Friday, August 11

Darasa la saba aliyewania urais kupitia CCM, hakutarajia kama Dk Magufuli angeshinda


Dar es Salaam. Aliyewania nafasi ya kugombea urais kupitia CCM mwaka 2015 kwa elimu yake ya darasa la saba, Ildephonce Birohe ameibuka na kusema katika kinyang’anyiro hicho hakutarajia kama Rais John Magufuli ndiye angeibuka mshindi.
Birohe (46) alitoa kauli hiyo katika mahojiano maalumu aliyofanya na Mwananchi nyumbani kwake Mtaa wa Gezaulole, Kata ya Gungu mjini Kigoma.
Alipoulizwa alikuwa anatarajia nani kuibuka kidedea miongoni mwa makada 41 waliojitokeza kuomba uteuzi wa chama hicho, alisita na kutabasamu kidogo, kisha akasema, “Nilitegemea ningeibuka mimi mshindi.”
Akifafanua zaidi, alisema katika mchuano ule ambao haukuwahi kutokea katika historia ya CCM, kila mgombea alikuwa na matumaini ya kuteuliwa kuwania urais.
Akijibu swali ni mgombea yupi alikuwa tishio kwake kwenye mchuano huo, Birohe kwa sauti ya chini, alisema “Hilo tuliache kama lilivyo.”
Kwa nini tuliache kama lilivyo? Akijibu swali hilo, kada huyo aliyekuwa amevalia sare rasmi ya CCM – suruali nyeusi, shati la kijani na kofia ya kijani, alisema CCM ina utamaduni wake, mgombea akishapitishwa na kuchaguliwa, wengine wote wanakuwa nyuma yake.

Mchuano ulivyompaisha
Kada huyo baada ya kupitia katika mchuano huo alitoka akiwa Birohe mwingine kwa kuwa Watanzania wengi walianza kumfahamu tofauti na alivyokuwa awali.
“Watanzania walianza kunifahamu katika habari za siasa, kwamba nilikwenda kugombea urais wa Tanzania,” alisema.
Alisema msukumo wa kuwania urais ulitoka moyoni mwake, tofauti na mawazo ya wengi kwamba huenda alitumwa kufanya hivyo.
“Msukumo huo unatoka moyoni mwangu, hautoki nje. Kila mtu anayo haki na uhuru wa kuchukua fomu kugombea urais, nilianza mchakato wa kuwania urais mwaka 2003 ili nigombee 2005, lakini sababu ambazo hazikuweza kuzuilika wakati ule haikuwezekana, nikajitokeza tena 2015,” alisema.
Alisema mwaka 2003 jina lake halikupewa fursa, lakini safari hii licha ya kukumbana na vikwazo vya wapambe waliokuwa hawataki apewe fomu, alifanikiwa.
“Walikuwapo watu wa pembeni waliokuwa wanataka nisipewe fomu, lakini kwa sababu Chama cha Mapinduzi ni chama pekee chenye mapendo, chenye demokrasia, nikapewa,” alisema.
Alisema baada ya kufanya uamuzi, alimwambia mkewe naye akahoji kwa mshangao.
“Aliniambia, ‘kweli utaweza kufika Dodoma’, nikasema nitaweza. Akasema, ‘utakwenda kuizunguka nchi nzima uiweze’, nikasema nitaweza. Akasema ‘haya, mimi nakutakia safari njema’,” alisema.

Gharama za fomu, kusaka wadhamini
Birohe ambaye anajishughulisha na kilimo cha kujikimu alisema hakuna mtu yeyote aliyemchangia fedha Sh1,000,000 za kuchukua fomu na nyingine alizosema nyingi zaidi za kuzunguka kutafuta wadhamini.
“Wakati ule yaliandikwa mengi, madai ya kupewa hela niliyasikia. Wengine walisema sikuwa na pesa nilikuja tu na 600,000, nahitaji kuongezewa 400,000, lakini mimi pesa nilikuwa nazo zote za kuchukulia fomu. Walijaribu kuzungumza mengi sana lakini mimi nilikaa kimya,” alisema.
Alisema maandalizi yake hayakufanyika kwa siku moja, bali yalichukua muda kuanzia mwaka 2000.
Kuhusu fedha za kuzunguka mikoani kutafuta wadhamini alisema alikuwa nazo zote, lakini licha ya kudai kwamba ni nyingi kuliko za kuchukua fomu hakutaka kutaja kiwango chake.
“Zipo za kuzunguka, yaani milioni moja hizo za fomu ni kiasi kidogo sana, hizo za kuzunguka mikoani ni kubwa zaidi, lakini hilo ni fumbo tuliache kama lilivyo... Kweli imeshapita miaka miwili, lakini tuliache, hakuna haja. Hili linabaki kama lilivyo,” alisisitiza Birohe.
Mbali na matumizi ya fedha, katika mzunguko huo wa kusaka fomu, Birohe alisema alikumbana na vikwazo kadhaa, akitolea mfano wa Kisarawe Mkoa wa Pwani, alipokuta wanachama wa kumdhamini wamechukuliwa kwenda kumdhamini mgombea mwingine.
“Nilipofika Kisarawe nilikuta hakuna mtu. Nilimpigia katibu wa wilaya akasema leo hatupo, akasema utusubiri. Niliondoka na kurudi Ilala hadi siku iliyofuata,” alisema.

Yaliyotokea Dodoma
Birohe alisimulia kwa nini alionekana kama anatangatanga alipowasili Dodoma kuchukua fomu. Alisema alipofika, moja kwa moja alikwenda benki kuchukua fedha, lakini alipokuwa kwenye foleni alipigiwa simu kwamba zamu yake imefika.
Ndipo akakimbia kwenda CCM makao makuu kuitika wito, kisha akarudi benki kuchukua fedha.
Hata baada ya kupata fedha na kulipia fomu, alisikika akiitikia simu akisema, “tayari mzee”. Alipoulizwa katika mahojiano, huyo mzee alikuwa ni nani, Birohe alisema alikuwa shemeji yake, ambaye hata hivyo, hakutaka kumtaja.
Alipoulizwa kama angefanikiwa Kura za Urais, angefanya jambo gani tofauti na anavyofanya Rais Magufuli, Birohe alisema hilo pia liachwe kama lilivyo na alipoulizwa kuhusu utendaji kazi Rais huyo, alisema kwa ujumla kuwa anafanya vizuri.
Kuhusu jambo gani katika maisha yake akipata fursa atapenda kulirekebisha, alisema ni suala la elimu ili aweze kupata elimu zaidi ya ile ya msingi aliyonayo.

Waangalizi wasaka suluhu na timu ya Raila Odinga Kenya


Nairobi. Waangalizi wa kimataifa wa Umoja wa Afrika (AU) na Jumuiya ya Madola wametoa ripoti zao za awali kuhusu uchaguzi Kenya na mazungumzo yao na kambi ya upinzani ya National Super Alliance (Nasa) iliyowasilisha madai kwamba kompyuta za Tume ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) ziliingiliwa na upande Jubilee ili kuvuruga matokeo ya kura.
Kiongozi wa ujumbe wa waangalizi wa Umoja wa Afrika, Thabo Mbeki alisema mgombea wa Nasa, Raila Odinga na ujumbe wake walikutana nao wakiwa na nyaraka za madai kuhusiana na Jubilee kuvamia kompyuta hizo.
Mbeki alisema waliwasikiliza na kuwaeleza kuwa watalifikisha suala hilo IEBC. Hata hivyo, alisema Nasa walitaka waangalizi hao wazifanyie kazi nyaraka hizo.
“Kwa mtu kama sina utaalamu wa teknolojia kuniambia nichunguze ni sawa na kuniambia nifanye kazi ambayo sina ujuzi,” alisema Mbeki.
Aliongeza kuwa kazi ya waangalizi ni kuangalia ni sio kuchunguza kwa kuwa jukumu lao ni kuangalia namna mchakato ulivyofanyika iwapo ulifuata sheria za nchi na taratibu za kuheshimu demokrasia walizojiwekea katika Umoja wa Afrika.
Alisema tuhuma zote zilizotolewa na Nasa wameziwasilisha kwa mamlaka husika ndani ya Kenya.
Kwa upande wake, mkuu wa ujumbe wa waangalizi wa Jumuiya ya Madola, Rais wa zamani wa Ghana, John Mahama alisema walikutana na Odinga na ujumbe wake ambao walitoa madai ya kompyuta za IEBC kuvamia huku wakiwa na nyaraka kama ushahidi wao.
Hata hivyo, Mahama alisema nao waliwaeleza kwamba hawana utaalamu wa teknolojia hiyo, lakini jukumu lao ni kuangalia kama utaratibu wa uchaguzi ulifuata sheria na katiba ya nchi na madai mengine ya ukiukwaji wa taratibu yana utaratibu wake uliowekwa kwa mujibu wa sheria.

Mwanafunzi awa mbunge
Aliyekuwa mgombea ubunge wa Igembe Kusini nchini humo, John Mwirigi (23) alishinda nafasi hiyo baada ya matokeo kutangazwa na IEBC.
Mwirigi ambaye anatajwa kuwa mbunge mwenye umri mdogo kuwahi kutokea aliwashangaza wengi katika kampeni ambapo alikuwa akitumia baiskeli na bodaboda.
Mbunge huyo mpya ambaye ni mwanafunzi wa Shahada ya Elimu katika Chuo Kikuu cha Mount Kenya alikuwa mgombea binafsi na hakuwahi kuwa na matangazo kwa kile kilichodaiwa ni kutokuwa na fedha za kufanyia kazi hiyo.
Katika matokeo hayo, Mwirigi alipata kura 18,867 huku mgombea wa Jubilee, Rufus Miriti akipata kura 15,411.

Wagombea wakubali matokeo
Aliyekuwa mgombea wa urais, Dk Ekuru Aukot amekubali kushindwa akifuatiwa na Dk Japheth Kavinga Kaluyu kukubali kushindwa juzi.
Dk Aukot alisema anaamini, “Wachache walipata fursa ya kusikika na wengi walishinda.”
“Jiwe la Daudi halikumuweza Goliathi wakati huu na asiyekubali kushindwa si mshindani.”
Licha ya kukubali kushindwa alitamka kuwa nchi hiyo isingekuwa na demokrasia bila ya Raila Odinga
Alimtaka Rais Kenyatta akitangazwa mshindi, aunde Serikali ya mseto na asiwabague wapinzani wake.
Pia, Dk Aukot alisema licha ya kushindwa kwake, lakini atawania tena urais mwaka 2022.

Nkurunziza ampongeza Kenyatta
Hata kabla ya matokeo rasmi ya uchaguzi nchini humo kutangazwa, Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza alituma ujumbe wa kumpongeza Uhuru Kenyatta kuwa mshindi katika akaunti ya Twitter.

Waangalizi wakubali
Mwenyekiti wa IEBC, Wafula Chebukati alisema taarifa za awali za waangalizi wa uchaguzi wa nchini humo na wale wa nje, wote wanakubali kwamba uchaguzi ulikuwa wa wazi, huru na wa haki.
“Tumefanya kila tuwezalo kuhakikisha uchaguzi umekuwa huru na wa haki,” alisema.
Kiongozi wa waangalizi wa uchaguzi wa Umoja wa Afrika (AU), Thabo Mbeki alisema shughuli ya upigaji kura nchini Kenya ilikuwa ya uwazi na waangalizi hao waliridhishwa na shughuli hiyo.
Hata hivyo alisema kulikuwa na changamoto kadhaa, mfano ingawa karatasi zilikuwa za rangi tofauti pamoja na masanduku, kulikuwa na rangi mbili ambazo zilikuwa zinakaribiana.
Hata hivyo, alisema maofisa wa uchaguzi waliwasaidia wapiga kura kutofautisha rangi hizo.
Mbeki aliipongeza pia Serikali na IEBC kwa kuhakikisha wafungwa wanapiga kura.
“Tunafahamu kwamba IEBC bado inahesabu na kukagua matokeo. Shughuli ya uchaguzi bado inaendelea, hivyo bado ni mapema. Hata hivyo, waangalizi wa AU wanafurahi kwamba uchaguzi ulikuwa wa amani, siku ya uchaguzi watu walifika kwa wingi na waliruhusiwa kupiga kura kwa kufuata taratibu za uchaguzi Kenya na zinazokubaliwa na AU,” alisema.

Thursday, August 10

NISHATI

WADAU WA NISHATI KUTOKA UMOJA WA ULAYA NA TANZANIA WAKUTANA KUJADILI MFUMO WA NISHATI KATIKA MAJENGO MAKUBWA NCHINI


Mtoa mada kutoka Mradi wa Matumizi bora ya Nishati katika Majengo Makubwa Kutoka Umoja wa Ulaya,Margareta Zidar akizungumza na Wadau wa Nishati katika semina Maalum iliyoandaliwa na Umoja wa Ulaya kwa kushirikiana na Wizara ya Nishati na Madini juu ya Matumizi ya Nishati katika Majengo Makubwa.



Mtoa mada kutoka Mradi wa Matumizi bora ya Nishati katika Majengo Makubwa Kutoka Umoja wa Ulaya, Lena Lampropoulou, akizungumza na Wadau wa Nishati katika semina Maalum iliyoandaliwa na Umoja wa Ulaya kwa kushirikiana na Wizara ya Nishati na Madini juu ya Matumizi ya Nishati katika Majengo Makubwa.



Wadau mbalimbali wa Masuala ya Nishati katika Majengo Makubwa wakiwa wanafuatilia mada katika Semina hiyo ya Nishati katika Majengo Makubwa



Wadau kutoka Wizara ya Nishati na Madini na Tasisi Binafsi wakifatilia mada mbalimbali zilizowasilishwa katika mkutano huo muhimu kwa ajili ya Nishati za Mjengo Makubwa



Wadau kutoka Wizara ya Nishati na Madini na Tasisi Binafsi wakifatilia mada mbalimbali zilizowasilishwa katika mkutano huo muhimu kwa ajili ya Nishati za Mjengo Makubwa



Wadau wa Masuala ya Nishati ya Majengo Makubwa kutoka nchini Tanzania na Ujumbe kutoka Umoja wa Ulaya wakiwa katika picha ya Pamoja mara baada ya ufunguzi wa Semina yao ya masuala ya Nishati katika Majengo Makubwa iliyofanyika Serena Hotel Dar es Salaam.

JESHI LA POLISI


MASAUNI AKAGUA UJENZI WA VITUO VYA POLISI, AFANYA MKUTANO NA ASKARI WA USALAMA BARABARANI NA MADEREVA BODABODA


Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akimuuliza maswali Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Hashim Mgandilwa, wakati alipotembelea Ujenzi wa Kituo cha Polisi Mjimwema, Wilayani Kigamboni   kukagua maendeleo ya ujenzi huo. Kulia ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Temeke, Gilles Muroto na anayefuatia ni Mkuu wa Utawala Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Benadict   Kitalika.



 Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Hashim Mgandilwa, akimuonyesha eneo linapotakiwa kujengwa kituo cha Polisi Kibada, Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, wakati wa ziara ya naibu waziri,wilayani Kigamboni, Dar es  Salaam.


 
Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia), akikagua moja ya chumba cha mahabusu ndani ya kituo cha Polisi Mwasonga, wakati wa ziara ya ukaguzi wa vituo vya polisi wilayani Kigamboni, jijini Dar es Salaam.Katikati ni Mkuu wa Wilaya hiyo, Hashim Mgandilwa.



 Muonekano wa nje wa Kituo cha Polisi cha Mwasonga kilichopo wilayani Kisarawe, kikiwa katika hatua za mwisho kabla ya ujenzi wake kukamilika.



 Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza na madereva bodaboda wakati wa ziara ya kikazi wilayani Kigamboni   ambapo aliwaasa madereva hao kufuata sheria za usalama barabarani pindi wafanyapo shughuli zao ili kuepuka ajali.



 Muendesha Bodaboda wa Wilaya ya Kigamboni, Said Athumani, akimuuliza maswali   Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (hayupo pichani), wakati wa Mkutano ulioitishwa na naibu waziri huyo wakati wa ziara ya kikazi wilayani humo. 



Muendesha Bodaboda wa Wilaya ya Kigamboni, Fredrick Swai, akimuuliza swali   Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (hayupo pichani), wakati wa Mkutano ulioitishwa na naibu waziri huyo wakati wa ziara ya kikazi wilayani humo. 
Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

SERIKALI YAMALIZA SINTOFAHAMU YA TANI 3,700 ZA TUMBAKU.


 SERIKALI imefanikiwa kumaliza sintofahamu ilikuwepo baina ya wakulima na wanunuzi wa tumbaku mkoani Tabora juu ya uwepo wa tani 3,700 zilizokosa soko.

Tani 3,700 zilikuwa zimekosa wanunuzi kwa sababu hazikuwa na mkataba kati ya wakulima na wanunuzi na hivyo kuhitaji utatuzi wa haraka wa Serikali ili kuinusuru tumbaku hiyo.

“Tumefanikiwa kuongea nao na tutauza zile tani 3,700 kwa wanunuzi,” alisema Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na kuamsha shangwe ukumbi mzima.

Waziri Mkuu alitoa ahadi hiyo jana jioni (Jumatano, Agosti 9, 2017) wakati akizungumza na wadau wa zao la tumbaku zaidi ya 600 wakiwemo wabunge, viongozi wa dini, chama na Serikali kwenye mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Isike-Mwanakiyungi, mjini Tabora.

Aliwashukuru wanunuzi kwa kukubali kumaliza tatizo hilo kwani litaleta ari mpya kwa wakulima na kuwafanya wajipange vizuri kwa msimu ujao. “Makampuni ya ununuzi yatapita kwenye maeneo yenu, WETCU watafuatilia na tumekubaliana nao kuwa tutafanya kazi pamoja,” alisema Waziri Mkuu.

Kufuatia sintofahamu hiyo, wiki iliyopita, wakazi wa mkoa huo waliomuomba Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli aingile kati ili kuwanusuru na adha ya zao hilo kukosa soko. Naye akawaahidi wananchi hao kwamba suala hilo atalikamilisha Waziri Mkuu.

Mapema, Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Bw. Aggrey Mwanri wakati akiwasilisha muhtasari wa taarifa ya mkoa huo alisema katika masoko ya tumbaku yanayoendelea, kuna tatizo la tumbaku kukosa  wanunuzi kwani hapakuwa na mkataba kati ya wakulima na wanunuzi.

“Tumbaku inayofikia kilo milioni 3.7 kwa sehemu kubwa ililimwa kwa ufadhili waWETCU Ltd, kwa fedha ambazo zilikuwa ziende APEX. WETCU walinunua pembejeo na kuwapa wakulima waliokuwa chini ya vyama sinzia, na sasa haina wanunuzi. Tunaomba ulisemee hilo ili tupate ufumbuzi wa suala hili,” alisema.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Wabunge wa Mkoa wa Tabora ambaye pia ni mbunge wa Urambo, Mheshimiwa Margareth Sitta aliiomba Serikali ikubali kuliangalia suala hilo la tani za ziada 3,700 kwani wakulima wamejaza tumbaku majumbani mwao na kwenye maghala.

“Wakulima wetu wanahitaji kuuza hii tumbaku ili wapate fedha za kuanzia msimu ujao wa kilimo. Lakini pia tunaomba liangaliwe suala la upangaji madaraja ya tumbaku, wasaidiwe kukabili bei isiyotabirika na kutatua ukosefu wa soko la uhakika,” alisema Mama Sitta.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
ALHAMISI, AGOSTI 10, 2017.

SEVEN OPPORTUNITIES IN THE UGANDA-TANZANIA PIPELINE PROJECT AND HOW TO PARTICIPATE.


7 Opportunities in the Uganda-Tanzania Pipeline Project and How to Participate.
THE EAST African oil pipeline (or the Uganda-Tanzania pipeline is the talk of the town now. Not only in East Africa but all over the globe.
The construction of this pipeline is officially on. Social and resettlement planning services have been undertaking it in Tanzania.

The sad reality is that people don’t know about the business opportunities available in the project.
More and more people keep wondering what the opportunities emerging in this project are and how they can be part of it.
“Do they offer equipment or provide services?” they ask themselves.
If you are among these people seeking to do business in this projects but have no idea how to get started, then no need to worry.
This article shows you some opportunities available in the project and how you can participate so that you can reap a substantial profit.
The Tanzania-Uganda Pipeline Opportunities
  1. Pipes and connection supplies: One of the opportunities in this project is to supply and manufacture seamless tubes and pipes (LSAW) and also supplying steel pipes.
  2. Chemical Supplies: For the construction of the pipelines, there are a lot of specialty chemicals needed, from corrosion inhibitors additives to scale remover to chemicals that reduce paraffin build up. You cannot run a pipeline without these things, and you can get them from China really cheap. Which means your profit margin may increase by 30-50 percent.
  3. Pipeline equipment supplies: These cover all materials that are required in the pipeline transportation system. It includes fittings, valves, scraper traps, insulating flanges, flow tee, pumping station, etc.
  4. Civil engineering works: These include building construction work, construction and maintenance of roads, construction and maintenance of drainage system, etc.
  5. Pipeline inspection services.
  6. Food supply.
  7. Security services.
Are you ready to utilize opportunities in this project? Here is how to grab the opportunities:
1. Identify the decision makers and influencers in this Uganda-Tanzania pipeline project.
The first step in pursuing opportunities in the Uganda-Tanzania pipeline is determining who the decision makers are.
Decision makers are the people who can approve or disapprove your proposal.
No matter how big a company is, there are decision makers who can approve or disapprove documents.
This can be easily achieved by making a list of key players in the project and starting to build long term relationship with them.
2. Demonstrate your experience.
You should demonstrate that you are the right person to execute the project you’re proposing.
You should demonstrate your capability and your experiences in executing similar project.
“What if my business is small and new n the industry?” you may ask.
Well, the answer is pretty simple. You still have a chance to tap opportunities in the Uganda-Tanzania pipeline project.
If your business is small and new, and you don’t have any experience or working history to be taken as references to the service you want to render, you should consider going into a joint venture with an experienced contractor in the oil and gas industry in such bidding venture. However inexperienced, you still have a chance to participate in this work.
You have learned the opportunities in the East Africa pipeline project and you now know how to access them.
If you want to learn more about the opportunities in the Tanzanian oil and gas sector and how you can grab them,