Saturday, August 5

Wadau wataka mfumo wa mitihani utazamwe upya


HALMASHAURI ya Mji wa Kibaha mkoani Pwani imehimizwa kuzingatia umuhimu wa kutenga asilimia moja ya mapato ya ndani kwa ajili ya kukabili changamoto zinazowakabili watu wenye ulemavu.
Hayo yalisemwa na Methew Chungu ambaye ni mwezeshaji wa mafunzo yaliyoandaliwa na Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemavu Tanzania (Shivyawata) Kibaha Mjini kwa wadau wa huduma za afya kwa watu wenye ulemavu.
Chungu alisema mapato hayo yatasaidia kuwapatia huduma mbalimbali watu wenye ulemavu zikiwemo za kiafya, elimu, kiuchumi na huduma nyingine za kiutu. Katibu wa Sivyawata Kibaha Mjini, Happiness Matagi alisema kwa sasa changamoto za upataji huduma kwa watu wenye ulemavu zimepungua ambapo kumwona daktari ni bure.
Matagi alisema kupitia kituo chao cha watu wenye ulemavu kilichopo Kwa Mfipa, wanatoa huduma mbalimbali zikiwamo za kiafya hasa kwa watu wenye ulemavu wa viungo pamoja na shughuli za ujasiriamali.
“Pale watu wenye ulemavu wanafanya shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na kufuma, kushona nguo na mradi wa matofali ambao uko mbioni kuanza lengo kuwakwamua watu wenye ulemavu ili wasijione wanyonge na hivyo, waachane na tabia ya kuombaomba ambayo itawafanya washindwe kujitegemea,” alisema Matagi.
Mwakilishi wa Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha, Dk Mariamu Mgaya alisema watu wenye ulemavu wamekuwa wakisaidiwa kwa namna mbalimbali ili kuhakikisha wanapata huduma za afya bila usumbufu kwa kuwapa kipaumbele.
Akijibu baadhi ya hoja, Ofisa Mipango wa Halmashauri ya Mji Kibaha, Amkauane Ngilangwa alisema katika bajeti iliyopitishwa, watu wenye ulemavu wametengewa Sh milioni 10. Alisema pia wanapatiwa vitu mbalimbali ikiwamo mafuta ya kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) ili ngozi zao zisiharibike, pamoja na fimbo kwa ajili ya wasioona.

Bomoabomoa kusomba nyumba za ibada 30, vituo vya afya vitano Dar

Mchungaji wa Kanisa la River Healing Ministry

Mchungaji wa Kanisa la River Healing Ministry of Tanzania, John Kyashama akionyesha kanisa hilo lililopo Kibamba Luguruni jijini Dar es Salaam jana, ambalo ni moja ya nyumba za ibada zilizowekwa x kwa ajili ya kuvunjwa ili kupisha upanuzi wa Barabara ya Morogoro. Picha na Salim Shao 
Zaidi ya nyumba 30 za ibada, vituo vya mafuta sita, vituo vya afya vitano, kituo cha polisi na ofisi ya Kata ya Msigani jijini Dar es Salaam ni kati ya majengo yatakayobomolewa ili kupisha upanuzi wa barabara ya Morogoro.
Wakala wa Barabara nchini (Tanroads) walisema muda wowote wanatarajia kuanza utekelezaji wa kubomoa nyumba zilizowekewa alama ya X katika barabara hiyo kwa madai kuwa tayari muda waliopewa wahusika kubomoa wenyewe umeshamalizika.
Mwananchi ilifanya tathmini kuanzia eneo la Kimara hadi Kiluvya jijini Dar es Salaam na kubaini kuwa makanisa 20 na misikiti 11 itakumbwa na bomoabomoa hiyo kikiwamo kituo cha maombi na maombezi cha Kanisa la Ufufuo na Uzima kinachomilikiwa na Askofu Josephat Gwajima kilichopo eneo la Mbezi Inn.
Makanisa mengine yatakayokumbwa na bomoabomoa hiyo ni Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Kibamba, KKKT Usharika wa Mbezi Luis, Roman Katholiki Kimara litakalobomolewa nusu, The River Hilling Ministry Of Tanzania la Kibamba, Anglikana Stop Over na Calvary Salvation Church lililopo Kibamba.
Makanisa mengine ni Kaprenan lililopo Kibamba, TAG - Suka, Pentekoste Of Tanzania Kiluvya, Nayoth Church Kiluvya, KLPT la Bwawani, Kapernan Centre Mbezi, TAG Carvary Tample Mbezi Inn, GRC Mbezi Inn na TAG Rejoice Center Mbezi.
Hata hivyo, baadhi ya makanisa yameshabomolewa kutii agizo la kubomoa kwa hiyari likiwamo la Moravian Kimara Stop Over na KKKT Kibamba ambako leo wanafanya ibada ya mwisho kabla ya kuhamia eneo jipya.
Misikiti itakayokumbwa na bomoabomoa hiyo ni Masjid Kilumbi Islamic Center - Kimara Mwisho, Dalul Mustafah wa Kimara Stop Over, Masjid Baitul Maamur, Masjid Jaaria, Masjid Baitul Maamur na Almasjid Nuur iliyopo Kiluvya.
Misikiti mingine ni Masjid Jaalia Gogan, Masjid Nuur Kibamba CCM.Pia immo misikiti mitatu ya Mbezi Inn, Mbezi Luis na Temboni.
Vituo vya mafuta vinavyotakiwa kubomolewa ni Henry Filling Station Mbezi kwa Yusuph, Camel Oil- Kibamba, Uduru Oil Station-Kibamba, Total Stop Over na Camel Oil Kimara Stop Over.
Mbali na hilo, vituo vya huduma za afya vitakavyoguswa ni Hospitali ya Boch na Kituo cha Afya cha Kimara vitakavyobomolewa nusu, Hospitali ya Neema iliyopo Kimara Stop Over, Kimara Centre Dispensary na Zahanati ya Arafa.
Wakizungumzia bomoabomoa hiyo, baadhi ya masheikh na wachungaji walisema wamepokea maagizo ya Serikali ya kutakiwa kuvunja majengo yao huku wengine, wakimuomba Rais John Magufuli kuwatazama kwa jicho la huruma.
Imamu wa Msikiti wa Jamsjid Jaria wa Kiluvya, Haidary Masenga alisema waumini wameathirika kisaikolojia kwa kutojua msikiti huo utakakohamishiwa kwa kuwa hakuna eneo walilopata.
“Ni kweli maendeleo yanahitajika na sisi hatupingi, lakini tunaomba tutazamwe kwa jicho la huruma tuachwe tuendelee kuabudu hapa. Mpaka sasa hatujui chochote tunasubiri tu hatima ya Serikali kama watavunja au la,” alisema.
Imamu Msaidizi wa Msikiti wa Kilumbi Islamic Center, Halfan Malima alimuomba Rais Magufuli kuwahurumia kwa kuwapa eneo jingine la ibada kwa kuwa bado hawajapata.
Kwa upande wake, Mchungaji wa KKKT Kibamba, Mshiu Wilness alisema kanisa limepokea agizo la kutakiwa kuhama na kubomoa jengo hilo na kwamba, tayari wameshapata eneo jingine ambalo wanatarajia kuhamia. Alisema leo kutakuwa na ibada ya mwisho kwa ajili ya kuondoka kwenye eneo hilo.
“Tumepokea, tunatarajia kuondoka na tutavunja kama tulivyoelekezwa,” alisisitiza kiongozi huyo.
Mchungaji wa Kanisa la The River Healing Ministry of Tanzania, John Kyashama alisema anaunga mkono agizo la Serikali la kubomoa nyumba, makanisa, misikiti ili kupisha upanuzi wa barabara.
Kyashama alisema hana kinyongo na Rais na anaunga mkono mipango ya maendeleo anayoifanya na anawashauri wachungaji wenzake waliokumbwa na bomoabomoa kukubaliana na hali hiyo kwa kuwa kinachofanywa na Serikali ni kwa nia njema na wananchi wake. “Si vizuri kuwa na kinyongo wala kugombana na utawala, kila mtu atii mamlaka za nchi,” alisema.
Mbali na nyumba hizo, pia Kituo Kikuu cha Polisi Mbezi Luis kitabomolewa huku Kamanda wa Polisi Kinondoni, Muliro Jumanne akisema kilijengwa kwa nguvu ya wananchi kutokana na mahitaji ya eneo hilo wakati huo.
Alisema kutokana na kuwekwa alama X, kituo hicho kitahamishiwa eneo la Gogoni kwa kuwa licha ya kuwa barabarani bado eneo lake ni dogo.
“Kituo hiki kitaondolewa hapa na kupelekwa kwenye kituo kingine cha Gogoni kilichojengwa chini ya mradi wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN),” alisema.
Alisema kituo hicho kipya pia kimeshirikisha nguvu za wananchi na ndicho kikubwa kwa Wilaya ya Ubungo.

Mbunge wa Tarime akamatwa, aachiwa


Kamatakamata ya wabunge wa upinzani imeendelea na jana ilimkumba John Heche wa Tarime Vijijini (Chadema), ambaye alishikiliwa na polisi kwa saa sita na kuachiwa akidaiwa kutoa kauli za uchochezi bungeni na kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Sirari wilayani Tarime.
Kamanda wa Polisi Tarime/Rorya, Henry Mwaibambe alisema jana kuwa licha ya kumwachia, kesho (Jumapili) atatakiwa kuripoti tena polisi.
Kukamatwa kwa Heche, kunafanya wabunge wa Chadema waliokamatwa na polisi katika kipindi cha siku 30 zilizopita kwa makosa mbalimbali ikiwamo uchochezi na kufanya mikutano bila kibali, kufikia sita.
Wengine waliokamatwa ni, Halima Mdee Julai 4 kwa madai ya kumkashifu Rais John Magufuli katika mkutano wake na wanahabari jijini Dar es Salaam.
Mdee alifuatiwa na Zubeda Sakuru (Viti Maalumu) na Cecil Mwambe wa Ndanda waliokamatwa Nyasa mkoani Ruvuma Julai 15 wakiwa na katibu mkuu wa chama hicho, Dk Vincent Mashinji pamoja na viongozi wengine watano kwa tuhumu za kufanya mkusanyiko usio halali.
Mbali na hao, pia yumo Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu aliyefuatia kukamatwa Julai 20 katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kwa tuhuma za uchochezi katika mkutano wake na wanahabari
Baada ya Lissu alifuata Pascal Haonga (Mbozi) aliyekamatwa Agosti 2, akidaiwa kufanya mkutano bila kibali katika eneo la Vwawa Mjini.
Akizungumza na mwandishi wetu muda mfupi baada ya kuachiwa na polisi, Heche alisema alishikiliwa kwa makosa mawili; kutoa kauli ya kuhamasisha zao la bangi liwe la biashara kama ilivyo mirungi nchini Kenya na kuhamasisha wananchi wakavamie mgodi, kauli aliyoitoa akiwa bungeni.
“Nilikwenda polisi mwenyewe saa nne asubuhi (jana) baada ya kusikia katibu wangu ameitwa, nilipofika nilisalimia vizuri na askari na wakanieleza kwamba afadhali nimefika, lakini wakati hayo yakiendelea ghafla niliona idadi ya polisi ikiongezeka na nikaambiwa nipo chini ya ulinzi,” alisema Heche.
Alisema baada ya hatua hiyo watu wake wa karibu walianza kufanya utaratibu wa dhamana na kufanikiwa kupata na polisi walimweza kwamba anatakiwa kuripoti tena kituoni hapo kesho saa nne asubuhi kwa ajili kuandika maelezo.
Hata hivyo, Heche alisema nyuma ya pazia ya kukamatwa kwake ni shinikizo la kisiasa linalofanywa na watu fulani wa Tarime kwa lengo la kumkomoa ili asitekeleze vyema majukumu yake.
“We mambo yametokea Machi na ishu nyingine nimezingumza bungeni eti leo wanakuja kunikamata. Nawaambia siwezi kunyamazishwa katika kutetea masilahi ya wananchi wangu. Nitahakikisha nitaendelea kuwapigania hadi wanufaike na rasilimali zao,” alisema.
Alisema polisi bado wanaishikilia simu yake moja ya mkononi kwa lengo la kuichunguza.
Awali, Mlimi Zablon ambaye ni katibu wa Heche alisema licha ya kumshikilia mbunge huyo pia walikwenda nyumbani kwake kufanya upekuzi uliochukua takribani saa moja.
Katibu wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema alilaani hatua hiyo akidai jeshi la polisi limekiuka Sheria ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge pamoja na Ibara ya 100, juu ya kinga aliyonayo mbunge.
“Inawezekanaje mbunge akamatwe kwa kauli aliyotoa ndani ya Bunge? Kwa hivyo tunalaani na tunamtaka Spika wa Bunge atoe tamko la kukamatwa kwake dhidi ya kauli aliyoitoa akiwa bungeni,” alisema Mrema.
“Kauli alitoa Februari iweje leo ndiyo wamkamate? Hali hii hatuwezi kukubaliana nayo, kwa sasa wanamshikilia Heche lakini wanasema wanamtafuta na Ester Matiko waliyekuwa naye katika mkutano huo,” alidai. Hata hivyo, polisi haijatangaza kumtafuta mbunge huyo wa Tarime Mjini.

Mjane aliyemlilia Magufuli akamatwa akiandaa banda la chakula


Mwanamke aliyeangua kilio mbele ya Rais John Magufuli wakati wa maadhimisho ya siku ya sheria jijini Dar es Salam, Februari 2, mwaka huu, Swabaha Shosi amekamatwa na polisi mjini hapa akiwa katika Uwanja wa Chongoleani. Swabaha ambaye baada ya tukio hilo alijizolea umaarufu na kupachikwa jina la ‘mjane wa Magufuli’ alikamatwa jana wakati akiandaa banda la kuuzia chakula kwa ajili ya kuwauzia watu watakaohudhuria sherehe za uzinduzi wa mradi wa bomba la mafuta kutoka Hoima nchini Uganda hadi Tanga.
Mwanasheria wa mwanamke huyo aliyejitambulisha kwa jina la Shukuru Khalifa alisema mteja wake alikamatwa mchana alipokuwa akiandaa banda hilo.
“Anasema akiwa Chongoleani wakati akiendelea na maandalizi, alipigiwa simu na mkuu wa polisi wa Wilaya ya Tanga akiulizwa yuko wapi, alipojibu alipo baada ya muda mfupi alifuatwa na askari akapelekwa kituo cha Chumbageni” alisema Shukuru. Mwanasheria huyo alisema alipokwenda katika kituo hicho kwa ajili ya kumdhamini alizuiwa kwa madai kwamba mwanamke huyo anadaiwa kufanya biashara eneo ambalo haliruhusiwi.
Shukuru alisema anadhani mteja wake alikamatwa baada ya vyombo vya dola kujenga hisia kwamba anaweza kuandaa bango ili kulionyesha kwa Rais Magufuli kama alivyofanya jijini Dar es salaam.
“Ukweli ni kwamba Swabaha hakuwa na nia ya kumwendea Rais, alikwenda kuweka banda ili afanye biashara kama ilivyo kwa wengine na alifuata taratibu zote akaruhusiwa,” alisema Shukuru.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Benedict Wakulyamba alipotafutwa kuelezea tukio hilo simu yake iliita bila kupokewa.

Bomba la mafuta kupita mikoa minane,vijiji 184


Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kaleman amesema mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima, Uganda hadi Bandari ya Tanga, utapita katika mikoa minane, vijiji 184 hapa nchini.
Amesema vijiji hivyo vinapatikana katika wilaya 24 zilizopo katika mikoa ya Kagera, Geita, Shinyanga, Tabora, Singida, Dodoma, Manyara na Tanga. Bomba hilo litakalogharimu Sh8 trilioni, litakuwa na urefu wa kilomita 1,450.
"Katika vijiji hivyo mradi utapita na wanakijiji watapitiwa na fursa za mradi, ajira 10,000 wakati wa ujenzi zitapatikana na itasaidia kupunguza umasikini,pia kuna megwati 35 zitapatikana kupitia mradi huu,"alisema.
Kauli hiyo ameitoa leo Jumamosi wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi katika mradi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima Uganda mpaka Chongoleani Tanga.
Wakuu wa mataifa, Yoweri Museveni na mwenyeji wake, Rais John Magufuli na Serikali wanaongoza sherehe hizo wakiwa wameambatana na na mawaziri, wabunge huku wananchi wakiwa wamejitokeza kwa wingi kufuatilia shughuli hiyo

Shigella aanza kutafuta ardhi ya makazi wa wawekezaji


Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martin Shigella amesema uongozi wa mkoa huo tayari umeshaanza kuandaa mazingira ya kusaidia upatikanaji wa maeneo ya ardhi kwa ajili ya ujenzi wa makazi ya wawekezaji wakati wa utekelezaji wa mradi wa bomba la mafutaghafi kutoka Hoima, Uganda, hadi bandari ya Tanga.
Shigella amesema mbali na hatua hiyo, pia imewahakikishia wawekezaji na Watanzania kupata maeneo ya ofisi zitakazohusika kwenye utekelezaji wa mradi huo.
Kauli hiyo ameitoa leo Jumamosi wakati wa sherehe za uwekaji jiwe la msingi la mradi huo zinazoendelea katika kijiji cha Chongoleani, mkoani Tanga. Katika sherehe hizo, Rais John Magufuli na mgeni wake, Yoweri Mseveni ambaye ni Rais wa Uganda wataweka jiwe hilo ikiwa ni hatua ya ufunguzi wa mradi
"Tumeshaanza kuhimiza watoto wetu waende vyuoni ili wapate ujuzi utakaowasaidia kuajiriwa wakati wa mradi, fursa zilizopo zitasaidia kuinua kipato cha wakazi na kupunguza umasikini,kwa hiyo mheshimiwa Rais wakati wa Tanga wanaomba useme neno moja tu na roho yao itapona,"alisema.

Askofu Gwajima anunua ndege ya Sh 2.64 bilioni


Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amenunua ndege yenye thamani ya Sh2.64 bilioni kwa ajili ya kusambaza injili.
Kabla ya Askofu Gwajima kusema kiasi alichonunulia ndege hiyo aliweka picha kwenye mtandao wake wa Instagram akiwa mbele ya ndege hiyo akisema hivi karibuni ataileta Tanzania kwa ajili ya kusambaza injili kwenye ufalme wa Mungu.
Akizungumza na Mwananchi jana jioni, Askofu Gwajima alisema aliijaribisha ndege hiyo juzi nchini Marekani kutoka uwanja mmoja kwenda mwingine.
Alisema taratibu za kimaandishi zikikamilika serikalini, ndege hiyo itakuwa nchini ndani ya wiki tatu.
“Heshima kwa Mungu wetu! Ni ya kwetu wote mdogo wangu, siku moja nikupeleke kwenda kuandika habari mahali,” Askofu Gwajima alimwambia mwandishi wa habari hii.

Kagame aibuka kidedea


Tume ya Uchaguzi nchini Rwanda inasema kuwa Paul Kagame ameshinda uchaguzi wa uraisi uliyofanyika jana Ijumaa nchini humo.
Tume hiyo imesema matokeo ya awali yameonyesha kuwa Rais Kagame alishinda kwa asilimia 98 ya kura ambazo tayari zimeshahesabiwa hadi hivi sasa.
Ushindi huo unamaanisha kuwa Rais Kagame ambaye amekuwa madarakani kwa miaka kumi na saba sasa ataendelea na awamu ya tatyu ya miaka saba.
Wafuasi wake wanamsifu Kagame kwa kuleta utulivu na maendeleo ya kiuchumi nchini humo baada ya mauaji ya kimbari ya mwaka 1994 ambapo maelfu ya watu waliuawa.
Wapinzani wa Kagame walikuwa ni Frank Habineza na Philippe Mpayimana.

Magufuli ampokea Museveni Chongoleani


Rais wa John Magufuli na Rais wa Uganda Yoweri Museveni wamewasili kijini Chongoleani mkoani tanga kwa ajili ya uwekaji wa jiwe la msingi kuzindua ujenzi wa bomba la kusafirisha mafura ghafi.
Bomba hilo litatumika kusafirisha mafuta hayo kutoka Hoima nchini Uganda ambako yatachimbwa hadi bandari ya Tanga.
Pamoja na marais hao wawili, shughuli hiyo pia inahudfhuriwa na viongozi wengine wa juu akiwamo makamu wa rais, Samia Suluhu hassan na waziri Mkuu, kassim majaliwa.
Naibu Spika wa Bunge, Dk Tulia Akcson pia anahudhuria shughuli hiyo sambamba na Waziri wa Uchukuzi Mawasiliano na Ujenzi, Profesa Makame Mbarawa pamoja na Spika wa zamani wa Bunge, Anne Makinda.
Baada ya kuweka jiwe la msingi eneo la Chongoleano, marais hao wawili wanatarajiwa pia kufanya hivyo huko Hoima katika tarehe itakayotangazwa baadaye.

Licha ya mahakama kuwapa dhamana, Chadema 51 waendelea kusota ndani


Usemi wa haki iliyocheleweshwa ni haki iliyonyimwa, ambao ni maarufu miongoni mwa wanasheria, huenda ukawa na maana kubwa kwa viongozi na wanachama 51 wa Chadema ambao wanaendelea kusota katika mahabusu ya Gereza la Wilaya ya Biharamulo tangu Julai 10, licha ya kutimiza masharti ya kuachiwa kwa dhamana.
Viongozi hao walikamatwa Julai 7 mwaka huu, baada ya polisi kuvamia kikao chao cha ndani kilichokuwa kinafanyika katika ukumbi wa Manzagata ulioko Kata ya Muganza wilayani Chato.
Baada ya kukamatwa, walifikishwa mahakamani Julai 10, kwa kosa la kusanyiko lisilo halali na kunyimwa dhamana baada ya upande wa mashtaka kuwasilisha hati ya kiapo iliyosainiwa na Mkuu wa Polisi wa Wilaya (OCD) ya Chato, Alex Mkama kupinga dhamana.
Hata hivyo, Julai 26 Mahakama mbele ya Hakimu Mkazi wa Wilaya ya Chato, Jovith Kato ilitupilia mbali ombi la zuio la dhamana baada ya kukubaliana na hoja za wakili wa utetezi, Siwale Yisambi kuwa Kifungu cha 148 (5) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai kilichotumiwa na upande wa mashtaka kuwasilisha zuio la dhamana hakiendani na ombi hilo.
“Pamoja na kukubaliana na pingamizi za upande wa utetezi, Mahakama hii inaruhusu washtakiwa kuachiwa kwa dhamana kwa sababu sheria inaelekeza kwamba ni marufuku mtu anayeshtakiwa kwa kosa la jinai kutendewa kama mwenye kosa hilo hadi pale itakapodhihirika pasipo shaka kuwa ana hatia,” alisema Hakimu Kato katika uamuzi wake.
Licha ya kuachiwa kwa dhamana, viongozi na wanachama hao wa Chadema wameendelea kusota mahabusu kwa kile kinachoelezwa kuwa Jeshi la Polisi lenye dhamana ya kuwaleta mahakamani, limekosa usafiri wa kuwatoa Biharamulo hadi mahakamani Chato ili kukamilisha utaratibu wa kuachiwa kwa dhamana.
Hadi jana, Hakimu Kato alikuwa amekamilisha kupitia barua 102 za wadhamini wa washtakiwa hao ambao kila mmoja alitakiwa kuwa na wadhamini wawili watakaosaini hati ya dhamana ya Sh500,000 kila mmoja.
Akizungumzia kwa simu juzi, Hakimu Kato alisema Mahakama imetimiza wajibu kwa kutoa dhamana kwa washtakiwa kwa kupitia na kujiridhisha juu ya usahihi wa barua za wadhamini, kazi ya kuwafikisha mahakamani washtakiwa imebaki mikononi mwa Jeshi la Polisi.
Akijibu malalamiko ya viongozi wa Chadema kuhusu washtakiwa kuendelea kusota mahabusu licha ya kutimiza masharti ya dhamana, hakimu huyo alisema suala hilo uulizwe uongozi wa Jeshi la Polisi kwani ndiyo wenye majibu ya kwa nini hauwafikishi washtakiwa hao mahakamani kulingana na hati za kuwatoa gerezani zinazotolewa na mahakama kila shauri linaposikilizwa.
“Kwa mara zote nne shauri hili liliposikilizwa, Mahakama imetoa hati za kuwatoa mahabusu na kuwafikisha mahakamani washtakiwa; lakini hawajaletwa kwa kile polisi wanachoeleza ni kukosekana kwa usafiri. Jukumu la kuwafikisha washtakiwa mahakamani ni la polisi kwa wale ambao wako mahabusu,” alisema Kato.
Juhudi za kumpata Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Mponjoli Mwabulambo ili azungumzie suala hilo ziligonga mwamba baada ya mwandishi kujaribu kumtafuta kwa simu bila ya mafanikio na baadaye kufika ofisini kwake ambako alielezwa kwamba alikuwa katika kazi za nje.
Alielekezwa aonane na Ofisa Mnadhimu wa Mkoa, Stanley Kalyamo ambaye hata hivyo, alikataa kuzungumza kwa maelezo kwamba Kamanda Mwabulambo yupo ndani ya mkoa hivyo aendelee kutafutwa.
Akizungumzia suala hilo, Makamu Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Ziwa Victoria, Ansbert Ngurumo alisema chama hicho kinaamini polisi wanafanya makusudi kutowafikisha mahakamani washtakiwa hao ili waendelee kusota mahabusu kinyume cha sheria kwa sababu wametimiza masharti ya dhamana.
Alihoji sababu ya polisi kuwapeleka washtakiwa hao mahabusu ya Wilaya ya Biharamulo katika Mkoa wa Kagera, umbali wa zaidi ya kilomita 100, badala ya Geita ambako ni karibu na kunafikika kirahisi.

Friday, August 4

A CLIMATE CHANGE INSPIRED PROJECT LAUNCHES IN DAR ES SALAAM


The Kilimanjaro Project, a climate change inspired project, held a meeting with environment stakeholders and members of the press to introduce the project. A prominent business leader, Mr. Ali Mufuruki was the guest of honor during the meeting which also served as the official launch of the project.

The Kilimanjaro Project is an art for change campaign for sustainable futures and climate change awareness, using Mount Kilimanjaro as an indicator that we are experiencing rapidly changing climates and environmental degradation. Through active partnerships, The Kilimanjaro Project will raise awareness through a communications campaign that will inspire sustainable behavioral change.

The Kilimanjaro Project Launch at Seacliff Hotel Dar es Salaam. From left are; An Advisory Board Member, Kelvin Twissa, Project Lead, Sarah Scott and Guest of Honour, Ali Mufuruki.

  The project will use Khangas as a tool to send message and raise awareness. In an installation planned to take place in October 2018, the kilimanjaro project lay six khangas up the six hiking trails of the mountain, each carrying a different message around key aspects of the environment; reforestation, waste management, conservation, water stewardship, and renewable energy. The six khangas will meet at the top of Mount Kilimanjaro, calling for people to come together.   

The Kilimanjaro Project is driven by the vision of better futures for coming generations. The main goal of the project is to raise awareness, enter dialogue, and create solutions around sustainable futures and climate change.


The Guest of Honour, Ali Mufuruki, addresses invited guests during the launch.

Other goals are participating in the Sustainable Development Goals by supporting conservation, tree planting, education and social enterprise / small business development in Tanzania; engaging local communities to participate in solutions for creating a climate resistant future; fundraising for related projects - conservation, reforestation and water resource management and creating active partnerships.

The first edition of the khangas, Tuje Pamoja- Let Us Come Together is available for sale in Dar es Salaam. Dar es Salaam residents can pay for the khangas through Mpesa 5588080 - The Kili Project and pick up khangas at selected points; The Novel Idea bookshop at Slipway, Masaki and at Clouds Media’s offices in Mikocheni. The event which was sponsored by Cool Blue Pure Drinking Water took place at Sea Cliff Hotel in Dar es Salaam on the morning of 3rd August and later in the day followed by a cocktail reception at Kilimanjaro Wonders Hotel in Marangu, Kilimanjaro.



The Project Lead, Sarah Scott, addresses invited guests during the launch. please upload a press release bellow

SSRA YASHIRIKI MAONESHO YA NANENANE YANAYOENDELEA KWENYE VIWANJA VYA NZUNGUNI MKOANI DODOMA


Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Uhamasishaji wa Mamlama ya Usimamizi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Sarah Kibonde Msika (wa pili kushoto) akifafanua jambo kwa wageni waliotembelea banda lao wakati wa Maonesho ya Nanenane yanayofanyika Kikanda katika viwanja vya Nzunguni Mkoani Dodoma.



Afisa wa Mamlama ya Usimamizi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Aminah Kisisa akigawa vipeperushi kwa moja ya wadau waliotembelea Banda la SSRA kwenye Maonesho ya Nanenane Kanda ya Kati.



Afisa wa Uhusiano na Uhamasishaji wa Mamlama ya Usimamizi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Ally Masaninga akifafanua kwa mmoja ya wadau waliotembelea banda la Mamlaka hiyo wakati wa Maonesho ya Nanenane Kanda ya Kati.



Sehemu ya wafanyakazi wa SSRA wakati wa Maonesho ya Nanenane



Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Uhamasishaji wa Mamlama ya Usimamizi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Sarah Kibonde Msika, akimkabidhi mfuko wa SSRA pamoja na Vipeperushi Mratibu wa Maonesho ya Nanenane Kanda ya Kati Bw, Mwinuka, Maonesho hayo yanaendelea Mkoani Dodoma



Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Uhamasishaji wa Mamlama ya Usimamizi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Sarah Kibonde Msika akiwa na wadau waliotembelea Banda la SSRA wakati wa Maonesho ya Nanenane Kanda ya Kati.



Timu ya Mamlama ya Usimamizi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) katika picha ya pamoja wakati wa Maonesho ya Nanenane Kanda ya Kati yanayofanyika katika Viwanja vya Nanenane Mkoani Dodoma.

KWA SIMU TOKA :LONDON- MAHOJIANO MAFUPI KUHUSU KENYA LONDON



DSTV YAZINDUA MSIMU MPYA WA SOKA, LIGI YA UINGEREZA KUTANGAZWA KWA KISWAHILI


Wakati vuguvugu la soka ulimwenguni likizidi kupanda, Kampuni ya Multichoice Tanzania kupitia king’amuzi cha DStv imezindua kampeni maalum ya Msimu mpya wa Soka ijulikanayo kama ‘Full vyenga Bila Chenga’  ambapo watanzania kupitia DStv wataweza kushuhudia mubashara michuano mikubwa ya soka ulimwenguli inayotarajia kuanza hivi karibuni ikiwemo Ligi kuu ya Uingereza (PL) na ligi ya Hispania (La Liga) pamoja na makombe mengine maarufu Duniani.

Pazia la ligi kuu ya uingereza litafunguliwa jumapili Agosti 6 kwa mtanange wa ngao ya jamii kati ya Arsenal na Chelsea mchezo ambao utaonyeshwa  mubashara kupitia DStv.
 Mkurugenzi mtendaji wa Multichoice Tanzania Maharage Chande akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni maalum ya Msimu mpya wa Soka ijulikanayo kama ‘Full vyenga Bila Chenga’, Jijini Dar es salaam.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa msimu mpya wa soka iliyofanyika katika ofisi za Multichoice Tanzania jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi mtendaji wa Multichoice Tanzania Maharage Chande  amesema kuwa msimu huu wa soka, DStv inawahakikishia wateja wake wote kuliona soka katika muonekano bora zaidi huku wakiweza kufuatilia michuano hiyo kwa matangazo yatakayorushwa kwa lugha ya Kiswahili.

“Msimu huu watanzania, kupitia DStv, siyo tu kwamba wataona michuano mbalimbali ya soka ulimwenguni mubashara, bali pia watayaona katika ubora wa hali ya juu yaani High Definition na zaidi ya yote, tutawapatia fursa watanzania kufuatilia ligi kuu ya Uingereza kwa lugha ya Kiswahili”.

Amesema DStv imeendelea kuboresha huduma zake ikiwemo kuongeza vipindi na kurekebisha bei za vifurushi ili kuhakikisha kuwa watanzania wengi zaidi wanapata fursa ya kujionea matukio mbalimbali muhimu katika Nyanja zote za maisha ikiwemo michezo na burudani. Ametoa mfano wa ligi ya Hispania La Liga ambayo inaonekana yote katika kifurushi cha Bomba. Pia baadhi ya mechi za ligi kuu ya Uingereza (PL) pia zitaonekana katika kifurushi cha Bomba.
Kwa upande wake, Meneja Masoko wa Multichoice Tanzania Alpha Mria amesema kampeni ya Full Vyenga bila Chenga inamaanisha kuwa wateja wa DStv, msimu huu wa soka wataweza kuliona soka kwa muonekano bora zaidi, yaani bila chenga. “Tunatambua kuwa washabiki wa soka sasa wanataka walione soka vyema, kana kwamba nao wapo uwanjani. Kwa DStv, sasa hata mtu akilambwa chenga utaiona vyema, hata kama mtu anatoka jasho utaliona. Hakuna wingu wala ukungu, ni ‘full vyenga bila chenga’  alisema Alpha.