi’s new head Joyce Banda. His television station Emmanuel TV continues to increase in popularity, especially across Africa where he is becoming a household name.

Tafrisi ya Mjengwa kuhusu Zitto Kabwe na saini za Wabunge 70 kumg'oa Pinda


Ndugu zangu,

Leo asubuhi wakati nikifanya ' jogging' kwenye mitaa ya Dar es Salaam niliwasikia watu wa kawaida kabisa wakijiuliza na kujadili; " inakuwaje Serikali iwalipe marehemu mishahara huku sisi tulio hai hatuna hata uhakika wa milo miwili ya siku?" Wanauliza watu wa mitaani.

Naam, nchi yetu imekumbwa na mafuriko ya habari. Kule bungeni Dodoma kuna moto unawaka. Zimeitishwa sanini 70 ili Jumatatu ipigwe kura ya kukosa imani na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. Ndio, kuna wanaotaka Pinda ang'oke, na labda kutolewa kafara, maana, siamini kama tatizo la msingi ni Pinda, bali ni la kimfumo zaidi. Na jana kuna mbunge wa CCM kayasema makali yafuatayo;

“Mheshimiwa Naibu Spika, inashangaza na kusikitisha kuwa nchi inatafunwa. Wanaofanya haya ni mawaziri wetu. Nchi inakufa na tuelewe kuwa Tanzania sio mali ya CCM, ni ya Watanzania wote.“Mawaziri wetu wamekuwa mchwa, wanaangamiza nchi na leo nitamtaja waziri anayeongoza kwa kutafuta fedha za Watanzania. Ni Waziri wetu wa Fedha, Mustafa Mkulo. Ameuza viwanja, amelidanganya Bunge baada ya kuivunja CHC,”- Deo Filikunjombe ( CCM) Bungeni jana.

Lakini ya jana yalitanguliwa na ya juzi; Mbunge mwanadamizi wa CCM Godfrey Zambi aliyasema makali haya;

" CCM inaweza kung'olewa madarakani katika uchaguzi wa mwaka 2015 endapo kasi ya ufisadi na ubadhirifu wa fedha za umma itaendelea kama ilivyo sasa"- Godfrey Zambi ( CCM, Mbozi Mashariki).

Kauli za wabunge hao wawili wa CCM zinatoa tafsiri ya kilio cha wabunge wa CCM kuomba msaada kwa anayeweza kuwasaidia. Inatoa tafsiri pia kuwa hicho ni kilio cha wabunge wengi wa CCM. Kwamba hayo ndiyo wanayaongea hata chini chini.

Ndio, wananung'unika na wameanza kuiona adhabu wanayokwenda kuipata kutoka kwa wananchi ifikapo 2015. Wanaona pia, kuwa ' kisungura' hiki kidogo kinachopatikana kila mwaka kinavyoliwa na wajanja na wengine kuachiwa mifupa.

Wabunge wa CCM na wengine wanaona jinsi baadhi ya mawaziri wa kutoka chama chao wanavyojiangalia wenyewe kwa kujikatia zaidi kasungura hako kadogo na hata minofu mingine kuikimbizia kwenye majimbo yao badala ya kuangalia majimbo mengine pia. Hakika, Wabunge wa CCM sasa wanatoa kilio cha kuomba msaada na kilichochanganyika na hasira na hofu ya kupoteza mamlaka ya kuongoza dola ifikapo mwaka 2015. Ndio, kuna wanaokiona chama chao kikielekea kwenye kuzama 2015. Kelele wanazopiga bungeni zimegeuka kama kelele za nyikani, hazisikiki. Wameanza sasa kuwa na ujasiri wa kuzomeana wazi wazi kwenye vikao vyao badala ya kusubiri kuzomewa na wananchi hadharani. Naam, CCM ya sasa inapata tabu hata kwenye kujua namna ya kuitumia misamiati mipya ya kisiasa, maana, kuna wanaojivua gamba, wanaovuliwa magamba na sasa kuna ' wanaojinyambua' magamba wakiwa ndani ya chama- 'Political evolution' ya namna fulani.

Na Mtego wa Zitto Kabwe kwa CCM?

Jana Mbunge Zitto Kabwe ameitega CCM. Ni mtego wa hatari. Saini zile 70 zina maana hii;
- Kama wabunge wa CCM hawatachangamkia kutia sahihi zao zikavuka hata mia na hamsini, basi, kuna ujumbe unaopelekwa kwa umma. Kuwa wabunge wa CCM ni maneno tu, hawana dhamira ya kweli ya kupambana na ufisadi. Wabunge wengi wa CCM hawataiepuka adhabu ya umma inaweza kuwa inawasubiri 2015.
- Kwa wabunge wa CCM kutia sahihi zao na hata Pinda kupigiwa kura ya wabunge kukosa imani nae ina maana pia kuwa wabunge hawana imani na bwana mkubwa aliyemteua Pinda. Busara haiwataki wabunge wa CCM kufikia hapo. Hilo halina maslahi kwa taifa.

Nini kitakachotokea?

Kuna matatu;
Mosi, Mawaziri wale watano wanaotuhumiwa kwa ufisadi na ubadhirifu wa mali ya umma wanaweza kuepusha aibu kwa Serikali kwa wao wenyewe kutangaza kujiuzulu. Ingawa hili ni gumu kufanyika katika nchi hii, lakini, wakati mwingine kuna lazima ya kufanyika- maana, hapo watakuwa wamemnusuru Waziri Mkuu na aliyemteua.

Pili- Likishindikana la kwanza, basi, kabla ya Jumatatu, Waziri Mkuu Pinda awe ameshajiandaa kufanya maamuzi magumu. Kujiuzulu na kulinda heshima yake na ya aliyemteua. Au kutolewe ' Tamko la Serikali' litakalobadili upepo unaovuma sasa bungeni.

Tatu: La kwanza na la pili yaweza yasifanyike, na badala yake. Rais anaweza kuyaona yanayotokea sasa bungeni kama fursa ya kufanya mabadiliko makubwa Serikalini mara akitua Dar kutoka ziara ya Brazil.

Naam, yumkini pale Diamond Jubilee, kabla ya Jumatatu, kuna watakaopewa kazi ya kusafisha ukumbi na kupanga viti tayari kwa Mkuu wa Nchi kusema jambo kubwa kwa taifa kupitia kwa ' Wazee wa Darisalama'.

Tuhuma za Ray kuhusika na kifo cha Kanumba

Baada ya taarifa kuenea kwamba mwigizaji Ray anahusika moja kwa moja na kifo cha mwigizaji marehemu Steven Kanumba, mwigizaji huyo amezungumza kwenye AMPLIFAYA ya CLOUDS FM na Millard Ayo na kusema yafuatayo:

“...nimekuqa nikizisikia sana hizi tuhuma, sio kweli kwa sababu Kanumba ni mdogo wangu wa karibu sana tumetoka mbali sana kimaisha mimi na yeye, nimekua na mazoea ya kuona vitu kila siku vinaandikwa ambapo juzi nilipigiwa simu na kuambiwa nitazame kwenye blog ya U-Turn ambayo anaimiliki huyu dada ambaye simfahamu anaitwa Mange Kimambi”

“...alikuwa ameandika kwamba amepata taarifa kutoka kwa polisi mmoja wa Oysterbay kwamba Ray ndio aliyepiga simu kwa Lulu siku ya kifo cha Kanumba kwa hiyo Lulu ametumika kufanya mauaji bila kujijua, na pia kukawa kuna swali kwamba kwa nini Ray alikua wa kwanza kufika kwa marehemu Kanumba. Mungu ndie anaejua...”

“...kwa hiyo anataka kuwadhihirishia Watanzania kwamba Ray ndiyo anahusika na hicho kifo, baada ya hilo nimeshirikiana na polisi na kushitaki na kufungua kesi ambapo hivi sasa ninapozungumza yupo polisi Oysterbay akihojiwa kwa sababu ameandika kitu ambacho bado kipo ndani ya uchunguzi, hana uhakika nacho sijui Lulu amekamatwa Coco Beach which is not true, sijui hizi habari kaipata wapi...”

“...sasa hii ni kutaka kunivunjia heshima, mimi nafanya kazi ya kuigiza ndio maisha yangu unapoandika kitu kama hicho kwenye internet inafika sehumu kubwa dunia nzima, sasa unategemea watu wanichukuliaje kama sio kunivunjia heshima, kunipotezea mashabiki wangu… nasema hili sitoweza kuliacha, nitalifanyia kazi na nitalifikisha mahakamani ili iwe fundisho, sitolichekea...”

Kwenye sentensi nyingine Ray amesema baadhi ya maoni yaliyotolewa na watu mbalimbali kwenye hiyo habari iliyoandikwa kwenye blogu hiyo, “maoni niliyoyasoma mengine yanamwambia yule dada kwamba anachokiandika kinaweza kum-cost kwenye maisha yake, na nyingine zinasema kwamba tuko tayari kumvamia Ray na kumuua, sasa hichi kitu ni hatari sana kwenye maisha yangu kwa hiyo nimemshitaki polisi na kuandika kwa kusema chochote kitakachonikuta hata nikipigwa jiwe na kuanguka mimi na-deal na huyo mwanamke kwa sababu yeye ndio mtu aliye-publish hivyo vitu watu wanichukulie mimi vinginevyo kabisa tofauti jinsi nilivyo na sihusiki kabisa na hicho kifo, kimsingi maisha yangu yapo hatarini lakini nasema haya ni maisha nitaendelea kuvumilia...”

Thursday, April 19

Ufisadi wa mabilioni kila kona

NI KWENYE MAGARI YA SERIKALI,TANESCO,MALIASILI,MABILIONI YA JK,AFYA NA MISHAHARA HEWA
Daniel Mjema Dodoma na Fidelis Butahe
WABUNGE jana waliijia juu Serikali kwa matumizi mabaya ya fedha za umma na ufisadi ulijitokeza kwenye taasisi zake mbalimbali katika mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, mwaka jana.

Hasira za wabunge hao zilitokana na ripoti tatu za Kamati za Bunge; Mashirika ya Umma (POAC), Serikali za Mitaa (LAAC) na Hesabu za Serikali Kuu (PAC) kuonyesha upotevu wa mabilioni ya shilingi yaliyotumika katika nyanja mbalimbali ikiwemo mishahara hewa na mikataba mibovu.

Mbunge wa Longido (CCM), Michael Laizer alisema ni aibu kila mwaka kuwa na ripoti za wizi wa mali za umma lakini Serikali inakaa kimya.

Alisema katika Halmashauri ya Wilaya ya Longido, mmoja wa maofisa wake aliidhinisha Sh11 milioni kwa ajili ya matengenezo ya gari. “Labda Serikali imechoka sasa inafanya makusudi fedha za wananchi zinaliwa lakini yenyewe inakaa kimya. Serikali itujibu hizi fedha zinazopitishwa kila mwaka zinakwenda wapi?” alihoji Laizer

Mbunge wa Viti Maalumu (CUF), Magdalena Sakaya alisema Serikali inapaswa kuona aibu kwa kutekeleza pendekezo moja tu kati ya 12 yaliyotolewa na Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita.

Alihoji suala la mishahara hewa kuendelea kujitokeza huku Serikali ikikaa kimya na kila mwaka CAG anatoa ripoti yake… “Kuna vitabu vya halmashauri za wilaya ambavyo CAG hakuvikagua kwa kuwa havikuonekana vilipo, sasa hapo tunakwenda wapi? Kuna Sh8 bilioni hazikufika katika halmashauri husika zimekwenda wapi? Wabunge tunatakiwa kuhoji na kupewa majibu sahihi.”

Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari alisema sasa Tanzania imekuwa kama Saccos kwa kuwa fedha za umma zinatafunwa bila utaratibu huku vielelezo vikitoweka kusikojulikana.

“Wakati wa uchaguzi wa wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki, mawaziri walijaa bungeni ila sasa tunajadili hatima ya Watanzania hawaonekani. Wabunge tuwe kitu kimoja tuibane Serikali itueleze hizi fedha zimekwenda wapi?” alisema Nassari.

Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Ester Bulaya alisema chama tawala kisipokuwa makini katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 kitahukumiwa na vijana.

“Serikali ndiyo chanzo cha fedha kutafunwa… inakuwaje Naibu Waziri wa Maji anasimama na kuahidi mambo mengi wakati anajua wazi kuwa fedha za kutekeleza miradi hazipo?” alihoji.

Alisema mwaka 2015, utakuwa mgumu kwa CCM kwa kuwa wakati huo vijana watakuwa asilimia 85 na wanaweza kukinyima kura kutokana na Serikali yake kushindwa kusimamia masuala ya msingi ya maendeleo.

Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee aliwataka wabunge kuacha kulalamika kwa kuwa wao ndiyo wenye rungu la kuishikisha adabu Serikali: “Tukilalamika wananchi waliotuchagua nao watatushangaa kwa kuwa wametutuma kuwawakilisha na si kulalamika.”

Alisema umefikia wakati wa wabunge kuweka itikadi za vyama vyao pembeni na kuwashughulikia mawaziri wa wizara husika ambazo zinaonekana kuwa tatizo.

Mbunge wa Mwibara (CCM), Alphaxard Lugola alimlipua Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo akisema alihusika katika uuzaji wa mali ya Serikali katika Kiwanja namba 10 Barabara ya Nyerere na kwamba anaingilia utendaji wa mashirika ya Serikali.

Alisema kuwa kiwanja hicho awali, ilikuwa kiuzwe kwa Shirika la Tanzania Motors chini ya Kampuni ya Mashirika Hodhi ya Umma (CHC) kwa Sh1.3 bilioni lakini baadaye Mkurugenzi Mkuu wa CHC alipewa barua kusitisha uuzwaji wa jengo hilo na kumtaka kuitisha mazungumzo upya na Morad Sadik, ambaye alikuwa akitaka kununua eneo hilo awali.

“Inakuwaje wizara inaingia utendaji wa taasisi au kampuni zilizopo chini yake?” alihoji.

Awali, baada ya Kipindi cha Maswali na Majibu, Wenyeviti wa Kamati hizo za Bunge; Zitto Kabwe (POAC), John Cheyo (PAC) na Augustine Mrema (LAAC), waliwasilisha ripoti za kamati zao zinazoonyesha kukithiri kwa vitendo vya ufisadi serikalini na matumizi mabaya ya fedha za umma.

Kamati ya PAC
Cheyo alisema kamati yake imebaini kuwapo kwa matumizi ambayo hayakupitishwa na Bunge na kutaja Maonyesho ya Sabasaba, Nanenane na Utumishi kama sehemu ambako fedha hizo zilitumika.

Alisema mwaka 2009/2010 Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, ilitumia fedha za matumizi ya jumla ya Sh1.10 bilioni kwa ajili ya Maonyesho ya Nanenane ambazo hazikuwamo kwenye bajeti iliyopitishwa na Bunge.

Alisema hata matumizi ya Sh21.63 bilioni zilizotumika kuendesha Mfuko wa Kukwamua Wananchi kiuchumi maarufu kama ‘mabilioni ya JK’ hazikuwapo katika bajeti iliyopitishwa na Bunge. Alipendekeza kuwa ili kuondoa hali hiyo, mfuko huo unatakiwa kuwa na mtu au taasisi ya kuusimamia badala ya kuachwa bila usimamizi.

Alisema kuwepo kwa udanganyifu na ukwepaji kodi kumeisababishia Serikali hasara ya Sh15.4 bilioni na Dola 2.6 milioni za Marekani.

Alisema Wizara ya Maliasili na Utalii na ilipoteza Sh874,853,564 baada ya kufanya uamuzi wa upendeleo wa kutoa kiwango cha chini cha mrabaha kwa mazao ya misitu.

Kuhusu magari ya Serikali, Cheyo alisema kumekuwa na matumizi yasiyo ya lazima katika uendeshaji na ukarabati wa magari hayo. Hadi Juni 30, 2010 Serikali ilikuwa inamiliki magari yenye thamani ya Sh5 trilioni.

Alisema mwendelezo wa ununuzi wa magari unaofanywa na Serikali unaongeza gharama za uendeshaji na kusisitiza kwamba matumizi hayo si ya lazima kwa Serikali yenye uchumi mdogo uliozidiwa na madeni.

Kuhusu ukaguzi wa magari uliofanywa na wakala chini ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS), PAC imependekeza kuwajibishwa kwa ofisa masuuli wa Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kuisababishia Serikali hasara ya Dola 18,343,540 za Marekani ambazo ni karibu Sh30 bilioni na kusisitiza: “Sh30 bilioni zilitumika kufanyia ukaguzi wa magari ambao haukuwepo.”

Alisema pia wamegundua kuwa Serikali inatumia fedha nyingi kwa ajili ya kukodi majengo ya wizara na kusisitiza kuwa moja inaweza kulipa kodi ya Sh485 milioni.

Alisema kuna watumishi hewa takriban 3,000 na kwamba Serikali haifahamu lolote kuhusu hali hiyo… “Kuna Sh1.8 bilioni ambazo hutumiwa na Serikali kwa ajili ya kulipa watumishi hewa. Pia imebainika kuwa Serikali haijui thamani ya majengo yake yaliyopo ndani na nje ya nchi.”

POAC

Zitto kwa upande wake, alielezea maeneo yenye matatizo sugu ya matumizi ya fedha ambayo yanahusisha ukiukwaji mkubwa wa Sheria ya Ununuzi wa Umma na kanuni zake.

Alitola mfano wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), ambalo kwa mwaka mmoja wa fedha linafanya ununuzi wenye thamani ya kati ya Sh300 bilioni hadi Sh600 bilioni.

Alisema kwa mwaka wa fedha 2009/2010, Tanesco ililitumia Sh1.8 bilioni ukilinganisha na Sh65 milioni zilizokuwa zimepangwa katika bajeti ya ukarabati wa gati mojawapo katika Kituo cha Bwawa la Mtera.

“Ongezeko hilo la gharama za ununuzi kwa ajili ya ukarabati, ni kiasi kikubwa na Kamati haikuridhika na majibu ya menejimenti hivyo kuagiza uchunguzi wa ndani ili kubaini uhalisia wa ununuzi huo,”alisema na kuongeza:

“Tumependekeza Tanesco ianze kutumia vyanzo vyake vya umeme na iache kununua umeme hasa wa kampuni ya IPTL kwani inatumia Sh62.4 kununua umeme katika kampuni hii kwa mwaka.”

Alisema Chuo Kikuu Kishiriki cha Mkwawa (MUCE) kilishindwa kuthibitisha kwa wakaguzi wa hesabu uwepo wa vifaa vya maabara vilivyonunuliwa ambavyo vina thamani ya Sh267 millioni.

Katika ripoti hiyo, Zitto alisema imebainika pia mkataba kati ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), na Kampuni ya Startimes unatakiwa kupitiwa upya ili uinufaishe TBC.

Pia aliugusia matumizi mabaya ya fedha katika Bodi ya Pamba ambako alisema kuwa kiasi cha Sh2 bilioni zilizotolewa na Serikali hazijulikani zilipo na wala hazikuwafikia wakulima wa zao hilo.

LAAC

Kwa upande wake, Mrema aliitaka Serikali ivunje mtandao wa wezi wa mali za umma na kuhoji inakuwaje inawakumbatia mafisadi?
Alihoji majalada ya watuhumiwa wa ufisadi kukaa zaidi ya miaka 10 katika Ofisi za Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Mkurugenzi Mkuu wa Mashtaka (DPP) na ile ya Makosa ya Jinai (DCI) wakati kesi za uchaguzi zimewekewa kikomo.

Alisema ripoti ya CAG kwa mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, 2010, inaonyesha kuwa Sh583.2 milioni zililipwa kama mishahara hewa kiasi ambacho alisema kingetosha kujenga madarasa 194.

Mrema alisema katika ripoti hiyo, imebainika kwamba Sh8 bilioni zilitumika katika ununuzi usiokuwa na nyaraka na ama wenye nyaraka pungufu hali inayoashiria kuwapo kwa wizi.

Aliwataja watumishi wa Halmashauri ya Kishapu akisema ni vinara wa ubadhirifu wa Sh6 bilioni na kudai kuwa walishirikiana na baadhi ya watumishi wa Benki ya NMB Tawi la Manonga, Shinyanga kuiba fedha hizo za umma.

Aliwataja watumishi hao kuwa ni Mweka Hazina, Muhdin Mohamed, Mtunza Fedha wa Halmashauri hiyo, Walugu Mussa, Boniface Nkumiming na Mhandisi wa Halmashauri, Leonard Mashamba.

Alisema fedha hizo zilitafunwa kwa kutumia nyaraka feki, uhamisho wa fedha bila idhini na kuzitumia kinyume cha malengo, uhamisho wa fedha ambao haukufika kwenye akaunti husika na malipo kwa walipaji wasiofahamika.

Mrema aliilaumu Serikali kwa kuwahamisha kutoka halmashauri moja kwenda nyingine na Serikali Kuu, watumishi wanaotuhumiwa kwa ufisadi badala ya kuwachukulia hatua za kisheria.

Kamati hiyo imependekeza Bunge likubali kuitaka Serikali kutoa maelezo ya kuridhisha ni kwa nini ubadhirifu huo umeachwa ukishamiri kwa miaka mitatu mfululizo bila wahusika waliotajwa na CAG kuchukuliwa hatua.

“Shida iliyopo hapa ni Serikali kuonekana inawakumbatia wahusika kwa kisingizio cha uchunguzi unaendelea… nini kinachochunguzwa badala ya kupeleka watu mahakamani na kumuita CAG kama shahidi?”

Thursday, April 12

Lazima tulinde haki za wasanii. Hotuba yangu Bungeni #kazizawasanii #hakizawasanii na zitto kabwe

MHE. KABWE Z. ZITTO:

Mheshimiwa Naibu Spika, nami nikushukuru kwa kunipa fursa ya kuchangia katika Muswada huu ambao unabadilisha Sheria Mbalimbali za Biashara. Kumekuwa kuna malalamiko mengi sana kwamba nchi yetu iko nyuma sana katika kuweka mazingira mazuri ya watu kuweza kusajili Makampuni, kupata leseni na kufanya biashara. Nakumbuka kwamba kwa miaka mitatu sasa mfululizo nchi yetu imekuwa ikipata alama ambazo si nzuri katika ripoti ya Benki ya Dunia inayoangalia mazingira ya biashara (Doing Business Report) ambapo ripoti ya mwaka 2012 inayoonyesha kwamba tumeshuka zaidi kutoka nafasi ya 125 duniani katika nchi 180 na zilizofanyiwa kazi mpaka nafasi ya 127. Kwa hiyo naamini kabisa kwamba mabadiliko haya ambayo tunayafanya yataweza kusaidia kupunguza muda ambao mtu anaweza akasajili biashara au kusajili Kampuni na kadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, ningependa kuanzia pale ambapo mzungumzaji aliyepita alianza kuzungumza na suala ambalo napenda leo nichukue muda mrefu na wa kutosha kabisa ni suala la biashara ya sanaa. Biashara ya sanaa kwa sababu ni biashara ambayo imekuwa haiangaliwi nami niseme kabisa kwamba tulichokishuhudia jana heroic funeral ambayo alifanyiwa marehemu Kanumba inadhihirisha kabisa kwamba Watanzania ni wapenzi sana wa sanaa. Kwa hiyo ni jukumu letu sisi kama wawakilishi wa wananchi, kama watunga sheria, kama watunga sera kupata ujumbe kutokana na umati wa Watanzania wa mkoa wa Dar es Salaam na waliotoka mikoa ya jirani na waliotoka mikoa ya mbali ambao walienda kumzika na kumpunzisha ndugu Kanumba jana. Kwa hiyo ule ni ujumbe ambao tunaupata na leo tunapoandika sheria hii tuwe na kumbukumbu tuangalie wananchi waliojitokeza kwenye mazishi yale na kuweza kuona tuweke sheria maalum ambazo zitaweza kuwasaidia na kuwalinda wasanii wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunafanya marekebisho kwenye merchandise marked act ambapo tunaangalia pamoja na mambo mengine copy right neighbouring right act, paterns act, trade and services marked acts na hizo zingine mbili ambazo kwa leo sitaweza kuzichangia. Nataka nichangie hasa copy right and neighbouring act. Katika hotuba yetu ya Kambi ya Upinzani Bungeni mwaka jana tulitoa mapendekezo maalum ya kuweza kuangalia namna ya kuweza kulinda kazi za wasanii waweze kufaidika na kazi zao tuzuie wizi wa kazi za wasanii ambao Watanzania wanashiriki kwa sababu tunapoenda kununua kazi ya msanii ambao una uhakika kazi hii sio original, una uhakika kazi hii ni ya kutengenezwa na wewe ukatoa fedha yako ukanunua maana yake ni kwamba unamwua msanii ambao ungepaswa kuweza kumsaidia. Sasa njia pekee ya kuweza kuzuia hali hiyo ni kuweka sheria jinsi ambavyo inavyopaswa kuwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nimegawa sekta hii katika maeneo matatu ambayo ni ya kawaida unayakuta sana katika sekta ya mafuta au madini. Kwamba kuna up stream, mid stream na down stream. Kwenye up stream ni pale ambapo msanii anatengeneza kazi yake, pale sioni shida kwa sababu msanii atakaa nyumbani kwake, atakaa wapi ataandaa kazi yake. Lakini kwenye mid stream kwenye studios ambapo wasanii wanaenda kurekodi na baada ya hapo kazi zao zinaenda kusambazwa hapa kuna shida kubwa sana na ni eneo ambalo ni lazima tuliwekee regulations. Lazima tuliwekee kazi maalum na ningependa katika hili eneo la part four bahati mbaya sheria niliyonayo ni ile ambayo ilichapishwa tarehe 29 Julai, 2011. Kwa hiyo mtaweza kuangalia, muangalie namna ambavyo tutaweka leo katika sheria jinsi ambavyo tutalinda mid stream part katikati hapa ya kazi ya msanii pale anapoenda kurekodi na kuhakikisha kwamba kinachozalishwa pale kinafahamika, msanii anakifahamu na lile pendekezo ambalo lilitolewa na Waziri wetu kivuli wa masuala ya Habari, Utamaduni na Michezo la stickers lianzie pale ili kuweza kujua ni kiwango gani ambacho kimezalishwa katika studio na kiwango gani ambacho kinaingia kwenye soko.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pili eneo ambalo ningependa Mheshimiwa Waziri liongezwe pia katika part four hii ni down stream part kwenye retail kwamba kazi ambayo inauzwa ya msanii biashara ile ya rejareja ya msanii iwe ni kazi ile ambayo ilizalishwa, kwa hili eneo pia tuweze kuliona namna ambavyo tutakavyoweza kulitilia nguvu katika sheria hii. Kwa maana hiyo ni kwamba nilikuwa napendekeza kwamba yale maeneo ambayo yameachwa ya Sheria ya Hatimiliki cap. 218 yachukuliwe na kuingizwa ndani ya mabadiliko haya ambayo tunayafanya ili kuweza kuhakikisha kwamba kazi za wasanii zinalindwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pili hivi sasa tumepata taarifa kwamba TRA wanaandaa regulations kwa ajili ya stickers. Lakini nimeongea na mmoja wa wasanii wa muda mrefu Ndugu John Kitime anasema tayari regulations zipo wanaita epigram zipo lakini bado hazijaanza kutekelezwa. Kwa hiyo nilikuwa nadhani kwamba Mheshimiwa Waziri kwa sababu yeye ndio Waziri wa Wizara ambayo yuko responsible kwa hili ukishirikiana na Waziri wa Fedha kuhakikisha kwamba zoezi hili la TRA la kuandaa regulations nyingine za stickers liunganishwe na regulations ambazo tayari zimeshatengenezwa na ziko tayari toka mwaka 2006 ili ndani ya mwaka wa fedha unaoanza tarehe 1 Julai, 2012 stickers ziwe tayari na kazi za wasanii ziweze kutambulika pale ambapo zinakuwa zimetengenezwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pili nadhani hili litamhusu sana Mheshimiwa Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwamba tayari kuna regulations kuhusiana na royalties ambazo broadcasters wanapokuwa wanacheza miziki hii zile regulations kwa ajili ya royalties hazijawa enforced na hasa haya Makampuni makubwa, televesheni kubwa, redio kubwa hazi-enforce hili. Kwa hiyo miziki na filamu na kadhalika za wasanii wetu zinapokuwa zinachezwa hawapati zile royalties ambazo zinatakiwa na kama tulivyosema kwamba hii ni biashara na ni biashara ambayo inaweza ikawafaidisha sana wasanii wetu. Nilikuwa naomba tu Waziri tena narejea kwamba natumia iliyokuwa published tarehe 29 Julai 2011 kwa mtu anaweza kuangalia namna ambavyo inakwenda.

Mheshimiwa Naibu Spika, kifungu cha 36 Prohibition to deal in counterfeit goods. Nimeangalia hapa orodha ya offence ambazo mtu atafanya kutokana na counterfeit sioni moja kwa moja mtu ambaye atahusika na wizi wa kazi za sanaa. Kwa hiyo nilikuwa naomba ile “a” mpaka “i” tutafute mahali ambazo tutaweka tuta-include copy right issues katika counterfeit act ili kuweza kuhakikisha kwamba tunaposema counterfeit hatutakuwa na maana tu ya bidhaa kama maji, bidhaa zingine hapana, lakini pili kazi ya msanii iweze kuwa included katika jambo hilo. Kwa hiyo tu-include katika ile “a” mpaka “i” masuala ya piracy, book leading na kadhalika yawe ndani ya sheria. Lakini lingine ambalo nimeliona hapa ni adhabu, sasa sijui itakuwepo kwenye amendment maana yake amendments nimezipata sasa hivi sioni adhabu kwa mtu ambaye hatakutwa anafanya biashara ya kazi ambazo zimeibwa za wasanii, sioni katika kifungu hiki cha prohibition to deal in counterfeit.

Kwa hiyo nilikuwa napendekeza sio tu adhabu ya kawaida iwe ni adhabu kali, adhabu ambayo ita-discourage kabisa watu kuiba kazi za wasanii wetu na kuweza kuziuza. Kwa hiyo nilikuwa nashauri kwamba nimeona kuna maeneo kuna faini za shilingi milioni 20, kuna miaka mitano jela sasa sina uhakika maana yake leo nimeiona sasa hivi kama hizi zinahusiana na hii yaku-deal na counterfeit. Kwa sababu hii section yote ya counterfeit imetajwa offences lakini haitaji adhabu. Kwa hiyo nilikuwa naomba Mheshimiwa Waziri na watu wa Idara ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali iongeze kipengele cha adhabu mara baada ya zile offences na iseme kabisa kwamba mtu yoyote at a written level atakayekutwa anauza ama ni CD au ni DVD ambayo ni Pirated ambayo ni counterfeit adhabu yake isiwe chini ya shilingi milioni 50. Hiyo ita-discourage kabisa kabisa kazi ambazo zinafanywa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini sio hivyo tu sio mtu tu atakayekutwa anauza lakini pia mtu yoyote atakayekutwa in possession kwa hiyo hata kama wewe umepita pale Ubungo vijana wamekuuzia lakini ni kazi ya wizi umekaa labda umempa lifti Polisi akaona akagundua kwamba hii ni kazi ulionunua ni ya wizi wewe ambao umekutwa in possession uadhibiwe ili kujenga mentality ya Watanzania kuacha kununua kazi ambazo ni za wizi dhidi ya wasanii wetu. Kwa hiyo haya ndiyo mapendekezo ambayo nilikuwa nayaomba tuyaweke kwa sababu kuna fedha nyingi sana kwenye sanaa.

Commitment ya Serikali kulinda wasanii wetu(hansard) by zittokabwe

WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA:

Napenda kutoa kauli ya Serikali, kwamba kutokana vikao vyote hivyo ambavyo nimesema kumi na sita vya Mawaziri lakini leo tena tumekutana mara ya kumi na saba, tumeazimia kwamba hotuba ya bajeti ya mwezi wa sita Mheshimiwa Waziri wa Fedha atalizungumzia jambo hilo na utekelezaji wa mambo yote pamoja na utengenezaji wa sticker, na jinsi ambavyo TRA watafanya jambo hilo yatawekwa bayana na mara baada ya bajeti speech kuanzia tarehe 1 Julai, kutakuwa na mabadiliko kubwa katika kazi za wasanii wa nchi yetu ya Tanzania.

Kwa hiyo nataka niwashukuru Waheshimiwa Wabunge, nataka tu watambue kwamba Serikali inaliona hilo Serikali iko pamoja na wao na ndiyo maana tumekutana namna hiyo na kwa hakika katika hili tuko pamoja kabisa na mtaona utekelezaji wake.

KAMATI YA BUNGE ZIMA

MHE. KABWE Z. ZITTO:

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeleta mapendekezo, Jedwali la Marekebisho kipengele hicho cha 38. Wakati Mheshimiwa Waziri anafanya winding up alitoa commitment ya Serikali kuhusiana na mabadiliko makubwa ya eneo la copyrights kwa ajili ya kulinda kazi za wasanii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba Mheshimiwa Waziri arejee ile commitment kabla sijaweza ku-move hii amendment. Tafadhali. Airejee kwa faida ya Taifa na kwa faida ya Bunge.

MWENYEKITI:

Mheshimiwa Waziri, Mheshimiwa Zitto pamoja na amendment aliyoleta, amezingatia sana kauli yako wakati unajibu hoja za Waheshimiwa Wabunge. Anaomba ile commitment ya Serikali ya kufanya marekebisho kwenye sheria ya copyright. Sasa hiyo commitment ya Serikali ndiyo itakayomsababisha yeye kuondoa jedwali lake la marekebisho ili sasa tuhoji kifungu hiki.

WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA:

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati ninafanya majumuisho nilisema kwamba mimi na Mheshimiwa Mkulo – Waziri wa Fedha na Mheshimiwa Nchimbi tumekutana mara nyingi sana kwa ajili ya suala hilo la kuangalia haki za wasanii Watanzania kwamba hazipotei. Lakini vile vile tumeagiza mamlaka zilizoko chini ya Wizara zetu; COSOTA kwa Viwanda na Biashara, TRA kwa upande wa Wizara ya Fedha na BASATA kwa upande wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wakae. Wamefanya vikao mara tatu. Kutokana na yaliyokubaliwa katika vikao vyote vya Waheshimiwa Mawaziri na wajumbe wa zile Kamati, Mheshimiwa Mwenyekiti, narudia commitment ya Serikali kwamba kwenye Bajeti ijayo, Serikali italeta mapendekezo makubwa ambayo yatakuwa yamezingatia maoni yote ambayo yametolewa na BASATA, COSOTA na TRA kuhusu namna bora ya kulinda haki za wasanii wa aina zote katika nchi yetu ya Tanzania.

MHE. KABWE Z. ZITTO:

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nataka hiyo commitment ili itakapofika siku ya bajeti tutumie Hansard hii kuhakikisha kwamba commitment hiyo imetekelezwa. Kwa maana hiyo nikwamba naondoa amendment yangu ambayo nimeileta.

MWENYEKITI:

Nakushukuru. Na nafikiri kwamba Serikali iko makini, inavyofanya commitment hapa inaelewa nini inachokifanya.

Tuesday, April 10

How to Stop Teeth Grinding

7 tips to overcome bruxism and save your teeth
Teeth grinding: Causes and consequences
My friend’s teeth grinding had started during a period of higher than normal stress in his life. But as he told me: “My life is good at the moment, so I don’t understand why it’s still happening!” Actually, a problem habit formed during stressful times often hangs around once the stress has lessened simply because it has become just that: a habit. Bad news if something isn’t done about it.
Teeth grinding and jaw clenching can unfortunately cause many different problems. When you grind your teeth, you wear away the tooth enamel. Too much wear and tear can lead to sensitive teeth, decay, and also damaged dental work. Continued and prolonged teeth grinding can damage the muscles and joints of the jaw, which could even cause osteoarthritis.
Of course the sooner you stop grinding your teeth, the less damage you do.
So what can be done to stop the rot? Well, here are some ideas I’ve used with teeth grinding clients over the years and, of course, my good friend. : )

Tip 1: Raise your awareness to stop teeth grinding
Take a couple of moments each day just to be aware of what your jaw is doing. Set your watch to check, say, once at 9am, once at 11am, then again at 3pm, 6pm, and just before you go to sleep. Your lips should be sealed but your teeth should not be touching. Consciously drop your jaw and let your whole lower face relax. Imagine that you are ‘re-setting’ your jaw and teeth to ‘behave’ for the next few hours - like programming your body. This will help change the teeth grinding pattern so that soon you’ll notice it’s been better without you having to think about it.

Tip 2: Get a night guard
No, not a security night watchman (unless you live in a really rough neighbourhood).
If teeth grinding has got to such a stage that you fear you might be doing damage, then consider asking your dentist to make a ‘night guard’ for you. This will be a plastic device to help redistribute the force from grinding, protecting your teeth from damage. And relax; you won’t look like Hannibal Lector. : )

Tip 3: Try a bit of mouth massage

Massage relaxes the body directly. In a sense, we can look upon massage as a communication to your body. Massage ‘says’: “Let go of tension and start to relax!” Massage works for stressed backs and necks and can also help calm your jaw muscles, easing away tensions. Before you retire for the night, take five minutes to gently massage your own face and jaw. Use gentle small circular rubbing motions with your hands to loosen everything up before you head off for Slumberland.

Tip 4: Stay away from alcohol
Teeth grinding tends to worsen after excessive alcohol consumption, so drink wisely. This may be partly because the quality of sleep is affected by heavy boozing sessions. More disturbed sleep means less rest and more nocturnal activity, which might include more teeth grinding.

Tip 5: Quit chewing gum and delicious pen lids
If you chew gum, then don’t - or at least, not very often. Constant chewing of gum (or pens, pen lids, or table legs…just kidding) just gets your jaws used to clamping. Remember, you want to re-condition them to be more relaxed and less active more of the time.

Tip 6: Stop teeth grinding by melting stress away
Because so much bruxism is caused by stress, it makes sense to relax deeply. Think of stress as like water in a bucket which you carry around with you. If you don’t empty it now and then, it can overflow from the slightest knock or nudge. It’s the same with stress: if you don’t ‘empty the stress’ by regular relaxation, then any small life knock can leave you feeling flooded with tension.
Mind and body relaxation will help calm the muscles of your whole body, including your jaw. Take time out once a day to listen to a relaxation CD. Or just close your eyes and focus on your breathing, then take your mind to each part of your body, imagining the different parts relaxing in turn.
If you know how to use self-hypnosis, then use this time to make suggestions to your own unconscious mind to stop teeth grinding.
Or let me help you relax quickly by clicking the free audio link below.

Tip 7: Really get what you need
We all have basic emotional and physical needs. If we consistently fail to meet these needs, we feel stressed. And, as you know, the more stressed you are, the more likely you are to grind your teeth. Being clear about what these needs are means you can work towards meeting them effectively.

You have a need:
For adequate and healthy nutrition, exercise, sleep, and water.
To feel safe and secure in life.
To regularly give and receive quality attention.
To feel a sense of influence and control over your life.
To feel part of a wider community.
To enjoy friendship, fun, love, and intimacy with significant people.
To feel a sense of status; basically, to feel you have a recognizable role in life. This also connects to a sense of competence and achievement.
To feel stretched but not stressed so you can avoid boredom and stagnation. This also enhances your self-esteem.
So if you do feel particularly stressed at present, think about how well the above needs are being met in your life. Meeting them better may help you quickly stop teeth grinding.
Follow these tips and teeth grinding will be a past irritation, not a current ‘nightmare’.

Share this article

Thursday, April 5

Maana ya matokeo Arumeru Mashariki by zittokabwe Matokeo ya Arumeru na kata za Mwanza, Songea na Mbeya ni mwanzo wa safari ya mwisho ya CCM na kwamba wanaondolewa madarakani kwa sababu wananchi wamekasirishwa, hasira ambazo fedha haiwezi kununua. Hasira ambayo matusi hayawezi kuifuta. Hasira ambayo vitisho havifui dafu. Hasira ya kutaka huduma bora. Hasira ya kuchoka na umasikini na kufukarishwa. Hasira ya kuchoshwa na ufisadi. Mhe Mwenyekiti Freeman Mbowe na Mhe Joshua Nassari Mnamo tarehe 11 Machi mwaka huu 2012 nikiwa ndani ya ndege natokea Arumeru kuzindua kampeni za uchaguzi mdogo wa jimbo la Arumeru Mashariki kwenda Kirumba Mwanza kuzindua kampeni za Udiwani katika kata ya Kirumba, niliandika makala kuhusu nini kitaamua mshindi katika uchaguzi ule. Nilianza makala yangu ile kwa kusema haya "Uchaguzi wa Ubunge Arumeru Mashariki ni kipimo cha namna wananchi mnavyoridhika na watawala, namna mnavyoridhika na mgawo wa Ardhi na namna mnavyoridhika na mgawanyo wa Maji katika Wilaya yenu". Haya maneno ilikuwa ni nukuu ya sehemu ya hotuba niliyotoa wakati namkaribisha Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA ndugu Freeman Mbowe kuzindua rasmi kampeni zetu. Ardhi ilikuwa ajenda kubwa sana. Washindani wetu wa CCM wakaona hatari ya hoja ya Ardhi na kuanza kutoa ahadi mbalimbali za kumaliza kero ya Ardhi. Hawakuaminika. Wananchi walisema, hawa wamemaliza miaka 50 bila kutatua kero hii, watawezaje kupata suluhisho sasa. Wakakataa. Hawakuichagua CCM na badala yake wakamchagua kwa kura nyingi sana ndugu Joshua Nassari, kijana wa miaka 26 tu kuwa Mbunge wa Jimbo Lao. Katika makala ile nilieleza wazi kwamba "Uchaguzi wa Arumeru ni uchaguzi kati ya kuwa na Ardhi au kuendelea kutokuwa nayo. Ni uchaguzi muhimu kwa watu wa Meru. Wasio na Ardhi watamchagua mgombea atakayesimamia mgawo wa Ardhi unaozingatia haki. Mgombea huyo ni mgombea wa CHADEMA ndugu Joshua Nassari. Sasa Nassari lazima aibebe ajenda Ardhi. Hana namna ni lazima awe sauti ya wananchi masikini waliofukarishwa na mfumo mbovu wa kugawa Ardhi ulioanzishwa wakati wa ukoloni na kuendelezwa chini ya Uongozi wa CCM. Ushindi wa CHADEMA katika uchaguzi wa Arumeru ni ishara ya dhahiri kabisa kwamba siku za CCM kuongoza Taifa letu zinahesabika. Ukilinganisha nguvu ya rasilimali watu na fedha ambayo CCM waliiweka huko Meru kulinganisha na CHADEMA unaona dhahiri kabisa kuwa fedha sio kigezo cha kushinda uchaguzi. Wananchi sasa wanataka masuala Yao yashughulikiwe. Hii pia imejionyesha katika chaguzi za Madiwani. CCM imepoteza nusu ya viti vya Udiwani vilivyokuwa vinagombewa. Katanza Lizaboni Songea, Kiwira Mbeya na Kirumba Mwanza zote zimeenda CHADEMA. Kata ya Msambweni Tanga imeenda CUF. CCM walipata kata katika Wilaya ya Bagamoyo, Bariadi na Temeke. Pia walipata kata katika manispaa ya Dodoma. Huu ni uchaguzi wa kwanza wa Madiwani ambao CCM imepoteza nusu ya viti vilivyokuwa vinagombewa toka mfumo wa vyama vingine uanze. Arumeru imekuwa jimbo la kwanza CCM kulipoteza kwa chama cha upinzani Tangu mwaka 1997 ambapo CCM walipoteza jimbo la Magu kwa chama cha UDP. Kwa CHADEMA hili ni jimbo la kwanza kulichukua kutoka CCM katika uchaguzi mdogo toka ianzishwe mwaka 1992. Itakumbukwa kwamba mwaka 2008 CHADEMA ilishinda jimbo la Tarime kwa kulirejesha maana kilikuwa linashikiliwa nacho. People's power Hivyo ni dhahiri kabisa kwamba siku za CCM kuwa madarakani zinahesabika. Ushindi wa Arumeru na Udiwani katika kata mbalimbali umeleta mageuzi makubwa ya kisaikolojia kwa wananchi kuliko hata ushindi wa Tarime. Ni wazi kabisa kuwa ushindi huu utafutiwa na mikutano wa kunadi chama katika mikoa mbalimbali nchini ikiwemo mikoa ya Kusini na ile ya Magharibi ambapo CHADEMA haijafanya operesheni. Kushindwa kwa CCM Arumeru pia kutal eta mpasuko zaidi ndani ya CCM na kuunganisha nguvu za wanasiasa ndani ya CHADEMA. Wakati CCM itakuwa inanyoosheana vidole kutafuta mchawi na hata wengine kufurahia kushindwa kwao (wakiamini ni kushindwa mmoja wa mahasimu wao), CHADEMA itakuwa inashikana mikono na kuimarisha mshikamano ili hatimaye kuchukua Dola ifikapo mwaka 2015. Jambo moja la dhahiri unaliona Baada ya uchaguzi wa Arumeru. Sasa ukipanda Basi kutoka Moshi kwenda Arusha, utopita ngome ya Chadema tu. Moshi mjini, Hai, Arumeru Mashariki na Arusha Mjini. Kwa waliomsoma Rais Museveni katika kitabu chake cha Sowing the Mustered seed, akitumia njia za Frelimo katika ukombozi, eneo hili sasa ni Liberated Zone. Ukanda uliokombolewa. Lengo langu ni kuonyesha kuwa hii ndio safari ya mwisho ya CCM na kwamba wanaondolewa madarakani kwa sababu wananchi wamekasirishwa, hasira ambazo fedha haiwezi kununua. Hasira ambayo matusi hayawezi kuifuta. Hasira ambayo vitisho havifui dafu. Hasira ya kutaka huduma bora. Hasira ya kuchoka na umasikini na kufukarishwa. Hasira ya kuchoshwa na ufisadi.

Matokeo ya Arumeru na kata za Mwanza, Songea na Mbeya ni mwanzo wa safari ya mwisho ya CCM na kwamba wanaondolewa madarakani kwa sababu wananchi wamekasirishwa, hasira ambazo fedha haiwezi kununua. Hasira ambayo matusi hayawezi kuifuta. Hasira ambayo vitisho havifui dafu. Hasira ya kutaka huduma bora. Hasira ya kuchoka na umasikini na kufukarishwa. Hasira ya kuchoshwa na ufisadi.

Mnamo tarehe 11 Machi mwaka huu 2012 nikiwa ndani ya ndege natokea Arumeru kuzindua kampeni za uchaguzi mdogo wa jimbo la Arumeru Mashariki kwenda Kirumba Mwanza kuzindua kampeni za Udiwani katika kata ya Kirumba, niliandika makala kuhusu nini kitaamua mshindi katika uchaguzi ule. Nilianza makala yangu ile kwa kusema haya
"Uchaguzi wa Ubunge Arumeru Mashariki ni kipimo cha namna wananchi mnavyoridhika na watawala, namna mnavyoridhika na mgawo wa Ardhi na namna mnavyoridhika na mgawanyo wa Maji katika Wilaya yenu".

Haya maneno ilikuwa ni nukuu ya sehemu ya hotuba niliyotoa wakati namkaribisha Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA ndugu Freeman Mbowe kuzindua rasmi kampeni zetu.
Ardhi ilikuwa ajenda kubwa sana. Washindani wetu wa CCM wakaona hatari ya hoja ya Ardhi na kuanza kutoa ahadi mbalimbali za kumaliza kero ya Ardhi. Hawakuaminika. Wananchi walisema, hawa wamemaliza miaka 50 bila kutatua kero hii, watawezaje kupata suluhisho sasa. Wakakataa. Hawakuichagua CCM na badala yake wakamchagua kwa kura nyingi sana ndugu Joshua Nassari, kijana wa miaka 26 tu kuwa Mbunge wa Jimbo Lao. Katika makala ile nilieleza wazi kwamba
"Uchaguzi wa Arumeru ni uchaguzi kati ya kuwa na Ardhi au kuendelea kutokuwa nayo. Ni uchaguzi muhimu kwa watu wa Meru. Wasio na Ardhi watamchagua mgombea atakayesimamia mgawo wa Ardhi unaozingatia haki. Mgombea huyo ni mgombea wa CHADEMA ndugu Joshua Nassari. Sasa Nassari lazima aibebe ajenda Ardhi. Hana namna ni lazima awe sauti ya wananchi masikini waliofukarishwa na mfumo mbovu wa kugawa Ardhi ulioanzishwa wakati wa ukoloni na kuendelezwa chini ya Uongozi wa CCM.
Ushindi wa CHADEMA katika uchaguzi wa Arumeru ni ishara ya dhahiri kabisa kwamba siku za CCM kuongoza Taifa letu zinahesabika. Ukilinganisha nguvu ya rasilimali watu na fedha ambayo CCM waliiweka huko Meru kulinganisha na CHADEMA unaona dhahiri kabisa kuwa fedha sio kigezo cha kushinda uchaguzi. Wananchi sasa wanataka masuala Yao yashughulikiwe. Hii pia imejionyesha katika chaguzi za Madiwani.

CCM imepoteza nusu ya viti vya Udiwani vilivyokuwa vinagombewa. Katanza Lizaboni Songea, Kiwira Mbeya na Kirumba Mwanza zote zimeenda CHADEMA. Kata ya Msambweni Tanga imeenda CUF. CCM walipata kata katika Wilaya ya Bagamoyo, Bariadi na Temeke. Pia walipata kata katika manispaa ya Dodoma.

Huu ni uchaguzi wa kwanza wa Madiwani ambao CCM imepoteza nusu ya viti vilivyokuwa vinagombewa toka mfumo wa vyama vingine uanze. Arumeru imekuwa jimbo la kwanza CCM kulipoteza kwa chama cha upinzani Tangu mwaka 1997 ambapo CCM walipoteza jimbo la Magu kwa chama cha UDP. Kwa CHADEMA hili ni jimbo la kwanza kulichukua kutoka CCM katika uchaguzi mdogo toka ianzishwe mwaka 1992. Itakumbukwa kwamba mwaka 2008 CHADEMA ilishinda jimbo la Tarime kwa kulirejesha maana kilikuwa linashikiliwa nacho.

People's power

Hivyo ni dhahiri kabisa kwamba siku za CCM kuwa madarakani zinahesabika. Ushindi wa Arumeru na Udiwani katika kata mbalimbali umeleta mageuzi makubwa ya kisaikolojia kwa wananchi kuliko hata ushindi wa Tarime. Ni wazi kabisa kuwa ushindi huu utafutiwa na mikutano wa kunadi chama katika mikoa mbalimbali nchini ikiwemo mikoa ya Kusini na ile ya Magharibi ambapo CHADEMA haijafanya operesheni.

Kushindwa kwa CCM Arumeru pia kutal eta mpasuko zaidi ndani ya CCM na kuunganisha nguvu za wanasiasa ndani ya CHADEMA. Wakati CCM itakuwa inanyoosheana vidole kutafuta mchawi na hata wengine kufurahia kushindwa kwao (wakiamini ni kushindwa mmoja wa mahasimu wao), CHADEMA itakuwa inashikana mikono na kuimarisha mshikamano ili hatimaye kuchukua Dola ifikapo mwaka 2015.

Jambo moja la dhahiri unaliona Baada ya uchaguzi wa Arumeru. Sasa ukipanda Basi kutoka Moshi kwenda Arusha, utopita ngome ya Chadema tu. Moshi mjini, Hai, Arumeru Mashariki na Arusha Mjini. Kwa waliomsoma Rais Museveni katika kitabu chake cha Sowing the Mustered seed, akitumia njia za Frelimo katika ukombozi, eneo hili sasa ni Liberated Zone. Ukanda uliokombolewa.

Lengo langu ni kuonyesha kuwa hii ndio safari ya mwisho ya CCM na kwamba wanaondolewa madarakani kwa sababu wananchi wamekasirishwa, hasira ambazo fedha haiwezi kununua. Hasira ambayo matusi hayawezi kuifuta. Hasira ambayo vitisho havifui dafu. Hasira ya kutaka huduma bora. Hasira ya kuchoka na umasikini na kufukarishwa. Hasira ya kuchoshwa na ufisadi.

Monday, April 2

CCM hali mbaya Arumeru

CHADEMA YAFANYA VIZURI KATA 11KATI YA 17, YASHINDA PIA UDIWANI MWANZA. SONGEA,MBEYA,CUF YAPETA TANGA

CHAMA Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeongoza kwenye kura za awali kwa mgombea wake, Joshua Nassari kupata kura nyingi katika kata 11 kati ya Kata 17 za Jimbo la Arumeru Mashariki.

Dakika chache kabla ya kutangaza matokeo hayo, baadhi ya wafuasi wa CCM waliokuwa wamefurika katika Ofisi za Mji Mdogo wa Usa River na baadhi ya polisi, walikuwa wameondoka eneo hilo, wakiwaacha wapambe wachache wa mgombea wao, Sioi akiwamo, Beno Malisa.

Huu ni uchaguzi wa kwanza mdogo kwa Chadema kushinda katika jimbo lililokuwa likishikiliwa na CCM na uchaguzi wa pili kwa chama hicho cha upinzani, kushinda katika uchaguzi mdogo baada ya ule uliofanyika katika Jimbo la Tarime, kuziba nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Chacha Wangwe.

Katika matokeo hayo yanayokusanywa na kujumlishwa katika ofisi za mji mdogo wa USA River, CCM, imefanya vema katika kata tatu ambako mgombea wake, Sioi Sumari amepata kura nyingi ikilinganishwa na Nassari.

Takwimu zinaonyesha kuwa Chadema wanaongoza katika kata za Akheri ambako ni nyumbani Kwa Sioi, Poli, USA-River, Mbuguni, Seela, Sing'isi, Nkoarua, Maji ya Chai, Kikwe, Maroroni, Nkoaranga, King'ori na Songoro ambako ni nyumbani Kwa Nassari. Jimbo la Arumeru Mashariki lina kata 17.

Mgombea wa CCM Sioi ameongoza katika kata za Makiba, Leguruki na Mkoandrua hadi saa 7:15 usiku jana ambapo msimamizi wa uchaguzi, Trasias Kagenzi alikuwa akisubiri masanduku ya kura kutoka kata mbili.

Kata ambazo masanduku na matokeo yake yalichelewa kutokana na umbali wa maeneo hayo ni Kikatiti na Ngarenanyuki.

Mbali na Chadema kuongoza Arumeru chama hicho pia kimeibuka kidedea katika uchaguzi mdogo wa udiwani katika mikoa ya Mbeya, Ruvuma na Mwanza.

CUF imeambulia kiti kimoja cha udiwani Tanga na CCM Dar es Salaam.

Katika tukio lingine, wakala wa Chadema katika chumba Cha kujumlisha kura, Godbless Lema, jana alilazimika kutumia nguvu dhidi ya msimamizi msaidizi wa kata ya Maroroni ambaye jina lake halikupatikana mara moja baada ya kumtuhumu kutaka kubadili tarakimu za matokeo kwenye fomu rasmi zilizowasilishwa.

"Yule msimamizi alikuwa akitaka kuchezea tarakimu katika fomu za matokeo kutoka kwenye kata yake bila kujua kama nilikuwa namfuatilia," alisema Lema.

Saturday, March 31

How to Stop Compulsive Lying

7 tips to stop you getting caught in your own tangled web
To control other people. People may lie about how much power/status they have and then threaten people with that fictitious power and influence.
For self-aggrandizement in order to make themselves appear wonderful, especially gifted, more interesting, or exciting - either through a sense of inadequacy or overly high self-esteem.
Through sheer force of habit - “Lying is as easy as breathing for me!”
Because you are reading this, I’m presuming you are sick of compulsively lying. So here are some ideas to help you start being more honest.
Tip 1: “To thine own self be true” - regardless of what others are doing
In the recent ‘expenses scandal’ in the UK, many cheating politicians defended their own public money pocketing by protesting that: “Everyone else had been doing it!” In some ways, lying has become more accepted and even expected.
In a recent survey in the UK, 41% of people said they would cash a winning lottery ticket even if it didn’t belong to them and more than two-thirds of people have stolen stationery from work (2).
You know what is honest, so be honest regardless of a dishonest group-think culture - don’t hide behind the excuse of widespread lying.
Tip 2: Remember the truth is often easier
“Always tell the truth. That way, you don’t have to remember what you said.” Mark Twain
Lying is a real strain. You have to remember so much and, no matter how elaborate your twisting and turning, you’ll eventually come unstuck. As Claire said on one of our sessions, “You know, it’s a relief not to lie!”
Cast off lying and you’ll find life instantly becomes much less stressful.
Tip 3: Know what lying is
It’s so easy to lie to ourselves about what lying is. Not telling the truth and remaining silent is a form of lying: ‘lying through omission’. In the same way, people may assume that failing to do the right thing is not the same as doing the wrong thing. In one research study in the UK, just 38% of items deliberately left in the street found their way back to their rightful owners (3).
Claire told me that one boyfriend had asked her why she hadn’t told him she’d cheated on him. She’d replied: “Because you didn’t ask!”
Don’t make excuses to yourself. Not telling the truth, when you know what it is, is lying.
Tip 4: Stop compulsive lying to protect your reputation (because the truth is out there)
Apart from all the ethical considerations, lying doesn’t work - not in the long run. Once you are unmasked as a habitual liar, you’ve blown it. People will take you far less seriously as a person. Trust may be impossible to ever win back.
As good old ‘honest Abe’ Lincoln said: “If you once forfeit the confidence of your fellow citizens, you can never regain their respect and esteem.”
Claire had destroyed the confidence of just about everyone and felt forced to move on to new pastures.
Stop and think: The truth has a way of making itself known, and when you lose people’s trust, you lose the power to be heard by other people - because they’ll stop listening. (Remember what happened to the boy who cried, "Wolf!")
Tip 5: Stop compulsive lying one step at a time
Claire had been lying for decades, all the time, every day. She was good at lying (which hadn’t stopped the truth from making itself known to the people in her life).
I asked her to start telling “small truths”, being honest here and there when normally she wouldn’t be. For example, when she spoke to someone new she was to tell that she had left school and become a hairdresser at 16 instead of her usual story of having picked up a Master’s degree in marine biology. She was to tell people her real town of origin and be honest about her parents (dropping the story of being adopted). Bit by bit, I encouraged her to start to tell small truths so truth telling, in itself, could become a habit.
Start by promising to yourself you’ll tell people three true things about yourself a day.
Tip 6: Stop compulsive lying by meeting your emotional needs honestly
Much human behaviour is unconsciously motivated by the need to meet emotional needs. We all have needs for a sense of safety and security, attention, status, meaning, excitement, intimacy and love, connection to others, self-esteem, and so forth. Now think about times when you’ve compulsively lied; times when the lies seemed to ‘come from nowhere’.
What was the drive behind the lying? Wanting to be included? Wanting to be thought highly of? Wanting to be loved, even? Wanting excitement? Really think about this.
Lying to get your life needs met is a form of stealing. Wanting to gain love, respect from others, or self-esteem without putting in real efforts is theft in a way.
Think about some real ways in which you can honestly meet these needs for self-importance, security, or whatever drive had been behind your lying. And make these the base from which you interact with others.
Tip 7: Use self-hypnosis to stop compulsive lying
For Claire, lying had come to feel a part of who she was; she called it “instinctive”. We worked hypnotically to great effect. I got her to hypnotically experience a type of situation in which she’d be typically tempted to tell a whopper and I helped her mentally rehearse telling the truth regardless of whether it was less “colourful” or exciting. Each time she did this, she felt an enormous flood of relief and felt closer to the person with whom she was communicating.
Claire emailed me months later to tell me that her new “real” life was going well and that “90% of the time I’m telling the truth and I’m getting more honest all the time; it feels natural now.”
Of course, she could have been lying to me, but I chose to believe her.
Share this article

Tupo Tayari Hata Kutumbukia Hata Ndani Ya Shimo La Kenge? (April Fool) Zingatio La Wiki ‘Abdun-Naaswir Hikmany Ujahili ulipokatwa panga zile enzi za Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), ulihakikisha umeondosha mambo yote ya kijahili kama vile kuwazika mabinti wakiwa hai, ribaa, uzinifu, pombe na mengineyo. Kwa hali zilizokuwepo sasa, yaonesha dhahiri kwamba ujinga uliopo leo umepindukia mipaka ya hizo enzi alizokuwa akiishi Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Makhalifa wake (Radhiya Allaahu ‘Anhum). Majahili wa siku hizo hawakuwa na siku maalumu za kuadhimisha afya, maji wala mfano wa hayo. Ujahili wao uligandana na kupata mali pamoja na starehe kwa njia zozote. Kwa ufupi hawakuwa na wakati wa kupoteza, iwe ni wajinga ama werevu. Na kwa hakika, ujinga wa akina Abu Jahal na wenziwe umeshavunjwa rekodi kwa kutufikia Siku ya Wajinga duniani. Juu ya ujinga wao kina Abu Jahal, hawakufikia hatamu ya kufanya ujinga kuwa ndio ibada yao kwa siku nzima. Leo imefikia wakati hata kiongozi mkuu wa nchi anafanyiwa mzaha wa kumtoa machozi, lakini akajifanya kucheka ilhali ndani ya nafsi yake anaungua kwa uchungu. Kwa lipi?! Ati ni April Fool! Ndugu Waislamu, hizi ni siku ambazo zimewekwa kuzidhibiti vyema akili za Waislamu ili wasiweze kuzitambua hila zinazofanywa dhidi yao. Yatosha Muislamu kuiharamisha siku hiyo kwa kupotezewa muda pamoja na kufanywa punguwani (mkosefu wa akili). April Fool ni siku iliyoanza kuadhimishwa huko Magharibi ikaenea ndani ya miji ya Waislamu kwa kasi sana na ikashtadi katika vyombo vya habari na kuendelea kwa uvumbuzi wa teknolojia haswa internet. Makafiri hukaa na kufurahi kwa kicheko cha juu wanapotuona nasi tunawasaidia kulisukuma gurudumu la ujinga. Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anasema kwamba hila za Mayahudi na Manaswara hazitafikia mwisho hadi watuone tupo sawa na wao: {{“Mayahudi hawatokuwa radhi nawe, wala Wakristo, mpaka ufuate mila yao”}} [Suratul-Aal-'Imraan: 120] Naye Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) anasema: ((Mtafuata desturi (mwenendo) za waliokuwa kabla yenu shibri kwa shibri na pima kwa pima hata wakiingia katika shimo la mburukenge (yaani ndani ya shimo lenye mnyama anayeweza kukudhuru) mutaingia nao.)) Wakauliza: “Je, unakusudia Mayahudi na Manasara?” Akasema: ((Ni nani wengine ikiwa si wao)) [Imesimuliwa na Al Bukhaariy na Muslim kutoka kwa Abu Sa‘iyd al-Khudriy]. Ni ajabu pale Muislamu anapoumia kwa kukosa kumfanya mwenziwe mjinga ndani ya siku hii, lakini si mwenye kuhuzunika kwa kuwaona Waislamu wanatolewa roho zao Palestina na Iraaq. Wala hana hisia kwamba Swalah za faradhi zinampita ama kuna Kitabu cha Allaah chahitaji kufanyiwa kazi. Tuelewe kwamba makosa mengi yamefanyika kwa kuiadhimisha siku hii, miongoni mwa hayo ni pale masikini walipotangaziwa kwenda kupokea msaada wa chakula katika kituo kimoja cha redio, na walipofika wakaambulia maneno hata wasiyoyafamu: "April Fool". Hii ni dhulma kubwa na dua'a ya mwenye kudhulumiwa hairudi. Basi ndugu zangu Waislamu, haujafikia wakati tukatubu madhambi yetu? Toba ambayo itatufanya kuacha kuwaona Makafiri ni bora na badala yake tukausimamisha Uislamu ndani ya majumba yetu, ukasimama mtaani na ukaenea nchini na duniani kote.

Zingatio La Wiki
‘Abdun-Naaswir Hikmany
Ujahili ulipokatwa panga zile enzi za Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), ulihakikisha umeondosha mambo yote ya kijahili kama vile kuwazika mabinti wakiwa hai, ribaa, uzinifu, pombe na mengineyo.
Kwa hali zilizokuwepo sasa, yaonesha dhahiri kwamba ujinga uliopo leo umepindukia mipaka ya hizo enzi alizokuwa akiishi Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Makhalifa wake (Radhiya Allaahu ‘Anhum). Majahili wa siku hizo hawakuwa na siku maalumu za kuadhimisha afya, maji wala mfano wa hayo. Ujahili wao uligandana na kupata mali pamoja na starehe kwa njia zozote. Kwa ufupi hawakuwa na wakati wa kupoteza, iwe ni wajinga ama werevu.
Na kwa hakika, ujinga wa akina Abu Jahal na wenziwe umeshavunjwa rekodi kwa kutufikia Siku ya Wajinga duniani. Juu ya ujinga wao kina Abu Jahal, hawakufikia hatamu ya kufanya ujinga kuwa ndio ibada yao kwa siku nzima. Leo imefikia wakati hata kiongozi mkuu wa nchi anafanyiwa mzaha wa kumtoa machozi, lakini akajifanya kucheka ilhali ndani ya nafsi yake anaungua kwa uchungu. Kwa lipi?! Ati ni April Fool!
Ndugu Waislamu, hizi ni siku ambazo zimewekwa kuzidhibiti vyema akili za Waislamu ili wasiweze kuzitambua hila zinazofanywa dhidi yao. Yatosha Muislamu kuiharamisha siku hiyo kwa kupotezewa muda pamoja na kufanywa punguwani (mkosefu wa akili). April Fool ni siku iliyoanza kuadhimishwa huko Magharibi ikaenea ndani ya miji ya Waislamu kwa kasi sana na ikashtadi katika vyombo vya habari na kuendelea kwa uvumbuzi wa teknolojia haswa internet.
Makafiri hukaa na kufurahi kwa kicheko cha juu wanapotuona nasi tunawasaidia kulisukuma gurudumu la ujinga. Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anasema kwamba hila za Mayahudi na Manaswara hazitafikia mwisho hadi watuone tupo sawa na wao:
{{“Mayahudi hawatokuwa radhi nawe, wala Wakristo, mpaka ufuate mila yao”}} [Suratul-Aal-'Imraan: 120]
Naye Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) anasema:
((Mtafuata desturi (mwenendo) za waliokuwa kabla yenu shibri kwa shibri na pima kwa pima hata wakiingia katika shimo la mburukenge (yaani ndani ya shimo lenye mnyama anayeweza kukudhuru) mutaingia nao.)) Wakauliza: “Je, unakusudia Mayahudi na Manasara?” Akasema: ((Ni nani wengine ikiwa si wao)) [Imesimuliwa na Al Bukhaariy na Muslim kutoka kwa Abu Sa‘iyd al-Khudriy].
Ni ajabu pale Muislamu anapoumia kwa kukosa kumfanya mwenziwe mjinga ndani ya siku hii, lakini si mwenye kuhuzunika kwa kuwaona Waislamu wanatolewa roho zao Palestina na Iraaq. Wala hana hisia kwamba Swalah za faradhi zinampita ama kuna Kitabu cha Allaah chahitaji kufanyiwa kazi.
Tuelewe kwamba makosa mengi yamefanyika kwa kuiadhimisha siku hii, miongoni mwa hayo ni pale masikini walipotangaziwa kwenda kupokea msaada wa chakula katika kituo kimoja cha redio, na walipofika wakaambulia maneno hata wasiyoyafamu: "April Fool". Hii ni dhulma kubwa na dua'a ya mwenye kudhulumiwa hairudi.
Basi ndugu zangu Waislamu, haujafikia wakati tukatubu madhambi yetu? Toba ambayo itatufanya kuacha kuwaona Makafiri ni bora na badala yake tukausimamisha Uislamu ndani ya majumba yetu, ukasimama mtaani na ukaenea nchini na duniani kote.