Saturday, August 12

Tume ya uchaguzi Kenya yashangazwa na matokeo ya upinzani

Tume ya Uchaguzi ya Kenya imesema ni mapema na ni kinyume cha sheria kwa mgombea wa upinzani Raila Odinga kujitangazia kuwa ameshinda uchaguzi wa Kenya.
Alhamisi, muungano wa upinzani wa NASA ulichapisha matokeo ambayo yanaonyesha kuwa Raila Odinga amemshinda Rais wa sasa Uhuru Kenyatta, ambapo pia waliitaka tume ya uchaguzi imtangaze Odinga kuwa ndiye Rais mteule.
Hata hivyo matokeo ya awali hadi sasa yaliyotangazwa na tume hiyo yanaonyesha Rais wa sasa Uhuru Kenyatta bado anaongoza dhidi ya mpinzani wake Raila Odinga.
Mwandishi wetu Anne Soy alifanya mahojiano na Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati.
Kwanza alimuuliza, je tume hiyo imepokea barua yoyote kutoka kutoka upinzani?

Trump: Jeshi la Marekani liko tayari kuikabili Korea Kaskazini

Donald Trump na Mike Pence Bedminster, New Jersey, on 10 August 2017Haki miliki ya pichaREUTERS
Rais wa Marekani Donald Trump amesema jeshi la Marekani liko tayari kukabiliana na Korea Kaskazini wakati wowote ule.
"Suluhu ya kijeshi sasa ipo, imepangwa na iko tayari, Korea Kaskazini wakidhubutu kuchukua hatua isiyo ya busara. Twatumai Kim Jong-un atachagua njia nyingine!" Trump ameandika kwenye Twitter.
Amesema hayo huku Korea Kaskazini ikimtuhumu kwa kukaribia kutumbukiza rasi ya Korea katika vita vya nyuklia.
Pyongyang inakamilisha kuandaa mpango wake wa kurusha makombora karibu na kisiwa cha Marekani cha Guam.
Idara ya mambo ya nje katika kisiwa hicho katika bahari ya Pasifiki imetoa mwongozo Ijumaa pamoja na ushauri kwa wakazi wa kisiwa hicho kuhusu jinsi ya kujiandaa kukiwa na tishio la makombora.
Idara hiyo imewaonya raia wake wajiepushe kutazama mwanga kutoka kwa kombora kwani unaweza "kupofusha".
"Lala sakafuni na ukinge kichwa chako. Iwapo mlipuko utakuwa umbali kiasi kutoka ulipo, inaweza kuchukua sekunde 30 au zaidi kwa wimbi la mlipuko wenyewe kukufikia."
Bw Trump ameandika hivyo kwenye Twitter baada ya kutishia mapema wiki hii kupitia Twitter kwamba "Korea Kaskazini wasidhubutu kutoa vitisho zaidi kwa Marekani. Watajibiwa kwa moto na ghadhabu ambayo ulimwengu haujawahi kushuhudia."
Aidha, Ijumaa, shirika rasmi la habari la Korea Kaskazini KCNA liliituhumu Marekani kwa "jaribio la kihalifu la kusababisha mkasa wa kinyuklia katika taifa hilo la rasi ya Korea."
Shirika hilo lilisema Marekani inafanya kila juhudi kufanyia majaribio silaha zake za nyuklia katika rasi ya Korea.
Marekani ndiyo "mpanga njama ya tishio hili la nyuklia, mraibu wa vita vya nyuklia," taarifa ya KCNA imesema.
Awali, alikuwa ameitahadharisha Korea Kaskazini kwamba inafaa kuwa na "wasiwasi sana" iwapo itatenda lolote kwa Marekani.
Alisema utawala wa taifa hilo utakuwa shida kubwa "ambayo ni mataifa machache sana yaliyowahi kukumbana nayo" iwapo "hawatabadilika".
Kadhalika Bw Trump alikuwa awali ameshutumu serikali za awali za Marekani akisema zilionyesha udhaifu sana zikikabiliana na Korea Kaskazini na pia akashutumu mshirika wa karibu wa Korea Kaskazini, akisema kwamba inafaa "kufanya juhudi zaidi."
Alisema: "Nawaambia, iwapo Korea Kaskazini itafanya jambo lolote hata kwa kufikiria tu kuhusu kumshambulia mtu tunayempenda au tunayewakilisha au washirika wetu au sisi wenyewe inaweza kuwa na wasiwasi sana, sana."
"Nitawaambia ni kwa nini...ni kwa sababu mambo yatawatendekea ambayo hawajawahi kufikirtia kwamba yanaweza kutokea."
Hata hivyo, aliongeza kwamba Marekani bado iko huru kushiriki katika mashauriano.
Aliongeza: "Nawaambia hivi, Korea Kaskazini inafaa kujiweka sawa au wataona shida kubwa kiasi ambacho ni nchi chache sana zilizowahi kushuhudia."
Andersen Air Force Base, Guam July 18, 2017Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionMarekani ina kambi ya jeshi la wanahewa la Andersen kisiwa cha Guam
Korea Kaskazini ilisema Jumatano kwamba inapanga kurusha makombora ya masafa wa wastani na ya masafa marefu kuelekea kisiwa cha Guam, ambapo kuna kambi ya ndege za kivita za kuangusha mabomu za Marekani.
Hata hivyo, kufikia sasa hakujakuwa na dalili zozote kwamba huenda kisiwa hicho cha Guam kikashambuliwa.
Map showing Guam

Kisiwa cha Guam na umuhimu wake

  • Kisiwa cha Guam kina ukubwa wa kilomita mraba 541 (maili mraba 209) na kinapatikana bahari ya Pasifiki kati ya Ufilipino na Hawaii.
  • Ni jimbo "lisilo na mpangilio wowote, na lisilojumuishwa kikamilifu" la Marekani, lenye wakazi karibu 163,000.
  • Kambi za jeshi la Marekani hutumia karibu robo ya ardhi ya kisiwa hicho. Marekani ina wanajeshi 6,000 kisiwa hicho na kuna mipango ya kuwasafirisha maelfu wengine huko.
  • Ni kituo muhimu katika shughuli za kijeshi za Marekani, ambapo huwezesha wanajeshi wa nchi hiyo kufika maeneo mengi muhimu Pasifiki, mfano eneo la bahari linalozozaniwa la South China Sea, rasi ya Korea na mlango wa bahari wa Taiwan.
Bw Trump alikuwa amewaambia wanahabari Jumanne kwamba: "Korea Kaskazini wasidhubutu kutoa vitisho zaidi kwa Marekani. Watajibiwa kwa moto na ghadhabu ambayo ulimwengu haujawahi kushuhudia."
Seneta mkongwe wa Marekani John McCain hata hivyo alikuwa na shaka kuhusu tamko la Trump.
"Viongozi wengi wakuu ambao nimewahi kuwaona, huwa hawatoi vitisho ikiwa hawako tayari kuvitekeleza na sina uhakika kwamba Rais Trump yuko tayari kuchukua hatua," alisema Bw McCain.
Korea Kaskazini ilikuwa imeghadhabishwa na vikwazo vipya ilivyowekewa na Umoja wa Mataifa siku ya Jumamosi.
Vikwazo hivyo vina lengo la kupunguza mapato kutoka kwa mauzo ya bidhaa nje ya Korea Kaskazini kwa theluthi moja.
KCNA imesema Korea Kaskazini, ambayo imefanyia majaribio silaha za nyuklia mara tano, itajibu vikali na kwamba "Marekani italipia" kwa kuchangia kutunga vikwazo hivyo.
Waziri mkuu wa Australia Malcolm Turnbull amesema taifa lake liko tayari kushiriki katika vita dhidi ya Korea Kaskazini iwapo nchi hiyo ya rasi ya Korea itatekeleza shambulio dhidi ya Marekani.
"Iwapo kutakuwa na shambulio dhidi ya Marekani, Mkataba wa Anzus wa mwaka 1951 utaanza kutekelezwa na Australia itajitokeza kuisaidia Marekani," alisema kwenye mahojiano na kituo kimoja cha redio, "vile vile ambavyo Marekani ingefika kutusaidia iwapo tutashambuliwa."

Wanawake washinda nyadhfa za Ugavana Kenya

Aliyekuwa waziri wa ugatuzi nchini Kenya Anne Waiguru
Image captionAliyekuwa waziri wa ugatuzi nchini Kenya Anne Waiguru
Aliyekuwa waziri wa ardhi nchini Kenya Charity Ngilu ni miongoni mwa wanawake watatu nchini Kenya wanaotarajiwa kuwa magavana wapya wa kaunti zao.
Ngilu ambaye aliwania wadhfa huo katika kaunti ya Kitui nchini Kenya kupitia chama cha Narc alimshinda Gavana Julius Malombe kwa wingi wa kura.
Mgombea mwengine mwanamke ambaye ameshinda wadhfa wa Ugavana ni aliyekuwa naibu wa spika bungeni Dkt Joyce Laboso .
Laboso amemshinda gavana Isaac Rutto ambaye ni miongoni mwa viongozi wakuu wa muungano wa upinzani Nasa.
Mwanamke huyo ambaye alikuwa akigombea wadhfa huo kupitia chama tawala cha Jubilee alikuwa ameshutumiwa na mpinzani wake aliyemtaka kuwania ubunge katika eneo la Nyanza alikoolewa.
Mgombea mwengine ni Anne Waiguru ambaye wakati mmoja alihudumu kama waziri wa maswala ya ugatuzi .
Waiguru ambaye alilazimika kujiuzulu katika wadhfa huo kutokana na madai ya ufisadi yaliomkabili anaendelea kupata ushindi dhidi ya Martha Karua aliyewahi wakati mmoja kugombea urais mbali na kuwa waziri..
''Nafurahi sana, watu wa Kirinyaga wanafurahi'', alisema huku kukiwa na pongezi na shangwe kutoka kwa wafuasi wake.
Ni miongoni mwa wanawake watatu ambao wanatarajiwa kuwa magavana na anasema kuwa safari yake fupi imekuwa ngumu.
''Imekuwa ngumu , ngumu sana, sijui ni mara ngapi nilitaka kujiondoa lakini nikaamua kusalia kwenye kinyanganyiro cha kuwania wadhfa huu''.
Anasema ushindi wake umetoa mfano wa mtoto wa kike kujitokeza na kuwania uongozi.
''Watoto wetu wa kike watasema nini iwapo tutajiondoa''?
Anasema kuwa lengo lake kuu ni kuimarisha kilimo katika kaunti hiyo.
Kwengineko wanawake wengine watatu wanaongoza katika kinyang'anyiro cha usineta nchini humo.
Susan Kihika na Margaret kamar ni wagombea wanawake wanaoongoza katika matokeo ya usineta katika kaunti ya Uasin Gishu na Isiolo.
Mjini Nakuru, Susan Kihika ambaye anagombea kupitia chama tawala cha Jubilee anaongoza akiwa mbele ya mgombea wa chama cha ODM Samuel Ogada.
Vilevile Margaret kamar wa chama cha Jubilee anaongoza dhidi ya mpinzani wake wa chama cha Independent .
Wanawake wengine walioshinda viti vya ubunge ni Mishi mboko wa likoni aliyemshinda Masoud Mwahima, Aisha Jumwa aliyeshinda kiti cha eneo bunge la kilifi na Naisuna lesuda aliyeshinda kiti cha eneo bunge la Samburu magharibi.
Aisha Jumwa wa chama cha ODM aliwashinda wanamume saba kushinda kiti cha eneo bunge la Malindi .
Phillip Charo of Jubilee Party got 14,219 votes while Willy Mtengo (Independent) was third with 6,658 votes.
Na katika kaunti ya Homabay Historia imeandikishwa baada ya wanawake watatu kuibuka washindi katika viti vya maeneo bunge ya kaunti hiyo.
Wabunge hao ni Millie Odhiambo wa Suba, Lilian Rongo wa Rangwe na Dr Eve Obara wa Kabondo Kasipul.
Watatu hao waliwashinda wagombea wengine katika mchujo wa chama cha upinzani cha ODM uliotawaliwa na wanaume katika jimbo hilo.

GRACA MACHEL AFUNGA MKUTANO WA MAENDELEO KWA WANAWAKE ,KIUCHUMI NA JAMII (WOMEN ADVANCE IN AFRICA)


Mjane wa Rais wa Zamani wa Afrika Kusini Mama Graca Machel akihutubia wakati wa kufunga Mkutano wa Maendeleo ya Wanawake kwenye Uchumi na Jamii(Women Advance in Africa ) Uliofanyika Jijini Dar es Salaam anakwa takribani siku tatu na kuwakutanisha Wanawake kutoka kila pembe ya Afrika
Mjane wa Rais wa Zamani wa Afrika Kusini Mama Graca Machel akihutubia wakati wa kufunga Mkutano wa Maendeleo ya Wanawake kwenye Uchumi na Jamii(Women Advance in Africa ) Uliofanyika Jijini Dar es Salaam anakwa takribani siku tatu na kuwakutanisha Wanawake kutoka kila pembe ya Afrika
Mjane wa Rais wa Zamani wa Afrika Kusini Mama Graca Machel akiteta jambo na Waziri Mkuu wa Zamani Nchini ,Jaji Joseph Sinde Warioba kabla ya kufunga Mkutano wa Maendeleo ya Wanawake kwenye Uchumi na Jamii(Women Advance in Africa ) Uliofanyika Jijini Dar es Salaam anakwa takribani siku tatu na kuwakutanisha Wanawake kutoka kila pembe ya Afrika
Baadhi ya Wanawake kutoka nchi Mbalimbali Walioshiriki Mkutano wa Maendeleo ya Wanawake kwenye Uchumi na Jamii(Women Advance in Africa ) Uliofanyika Jijini Dar es Salaam anakwa takribani siku tatu na kuwakutanisha Wanawake kutoka kila pembe ya Afrika
Waziri Mkuu Mstaafu ,Jaji Joseph Sinde Warioba akizungumza jambo na Mwanaharakati wa siku nyingi Getrude Mongela wakati wa Kufunga Mkutano wa Maendeleo ya Wanawake kwenye Uchumi na Jamii(Women Advance in Africa ) Uliofanyika Jijini Dar es Salaam anakwa takribani siku tatu na kuwakutanisha Wanawake kutoka kila pembe ya Afrika 
Baadhi ya Wanawake kutoka nchi Mbalimbali Walioshiriki Mkutano wa Maendeleo ya Wanawake kwenye Uchumi na Jamii(Women Advance in Africa ) Uliofanyika Jijini Dar es Salaam anakwa takribani siku tatu na kuwakutanisha Wanawake kutoka kila pembe ya Afrika

DIWANI WA KATA SAMBASHA ( CCM) AACHIWA KWA DHAMANA DHIDI YA KESI INAYOMKABILI


Na Vero Ignatus.Arusha

Mahakama ya Hakimu mkazi Arusha imemsomea mashtaka mawili aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa umoja wa vijana (UVCCM) Lengai Ole Sabaya ambaye pia ni diwani wa kata ya Sambasha Wilaya ya Arusha vijijini .

Miongoni mwa makosa hayo aliyosomewa mahakamani hapo kosa la kwanza alituhumiwa kujifanya Afisa mtumishi wa serekali (TISS)huku kosa la pili ikiwa kugushi moja ya nyaraka za serekali(kitambulisho ).

Akisoma mashtaka hayo mahakamani hapo Wakili wa serekali Penina Joakim amesema kuwa Mnamo May 18 katika hotel ya Skyway iliopo makao mapya jijini Arusha Mshitakiwa alijitambulisha kama Afisa utumishi wa idara ya usalama wa taifa na kufanya Utapeli .

Wakili Penina alitaja kosa la pili ambalo Mshitakiwa Lengai Ole Sabaya alisomewa kuwa ni kugushi kitambulisho cha idara ya usalama wa Taifa kilichokuwa kikisomeka jamuhuri ya muungano wa Tanzania idara ya usalama wa Taifa (TISS) Lengai Ole Sabaya kikosi maalumu Agent (undercover)chenye code no MT 86117 huku akitambua kuwa ni kinyume cha kisheria .

Hata hivyo mara baada ya kusomewa mashtaka hayo mahakamani hapo mtuhumiwa alikana mashtaka ndipo Hakimu Mkazi aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo Nestory Barro alisema dhamana ipo wazi iwapo wathamini watakithi vigezo vinavyotakiwa na mahakama hiyo.

Hata hivyo Mshitakiwa alipata dhamana baada ya kukithi vigezo vilivyowekwa na mahakama ambapo ilikuwa ni wadhamini wawili wenye sifa ambapo kwanza awe mtumishi wa serikali pili awe na mali isiyohamishika yenye thamani ya shilingi milioni tatu kwa kila mmoja.

Hata hivyo wakili Edina Mndeme anayemtetea Lengai Ole Sabaya amesema kuwa mteja wake amekuwa akifikishwa mahakamani na amesomewa mashitaka yaleyale na hii ni mara ya nne .

Kesi imeaihishwa na hakimu mkazi hadi itakapotajwa tena 30/8/2017 ambapo uchunguzi unatarajiwa kukamilika na kesi hiyo kuanza kusikilizwa.
Aliyewahi kuwa mwenyekiti wa UVCCM,na Diwani wa Kata ya Sambasha mkoa wa Arusha Lengai Ole Sabaya (aliyevaa suti nyeusi)akiwa nje ya mahakama mara baada ya kuachiwa kwa dhamana kutokana na kesi inayomkabili.Picha na Vero Ignatus Blog.
Aliyewahi kuwa mwenyekiti wa UVCCM,na Diwani wa Kata ya Sambasha mkoa wa Arusha Lengai Ole Sabaya (aliyevaa suti nyeusi)akizungumza na vyombo vya habari nje ya mahakama.Picha na Vero Ignatus Blog.
Akizungumza na mwenyekiti wa CCM katika kata ya Sambasha Lesion Letionoki Njoki.Picha na Vero Ignatus Blog.

Akisalimiana na wananchi wa kata ya Sambasha mara baada ya kuachiwa kwa dhamana.Picha na Vero Ignatus Blog.

UCHAGUZI MKUU TFF- MAGUFULI NDIYE ATAKAYE TULETEA RAIS WA KUKUMBUKWA TFF



.
Na Honorius Mpangala.

Ni katika utawala wa Rais wa awamu ya tano Dodoma imerejesha Hadhi yake kama makao makuu ya nchi tangu ilivyokuwa hivyo kwa zama za Mwalimu J. K. Nyerere. Hadhi ya Dodoma inamfanya kila mmoja atamani kuishi Dodoma.

Ni katika utawala wa awamu ya tano ambapo uchaguzi wa TFF unawaingiza viongozi wapya madarakani. Hakuna asiyeijua kasi ya kiutendaji pamoja na heshima ya ofisi za umma zilivyo kwa sasa.

Viongozi watakao chaguliwa moja kwa moja wataingia madarakani kwa kutambua kiongozi mkuu wa nchi ni nani. Hakuna kiongozi ambaye atakuja kufanya tofauti katika utawala huu kama ikitazamwa viongozi watangulizi hadi niandikapo wako rumande.

Wanataka kutufikisha sehemu fulani wanatuhaidi mabadiliko lakini kitu pekee ambacho tutapaswa kujiandaa nacho ni pale tutakapo ambiwa mambo yanayohusu fedha lazima yakaguliwe na CAG.Hili ni jambo la kujipanga nalo na kwa viongozi watakao ingia madarakani naamini lazima akili yao itakuwa imesoma alama za nyakati na kutambua mahitaji yaliyopo sasa.

Ikiwa kama shirikisho linahitaji mchango wa serikali katika kufanikisha Yale matarajio basi wasisite kutoa ushirikiano pia itakapofika wakati wa kuhitaji ukaguzi wa kiofisi.Miongoni mwa mambo yanayoendelea katika shirikisho letu ni upatikanaji watu mwenye weredi katika kusukuma maendeleo ya soka letu.

Wakati Rais mstaafu Bemjamini William Mkapa anatoweka madarakani mwaka 2005 alicha Uwanja wa taifa. Wakati Rais mstaafu pia Jakaya Kikwete anatoweka madarakani mwaka 2015 aliacha utaratibu wa Kocha mkuu wa timu ya taifa akilipwa mshahara na serikali. 

Awamu ya nne licha kufanikisha kwa kuzisaidia timu zetu za taifa kwa kuwaleta walimu toka nje ya Tanzania lakini tulikosa watu wa kuwachunguza watu tuliowapa mamlaka ya kusimamia vyama hivyo vya Michezo.

Alikuja kocha wa ngumi toka nchi ya Cuba hadi Leo hakuna mwenye majibu yaliyonyooka aliondoka vipi. Sio kocha wa ngumi tu bali hata kocha wa Netball alikuja hapa nchini lakini Uswahili wa viongozi wetu hakuna ambaye alielewa.

Awamu hii Rais kafanikiwa kumshawishi mfalme wa Morocco kuweza kufanikisha upatikanaji wa uwanja wa Michezo pale Dodoma. Ni kitu kikubwa sana kufanyika ambacho kitaifanya Dodoma kujikuta ikimpa heshima ya juu Rais wetu kwa maamuzi yake na Uzalendo wake kwa taifa lake.

Katika kipindi hiki ndipo niligundua Waziri wa wizara ya Michezo anawasiliana na watu wa FIFA na kuwaeleza kila wafanyalo kwa shirikisho la Mpira la Tanzania ni lazima serikali ifahamishwe. Hali hii itapelekea kufanikisha mambo mengi yaliyokuwa yanaelekeza katika utekelezaji wa miradi ya TFF.



Kwa viongozi watakao ingia madarakani watakuwa na uwepesi wa kazi kutokana na kuzisoma nyakati na kujua mahitaji na kiu ya watanzania katika msuala ya Michezo. Nina hakika kwa kiongozi yeyote atakaye fanikiwa kuingia katika uongozi atakuwa amesoma nyakati vyema.Utendaji wa shirikisho utakuwa na ufanisi sana.

Soka letu linahitaji MTU amayeweza kujitoa kwaajili ya watu ili kufanikisha ndoto zao. Tunahitaji MTU anatakaye tambua uwezo na kipaji cha vijana walioko kwenye mfumo wa kimakuzi katika soka. Hadi sasa ilikuwa inashangaza vijana waliokuwa wamepelekwa katika vituo vya kulelewa kisoka kutotumika. Wako waliopelekwa Nchi ni Ghana na mwingine pale Dakar Senegal lakini hakuna anayeonekana kuwakumbuka vijana wale.

Ni kama tunapiga konzi kwenye kinyago na hatimaye tunaumia wenyewe. Tunahitaji atakaye tujuza kuwa hiki ni kinyago na tuachane nacho kukipiga makonzi. Shirikisho lenye uthubutu katika utendaji ndio mafanikio ya soka letu.Natamani kuona serikali ikiwa na mamlaka ya kushirikiana na TFF katika kufanikisha kila jambo. Kwa taasisi iliyo chini ya serikali ingekuwa safi kuona mkaguzi wa hesabu za serikali akifanya kazi katika nyanja mbalimbali katika masuala ya Michezo.

Hoja ya kusambaza mpira nchi nzima itaweza kusaidia hata kufanya hata baadhi ya maeneo yanayo onekana hayana soka basi watacheza soka. Kuto kuwa na soka ni hali ya mikoa kutokuwa vilabu kwa daraja la kwanza la pili hata ligi kuu.

Rais wa TFF unayekuja pamoja na wajumbe wako jambo pekee la kuweka kichwani ni kwamba Rais Wa jamhuri ya muungano wa Tanzania John Pombe Joseph Magufuli anakusubili mfanye kazi mfanikishe ujenzi wa Uwanja wa Michezo pale Dodoma.


RAIS DKT JOHN POMBE MAGUFULI AMTEUA BERNARD HEZRON KONGA KUWA MKURUGENZI MKUU WA NHIF


Mkurugenzi Mkuu wa NHIF,Bw.Bernard Hezron Konga


DKT.SHEIN AKUTANA NA UJUMBE WA KATIBU MKUU WA JUMUIYA YA MADOLA




Na  Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
JUMUIYA ya Madola imeahidi kuendelea kuiunga mkono Zanzibar katika kuimarisha sekta mbali mbali za maendeleo kama ilivyo kwa wanachama wengine wote 52 wa Jumiya hiyo.
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola Baroness Patricia Scotland aliyasema hayo leo wakati alipofanya mazungumzo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein Ikulu mjini Zanzibar.
Katika maelezo yake Katibu Mkuu huyo alieleza kuwa Jumuiya ya Madola inaendelea kutekeleza mipango na mikakati kabambe ambayo imeiweka kwa wanancha wake ikiwemo Tanzania ambapo Zanzibar pia, ni miongoni mwao.

Baroness  Scotland alitumia fursa hiyo kutoa pongezi kwa Rais Dk. Shein kwa juhudi kubwa anazozichukua katika kuhakikisha Zanzibar inakuza uchumi na kuimarisha amani na utulivu na kusisitiza kuwa Jumuiya anayoiongoza haitokuwa nyuma kumuunga mkono.
Aidha, Bi Scotland alimueleza Dk. Shein miongoni mwa mipango ya Jumuiya hiyo kwa nchi wanachama wake wote 52 ikiwa ni pamoja na kuongeza fursa katika sekta ya biashara nan uchumi, kuwasaidia wanawake, vijana, upatikanaji ajira kwa vijana, elimu, kutunza mazingira, uwezeshaji na mengineyo.
Aliongeza kuwa uchumi kwa nchi wanachama wa Jumuiya hiyo umekuwa ukiimarika kwa kiasi kikubwa kwa zile nchi za Bara la Afrika na hata nchi za Bara la Asia uchumi wake umeimarika kwa asilimia 5 hadi asilimia 8.

Katika mazungumzo hayo, Bi Scotland alimueleza Dk. Shein kuwa miongoni mwa maeneo yaliopewa kipaumbele na Jumuiya hiyo ni katika kuhakikisha nchi zake wanachama zinaimarika kiuchumi ni pamoja na miundombinu na nishati.
Akieleza juu ya Jumuiya hiyo ilivyoweka mikakati katika kusaidia katika kupambana na changamoto ya hali ya mabadiliko ya tabia nchi hasa kwa nchi za Visiwa, Bi Scotland alitoa mfano wa nchi yake ya kisiwa cha Jamhuri ya Dominica jinsi ilivyopata athari zilizotokana na hali hiyo.

Nae Rais Dk. Shein kwa upande wake alitoa pongezi kwa kiongozi huyo kwa ujio wake hapa Zanzibar sambamba na juhudi kubwa zinazochukuliwa na Jumuiya hiyo katika kuendelea kuiounga mkono Zanzibar.

Dk. Shein kwa upande wake alimueleza kiongozi huyo kuwa Zanzibar iko salama na usalama wake unatokana na kuwepo kwa amani na utulivu mkubwa hatua ambayo inapelekea hata uchumi wake kuzidi kuimarika siku hadi siku.
Aliongeza kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeweza kupata mafanikio makubwa katika kuimarisha uchumi wake kutokana na sekta ya utalii, sekta ambayo bila ya kuwepo kwa amani na utulivu ni vigumu kuimarika.
Dk. Shein alitumia fursa hiyo kueleza juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar jinsi inavyochukua hatua katika kuimarisha sekta za maendeleo na kueleza azma ya ujenzi wa bandari mpya ya Mpiga Duri pamoja na kuuimarisha uwanja wake wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume kwa kujenga jengo jipya la abiria.
Aidha, Dk. Shein alieleza mafaniki yaliopatikana katika kuimarisha demokrasia na utawala bora hapa nchini huku akimueleza juhudi zilizochukuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kutunga sheria ya maadili kwta viongozi  wa umma.
Dk. Shein, pia, alitumia fursa hiyo kumueleza Katibu Mkuu huyo hatua zinazochukuliwa na Serikali anayoiongoza katika kupambana na vitendo vya udhalilishaji wa akina mama na watoto sambamba na juhudi za Serikali za kuanzisha Pencheni Jamii kwa wazee kuanzia miaka 70, jambo ambalo Bi Scotland alilipongeza.
Pia, alimueleza hali ya mabadiliko ya tabia nchi jinsi inavyoathiri mazingira ya Zanzibar hasa katika kasiwa cha Pemba na sehemu nyenginezo na kueleza hatua zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali pamoja na Jumuiya za Kimataifa katika kupambana na hali hiyo huku akitolea mfano mkutano wa nchi zinazoendelea za visiwa (SIDS) uliofanyika mwaka 2014 huko Samoa na maazimio yake juu ya hali hiyo.
Akijibu masuali ya waandishi wa habari baada ya mazungumzo hayo, Bi Scotland aliwataka wapinzani kushirikiana na Serikali anayoiongoza Dk. Shein kwa lengo la kuwaletea maendeleo endelevu wananchi wa Zanzibar na kusisitiza kuwa Zanzibar inafaidika na misaada ya Jumuiya hiyo kupitia Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Jumuiya ya Madola  ilianzishwa karne ya 20 kwa lengo la kuikutanisha Uingereza na yaliyokuwa makoloni yake duniani kwa jukumu la kuhakikisha wanachama wake wanajikwamua katika Nyanja mbali mbali za kimaendeleo ikiwemo kisiasa, kiuchumi, kijamii, michezo na burudani huku Malkia wa Uingereza akiwa ndiye Kiongozi Mkuu wa Jumuiya hiyo.
  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akisalimiana na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola  Bibi Patrica  Baroness Scotland alipofika Ikulu Mjini Unguja leo akiwa katika ziara ya siku moja na ujumbe aliofuatana nao.
  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) alipokuwa akisisitiza jambo wakati akizungumza na  Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola  Bibi Patrica  Baroness Scotland alipofika Ikulu Mjini Unguja leo akiwa na ujumbe aliofuatana nao katika ziara ya siku moja. 
/Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akiagana na mgeni wake mara baada ya kumaliza mazungumza na  Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola  Bibi Patrica  Baroness Scotland alipofika Ikulu Mjini Unguja leo. 
Picha na Ikulu

MAREKANI KUPITIA SHIRIKA LAKE LA MISAADA LA USAID YAIPATIA TANZANIA DOLA MILIONI 225 KWA AJILI YA MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO


Siku moja baada ya Marekani kutangaza kutoa fedha za nyongeza katika mwaka ujao kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo hapa nchini, nchi hiyo imetiliana saini na Wizara ya Fedha na Mipango makubaliano ya kutoa Dola Milioni 225. 
Fedha hizo zitaelekezwa katika sekta mbalimbali zikiwemo Elimu, Afya, Kilimo na Utawala bora. 
Hafla ya kutiliana saini makubaliano hayo imefanyika katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam kati ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bw. Doto James na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo la Marekani (USAID) hapa nchini Bw. Andy Karas. 

Akizungumza baada ya kutiliana saini makubaliano hayo Bw. Doto James ameishukuru Marekani kwa kuendeleza uhusiano mzuri uliopo na Tanzania na amesema fedha hizo zitasaidia kuimarisha juhudi za Serikali kuwaletea maendeleo wananchi. 
Nae Bw. Andy Karas amesema Serikali na watu wa Marekani wanafurahishwa na kuendelea kwa ushirikiano mwema kati yao na Serikali ya Tanzania katika maendeleo na ameahidi kuwa ushirikiano huo utadumishwa. 
Hafla ya kutiliana saini makubaliano hayo imehudhuriwa na Kaimu Balozi wa Marekani hapa nchini Mhe. Dkt. Inmi Patterson ambaye amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa kufanikisha upatikanaji wa fedha hizo. 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Doto James (wa kwanza kushoto) akisaini mkataba wa Makubaliano (Strategic Assistance Agreement )na Mkurugenzi wa Shirika la Misaada la Marekani nchini USAID Andy Karas(katikati) kuhusu utoaji wa fedha hizo dola za kimarekani Millioni 225 , tukio lililofanyika katika Ofisi za Hazina jijini Dar es Salaam. Wakwanza kulia ni Kaimu Balozi wa Marekani hapa nchini Dkt. Inmi Patterson akishuhudia.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Doto James (wakwanza kushoto) akibadilishana mkataba ya makubaliano (Strategic Assistance Agreement) na Mkurugenzi wa Shirika la Misaada la Marekani nchini USAID Andy Karas katika Ofisi za Hazina jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Doto James (wakwanza kushoto) akipiga makofi pamoja na Mkurugenzi wa Shirika la Misaada la Marekani nchini USAID Andy Karas(katikati), na Kaimu Balozi wa Marekani hapa nchini Dkt. Inmi Patterson mara baada ya kusaini mkataba wa makubaliano (Strategic Assistance Agreement ) katika ofisi za Hazina jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Doto James akimshukuru Kaimu Balozi wa Marekani hapa nchini Dkt. Inmi Patterson mara baada ya kusaini mkataba huo utakaowezesha Tanzania kupatiwa fedha hizo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Doto James akimshukuru Mkurugenzi wa Shirika la Misaada la Marekani nchini USAID Andy Karas mara baada ya tukio hilo la mkataba wa makubaliano katika Ofisi za Hazina jijini Dar es Salaam.