Thursday, August 17

Mamia ya watu wazikwa, Sierra Leone

Maeneo ya milimani ndio yaliyoathirika zaidiHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionMaeneo ya milimani ndio yaliyoathirika zaidi
Wiizara ya afya nchini Sierra Leone imesema takriban nusu ya maiti 400 zitokanazo na maporomoko ya udongo na mafuriko nje ya mji wa Freetown tayari zimezikwa.
Serikali ilisema mazishi ya pamoja yangeahirishwa hadi leo ili kutoa fursa kwa ndugu na jamaa kutambua miili ya maiti ya waathirika.
Lakini mkuu wa wataalamu wa magonjwa kutoka mjini Freetown ameiambia BBC kwamba baadhi ya mazishi yalikuwa yamefanyika.
Imefahamika kuwa mazishi hayo yamehusisha miili ambayo tayari ilitambuliwa au ilikuwa imeharibika kabisa.
Watu wapatao mia sita mpaka sasa bado hawajulikani walipo.
Rais wa Sierra Leone ametangaza siku saba za maombolezi.
Nathaniel Williams ni daktari katika hospitali kuu ya Connaught, iliyopo Freetown, anasema hivi sasa kuna tahadhari kubwa ya kutokea magonjwa ya milipuko kama vile kipindupindu.
Ameongeza kusema kuwa hivi sasa kunahitajika madawa na vyakula, kwa wale walioathirika.
Hata hivyo, Umoja wa Mataifa nchini humo umesema tayari umeweka mikakati ya kuweza kukabiliana na magonjwa ya milipuko iwapo yatatokea.

Trump azidi kukosolewa

Rais wa Marekani Donald TrumpHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionRais wa Marekani Donald Trump
Rais Donald Trump amezidi kukosolewa juu ya kusisitiza kwake kwamba pande zote ni za kulaumiwa kwa ghasia za mauaji baina ya waandamanaji wa mrengo wa kulia na wapinzani wao katika mji wa Charlottesville.
Viongozi wa masuala ya biashara wamejiuzulu kutoka majopo mawili ya ushauri kufuatia kauli hizo suala lililomfanya Trump atangaze kuwa bodi zote mbili zimefutwa.
Katika hatua nyingine, Makamu wa Rais wa Marekani Mike Pence ametetea hatua hiyo ya Trump, kwa kusema kuwa Rais huyo aliweka wazi kwamba tukio hilo ni janga.
Aidha akizungumza akiwa nchini Chile Pence ametangaza kukatiza ziara yake, America ya kusini, ili aweze kuungana na Rais Trump siku ya Ijumaa katika mkutano kujadili mikakati ya kiusalama, nchini Afghanistan na Asia kwa ujumla.

Bi Mugabe aomba kinga ya kidiplomasia dhidi ya kesi

Mugabe na mkewe
Image captionMugabe na mkewe
Serikali ya Zimbabwe imemuombea mkewe Mugabe kinga ya kidiplomasia dhidi ya kesi ya ushambuliaji inayomkabili nchini Afrika kusini , maafisa wa polisi wa taifa hilo wamesema.
''Grace Mugabe alikuwa bado yupo Afrika Kusini'' iliongezea wakipinga ripoti za awali kwamba alikuwa amerudi nchini Zimbabwe.
Mwanamitindo mwenye umri wa miaka 20 amemtuhumu bi Mugabe kwa kumshambulia katika hoteli moja mjini Johannesburg.
Polisi walitarajia kwamba bi Mugabe angejiwasilisha kwao mwenyewe siku ya Jumanne lakini hakufanya hivyo.
''Serikali ya Zimbabwe imewasilisha ombi la kumlinda kidiplomasia'', wizara hiyo ilisema katika taarafa yake.
Hatahivyo Afrika Kusini bado ilikuwa inataka kuhakikisha kuwa kinga hiyo amepatiwa kulingana na sheri, wizara hiyo iliongezea.
Mazungumzo yalikuwa yanaendelea na mawawikili wa Bi Mugabe na ubalozi wa Zimbabwe kuhusu swala hilo, ilisema taarifa.
Akizungumza mbele ya kamati ya bunge mapema, kaimu mkuu wa polisi Lesetja Mothiba alisema kuwa bi Mugabe ni shari aende mahakamni.
Mwanamitindo aliyepigwa na bi MugabeHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionMwanamitindo aliyepigwa na bi Mugabe
Hajatoa tamko lolote tangu maafisa wa polisi waanze kumchunguza kuhusu madai hayo ya unyanyasaji.
Serikali ya Afrika Kusini inakabiliwa na shutuma kali iwapo itamwachilia huru bi Mugabe.
Hilo lilitokea 2015 wakati iliposhindwa kumkamata na baadaye kumkabishi rais wa Sudan Omar el Bashir katika mahakama ya ICC.

Nyumba 1,300 kuondoka, CCM Kibamba yavunjwa

Tingatinga la Wakala wa Barabara Tanzania

Tingatinga la Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) likibomoa Ofisi ya CCM Kata ya Kibamba, Dar es Salaam jana. Picha na Ericky Boniphace 


Dar es Salaam. Bomoabomoa ni balaa. Imeelezwa kuwa bomoabomoa inayoendelea eneo la Mbezi hadi Kiluvya itazikumba zaidi ya nyumba 1,300 yakiwamo mahekalu ya vigogo, nyumba za ibada na vituo vya mafuta.
Ubomoaji huo ni wa kupisha hifadhi ya Barabara ya Morogoro inayoanzia Kimara hadi Kiluvya na nyumba zilizo umbali wa mita 121.5 kutoka katikati ya barabara kila upande, zitabomolewa.
Mmoja wa wasimamizi wa ubomoaji huo kutoka Tanroads ambaye hakutaka kutajwa gazetini alisema wanatarajia kubomoa nyumba zaidi 1,300, “Tayari tumebomoa nyumba zaidi ya 50 na tunaendelea kubomoa kwani zoezi hili ni endelevu na baadhi ya wananchi wanabomoa wenyewe.”
Msimamizi huyo pia alisema mbali na kubomoa nyumba pia wanawakamata wafanyabiashara wadogo, “Mpaka sasa tumekamata wafanyabiashara zaidi ya 1,000 na tunaendelea kuwakamata. Tunafanya hivi kwa sababu tulishawaambia waondoke katika maeneo haya, lakini wanaonekana kukaidi.”
Alisema wanapowakamata wanawapeleka polisi kwa hatua zaidi za kisheria na wengine hutozwa faini.
Akizungumzia kubomolewa kwa nyumba hizo Meneja wa Tanroads Mkoa wa Dar es Salaam, Julius Ndyamukama alisema walitoa notisi kwa nyumba zaidi ya 1,000 zitakazobomolewa katika eneo hilo.
Hali ilivyokuwa
Jana, mwandishi wetu alishuhudia Tanroads wakibomoa baadhi ya nyumba na kuwakamata wafanyabiashara hao na kubomoa baadhi ya majengo hayo yaliyo ndani ya hifadhi ya barabara ikiwamo Ofisi ya CCM Kibamba hali iliyozua taharuki.
Walianzia kwa Hassan Said eneo la Mbezi kwa Msuguri anayefyatua matofali na kubomoa visima viwili vya maji na banda la kuhifadhia vifaa.
Baba wa mmiliki wa eneo hilo, Yusuph Omari alisema hawakupewa taarifa kama wanakwenda kubomoa jana, “Tulishaambiwa tangu zamani tuondoe vitu lakini leo (jana) hawakutwambia kama wanakuja.”
Bomoabomoa hiyo ilihamia Mbezi Mwisho kwa wafanyabiashara ambao walikuwa wamepanga bidhaa zao katika eneo la hifadhi. Waliwakamata pamoja na kutwaa bidhaa zao na kuzipakia kwenye gari la polisi.
“Hawa wanapanga biashara barabarani kiasi ambacho kinaleta usumbufu kwa watembea kwa mguu. Tunawakamata ili kulinda usalama maana wanaweza kusababisha hatari barabarani,” alisema msimamizi wa bomoabomoa hiyo.
Wakati kazi hiyo ikiendelea, wananchi na baadhi ya wafanyabiashara hao walikuwa wakikimbia ovyo. Wapo walioacha vibanda vyao wazi na wengine wakijitahidi kuokoa mali zao kwa kubeba na kukimbia.
Baada ya hapo, safari iliendelea hadi Kibamba CCM. Hapo, kazi ya kubomoa baadhi ya majengo ikiwamo ofisi ya CCM Kata ya Kibamba ilianza.
Akizungumza kabla ya jengo hilo kubomolewa katibu wa chama hicho Kata ya Kibamba, Abdallah Yakub alisema ofisi hiyo haikuwapo ndani ya mita 60, bali sheria ya mita 121.5 ndiyo imewafuata, “Kwa kuwa wametufuata inabidi tulipwe. Awali, walisema watatulipa ila hatujui hadi sasa kama tunalipwa au la.”
Awali, Yakub alisema muda wa kubomolewa kwa jengo hilo waliopewa na Tanroads ulikuwa haujafika hivyo wasingeweza kuligusa jana lakini wakati akisema hayo, lilibomolewa mbele ya macho yake.
Wakati bomoabomoa ikiendelea Kibamba, wananchi walikuwa wakihaha kuhamisha vitu vyao huku wengine wakionyesha kukata tamaa ya maisha.
Mmoja wao, Mwamvita Njau alisema hawajui wanaelekea wapi kwani hawakutarajia kama nyumba yao ingebomolewa jana.
“Tunaishi kama wakimbizi, vitu vyetu vipo nje. Tungelipwa tungeenda kutafuta sehamu nyingine. Tunaomba Serikali ituangalie kwa jicho la huruma. Hatuna kosa, tuliishi hapa miaka mingi basi wangetwambia kwamba sehemu hizi hazitakiwi kujengwa.”
Pingamizi kuamriwa Agosti 30
Wakati bomoabomoa hiyo ikiendelea, hatima ya maombi ya wakazi wa Kimara Stop Over na Mbezi ya kibali cha kufungua kesi ya uwakilishi kupinga kubomolewa kwa nyumba zao kupisha upanuzi wa barabara ya Morogoro sasa itajulikana Agosti 30 Mahakama itakapotoa uamuzi wa pingamizi la Serikali.
Wakazi hao zaidi ya 200 wa Kimara Stop Over na Mbezi, wamefungua maombi Mahakama Kuu Divisheni ya Ardhi, wakiomba kibali cha kuwakilishwa na Ephrahim Kavishe na wenzake wanne kufungua kesi kupinga operesheni hiyo.
Hata hivyo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), ambaye ni mmoja wa wajibu maombi hayo amewawekea pingamizi, akiiomba Mahakama iyatupilie mbali maombi hayo huku akianisha kasoro mbalimbali za kisheria.
Jana baada ya mvutano wa hoja za kisheria kwa mawakili wa pande zote, Jaji Crencecia Makuru alipanga kutoa uamuzi wake dhidi ya pingamizi hilo Agosti 30, uamuzi ambao ndiyo utakaotoa hatima ya maombi hayo.
Kama mahakama hiyo itakubaliana na hoja za pingamizi hilo la Serikali, basi huenda ikayatupilia mbali maombi hayo, jambo ambalo litawafanya waanze upya mchakato wa kuomba kibali hicho kabla kufungua kesi ya msingi kupinga bomoabomoa hiyo.
Lakini ikiwa itakubaliana na majibu ya hoja za pingamizi hilo zilizotolewa na wakili waombaji hao na kutupilia mbali hoja za pingamizi la Serikali, mahakama itaanza kusikiliza maombi hayo ya uwakilishi, kisha kutoa uamuzi wa ama kuwakubalia au la.
Imeandikwa na Jackline Masinde, Asna Kaniki, James Magai na Hidaya Nyanga.

Waasi wa LRA wawateka watu 40 DR Congo

Mkuu wa LRA Joseph Kony
Image captionMkuu wa LRA Joseph Kony
Waasi wa kundi la LRA wamewateka takriban watu 10 na hadi 40 kutoka kijiji cha Kunu katika jimbo la kaskazini mashariki mwa DR Congo kulingana na kitengo cha habari cha AFP .
Kitengo hicho kilimnukuu afisa Dungu Christophe Ikando akisema walijitambulisha kuwa wale wa LRA.
''Tunashutumu utekaji wa watu 10 kutoka kijiji cha Kunu na watu waliojihami kwa bunduki ambao walijitambulisha kuwa waasi wa LRA''
Idhaa ya redio ya Umoja wa Mataifa inasema kuwa takriban watu 40 walitekwa ikiwemo maafisa wawili wa tume ya uchaguzi nchini humo.
Ettiene Akangiambe ambaye ni afisa mkuu wa tume hiyo ya CENI alitibitisha habari hizo.
''Maajenti wetu wawili ambao walikuwa wakirudi kutoka katika kituo cha kusajili wapiga kura walivamiwa na watu hao waliojihami''.
Amesema kuwa ajenti mmoja alifanikiwa kutoroka.
Waasi wa LRA wanekuwa wakifanya operesheni zao nchini Uganda, DR Congo na Jamhuri ya Afrika ya kati CAR na Sudan kwa miongo kadhaa lakini uwepo wao umepungua kufuatia operesheni za kieneo na zila za majeshi ya kimataifa.
Umoja wa mataifa unakadiria kwamba LRA limewaua takriban watu 100,000 na kuwateka watoto 60,000 tangu lianzishwe na Joseph Kony 1987.
Mnamo mwezi Mei , wanajeshi wa Uganda na wenzao wa Marekani walitangaza kwamba wanasitisha operesheni yao ya kumsaka Kony ambaye alipatikana na hatia ya uhalifu wa kivita 2005 na uhalifu dhidi ya binaadamu na mahakama ya kimataifa kuhusu uhalifu wa kivita ICC mjini The Hague.
Wasiwasi wa kisiasa umekuwa ukiongezeka DR Congo huku shinikizo za kumtaka rais Kabila kuandaa uchaguzi mkuu zikiendelea.
Muda wake wa kutawala ulikamilika mwezi Disemba mwaka uliopita na makubaliano ya kuandaa uchaguzi mwengine mwishoni mwa 2017 yaliafikiwa.

Pogba amhurumia Neymar kelele za mashabiki asipofunga mabao



England. Mshambuliaji wa Manchester United, Paul Pogba (24) amesema msimu uliopita alipata kashikashiyamashabikikutokananakilamtuakimhusishana thamani yake ya usajili na kiwango cha uwanjani.
Pogba alisema sasa mzigo huo ameupokea Neymar ambaye anashikilia rekodi ya mchezaji ghari kusajiliwa na PSG kwa thamani ya Pauni 198 milionimsimuwa 2017/18.
Neymar alikuwa Paris Ufaransa ambako mashabiki wa PSG walijumuika kushehekea uhamisho wake,hukua kitumia nafasihiyokupiga mpira kwenyekiti maalumu alichoandaliwa,ambapo fedha zitakazopatikana kwenye sherehe hiyo zitatumika kuwasaidia waathirikawa mafuriko SieraLione.

Waasi wa LRA wawateka watu 40 DR Congo

Mkuu wa LRA Joseph Kony
Image captionMkuu wa LRA Joseph Kony
Waasi wa kundi la LRA wamewateka takriban watu 10 na hadi 40 kutoka kijiji cha Kunu katika jimbo la kaskazini mashariki mwa DR Congo kulingana na kitengo cha habari cha AFP .
Kitengo hicho kilimnukuu afisa Dungu Christophe Ikando akisema walijitambulisha kuwa wale wa LRA.
''Tunashutumu utekaji wa watu 10 kutoka kijiji cha Kunu na watu waliojihami kwa bunduki ambao walijitambulisha kuwa waasi wa LRA''
Idhaa ya redio ya Umoja wa Mataifa inasema kuwa takriban watu 40 walitekwa ikiwemo maafisa wawili wa tume ya uchaguzi nchini humo.
Ettiene Akangiambe ambaye ni afisa mkuu wa tume hiyo ya CENI alitibitisha habari hizo.
''Maajenti wetu wawili ambao walikuwa wakirudi kutoka katika kituo cha kusajili wapiga kura walivamiwa na watu hao waliojihami''.
Amesema kuwa ajenti mmoja alifanikiwa kutoroka.
Waasi wa LRA wanekuwa wakifanya operesheni zao nchini Uganda, DR Congo na Jamhuri ya Afrika ya kati CAR na Sudan kwa miongo kadhaa lakini uwepo wao umepungua kufuatia operesheni za kieneo na zila za majeshi ya kimataifa.
Umoja wa mataifa unakadiria kwamba LRA limewaua takriban watu 100,000 na kuwateka watoto 60,000 tangu lianzishwe na Joseph Kony 1987.
Mnamo mwezi Mei , wanajeshi wa Uganda na wenzao wa Marekani walitangaza kwamba wanasitisha operesheni yao ya kumsaka Kony ambaye alipatikana na hatia ya uhalifu wa kivita 2005 na uhalifu dhidi ya binaadamu na mahakama ya kimataifa kuhusu uhalifu wa kivita ICC mjini The Hague.
Wasiwasi wa kisiasa umekuwa ukiongezeka DR Congo huku shinikizo za kumtaka rais Kabila kuandaa uchaguzi mkuu zikiendelea.
Muda wake wa kutawala ulikamilika mwezi Disemba mwaka uliopita na makubaliano ya kuandaa uchaguzi mwengine mwishoni mwa 2017 yaliafikiwa.

Watoto wa Lucky Vincent kurejea nyumbani kesho

Balozi wa Tanzania nchini Marekani Wilson

Balozi wa Tanzania nchini Marekani Wilson Masilingi akiwa na watoto Sadia, Doreen na Wilson pamoja na mama zao mjini Sioux City, Iowa nchini Marekani jana. Watoto hao ambao ni manusura wa ajali ya basi Shule ya Lucky Vincent ya jijini Arusha lililopoteza maisha ya wanafunzi 32, walimu wawili na pamoja na dereva wa basi hilo Mei 6 na kupelekwa nchini Marekani na Shirika la Samaritan Purse kwa matibabu wanatarajiwa kurudi nchini Ijumaa asubuhi kupitia Uwanja wa KIA . Picha na Mpiga Picha maalum 
Arusha. Wanafunzi watatu wa Shule ya Msingi Lucky Vincent ya jijini hapa waliopelekwa Marekani kwa matibabu baada ya kuumia katika ajali iliyotokea Mei mwaka huu wanatarajiwa kurejea nchini kesho, lakini moja wa wazazi wao ameshauri wangeendelea kubaki huko kupewa matibabu.
Baba mzazi wa Doreen, Elibariki Mshana alisema anaamini mtoto wake atakuwa katika hali nzuri zaidi, lakini kwa namna anavyoona picha zake anazopata, anaona kwamba ingekuwa bora kama angeendelea kupata matibabu huko.
Doreen na wenzake wawili, Sadia Awadh na Wilson Tarimo, walinusurika katika ajali mbaya ya basi iliyosababisha vifo vya wanafunzi wenzao 32, walimu wawili na dereva mmoja iliyotokea Mei 6 katika eneo la Mlima Rhotia wilayani Karatu.
Mbunge wa Singida Kaskazini ambaye pia ni mwenyekiti mwenza wa taasisi ya Siouxland Tanzania Educational Ministries (Stemm), Lazaro Nyalandu alisema jana kuwa Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuongoza mapokezi hayo kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).
Wanafunzi hao walipelekwa Marekani Mei 14 kwa ajili ya matibabu yaliyoratibiwa Stemm kwa kushirikiana na shirika la ndege la Samaritan Purse linaloongozwa na Mchungaji Franklin Graham wa Marekani ukiwa ni msaada wa taasisi yake kwa Watanzania.
Wamekuwa wakipata matibabu katika mji wa Sioux, Jimbo la Iowa na baadaye Doreen alihamishiwa katika kituo cha Madona, kilichopo katika Jimbo la Nebraska kwa ajili ya mazoezi zaidi kutoka kwa wataalamu wa uti wa mgongo.
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Nyalandu jana, ndege itakayowarudisha watoto hao ambao wameambatana na wazazi wao watatu, daktari bingwa Elias Mashala na muuguzi kutoka Hospitali ya Mount Meru, itawasili saa tatu asubuhi.
Mara baada ya kutua kwenye uwanjani wataelekea katika eneo maalumu lililotengwa kwa ajili ya familia za watoto hao pamoja wa wageni wachache kutoka katika Kijiji cha Mbuguni, Wilaya ya Arumeru (STEMM Village) ambako mjumbe wa Bunge la Congress la Marekani, Steve King na mke wake watahudhuria.
Nyalandu ambaye tangu watoto hao wakiwa Marekani amekuwa akituma taarifa za maendeleo yao kupitia mtandao wa Facebook, jana pia aliandika ujio wao kwenye ukurasa wake huo akiwaomba wananchi kujitokeza kuwapokea.

Usain Bolt aitwa kujiunga timu ya soka Burton Albion


England. Mwanariadha Usain Bolt amepewa ofa kujiunga na klabu ya Ligi Daraja la Kwanza England ya Burton Albion, baada ya kutangaza kustaafu akiwa kwenye mashindano ya Riadha ya Dunia yaliyomalizika London wiki iliyopita Jumapili.

Usain Bolt amestaafu riadha, huku akifanya vibaya kwenye mbio za miata 100 na 400 alizokimbia kwenye mashindano hayo.
Kocha wa Burton, Nigel Clough amesema anafahamu rekodi ya mwanariadha huyo ambaye amewahi kucheza soka wakati akiwa mdogo hivyo amempa muda wa kutafakari kuhusu ofa ya kujiunga na klabu hiyo.

Mawakili wazungu wakwamisha dhamana ya Bilionea wa IPTL

Mshitakiwa Sethi akitoka mahakamani kusikiliza
Mshitakiwa Sethi akitoka mahakamani kusikiliza kesi inayomkabili. Picha ya Maktaba 
Dar es Salaam. Mawakili kutoka nje ya nchi wanaomtetea bilionea wa kampuni ya kufua umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), Harbinder Singh Sethi, kuhusu kupewa dhamana, jana walikwamisha usikilizwaji wa maombi hayo.
Bilionea huyo na mwenzake James Rugemalira, wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi wakidaiwa kuchota mabilioni ya fedha kutoka katika Akaunti ya Tegeta Escrow ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), isivyo halali.
Pia, wanakabiliwa na mashtaka ya utakatishaji fedha ambayo ni miongoni mwa mashtaka yasiyo na dhamana, lakini washtakiwa, kila mmoja kwa wakati wake wameamua kusaka dhamana katika Divisheni ya Makosa ya Uhujumu Uchumi na Rushwa, maarufu kama Mahakama ya Mafisadi.
Hata hivyo, Mkurugenzi wa Mashtaka amemuwekea pingamizi bilionea huyo katika maombi yake hayo, ambalo lilipangwa kusikilizwa jana na Jaji Winfrida Korosso, lakini usikilizwaji wa pingamizi hilo ulikwama baada ya bilionea huyo kuamua kuyaondoa mahakamani maombi hayo.
Seth aliamau kuyaondoa mahakamani maombi hayo kutokana na kuhusisha mawakili kutoka nchini Afrika Kusini, ambao aliwakodi kuongeza nguvu kwa kushirikiana na mawakili wazawa kumpigania katika dhamana yake hiyo.
Maombi ya kuyaondoa maombi hayo mahakamani yalitolewa na kiongozi wa jopo la mawakili wanaomtetea bilionea huyo, Melkizedeck Lutema, baada ya kubainika mawakili hao wa nje hawakuwa na sifa za kufanya kazi nchini.
Ingawa mawakili hao walikuwa hawajatambulishwa mahakamani, lakini katika nyaraka mbalimbali zinazohusiana na maombi hayo, wametajwa kuwa miongoni mwa mawakili wake.
Kutokana na kasoro hiyo Wakili Lutema aliiomba mahakama iyaondoe maombi hayo kwa lengo la kuanza upya mchakato wa kuyawasilisha mombi ambalo mahakama iliridhia.
Wakili wa Serikali Mkuu, Dk Zainabu Mango, alisema mawakili hao hawana cheti cha kufanya kazi katika mahakama za hapa nchini kutoka kwa Jaji Mkuu.
Wakili Mango alisema kuwa ili wakili kutoka nje ya nchi aruhusiwe kufanya kazi katika mahakama za ndani ni lazima aombe kibali kutoka kwa Jaji Mkuu ambacho analazimika pia kukilipia, jambo ambalo mawakili hao hawakuwa wamelifanya.
Seth na Rugemalira wanakabiliwa na kesi hiyo ya uhujumu uchumi yenye jumla ya mashtaka 12 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kwa mujibu wa sheria za Tanzania mashtaka hayo hayana dhamana na hadi sasa washtakiwa wanasota mahabusu.

Zitto adai ahadi ya kuleta bombadier mpya yayeyuka


Dar es Salaam. Ahadi ya Serikali ya kununua ndege ya tatu ambayo ilitakiwa kufika nchini Julai, imeshindwa kutekelezwa hadi sasa na Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe amehoji kulikoni.
Mwaka jana, Serikali ilinunua ndege mbili aina ya bombadier na kuzikabidhi kwa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) kwa ajili ya uendeshaji.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa na Naibu wake, Mhandisi Edwin Ngonyani kwa nyakati tofauti walikaririwa wakisema ndege hiyo itawasili Julai na kufanya idadi ya ndege za ATCL kuwa nne.
Hata hivyo, Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe katika ukurasa wake wa Twitter jana alimuliza Profesa Mbarawa kuhusu ndege hiyo.
“Serikali iliahidi bungeni kuwa Julai 2017 mtapokea ndege nyingine ya Bombadier, leo ni Agosti iko wapi, lini itafika, nini kimetokea,” aliuliza Zitto
Profesa Mbarawa alimjibu kuwa “ni kweli kabisa ahadi ilikuwa Julai kuna taratibu za mwisho zinafanywa kabla ya kuwasili hivyo itawasili tu.”
Baada ya majibu hayo, Zitto alitaka kufahamu kutoka kwa Profesa Mbarawa ni lini ndege hiyo itawasili.
“Sababu za kuchelewa ni nini, delay (kuchelewa) ya mwezi mzima siyo dalili nzuri ndugu waziri, ni kwa sababu hamjalipa au zimezuiwa na wanaotudai,” aliuliza Zitto.
Alipopigiwa simu ili azungumzia suala hilo, Profesa Mbarawa hakupatikana lakini Naibu wake, Mhandisi Ngonyani alitaka aachwe ili atafute taarifa halisi za ndege hiyo.

Kilichojificha nyuma ya mabango ziara za viongozi

Rais John Magufuli, akisoma mabango yenye
Rais John Magufuli, akisoma mabango yenye ujumbe mbalimbali  wakati wa mkutano wake wa hadhara uliofanyika Julay 22, kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma. 


Dar es Salaam. Mapema wiki hii, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alitaka wananchi wanaokwenda kwenye mikutano ya hadhara wakiwa wamebeba mabango, wasizuiwe na badala yake waachiwe wayanyooshe ili kueleza hisia zao.
Alisema hayo wakati kukiwa na ongezeko kubwa la wananchi kuibuka na mabango, hasa kwenye ziara za Rais John Magufuli, ambaye amekuwa akiyasoma hadharani na wakati mwingine kuagiza yapigwe picha ili ayasome baadaye na kuyafanyia kazi.
Kasi hiyo ya kuongezeka kwa mabango ilikuwa kubwa wakati Rais alipokuwa katika ziara ya mikoa ya Kanda ya Magharibi, kiasi cha kuonekana kama vurugu mkoani Kigoma na mikutano iliyofuata mkoani Tabora, Rais aliwataka wasiyaonyeshe.
Na wakati fulani alisema, “hayo mabango yenu mkatandike kwenye vitanda vya wake zenu,” wakati walipoyanyoosha katika moja ya mikutano yake mkoani Tabora.
Vitendo hivyo vinaelezewa na wachambuzi wa siasa kuwa vinatokana na ama wananchi kutopata fursa ya kutoa maoni yao, au watendaji kutowajibika ipasavyo au tabia ya Rais Magufuli kuchukua hatua papo hapo.
“Kubanwa kwa demokrasia, kama kuzuia mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa kumewakosesha wananchi fursa kutoa maoni yao,” alisema Profesa Gaudence Mpangala wa Chuo Kikuu cha Ruaha (Rucu).
“Huko nyuma, wananchi walipata fursa ya kutoa maoni yao, ingawa sasa utawala huu umeonyesha nia ya kutatua kero, kama alivyotoa ardhi kwa wananchi huko Tanga.
“Watu wamekosa fursa ya kutoa maoni yao katika mikutano ya hadhara, maandamano na makongamano, ndiyo maana wanapopata nafasi kama hiyo wanajitokeza kwa wingi.”
Alisema kutokuwapo kwa mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa, kumewafanya wananchi kukosa fursa ya kutoa maoni na kero zao.
Hata hivyo, Profesa Mpangala alisema kitendo cha Rais kutatua matatizo ya wananchi pale anapoyasikia kinaweza pia kusababisha hali hiyo kuzidi kuongezeka. “Kero za wananchi zipo kwa muda mrefu na hiyo imetokana na kipindi cha ubepari mamboleo tangu miaka ya tisini ambako vitendo vya rushwa na ufisadi na kutolindwa kwa haki za watu vilikithiri,” alisema Profesa Mpangala.
“Rais Magufuli ameonyesha dhamira ya kupambana na madhambi hayo ndiyo maana wananchi wanamfuata na mabango yao.”
Serikali ilipiga marufuku mikutano ya hadhara na ya ndani mwaka jana, kabla ya kuruhusu mikutano ya wabunge, ikizuia wabunge kutoka maeneo mengine kuhudhuria nje ya majimbo yao.
Wananchi hunyoosha juu kwa bidii mabango hayo wakati viongozi wa juu wa Serikali wanapohutubia na huonekana kuwabughudhi au kutibua mtiririko wa hotuba zao, ambazo hulenga kueleza mikakati ya Serikali na mafanikio yaliyokwishapatikana.
Akiwa kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma Julai 23, idadi ya wananchi waliovamia sehemu ya kati ya uwanja kujaribu kumkaribia Rais ili aone ujumbe wao ilikuwa kubwa.
Kitendo hicho kiliwafanya askari wakimbilie kuwazuia wasizidi kusogelea jukwaa, lakini Rais akawataka askari waachie wayanyooshe juu na yeye kushuka jukwaani kwenda kuyasoma.
Baadhi yalizungumzia kuhusu migogoro ya ardhi, mirathi, kubambikiwa kesi, bomoabomoa, kutolipwa fidia na kunyang’anywa mashamba.
Baada ya kuyasoma, Rais aliwaambia wananchi hao kuwa atayashughulikia, lakini akasema mengine ni kutokana na kufuata sheria.
“Kama ubomoaji nyumba, hata mimi nabomoa kama umejenga kinyume cha sheria,” alisema Rais siku hiyo.
Hakurudia kuyasoma katika mikutano iliyofuata mkoani Tabora zaidi ya kuwahimiza wananchi wayashushe.
Hata hivyo, akiwa mkoani Tanga, Rais Magufuli alionyesha kukerwa na baadhi ya mabango yaliyolalamikia mishahara midogo wanayolipwa katika maeneo yao ya kazi, alipokuwa akizungumza na wakazi wa Kata ya Pongwe wakati akielekea Chongoleani kwa ajili ya uwekaji wa jiwe la msingi la mradi mkubwa wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Uganda.
“Ndugu zangu niwaambie, mimi si mpole kiasi hicho, kama mnavyofikiria. Nasema kama mnaona mshahara ni mdogo, acheni kazi nendeni mkalime,” alisema Rais.
Matumizi ya mabango pia yameonyesha wananchi kutafuta suluhisho la kero zao sugu wakiamini kuwa viongozi hao ndiyo pekee wanaoweza kuwasaidia.
Hali kama hiyo pia ilitokea Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa wilayani Sikonge, Tabora ambako alitaka wananchi waruhusiwe kuyaonyesha baada ya kuona askari wanawazuia.
“Siku nyingine msirudie na kuanzia sasa waacheni wananchi waonyeshe mabango yao kwa kuwa ndiyo njia wanayotumia kuonyesha hisia zao kwa yale wanayokumbana nayo na kuwasababishia kero,” alisema Majaliwa.
Mabango siyo tu yamekuwa yakitumika kwa viongozi hao wa juu, bali hata kwa viongozi wengine kama ilivyokuwa kwa wajumbe wa Kamati Maalumu ya Bunge inayochunguza madini ya Tanzanite ilipofika Mererani katika machimbo hayo.
Moja ya mabango ambayo wananchi walibeba ni lile lililosema “Tuko tayari kulipa kodi kumsaidia Rais lakini tuangaliwe.”
Akizungumzia suala hilo mhadhiri mwandamizi wa sayansi ya Siasa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Alexander Makulilo alisema wananchi wengi wanamuona Rais kama tegemeo lao baada ya kukosa misaada wanayoitarajia kutoka kwa watendaji wa ngazi za chini.
“Rais kajipambanua kusaidia tabaka la watu wa chini na tabaka hilo linatambua hivyo. Kwa mantiki hiyo linachukua fursa hii ili kutatuliwa matatizo yao,” alisema Dk Makulilo.
“Watendaji wa ngazi za chini wameshindwa kuwasikiliza na kutoa ufumbuzi madhubuti kwa matatizo ya tabaka la chini. Hivyo tabaka hili linamuona Rais kama mkombozi wa wanyonge.
“Awamu ya tano na hususani, Rais amekuwa akitoa ufumbuzi wa haraka kwa matatizo. Rais hapendi kusikia lugha ya michakato.”

Rais wa Jamhuri ya Guinea Bissau ameahidi nchi yake itaridhia itifaki


Raisi wa Mahakama akitambulisha Jaji Matusse kwa Raisi was Guinea Bissau Ikulu. Kushoto wa pili ni Makamu wa Raisi wa Mahakama Jaji Ben Kioko.

 Rais wa Jamhuri ya Guinea Bissau Mheshimiwa Jose Mario Vaz ameahidi kuwa, nchi yake itaridhia itifaki iliyoanzisha mahakama ya Afrika ya haki za  binadamu na watu (AfCHPR) mapema iwezekanavyo .

Akizungumza na ujumbe wa mahakama hiyo ulioko katika ziara ya kikazi nchini Guinea Bissau, Rais Vaz alisema hatua hiyo inatokana na ukweli kwamba Guinea Bissau ilikuwa miongoni mwa nchi za mwanzo za umoja wa Afrika kutia saini itifaki iliyoanzisha AfCHPR mwaka 1998.

Katika mazungumzo yake na ujumbe huo ulioongozwa na rais wa AfCHPR mheshimiwa Jaji Sylvain Ore kiongozi huyo wa Guinea Bissau alielezea kuridhishwa kwake na madhumuni ya kuanzishwa kwa mahakama ya Afrika ya haki za binadamu na watu na kuongeza kuwa masuala ya haki za binadamu yana umuhimu mkubwa katika kufikiwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika nchi za Afrika na kuwaondoa wananchi wake katika lindi la umaskini na ufukara.

“Ahadi yangu ni kuhakikisha kuwepo kwa haki za binadamu katika nchi yangu” alisisitiza Rais Vaz.

Ujumbe wa AfCHPR pia ulikutana na waziri mkuu wa Guinea Bissau Mheshimiwa Umario Sissoco Embalo ambaye alisema mamlaka husika za nchi yake zitaandaa nyaraka zinazohitajika ili kuzipeleka katika bunge la taifa nchini humo kwa lengo la kuridhia itifaki iliyoanzisha mahakama ya Afrika ya haki za binadamu na watu.

“Mimi ni muumini mkubwa wa umajumui wa Afrika (Pan-Africanism) na nitafanya kila linalowezekana kuimarisha taasisi za umoja wa afrika” alisisitiza waziri mkuu huyo.

Rais wa AfCHPR jaji Ore na ujumbe wake ambao umejumuisha Makamu wa rais wa mahakama hiyo Mheshimiwa Jaji Ben Kioko, Mheshimwa Jaji Angelo Matusse na baadhi ya maafisa wa ofisi ya msajili wa AfCHPR pia ulikutana na Jaji Mkuu, waziri wa masuala ya jamii na pia kamisheni ya haki za binadamu ya Guinea Bissau.

Jaji Ore alisema ilikufanikisha malengo ya mahakama na pia kuimarisha mfumo wa haki za binadamu barani Afrika nchi nyingi za umoja wa afrika hazina budi kuridhia itifaki iliyounda AfCHPR kwa mujibu wa kifungu cha 34(6) na kutoa tako rasmi la kutambua na kukubali a mamlaka ya mahakama kuweza kupokea kesi za watu binafsi na mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs)

Hadi sasa ni Nchi 30 tu kati ya nchi 55 wanachama wa AU ndio zimeridhia itifaki husika.

AfCHPR yenye makao yake makuu jijini Arusha iko nchini Guinea Bissau kwa ziara ya kikazi ya siku 2 ili kukutana na viongozi na wadau mbalimbali kwa lengo la kuitangaza mahakama hiyo.

Wednesday, August 16

MRADI WENYE FURSA KEDEKEDE WATANZANIA WANAPASWA KUZICHANGAMKIA



Hivi Karibuni, Rais wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli na Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda kwa pamoja waliweka jiwe la msingi la Ujenzi wa Bomba la Mafuta Ghafi kutoka Hoima nchini Uganda hadi Tanga Tanzania. Katika Makala hii pamoja na mambo mengine Mwandishi Said Ameir wa Idara ya Habari- MAELEZO anaeleza kwani nini mradi huu ni kipimo cha utayari na ujasiri wa watanzania katika kuchangamkia fursa.

Mradi huu unaojulikana kama Mradi wa Bomba la Kusafirisha Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) unatekelezwa kwa ubia kati ya washirika wa sekta binafsi na sekta za umma za nchi za Tanzania na Uganda.

Washirika hao ni Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Kampuni ya Taifa ya Petroli ya Uganda (UNOC), Kampuni ya Mafuta ya Total ya Ufaransa, Kampuni ya TULLOW yenye makao makuu yake London nchini Uingereza na Kampuni ya China National Offshore Oil Company (CNOOC).

Bomba ambalo litagharimu dola za kimarekani 3.5 bilioni, sehemu yake kubwa yaani kilomita 1,115 kati ya kilomita 1,445 litajengwa katika ardhi ya Tanzania na kupita mikoa 8, wilaya 24 na vijiji 184.

Kutokana na hali hiyo, inaelezwa kuwa, mradi huu wakati wa ujenzi na utakapokamilika, utatoa na fursa nyingi za kiuchumi ambazo zitasaidia sana kuchangamsha shughuli za kiuchumi hivyo kuchangia ukuaji uchumi na kuinua kiwango cha maisha ya watanzania kwa namna mbalimbali.

Mradi huu ni mfano wa ushirikiano kati ya nchi za Tanzania na Uganda na kwa upande mwingine ni mfano mzuri wa ushirikiano kati ya sekta binafsi na sekta za umma katika nchi hizi. 
Katika hatua mbalimbali za utekelezaji wake, mradi huu utahitaji ushiriki wa sekta binafsi katika nchi zote mbili na wakati mwingine hata taasisi nyingine za umma ambazo zinatoa huduma zitakazohitajika na mradi.

Kwa hiyo, wakati tukisifia kuwa ni mfano wa mradi wa ubia wa sekta ya umma na sekta binafsi katika nchi zetu, watanzania hawana budi kuelewa kuwa wana wajibu mkubwa wa kuzitumia vyema fursa za mradi huu.

Kwa Tanzania, mradi huu unaweza kuonesha picha halisi ya ushirikiano wa sekta hizo kwa kuzingatia namna makampuni na taasisi za humu nchini zitakavyoweza kushiriki na kufanikisha mradi huu.

Kwa maana nyingie ni mradi ambao unaweza kutumika kupima utayari, umakini, uwezo na ujasiri wa watanzania katika kuchangamkia fursa za kiuchumi.

Kama alivyoeleza Rais Magufuli wakati wa sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi kuwa katika mradi huu, Serikali imesamehe mambo mengi ili uweze kutekelezwa kwa kuishirikisha Tanzania. Wataalamu wa nchi walichambua na kupembua hadi kubaini kuwa kusamehe huko kutafidiwa na fursa nyingi zitakazoletwa na mradi huu.

Kwa maana hiyo bila ya watanzania kuchukua hatua madhubuti za kuhakikisha wanazitumia kadri itakavyowezekana fursa hizo uamuzi huo wa Serikali kusamehe hivyo ilivyovisamehe hautakuwa na maana yeyote.

Kuja kwa mradi huu Tanzania, watanzania hawana budi kuipongeza Serikali chini ya Rais John Pombe Magufuli kwa jitihada kubwa kwa kutumia ushawishi wa kisiasa, kidiplomasia, uchumi na ukaribu wa viongozi wa nchi hizo mbili pamoja na hoja nyingine hadi kufanikisha mradi huu kuja Tanzania.

Jitihada hizi ni kielelezo cha dhamira ya kweli iliyonayo Serikali ya Awamu ya Tano ya kutafuta kila aina ya fursa za kiuchumi ambazo zitasaidia kutimiza ahadi zake kwa watanzania ya kujenga Tanzania yenye uchumi imara.

Serikali imejitwika mzigo mkubwa wa kushiriki katika kutekeleza mradi huu mkubwa wa aina yake lakini imefanya hivyo kwa kuamini kuwa watanzania wako tayari na wako imara kuupokea kwa hali na mali.

Imeelezwa mara kwa mara kuwa mradi huu utaliingizia taifa mapato makubwa, utaleta tekinolojia na utalaamu na fursa za kiuchumi ambazo watekelezaji wake kwa kiwango kikubwa ni kutoka sekta binafsi. Kwa mnasaba huo, Serikali hapa imefanya zaidi ya wajibu wake ambao ni wa kujenga mazingira mazuri ya kuvutia uwekezaji.

Wale wahenga wa Cambrigde walisema“give us the tools and lets finish the job” na hivi ndivyo ilivyofanya Serikali kwa mradi huu. Imeleta mradi na kufungua fursa tele ambazo watanzania wanapaswa kuzitumia kujenga kiuchumi wao binafsi na uchumi wa taifa.

Haitakuwa na maana hata kidogo katika ngazi ya serikali na katika ngazi ya Mtanzania mmoja mmoja kufika wakati fursa za mradi huu kuchukuliwa na wageni kwa sababu zozote na katika mazingira yeyote yale. Ikifikia hatua hiyo watanzania watakuwa wamewaangusha viongozi wao.

Hii kutokana na mazingira ambayo Serikali imeyaweka kuwawezesha watanzania kushiriki katika sekta ya mafuta na gesi asilia. Mbali ya kupitisha Sheria ya Local Content Act ya 2015 ambayo inasisitiza ushiriki wa watanzania lakini zaidi dhamira ya kweli ya kisiasa iliyonayo uongozi wa Serikali ya kuhakikisha kuwa watanzania wanafaidika ipasavyo na mradi huu.

Ni jambo la kutia moyo kuona kuwa baadhi ya Taasisi za Serikali na za sekta binafsi zimeshaanza maandalizi au zimejitokeza kuwaandaa watanzania kuchangamkia fursa hizo na kuhakikisha wanazitumia vyema.

Miongoni mwa taasisi hizo ni Jumuiya ya Watoa Huduma katika Sekta ya Mafuta na Gesi (ATOGS) ambayo inawakusanya pamoja watoa huduma katika sekta hiyo ambapo lengo lake kubwa ni kuhakikisha kuwa fursa za mradi huo zinatumika ipasavyo kwa manufaa ya muda mfupo na mrefu ya watanzania.

ATOGS, kama taasisi nyingine zitakazoelezwa baadae, imeonesha mfano wa utayari kwa kuwa na mpango mkakati wake ambao unalenga kuwawezesha watoa huduma wa humu nchini wanapata fursa hizo kwa kuwasaidia kwa namna mbali mbali tangu hatua za awali za kuwania fursa hizo hadi utekelezaji wake.

Makamu Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Abdulsamad Abdulrahim katika moja ya mikutano na waandishi wa habari alisema taasisi yake imejipanga kuwajengea uwezo watoa huduma na kutoa wito watoa huduma hao kwa waliokuwa bado hawajajiunga wajiunge na taasisi hii kwa minajili ya kufaidika na uwezeshaji wao.

Halikadhalika, Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) nalo linaeleza kuwa limejidhatiti kuhakikisha kuwa watanzania watakaobahatika kupata fursa za kutoa huduma katika mradi huo hawashindwi kwa kukosa fedha za kutekeleza kandarasi zao.

“Hatutaki kusikia mtanzania amekosa fursa hii kwa sababu ya kukosa fedha …ukibahatika njoo kwenye Baraza tutakushauri… Serikali ina mifuko 17 yenye fedha za kutosha kukuwezesha” anaeleza Mkurugnezi wa uwezeshaji wa NEEC Bwana Edwin Chrisant.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF) Bwana Godfrey Simbeye aliwaambia waandishi wa habari kuwa taasisi yake imejipanga kuhakikisha kuwa mikataba ya kandarasi itakayofikiwa inazingatia maslahi ya pande zote na utekelezaji wake unafanyika kulingana na vipengele vya mikataba.

Dhamira hizi zilizoelezwa na taasisi hizi muhimu nchini, hapana shaka yoyote kuwa ni habari njema inayoashiria matumaini makubwa na kuonesha sasa watanzania wameamka na wamedhamiria kujenga Tanzania mpya kwa kila mmoja kwa nafasi yake kuyatumia mazingira yaliyopo kujenga uchumi wa taifa.

Kama kweli taasisi hizi zitatekeleza yale ziliyojipangia ikiwemo kuwapatia watoa huduma msaada wa kitaalamu, huduma za kisheria, kifedha, viwango na vigezo katika manunuzi, utaalamu, kuwaunganisha na wabia, kuwajengea uwezo vijana wasomi ili waweze kushika nafasi zitakuwa zimetoa msaada mkubwa kwa nchi.

Kwa hakika mradi huu kama ilivyoelezwa awali utakuwa kigezo muhimu kupima utayari, umakini na uwezo wa sekta binafsi kuchangamkia fursa zinapotokea na mafanikio ya ushiriki wa sekta hiyo huenda ukawa mwanzo mzuri wa kuupa mgongo utamaduni ulizoeleka wa watanzania kulalamika hususan kuilalamikia Serikali kuwa haiwapi fursa kama hizi.

Wahenga walisema “shike shike na mwenyewe nyuma” kwa hili Serikali zimefanya wajibu wake sasa mpira uko kwa wadau katika sekta binafsi kuucheza kwa zitumia fursa na ni vyema kukumbuka kuwa “mso matendo hula uvundo” hivyo watanzania wachangamkie fursa wasije wakajikuta karamu imekwisha ‘wakaramba vyungu.

 Ni vyema pia kutanabahisha kuwa fursa za mradi huu haziko kwa watoa huduma kama hao pekee ambao wao ni wafanyabiashara na wataalamu ambao tayari wanajielewa, wana uwezo na wako katika sekta hiyo hivyo tunaweza kusema wana angalau uzoefu.

Lakini ukweli hi kuwa fursa za mradi huu zimetapakaa kila mahala katika ngazi mbali mbali kuanzia wakulima wa jembe la mkono, wafugaji wadogo wadogo, mafundi mchundo, hadi vibarua wa ujenzi. Hivyo taasisi zinazohusika zinapaswa pia kuliangalia kundi hili kubwa na kuhakikisha linashiriki vyema.

Hii ni kwa sababu, inapozungumziwa ajira elfu kumi na ajira nyingine zaidi ya elfu thelathini nyingi zinawagusa watanzania wa kundi hili. Ikumbukwe kuwa kundi hili ambalo ndilo litakalokuwa karibu na mradi ndilo litakalokuwa la kwanza kulalamika pindi litakapokosa fursa na kujikuta halina namna ya kushiriki na kufaidika.

Utekelezaji mzuri na wenye ufanisi wa mradi huu kwa kushirikisha sekta binafsi nchini utakuwa kigezo cha kufungua milango kwa miradi mingine mikubwa ya aina hii humu nchini.



Watanzania hawana budi kumpongeza Rais Magufuli kwa jitihada zake za kujenga Tanzania Mpya yenye matumaini mapya. Hakika Tanzania yenye uchumi wa kati na ya viwanda inawezekana, kama kila mmoja atatimiza wajibu wake.