Haki miliki ya pichaREUTERSImage captionColo alifariki akiwa na umri wa miaka 60 na kuushi miaka mingi zaidi kuliko sokwe wengine
Sokwe anayefahamika kuwa mzee zaidi na ambaye ni wa kike kwa jina Colo, ameaga dunia nchini Marekani akiwa na umri wa miaka 60.
Colo aliaga dunia akiwa amelala katika hifadhi ya Columbus kwenye jimbo la Ohio chini ya mwezi mmoja baaada ya kusherehekea siku ya kuzaliwa.
Alizaliwa kwenye hifadhi hiyo mwezi Disemba mwaka 1956, na inaaminiwa kuwa sokwe wa kwanza kuzaliwa akiwa kwenye hifadhi.
Hofadhi ya Columbus katika taarifa, ilisema kuwa Colo alikuwa ni balozi wa sokwe wengine, aliyewafunza watu kuhusu familia hiyo ya wanyama iliyo kwenye hatari ya kuangamia.
Sokwe Colo akifurahia keki yake
"Colo alibadili mawazo ya watu wengi ambao walifika kumuona pamoja na wale waliomuhudumia katika maisha yake," taarifa hiyo ilisema.
Hifadhi hiyo ilisema kuwa maiti yake itachomwa na majivu kuziwa eneo hilo.
Mwezi Disemba mamia ya watu walitembelea hifadhi ya Columbus kumuimbia Colo wimbo wa kuzaliwa na kumtazama akifurahia keki yake.
Haki miliki ya pichaTERENCE FUH NEBA, WWF CENTRAL AFRICAN REPUBLICImage captionMbali na kuhifadhiwa, Sokwe huwa bado wanakuwa hatarini
Ijumaa kutakuwa na mkesha kuomboelza kifo cha Sokwe mkubwa zaidi nchini Uganda ambaye amekufa akiwa na miaka 54
Mwaka 1964, zakayo alikuwa na mwaka mmoja alipokutwa ametelekezwa magharibi mwa Uganda.Kituo cha elimu ya Hifadhi ya wanyamapori kimesema kuwa alitunzwa na wataalam na baadae alifikishwa kwenye hifadhi ya taifa akiwa na miaka 13.
Zakayo aliishi sehemu kubwa ya maisha yake katika hifadhi ya Entebbe, ingawa hapo kwa mujibu wa mamlaka nchini humo, alikuwa hatarini.Watalii walikuwa wanampa sigara na pombe ili awafurahishe.
Hifadhi hiyo kwa sasa imeboreshwa na Zakayo anayeitwa 'Babu' wa Sokwe wote nchini Uganda aliweza kuishi kwa raha
Wataalam wa uhifadhi wamemsifu Zakayo kwa kuwa balozi wa sokwe na wanyama wengine nchini Uganda.Wanasema wasifu wake ulisaidia kujipatia fedha kwa juhudi za uhifadhi na kuongeza idadi ya watalii
Mabaki ya Zakayo yatatunzwa kwa ajili ya utafiti na elimu.
Sokwe barani Afrika
Maisha ya Sokwe katika misitu barani Afrika hutegemea miti.
wanasayansi wameeleza hayo kutokana na utafiti walioufanya
utafiti ulibaini kuwepo kwa sokwe wengi kuliko wanyama wengine.
Haki miliki ya pichaEMMA STOKES/WCSImage captionSokwe katika nchi ya Cameroon,Afrika ya kati na Congo wanakabiliwa na tishio la ujangili
Hata hivyo , wanyama hao wengi wako kwenye maeneo yasiyo na usalama,ambapo huwa hatarini kuuawa na majangili,Ebola na uharibifu wa mazingira
Hali hiyo pia imewakuta sokwe wa kwenye misitu ya nchini Cameroon,Afrika ya kati ,Jamuhuri ya kidemokrasia ya Congo, Guinea ya Ikweta na Gabon.
Silaha inamaanisha uwindaji: vijidudu inaamisha Ebola:na miti inaashiria kuwa wanyama wanahitaji msitu kuweza kuishi,amesema Dokta Fiona Maisels,Mwanasayansi wa hifadhi kutoka taasisi ya hifadhi ya wanyama.
Ikiwa misitu itakatwa.Ikiwa misitu itabadilishwa na kuwa kwa ajili ya kilimo, hakutakuwa na sokwe.
Kwa mujibu wa jarida la kisayansi, Watafiti wa kimataifa wanasema viumbe wa aina hii wanahitaji uangalizi zaidi ya wanaoupata.
Jitihada za uhifadhi lazima zizingatie kuimarisha hatua za kupiga vita ujangili, hatua za kudhibiti magonjwa na kutunza mazingira, wameeleza.
Haki miliki ya pichaRAFIKIImage captionMaudhui ya filamu hiyo yanahusu mapenzi ya jinsia moja
Bodi la Filamu la Kenya (KFCB) imeipiga marufuku filamu iitwayo 'Rafiki' inayogusia masuala ya mapenzi ya jinsia moja.
Filamu hiyo ni ya kwanza kutoka Kenya kuchaguliwa ili kuonyeshwa katika tamasha la kimataifa la Cannes mwaka huu.
Tamasha la Cannes, ni miongoni mwa matamasha ya filamu makubwa duniani ikiwa pamoja na tamasha la Oscars. Wanafilamu,watayarishaji na waongozaji wa filamu wanakutana sio tu kushindanisha filamu lakini pia ni nafasi kubwa ya kuuza filamu zao kwa makampuni makubwa.
KFCB imepiga marufuku filamu hiyo kuonyeshwa hadharani au kutangazwa kwenye televisheni na kusambazwa, ikisema maudhui ya filamu hiyo inayoonesha mapenzi ya jinsia moja kati ya wanawake wawili, inakiuka sheria za Kenya.
Filamu hiyo imeandikwa na kuongzwa na Wanuri Kahiu aliyetangaza habari hizo za kupigwa marufuku kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter, akisema "niliamini kuwa watu wazima Kenya wamenyimwa haki zao za kujichagulia maudhui wanayoyataka kuyaona"
I am incredibly sorry to announce that our film RAFIKI has been banned in Kenya. We believe adult Kenyans are mature and discerning enough to watch local content but their right has been denied. #Cannes2018#AKenyanFirst
Hadithi ya Rafiki ni kuhusu wasichana wawili Kena na Ziki, marafiki wa karibu ambao baadae walikuwa wapenzi. Familia zao wako katika pande tofauti za kisiasa.
Wanakutana na shinikizo kubwa ambalo linaathiri urafiki wao. Hali hii inawafanya kufanya maamuzi magumu baina ya furaha yao au usalama wao.
KFCCB inasema kuwa " baadhi ya picha zinazoonyesha mapenzi ya jinsia moja zinakiuka sheria, utamaduni na maadili ya Wakenya. Inajaribu kuhalalisha mapenzi ya jinsia moja kati ya wanawake"
Bodi hiyo imeonya kuwa mtu yeyote atayekutwa na filamu hiyo atachukuliwa hatua za kisheria.
Wanaharakati wanaotetea mapenzi ya jinsia moja waliandika kwenye mtandao wa Twitter wakishutumu bodi hiyo .
This begs the question, had the film not been nominated (FYI We are so proud of Wanuri and the team), would @EzekielMutua still celebrate her? The the film and our diversity? #QueerFilm Wanuri Kahiu's film 'RAFIKI' to premiere at Cannes Film Festival https://youtu.be/DkJrjURBqWI
Mwezi Juni mwaka uliopita, bodi hiyo ilipiga marufuku baadhi ya vipindi vya televisheni katika ving'amuzi vya DSTV na GOTV vilivyosemekana kuunga mkono mapenzi ya jinsia moja.
Vitendo vya mapenzi ya jinsia moja ni kinyume ya sheria kama nchi nyingi barani Afrika. Tendo la ngono kati ya watu wa jinsia moja inahukumu ya miaka 14 gerezani nchini Kenya.
Mwezi uliopita, mahakama ya Kenya iliamua kwamba kitendo cha kuwalazamisha kuwapima kwa nguvu sehemu za siri za wanaume ilikubaini kama wanajihusisha na mapenzi ya jinsia moja, ni kinyume cha sheria .
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionTanuru zinazotumiwa kuchoma wafu
Mwanasiasa na mpiganiaji wa vyama vingi Kenneth Matiba ambaye mwili wake utachomwa siku ya Ijumaa anajiunga na orodha ya watu maarufu nchini Kenya ambao wametaka kutozikwa kulingana na tamaduni nchini Kenya.
Mwili wa mwanasiasa huyo ambaye amesifiwa kama mpiganiaji wa uhuru wa pili utachomwa katika makaburi ya Langata siku ya Ijumaa, kulingana na matakwa yake, familia imesema.
Na katika miaka ya hivi karibuni, baadhi ya wanasiasa, viongozi wa makanisa na wanamichezo maarufu pia wameamua kuchagua njia hiyo wengine wakienda kinyume na matakwa ya familia zao na jamii.
Askofu wa zamani wa kanisa la Anglikana alianzisha mjadala kuhusu kifo katika kanisa hilo ambalo aliloliongoza na miongoni mwa Wakenya 2005, mwili wake ulichomwa kulingana na na kile ambacho familia yake inasema ni wasia wake.
Miaka mitatu awali mwili wa mkewe Mary Kuria ulikuwa umechomwa. Mwili wa bi Mary Nyambura Kuria ulichomwa na kuwa majivu katika eneo la Lang'ata siku mbili tu baada ya kufariki katika hospitali ya Nairobi.
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionJumba la tanuru
Kila uchao idadi ya watu wanaoamua kuteketezwa moto wanapofariki inaongezeka ikilinganishwa na wanaoamua miili yao izikwe.
Kuna sababu nyingi zinazochangia uamuzi huo:
Gharama: Kwa jumla gharama ya kuchomwa ni chini ya ile ya kuzikwa. Huhitaji kaburi katika kuchoma maiti wala jiwe la kaburini , na vifaa vinavyotumika katika kuteketeza maiti ni vya bei rahisi ikilinganishwa na kuzika katika majeneza. Nchini Kenya gharama ya kuchoma maiti ni kati ya dola 1000 - 2200.
Nafasi za makaburi: Suala la nafasi za makaburi au ardhi wanakozikwa maiti ni changamoto kubwa hususan katika maenoe ya miji . Kuna ardhi kidogo sana za kuzika na jamii huwana wasiwasi kuuza ardhi zao kwa minajili ya kugeuza kuwa eneo la kuzika maiti.
Ni njia rahisi: Kuchoma maiti kunaondosha wasiwasi na kero za kutafuta ardhi, majeneza kuandaa mazishi, kama kutafuta wabeba Jeneza, tofuati na kuchoma mwili ambapo majivu ya mwisho huhifadhiwa katika jagi dogo ambalo ni rahisi kulibeba kwa mkono.
Wasiwasi wa kimazingira: Kwa kawaida kemikali hutumiwa katika kutayarisha mwili uzikwe ardhini. Kweli huwa kuna hewa mkaa/chafu nyingi mwili unapochomwa lakini kadri teknolojia inavyoendelea kukuwana vifaa kuboreshwa, athari kwa mazingira inaongezeka. Hatahivyo bado kuna mjadala, lakini kwa jumla inaonekana ni bora kwa mazingira kuchoma kuliko kuzika maiti.
Tamaduni na imani: Tamaduni na imani za jamii ni muhimu na baadhi ya imani kama Wahindu ni sharti maiti achomwe. Kwa wengine familia huamua kumuaga mtu anapofariki kwa njia ya ki aina yake.
Habari za kuchomwa kwake zilijiri bila kutarajiwa kwa waombolezaji ambao walikutana katika kanisa la All Saints Cathedral mjini Nairobi kwa hafla ya kutoa shukrani.
Uamuzi huo ulisababisha mjadala katika kanisa hilo kuhusu uchomaji wa miili , huku wanachama wengi wakipinga wazo hilo.
Peter Habenga Okondo
Muongo mmoja uliopita, aliyekuwa waziri wa KANU Peter Okondo pia alikuwa amechomwa katika zoezi ambalo lilizua migawanyiko kati ya familia ya waziri na jamii yake ya Banyala.
Idadi kubwa ya wanakijiji waliwasili mjini Nairobi kabla ya kugundua kwamba mkewe alikuwa tayari ameuchoma mwili wake
Joshua Okuthe
Tatizo kama hilo lilionekana kufuatia kuchomwa kwa mwili wa msimamizi wa michezo wa zamani Joshua Okuthe. Mkewe wa kwanza Ruth Florence aliuchoma mwili wa mumewe mwenye umri wa miaka 62 mnamo mwezi Julai 9 2009 katika makaburi ya kariokor siku nne baada ya kifo chake.
Familia yake ililazimika kuzika jeneza tupu nyuma ya chumba chake cha kulala mjini Tamu, Wilaya ya Muhoroni kwa kuwa alitaka achomwe kulingana na wasia wake.
Wangari Maathai
Haki miliki ya pichaREUTERSImage captionWangari Maathai
Mshindi wa tuzo ya Nobel marehemu Wangari Maathai alichomwa 2011 katika sherehe kubwa iliofanywa katika faragha za tanuru ya Kariokoo.
Familia ya mwanamazingira huyo na serikali zilikubali kuuchoma mwili huo kabla ya mabaki yake kuhifadhiwa katika Taasisi ya Wangari Maathai kuhusu amani na utafiti wa mazingira, kulingana na matakwa yake.