Friday, December 7

Jaji Mark Bomani awashukia polisi

ASEMA WANATUMIA ZAIDINGUVU KULIKO MAARIFA
KUJIRUDIA kwa matukio ya polisi kutumia silaha za moto dhidi ya raia, kumepokewa kwa hisia tofauti, huku Mwanasheria Mkuu wa Kwanza wa Serikali, Jaji Mark Bomani akilitaka jeshi hilo kuacha kutumia nguvu wanapokuwa katika operesheni zao.Wakizungumza jana kwa nyakati tofauti kuhusu tukio la hivi karibuni la kupigwa risasi mwandishi wa habari wa gazeti la Tanzania Daima, watu wa kada mbalimbali walisema, kitendo cha polisi kutumia nguvu sio busara.
Jaji Bomani kitendo cha polisi kutumia nguvu badala ya busara katika operesheni zao kinaweza kuleta uhasama kati ya wananchi na jeshi hilo.
“Kwa ujumla matumizi ya nguvu kwa polisi si mazuri  na nadhani tunatakiwa kubadilika katika hilo.” alisema Jaji Bomani. 
Bomani alieleza kuwa  kwa ujumla polisi wanatumia vibaya silaha zao ingawa bado hajapata uhakika wa jinsi  tukio la kujeruhiwa kwa Matutu lilivyokuwa .
Alisema tukio la Mwangosi lilikuwa baya zaidi lakini picha anayoiona na kuihusisha na tukio la juzi, ni kuwa kuna matumizi mabaya ya mashambulizi ya polisi kwa raia.
Hata hivyo wakati Jaji Bomani akieleza hayo Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Jaji mstaafu Amiri Ramadhan Manento  alisema kila tukio linalofanywa na polisi linatakiwa kufanyiwa uchunguzi kabla ya kuanza kulizungumzia.
Jaji Manento alisema akiwa ni mwanasheria hawezi kutoa hitimisho ya tukio la kujeruhiwa kwa Matutu kabla ya uchunguzi wa kisheria kufanyika.
“Tunahitaji kujua mambo mengi, ya michakato ya makosa ya jinai, (criminal procedure) kwa mfano polisi walipoingia walifanya nini, walipotoka, ni maneno gani walimuuliza mtu wa kwanza waliyekutana naye.
Tunahitaji kujua iwapo walitumia kizuizi cha usalama(safe cage) katika silaha zao au la” alisema Jaji Manento
Alisema kulingana na taarifa zilizopo katika magazeti bado unahitajika uchunguzi wa kujua  ni namna gani polisi waliingia ndani ya nyumba hiyo.
Aidha Jaji huyo mstaafu alisema hawezi kuwahukumu polisi moja kwa moja kwani hakuna ushahidi kuwa walikuwa wakimwinda mwandishi, bali inawezekana waligundua kuwa ni mwandishi baada ya kumjeruhi.
Alisema hili ni tukio la tofauti na lile la kuuwa kwa Mwangosi kwani Mwangosi alikuwa kashika vifaa vyake vya kazi lakini hapa Matutu hakuwa na kitambulisho chochote kuwa ni Mwandishi.
“Unajua polisi wanafuata amri na sheria na wapo kwa ajili ya kulinda raia wake, hivyo hatuwezi kusema kuwa walikuwa wakimwinda mwandishi, kwa sababu hata polisi naye amejeruhiwa kwa panga katika tukio hilo,” alisema Jaji Manento
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Dk Kitila Mkumbo alisema kuwa jeshi la Polisi limekuwa halifanyi kazi zake kwa kufuata weledi hali inayosababisha kuongezeka kwa matukio ya raia kupigwa risasi na Taasisi ya serikali yenye dhamana ya kuimarisha usalama wa raia hao.
“Matukio haya yanaweza kuathiri amani ya nchi kwa sababu wananchi wakikosa imani na serikali yao wanaweza kufanya jambo lolote bila kufuata sharia, matokeo yake amani inatoweka” alisema Dk Mkumbo.
Dk Mkumbo aliongeza kuwa ni vema IGP Saidi Mwema akatilia mkazo juu ya kufanya kazi kwa weledi ili kuimarisha utendaji kazi wa jeshi la polisi na kulipa taswira mpya katika jamii.
Mkuu wa Idara ya Fedha waskuli ya Biashara chuoni hapoDk Esther Ishengoma alisema kuwa jeshi la Polisi linadhamana ya kulinda usalama wa raia na mali zao, litaendelea kubeba dhamana hiyo, jambo la msingi ni kudhibiti nidhanu ya askari wanapokuwa wakitekeleza majukumu yao.

“Ukiangalia matukio yanayotokea utaona kuna baadhi ya askari polisi wanaolichafua jeshi kwa kufanya mambo kinyume cha sheria, ni vema suala la nidhamu likaimarishwa ili kuongeza ufanisi,” alisema Dk Ishengoma.
Mkazi wa Mbagala Mtongani Solomon Isaiah alisema matendo yanayofanywa na polisi ya kujeruhi na kuua raia  ndani ya kipindi kifupi ni dalili za kutokuwepo utawala bora nchini na usimamizi mzuri wa ngazi za juu ndani ya Polisi.
“Hawa polisi hawajitakii kufanya hivyo bali wanatekeleza amri za viongozi wao wa ngazi za juu, hivyo basi lawama, hatua za kisheria  na mabadiliko yafanyike kwenye ngazi hizo za juu za polisi ndipo wahamie kwa polisi wenyewe” alisema Isaiah.
Matukio ya kuua na kujeruhi raia yanayotekelezwa na jeshi la polisi yamezidi kuongezeka siku hadi siku nchini licha ya wadau na wananchi kupigia kelele matendo hayo hali ambayo imezidi kugharimu maisha ya Watanzania wengi wasio na hatia kwa kuchukua sheria mkononi.
Hivi karibuni Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kiliazimia kuishtaki Serikali kwa Mahakama ya Kimataifa ya masuala yaUhalifu(ICC) ili ichukue hatua zaidi juu ya mfululizo wa matukio ya kutisha yanayofanywa na jeshi la polisi kwa Wananchi baada ya Serikali kushindwa kuchukua hatua stahiki.
Kauli hizo imekuja siku moja baada ya polisi kulizungumzia tukio hilo kwamba lilitokea wakati wakiwa wanajihami.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kinondoni Charles Kenyela akizungumzia tukio la mwandishi huyo kupigwa risasi alisema alijeruhiwa baada ya kuanza kumshambulia askari kwa Panga.
Hata hivyo ufafanuzi wa kamanda huyo unatofautiana na ule wa Matutu na mashuhuda wa tukio hilo, ambao walisema kuwa polisi walivamia nyumba ya mwandishi huyo iliyopo maeneo ya Kunduchi huku wakimtaka mwanamke mmoja waliyemtaja kwa jina la mama J.
Katika maelezo yake Matutu alisema polisi hao walifika nyumbani kwake wakimtaka mkewe baada ya kumfananisha na mtu mwingine, kwamba wakati akiwa katika harakati za kumtenganisha mke polisi hao baada ya kuhisi  huenda wakawa majambazi ndipo polisi hao wakampiga risasi ya b

Monday, November 19

RIPOTI YA TUME YA KUCHUNGUZA AJALI YA MELI YA MV. SKAGIT YAWEKWA HADHARANI.


Katibu Mkuu Kiongozi wa Serekali ya Mapinduzi Zanzibar Dk. Abdulhamid Yahya Mzee, akionesha ripoti ya Tume ya Uchunguzi wa kuzama kwa Meli ya MV Skagit katika bahari ya Zanzibar ikitokea Dar-es- Salaam, ripoti hiyo tayari imeshakabidhiwa kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, Ikulu Zanzibar. Katibu Mkuu Kiongozi amesema ripoti hiyo itakuwa katika Makumbusho ya Nyaraka za Kale Kilimani.
Na RAMADHANI ALI-HABARI MAELEZO             
Tume iliyoundwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kuchunguza ajali ya meli ya MV. Skagit iliyotokea tarehe 18.7.2012 ilipokuwa ikitokea Dare s Salaam kwenda Zanzibar imependekeza kuchukuliwa hatua za kisheria na kinidhamu watu saba kwa makosa mbali mbali yaliyochangia kutokea kwa ajali hiyo ili kuhakikisha kunakuwepo uwajibikaji kwa wamiliki wa vyombo vya usafiri wa baharini na watendaji wa Taasisi zinazosimamia suala hilo na kuepusha ajali za mara kwa mara.
Akitoa taarifa ya Tume hiyo kwa Waandishi wa Habari katika Ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo Mnazimmoja, Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Abdulhamid Yahya Mzee amewataja watu waliopendekezwa kuchukuliwa hatua za kisheria ni mmiliki wa MV.Skagit ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa  Kampuni ya Seagull Sea Transport Said Abdul-rahman Juma, Nahodha wa meli hiyo Makame Mussa Makame na Meneja wa Kampuni hiyo tawi la Dar es salaam Omar Hassan Mkonje.
Amesema kutokana na matendo yao ya kuwa karibu mno na sababu zilizopelekea kutokea kwa ajali hiyo, Tume imependekeza watu hao washtakiwe kwa kosa la kusababisha vifo kutokana na uzembe.
Mmiliki wa kampuni hiyo amefanya kosa la  kufanya biashara ya usafiri wa baharini kwa kutumia chombo ambacho hakikusajiliwa kwa mujibu wa sheria na kutumia chombo ambacho hakikutimiza masharti ya ukaguzi kwa mujibu wa sheria ya usafiri wa baharini Zanzibar namba 5 ya mwaka 2006, kumuajiri nahodha bila ya kuwa na cheti cha umahiri cha daraja la tano  na kuruhusu meli kupakia idadi kubwa ya abiria kinyume na uwezo wake.
Abdulhamid amesema taarifa hiyo imesema Nahodha Makame Mussa ametenda kosa la kuendesha meli akiwa hana cheti, kushindwa kuwaandaa abiria  kujiokoa wala kutoa taarifa ya dharura, kuendesha meli hali ya kuwa si salama na kuruhusu kupakia abiria 431 badala ya 250 iliyoainishwa kwenye cheti cha abiria.
Watu  waliopendekezwa kuchukuliwa hatua za kinidhamu ni  aliekuwa Mkaguzi wa meli na Kaimu Mrajisi wa meli kutoka Mamlaka ya usafiri wa baharini Zanzibar Juma Seif Juma, Mkaguzi wa kujitegemea Capt. Saad Shafi Adam na Maafisa wa usalama wa bandari ya Dar es Salaam Johari Mikidadi  Ndumbati na Peter Ndimbwa Mwasi kwa kushindwa kudhibiti uingizaji wa abiria katika meli ya MV. Skagit siku iliyopata ajali ikiwa ni kinyume na majukumu yao ya kazi.
Taarifa hiyo imetoa mapendekezo ya kuimarisha Sheria na kanuni za usafiri wa baharini namba 5 ya 2006 kwa kuvifanyia marekebisho baadhi ya vifungu ikiwemo kuweka utaratibu wa kisheria utakaowalazimisha wafanyabiashara wa usafiri wa baharini kuwa na utaratibu wa kuuza tiket za safari pamoja na kutengeneza urodha ya wasafiri kwa njia ya electroniki na kuweka utaratibu wa kisheria unaowalazimisha uongozi wa kampuni unaoendesha biashara ya usafiri wa baharini kuwa na taaluma ya masuala ya usafiri wa baharini.
Aidha Abdulhamid amesema Tume hiyo imependekeza Kampuni kuwalipa fidia abiria wote waliokuwemo ndani ya meli.  Kwa  waliofariki walipwe thamani ya kiwango cha mshahara wa chini cha muda wa miezi 80 na walionusurika na kupata ulemavu walipwe asilima 75 ya kiwango cha waliofariki na watu wengine walionusurika bila ya kupata majeraha yoyote walipwe asilimia 50 ya kiwango   walicholipwa waliofariki.
Katika ajali hiyo watu 81 wakiwemo raia watatu wa kigeni walifariki na maiti zao zilipatikana na kuzikwa,  212 walipotea na 154 waliokolewa wakiwa hai wakiwemo raia 15 wa kigeni.
Katibu Mkuu Kiongozi amesema Tume imeeleza sababu za kutokea ajali hiyo kuwa ni upepo mkali, muundo wa meli ilioruhusu abiria wengi kukaa juu, mwendo wa kasi, nahodha kukosa ujuzi na umahiri na abiria kuwa wengi kupita kiwango chake.
Amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imekubaliana na mapendekezo yote yaliyotolewa na Tume hiyo iliyokuwa na wajumbe 10 chini ya mwenyekiti wake Jaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar Abdulhakim Ameir Issa.

Tuesday, October 23

the streets of Arusha, Tanzania – www. Benwilhelmi.com

A beautiful early morning with a great light. Colors were bright and intense. I was simply walking around shooting in digital but I was also equipped with a Leica M and Kodachrome film as a historic tool But I’ll have to wait to develop these special films in the US. Another day, it was the Rolleiflex in B/W as a complement. I’ve said it before but I just love using older equipment, some of the very equipment that has created the visual 20th century. Another philosophy.
US style school bus but English make. There are 2 accredited (and expensive) international schools in Arusha. A 3rd one only pretends to be. Africa can be cheap to live for ex-pats, except for the kids. My ex boss with 3 daughters at various school level said once he was paying a total of 40.000$ a year for them. No wonder our salaries were not the best in TZ… add the flights home usually once a year, a medical insurance…
the use of helmet is still not perceived as a must. Coming very slowly, but very. Here is one the new moto-cabs that appeared all over town a few months ago. No licensing, no rules but they are already considered hazardous. This is Clocktower, one of the roundabouts in town. I think roundabouts are better suited for the undisciplined drivers here, and cheaper than the only 2 crossroads with lights and it works the same I guess.
I’m always puzzled how the West is copied first for its craps it has to offer to 3rd world countries, like ugly advertising in any form, cheap entertainment like Madonna or Rambo or rap music, lack of planning or foreseeing, consumerism…I mean “ to keep up with the Joneses” existed before, they just replaced the cows and the wives by Mercedes and mistresses and golden watches and whatever is bling bling…for those who jump on the band wagon, I usually pee on Mr Politically Correct. Anyway this is not even racism, white “nouveaux riches” just follow the same pattern more often than not, right?
dangerous driver in the making…
Clocktower and the new movie boards that show wildlife scenes. I thought initially that this would be a distraction for drivers but it seems that they couldn’t get worse so the accident rate didn’t rise. Now I don’t mind it’s there in full sight, maybe kids will develop some wildlife awareness…
another roundabout, again with a wildlife theme.
many town have a monument for the armed forces.
luckily the soldiers fight better than they create monuments, always built in the same papier-mâché style. Ugly, looks like done by kindergarten kids. But hey, they kicked Amin Dada’s fat butt out of Uganda in 1978, not bad at all.
view of Mount Meru towards the NE. This tricycle is also part of a new arrival. All the rage in Dar es Salaam as taxis mostly, they arrive slowly in Arusha.
common scenery, street vendor pushing an Ali Baba cartwheel.
one of my enemies…well no these drivers are everybody’s enemies. If killing was permitted, they’d be high on the victims’ list. The guy in blue and his peers are the clowns I watch the most: he has the job to attract and prey on potential passengers, so he is the one banging on the door to tell the driver to stop, who happily obliges without thinking and looking for anything else. I don’t even notice but I have developed an instinct to bring my fingers around the brake levers without thinking when I spot one of these dala dalas or matatus (still waiting and hoping for my eyes to develop like chameleon’s eyes though). But finally, after 11 years, I may think it is safer to ride here than in Europe. Here I’m always, just always on high alert as if surrounded by hitmen. Whereas in Europe I might expect some form of politeness and consideration from drivers and relax a bit too much…then I’d get hit by the clumsy one who didn’t pay attention…

Tuesday, August 28

SOON MOROGORO ROAD DAR ITAKUWA HIVI


HII NDIYO MANZESE MPYA

VITUO VYA MABASI VITAKUWA HIVI

EXPRESS TRAINS

MABASI YAENDAYO KWA KASI



Sunday, June 17

Chadema, CUF waungana kuikataa Bajeti

MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba ameungana na wenyeviti wa vyama vingine vya siasa vya upinzani kupinga Bajeti ya Serikali ya 2012/2013, akisisitiza kuwa kamwe chama chake na wabunge wake, hawataiunga mkono.

Lipumba aliiponda Serikali akisema kuwa nchi inahitaji uongozi wenye uwezo wa kusimamia rasilimali za nchi na matumizi ya fedha za umma.

Aliikosoa Serikali akisema imeshindwa kubuni vyanzo vipya vya mapato huku kukiwa na udhaifu mkubwa katika usimamizi wa matumizi ya fedha za umma zinazokusanywa kutoka katika vyanzo vya mapato vilivyopo.

Kwa kauli hiyo, Lipumba ameungana na wenyeviti wenzake wa vyama vya upinzani, Freeman Mbowe wa Chadema na James Mbatia wa NCCR-Mageuzi ambao pia waliiponda Bajeti hiyo wakisema haina jipya.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti baada ya kuwasilishwa kwa Bajeti hiyo Alhamisi usiku, wenyeviti hao walisema hakuna matumaini kwa Watanzania kupitia Bajeti hiyo kwani fedha nyingi zimelundikwa kuwanufaisha wachache huku umma ukiambulia patupu.

Kwa upande mwingine, wabunge wa CCM juzi walikutana kwa zaidi ya saa tano katika kikao ambacho waliibua hoja ya kutaka kuchunguzwa kwa Mfuko Mkuu wa Serikali kwa maelezo kwamba kuna dalili za kuwapo ufisadi.

Habari kutoka ndani ya kikao hicho kilichoongozwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda zinasema msingi wa hoja hiyo iliyotolewa na Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka na kuungwa mkono na wabunge wengine, ni kutokuwapo kwa uwiano kati ya fedha zilizokusanywa na Mamlaka ya Mapato (TRA) pia kutoka kwa wahisani na zile zilizopelekwa katika wizara na idara za Serikali.

Prof Lipumba

Akizungumza na waandishi wa habari, Profesa Lipumba akizungumza na waandishi wa habari jana katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi za Upinzani Bungeni, alisema CUF ina sababu za msingi kupinga Bajeti hiyo kwa sababu hailengi kumsaidia kabwela kuondokana na umaskini na gharama kubwa za maisha.

“Bajeti ya mwaka 2011/12 Serikali ilieleza kwamba inatambua changamoto zinazowakabili wananchi, lakini hadi sasa hali bado ni ngumu. Mfumuko wa bei umefikia asilimia 20, bei ya mafuta bado ipo juu. Mfumuko wa bei ya chakula umefikia asilimia 24 na sasa inasababisha asilimia 50 ya mapato ya Watanzania wengi kutumika kwa chakula,” alisema Prof Lipumba.

Profesa Lipumba alisema, Serikali imekuwa bingwa wa misamiati katika bajeti na kutangaza mambo mengi, bila kujali vipaumbele ambavyo imeshindwa kuvitekeleza.

“Tunasema sekta muhimu kama kilimo, katika jedwali namba 26 katika bajeti, la mgawo wa fedha, bado fedha zilizotengwa kwa kilimo ni kidogo tofauti hata na makubaliano na nchi za SADC ambayo yanapendekeza nchi kutenga walau asilimia 10 ya bajeti yake, ili kuhakikisha kilimo kinaongezwa na kuondoa tatizo la uhaba wa chakula,” alisema.

Alisema kuna miradi inayotengewa fedha kila wakati wa Bajeti, kama wa kuzalisha Megawati 61 za umeme wa Nyakato, Mwanza na ule wa Kinyerezi, lakini kwa miaka mitano sasa, hakuna kilichokamilika.

Matumizi hewa

Alisema katika Bajeti ya mwaka 2011/12 Serikali ilipanga kufanya sensa ya watumishi kulipwa mishahara madirishani ili kubaini wafanyakazi hewa, lakini katika Bajeti ya mwaka huu, mpango huo haujaelezwa kabisa, wala hatua iliyofikiwa mwaka uliopita.

Alisema tatizo kubwa linaloikabili Serikali ni ombwe la uongozi, hakuna nidhamu ya matumizi ya fedha za umma, viongozi wanajiamulia mambo bila kuulizwa zikiwamo safari za nje na kulipana posho bila kuwa na utaratibu.

Profesa Lipumba alisema inashangaza katika hesabu za Bajeti iliyopita, kuna fedha nyingi zimetajwa kukusanywa ndani na nje ya nchi, lakini bado kuna miradi iliyopewa fedha chini ya asilimia 30 ya mahitaji.

Alisema kukosekana ubunifu katika Bajeti, kumesababisha Serikali kuanzisha kodi ya wenye magari ambao watataka kuweka majina yao badala ya namba na kwamba makadirio yake ya Sh5 milioni zilizopangwa zitawezesha kupatikana kwa watu 10 tu badala ya kupunguza kodi hiyo ili kupata watu wengi zaidi.

“Hapa inaonyesha ni jinsi gani uandaaji wa Bajeti yetu una matatizo. Kama unaweza kupanga kodi ya Sh5 milioni na ukategemea kupata watu 10, kwa nini kodi hiyo isipunguzwe na kupata watu wengi zaidi, sidhani hata hawa wanaoandaa Bajeti kama hii wanaipitia vizuri,” alisema Profesa Lipumba.

Mfumo wa Bajeti

Profesa Lipumba alisema mfumo wa Bajeti ya Tanzania unakabiliwa na matatizo mengi, kwanza, kutoshirikisha wadau kwa muda mwafaka, kukosa mipango ya kupata vyanzo vipya vya kodi na kutopangwa kwa uwiano mzuri wa makusanyo na matumizi na kuandaliwa kwa vipaumbele.

Alieleza kuwa inashangaza Serikali, katika Bajeti kueleza mapato ya ndani kuwa taifa linatarajia kukusanya kiasi cha Sh8.7 trilioni lakini hapohapo matumizi ya kawaida yanakuwa Sh10.3 trilioni.

“Serikali inahitaji kukusanya fedha za ndani walau ziweze kutumika katika matumizi yote ya kawaida kabla ya kuomba misaada kwa wahisani,”alisema Lipumba.

Alisema kwa Serikali kuendelea kutenga fedha kidogo kwa mambo ya maendeleo kiasi cha Sh4.5 trilioni pekee ni tatizo kwani ni asilimia 30 tu ya fedha zote na kulingana na mipango ya Serikali na mahitaji yake inapaswa ifikie walau asilimia 40.

Alisema Bajeti hiyo inapishana sana na Mpango wa Serikali wa miaka mitano, Mpango wa Kupunguza Umaskini na Kukuza Uchumi Tanzania (Mkukuta) namba mbili na Malengo ya Milenia.

“Serikali inapaswa kuacha kuwa bingwa wa siasa kwa kutangaza mambo mengi bila kuwa na uwezo wa kuyatekeleza. Kama sasa katika taarifa ya hali ya uchumi iliyotolewa bungeni na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wassira kuwa Serikali ina mpango wa kuanza kutekeleza mpango wa ujenzi wa Reli ya Arusha- Musoma, Mtwara – Mbamba Bay, wakati reli muhimu kama ya kati bado inawashinda, kila siku inaelezwa utafanyika ukarabati mkubwa,” alisema Lupumba.

Mbowe na Mbatia

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema, “Hakuna mkakati wa makusudi wa kupunguza matumizi ya Serikali. Ahadi ya Serikali ya kupunguza matumizi kwa kupunguza posho zisizo na tija na matumizi mengine haikutekelezwa.”

Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Upinzani Bungeni, alisema ameshangazwa na kutokuwapo nyongeza za mishahara kwa watumishi wa umma, badala yake fedha nyingi kulundikwa katika matumizi ya kawaida ya Serikali.

“Mfumo wa kodi kama mlivyosikia ni mbaya kabisa, hakuna kinachoashiria kwamba mkulima wa kawaida atapunguziwa mzigo na badala yake wanaendelea kuwanufaisha wafanyabiashara wa vyakula kwa kuwaruhusu kuagiza nje bila kodi, hiki naweza kusema ni kichekesho,” alisema Mbowe na kuongeza:

“Hakuna ubunifu kwenye kupanua wigo wa kodi. Tungeweza kusikia katika construction (ujenzi) ambayo inakua haraka na inachukua asilimia 18 ya pato la taifa kwamba tungetoza kodi huko, badala yake ni yaleyale ya siku zote, kodi kwenye sigara, vinywaji na bia.”

Naye Mwenyekiti wa NCCR- Mageuzi, James Mbatia alisema kwamba, lazima Serikali ijifunze kubadilika, kwani kilichotangazwa kwenye Bajeti yake ni marudio ya miaka yote.

“Huwezi kuchukua hela zote ukaulundikia utawala halafu ukawaacha wananchi bila kitu, hicho ndicho tulichokiona leo. Sh10 trilioni ni kwa ajili ya mishahara na watumishi na matumizi ya kawaida, maendeleo ambako ndiko wananchi waliko kumeachwa tena kutegemea fedha za wafadhili,” alisema Mbatia ambaye pia ni Mbunge wa kuteuliwa na Rais.

Alisema, hata fedha zilizotengwa kwa ajili ya kujenga reli ni kidogo kwani mahitaji ni Sh3 trilioni na Serikali imetenga Sh1 trilioni kwa ajili ya kugharimia sekta nzima ya miundombinu.

Thursday, May 31

Unusual Words

A by no means exhaustive list of rare, obscure, strange and sometimes funny words and their meanings that only seem to crop up in crosswords and dictionaries. Words that are used so seldom, you wonder who invented them and why.

A
abacinate To blind by putting a hot copper basin near someone's eyes
abderian Given to incessant or idiotic laughter
abecedarian A person who is learning the alphabet
abligurition Excessive spending on food and drink
accubation The practice of eating or drinking while lying down
adelphepothia An incestuous desire for one's sister
adelphirexia An incestuous desire for one's nephew
adelphithymia An incestuous desire for one's niece
adoxography Skilled writing on an unimportant subject
aeolist A pompous windy bore who pretends to have inspiration
agelast A person who never laughs
agerasia The state of looking younger than one actually is
agraffe The wire that holds the cork in a champagne bottle
algerining Prowling around with the intent to commit burglary
alphamegamia The marriage between a young woman and an older man
anopisthography The practice of writing on one side of the paper
apodyopsis The act of mentally undressing someone
autohagiographer One who speaks or writes in a smug fashion about their own life and accomplishments
autolatry The worship of one's self
autotonsorialist One who cuts their own hair

B
basorexia An overwhelming desire to neck or kiss
bathykolpian Deep-bosomed
batrachophagous One who eats frogs
blandiloquent Speaking in a flattering or ingratiating manner
bletcherous Pertaining to something poorly or disgustingly designed
bombilate To loudly hum or buzz continuously
borborygmus The rumbling sound of gas passing through the intestine
brevirostrate Having a short nose
bromidrosis Strongly smelling perspiration
brontide The low rumbling of distant thunder

C
cachinnation Loud or hysterical laughter
cacoethes A bad habit or insatiable urge
cagamosis An unhappy marriage
callipygean Having well-shaped buttocks
cancatervate To heap up into a pile
capernoited Slightly intoxicated or tipsy
cataglottism Kissing using the tongue, French kissing
causeuse A sofa built for two people
charientism An artfully veiled insult
cheiloproclitic Being attracted to a person's lips
chirotonsor An alternate title for a barber
cleptobiosis The act of plundering food
clithridiate Key-hole-shaped
colposinquanonia Estimating a woman's beauty based on her chest
concilliabule A secret meeting of people who are hatching a plot
cruciverbalist One who loves doing crossword puzzles

D
dactylion The tip of the middle finger
dactylonomy Counting using one's fingers
decubitis The act or attitude of lying down
defenestrate To throw out of a window
dehisce To burst open, as the pod of a plant
dentiloquent Pertaining to one who talks through their teeth
dephlogisticate To make something fireproof
digamy A second marriage after the death or divorce of a previous spouse
dippoldism The act of beating or whipping school children
dompteuse A woman who trains animals

E
eccedentesiast One who fakes a smile, as on television
emunction The act of removing obstructions from or cleaning bodily passages
estrapade A horses's attempt to remove its rider
exsibilation The collective hisses of a disapproving audience

F
farctate The state of being stuffed with food (overeating)
filipendulous Suspended by a single thread
floccinaucinihilipilification The categorising of something that is useless or trivial
fuscoferuginous Having a dark rusty colour

G
gambrinous Being full of beer
gargalesis Heavy tickling
gargalesthesia The sensation caused by tickling
ginglyform Hinge-shaped
gongoozler An idle spectator
gossypiboma A surgical sponge accidently left inside a patient's body
gowpen A double handful
grapholagnia The urge to stare at obscene pictures
gymnophoria The sensation that someone is mentally undressing you

H
hadeharia The practice of constantly using the word "Hell" in speaking
hamartithia Being likely to make a mistake
hippopotomonstrosesquipedalian Pertaining to extremely long words
honorificabilitudinitatibus With honour

I
inaniloquent Speaking foolishly or saying silly things
interfenestration The space between two windows

J
jentacular Pertaining to breakfast
jumentous Smelling like horse urine

K
knismesis Light tickling
krukolibidinous The act of staring at someone's crotch
kyphorrhinos Having a nose with a bump in it

L
lalochezia The use of foul or abusive language to relieve stress or ease pain
lethologica The inability to recall a precise word for something
liripip The long tail of a hood in medieval or academic costume
lygerastia The condition of one who is only amorous when the lights are out

M
maledicent One who is addicted to abusive speech
mallemaroking The carousing of seamen on board Greenland whaling ships
mammothrept A child who is raised and spoiled by their grandmother
maritodespotism Tyrranical rulership of a woman by her husband
matronolagnia An attraction to older women, especially ones who have children
misocapnist One who hates the smell of tobacco smoke
misodoctakleidist Someone who hates practicing the piano
mulligrubs A state of depression or low spirits
mumpsimus One who sticks obstinately and wrongly to their old ways
mytacism The incorrect or excessive use of the letter M

N
nelipot Someone who walks without shoes
nepheligenous Producing clouds of tobacco smoke
nidorosity Belching with the taste of undigested meat
nudiustertian Pertaining to the day before yesterday

O
oculoplania Letting one's eyes wander while assessing someone's charms
onychophagy The habit of biting one's fingernails

P
pandiculation Stretching and yawning before going to bed or after waking up
petrichor The smell of rain on dry ground
philosophunculist One who pretends to know more than they do to impress others
pogonotomy The act of cutting a beard
polyphloisboian Making a lot of noise or loud racket
preantepenultimate Fourth from last
prosopography The description of a person's appearance
psithurism The sound of wind in trees or rustling leaves
pyknic Short and fat

Q
qualtagh The first person you see after leaving your house
quidnunc One who always wants to know what is going on
quomodocunquize To make money by any means possible

R
recumbentibus A knockout blow, either verbal or physical
runcation The act of weeding

S
sabrage The act of opening a bottle with a sabre
saprostomous Having bad breath
scacchic Pertaining to the game of chess, or to chess pieces
sciapodous Having huge feet
scolecophagous One who eats worms
sgiomlaireached The habit of dropping in at mealtimes
skoptsy The act of self castration
slubberdegullion A filthy, slobbering person
sphallolalia Flirtatious talk that leads nowhere
steatopygic Having a fat behind
strikhedonia The pleasure of being able to say to hell with it

T
tachyphagia Fast eating
tarantism An urge to overcome melancholy by dancing
tetrapyloctomy The act of splitting a hair four ways
thelemic Permitting people to do as they like
tibialoconcupiscent Having a lascivious interest in watching a woman put on stockings

U
ulotrichous Having very wooly hair
ultracrepidarian Of one who speaks or offers opinions on matters beyond their knowledge
usufructuary A person who has use or enjoyment of something, especially property

V
ventripotent Big-bellied, gluttonous
vesthibitionism The flirtatious display of undergarments by a woman
vigesimation The act of killing every twentieth person
viraginity Masculine qualities in a woman

W
wanweird An unhappy fate
witzelsucht A feeble attempt at humour

X
xenobombulate To malinger
xerophagy A diet of bread and water
ximelolagnia The urge to stare at women who are sitting with crossed legs
xylopolist One who sells wood products

Y
yclept By the name of; called

Z
zenzizenzizenzic A number raised to the eighth power

Friday, May 18

'Amali Za Kutenda Na Ya Kujiepusha Nayo Katika Mwezi Mtukufu Wa Rajab

Nasiha Za Minasaba Mbalimbali AlhamduliLLaah. Inapasa tumshukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Kutupa umri hadi kutufikisha mwezi mtukufu wa Rajab ambao ni fursa kwetu kutenda mema yatakayotuchumia thawabu nyingi kuliko miezi mingine. Mema ambayo hatuna budi kuyatenda kwa ajili ya kujenga Aakhirah yetu kabla ya siku hii kufika. Siku ambayo hakuna mmoja wetu yeyote atakayeweza kuikwepa. Basi hebu kila mmoja wetu ajiulize: "Nimetanguliza nini kwa ajili ya siku hiyo?" Siku ambayo safari yake ni ndefu mno. Vyovyote tutakavyobeba kama ni zawadi huko Aakhirah, hazitoshi wala hatuna hakika nazo kama zitapendekezeka au zitakuwa na thamani huko tuendako ambako kuna makazi ya milele tusiyokuwa na hakika nayo; ima moto au Pepo. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala): (( يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّهَ وَلْتَنظُرْ نَفْسٌ مَّا قَدَّمَتْ لِغَدٍ وَاتَّقُوا اللَّهَ إِنَّ اللَّهَ خَبِيرٌ بِمَا تَعْمَلُونَ)) ((Enyi mlioamini! Mcheni Allaah, na kila nafsi iangalie inayoyatanguliza kwa ajili ya Kesho. Na mcheni Allaah, Hakika Allaah, Anazo khabari ya mnayoyatenda)) [Al-Hashr: 18]. Vile vile ni miezi miwili tu imebakia kutufikia mgeni wetu tunayemsubiri kwa hamu kila mwaka, mwezi mtukufu wa Ramadhaan. Kwa hiyo ni fursa nyingine pia kujitayarisha kuupokea mwezi huo kwa kujizoesha ibada mbali mbali kama Swawm, tahajjud, na pia kutenda mema mengi ili tutakapofikia mwezi wa Ramadhaan tuwe na nguvu za kufanya zaidi ya tuliyoyazoea kutenda katika miezi hii iliyobakia miwili ijayo. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala): (( إِنَّ عِدَّةَ الشُّهُورِ عِندَ اللّهِ اثْنَا عَشَرَ شَهْرًا فِي كِتَابِ اللّهِ يَوْمَ خَلَقَ السَّمَاوَات وَالأَرْضَ مِنْهَا أَرْبَعَةٌ حُرُمٌ ذَلِكَ الدِّينُ الْقَيِّمُ فَلاَ تَظْلِمُواْ فِيهِنَّ أَنفُسَكُم )) ((Hakika idadi ya miezi kwa Allaah ni miezi kumi na mbili katika hukumu ya Allaah, tangu Alipoumba mbingu na ardhi. Katika hiyo iko mine mitakatifu. Hiyo ndiyo Dini iliyo sawa. Basi msidhulumu nafsi zenu humo)) [At-Tawbah: 36] Miezi minne hiyo imetajwa katika Hadiyth ifuatayo: عَنْ أَبَى بَكْرَة أَنَّ رَسُول اللَّه - صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ - قَالَ فِي حَجَّة الْوَدَاع : (( إِنَّ الزَّمَان قَدْ اِسْتَدَارَ كَهَيْئَتِهِ يَوْم خَلَقَ اللَّه السَّمَوَات وَالْأَرْض السَّنَة اِثْنَا عَشَر شَهْرًا مِنْهَا أَرْبَعَة حُرُم : ثَلَاث مُتَوَالِيَات ذُو الْقَعْدَة وَذُو الْحِجَّة وَالْمُحَرَّم وَرَجَب مُضَر الَّذِي بَيْن جُمَادَى وَشَعْبَان)) صَحِيح الْبُخَارِيّ Kutoka kwa Abu Bakrah ambaye amesema: "Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa wa sallam) amesema alipokuwa katika Hijjah ya kuaga (Hijjah wa mwisho): ((Mgawanyo wa nyakati umerudi kama ulivyo (wakati) Allaah Alipoumba mbingu na ardhi. Mwaka una miezi kumi na mbili, minne ambayo ni mitukufu; mitatu inafuatana pamoja (nayo ni) Dhul-Qa'adah, Dhul-Hijjah na Muharram, na (wa nne ni) Rajab wa (kabila la) Mudhwar ambao upo baina ya Jumaada na Sha'abaan)) [Al-Bukhaariy] Katika miezi yote kumi na mbili Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Ameichagua hii minne na Ameifanya kuwa ni mitukufu na kusisitiza kuitakasa, na kwamba dhambi zitakazofanyika humo ni zaidi na hali kadhalika thawabu za vitendo vyema zinakuwa maradufu na zaidi. [Atw-Twabariy 14: 238] Ni sawa kama Anavyoonya Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) kufanya maasi katika sehemu tukufu Alipotaja Masjidul-Haraam (Msikiti Mtukufu Makkah): ((إِنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا وَيَصُدُّونَ عَن سَبِيلِ اللَّهِ وَالْمَسْجِدِ الْحَرَامِ الَّذِي جَعَلْنَاهُ لِلنَّاسِ سَوَاء الْعَاكِفُ فِيهِ وَالْبَادِ وَمَن يُرِدْ فِيهِ بِإِلْحَادٍ بِظُلْمٍ نُذِقْهُ مِنْ عَذَابٍ أَلِيمٍ)) ((Hakika wale waliokufuru na wakazuilia Njia ya Allaah na Msikiti Mtakatifu, ambao tumeufanya kwa ajili ya watu wote sawasawa, kwa wakaao humo na wageni. Na kila atakayetaka kufanya upotofu humo kwa dhulma, basi Tutamwonjesha adhabu iumizayo)) [Al-Hajj: 25] Qataadah amesema kuhusu kauli ya Allaah: (( فَلاَ تَظْلِمُواْ فِيهِنَّ أَنفُسَكُم)) ((Basi msidhulumu nafsi zenu humo)) "Dhulma itakayotendeka katika miezi mitukufu ni mbaya na kubwa (au hatari) kuliko dhulma itakayotendeka katika miezi mingine. Hakika dhulma daima ni makosa, lakini Allaah Hufanya baadhi ya vitu kuwa ni vizito kuliko vingine kama Anavyopenda". Akaendelea kusema: "Allaah Amechagua baadhi ya viumbe Vyake na baadhi ya vitu kuwa bora zaidi kuliko vingine. Amechagua Wajumbe kutoka Malaika na kutoka binaadamu. Vile vile Amechagua baadhi ya kauli Zake kuwa ni bora kuliko nyingine, Misikiti kuwa bora kuliko sehemu nyingine za ardhi, Ramadhaan na miezi mitukufu kuwa bora kuliko miezi mingine, siku ya Ijumaa kuwa ni bora kuliko siku nyingine, na usiku wa Laylatul-Qadr kuwa ni bora kuliko masiku mengine. Kwa hiyo takasa vile Alivyovitakasa Allaah, kwani kufanya hivyo ni vitendo vya watu wenye akili na wenye kufahamu" [Tafsiyr ya Ibn Kathiyr] Miongoni mwa yaliyokatazwa katika miezi hii mitukufu ni kama Anavyosema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala): (( يَسْأَلُونَكَ عَنِ الشَّهْرِ الْحَرَامِ قِتَالٍ فِيهِ قُلْ قِتَالٌ فِيهِ كَبِيرٌ وَصَدٌّ عَن سَبِيلِ اللّهِ وَكُفْرٌ بِهِ وَالْمَسْجِدِ الْحَرَامِ وَإِخْرَاجُ أَهْلِهِ مِنْهُ أَكْبَرُ عِندَ اللّهِ وَالْفِتْنَةُ أَكْبَرُ مِنَ الْقَتْلِ )) ((Wanakuuliza juu ya kupigana vita katika mwezi mtakatifu. Sema: Kupigana vita wakati huo ni dhambi kubwa Lakini kuzuilia watu wasiende katika Njia ya Allaah na kumkanusha Yeye, na kuzuilia watu wasiende kwenye Msikiti Mtakatifu na kuwatoa watu wake humo, ni makubwa zaidi mbele ya Allaah. Na fitina ni mbaya zaidi kuliko kuua..))[Al-Baqarah: 217] Hivyo basi katika mwezi mtukufu wa Rajab, maasi na mema yafuatayo yanatupasa kuzingatia: Maasi Mengine Ambayo Tunatakiwa Tujikumbushe Kuyaacha: - Kuiba; - Kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) kama kwenda kwa wachawi na waganga na kuwaamini wanayoyatabiri kwa watu; - Kuzini; - Kulewa; - Kumdhulumu mtu haki yake; - Kugombana, kutukanana, kuvunjiana heshima, kudharauliana n.k.; - Kusengenya (Ghiybah); - Kusema uongo, na kila aina ya uovu mwengine. Mambo Mema Ya Kukumbushana Kufanya Katika Mwezi Huu Mtukufu - Kuongeza Sunnah za Swalah; *(tazama maelezo chini) - Kufunga Swawm za Sunnah kama Jumatatu na Alkhamiys, Masiku meupe (Ayyaamul-biydhw) (tarehe 13, 14 na 15) na Swawm ya Nabii Daawuud (kufunga kila baada ya siku moja); - Kujielimisha mambo ya Dini kwa kusoma vitabu na kusikiliza mawaidha; - Kuomba Maghfirah na Tawbah; - Kufanya kila aina ya dhikr (kumkumbuka na kumtaja Allaah), kwa kusoma Qur-aan kwa wingi, kumshukuru, kumtukuza, kuomba du'aa n.k.; - Kuwasiliana au kutembeleana na ndugu na jamaa; - Kutenda wema kwa jirani, marafiki na watu wote kwa ujumla; - Kutoa sadaka; - Kulisha masikini; - Kupatanisha waliogombana; - Kuamrishana mema na kukatazana maovu, na mengi mengineyo katika vitendo vyema. * Swalah za Sunnah Ratiba Ya Swalah Za Sunnah Zilizosisitizwa Na Zisizosisitizwa ALFAJIRI Kabliya Rakaa 2 ADHUHURI Kabliya Rakaa 4 Baadiya Rakaa2 ALASIRI Kabliya Rakaa 4 MAGHARIBI Kabliya Rakaa 2 Baadiya Rakaa 2 'ISHAA Kabliya Rakaa 2 Baadiya Rakaa 2 Fadhila Zake: (( مَا مِنْ عبْدٍ مُسْلِم يُصَلِّي للَّهِ تَعَالى كُلَّ يَوْمٍ ثِنْتَيْ عشْرةَ رَكْعَةً تَطوعاً غَيْرَ الفرِيضَةِ ، إِلاَّ بَنَى اللَّه لهُ بَيْتاً في الجَنَّةِ ، أَوْ : إِلاَّ بُنِي لَهُ بيتٌ في الجنَّةِ )) رواه مسلم * ((Hatoswali mja Rakaa 12 zisizo za fardhi kwa siku, ila atajengewa [na Allaah] nyumba peponi)) [Muslim] Nazo ni hizo Muakkadah (Zilosisitizwa) jumla yake ni 12 (( ركْعتا الفجْرِ خيْرٌ مِنَ الدُّنيا ومَا فِيها )) رواه مسلم ** ((Rakaa mbili (za Sunnah) kabla ya Alfajiri ni kheri kuliko duniya na yaliyomo ndani yake) [Muslim] ‏‏((ما من عبد يسجد لله سجدة إلا كتب الله له بها حسنة ومحا عنه بها سيئة ورفع له بها درجة فاستكثروا من السجود)) رواه ابن ماجه ((Mja yeyote atakayesujudu sijda moja ataandikiwa wema mmoja, na atafutiwa baya moja, na atapandishwa daraja yake, kwa hiyo zidisheni kusujudu)) [Ibn Maajah] Swalah ya Tahajjud (( أفضل الصلاة بعد الفريضة صلاة الليل)) رواه مسلم ((Swalah iliyo bora kabisa baada ya Fardh ni Swalah ya usiku)) [Muslim] Swalah Ya Dhuhaa na Swalah Ya Witr عـَن أبي هـُريْرَة رضيَ الله عنه قال : أوصـَانـِي خـَليلي صـَلـَّى الله عليه وسلم بـِصـِيامِ ثـَلاثـَة ِ أيـَّام ٍ مـِنْ كـُل شـَهر ٍ، وَ ركـْعـَتي الضـُّحى ، وأنْ أوتـِرَ قبلَ أنْ أرقـُـد " ـ متفق عليه ـ Kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ‘anhu) kwamba “Ameniusia rafiki yangu Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam [mambo matatu]; kufunga siku tatu katika kila mwezi, Rakaa mbili Dhuhaa na niswali Witr kabla ya kulala” [Al-Bukhaariy na Muslim] Tunamuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Atuwezeshe kujitenga na maasi na kuzidisha mema katika mwezi huu mtukufu na Atufikishe Ramaadhaan. Aamiyn

Wednesday, May 16

Mzee Makamba awarushia kombora Nape, Pinda

Midraji Ibrahim, Dodoma BAADA ya ukimya wa muda mrefu, Katibu Mkuu mstaafu wa CCM, Yusuf Makamba ameibuka katika kikao cha Halmashauri Kuu ya chama hicho (Nec) na kumtuhumu Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye kwamba amekigeuza chama kuwa mali yake binafsi. Taarifa kutoka ndani ya kikao hicho, zimesema kwamba Makamba alisema hatua ya Nape kugeuza chama hicho kama taasisi yake binafsi ndiyo ambayo imesababisha kikose mwelekeo. Makamba licha ya kuelekeza mashambulizi yake kwa Nape, alimrushia pia kombora Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kuwa ana uhusiano mdogo na wananchi. “Mzee (Makamba) amesema hivi sasa CCM imekuwa kama jogoo anayepelekwa kwa mganga, kila anakoelekezwa ndo huko, hali hiyo ndiyo inakikumba CCM hivi sasa. Amemweleza Nape kuwa amegeuza chama kama mali yake binafsi, anafanya mambo nje ya utaratibu na anaangaliwa tu.” Makamba alidai kuwa badala ya sekretarieti kushughulikia matatizo ya chama, imekuwa ikihangaika na watu kwa sababu ya kutofautiana nao misimamo na wakati huo wakijidai kuzika tofauti ili kukiimarisha. Nape alipoulizwa kuhusu suala hilo alipuuza na kusema: “Si kweli, lakini ninyi andikeni tu maana tumewazoea.” Alipotakiwa kueleza kama Kingunge na Makamba walisema nini dhidi yake katika kikao cha Nec alijibu: “Walikuwapo, lakini hakuna kati yao aliyenitaja hata kwa jina.” Nape alitumia muda mwingi kulalamika kuwa taarifa nyingi ambazo zimekuwa zikitolewa kutoka ndani ya mkutano huo uliomalizika jana zimetoka kwa watu aliowataja kuwa wana maslahi nazo binafsi na kuhoji,” Kwa nini msiwe mnasubiri taarifa rasmi (za chama) ili habari iwe ya ukweli zaidi?” Mkongwe mwingine wa chama hicho, Kingunge Ngombale-Mwiru, ambaye anadaiwa kusikitishwa na vitendo vya rushwa na ugomvi vinavyoendelea ndani ya chama huku vikiangaliwa na viongozi kama vile vinakistawisha wakati vinakiporomosha. Kingunge alidai kuwa hivi sasa chama hicho kimetawaliwa na matajiri ambao ndiyo wanaopata nafasi za uongozi na maskini wanawekwa kando. Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Hamis Mgeja aliunga mkono suala la Pinda kuwa na uhusiano mdogo na wananchi na kwamba, amekuwa mkimya zaidi na hamsaidii Rais Jakaya Kikwete. “Yule Mwenyekiti wa Shinyanga, amemweleza Pinda kuwa ng’ombe wakila mazao mtu wa kwanza kuchapwa viboko ni mchungaji, halafu mmiliki anatozwa faini baadaye. Hivyo, alitakiwa kuwajibika kwanza kabla ya mawaziri walioondolewa,” kilidokeza chanzo chetu. Mgeja alidai kuwa uwajibishwaji wa mawaziri, haukuzingatia haki kwa sababu George Mkuchika, Profesa Jumanne Maghembe na Hawa Ghasia walilalamikiwa, lakini kilichofanywa ni kutoa kafara wengine na hao kubadilishiwa wizara. Pia, inadaiwa kuwa Mwenyekiti Kikwete aliwataka wajumbe kuzika tofauti zao ili kuweka msimamo wa pamoja kwa ajili ya ushindi kwenye Uchaguzi Mkuu ujao wa 2015 na kwamba adui namba moja wa CCM hivi sasa ni Chadema. Rushwa yakishtua chama Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye alisema Nec imejadili changamoto zinazokikabili chama kwenye uchaguzi unaoendelea na kubaini kuwa rushwa imekithiri. Nape alisema tishio la rushwa ni kubwa na mgombea atayakayethibitika kujihusisha na vitendo hivyo rushwa ataondolewa mara moja, huku viongozi na watendaji wakitahadharishwa kuchukuliwa hatua za nidhamu. “Kwa kisingizio cha kuwasalimia wajumbe, kuwapa nauli au kujitambulisha. Mgombea atakayethibitika anazunguka au amezunguka ataondolewa bila kuchelewa katika orodha ya wagombea,” alisema na kuongeza: “Kwa watendaji na viongozi wa chama ngazi zote kuanzia sasa ni marufuku kuwatembeza ndani ya maeneo yao, kwa nia ya kuwatambulisha kwa wapiga kura. Mtendaji au kiongozi atakayebainika anakiuka agizo hili, atachukuliwa hatua za nidhamu mara moja.” Pia, Nape alisema kuanzia sasa ni marufuku kwa watendaji na viongozi wa chama ngazi zote kuwaitia wagombea, wajumbe wa mikutano ya uchaguzi kwa lengo lolote, kwani vikao vya aina hiyo havimo katika katiba. Alisema vikao vya aina hiyo ni haramu na vinapalilia rushwa na kuongeza kwamba wanachama wa CCM wanatakiwa kupiga vita rushwa na kutoa taarifa ya vitendo hivyo katika ofisi za chama na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru). Aliitaka Takukuru kutomuonea aibu au kumuogopa mtu anayejihusisha na vitendo vya rushwa badala yake wamchukulie hatua. Mishahara na chakula Kuhusu mishahara ya watumishi wa umma na mfumuko wa bei ya chakula, Nape alisema Nec imeagiza Serikali kuhimiza waajiri kupandisha mishahara na malipo mengine kwa wafanyakazi wao ili waweze kumudu gharama za maisha. Alisema gharama za maisha zimepanda na mishahara inayolipwa haiendani na hali halisi. Alisema nayo Serikali inatakiwa nayo kupandisha mishahara kwa watumishi wake. “Serikali idhibiti malipo ya huduma ya ndani kwa kutumia fedha za kigeni, hasa Dola ya Marekani. Pia, iongeze udhibiti wa maduka na hoteli zinazofanya biashara ya fedha za kigeni ili kuondoa hujuma kwa uchumi wa nchi inayofanywa kutokana na uhuru uliokithiri katika biashara hii,” alisema. Nape alisema Serikali inatakiwa kuweka jitihada zaidi za kudhibiti ulanguzi wa bidhaa muhimu na upandishaji holela wa bei za vyakula, kodi za nyumba na usafiri. Alisema Nec imeagiza Serikali kuendelea kuchukua hatua za muda mrefu na kati za kukabiliana na tatizo la mfumuko wa bei. “CCM inaiagiza Serikali kuchukua hatua za haraka na muda mfupi ikiwamo kuangalia upya baadhi ya kodi katika vyakula pamoja na Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) katika sukari,” alisema Nape. Pia, Nape alisema wameagiza Serikali kupitia upya utaratibu wa ruzuku ya mbegu na mbolea ili upanuliwe kunufaisha wakulima wengi. Alisema Nec imeitaka Serikali iongeze kasi ya utekelezaji wa mpango wake wa kuongeza uwezo wa kuhifadhi chakula nchini, hasa kupitia Mamlaka ya Hifadhi ya Nafaka ya Taifa (NFRA), ikiwamo kujenga maghala zaidi ya mazao ya chakula maeneo ya uzalishaji na kutenga fedha nyingi zaidi kwa ununuzi wa mazao hayo. “Wakati wa uhaba wa vyakula maeneo ya mijini, kasi ya kupeleka chakula maeneo hayo iongezwe na utaratibu mzuri zaidi wa usambazaji chakula utumike ili walaji na siyo wasafirishaji na wasindikaji, wanufaike,” alisema.

Monday, May 14

Losing Jerusalem

Visiting Jerusalem is up for debate now, and it's good that it is being taken up and understood now. The question is not whether to visit Jerusalem or not, rather it is visiting it under Israeli's occupation. Islamic scholars have different opinions on this, all of which are respected. Let's look at it from the religious perspective first. Jerusalem has always been a sacred place as mentioned in the Holy Quran "... to Masjid Al-Aqsa, whose surroundings we have blessed..." (17:1). It is the land of prophets all of whom are revered and respected. This mosque is the place where all the prophets (May Allah be pleased with them all) met on the night of Isra. When the Holy prophet (PBUH) migrated to Madinah, the Muslims prayed in its direction for more than one and a half year. Being host to the third holiest place of Islam, Jerusalem is equally dear to Muslims, as it is for Jews and Christians. The holy Prophet (PBUH) has specifically mentioned Al-Aqsa Mosque to be visited along with the ones in Makkah and Madinah. So it's more important for Muslims to try and visit there if conditions allow. Though under Israeli occupation, we can still go there via Jordan. According to some scholars, it's like recognizing Israel, and they have a valid point too - in accepting the norms and procedures formed by the occupying Israeli government. But let's look at the other side as well. All these decades we have been "not recognizing Israel", but have also been losing an opportunity to visit Al-Quds. So just by going there, do we "recognize Israel"? No, as long as you are just going to fulfill your religious duty. We have the treaty of Hudaibiyah as an example, where the holy Kaabah was still in control of the Quraysh, but the Prophet (PBUH) and his companions made a pact with them, stayed in Makkah for three days and performed their pilgrimage. Did they recognize the Quraysh's ownership of the Kaabah? Definitely not.
Babri Masjid as it stood once in India Now coming to the political and strategic aspect - Israel has long been trying to drive out all the Palestinians from the remaining lands they hold. And it has been blocking all attempts to even talk of return of refugees to their own country. The only aim is to declare and let the whole world accept Israel as a Jewish state. More importantly there have been concerted efforts to Judaize the surroundings of the Al-Aqsa Mosque. Now if Muslims continue to isolate Jerusalem and Al-Quds, just because its under Israel, will it not boost their efforts to Judaize the whole of Jerusalem? The more number of Muslims visiting Al-Aqsa, the more Islamic right it retains. Of course, the struggle against the Israeli occupation can continue, but the more we shun Jerusalem the stronger will be the Judaization of Jerusalem. If we are honest with ourselves and with the Palestinians, we really don't see even a rare chance of Israel returning back the occupied territories in decades to come. So how long will we be leaving Jerusalem alone? And what do we say about the Muslim countries who already have either full diplomatic ties with Israel or have some tacit (hand in glove) understanding with Israel? Refrain from them as well? An interesting example should be of significance here: The destruction of historic Babri Masjid in India at the hands of right wing Hindu fanatics. The controversy and court cases over this issue were in existence ever since the British rule in India. At one time a court declared the complex locked for both Hindus and Muslims. And after decades the locks were opened and Hindus given access to perform their worship, thereby reducing the Muslims' chances of winning back the right to offer prayers in the Masjid. One of the significant stands taken by right wing propaganda in the run up to opening the locks for Hindus was - "No Muslim prayers were offered there for so many decades, No Muslim ever entered there so it cannot be a Masjid".

Saturday, May 12

ELIMU YA MADRASA TANZANIA:

BISMILLAHIR RAHMANIR RAHIIM
Historia, Matatizo na Taaluma za Walimu
MUHTASARI:
- Madrasa na Kazi zinazonasibishwa nazo.
- Historia ya Elimu ya Madrasa Tanzania.
- Sahihisho kwa madrasah zetu.
- Taaluma muhimu kwa walimu na madrasah.
· Njia na mbinu zakufundishia.
· Uendeshaji wa Madrasah kwa ujumla.
· Saikolojia ya watoto na malezi.
· Maarifa katika fani wanazofundisha.

1.0 UTANGULIZI

1.1 Neno la Awali
Kwa muda mrefu sasa taasisi muhimu ya kiislam, taasisi ya “madrasa” imeachwa na kupoteza hadhi yake. Pamoja na hilo, taasisi hii imeacha pengo kubwa ambalo halizibiki kwa urahisi ila kwa kuinua hadhi ya Madrasa zetu.
Umma wa Waislam unazidi kupata kizazi kinachokosa haki za kimsingi za kuandaliwa kama madhalifa. Mwenyezi Mungu katika Qurani 51:56 ametwueleza “SIKU WAUMBA MAJINI NA WATU ILA WANIABUDU” ili kutekeleza lengo hilo, waislamu lazima waipe hadhi Madrasa. Kadhalika ili kufikia hadhi yetu wanaadam kama inavyoelezwa katika Quran 2:30 waislam lazima tuipe madrasah, hadhi yake sahihi. Kwa sababu hizo, kuna haja ya kufanya fikra juu ya kuinua hadhi ya madrasa zetu kwa ajili ya kuuendeleza umma wa kiislam utapotea na kuacha wanaoitwa Waislam lakini ummah wa kiislam haupo.

1.2 Maana ya Madrasa
Ilivyozoeleka, madrasa ni kituo cha kiislam ambapo watu hupata elimu juu ya mambo ya msingi katika uislam. Wengine wameita Shulel za Quran, wengine wamesema, vyuo vya Quran, na wengine wanaelewa kuwa madrasa ni vituo vya watoto ambapo masomo ya Quran, kusoma na kukandika hufundishwa.

1.3 Kazi zinazonasibishwa na Taasisi ya Madrasa
Madrasa zetu Tanzania, kwa muda mrefu tangu Historia ya kuingia kwa uislam nchini zimenasibishwa na kazi zinazofanywa na taasisi hii. Kwa ujumla madrasa zetu zimejikita katika taaluma zifuatazo:-
(i) Kuandika herfu za kiarabu.
(ii) Kuzisoma herfu za kiarabu.
(iii) Kutafsiri llugha ya kiarabu.
(iv) Kusoma Quran kwa ghaibu au kwa kutazamia.
(v) Jinsi ya kufanya ibada maalum na kanuni zake. Mfano, ibada, swala, swaum, hija na utoaji zakat na sadakat.

1.4 Athari za Madrasa kujikita katika shughuli hizo
Kwa kuwa Madrasa ni vituo vya elimu ya kiislam, na kwa vile madrasa zinaoa elimu hizo tu, basi elimu ya kiislam inafahamika kuwa ni ile tu inayohusiana na:
- Kusoma na kuandika Quran.
- Kukariri sura za Quran na tafsiri zake.
- Kanuni za utekelezaji wa nguzo tano.
- Kukariri hadithi kadhaa za Mtume (s.a.w).
- Kukariri visa vilivyo katikak lugha ya kiarabu.
Matokeo ya hilo, Uislam nao umeeleweka kukwa ni mambo ya kimaisha yanayohusiana na shughuli hizo tu. Nje ya shughuli hizo si vitu vya lazima katika uislam. Mfano kuksimamisha dola ya kiislam.

2.0 HISTORIA YA ELIMU YA MADRASA TANZANIA KWA UFUPI
Ø Historia ya Elimu ya Madrasa Tanzania inanasibiana na Historia ya kuenea kwa uislam katika Afrika Mashariki kuanzia Pwani hadi bara.
Ø Elimu itolewayo na Madrasa zetu ilichipuka tangu wakati walivyoanza kuja Waarabu kutoka Saudia, Oman, Uajemi, Hadhramaut na Yemen.
Ø Karne ya 9 na 10 wahamiaji kutoka Saudia walianza kusihi BENADIR (Pwani ya Somalia).
Ø Karne ya 12 Waarabu wageni (Afro-arabs) walianza kufika hadi mji wa Kilwa.
Ø Karne ya 12 wageni kutoka Hadhramawt na Yemen waliingia Afrika Mashariki. Wageni hawa nao pia walitoa elimu inayohusu uislam. Lakini kufahamu uzito wa elimu waliyoitoa kunategemea ufahamu wa sababu zilizowaleta Afrika Mashariki. Hawakuja kueneza uislam na kuufundisha uislam. Bali wali kuja kutokana na:
(i) Njaa iliiyokuwapo Arabuni wakati huo.
(ii) Ukame huko Arabuni.
(iii) Ukandamizaji wa Kisiasa uliotawala huko.

2.1 Kustawi kwa Elimu ya Madrasa Afrika Mashariki
Ø Mwaka 1332, Mwarabu aitwaye IBN BATUTA alipotembelea Kilwa alikuta mji umekaliwa waliokuwa wakitumia lugha ya Kiswahili.
Ø Baadaye miji ya Tanga, Dar-es-Salaam, Mombasa, Lamu, Malindi, na Mikindani vikawa vituo vya kueneza uislam na elimu ya kiislam katika miji ya Tanzania, Kenya, Uganda, Rwandda, Zaire, Msumbiji, Malawi na Burundi.

2.2 Maarifa yaliyotolewa na njia za kufundishia
Ø Maarifa yaliyotolewa na kuonekana hayo ndiyo maarifa ya uislam ni pamoja na:
(i) Zipi ni nguzo za imani na maana yake.
(ii) Zipi nguzo za Swala na maana yake.
(iii) Namna ya kusoma Quran, lugha ya kiarabu na vira kadhaa.
(iv) Sirah ya Mtume (s.a.w)
(v) Kanuni zinazotawalal utendaji wa Ibada Maalumu.
Ø Maarifa haya yalifundishwa kwa njia kuu ya Kipurure. Mwanafunzi hakusoma kwa kuwa mdadisi sana. Wanafunzi walikasirishwa waliyofundishwa.
Ø Walimu wa kufundisha hayo, ni wale tu, walioonekana wanaweza kuyasoma hayo. Hakukuwa na mazingatio kuhusu uwezo na ujuzi wa mfundishaji kufikisha maarifa anayoyatoa.
Ø Kwa sababu hizo, pia njia kuu ya kudhibiti nidhamu, ilibaki kuwa ni viboko tu.
Ø Kwa ujumla taaluma kuu za elimu ya Madrasa zilizotawala ni KUSOMA, KUANDIKA, KUIFADHI na KUIGA ambazo zilitolewa na walioweza kuzipata taaluma hizo.

2.3 Dosari za Elimu ya Madrasa iliyotolewa wakati wa Waarabu
Utangulizi
Ø Dosari hizo zimetokana na asili ya kuenea kwa dini na elimu ya Kiislam Afrika Mashariki, hususan Tanzania.
Ø Tatizo linakuja kwa vile Uislam na elimuk ya Kiisam:-
(i) Vilenea katika taratyibu za walioeneza kkujitafutia maisha yao wala si kwa madhumini ya kufanya umisionari.
(ii) Vilienezwa na wailam ambapo hawakuwa na maandilizi ya kufanya hivyo hivyo hakukuwa na matayarisho yoyote ya malengo ya kieleimu.
Ø Matokeo yake uislam ulifundishwa ili kupata wenzi na washirika katika mas[ala ya kijamii kama vile:
o Misiba
o Harusi n.k..
· Utangulizi

(i) Zilifundishwa Taaluma chache tu.
Mfano: Kusoma, Kuandika, Kukariri Quran.
Taaluma hizo si pana kiasi cha kuwawezesha wanafunzi kuuhani uislam kifikra, au vyovyote Taaluma hizo hazimwezeshi mwanafunzi kumudu changamoto zinazoibuka kila kukicha; Japo uislam haushindwi na changamoto yoyote ile.
(ii) Njia za kuendeleza nidhamu, na maadili zilikuwa viboko tu, ukali tu, pasi na kuchunguza tatizo kwa lengo la kkuondoa tatizo hilo na kusaidia.
(iii) Njia za kkufundishia hazikuzingatia umuhimu wa kuendeleza na kuhusisha nyanja tatu za kujifunza.
(a) Nyanja ya ung’amuzi (Cognitive domain).
(b) Nyanja ya matendo (Psychomotoar domain)
(c) Nyanja ya kuhusisha (Affective domain)
Kila nyanza hapo inaumuhimu katikak uislam wa mtu mmoja mmoja au jamii na hatimaye Ummah.
(iv) Hakukuwapo chombo maalum cha kijamii, kinachosimamia swala zima la utoaji wa Elimu hii. Matokeo yake kila mmoja alifundisha kadiri na namna alivyodhani ni sawa.

2.4 Athari za dosari hizo
(i) Kukosekana kwa taaluma muhimu za kifiqih
Mfano:
- Taaluma inayowezesha kkuhusianisha mazingira na fatwa kadhaa za kifiqih.
- Taaluma inayofafanua hukumu kadhaa za kifiqih na yanayotokea katika maisha. Katika hili, kumekosekana taaluma ya kubainisha tofauti ya RIRA na HIBA.
(ii) Watu wachache sana ndio waliweza kwendelea na elimu ya Madrasa kwa
kiwango cha juu kwa kulinganisha na waislam wengine.
Mfano:
Ni Masheikh wachache waliweza kkufikia kiwango Fulani. Matokeo hata vitu vidogo vidogo kuweza kufahamika kwa waislam wote, vinafahamika na masheikh tu.

(iii) Kuibuka kwa Matabaka miongoni mwa waislam kutokana na dosari hizo,
kumeibuka matabaka kadhaa mingoni mwa waislam.

Mfano:
o Tabaka la wasomi wa elimu katika mfumo huu wa madrasa tu.
o Tbaka la waliosoma elimu ya madrasa kidogi na elimu ya kisekula kidogo.
o Tabaka la waliosoma kiasi elimu ya kisekula na kukosa elimu ya madrasa lakini badaye (ukubwani) wakajifunza elimu ya uislam kwa mfumo mwingine.
Mahusiano ya matabaka haya hayasaidii kuendeleza uislam na waislam wa kiislam, ni sumu kwa maendeleo ya jamii ya kiislam.

3.0 MATATIZO YANAYOIKABILI ELIMU YA MADRASA TANZANIA
i) Utangulizi
Taasisi ya Madrasah inazidi kukpoteza hata hadhi yake ndogo iliyokuwa nayo.
Mfano:
Jamii haiipi hadi na thamani stahiki licha ya kuwa madrasa ni taasisi muhimu katika kurithisha mila, na mfumo mzima wa uislam toka kizazi hadi kingine. Wazazi wa watoto wa kiislam leo hii hawana hari ya kupeleka watoto wao kwenye vituo vya madrasa. Wala wazazi hao hawana hata haja ya kujua mikati ya madrasa zinazowazunguka.

(ii) Matatizo

Matatizo yanayoikabili elimu ya madrasa ni:

3.1
Matatizo ya Kitaasisi (Institutional Problems)

(a) Hakuna mfumo wa uendeshaji elimu ya madrasa. Mfumo huo
Mfumo huo hautoi picha halisi juu ya nani hasa ndiye mratibu au msimamizi wa elimu ya Madrasa. Kwa sababu hiyo hakuna upimaji wala tathimini yoyote ili kuelewa mustak bal wa elimu hii muhimu
(b) Kukosekana kwa “usare” (uniformity) katika ufundisjaji.
Matokeo yake anapohama motto kwenda madrasa nyingine anaathirika kitaaluma.
(c) Hakuna utaratibu fasaha/muafaka wa kuwahusisha wazazi wa Kiislam katika kujadili maendeleo na kutathimini uendeshaji wa madrasa. Athari yake ni wazazi kutojihusisha na uendelezaji wa madrasa zetu na ufuatiliaji wa taaluma muhimu zipatikanazo.
(d) Kukosekana kwa utaratibu wa kubadilishana mawazo baina ya walimu tofauti tofauti, juu ya uboreshaji wa njia za ufundishaji na mafanikio katika uendeshaji madrasa.
(e) Kukosekana kwa mipango inayohusiana na madrasa, wanafunzi na walimu. Athari yake ni kupungua kwa idadi ya wanafunzi na walimu wa madrasa.
(f) Kukosekana kwa utaratibu maalumu juu ya vigezo vinavyomuwezesha mtu kuwa mwalimu. Kwa kawaida yeyote anayejua kusoma na kuandika herufi za kiarabu, kusoma Quran na mambo kadhaa katika Ibada maalumu za kifiqih, aweza kuwa mwalimu hata kama sifa za kitabia, na uwezo wa kkurithisha elimu kwake ni vikwazo.

TANBIH:
Aina za walimu zaweza kkuwa kama ifuatavyo:-
(i) Mwenye sifa (Qualified) – Anazo sifa kitabia, anaweza na ujuzi wa kkufundisha na ana elimu.
(ii) Mwenye sifa (Underqualified) – Anayo elimu ila hana mbunu bora za ufundishaji.
(iii) Asiye na sifa (Unqualified) – Hana sifa hata kidogo. Huyu ni hatari sana.

Matatizo ya Kijamii
(a) Fikra za watu juu ya elimu ya madrasa na thamani yake
- Jamii na mtu mmoja mmoja wanachukulia elimu ya msingi ya madrasa ni kusoma Quran na kujua kanuni muhimu za utekelezaji wa Ibada maalumu kama vile Swala, hija, swala ya maiti, kushona sanda na kadhalika.
- Athari yake ni kuwa, mara baada ya watoto kufikia ngazi hiyo huonekana imetosha na kwamba, wana elimu ya kutosha juu ya uislam. Elimu kuhusu uislam inapungua miongoni mwa waislam.
(b) Uchumi duni kwa wazazi na walimu
- Umaskini na kipato kidogo kwa walimu wa madrasa inakuwa tatizo kubwa kwa uendeshaji wa madrasa zetu. Hali hii husababisha walimu wa madrasa kutenga muda kidogo sana kwa ajili ya kazi ya madrasa. Kadhalika kujituma juu ya kuboresha madrasa hupungua.
- Vile vile pato la wazazi kuwa dogo huchangia tatizo. Mara nyingi watu wenyekipato cha chini ndio wanaopeleka watoto wetu madrasa na wenye uwezo na wito wa kiislam wao huwaajiri walimu wa kuwafundisha watoto nyumbani. Kwa sababu hiyo, wazazi wengi hawana uwezo wa kkuchangia fedha muhimu kwa ajili ya madrasa. Wakati mwingine mchango wao huwa kidogo na mgumu kupatikana.
- Athari ya hayo, ni kudorora kwa madrasa zetu na kupatikana kwa watoto, mabarabara, vijana wasio na elimu sahihi ya msingi kuhusu uislam na hatimaye kuporomoka kwa maadili.
(c) Mfumo wa elimu ya nchi na utaratibu wa kisekula
Mfumo wa elimu ya kisekula umembana kiasi motto anayesoma madrasa kutokana na utaratibu ulivyo. Uendeshaji wa elimu ya kisekula umezaa desturi ya “Tuition” (masomo ya ziada), desturi amabyao sit u inamfanya motto achoke bali pia inamkosesha muda wa kuhudhuria katika madrasa zetu.

Mfano:
Mtoto wa darasa la kwanza na pili wanaingia shule kwa zamu, mara asubuhi, mara saa tano, mara mchana. Hii inaleta ugumu kwa madrasa kuratibu jinsi ya kuwasaidia watoto.
Mtoto wa darasa la kwanza atokapo shule, anapumzika kidogi, kasha anaenda “Tuition” masomo ya zaida.
Mtoto wa darasa la tano hadi saba, anakosa muda kabisa. Muda wote, kutwa mzima anashughulishwa na elimu ya kisekula na usiku anajisomea nyumbani.
Athari ya tatizo hili ni kushuka kwa mahudhurio ya watoto katika madrasa zetu, na mara nyingine kuwapo kwa mahudhuria yasiyotabirika na kuelezeka. Mara kuna mahudhurio ya kuridhisha mara mabaya.
(d) Shughuli za Kijamii miongoni mwa Waislam
- Ndani ya jamii ya Kiislam, inapotokea shughuli kama vile harusi na kadhalika, madrasah nyingi kuhusishwa. Mfano kuandaa kaswida kwa ajili ya maulidi harusini. Hili hupunguza za muda wa ufundishaji na kujifunza katika madrasa zetu.
- Athari yake ni kuongezeka kwa tatizo katika madrasa zetu. Wazizi wengine huona kua hakuna haja ya watoto kusoma madrasa hizo.

4.0 SOLUHISHO KWA MADRASA ZETU

4.1 Utangulizi
- Ni vigumu kuliondoa tatizo hili kwa kulifanya jukumu hilo kuwa la watu Fulani tu. Mfano, kulifanya liwe jukumu la masheikh tu, au jukumu la walimu tu, au la wazazi tu. Inapaswa kuwa ni tatizo linalomgusa kihisia kila muislam.
- Kwa hakika elimu hii ni muhimu sana kwa maendeleo ya uislam na waislam kiitikadi, kitaaluma, kielimu n.k.

4.2 Mfumo
- Kunahaja ya kuudhurusi mfumo wa elimu ya madrasa na kuangalia namna ya kuuendeleza na kuuboreha kwa manufaaa ya kikazi cha kiislam.
- Mfumo wa madrasa zetu uendane kabisa na haja iliyopo katika jamii kwa lengo la kuwaendeleza watoto kitaaluma.

4.3 Walimu
- Kuwepo na mpango maalumu wa kuwaendeleza walimu kielimu, kitaaluma na kiuchumi ili kuwaongezea hari ya kujituma na kukfikiri kwa ajili ya maendeleo ya taasisi hii muhimu, “madrasati”.
Mfano:
Kuwepo kwa warsha, makongamano na semina ili kuwawezesha walimu kushirikiana ujuzi na mbinu za kufundishia na kuendeshea madrasa zetu.
- Walimu wawe wabunifu kiuchumi ili waweze kujikwamua kiuchumi na kuendeleza madrasa zetu.
- Walimu wasijione kuwa wao ni waislam au watu wa daraja la chini sana kimaisha. Bali wajione wao ni watu muhimu na kazi yao ni jukumu lao si jukumu la mtu Fulani na wala hawafanyi kazi hiyo ili tu kuwaridhisha watu Fulani bali ili kumridhisha allah (s.w).

4.4 Jamii ya Kiislam
- Ifanye fikra juu ya jinsi ya kuboresha na kuendeleza madrasa zetu na watoto wetu katika taaluma muhimu za kiislam.
- Jamii nzima ieleweshwe juu ya nafasi sahihi ya Madrasa na Elimu ya Madrasa kwa maisha yua Waislam nchini.

4.5 Taasisi za Kiislam
Zishirikiane kuona jinsi ya kutatua matatizo hayo.

5.0
TAALUMA MUHIMU KWA WALIMU WA MADRASA

5.1 Utangulizi
Kila nyanja inahitaji taaluma Fulani ili kuifanya nyanja hiyo iwe makini na yenye manufaa kwamaisha na ummah kwa ujumla. Hata mitume (radhi za Allah ziwafikie) walipewa taaluma maalumu kwa kazi zao. Katika maisha yetu tunahitaji taaluma zinazowezesha watu kutekeleza majukumu yao katika mazingira wanayoishi.
Mfano:
Mwalimu wa madrasa anahitaji taaluma juu ya;
(i) Uendeshaji wa madrasa.
(ii) Ufundishaji.
(iii) Saikolojia ya watoto na malezi.
(iv) Taaluma inazofundisha kama vile Fiqih, Tareikh, Qurani, Kiarabu, Tawhiid, Sirah, Akhlaq n.k.

5.2 Njia za kkufundishia (Muhtasari)
Zipo njia kadhaa Bwana Mtume (s.a.w) amekuwa akizitumia katika kufundishia watu. Pia Quran imeeleza njia kadhaa kwa ajili ya ufundishaji na uchamasishaji. Kwa muhtasari njia hzo ni pamoja na zifuatazo.

(a) Simulizi (Narration)
- Hii ni njia ambayo mwalimu anafundisha kwa kutumia visa vya kubuni au visa halisi. Njia hii inafaa sana kutumika hususan kwa watoto wadogo.
- Katika Quran njia hii imetumika kutafundisha mara kadhaa. Kanuni na njia yenyewe katika Quran zimeelezwa katika “NJIA ZA KUFUNDISHIA KATIKA MADRASA ZETU”. Hapa ni muhtasari tu.
- Njia hii yaweza kutumika katika kufundisha Sira ya Mtume, Akhlaq, Tareikh, Fiqih hata tawhiid. Alimradi mwalimu afahamu jinsi ya kuitumia njia hiyo kwa ufanisi.
(b) Uelezeaji (Description)
- Njia hii hutumika kuelezea dhana au wazo Fulani katika uislam. Muhimu kwa mwalimu ni kuifahamu misingi ya njia hii pamoja na kuelewa mazingira yanayofaa kwa njia hii.
Mfano:
(i) Ili kutoa maf’hum nzuri kuhusu “UISLAM” kama dini njia hii yafaa kutumika.
(ii) Ili kufunldisha vizuri, mazingira ya vita vya Badr, Uhud, Khandaq n.k. kwa lengo la kkufundisha mazingatio yanayopatikana, mwalimu aweza kutumia njia ya UELEZEAJI (Description)
- Kadhalika, cha muhimu ni maarifa kuhusu njia hii.
(c) Njia ya Uoneshaji (Demonstration)
- Ni njia inayotumika kufundishia mada zinazolenga kutoa ujuzi kwa wanafunzi kutenda matendo maalum:
Mfano:
(i) Swala la mait.
(ii) Swala la Faradh na Sunnah.
(iii) Kushona Sanda.
(iv) Kuosha Maiti.
(v) Kuchukua Udhu n.k.
- Mada kama hizi zikifundishwa pasipokutumia njia hizi, ueleo wa wanafunzi unaathirika.
- Mwalimu anatakiwa kuifahamu njia hii kwa madhumuni ya kuitumia kwa ufanisi.
(d) Njia ya ugunduzi na udadisi
- Njia hii inamtaka mwalimu aoneshe tatizo kasha aongeze wanafunzi katika kugundua suluhisho. Kwa kufanya hivi, milki ya ung’amuzi (Cognitive Facult) itakuwa imeendelezwa. Quran inasisitiza matumizi ya milki ya ung’amuzi (Cognition domain).
Mfano:
(i) Baada ya kufundisha “Tawhid” – Mwalimu anaweza kutoa habari ya kweli kuhusiana na tawhiid kasha wanafunzi wakajadili kwa mnasaba wa tawhid.
(ii) Mwalimu aweza kufundisha “Tareikh” – Hijar kutoka Makka kwenda Madina, alafu wanafunzi watatakiwa kugundua wanachojifunza.
(iii) Mwalimu awezatoa tatizo liliopo katika jamii kwa mnasaba wa uislam, kasha akawataka wanafunzi waonyeshe sabbu na suluhisho.
(e) Njia ya Kuhidadhi
- Hii ni muhimu sna katika elimu na maarifa ya kiislam. Mwalimu anatakiwa kuwawezesha wanafunzi kuhifadhi katika mada kadhaa.
Mfano:
(i) Ktika Swala, mwalimu atumie njia rahisi kwa wanafunzi kuhifadhi.
(ii) Katika Wudhuu, mwalimu atumie njia hii pia ili wnafunzi waweze kuhifadhi maneno muhimu.
(iii) Katika Dua, wanafunzi wahifadhishwe dua.
(iv) Katika Tarekh, wanafunzi wahifadhishwe aya na hadithi mbalimbali zinazonasibiana na matukio katika mada. Mathalani, kufundisha Mkataba wa hudaybiya, Quran 48:1. 48:18 ni vema zikahifhadhiwa. Pia katika kufundisha AKHLAQ mwalimu awahifadhishe watoto, Sura ya 64.4 ikiwekana, kulingana na umri wa watoto, Pia wahifadhi Quran 33:21.
(f) Njia za Kufundisha Quran
Njia na mbinu pamoja na mikakati ni muhimu sana katika ufundishaji wa usomaji Quran, vinginevyo motto atosoma muda mrefu sana ili kuelewa. Baadhi ya mbinu za kufundishia ni pamoja na kusoma herufi bila irobu kwa njia ya ubao, kadi, daftari n.k.

MUHIMU:
- Mwalimu afundishe kwanza herfu bila irabu. Yaani: ALIF, BE …….
- Kisha afundishe Irabu. Yaani: FAT’HA, KISRA, ……
- Afundishe kuchanganya herufi hizo na rabu;
Mfano: BE FAT’HABA, TE FAT’HATA …….
- Mwalimu atumie michezo kadhaa kwa watoto kuzitambua herufi.
Mfano: NGAZINGAZI, KIKAPU, UPANGAJI, GURUDUMU ZA GARI, NYUMBA …. n.k.
- Mwalimu afundishe kuchanganya SILABI ili kupata neno. Ni vizuri Mwalimu akaanza na kinachoeleweka kwenda kisichoeleweka.
Mfano: Kumwezesha motto kuandika BABA kwa herufi za Kiarabu, kasha aandike neno la kiarabu kwa herfu hizo.

6.0 HITIMISHO
Mwalimu anapaswa sit u kujua anachokifundisha, bali pia kufahamu na kuweza kutumia njia na mbinu muafaka. Kwa kawaida hatupaswi kulenga kusema sana, au kueleza mengi, bali tulenge kuwezesha mengi kufahamika kwa urahisi zaidi.

7.0 MWISHO
Kwa muda mrefu MADRASA zimesahaulika na kusababisha athari mbaya. Ili kuzikuisha tunapaswa kuzingatia kazi zinazotakiwa kukfanywa na madrasa na zipi zinafanywa. Kuelewa tatizo kwa undani. Historia ya Madrasa Tanzania ni muhimu kufahamika ili kurudisha mzizi wa tatizo. Kadhalika, Matatizo yanayoikabili taasisi ya Madrasa na ufumbuzi wake ni muhimu vikajadiliwa. Aidha , kuna haja ya kukumbuka taluma muhimu kwa walimu wa Madrasah na kuona kama wengi wanazo. Kama si hivyo, basi mikakati iwepo kuwawezesha walimu wa Madrasa kuendesha madrasa zetu (Uendeshaji Madrasa) pamoja na kuwa na mbinu bora za kufundishia katika madrasah zetu.
Mbinu zilizomo humu ni muhtasari tu, hazijaelezwa zote. Na wala hazijafafanuliwa hasa.
ALLAH NDIYE MJUZI WA YOTE

Saturday, May 5

Mawaziri, hakuna sherehe, nendeni mkawajibike! by zittokabwe

Juhudi za kurejesha misingi ya uwajibikaji katika utumishi wa umma zimeanza kuzaa matunda Baada ya Rais kutekeleza shinikizo la Bunge la kuwafukuza kazi baadhi ya Mawaziri ambao Wizara zao zimetuhumiwa kwa ubadhirifu wa fedha za umma, rushwa na utendaji mbovu. Mawaziri 6 wamefukuzwa kazi baada ya kugoma kujiuzulu wao wenyewe, manaibu Waziri 2 wamefukuzwa pia.

Ndugu George Mkuchika alitakiwa kujiuzulu, akajiuzulu lakini Rais amemrudisha kwenye Baraza kama Waziri wa Utawala Bora. Yeye nampongeza kwani hakuwa na makuu ya kuanza kujitetea kama wengine. Atakuwa ametoa funzo kwa wenzake.

Kwa kawaida wateule hufanya sherehe kwa kuteuliwa kwao. Nitawashangaa watakaofanya sherehe safari hii kwani hakuna cha kufurahia. Nitawashangaa Watakaokwenda kuapa na Maua kwa furaha kwani furaha itakuwa ya muda mfupi tu. Mkutano wa Bunge wa Bajeti ni mwezi ujao tu na Wateule wote watakuwa kikaangoni. Too short honeymoon.

Hakuna cha kusherehekea kwa sababu nchi in a changamoto nyingi sana. Changamoto ya kuzalisha umeme wa kutosha na kuusambaza kwa wananchi wengi, changamoto ya kukuza uchumi wa vijijini na kukuza uzalishaji viwandani ili kutengeneza ajira kwa vijana, changamoto ya kuongeza mapato ya Utalii kutoka katika hifadhi zetu na kuvutia watalii zaidi katika nchi yetu.

Nimewapigia simu wateule wengi na kuwaambia, siwapi pongezi Bali nawatakia kazi njema. Nawatakia uwajibikaji mwema. Uwajibikaji ndio msingi wa kupambana na rushwa, uvivu na uzembe.

Kwa Waziri wa Fedha, ambaye mimi ni Waziri Kivuli wake (Kama Kiongozi wa Upinzani Bungeni hataniwajibisha pia), namwambia uteuzi wake ni changamoto kubwa sana katika maisha yake.

Hivi sasa eneo lenye Bajeti kubwa kuliko zote nchini ni huduma kwa Deni la Taifa (services to national debt). Lazima kuangalia upya Deni la Taifa. Hivi sasa Deni la Taifa ukijumlisha na Dhamana za Serikali (government guarantees) limefikia tshs 22trn mpaka Desemba 2011. Nimewahi kutaka ukaguzi Maalumu katika 'account' ya Deni la Taifa. Linarejea wigo huu. Tunalipa takribani 1.9trn tshs kwa mwaka kuhudumia Deni la Taifa. Zaidi ya Bajeti ya miumbombinu, Afya, Maji, Umeme nk.

Mfumuko wa Bei, misamaha ya kodi na kodi zinazozuia watanzania kujiajiri ni changamoto kubwa sana Wizara ya Fedha lazima ihangaike nayo.

Usimamizi wa Mashirika ya Umma kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina na hasa usimamizi wa Hisa za Serikali katika kampuni binafsi ni masuala yanayohitaji masuluhisho sasa na sio baadaye.

Kwa Mwalimu wangu Dkt. Mwakyembe, utakumbukwa kwa Jambo moja tu. RELI. 'make our Railway system work'. Hutakuwa na 'legacy' nyingine isipokuwa Reli maaana Bandari bila Reli ni sawa na Bure.

Tunatumia zaidi ya tshs 300bn kwa mwaka kukarabati barabara wakati tunahitaji tshs 200bn kukarabati Reli iweze kusafirisha mzigo kwenda Bandarini na kukupa Bandarini.

Ndio maana nasema hakuna Jambo la kusherehekea maana wajibu mliopewa na Rais ni mtihani mkubwa kwenu katika kukitumikia Taifa letu. Msipowajibika, mtakumbwa na fagio la chuma!

Mkisha kula kiapo, kimbieni kazini. Nothing to celebrate. Hit the ground running.

ZZK

Dar-es-Salaam

Jumamosi, Mei 5 2012

Friday, April 20

TB Joshua again: Delivers man from shocking addiction!

This post and link to the video below were shared to us by Ihechukwu Njoku -- Controversial Nigerian Prophet T.B. Joshua can’t seem to stay out of the news. However, this time it’s not concerning a prophetic utterance or political visitor.

On Sunday 15th April 2012, Joshua’s popular church in Lagos was witness to a disgusting yet dramatic case of a man with a truly repulsive addiction. Mr Mukaila Malomo, a Nigerian who lived in Germany for 16 years, confessed to being addicted to regularly taking a sickening concoction of faeces, semen and urine.

According to Malomo, a graduate from the London School of Journalism, it all started one night in a prison cell in Germany. "I woke up in the middle of the night and a very wicked demon instructed me to get up from my bed,” he told the bewildered SCOAN congregation. “This strange voice said that I should go to the toilet, defecate and mix it with my sperm and urine. I mixed my urine, sperm and faeces and swallowed everything.”

Malomo, who worked in a reputable organic salad company in Munich before a drunken brawl landed him in prison, explained that an unusual anger and desire to fight immediately followed. “After I swallowed it, a very strange power came over me. I felt as if I was a small god. It overcame me and I became very strong and angry - as if there's an extra power from another world entering my body. I was ready for war. Ever since then, for over 15 years, I have been addicted to eating my faeces, urine and sperm. I can’t stop it.”

He continued his sordid tale, explaining how each indulgence in the addiction would result in further violence. “After my release from prison, I was always fighting in Germany. Sometimes, the police would have to cover the whole street to try and stop me - and I was using only a bottle. I kept on stabbing without getting tired – because of this power that entered me.”

People present in the church could scarcely contain their shock as Malomo’s revelations continued. “It is not only my own faeces; on many occasions, I visited public toilets here in Nigeria and Germany and ate from there.” He described the mixture as food to him. “I enjoy it. I don't even perceive any smell. I eat it as if I eat eba (Nigerian cuisine) or something like that.”

Malomo, married to a German Hungarian lady who gave birth to his only son while in prison, described how he had kept this addiction a total secret from the world around him. “As I am eating it, that evil spirit will be telling me that this thing is only for me, that nobody should know, otherwise the power will go.”

Joshua proceeded to tell his congregation and the viewers worldwide watching the live broadcast via Christian television station Emmanuel TV that a video clip would be shown to verify Malomo’s confession. Stating that it was too graphic for him to witness, he covered his face and advised viewers without strong stomachs to do likewise. The clip showed Malomo mixing his own urine and faeces together and then drinking the revolting contents with apparent ease and delight. People within the auditorium vomited at the sight, distressed at the level of degradation the addiction had rendered on Malomo.

Joshua then called on the congregants to join together in supplication and proceeded to pray for the ‘demon’ within Malomo to come out! Falling to the floor, Malomo’s body began vibrating uncontrollably and uncannily. Asked to explain what was happening, Malomo said he felt as if something was leaving his body.

Joshua then instructed Malomo to go to the church’s public toilet to see how his reaction towards human waste had changed following the prayer. Merely perceiving the odour of other’s defecation caused Malomo himself to vomit. He returned to the church, testifying that all desire for his former addiction had vanished as the realization of his earlier actions dawned upon him.“Apart from being irritated by the odour, I feel ashamed, in the sense that – how can a human being be eating faeces,” he told the congregation, as he joined Joshua in a joyful dance.

SCOAN has now controversially released the video on popular video-sharing site YouTube and via their Facebook account which has garnered well over 100,000 fans in just four months. Although Malomo’s case appears to be the most extreme, many with strange addictions claim to have been delivered at Joshua’s ministry over the last few months, including those addicted to drinking kerosene, eating ice cubes, sand, charcoal, mothballs and soil.

T.B. Joshua has set social networks and local media ablaze in recent months, especially with his prediction concerning the death of the late Malawian president Bingu wa Mutharika and revelations of his relationships with African leaders such as Ghana’s John Atta Mills, Zimbabwe’s Morgan Tsvangarai and Malawi’s new head Joyce Banda. His television station Emmanuel TV continues to increase in popularity, especially across Africa where he is becoming a household name.

Tafrisi ya Mjengwa kuhusu Zitto Kabwe na saini za Wabunge 70 kumg'oa Pinda


Ndugu zangu,

Leo asubuhi wakati nikifanya ' jogging' kwenye mitaa ya Dar es Salaam niliwasikia watu wa kawaida kabisa wakijiuliza na kujadili; " inakuwaje Serikali iwalipe marehemu mishahara huku sisi tulio hai hatuna hata uhakika wa milo miwili ya siku?" Wanauliza watu wa mitaani.

Naam, nchi yetu imekumbwa na mafuriko ya habari. Kule bungeni Dodoma kuna moto unawaka. Zimeitishwa sanini 70 ili Jumatatu ipigwe kura ya kukosa imani na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. Ndio, kuna wanaotaka Pinda ang'oke, na labda kutolewa kafara, maana, siamini kama tatizo la msingi ni Pinda, bali ni la kimfumo zaidi. Na jana kuna mbunge wa CCM kayasema makali yafuatayo;

“Mheshimiwa Naibu Spika, inashangaza na kusikitisha kuwa nchi inatafunwa. Wanaofanya haya ni mawaziri wetu. Nchi inakufa na tuelewe kuwa Tanzania sio mali ya CCM, ni ya Watanzania wote.“Mawaziri wetu wamekuwa mchwa, wanaangamiza nchi na leo nitamtaja waziri anayeongoza kwa kutafuta fedha za Watanzania. Ni Waziri wetu wa Fedha, Mustafa Mkulo. Ameuza viwanja, amelidanganya Bunge baada ya kuivunja CHC,”- Deo Filikunjombe ( CCM) Bungeni jana.

Lakini ya jana yalitanguliwa na ya juzi; Mbunge mwanadamizi wa CCM Godfrey Zambi aliyasema makali haya;

" CCM inaweza kung'olewa madarakani katika uchaguzi wa mwaka 2015 endapo kasi ya ufisadi na ubadhirifu wa fedha za umma itaendelea kama ilivyo sasa"- Godfrey Zambi ( CCM, Mbozi Mashariki).

Kauli za wabunge hao wawili wa CCM zinatoa tafsiri ya kilio cha wabunge wa CCM kuomba msaada kwa anayeweza kuwasaidia. Inatoa tafsiri pia kuwa hicho ni kilio cha wabunge wengi wa CCM. Kwamba hayo ndiyo wanayaongea hata chini chini.

Ndio, wananung'unika na wameanza kuiona adhabu wanayokwenda kuipata kutoka kwa wananchi ifikapo 2015. Wanaona pia, kuwa ' kisungura' hiki kidogo kinachopatikana kila mwaka kinavyoliwa na wajanja na wengine kuachiwa mifupa.

Wabunge wa CCM na wengine wanaona jinsi baadhi ya mawaziri wa kutoka chama chao wanavyojiangalia wenyewe kwa kujikatia zaidi kasungura hako kadogo na hata minofu mingine kuikimbizia kwenye majimbo yao badala ya kuangalia majimbo mengine pia. Hakika, Wabunge wa CCM sasa wanatoa kilio cha kuomba msaada na kilichochanganyika na hasira na hofu ya kupoteza mamlaka ya kuongoza dola ifikapo mwaka 2015. Ndio, kuna wanaokiona chama chao kikielekea kwenye kuzama 2015. Kelele wanazopiga bungeni zimegeuka kama kelele za nyikani, hazisikiki. Wameanza sasa kuwa na ujasiri wa kuzomeana wazi wazi kwenye vikao vyao badala ya kusubiri kuzomewa na wananchi hadharani. Naam, CCM ya sasa inapata tabu hata kwenye kujua namna ya kuitumia misamiati mipya ya kisiasa, maana, kuna wanaojivua gamba, wanaovuliwa magamba na sasa kuna ' wanaojinyambua' magamba wakiwa ndani ya chama- 'Political evolution' ya namna fulani.

Na Mtego wa Zitto Kabwe kwa CCM?

Jana Mbunge Zitto Kabwe ameitega CCM. Ni mtego wa hatari. Saini zile 70 zina maana hii;
- Kama wabunge wa CCM hawatachangamkia kutia sahihi zao zikavuka hata mia na hamsini, basi, kuna ujumbe unaopelekwa kwa umma. Kuwa wabunge wa CCM ni maneno tu, hawana dhamira ya kweli ya kupambana na ufisadi. Wabunge wengi wa CCM hawataiepuka adhabu ya umma inaweza kuwa inawasubiri 2015.
- Kwa wabunge wa CCM kutia sahihi zao na hata Pinda kupigiwa kura ya wabunge kukosa imani nae ina maana pia kuwa wabunge hawana imani na bwana mkubwa aliyemteua Pinda. Busara haiwataki wabunge wa CCM kufikia hapo. Hilo halina maslahi kwa taifa.

Nini kitakachotokea?

Kuna matatu;
Mosi, Mawaziri wale watano wanaotuhumiwa kwa ufisadi na ubadhirifu wa mali ya umma wanaweza kuepusha aibu kwa Serikali kwa wao wenyewe kutangaza kujiuzulu. Ingawa hili ni gumu kufanyika katika nchi hii, lakini, wakati mwingine kuna lazima ya kufanyika- maana, hapo watakuwa wamemnusuru Waziri Mkuu na aliyemteua.

Pili- Likishindikana la kwanza, basi, kabla ya Jumatatu, Waziri Mkuu Pinda awe ameshajiandaa kufanya maamuzi magumu. Kujiuzulu na kulinda heshima yake na ya aliyemteua. Au kutolewe ' Tamko la Serikali' litakalobadili upepo unaovuma sasa bungeni.

Tatu: La kwanza na la pili yaweza yasifanyike, na badala yake. Rais anaweza kuyaona yanayotokea sasa bungeni kama fursa ya kufanya mabadiliko makubwa Serikalini mara akitua Dar kutoka ziara ya Brazil.

Naam, yumkini pale Diamond Jubilee, kabla ya Jumatatu, kuna watakaopewa kazi ya kusafisha ukumbi na kupanga viti tayari kwa Mkuu wa Nchi kusema jambo kubwa kwa taifa kupitia kwa ' Wazee wa Darisalama'.

Tuhuma za Ray kuhusika na kifo cha Kanumba

Baada ya taarifa kuenea kwamba mwigizaji Ray anahusika moja kwa moja na kifo cha mwigizaji marehemu Steven Kanumba, mwigizaji huyo amezungumza kwenye AMPLIFAYA ya CLOUDS FM na Millard Ayo na kusema yafuatayo:

“...nimekuqa nikizisikia sana hizi tuhuma, sio kweli kwa sababu Kanumba ni mdogo wangu wa karibu sana tumetoka mbali sana kimaisha mimi na yeye, nimekua na mazoea ya kuona vitu kila siku vinaandikwa ambapo juzi nilipigiwa simu na kuambiwa nitazame kwenye blog ya U-Turn ambayo anaimiliki huyu dada ambaye simfahamu anaitwa Mange Kimambi”

“...alikuwa ameandika kwamba amepata taarifa kutoka kwa polisi mmoja wa Oysterbay kwamba Ray ndio aliyepiga simu kwa Lulu siku ya kifo cha Kanumba kwa hiyo Lulu ametumika kufanya mauaji bila kujijua, na pia kukawa kuna swali kwamba kwa nini Ray alikua wa kwanza kufika kwa marehemu Kanumba. Mungu ndie anaejua...”

“...kwa hiyo anataka kuwadhihirishia Watanzania kwamba Ray ndiyo anahusika na hicho kifo, baada ya hilo nimeshirikiana na polisi na kushitaki na kufungua kesi ambapo hivi sasa ninapozungumza yupo polisi Oysterbay akihojiwa kwa sababu ameandika kitu ambacho bado kipo ndani ya uchunguzi, hana uhakika nacho sijui Lulu amekamatwa Coco Beach which is not true, sijui hizi habari kaipata wapi...”

“...sasa hii ni kutaka kunivunjia heshima, mimi nafanya kazi ya kuigiza ndio maisha yangu unapoandika kitu kama hicho kwenye internet inafika sehumu kubwa dunia nzima, sasa unategemea watu wanichukuliaje kama sio kunivunjia heshima, kunipotezea mashabiki wangu… nasema hili sitoweza kuliacha, nitalifanyia kazi na nitalifikisha mahakamani ili iwe fundisho, sitolichekea...”

Kwenye sentensi nyingine Ray amesema baadhi ya maoni yaliyotolewa na watu mbalimbali kwenye hiyo habari iliyoandikwa kwenye blogu hiyo, “maoni niliyoyasoma mengine yanamwambia yule dada kwamba anachokiandika kinaweza kum-cost kwenye maisha yake, na nyingine zinasema kwamba tuko tayari kumvamia Ray na kumuua, sasa hichi kitu ni hatari sana kwenye maisha yangu kwa hiyo nimemshitaki polisi na kuandika kwa kusema chochote kitakachonikuta hata nikipigwa jiwe na kuanguka mimi na-deal na huyo mwanamke kwa sababu yeye ndio mtu aliye-publish hivyo vitu watu wanichukulie mimi vinginevyo kabisa tofauti jinsi nilivyo na sihusiki kabisa na hicho kifo, kimsingi maisha yangu yapo hatarini lakini nasema haya ni maisha nitaendelea kuvumilia...”