Wednesday, June 7

WATOTO WENYE MATATIZO KUPATIWA MATIBABU NCHINI

WATOTO wenye matatizo ya usikivu watapata matibabu ya kupandikizwa vifaa vya usikivu hapa nchini katika Hospitali ya taifa ya Muhimbili badala ya kwenda nje ya nchi kwa matibabu kama ilivyokuwa awali.

Hayo yamesemwa na Waziri wa afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati alipozindua huduma hiyo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili leo jijini Dar es salaam.

“Serikali haitapeleka mgonjwa mwenye matatizo ya kusikia nje ya nchi kwa ajili ya kupandikizwa vifaa vya kusikia na badala yake atatibiwa nchini ili kupunguza rufaa za wagonjwa wan je ya nchi” alisema Mh. Ummy.

Aidha Waziri Ummy amesisitiza juu ya umuhimu wakujiunga na mfuko wa Afya wa Jamii wa NHIF ili kupata fursa ya kutibiwa kwa gharama ndogo zaidi, huku akisisitiza kuwa wananchi wote watakaokuwa na kadi ya NHIF wataweza kupata matibabu ya upandikizaji wa kifaa cha kusikia bure kupata huduma hii.

Mbali na hayo Mh. Ummy ameahidi kuwa Serikali kupitia Wizara yake ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kuunga mkono kwa kuisaidia hospitali ya Muhimbili ili kuendelea kufanikisha upasuaji wa Watoto hivyo kupunguza gharama inayopata Serikali kusafirisha Watoto hao nje ya nchi pindi wapatapo matatizo hayo.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Muhimbili Lawlence Mseru amsisitiza kuwa moja kati ya mipango ya Hospitali ya Muhimbili ni kuhakikisha kuwa wanapunguza idadi ya wagonjwa wanaokwenda kutibiwa nje ya nchi kila mara jambo linaloigharimu Serikali pesa nyingi. 

Aidha Dkt. Mseru aliongeza kuwa licha ya kufanikisha tukio hilo la Kihistoria wanaomba Serikali kupitia Wizara ya Afya kusaidia kuboresha Wodi za Wagonjwa mahututi, ununuzi wa Vifaa tiba, kuongeza vyumba vya upasuaji jambo litalopunguza msongamano wa shughuli za hospitali pia kuongeza Wataalamu waendao nje ya nchi kwaajili ya mafunzo ili kuendeleza huduma katika nchi yetu jambo litakalosaidia kuwa na Wataalamu wengi hivyo kuweza kufanikisha huduma kwa wagonjwa wengi zaidi.

Nae Prof. Sunil Narayan Dutt kutoka Hospitali ya Apollo nchini India ameipongeza Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa jitihada inayoonesha hasa katika kutetea haki za watoto.

Kwa upande Bi. Hilda Bohela ambae ni mzazi wa Apulie Bohela aliyepata huduma hiyo nchini amewasihi wazazi wenzie kuwapeleka watoto kufanyiwa uchunguzi pindi waonapo hali isiyokuwa yakawaida kwa watoto wao na kuachana na mila potofu jambo linalopelekea watoto wengi kupata ulemavu .



waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watot, ummy Mwalimu (katikati) akizungumza leo jijini Dar es Salaam kwenye uzinduzi wa Upasuaji wa Upandikizaji Kifaa cha Usikivu (Cochlear-Implant) kulishoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Profesa Lawrence Museru na kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini Hospitali ya Taifa ya Muhimbili(MNH), Profesa Charles Majinge.
waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, ummy Mwalimu akiwajulia hali wagonjwa waliolazwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili leo jijini Dar es Salaam.
waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, ummy Mwalimu akiwasili katika hospitali ya Taifa Muhimbili leo jijini Dar es Salaam. 
waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, ummy Mwalimu akiwa katika picha ya pomoja na watendaji wa hospitali ya Taifa Muhimbili leo jijini Dar es Salaam.Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii.

Tuesday, June 6

Cisco kuzikwa kesho Kisutu


Balozi Abdul Cisco Mtiro enzi za uhai wake 

By Ephrahim Bahemu, Mwananchi
Dar es Salaam. Mwili wa aliyekuwa Mkuu wa Itifaki Ikulu katika Serikali ya awamu ya tatu na nne, Balozi Abdul Mtiro ‘Cisco’ utazikwa kesho, Jumatano, katika makaburi ya Kisutu jijini hapa.
Cisco ambaye pia aliwahi kuwa Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Ufilipino, Cambodia na Singapore, alifariki juzi katika Hospitali ya Agha Khan alikokuwa akipatiwa matibabu.
Omar Mtiro ambaye  ni mtoto wa kwanza wa marehemu Cisco kati ya wanne, amesema mazishi  yatafanyika kesho  saa 7.00 mchana katika makaburi ya Kisutu.
Omar amesema kabla ya maziko, mwili wake utapelekwa nyumbani kwake Mikocheni B saa 5.00 asubuhi kwa ajili ya kufanyiwa kisomo na sala.
Kuhusu chanzo cha kifo chake Omar amesema, “suala la chanzo cha kifo chake nisingeependa kukizungumzia ibaki kuwa ‘privacy’ (faragha), lakini mzee aliumwa kwa wiki mbili hadi anafikwa na mauti.”
Kufuatia kifo hicho juzi Rais John Magufuli alituma salamu za rambirambi kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki na mabalozi wengine kwa kuondokewa na mpendwa wao.


MAREHEMU NDESAMBURO AZIKWA LEO KIJIJINI KWAKE MKOANI KILIMANJARO


Gari lililobeba mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Phillemon Ndesamburo likielekea kwenye kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Kiboriloni kwa ajili ya kuombewa. Maziko ya Marehemu Ndesamburo yanafanyika leo nyumbani kwake mtaa wa  KDC- Moshi,mkoani Kilimanjaro.
Gari lililobeba mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Phillemon Ndesamburo likiingia kwenye kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Kiboroloni.
Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe akiiingia katika kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Kiboroloni kwa ajili ya kumuaga aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Phillemon Ndesamburo.
Viongozi mbali mbali wa Chadema wakiingia katika kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Kiboriloni.
Viongozi mbali mbali wa Chadema wakiingia katika kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Kiboriloni. Waziri mkuu wa Zamani ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa akiingia kanisani.
Wabunge wa Chadema wakiwa wamejipanga kupokea mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Phillemon Ndesamburo katika kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Kiboriloni.
Wajukuu wa Marehemu Phillemon Ndesamburo wakielekea kanisani.
Mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Phillemon Ndesamburo ukiingizwa kanisani.
Waziri mkuu wa Zamani ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa akibadilishana mawazo na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi katika ibada ya kumuaga aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Phillemon Ndesamburo.
Viongozo wa Chadema wakiwa katika ibada ya kumuombea aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Phillemon Ndesamburo.
Mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Phillemon Ndesamburo ukiwa kanisani tayari kwa maombezi.
Mke wa Marehemu aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Phillemon Ndesamburo (wa pili toka kushoto) akiwa kanisani.

RAIS DKT. MAGUFULI AMUAPISHA MHE ANNA ELISHA MGHWIRA KUWA MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO LEO



 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Anna Elisha Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Anna Elisha Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Ikulu jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Elisha Mghwira Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi ,Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Elisha Mghwira, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Dar es Salaam pamoja na viongozi wengine Ikulu jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara Rodrick Mpogolo akimkabidhi Ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi CCM Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Elisha Mghwira huku Rais Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ,Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ally Salum Hapi pamoja na wakuuu wa Wilaya za Ubungo na Ilala wakipiga makofi. Picha na IKULU

VIJANA WATOA SIRI KUFICHUA MITANDAO YA UHALIFU NCHINI


TAA 2















Zaidi ya vijana wapatao  1230  wametoa siri nzito kwa  Maaskofu na Mashekhe  kutoka katika Kamati ya Kitaifa ya Maadili , Amani na Haki za Binadamu kwa Jamii ya Madhehebu ya Dini  Nchini  kufichua mtandao  haramu  wa watu  wanaoendesha mauaji na uhalifu mwingine kwenye   mikoa  13, nchini kama njia muhimu ya kumpongeza IGP mpya, Saimoni Sirro.

 Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Askofu William Mwamalanga, siri hiyo imetolewa  jana  na vijana hao katika   siku ya  tatu  mkutano wa kujenga maadili kwa vijana unao fanyika Mbagala, jijini Dar es Salaam na kuwashirikisha   vijana  wa madhehebu mbalimbali ya dini  kutoka katika  mikoa ya Pwani, Tanga, Lindi,  Morogoro,Dar es Salaam  ambapo wameyataja maeneo ya Mkuranga, Rufiji  Kigamboni, Kibiti, Msata, Tanga mjini, Pemba na Unguja kuwa maeneo hatari yanayowajengea vijana imani za  kigaidi.

 Aidha, Askofu Mwamalanga alisema kuwa vijana 147  wa kiislamu wanaohudhuria mkutano huo  wamewataja  baadhi ya watu  ambao ni   hatari  na wamekuwa wakieneza elimu ya mauaji  kwenye  misikiti mbali mbali nchini kwa kuiita Serikali ya Awamu ya Tano jina la katili na kwamba elimu hiyo imesambazwa kwa kasi  katika mikoa ya  Kagera, Tanga, Mwanza, Arusha, Pemba, Unguja, Dar es Salaam, Lindi, Mtwara, Morogoro, Iringa, Singida, Dodoma, Pwani na Kigoma huku vikosi vya vijana vikiandaliwa kufanya mauaji  mara baada ya mufungo mtukufu wa Ramadhani kama yale ambayo yamekuwa yakifanywa  Mukuranga, Kibiti  na Rufiji. 

Vijana hao wanamuomba  IGP  Sirro kuwachukulia hatua kali maafisa wa jeshi hilo ambao wanatumia jeshi kupandikiza Umngiki, na  kwamba wana imani na IGP Sirro amabaye kwa mujibu wa hao vijana hatamwangusha Rais  Magufuli na watanzania kwa ujumla.

Akifunga  Mkutano huo  Askofu Mwamalanga  amemtaja IGP  Sirro kama polisi mahiri wa maadili na jemadali  mweledi wa mapambano hivyo amewataka  vijana kote nchini kumuunga mkono kwa kuwafichua polisi wote wanaoenzi uhalifu. “Tusipofanya hivyo tutakuwa  kama  pipa zuri  tunalo jaza maji wakati tukijua chini limetoboka”,alisema Askofu Mwamalanga na kuongeza kuwa raia wema ni asilimia 99.9  wahalifu ni 0.1   hii ina maana kuwa ukiondoa polisi wahalifu  ndani ya jeshi hilo wahalifu ni wachache mno  mitaani  watayeyuka wenyewe. 

Aidha,  Askofu huyo amewahimiza vijana na viongozi wa dini kushiriki kwenye mafunzo hayo kote nchini ili  wapewe ufahamu wa elimu ya maadili ya kweli  ili wawe walinzi wa taifa na kupenda amani  na kuweka uchu wa kuchukia rushwa  na kujiwekea  mitazamo ya kupenda kazi za baraka.

Kiongozi huyo wa dini amekemea vikali nyumba za ibada   kugeuzwa  eneo la mafunzo ya uhalifu kwani ni aibu kwa msikiti au kanisa kufanya  mafunzo ya kigaidi  ndani  ya  nyumba  za ibada  kufanya hivyo ni ibada ya sanamu, watu wa jinsi hiyo hawana uhusiano wowote na Mwenyenzi MUNGU ambaye kusudi lake ni kuondoa uovu kwa mwanadamu.

Hivi karibuni yametokea mauaji ya viongozi wa Chama Tawala maeneo ya Kibiti, Mukuranga na Rufiji na kufanya wakazi wa maeneo hayo kuishi kwa wasiwasi na mashaka juu ya maisha yao. Wakati akiipishwa kuwa IGP, Kamanda Simon Sirro alisema kupambana na kuondoa uhalifu kwa kushirikiana na raia wema ni moja ya vipaumbele vyake.

MZEE NDESAMBURO AKITOLEWA HESHIMA ZA MWISHO


Sanduku lenye Mwili wa Marehemu wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Marehemu Phillemon Ndesamburo,ukiandaliwa tayari kwa kuagwa katika uwanja wa Majengo,mjini Moshi mkoani Kilimanjaro mapema leo mchana.
  Gari lililobeba mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Phillemon Ndesamburo lilielekea katika viwanja vya Majengo kwa ajili ya kuagwa mwili huo.
Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa akiwapungia mkono wananchi waliofika kwenye uwanja  huo mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Majengo kwa ajili ya kuagwa mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Marehemu Phillemon Ndesamburo.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe akiwasili atika viwanja vya Majengo kwa ajili ya kuagwa mwili wa  aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Marehemu Phillemon Ndesamburo.
Wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wakiwa wamebeba jeneza lililobeba mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Marehemu Phillemon Ndesamburo. 
Viongozi mbalimbali wa Kisiasa na dini wakiwa wamesimama mara baada ya mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Marehemu Phillemon Ndesamburo kuwasili uwanjani hapo



 Baadhi ya wakazi wa mji wa Moshi mkoani Kilimanjaro wakiwa kwenye uzuni mara baada ya mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Phillemon Ndesamburo ulipokuwa unaelekea katika viwanja vya Majengo kwa ajili ya kuagwa mwili huo. 



  
  

Monday, June 5

Sipati picha Chadema bila Ndesamburo



Mengi yamekwishasemwa kuhusu kifo cha Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Kilimanjaro, Philemon Ndesamburo. Sifa zake nyingi zimetajwa, zikihusisha ni mcgangio kiasi gani alikuwa nao kwa chama hicho na kwa taifa kwa ujumla.
Pamoja na hayo yote, jambo ambalo wengi wanajiuliza ni baada ya kifo hicho cha ghafla cha mfadhili mkuu wa chama na mwana mikakati ya ushindi, Chadema mkoa wa Kilimanjaro itakuwaje bila yeye?
Mipango mingi ya kimkakati na kifedha ilimtegemea Ndesamburo kwa kiwango kikubwa. Alikuwa akirusha helkopta yake katika majimbo mbalimbali ya mkoa Kilimanjaro ili kutafuta ushindi kwa chama.
Ndesamburo aliyekuwa na kadi namba 10 ya uanachama wa Chadema, akiwa Mbunge wa Jimbo la Moshi Mjini kwa vipindi vitatu (2000-2015), alifadhili sehemu kubwa ya kampeni ya madiwani waliounda halmashauri ya Manispaa ya Moshi kwa kipidi chote hicho.
Kwa maneno mengine, mtu anaweza kusema kwa Kilimanjaro, Ndesamburo ndio alikuwa Chadema na Chadema ilikuwa Ndesamburo, bila yeye chama kisingeweza kufurukuta dhidi ya CCM.
Aliyekuwa katibu wake wa nafasi ya ubunge kwa vipindi vyote vitatu ambaye pia ni Katibu wa Chadema mkoa Kilimanjaro, Basil Lema anasema itachukua muda kumpata mtu wa aina ya Ndesamburo.
Sifa ndani ya chama
Lema anasema kuna sifa kuu tano za Ndesamburo, ambazo inawezekana ikachukua muda mrefu kupata mtu wa kuzifikia na hivyo pengo lake kuiathiri sana Chadema. “Kikubwa sana ambacho kitaonekana ni kwamba Ndesamburo alikuwa ni mtu mwenye ushawishi mkubwa. Alipewa hata jina la Koffi Annan alipofanikiwa kusuluhisha mgogoro wa uongozi huko Rombo,” anasema.
“Kweli tumempoteza mtu aliyekuwa na uwezo wa kuzileta pande zinazokinzana mezani zikasikilizana. Lakini tumempoteza mtu mwenye nguvu ambaye akikuita unakwenda ukiwa na hofu.”
“Hofu kwa maana ya busara zake nyingi, hofu kwa maana ya umri wake mkubwa na hofu kwa maana ya sifa aliyonayo kwa jinsi alivyoijenga ngome imara ya Chadema,” anasema Lema na kuongeza:
“Unaenda ukiwa na hofu kuwa aliyekuita ndiye mwenye chama na amekifikisha hapo kilipo yeye mwenyewe. Hiyo hofu lazima ikupate unavyomfuata pale ofisini kwake Keys au nyumbani.”
“Pia hofu kutokana na nguvu yake ya kifedha kwamba yeye ni mfadhili mkuu wa chama. Ni mfadhili wetu binafsi.”
“Sasa anapokuita, umeitwa na mamlaka ya fedha pia.”
“Lazima uangalie amekuita mwenye pesa na hiyo ni nature (asili). Tunawaheshimu watu wenye pesa. Anapendwa sana na anaheshimiwa sana kwa hiyo akikuita unajua umeitwa na kipenzi cha watu.”
“Kwa hiyo watu watakushangaa sana kama unapambana na mtu anayeheshimika sana na mtu unique (wa kipekee) na mtu mwema. Wewe ndio unaonekana wa ajabu.”
“Pia alikuwa ni mwana mikakati ya ushindi, mimi nimekuwa katibu wake. Ningekuwa na sababu nyingi za kufikia juu kabisa kwenye hatima yangu ya kisiasa lakini nilibaki naye.”
“Nilikuwa navutwa mno kufanya kazi na mtu mwenye mipango na mikakati yenye akili sana. Ndesamburo ni mjanja ni mtu wa mikakati mno. Anapanga mikakati ya miaka 10 mbele na inakua.”
“Anapanga kuanzia mbinu, gharama na wahusika. Sasa hayupo tuna kazi ngumu. Tunahitaji mwana mikakati, tunahitaji msuluhishi sasa hayupo ni hatari kwetu. Na inawezekana chama kikateketea kwa kukosa msuluhishi,” anasema Lema ambaye mwaka 2015 alijitosa kumrithi Ndesamburo lakini akalazimika kuondoa jina lake baada ya kuombwa na Ndesamburo.
Nini kitainusuru Chadema
Katibu huyo anasema hakuna mtu binafsi ambaye ni mbadala wa Ndesamburo, kinachotakiwa ni chama kuheshimu katiba, kanuni na maadili.
“Kwa kuwa chama kilidekezwa kuanzia makao makuu kikijua kuna mbeleko ya kubeba mizigo, uchafu, uvunjaji wa katiba kikijua yupo mbebaji,” anasema Lema na kuongeza:
“Basi itabidi chama kianze kuwa mtiifu sana kwa katiba, kanuni na maadili kushughulikia wakosaji mara moja. Kisiendelee kuamini yuko Ndesamburo kwamba atamaliza tatizo la Kilimanjaro.”
“Hayupo tena. Mbadala wa Ndesamburo ni katiba, maadili na kanuni za chama. Ugonjwa ulioingia kwenye chama unaopambana na mikakati ni tamaa ya madaraka.”
“Ndesamburo ameondoka, kama chama hakitarithi mila za kuenzi na kuheshimu wana mikakati lazima watu wenye tamaa ya madaraka wajenge ufalme wao kwa kuwa hakuna mtu wa kuwatisha tena.”
“Matokeo yake chama kitapasuka vipande vipande, migogoro itakuwa mikubwa na itaanzishwa na wenye fursa ya uongozi wakitengeneza ufalme wao.”
CCM waitabiria Chadema shida
Sio wana Chadema pekee wanaoona kivuli cha Ndesamburio, washindani wao CCM pia wanaona kuondoka kwa Ndesamburo kunaweza kukiteteresha chama hicho katika Mkoa Kilimanjaro kutokana na kumpoteza mtu mwenye ushawishi wa usuluhishi.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Moshi Mjini, Priscus Tarimo anasema inahitajika kazi ya ziada kuwarudisha wanachama na viongozi katika kundi moja, kama kweli wanataka Chadema ibaki imara.
“Kwa kweli itakuwa ni ngumu maana ushawishi wake haukuwa ndani ya chama tu, bali zaidi nje ya chama. Watu walikuwa wanamkubali, mzee mtu mzima (Ndesamburo) akisema kitu anamaanisha,” anasema Tarimo
Anaongeza, “Kwa hiyo heshima ya Chadema Moshi ilikuwa inamtegemea sana Ndesamburo kama mtu, si chama. Hapa ndipo utagundua umuhimu wa yule mzee licha ya hapa mwishoni kuanza kubeza kazi yake.”
“Ukiangalia katika vipindi vya nyuma Rais anashinda wa CCM na Baraza la Madiwani linakuwa la CCM lakini alipoingia kuwa mbunge ndio akabadili, baraza likawa la Chadema.”
“Heshima yake ilikuwa yeye kwanza kabla ya chama na hiyo ndiyo ilisababisha Chadema ikawa na nguvu hapa Moshi. Kwa kweli bila yeye Chadema itakuwa na kazi ya kufanya,” anasisitiza Tarimo.
Tangu kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu mwaka 2015, Chadema Moshi mjini hawakurudi wamoja, kulikuwapo kundi linalomtii Ndesamburo na jingine linalomuunga mkono mbunge, Jaffar Michael.
Lakini kitendo cha baadhi ya wabunge akiwamo Anthony Komu wa Moshi Vijijini, kumpinga waziwazi Ndesamburo asigombea uenyekiti wa Chadema Kanda ya Kaskazini kwa sababu ya umri, nacho kilichochea zaidi mgogoro.
Nguvu ya Ndesamburo
Kada huyo maarufu kwa jina la ‘Ndesa Pesa’ kutokana na kumiliki vitega uchumi kadhaa ndani na nje ya nchi, ndiye anayetajwa kukijenga chama hicho mkoani Kilimanjaro na kuwa na nguvu kubwa.
Katika Uchaguzi Mkuu 2015 ambapo Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa alipeperusha bendera ya Ukawa katika nafasi ya urais, Mkoa wa Kilimanjaro ni miongoni mwa mikoa iliyofanya vizuri.
Akiwa ni mwenyekiti wa mkoa, Ndesamburo pamoja na viongozi wenzake, walimwezesha Lowassa kupata kura 266,636 dhidi ya 167,691 alizopata Rais John Magufuli na kuzoa majimbo saba kati ya tisa.
Si hivyo tu, ni chini ya utawala wake, Ndesamburo aliiwezesha Chadema kupata wabunge tisa, madiwani 145, vitongoji 910, vijiji 472 na mitaa 38 katika uchaguzi wa mitaa 2014 na Uchaguzi Mkuu wa 2015.
Lakini kubwa zaidi, katika uchaguzi huo, Chadema iliibuka mshindi katika majimbo ya Hai linaloongozwa na Freeman Mbowe na Rombo linaloongozwa na Joseph Selasini.
Mbali na majimbo hayo, Chadema ilishinda katika majimbo ya Same Mashariki kwa Naghenjwa Kaboyoka; Dk Godwin Mollel wa Siha na Anthony Komu (Moshi Vijijini).
Kubwa zaidi ambalo bado litabaki katika vichwa vya wengi, ni kitendo chake cha kumtangaza Jaffar Michael kama mrithi wake na akampigania hadi akashinda katika uchaguzi huo wa 2015.
CCM wakati huo ikimtegemea mfanyabiashara tajiri nchini, Davis Mosha iliamini kwa kutumia mwanya huo wa Ndesamburo kustaafu ubunge ingeweza kushinda lakini haikuwa hivyo.
Kwa hiyo, kuondoka kwa Ndesamburo hakika kutaifanya Chadema ifanye kazi ya ziada na kuja na mikakati mipya ya kuwaaaminisha wananchi kuwa bila Ndesamburo mambo yataenda kama uilivyokuwa.
Meya wa Manispaa ya Moshi (Chadema), Ray Mboya alisema Ndesamburo alikuwa ni baba wa Jimbo la Moshi mjini na kifo chake kimewashtua wengi kwa kuwa aliamka asubuhi akiwa mzima wa afya.
Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa alisema chama kimepoteza mtu aliyekuwa na mchango mkubwa.
“Alikuwa na mchango mkubwa ndani ya chama chetu. Kwa muda mrefu amekuwa akikisaidia chama. Wakati mwingine tumekuwa tukitumia chopa yake,” alisema.
“Pengo kubwa sana kwa sisi, busara zake, mawazo yake kwa kweli tuta-miss sana. Lakini kwa sababu wote tutapita njia hiyo hiyo, hatuna la kufanya.”
Mbunge wa viti maalumu (CCM), Martha Mlata alisema Ndesamburo alikuwa mzalendo wa kweli na kama kuna jambo ambalo wapinzani wanatakiwa kujifunza ni yale mazuri ambayo amefanya wakati wa uhai wake.
“Nakumbuka wakati wote alipokuwa mbunge hajawahi kusikika akikashifu wala kusema maneno makali bungeni. Kama alikuwa anataka kushauri jambo, alitumia maneno ya hekima na busara. Wapinzani wakitaka kuheshimika wafuate mazuri aliyoyafanya mzee Ndesamburo. ‘Tulimmisi’ bungeni lakini tutaendelea kumkumbuka sana kwa hekima na busara zake,” alisema.
Mbali na wanasiasa, Ndesamburo alijenga jina hata nje ya chama kama anavyoeleza Askofu wa Kanisa la Victorious, Dk Sixbert Mkelemi kuwa kanisa limepokea kwa masikitiko kifo chake kwa kuwa alikuwa mmoja wa wadhamini wa Umoja wa Kongamano la Makanisa Afrika.