Saturday, December 2

Kivumbi uchaguzi mdogo


Dar es Salaam. Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza ratiba ya uchaguzi mdogo katika majimbo ya Singida Kaskazini, Longido na Songea Mjini na kata sita za Tanzania Bara ambao utafanyika Januari 13 mwakani.
Akitoa taarifa kwa umma jijini Dar es Salaam leo Jumamosi, Makamu Mwenyekiti wa NEC, Jaji mkuu mstaafu wa Zanzibar, Hamid Mahmoud Hamid amesema tume imetangaza uchaguzi huo baada ya kupokea barua kutoka kwa Spika ya kwamba nafasi ziko wazi.
Jimbo la Singida Kaskazini liko kutokana na kujivua  uanachama wa CCM aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Lazaro Nyalandu, Songea Mjini baada ya kifo cha Leonidas Gama na Longido baada ya Mahakama kufuta matokeo ya uchaguzi yaliyokuwa yamempa ushindi Onesmo Ole Nangole.
Akizungumzia uchaguzi wa kata sita amesema waziri mwenye na serikali za mitaa kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 13(1) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Sura ya 292, aliitaarifu Tume kuwepo nafasi wazi za madiwani katika kata hizo Tanzania Bara
Alizitaja kata zinazohusika katika uchaguzi huo kuwa ni Kimandolu(Arusha), Kihesa (Iringa), Bukumbi (Uyui), Kurui (Kisarawe), Keza (Ngara) na Kwagunda (Korogwe).
 Amesema utoaji fomu za uteuzi katika majimbo hayo na kata hizo sita utakuwa ni kati ya Desemba 12 hadi 18, 2017 wakati katika jimbo la Songea Mjini utoaji fumo utakuwa kati ya Desemba 14 hadi 20 mwaka huu.
Alifafanua kuwa kwa upande wa kampeni za uchaguzi huo katika majimbo ya Singida Kaskazini na Longido na kata zote sita zitaanza Desemba 19 na kumalizika Januari 12. 
Katika jimbo la Songea Mjini, amesema kuwa kampeni za zitaanza tarehe 21 Desemba, 2017 na kumalizika tarehe 12 Januari, 2018 wakati siku ya uchaguzi katika majimbo yote matatu na kata zote sita itakuwa tarehe 13 Januari, 2017.
Jaji Hamid alivikumbusha vyama vya siasa na wadau wote wa uchaguzi wazingatie sheria, kanuni, taratibu, miongozo na maelekezo yote wakati wa kipindi cha uchaguzi mdogo wa majimbo hayo na kata sita.

Takwimu za PEPFAR zaonyesha ukimwi umedhibitiwa

Ambassador Michael Raynor
Leo ni siku ya Ukimwi Duniani. Kila mwaka, Dunia huadhimisha siku ya Ukimwi Disemba 1 ikiwa ni wakati wa kukumbuka wale waliokufa kutokana na maradhi hayo.
Wachambuzi wa masuala ya kiafya wanasema kuwa pia ni wakati ambao hutumika kuonyesha juhudi na azma ya mataifa kuwasaidia wale wanaoishi na virusi vya HIV, kufanya kazi kwa pamoja kuzuia kuenea kwake na hatimaye kumaliza maambukizo.
Matamko kutoka nchi mbalimbali yanasema siku ya Ukimwi Duniani pia ni wakati wa kusheherekea na kuwashukuru watafiti, wahudumu, familia, marafiki na jamii ambao wanafanya kazi kwa pamoja kutokomeza changamoto kubwa.
Kwa upande wake Serikali ya Marekani imesema kupitia Mpango wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na Ukimwi (PEPFAR) siyo kwamba imeokoa na kuboresha maisha ya mamilioni ya watu, lakini pia imetengeneza mpango wa dunia katika kukabiliana na HIV/AIDS.
Balozi wa Marekani nchini Ethiopia Michael Raynor amesema Takwimu za hivi karibuni za PEPFAR zinaonyesha kuwa dunia inapiga hatua katika kudhibiti maradhi ya HIV/AIDS.
Hili linaonekana katika nchi ambazo bado zinaelemewa na mzigo mkubwa wa kukabiliana na maradhi haya—kitu ambacho kilikuwa kinaonekana ni vigumu kudhibiti siyo muda mrefu uliopita. Lakini pamoja na mafanikio hayo huu siyo wakati wa kujibweteka.
Balozi huyo amesema kuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Rex Tillerson wakati wa Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa 2017, alizindua Mkakati wa PEPFAR mpya kwa ajili ya kusukuma udhibiti wa HIV/AIDS (2017-2020).
“Mkakati huo unaonyesha ushujaa na nia na msimamo wetu thabiti juu yale tunayotaka kuyafikia. Inathibitisha kuwa serikali ya Marekani, kupitia PEPFAR, itaendelea kusaidia juhudi za kudhibiti maambukizi ya ukimwi katika nchi zaidi ya 50."
Pia ni kuhakikisha wanapata huduma za tiba ya Ukimwi kwa wanajamii wote wakiwemo makundi yaliyo hatarini kutokana na maambukizo, amesema Michael Raynor.
Ameongeza kuwa huko Ethiopia, PEPFAR imewekeza takriban Dola bilioni 2 kusaidia kukabiliana na HIV/AIDS.
“Hivi leo juhudi zetu zimewezesha kuwapatia dawa za kurefusha maisha ya waathirika wa ukimwi kwa Waethopia 433,909, wakiwemo watoto," amesema.
Taarifa ya PEPFAR inaonyesha kuwa taasisi hiyo imeweza kuwezesha wanawake wajawazito takriban milioni moja nchini Ethiopia kupima ukimwi na kupata ushauri nasaha na pia imehakikisha kuwa zaidi ya watoto mayatima 280,000 na watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi na wale wanaowalea wanapata uangalizi na msaada wa huduma muhimu wanazohitaji.

Ujumbe wa al-Qaeda unaonyesha mpasuko baina vikundi vya jihadi




Mpiganaji wa al-Qaeda nchini Syria
Kikundi cha kigaidi cha al-Qaida kimetoa ujumbe mpya wa sauti ya kiongozi asiyetabirika ambaye analikosoa kundi la wapiganaji Jihadi wa Syria lijulikanalo kama Liberation of the Levant Organisation.
Kundi hilo pia linajulikana kwa jina jingine maarufu Hayat Tahrir al-Sham (HTS), na kiongozi wa al- Qaeda anawalaumu kwa kuwashambulia wapiginaji jihadi waandamizi wenye mafungamano na al-Qaeda huko Syria.
Katika sauti ya video hiyo ya dakika 35 “Ayman al-Zawahiri anasema na tupigane nao kwa msimamo moja, wakati akipinga uamuzi wa HTS kusitisha mafungamano rasmi na al-Qaeda 2016 na kutoweka ahadi yao ya mafungamano ya pamoja kama ni sehemu ya kikundi cha kigaidi ndani ya Syria. Sauti ya Amerika,VOA, haikuweza kuthibitisha ukweli wa video hiyo.
“Kwa nini upendo huu umepotea kati yetu na umerithiwa na migogoro, ukatili wa mioyo, njama za kuvunja kiapo chetu cha ushirikiano, na kuwadharau ndugu zetu na kutaka kuwaondoa nchini, kuwazuilia na hata kuwateka?
Al-Zawahiri amesema hayo alipokuwa anawahutubia viongozi wa HTS katika ujumbe wake, uliokuwa umeandikwa katika vyombo vya habari vya al-Qaeda vinavyofanyapropaganda vya al-Sahab Foundation Jumanne.
HTS ambayo mwanzoni ilikuwa inajiita al-Nusra Front, ilijibadilisha mwaka jana na baadae kuungana na vikundi kadhaa vidogo vya upinzani na kuunda umoja wao.
Ripoti iliyoandaliwa na Taasisi ya utafiti wa kivita wiki iliyopita imedai kuwa kikundi hicho imetumia fursa ya hatua ya jumuiya ya kimataifa kukishinda kikundi cha Islamic State kama ni nafasi ya kuongeza kwa kiwango kikubwa himaya yake upande wa Kusini mwa Syria, ikiimarisha udhibiti wa maeneo mengi ya kaskazini mashariki ya jimbo la Idlib.
Al-Zawahiri amesema yeye hakuidhinisha kujitoa kwa kikundi cha HTS kutoka katika mtandao wa al-Qaida. Anaelezea kuwa ni “kosa kubwa sana” walilofanya viongozi wa HTS kufanya ushirikiano wao naye kuwa siri kwa ajili ya kuepuka mashambulizi ya majeshi yanayoongozwa na Marekani.
Mnamo August, Michael Ratney, afisa wa ngazi ya juu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani ambaye anashughulikia sera ya Syria, amesema kikundi cha Nusra na viongozi wake watakuwa ni walengwa wa Washington hata kama watajibadilisha na kutumia majina mapya kwa ajili ya kuepuka mashambulizi ya majeshi ya Marekani na nchi nyingine yanayopambana kuutokomeza ugaidi katika eneo hilo.

Zimbabwe: Mnangagwa atangaza baraza jipya la mawaziri

Rais wa Zimbabwe Emmerson Mnangagwa ametangaza baraza lake jipya la mawaziri. Maafisa wakuu wa jeshi na makada wa chama tawala cha ZANU PF ndio wamepewa nafasi katika baraza hilo lenye mawaziri 22.

Simbabwe Emmerson Mnangagwa in Harare, 2014 (picture-alliance/AP Photo/T. Mukwazhi)
Wakosoaji  nchini Zimbabwe wanasema fungate fupi baada ya harusi imemalizika na ukweli wa mambo sasa unadhihirika, kilichotarajiwa ni kwamba Rais Emmerson Mnangagwa angelichanganya baraza lake, lakini kuna ishara chache mno za mabadiliko. Akizungumza na waandishi habari muda mfupi kabla baraza jipya la mawaziri kutangazwa, kiongozi mkuu wa upinzani Morgan Tsvangirai alisema Mnangagwa alikuwa na nafasi ya kuonyesha kuwa yeye ni tofauti na Mugabe lakini hapakuwepo na majadiliano yoyote baina yao na uongozi huo mpya.
Ishara haba za mabadiliko
Tsvangirai anasema hakuna mabadiliko hadi sasa na jambo ambalo linatia wasiwasi ni jinsi rais mpya alivyoanza. Tsvangirai amesema kuna wasiwasi juu ya msingi anaojaribu kuuweka rais huyo mpya wa Zimbabwe katika kuyashughulikia mambo na kutoa mpango madhubuti wa kufufua uchumi.
Morgan Tsvangirai kiongozi mkuu wa upinzani wa Zimbabwe (Getty Images)
Kiongozi mkuu wa upinzani wa Zimbabwe Morgan Tsvangirai
Mnangagwa amemchagua meja jenerali Sibusiso Moyo, kamanda wa jeshi ambaye wiki mbili zilizopita alitangaza kwenye televisheni hatua ya wanajeshi ya kuingilia kati baada ya nchi hiyo kukabiliwa na mkwamo wa kisiasa hatua ambayo hatimaye wiki iliyopita ilisababisha kuufikisha mwisho utawala wa kiongozi maarufu wa zamani wa nchini Zimbabwe Robert Mugabe. Rais huyo mpya pia amempa nafasi ya uwaziri wa ardhi na kilimo jemadari Perrance Shiri aliyehudumu kwa muda mrefu kwenye kikosi cha jeshi la anga la Zimbabwe.
Chinamasa arejea katika wizara ya fedha
Kulingana na taarifa zilizotolewa rais Mnangagwa hata hivyo amewabakisha mawaziri wachache kutoka kwenye baraza la zamani la aliyekuwa rais wa nchi hiyo Robert Mugabe miongoni mwao ikiwa ni Patrick Chinamasa ambaye amerudishwa kuhudumu kama waziri wa fedha, wizara aliyokuwa anaishikilia kabla ya kuondolewa wakati Mugabe alipofanya mabadiliko katika baraza la mawaziri manamo mwezi Oktoba.
Meja jenerali Sibusiso Moyo wa jeshi la Zimbabwe (Reuters/ZBC)
Meja jenerali Sibusiso Moyo
Chris Mutsvangwa kiongozi wa mashujaa katika harakati za ukombozi wa Zimbabwe za mwaka 1980 na aliyeongoza katika juhudi za kumlazimisha Mugabe aachie madaraka ndiye waziri mpya wa habari. Hata hivyo rais Mnangagwa hakuwajumuisha wapinzani katika baraza hilo la Mawaziri.
Wakili mmoja ambaye pia ni mkosoaji Alex Magaisa aliweka kwenye mtandao wake wa Tweeter picha ya rais wa zamani wa Zimbabwe Robert Mugabe na mkewe Grace wakiwa wanacheka pamoja na ujumbe wa maneno uliosema "pale walipoliona baraza la mawaziri”.
Biti: Kipindi cha fungate kimekwisha
Naye aliyekuwa zamani waziri wa fedha Tendai Biti ameandika ujumbe kwenye Tweeter uliosema kipindi cha fungate kimekwisha hata kabla hakijaanza na kumalizia kwa kusema "Ni aibu! Ni sawa na kupoteza nafasi adimu”.
Mnangagwa, mwenye umri wa miaka 75, aliapishwa Ijumaa iliyopita baada ya matukio makubwa katika nchi hiyoya kusini mwa Afrika pale jeshi lilipoidhibiti nchi ya Zimbabwe na kusema walitaka kuwakamata wahalifu katika serikali waliokuwa wanamzunguka Mugabe mwenye umri wa miaka 93.

Je ni nini lengo la Kim Jong Un wa Korea Kaskazini kwa Marekani?

Korea kaskazini inadai kuwa makombora yake yanaweza kufikia kila kona ya Marekani. Lakini je hilo ndilo analolitaka kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong Un?

Nordkorea Kim Jong-Un (Getty Images/AFP/STR)
Lengo lake pekee ni kudhibiti mamlaka yake madarakani, anasema, Jürgen Hanefeld anayeongoza ofisi ya mashariki mwa Asia ya kituo cha umma cha Ujerumani ARD huko mjini Tokyo nchini Japan. 
Miaka minne iliyopita wakati Kim Jong Un alipotangaza kwamba mpango wa makombora wa Korea Kaskazini utakamilishwa mwishoni mwa 2017, hakuna mtu aliyemsikiliza. Alichukuliwa kama ni mwenda wazimu au mtu asiyetabirika. Wengine walipuuza uwezo wake wa kutawala, wakijiuliza kwa muda gani angeweza kuwa mamlakani?
Na Kim alipotangaza kwamba Korea ya Kaskazini inaelekea kuwa na silaha za nyuklia miaka miwili baadaye, na kwamba alikuwa tayari kuongea na Marekani kuhusu upunguzaji wa silaha za kivita, kila mmoja alimcheka.
Hata hivyo, sasa vicheko vimepungua na kila mtu anapaswa kukabiliana na ukweli kwamba jamaa huyo anapaswa kuchukuliwa kwa uzito.
Siku ya kihistoria?
Jürgen Hanefeld (NDR/Christian Spielmann)
Jürgen Hanefeld anayeongoza ofisi ya mashariki mwa Asia ya kituo cha umma cha Ujerumani ARD huko Tokyo
Bila shaka hakuna mtu anayejua kama makombora yake yanaweza kuisambarisha miji ya New York au Washington, DC. Lakini je tunataka kujua kweli?
Je, si itakuwa jambo la maana zaidi kutathmini hatari badala ya kukubali? Kwa hatua hii hatuwezi kujua kama jaribio la kombora la Jumatano itakumbukwa kama siku ya kihistoria lakini inawezekana.
Korea Kaskazini imejitangaza yenyewe kuwa na nguvu za nyuklia! Hiyo sio maana tu ya tishio kubwa, pia inatoa fursa.
Kila mtu anajua kwamba hata kama makombora ya nyuklia ya Korea Kaskazini yanaweza kugonga mahali popote Marekani, wangeweza tu kufanya mara moja.
Baada ya hapo hapatakuwa na Pyongyang tena, wala Korea kwa jambo hilo - Kaskazini au Kusini.
Kwa hiyo Kim anataka nini? Anataka tu kujikinga. Anataka kudhibiti mamlaka yake madarakani. Na hiyo ndiyo sababu anataka kukutana na Marekani kama taifa lenye nguvu sambamba na Marekani.
Na sio Korea Kusini, nchi ambayo Marekani inaidhibiti angalau kijeshi.
Na sio na china ambayo imekuwa ikiiunga mkono na kusitasita ikizingatia maslahi yake ya kiuchumi na mikakati wa umuhimu wa eneo hilo kwa China.
Hapana, Kim dhidi ya Donald Trump ni mchezo ambao Korea Kaskazini inawekeza fedha zake.
Hii ni kuhusu amani
Mtu anaweza kudhani ni kiburi lakini inaonekana kwa mtamazo mwengine, hakuna njia nyingine mbadala.
Trump hana uwezo wa kufanya kitu chochote – haijalishi ndege ngapi za kivita anazituma na licha ya faida kubwa ya kijeshi ya nchi yake - isipokuwa kama yuko tayari kuiweka Korea Kusini hatarini na hatimaye kusababisha kitisho cha kutokea kwa vita vya dunia ya tatu.
Je si ingekuwa bora angeweka kando kiburi chake kama rais wa marekani angeketi chini na kuzungumza na Kim badala ya kutumia mtandao wa Twitter?
Haitokuwa mara ya kwanza kwamba rais wa Marekani anakaa chini na viongozi dikteta ili kuwashawishi wajirekebishe.
Mara nyingi mikutano hiyo na viongozi hao ni kuhusu mafuta, silaha au fedha. Wakati huu ni juu ya jambo muhimu zaidi: Amani.

Utafiti: Upara na nywele za kijivu ni ishara za magonjwa ya moyo

'Upara na nywele za kijivu ni ishara za magonjwa ya moyo'
Image caption'Upara na nywele za kijivu ni ishara za magonjwa ya moyo'
Wanaume wanaokuwa na upara kichwani mbali na wale wenye nywele za rangi ya kijivu wako katika hatari kubwa ya kupatikana na magonjwa ya moyo miongoni mwa wanaume walio chini ya umri wa miaka 40, utafiti unasema.
Utafiti uliofanyiwa zaidi ya vijana 2000 nchini India ulionyesha kuwa wengi waliokuwa na ugonjwa wa moyo walikuwa na upara na nywele za kijivu ikilinganishwa na wanaume walio na nywele kichwani.
Utafiti huo wa Idara ya magonjwa ya moyo barani Ulaya utasomwa katika kongamano la kila mwaka la magonjwa ya moyo nchini India.
Lakini wakfu wa Uingereza unaosimamia magonjwa ya moyo umesema kuwa sababu nyengine hatari pia ni muhimu.
Daktari Mike Knapton, aliambia BBC: Utafiti huu unasema kuwa miongoni mwa wanaume wenye upara na nywele za kijivu unaweza kuwagundua wale walio na hatari ya matatizo ya magonjwa ya moyo.
Hatahivyo hilo sio jambo ambalo linaweza kubadilishwa na watu, wakati ambapo unaweza kudhibiti hali ya maisha mbali na sababu zinzoweza kuhatarisha maisha kama vile viwango vya juu vya mafuta na shinikizo la damu.Hivi ni vitu muhimu zaidi kufuatilia.

Hawaii yafanyia jaribio king'ora cha kuonya shambulizi la nyuklia

A tsunami warning tower in between palm trees at Kakaako Waterfront Park in Honolulu, Hawaii, November 28, 2017Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionHawaii yafanyia jaribio king'ora cha kuonya kuhusu shambulizi la nyuklia
Kwa mara ya kwanza tangu kumalizika kwa vita baridi jimbo la Hawaii nchini Marekani limefanyia jaribio king'ora cha kuonya kuhusu shambulizi la nyuklia
Hatua hiyo ilichukuliwa baada ya jaribio la kombora la masafa marefu lililofanywa na Korea Kaskazini mapema wiki hii.
Hawai kawaida ina ving'ora ambavyo huonya kuhusu majanga ya asili kama tsunami.
Kingora cha nyuklia kina mlio tofauti ambacho huwaonya watu kusalia manyumbani wakisubiri ushauri zaidi.
Lakini king'ora hicho kilisikika tena Ijumaa na kitarudiwa klila jumatatu ya kwanza ya mwezi.
Kombora linalorushwa kutoka Korea Kaskazini linaweza kushambulia Hawaii ndani ya dakika 20 baada ya kufyatuliwa.
Hivi majuzi Korea ilifyatua kombora mpya la masafa marefu ambalo inadai kuwa linaweza kushambulia ndani ya Marekani.
Map locator
Image captionKombora linalorushwa kutoka Korea Kaskazini linaweza kushambulia Hawaii ndani ya dakika 20

Panya na mende ni tatizo Ikulu ya White house Marekani

Panya na mende ni tatizo kubwa katika ikulu ya Whotehouse nchini Marekani
Image captionPanya na mende ni tatizo kubwa katika ikulu ya Whotehouse nchini Marekani
Panya, mende, wadudu na vyoo vilivyovunjika ni miongoni mwa vitu vingi vilivyoripotiwa kwa wafanyikazi wa kufanya marekebisho katika ikulu ya Whitehouse nchini Marekani.
Ripoti ya vitu vinavyofaa kurekebishwa katika ikulu ya White house iliopatikana na chombo cha habari cha NBC Washington ilishirikisha ripoti nyengine ya mwaka uliopita kutoka kwa utawala wa rais Obama.
Panya wanadaiwa kuonekana katika chumba cha kulia cha maafisa wa jeshi la wanamaji.
Walionekana katika majengo, kulingana na Brian Miller, aliyekuwa inspekta jenerali wa kikosi cha huduma za jumla ambacho husimamia marekebisho katika jumba hilo la rais.
''Mtu yeyote kati yetu ambaye anamiliki nyumba ya zamani anajua kwamba inahitaji kazi nyingi''.
Mende walikuwa tatizo katika chumba cha kulia huku wadudu wakionekana katika nyumba anayoishi afisa mkuu wa jeshi kulingana na ripoti hiyo.
Wadudu na mende pia walionekana katika chumba cha wanahabari.
Mbali na kukabiliana na wadudu ,ripoti hiyo ya marekebisho ya Ikulu inaonyesha kazi nyingi zilizohitajika kufanyika baada ya utawala mpya kuingia mwanzoni mwa mwaka huu.

Wanaume wanaotoa talaka 3 'kwa mpigo' kufungwa jela India

Utamaduni unashirikisha mwanamume wa Kiislamu anayetamka talaka mara tatu kwa njia nyingi ikiwemo kupitia ujumbe ama barua pepe.Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionUtamaduni unashirikisha mwanamume wa Kiislamu anayetamka talaka mara tatu kwa njia nyingi ikiwemo kupitia ujumbe ama barua pepe.
Wanaume waliopo katika ndoa ambao hujaribu kutoa talaka ya 'hapo kwa hapo' huenda wakahukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela chini ya rasimu ya sheria zinazopendekezwa nchini India.
Utamaduni unashirikisha mwanamume wa Kiislamu anayetamka talaka mara tatu kwa njia nyingi ikiwemo kupitia ujumbe ama barua pepe.
Ilitangazwa kuwa kinyume na katiba na mahakama ya juu ya India mwezi Agosti lakini maafisa wanasema kuwa imetekelezwa tangu wakati huo.
Sheria hiyo pendekezi inatoa faini na usaidizi kwa wanawake walioathirika.
Muswada wenye sheria rasimu za kuwalinda wanawake sasa umetumwa kwa serikali za kijimbo kwa majadiliano.
Muswada huo utapiga maraufu italaka kwa mujibu wa hukumu ya mahakama ya juu na kutoa sheria za marupurupu mbali na usimamizi wa mwanamke aliyeathirika.
Sheria hizo zimewekwa ili kuhakikisha kuwa ''iwapo mume atamtaka mkewe kuondoka katika nyumba wawanayoishi basi atatoa ulinzi wa kisheria.
Chini ya sheria hiyo wale watakaopatikana na hatia hawataruhusiwa kuachiliwa kwa dhamana.
Vilevile watapiga marufuku sheria hiyo kwa njia yoyote ile ikiwemo kupitia maandishi ama ujumbe.

Trump kutambua Jerusalem ni mji mkuu wa Israel

Donald Trump kutambua Jerusalem kama mji mkuu wa Israel
Image captionDonald Trump kutambua Jerusalem kama mji mkuu wa Israel
Maafisa nchini Marekani wanasema kuwa Rais Trump anatarajiwa kutangaza wiki ijayo kuwa Marekani inatambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel hatua ambayo wakosoaji wanasema kuwa itachochea mzozo zaidi katika eneo hilo.
Hali kamili ya mji huo inakumbwa na utata huku pande zote mbili za Israel na Palestina zikidai kuwa ndio mji wao mkuu.
Trump alitoa ahadi ya kampeni ya kuhamisha ubalozi wa Marekani kutoka Tel Aviv hadi Jerusalem.
Mji wa Jerusalem
Image captionMji wa Jerusalem
Mwandishi wa BBC anasema kwa kutambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel, Trump anaashiria hatua ya kutekeleza ahadi yake ya kampeni.

RAIS WA ZANZIBAR DK SHEIN AHUDHURIA MAULID YA KUZALIWA MTUME MUHAMMAD SAW ZANZIBAR

MAKAMU wa Rais Mstaaf Dkt Mohammed Gharibi Bilal akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe.Ayoub Mohammed Mahmoud, wakati akiwasili katika viwanja vya maisara kuhuhudhuria sherehe za Maulid ya Kuzaliwa Mtume Muhammad SAW, yaliofanyika Kitaifa katika viwanja vya maisara Zanzibar
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Al hajj Ali Mohamed Shein, akisalimia na Mwenyekiti wa Kamati ya Maulid ya Mfungo Sita Zanzibar Sheikh Shirali Champsi alipowasili katika viwanja vya maisara Zanzibar kuhudhuria katika sherehe za Maulid ya kuzaliwa Mtume Muhammad (S.A.W)


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Al hajj Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Makamu wa Rais Mstaaf Dkt. Mohammed Gharib Bilal alipowasili katika viwanja vya maisara kuhudhuria Maulid ya Kuzaliwa Mtume Muhammad (S.A.W) yaliofanyika katika viwanja vya maisara Zanzibar.


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Al Hajj Ali Mohamed Shein, akiwa na Viongozi mbalimbali wa Dini na Serikali wakiwa wamesimama wakati wakutoa Salamu za kumkaribisha qaswida iliokuwa ikisomwa na Madrasatul E Itiswam ya Chukwani Zanzibar
MKE wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein akiwa na Wananchi na Viongozi wakisimama wakati wa kutoa salamu ya kumkaribisha Mgeni Rasmin Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Alhajj Ali Mohamed Shein alipowasili katika viwanja hivyo kuhudhuria Maulid ya Kuzaliwa Mtume Muhammad (S.A.W)


WANAFUNZI wa Madrasatul E’itiswam ya Chukwani Zanzibar wakisoma Qwasid ya Salamu ya kumkaribisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Al Hajj, Ali Mohamed Shein, katika viwanja vya maisra Zanzibar.


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Alhajj Ali Mohamed Shein, alkisoma ratiba ya hafla ya Maulid ya kuzaliwa Mtume Muhammad (S.A.W) yaliofanyika katika viwanja vya maisara kushoto Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi na kulia Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji.
KADHI Mkuu wa Zanibar Sheikh Khamis Haji akitowa maelezo kabla ya kuaza kwa hafla ya Maulid ya kuzaliwa Mtume Muhammad (S.A.W) yaliofanyika katika viwanja vya maisara Zanzibar
BAADHI ya waalikwa katika hafla ya Maulid ya kuzaliwa Mtume Muhammad (S.A.W) wakifuatilia hafla hiyo katika viwanja vya maisara Zanzibar.Picha na Ikulu

BALOZI SEIF IDDI MGENI RASMI BARAZA LA MAULIDI RUANGWA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mwenyekiti wa Wanawake Waislaam Tanzania, Shamim Khan baada ya kushiriki Katika Baraza la Maulidi ya Mtume Muhammad (S.A.W) kwenye uwanja wa Shule ya Msingi ya Likanglal wilayani Ruangwa Desemba 1, 2017.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwapungia washiriki wa Baraza la Maulidi ya Mtume Muhammad (S.A.W) baada ya kushiriki Baraza hilo kwenye uwanja wa Shukle ya Msingi Likangala wilayani Ruangwa Desemba 1, 2017.
Baadhi ya washiriki wa Baraza la Maulidi ya Mtume Muhammad (S.A.W) wakimsikiliza Mgeni Rasmi, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi wakati alipohutubia kwenye uwanja wa Shule ya Msingi ya Likangala wilayani Ruangwa Desemba 1, 2017
Mke wa Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa akisalimiana na Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhandisi Stella Manyanya (wapili kushoto) na kulia ni Mwenyekiti wa Wanawake Waislaam, Shamim Khan wakati alipowasili kwenye uwanja wa Shule ya Msingi ya Likangala kushiriki katika Baraza la Maulidi ya Mtume Muhammad (S. A.W). Mgeni Rasmi kaaika Baraza hilo alikuwa ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiongozana na Mgeni Rasmi katika Baraza la Maulidi ya Mtume Muhammad (S.A.W), Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi kuingia kwenye uwanja wa Shule ya Msingi ya Likangala wilayani Rungwa Desemba 1, 2017.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiteta na Mgeni Rasmi katika Baraza la Maulidi ya Mtume Muhammad (S.A.W),Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi kwenye uwanja wa Shule ya Msingi ya Likangala wilayani RUangwa Desemba 1, 2017.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza katika Baraza la Maulidi ya Mtume Muhammad (S.A.W) yaliyofanyika kwenye uwanja wa Shule ya Msingi ya Likangala wilayani Rungwa Desemba 1, 2017. Mgeni Rasmi katika Maulidi hayo alikuwa ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi.
Mke wa Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa (wapili kushoto) na baadhi ya Viongozi walioshiriki katika Baraza la Maulidi ya Mtume Muhammad (S.A.W) wakimsikiliza Mgeni Rasmi Balozi Seif Ali Iddi wakati alipiwahutubia kwenye uwanja wa Shule ya Msingi ya Likangala wilayani Ruangwa Desemba 1, 2017. Wengine kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Wanawake Waislaam Tanzania, Shamim Khan, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Ikupa Stella Alex , Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhandisi Stella Manyanya na Mbunge wa Viti Maalum,Hamida Muhammad Abdallah
Askofu Mkuu, Bruno Ngonyani wa Jimbo Katoliki la Lindi akizungumza katika Baraza la Maulidi ya Mtume Muhammad (S.A.W) yaliyofanyika kwenye uwanja wa Shule ya Msingi ya Likangala wilayani Ruangwa, Desemba 1, 2017.


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiteta na Mgeni Rasmi katika Baraza la Maulidi ya Mtume Muhammad (S.A.W),Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi kwenye uwanja wa Shule ya Msingi ya Likangala wilayani RUangwa Desemba 1, 2017. Kushoto ni Mufti Mkuu wa Tanzania, Abubacary Zubeiry Ally.


Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu