Saturday, March 3

Makatibu wakuu 12 watembelea Hifadhi ya Ziwa Manyara

Mwenyekiti wa makatibu wakuu hao, Katibu mkuu
Mwenyekiti wa makatibu wakuu hao, Katibu mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Maimuna Tarishi  
Arusha. Makatibu wakuu wa wizara 15 pamoja na baadhi ya watendaji wa wizara hiyo watembelea Ziwa Manyara kuona hali halisi ya uharibifu wa ambao unatishia kukauka kwa ziwa hilo.
Mwenyekiti wa makatibu wakuu hao, Katibu mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Maimuna Tarishi amesema lengo la ziara hiyo ya kazi ni kujionea uharibifu wa ziwa na kuishauri Serikali.
Amesema hivi karibuni mawaziri ambao wizara zao zinahusiana na ziwa hilo walikutana na kupokea changamoto za ziwa hilo na waliagiza makatibu wakuu kutembelea na kupata hali halisi na baadae kuishauri Serikali.
Mkurugenzi mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa), Allan Kijazi amesema ziwa Manyara lipo hatarini kukauka kutokana na kuongezeka shughuli za kibinaadamu pembezoni mwa ziwa.
Amesema shughuli hizo pia zimeathiri mapito na mtawanyiko wa wanyama katika eneo la ikolojia ya hifadhi za Manyara na Tarangire.
Ziara ya makatibu wakuu inaendelea muda huu na inashirikisha watendaji wa Serikali, ofisi ya mkuu za wakuu wa mikoa Arusha na Manyara, ofisi ya mwanasheria mkuu wa Serikali na maofisa wa  wizara hizo.

HEKAYA YA MLEVI : Ukiona wanatupiana maandazi ujue wameshiba



GASTON NUNDUMA
GASTON NUNDUMA 
Babu mmoja aliokota jiwe. Akalibandika karatasi iliyosomeka: “Hili ndilo jiwe alilojisugulia Mkwawa”. Akampa mjukuu wake alitembeze kwenye mitaa ya uswazi kwa nia ya kujua thamani yake. Akamwambia kuwa watu wakiulizia bei asiongee neno zaidi ya kunyoosha vidole vitatu.
Mzee aliona mbali sana. Alijua wazee wa bandari wangejifanya kuwa wao walikuwa wakinywa “chimpumu” na Mkwawa halafu wangemhoji jinsi alivyolipata jiwe hilo. Hatimaye wangemnyang’anya na kulitia sokoni kwa maelezo yaleyale yaliyoandikwa na babu. Hivyo dogo akaekti ububu.
Watu walimsimamisha na baada ya kusoma sifa za jiwe wakamuuliza bei. Dogo akanyoosha vidole vitatu hewani. Wakasema “aha! Buku tatu. Bei ya mwisho je? Je bei ya kuuzia?” Dogo akarudia vidole vilevile vitatu.
Walipotaka kununua dogo aliondoka na jiwe lake na kurudi kwa babu. Babu akamwambia, “Sasa hivi nenda mitaa ya uzunguni. Ukiulizwa bei ufanye kama nilivyokuagiza.” Dogo akaingia Oysterbay na Masaki. Aliponyoosha vidole vitatu wakasema “Elfu thelathini? Niuzie…”
Akarudi tena kwa babu. akaambiwa “Sasa tembea kwenye balozi za mamtoni ukafanye vilevile. Lakini sasa usirudi nalo, liuze huko.” Dogo akaingia ubalozini.
Kama kawaida alipoulizwa bei akanyoosha vidole vitatu. Balozi akasema “Laki tatu? Tafadhali niuzie…” Akachukua hela na kurudi kwa babu. Maisha yakaendelea. Yule balozi alilipeleka jiwe Ulaya na kuliweka kwenye soko la vitu vya kale vilivyovumbuliwa barani Afrika.
Siku moja dalali wa Kiswahili alipita kwenye soko hilo, akalinunua jiwe hilo kwa dola zenye thamani ya shilingi milioni tatu za Kitanzania. Alijua kwa sifa za jiwe hilo asingekosa shilingi milioni thelathini kutoka serikalini ili jiwe likahifadhiwe kwenye Makumbusho ya Taifa.
Tunajifunza kuwa thamani ya kitu hupandishwa na watu kulingana na mazingira ya soko. Kuna koti ulitaka kuuziwa pale Tandika lakini ukalikwepa kwa madai ya viwango. Likapelekwa dry cleaner na ukaletewa ofisini kwako kule Kivukoni ukalinunua kwa bei mara kumi ya ile uliyotajiwa Tandika.
Au hujui kwamba zile kauzu za pakti unazozinunua shilingi elfu mbili Posta na Feri ndio zilezile zinazouzwa kwenye genge la jirani tena kwa shilingi mia tano tu? Au ni kwa sababu kwenye pakti kuna tangazo linalosema dagaa wanaongeza kinga ya mwili na nguvu za kiume? Yaleyale ya “jiwe aliloogea Mkwawa”.
Kwa hili nawapongeza wajasiriamali. Wanajua kuwa uongo wa sangoma ndiyo tiba ya mgonjwa. Lakini kwa leo inanibidi nirudi kuwa mzalendo mwenye kutazama maslahi mapana ya Taifa langu kwanza.
Mtu yeyote mwenye busara hakosi bustani ya mboga nyumbani kwake. Akikosa basi ni kwa sababu iliyo nje ya uwezo wake; pengine kiwanja alichoweza kununua kilimtosha kuinua mjengo tu bila kuacha mahali pa kucheza watoto.
Bustani ingembeba akapata angalau mboga orijino maana hizi za mtaani hazieleweki kabisa. Vilevile atapata utelezi kidogo wakati vyu… wakati hali imekuwa ngumu. Unaweza kuamka na maganda ya karanga mfukoni bila senti ukasonga unga uliobaki jana kwa tembele la bustanini kuliko kumsomesha mgogo buchani. akukopeshe nyama. Mwaka 1985 Mwalimu Nyerere alizindua kiwanda cha kutengeneza karatasi huko Mufindi Mkoani Iringa. Bila shaka alizingatia mahitaji ya karatasi yalivyokuwa yakipanda. Kwanza wasomi walikuwa wakiongezeka kila muhula. Wasomi wote (kuanzia vyuoni hadi chekechea) hawakuweza kufanya lolote pasipokuwa na karatasi. Hata huku mtaani wakati vita ya taka sugu kama plastiki ikipamba moto, karatasi ilikuwa mkombozi kwenye mifuko, na mapambo.
Pia kuna mtu alinieleza kuwa bi mkubwa wake alikuwa akitumia mkaa wa karatasi tangu akiwa mwanamwali. Aliloweka karatasi na maboksi kwa siku kadhaa, akayachanachana ndani ya maji na kuyakamua katika mfano wa matonge ya ugali. Kisha akayaanika juani. Kitu tayari. Huyu atunukiwe shahada ya mazingira.
Kile kiwanda kilifanya kazi nzuri kiasi kwamba Tanzania iliuza karatasi hadi nje. Lakini pia tulipata vifungashio vya bidhaa za viwandani (kwa maana ya maboksi na mifuko).
Lakini mwaka 2004 kiwanda kikauzwa kimya kimya kwa Wakenya kwa madai ya kutozalisha vizuri. Sijui ni nani anayeukata mkono wa mtoto wake kwa sababu ati kaunyea! Lakini kwa sababu yaliyopita si ndwele, tutazame yanayotokea sasa. Ukiyakosa maji ndipo utajua umuhimu wake.
Hivi sasa tunategemea karatasi za Afrika Kusini, lakini hasa za China. Kutokana na desturi ya Wachina, kuanzia tarehe 23 mwezi wa 12 hadi tarehe 15 mwezi wa Januari Wao huwa likizoni kuadhimisha sikukuu ya mwaka mpya wa kijadi.
Hali hii inatuathiri sana kwa sababu hakuna mizigo inayoingia wakati sisi hutumia makontena mengi sana ya karatasi katika muda mfupi. Kwa uhaba huo bei hupanda hadi mara tatu ya bei elekezi. Wengi wanashindwa kununua na elimu ya watoto wao inayumba kwa sababu wakizikosa wanafukuzwa shuleni.
Huwa najiuliza Wakenya waliona nini ambacho sisi wenye kiwanda tulishindwa kukiona. Bila shaka wao wana upeo wa babu aliyeuza jiwe. Tangu enzi zile walitukimbiza sana na bidhaa zao kama mafuta ya Blue Band dhidi ya Tan Bond yetu kwa jinsi walivyojua kuongeza thamani.
Japokuwa hatushadadii yaliyopita lakini “Tanzania ya Viwanda” isipofanya “ndwele” sijui kama tutafika.

Kufungiwa ‘chura wangu’ sielewi hadi sasa


Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Snura Mushi, amesema hadi sasa haelewi ni kwanini nyimbo zake mbili zimefungiwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).
Akizungumza na MCL Digital, leo Machi 3, Snura amesema kufungiwa kwa nyimbo zake mbili ya ‘Chura’ na ‘Nimevurugwa’ kumemchanganya na wala haelewi hadi sasa nini sababu ya kufikiwa kwa hatua hiyo na mamlaka hiyo ya Serikali.
Akitolea mfano wa wimbo wa ‘chura’ Snura amesema video yake ilipofungiwa alitakiwa kuirekebisha na alifanya hivyo na kisha ikahaririwa na vyombo vyote ikiwamo Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) na TCRA wenyewe na kumruhusu kuionyesha.
“Lakini juzi nashangaa kati ya nyimbo 15 zilizofungiwa yangu hiyo ya chura nayo ilikuwa mojawapo hadi najiuliza kumetokea nini hasa hadi wanipe adhabu hiyo kubwa kwangu,” amesema Snura.
Wakati kwa wimbo wake wa ‘Nimevurugwa’ amesema ana uhakika hakuna tusi lolote ndani ya wimbo huo na kueleza hata video yake haoni kama ina shida.
Pia msanii huyu ameeleza pamoja na yote hayo hajapewa barua hadi sasa kama ilivyo taratibu msanii unapotaka kufungiwa nyimbo yako na wala Basata haijamuita kumweleza tatizo lake ni nini hasa.
Kutokana na hatua hiyo, MCL Digital, pia iliweza kuongea na Mkurugenzi wa TCRA, Mhandisi James Kilaba, ili kujua ni vigezo gani walivyotumia katika kuzifungia nyimbo walizozitaja ukizingatia nyingine zilishafungiwa kipindi cha nyuma na wasanii kulipishwa faini.
Katika majibu yake, Mhandisi Kilaba, amesema swali hilo waulizwe Basata kwa kuwa wao ndio waliwapelekea malalamiko kuhusu nyimbo hizo na kwa kuwa moja ya  kazi yao ni kusimamia redio na televisheni ndio wakaamua kuchukua hatua hiyo ya kuviandikia barua vyombo hivyo kuacha kuzionyesha na kuzicheza.
Wakati Katibu Mtendaji wa Basata, Godfrey Mngereza, amesema walichukua hatua ya kupeleka malalamiko yao TCRA, baada ya kuona pamoja na kuzifungia nyimbo hizo lakini bado baadhi ya vituo vya redio na televisheni ziliendelea kuzicheza na wao hawana mamlaka ya kuvichukulia hatua vyombo hivyo zaidi ya kuishia kwa wasanii.
Februari 28 TCRA iliandika barua kwa vituo vya redio na televisheni ikiviagiza visitishe kuonyesha nyimbo 15 za wasanii kadhaa kutokana na kuwa na maudhui ambayo yanaenda kinyume na maadili na kanuni za Huduma za Utangazaji (Maudhui) 2005.
Nyimbo hizo na jina la msanii aliyeimba kwenye mabano ni  Hallelujah na Wakawaka (Diamond), Kibamia (Roma Mkatoliki), Pale Kati patamu, Maku (Makuzi) na Mikono Juu (Ney wa Mitego), Hainaga Ushemeji (Manifongo), I am Sorry JK (Nikki Mbishi).
Nyingine ni Chura na Nimevurugwa (Snura), Tema mate tumchape (Madee), Uzuri wako (Jux), Nampa papa (Gigy Money), Nampaga (Baranaba) na Bongo Bahati mbaya (Young D).

Majaliwa awataka wakulima wa ufuta kuuza zao hilo mnadani


Ruangwa. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka wakulima wa ufuta katika mikoa inayolima zao hilo nchini kuuza kwa kutumia njia ya minada na si mashambani.
Ametoa agizo hilo leo (Jumamosi, Machi 03, 2018) wakati akizungumza kwa nyakati tofauti na wananchi wa vijiji vya Nachihungo, Narung’ombe na Chikwale.
Waziri Mkuu ambaye yuko wilayani Ruangwa kwa ziara ya kikazi amesema ili wakulima wapate tija ni vema wakauza ufuta wao kwa kupitia minada kama inavyofanyika katika zao la korosho.
“Usikubali kumuuzia mtu yeyote ufuta wako ukiwa shambani kwa sababu bei atakayonunulia ni ndogo kulinganisha na soko, naamini ufuta wote ukiuzwa katika minada mtaona faida,” amesema.
Kufuatia agizo hilo amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, Andrea Chezue aandae utaratibu wa maeneo ya kukusanyia ufuta na kufanyia minada.
Amesema ufuta unaolimwa nchini ni bora na unapendwa sana duniani hivyo wasiwe na wasiwasi. Baadhi ya mikoa inayolima ufuta kwa wingi ni Lindi, Pwani, Dodoma, Manyara, Kigoma na Singida.
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema vijiji vyote visivyokuwa na umeme nchini vikiwemo vya wilaya ya Ruangwa vitaunganishiwa katika Mradi wa Umeme Vijijini (REA) awamu ya tatu.
Amesema wananchi waendelee kuwa na subira kwa sababu tayari mkandarasi ameshaanza kazi ya kuunganisha umeme katika vijiji vingine vya wilaya hiyo na atafika kwenye maeneo yao.
Alibainisha kuwa mkakati wa Rais John Magufuli ni kuhakikisha wananchi wote nchini wanaunganishiwa nishati ya umeme kwenye majumba yao, hivyo waendelee kuwa na subira na kushirikiana na Serikali yao.
Kuhusu suala la upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama alisema, “Huduma ya upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi ni miongoni mwa vipaumbele vya Serikali ya Awamu ya Tano, hivyo vijiji vyote vitapata maji.”
Pia alitumia fursa hiyo kuwahamasisha wananchi kote nchini kutunza vyanzo vya maji ili kuliepusha taifa kugeuka jangwa pia miradi inayoletwa na Serikali iwe endelevu.

Mama ajifungua watoto wanne kwa mpigo Dar


Dar es Salaam. Ofisa Tarafa wa Kibamba, wilayani Ubungo, Beatrice Mbawala amejifungua watoto wanne kwa mpigo katika Hospitali ya Agha Khan, jijini hapa.
Beatrice amejifungua watoto hao wakiwa njiti mwezi mmoja uliopita.
Akizungumza hospitalini hapo, leo Machi 3, baba wa watoto hao, Julius Mbawalla amesema familia yake ina furaha kupokea watoto wanne na kwamba jukumu lake kubwa ni kuhakikisha mkewe anapata huduma muhimu ili aweze kumudu kuwanyonyesha.
Daktari Bingwa wa Watoto katika hospitali ya Agha Khan, Dk Mariam Mgonja amesema afya za watoto zimeimarika na tayari wameruhusiwa kwenda nyumbani.

Operesheni za UN zasitishwa mjini Rann,Nigeria

Wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa nchini Nigeria
Image captionWafanyakazi wa Umoja wa Mataifa nchini Nigeria
Umoja wa Mataifa umeeleza kwa kina kuhusu sababu za kusitisha operesheni za kibinaadam mjini Rann nchini Nigeria baada ya shambulio la siku ya Alhamisi ambalo linadaiwa kutekelezwa na wanamgambo wa kiislamu, Boko Haram.
Zaidi ya wafanyakazi 50 wa misaada walikuwa wakitoa usaidizi kwa takriban watu 80,000 mjini Rann, mji uliotengwa, hakuna mtandao wa simu.
Msemaji wa UN nchini Nigeria, Samantha Newport amesema shambulio la siku ya Alhamisi liligharimu maisha ya wafanyakazi wa misaada watatu, watatu walijeruhiwa, wengine hawajulikani walipo.
''kutokana na hilo Umoja wa Mataifa umeamua kusitisha kwa muda operesheni zake mjini Rann pekee kwa muda wa juma moja''.Ameeleza
Samantha amesema inaonekana shambulio hilo lilikusudiwa kulenga wanajeshi, hivyo kwa bahati mbaya wafanyakazi wa UN ilitokea tu walikuwepo hapo kwenye eneo baya na kwa wakati mbaya.

Ni kwa nini wacheza utupu huhudhuria mazishi nchini China

File photo of a pole dancer in ChinaHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionThe Chinese government is trying to crack down on what it calls "obscene performances"
Muziki unacheza kwa sauti, wacheza utupu wakicheza densi na umati ukishangilia. Katika sehemu zingine huko China hili ndilo unaweza kuliona wakati wa mazishi.
Mapema mwaka huu, China alianza tena kuwakamata wacheza utupu wanaocheza densi kwenye mazishi, harusi na kwenye mahekalu.
Hio sio mara ya kwanza mamlaka zimejaribu kuzuia tabia hizo lakini bado hazijanafikiwa

Mbona watu huwaajiri wacheza utupu?

Wacheza utupu hutumiwa kuwavutia watu wnaaohudhuria mazishi kwa sababu uwepo wa watu wengi kwenye mazishi huonekana kama heshima kwa marehemu.
Imani nyingine zinasema kuwa suala hilo na la kuabudu.
Imani nyingi ni ile kuwa kuwaajiri wacheza utupu kunaweza kuonekana kama ishara ya utajiri.
Maeneo ya vijijini nchini China ndiyo yenya tabia ya kutumia pesa nyingi hata kuliko mapata, kuwalipa wuigizaji, waimbaji, wachekeshaji na wacheza utupu kuwatumbuiza wale waliofiwa.

Shughuli hii ni maarufu?

Tamaduni hiyo inapatikana sana maeneo ya vijijini ya China na ni maarufu zaidi nchini Taiwan ambapo ilianzia.
"Tamaduni hii ya wacheza utupu kwenye mazishi kwanza lilipata umaarufu nchini Taiwan mwaka 1980," msomi wa chuo cha South Carolina Marc Moskowitz aliiambia BBC.
Tamaduni hii imepata umaarufu nchini Taiwan lakini nchini China serikali imeizuia na watu wengi hawafahamu kuihusu.
This picture taken on 3 January 2017 shows a pole dancer performing on top of a jeep during the funeral procession of former Chiayi City county council speaker Tung Hsiang in Chiayi City, southern Taiwan.Haki miliki ya pichaAFP/GETTY IMAGES
Image captionPole dancers have also performed in funeral processions in Taiwan

Makampuni yashinikizwa kutowekeza kwa watengeneza silaha Marekani

Makampuni yanayouza silaha yatakiwa kuhakikisha usalama wa matumizi ya silaha unakuwepo
Image captionMakampuni yanayouza silaha yatakiwa kuhakikisha usalama wa matumizi ya silaha unakuwepo
Kampuni kubwa ya usimamizi katika uwekezaji imeweka shinikizo dhidi ya makampuni yanayotengeneza na kuuza silaha baada ya tukio la mashambulizi katika shule ya Florida.
Kampuni ya Black Rock imekuwa ikiwashawishi wawekezaji kutowekeza kwenye makampuni ya kutengeneza silaha na amekuwa akiyauliza makampuni ni namna gani huwa wanachunguza matumizi salama ya silaha.
Shirika hilo limesema jambo linatakiwa kufanyika baada ya tukio la Florida ambapo watu 17 walipoteza maisha.
Shirika hilo ni mdau mkubwa katika viwanda vikubwa viwili vya kutengeneza silaha nchini Marekani.
Black Rock inaamini kuwa tukio hilo linahitaji mwitikio kutoka kwenye sekta zote, za uma na binafsi.

Mkuu wa Kampuni ya Nishati ashutumiwa kumuua mwanaharakati wa mazingira

Mwanaharakati Caceres ni miongoni mwa wengine 100 waliouawa katika kipindi cha muongo uliopitaHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMwanaharakati Caceres ni miongoni mwa wengine 100 waliouawa katika kipindi cha muongo uliopita
Polisi nchini Honduras inamshikilia Mkuu wa Kampuni ya masuala ya nishati akishukiwa kupanga mauaji ya mwanaharakati wa mazingira.
Berta Caceres aliuawa kw kupigwa risasi nyumbani kwake miaka miwili iliyopita
Mwanamama huyo alipinga vikali mradi wa ujenzi wa bwawa.
Roberto David Castillo ni rais wa Kampuni iitwayo Desa, kampuni hiyo ilikuwa inajenga bwawa.
Kampuni hiyo imeshutumiwa na kukemewa vikali kimataifa pia zilifanyika kampeni za mashirika mbalimbali yasiyo ya kiserikali yakikemea tukio hilo.
Imeripotiwa kuwa Castillo alikua mwanajeshi, afisa wa intelijensia.
Mkuu wa Kampuni ya Nishati anayeshutumiwa kupanga njama za mauajiHaki miliki ya pichaAFP
Image captionMkuu wa Kampuni ya Nishati anayeshutumiwa kupanga njama za mauaji
Watu wengine wanane wameshtakiwa kutokana na mauaji hayo, wakiwemo polisi na wafanyakazi wa Desa.
Familia ya Caceres imesisitiza kuwa aliuawa kwa sababu za kiuchumi.
Inasema Caceres kwa miezi mingi amekuwa akipata vitisho kutoka kwa Polisi,wanasiasa na Kampuni za ujenzi.
Mwezi Novemba mwaka 2017, ripoti ya kurasa 92 kutoka kwa wataalamu wa kimataifa ilihitimisha kuwa Kampuni hiyo na mawakala walipanga kumuua mwanaharakati huyo.
Mwanaharakati Caceres atakumbukwa kwa kupigania haki za jamii ya wachache katika hali ya amani na mwaka 2015 alishinda tuzo ya Goldman, moja kati ya tuzo muhimu za masuala ya mazingira.
Majaji wa walisema kuwa aliongoza kampeni ya watu wa jamii ya Lenca nchini Honduras kampeni ambayo ilifanikiwa na kushinikiza mjenzi wa bwawa kubwa zaidi duniani kuondoka kwenye bwawa la Agua Zarca.
Bwawa hilo lingeleta madhara kama mafuriko na kukata miundo mbinu ya kusambaza maji, chakula dawa kwa ajili ya jamii ya Lenca.
Caceres ni mmoja kati ya wanaharakati 100 wa masuala ya ardhi waliouwawa nchini Honduras katika kipindi cha muongo uliopita.

Waandamanaji wakabiliana na Polisi Ukraine

Takriban watu 100 wamekamatwa na Polisi baada ya kutokea vuruguHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionTakriban watu 100 wamekamatwa na Polisi baada ya kutokea vurugu
Watu kadhaa wamejeruhiwa mjini Kiev nchini Ukraine, wakati wa makabiliano kati ya waanamanaji wanaoipinga serikali na Polisi.
Vyombo vya habari nchini humo vimesema makabiliano hayo yalianza wakati waandamanaji walipowasha moto matairi ili kuwazuia maafisa wasifanyie ukaguzi Kambi ya waaandamanaji iliyokuwa nje ya Bunge.
Polisi wa Ukraine wamesema watu 50 wamekamatwa.Wamesema walikuwa wanafanyia uchunguzi kambi hiyo ili kupata ushahidi kuhusu makabiliano yaliyofanyika jumatatu iliyopita na kusababisha maafisa polisi kadhaa kujeruhiwa.
Katika kamatakamata hiyo Polisi wamekamata maguruneti ya kurushwa kwa mkono yaliyokuwa kwenye turubai la kambini hapo.

RAIA WA CHINA ALIPA MILIONI 110/- KUKWEPA KWENDA JELA MIAKA 20


MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuhukumu Raia wa China, Liu Xiu Feng kutumikia kifungu cha miaka 20 jela ama kulipa faini ya Sh.milioni 110 baada ya kukiri kosa la kukutwa na meno ya Simba mawili.

Hukumu hiyo imesomwa leo na Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi baada ya Wakili wa Serikali Mwandamizi, Mutalemwa Kishenyi kueleza mshtakiwa huyo amekiri kosa.

Hakimu Shaidi amesema kutokana na mshtakiwa huyo kukiri kosa Mahakama inamuhukumu kutumikia kifungo cha miaka 20 gerezani ama kulipa faini ya sh.milioni 110."Mahakama inakuhukimi kutumikia kifungo cha miaka 20 jela ama ulipe faini ya Sh.milioni 110," amesema Hakimu Shaidi.

Baada ya kutolewa hukumu hiyo, mshtakiwa Feng aliepuka kwenda jela baada ya kulipa faini hiyo ya Sh.milioni 110.

Raia huyo wa China alikuwa akikabiliwa na kosa la kukutwa na meno mawili ya Simba katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA).Alikutwa na meno hayo Februari 7,mwaka 2018 ambapo yanathamani ya Sh.milioni 11, 029,900.

ALIYEKUWA MWANAJESHI, WENZAKE WAHUKUMIWA KWENDA JELA MIAKA 20


ALIYEKUWA mwanajeshi wa Jeshi la Wananchi Tanzania(JWTZ),Ex MT 66807 na wenzake watatu wamehukumiwa kwenda jela miaka 20 baada ya kupatikana na hatia ya kukutwa na meno ya Tembo yenye thamani ya Sh.198.

Hukumu hiyo imesomwa leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi  Kasonde.Watuhumiwa wengine waliohukumiwa kifungo hicho ni Bakari na Shafii Muhibu Muhibu.

 Hata hivyo, Mahakama imemuachia huru Asha Hassan Ulaya, aliyekuwa akishtakiwa na wenzake hao baada ya upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha mashtaka bila ya kuacha shaka yoyote kuwa naye alihusika kwenye tukio hilo.

Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Kasonde amesema upande wa mashtaka kupitia mashahidi wake nane wameweza kuthibitisha mashtaka dhidi ya washtakiwa hao watatu pasipo kuacha shaka yoyote kuwa wametenda kosa.

"Mahakama inawahukumu washtakiwa wote watatu kutumikia kifungo cha miaka 20 jela kila mmoja kwenye shtaka la kwanza na vilevile shtaka la pili miaka 20,"amesema Hakimu Kasonde.Pia Mahakama imeamuru meno ya Tembo yarudishwe kwa Mkurugenzi wa Wanyama pori na gari aina ya Suzuki waliyokamatwa washtakiwa waliyotumia kubebea meno hayo itaifishwe na Serikali.

Katika hati ya mashtaka, inadaiwa, Juni 2, mwaka 2016 huko Mbagala Kibondemaji wilayani Temeke jijini Dar es Salaam, washtakiwa wote walikamatwa na vipande 10 vya meno ya Tembo.Pia washtakiwa hao walikuwa wanadaiwa kukubali kisafirisha meno hayo ya Tembo yenye thamani ya Sh. milioni 198,mali ya Serikaliya Tanzania.

Washtakiwa hao wanadaiwa kukutwa na nyara hizo za Serikali bila ya kuwa na kibali kutoka kwa Mkurugenzi wa wanyama pori.

UCHAGUZI K’NDONI, SIHA: RIPOTI YAFICHUA MAZITO



ZIKIWA zimepita siku kadhaa tangu ulipofanyika uchaguzi mdogo katika majimbo ya Kinondoni na Siha, taarifa ya tathmini ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), imeibua mazito.
Kati ya yaliyobuliwa katika taarifa hiyo ni tukio la kuibwa kwa sanduku la kura na watoto wadogo kupandishwa kwenye majukwaa ya kampeni jambo ambalo ni kinyume cha sheria.
Mbali na hilo, katika ripoti hiyo ya tathmini inadaiwa baadhi ya viongozi wa Serikali akiwamo waziri mmoja (jina linahifadhiwa), alitumia gari la Serikali katika kampeni kwenye uchaguzi wa Kinondoni.
Kutokana na hali hiyo, tathmini ya LHRC imetoa kasoro 11 katika uchaguzi huo wa marudio ambao walidai vyama vya upinzani viligandamizwa tofauti na chama tawala.

Wachumi watoa jibu Taifa kuondokana na utegemezi


Wakati kiwango cha utegemezi kiumri kwa Watanzania ni asilimia 92, wataalamu wa uchumi wameshauri mbinu zinazoweza kutumika kuondokana na hali hiyo ili kufikia Tanzania ya uchumi wa viwanda.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na Mwananchi jana, wachumi hao walisema ni hatari kwa Taifa lolote duniani kuwa na kiwango kikubwa cha utegemezi pamoja na kuwatumia wataalamu maeneo sahihi ya taaluma zao.
Juzi, taarifa ya makisio ya idadi ya watu nchini iliyotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) na kuzinduliwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango ilieleza kuwa Tanzania inakadiriwa kuwa na idadi ya watu 54.2 milioni huku ongezeko kwa mwaka likiwa ni wastani wa watu 1.6 milioni.
Dk Mpango alisema kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012, kiwango cha utegemezi kinaonyesha kati ya Watanzania 100 wenye umri wa miaka 15 hadi 64 wanategemewa na watu 92 wenye umri wa chini ya miaka 15 na juu ya 65 ikilinganishwa na asilimia 40 ya nchi zinazoendelea.
Alisema kiwango kikubwa cha utegemezi kinachotokana na idadi kubwa ya watoto ni changamoto kwa maendeleo ya nchi yoyote duniani, huku akieleza kwamba sera ya maendeleo ya watu hailazimishi kuzaa idadi fulani ya watoto isipokuwa inatahadharisha wazazi kupata watoto wanaoweza kumudu kuwalea.
Jana, walipotakiwa kuchambua utegemezi huo na maana yake kiuchumi, Profesa wa Uchumi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salam (UDSM), Benedict Mongula alisema suala la utegemezi si geni hasa katika suala la idadi ya watu huku akieleza namna ya kulitatua.
“Tukuze uchumi wetu kwa kuongeza uwekezaji na uzalishaji ikiwamo kuongeza juhudi na maarifa, kuongeza tija ya uzalishaji katika eneo la kilimo ili kisaidie na tunapoingia katika uchumi wa viwanda tuingie kwa makini tusije kuingia na kurudi kama huko nyuma,” alisema Profesa Mongula na kuongeza:
“Tuongeze uwekezaji hasa wa Watanzania wenyewe na kutoka nje, viwanda vyetu tunavyoanzisha tuvitafutie soko la kutosha. Tuhakikishe kunakuwa na sera maalumu ya kuvisaidia viwanda kuendelea. Sera nzuri katika kilimo ili wakulima wadogo na wakubwa waweze kunufaika.”
Profesa Mongula anaungwa mkono na Profesa mwingine wa uchumi wa chuo hicho, Haji Semboja aliyesema hakuna haja ya kulalamika na utegemezi kwani Tanzania imejaliwa kuwa na rasilimali nyingi ikiwamo ardhi, madini, bahari na nyinginezo ambazo zikitumika vizuri zitamaliza suala la ukosefu wa ajira.
Alisema kinachotakiwa kufanyika ni Bunge, Mahakama na Serikali kusimamia na kutekeleza sera na sheria zilizopo kwa ukamilifu na watendaji wanaosimamia taasisi mbalimbali kutekeleza majukumu yao ipasavyo.
“Wakati mwingine mambo yanashindwa kutekelezwa na kubaki kurukaruka au kurukia rukia kutokana na aina ya watendaji tuliona nao, mfano mimi ni Profesa wa eneo fulani, lakini nakuwa nasimamia taasisi isiyoendana na taaluma yangu, ndiyo utakuta narukaruka au narukiarukia mara hili mara lile,” alisema Profesa Semboja na kuongeza:
“Tanzania haina tatizo sasa na kwamba ni maskini hapana, rasilimali tulizonazo na namna tunavyozitumia. Tatizo ni ku- transform (kubadilisha) tulichonacho. Kuna maeneo mengine hayaendi vizuri. Ukiona hayaendi ukifuatilia ni suala la utawala. Wanaopaswa kukaa pale utagundua si wa professional (wataalamu wa fani) yao na ingependeza kuona watu sahihi eneo fulani ili kuepuka kurukiarukia mambo.”
Mchumi kutoka Taasisi ya Tanzania Music (Tamufo), Dk Donald Kisanga alisema kiuhalisia baadhi ya mila na desturi zilizopo zinachangia kuwapo kwa kundi kubwa la utegemezi jambo linalohatarisha uchumi.
“Serikali inahitaji rasilimali watu iliyoelimika, hivyo lazima kuwekeza kwenye elimu,” alisema.
Pia, alishauri kuwapo kwa mfumo wa kuandaa mazingira mazuri ya watu kujiajiri badala ya kubweteka na kusubiria ajira rasmi zinazowafanya waendelee kuwa tegemezi wakati zinapokosekana
Mtaalamu wa uchumi kutoka Taasisi ya Nnyaka Production, Dk Godwin Maimu alisema athari za utegemezi ni kubwa hasa wakati huu ambao Serikali ina mikakati ya kuingia kwenye uchumi wa viwanda. “Utegemezi unaathiri mitaji, unahamisha fedha za uwekezaji kuwa za matumizi na hii ni hatari kubwa kiuchumi, wanaotegemewa hawataweza kuendelea kuzalisha kwa sababu kila kinachopatikana kinaingia kwenye matumizi,” alisema.
Alisema hakuna taifa lolote linaloweza kuendelea duniani kama kundi la utegemezi ni kubwa kuliko la wanaotegemewa.
Ili kuondokana na dhana hiyo ya utegemezi, Dk Maimu alisema lazima Serikali ikubali kubadilisha mitalaa yake ya kufundishia na kuwekeza kwenye elimu ya vitendo badala ya nadharia inayotumika sasa.
Dk Maimu alisema wanafunzi wanapomaliza masomo yao wanapaswa kuwa na ujuzi utakaowasaidia kujitegemea, kwa sababu wengi watakuwa wamefundishwa ili wanapohitimu waweze kujitegemea. “Wanafunzi wasifundishwe kukariri, walau elimu nadharia iwe kwa asilimia 30 tu na vitendo iwe asilimia 70. Hii itasaidia kuondokana na utegemezi kwa sababu baada ya miaka kadhaa wanafunzi watakaokuwa wanahitimu watakuwa na ujuzi,” alisema.
Alisema hakuna taifa lolote linaloweza kujivunia kasi ya maendeleo kama watu wake wataendelea kuzaliana kupita kiasi.
Dk Maimu alisema utegemezi unanyima wigo mpana wa uwekezaji kwa sababu wanaotegemewa kuwekeza hubaki kwenye hatua ya chini, hivyo kutoingia kwenye ushindani wa kiuchumi kwa kuwa mitaji yao haitaweza kukua.
Alisema ipo haja kwa jamii kuelimishwa namna ya kuwaandaa watoto wao kujitegemea hasa wanapofikia umri wa kutakiwa kufanya hivyo.
“Kuna wategemezi ambao umri wao sio wa kuwa tegemezi hawa lazima watengenezewe mazingira ya kutokuwa tegemezi, hata kwa kupelekwa kwenye vyuo vya ufundi ili mwisho wa siku, utegemezi huu uondoke,” alisema.
Katika ukurasa wetu wa facebook, baadhi ya wachangiaji wamezungumzia idadi hiyo ambapo Leung Ka Yan alisema “lugha rahisi asilimia 92 ya watanzania hawana uwezo wa kuishi kwa kujitegemea wenyewe.”

Taasisi tatu nchini zatupiana mpira mabasi 70 Dart kuingia barabarani


 Taasisi tatu zote zikiwa na masilahi katika usafiri na usafirishaji zimegongana huku Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (Dart) na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri Nchi Kavu na Majini (Sumatra) wakidai hawajapata maombi ya kibali cha kuruhusu magari mapya 70 kuingia barabarani.
Dart na Sumatra zimelaumiwa kupitia taarifa iliyotolewa juzi baada ya Kampuni ya Mabasi Yaendayo Haraka (Udart), kusema kuchelewa kuingia barabarani kwa mabasi hayo waliyoyaleta hivi karibuni kunatokana na uchelewaji wa kibali kutoka Sumatra na Dart.
Akizungumza jana na gazeti hili, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Udart, Deus Bugaywa alisema mabasi hayo yataingia barabarani mara tu baada ya kupata vibali kwa mamlaka zinazohusika.
Alizitaja mamlaka hizo kuwa ni Dart ambao anadai ndio hasa wasimamizi wa mradi na Sumatra wenye mamlaka ya kutoa leseni za mabasi kuingia barabarani.
“Ni imani yetu kwamba vibali hivyo vikitoka, basi tutawaondolea kero abiria wetu na tunawaomba kuwa na subira kwani ili mradi mabasi hayo tayari yapo hapa nchini hakuna litakaloshindikana, ni muda tu,” alisema.
Hata hivyo, gazeti hili liliwatafuta kwa nyakati tofauti na kwa njia ya simu wakurugenzi wa mamlaka hizo ili kujua sababu ya kuchelewa kutoa vibali hivyo, ikizingatiwa mabasi hayo yana wiki mbili hadi sasa tangu yaingizwe nchini ambapo yule wa Dart, Ronald Lwakatare alisema anachojua ni kuwa hajapata maombi ya kuombwa kibali kwa ajili ya mabasi hayo na kuahidi kwamba endapo yatamfikia ataharakisha kukitoa. “Hapa wewe ndio unaniambia kuwa mabasi hayo hayajaingia barabarani kwa sababu ya kibali, lakini kwa kumbukumbu yangu mpaka sasa sijaona maombi yoyote mezani kwangu yanayohusu mabasi hayo kutaka kuruhusiwa kuingia barabarani, labda kama yamekuja muda huu ambao nipo nje ya ofisi,” alisema.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mkuu wa Sumatra, Gilliard Ngewe alisema hajapata maombi yoyote na kwamba, kwa kawaida wanayapata kupitia Dart ambao ndio wasimamizi wakuu wa mradi.