Friday, October 20

Kwa Picha: Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa Kenya

Rais Uhuru Kenyatta amewaongoza wananchi kuadhimisha Sikukuu ya Mashujaa ambayo huadhimishwa kila 20 Oktoba.
Sikukuu hiyo hutumiwa kuwakumbuka na kuwatambua mashujaa waliopigania uhuru pamoja na Wakenya wengine waliotoa mchango wa kipekee kwa taifa baada ya uhuru.
Maadhimisho ya Mashujaa
Rais Kenyatta baada ya kuwasili uwanja wa Uhuru Park, Nairobi.
Kenyatta
Wananchi walipekuliwa na vikosi mbalimbali vya usalama vikisaidiwa na vijana wa huduma kwa taifa kabla ya kuingia uwanjani.
Usalama
Mkuu wa Majeshi Samson Mwathethe (kulia) hapa anaonekana akisalimiana na waziri wa mambo ya nje Amina Mohamed.
Mwathethe
Mwanasheria Mkuu Prof Githu Muigai akiingia uwanjani, kofia kichwani na macho yake akiyaelekeza kwa kamera...
Muigai
Mwanamume huyu alionekana kujiandaa kuliombea taifa, mkono wa kulia anaonekana kuinua Biblia na kushoto simu yake. Rais Kenyatta ametangaza Jumapili kuwa siku ya maombi ya taifa kuiombea nchi hiyo kabla ya uchaguzi mkuu unaopangiwa kufanyika Alhamisi.
Mwumini
Waliohudhuria walitumia siku zao kujiwekea kumbukumbu.
Piga picha
Jeshi
Hawa ni askari wa magereza.
Askari wa magereza
Kulikuwa pia na burudani.
Bendi
Jeshi
Mwanajeshi
Kikosi cha polisi kilikuwa kimewakilishwa ilivyo...
Mbwa

No comments:

Post a Comment