Rais Uhuru Kenyatta amewaongoza wananchi kuadhimisha Sikukuu ya Mashujaa ambayo huadhimishwa kila 20 Oktoba.
Sikukuu hiyo hutumiwa kuwakumbuka na kuwatambua mashujaa waliopigania uhuru pamoja na Wakenya wengine waliotoa mchango wa kipekee kwa taifa baada ya uhuru.

Rais Kenyatta baada ya kuwasili uwanja wa Uhuru Park, Nairobi.

Wananchi walipekuliwa na vikosi mbalimbali vya usalama vikisaidiwa na vijana wa huduma kwa taifa kabla ya kuingia uwanjani.

Mkuu wa Majeshi Samson Mwathethe (kulia) hapa anaonekana akisalimiana na waziri wa mambo ya nje Amina Mohamed.

Mwanasheria Mkuu Prof Githu Muigai akiingia uwanjani, kofia kichwani na macho yake akiyaelekeza kwa kamera...

Mwanamume huyu alionekana kujiandaa kuliombea taifa, mkono wa kulia anaonekana kuinua Biblia na kushoto simu yake. Rais Kenyatta ametangaza Jumapili kuwa siku ya maombi ya taifa kuiombea nchi hiyo kabla ya uchaguzi mkuu unaopangiwa kufanyika Alhamisi.

Waliohudhuria walitumia siku zao kujiwekea kumbukumbu.


Hawa ni askari wa magereza.

Kulikuwa pia na burudani.



Kikosi cha polisi kilikuwa kimewakilishwa ilivyo...

No comments:
Post a Comment