Monday, March 12

Naibu Waziri ahimiza Watanzania kupima afya zao

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Faustine Ndugulile amewataka Watanzania kuwa na utamaduni wa kupima afya zao angalau mara moja kwa mwaka ili kubaini kwa haraka endapo ugonjwa utaingia mwilini.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Machi 12, 2018, Dk Ndugulile amesema watu wengi wamekuwa wakiathirika na kupoteza maisha kwa sababu ya kukosa matibabu kwa wakati.
“Magonjwa kama kisukari, kiharusi, shinikizo la damu, shinikizo la macho yamekuwa yakiongezeka sana lakini watu wanashindwa kuyabaini mapema kwa sababu hawana utamaduni wa kufanya vipimo mara kwa mara,” amesema.
Amesema ugonjwa huo una athari kubwa unapoingia kwenye macho ya binadamu lakini wengi hawafahamu kwa sababu unaingia taratibu na si rahisi kuonekana kwa haraka.
Kwa mujibu wa Dk Ndugulile takribani watu 1,740,000 nchini wana matatizo ya kutoona vizuri lakini kwa mwaka 2017 watu 13,420 pekee ndiyo walihudhuria kwenye vituo vya afya wakiwa na tatizo la shinikizo la macho.
Takwimu za Shirika za Afya Duniani (WHO) zinaonyesha ifikapo mwaka 2020 idadi ya watu wasioona kutokana na ugonjwa wa shinikizo la macho itafikia 11.2 milioni.
Amesema waathirika wakubwa wa ugonjwa huo ni watu wenye umri kuanzia miaka miaka 40 na kwa kiasi kikubwa husababisha upofu.
Dk Ndugulile amewataka wananchi kutumia maadhimisho ya siku ya afya ya macho yaliyobebwa na kauli mbiu ‘Okoa uoni wa macho yako’ kwenda kwenye vituo vya afya kwa ajili ya kupata vipimo na tiba.
“Ukiwahi ugonjwa huu katika hatua za mwanzo uwezekano wa kupona ni mkubwa sana, niwasihi Watanzania wapime afya zao na ukiona una dalili zozote kwenye macho yako ni vyema ukaenda hospitali kabla ya kufikia kwenye upofu,”
“Mwaka huu hatutakuwa na yale maadhimisho ya kutoa huduma za wazi hizo fedha ni bora zitibu watu vituoni, kwa hiyo tumieni wiki hii kuanzia Machi 11 hadi 17 kwenda kwenye vituo vya afya,” amesema Dk Ndugulile

Dondoo
Watu 253 milioni wana tatizo la kutoona vizuri
Kati yao watu 36 milioni hawaoni kabisa
Ifikapo 2020 idadi ya watu wasiiona kutokana na shinikizo la macho inakadiriwa kufikia 11.2 milioni.

Spika apangua kamati za Bunge


Dar es Salaam.  Spika Job Ndugai amefanya uteuzi wa wajumbe wa kamati za kudumu za Bunge. 
Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa leo Machi 12,2018 inasema Spika amefanya uteuzi huo kwa mujibu wa Ibara ya 96 ya Katibu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Taarifa hiyo imesema ibara hiyo imeweka wazi kwamba, Kanuni za Kudumu za Bunge zinafafanua muundo wa shughuli za Kamati za Bunge.
“Kwa msingi huo Kanuni ya 118 ya Kanuni za kudumu za Bunge, Toleo la Januari, 2016 imeweka Kanuni za Kudumu za Bunge zenye muundo na majukumu mbalimbali kama yanavyofafanuliwa katika nyongeza ya nane. Uteuzi wa wabunge kwenye kamati mbalimbali unaonekana utaratibu katika Kanuni ya 116.”
“Kanuni ya 116(1) inaweka utaratibu kwamba, ujumbe kwenye Kamati za Kudumu za Bunge utadumu mpaka mwisho wa Mkutano wa Kumi wa Bunge ambao ni nusu ya kwanza ya maisha ya Bunge,” anasema Spika Ndugai.
Katika uteuzi huo, wajumbe mbalimbali wamerejea katika kamati zao, wengine wakibadilishwa huku baadhi ya wenyeviti waliokuwa wakiongoza baadhi ya kamati wameondolewa.
 “Kwa mamlaka niliyopewa na Kanuni ya 115(3) na kwa kuzingatia vigezo vilivyoanishwa katika Kanuni ya 116(5) nimefanya uteuzi mpya wa ujumbe katika Kamati za Kudumu za Bunge. Wajumbe wa kila kamati wanawajibika kuchagua mwenyekiti na makamu mwenyekiti kwa mujibu wa Kanuni ya 116(10) kuwa viongozi wao,” amesema.

Rais Magufuli aeleza sababu kutosafiri nje ya nchi


Akiwa ametimiza siku 859 madarakani, Rais John Magufuli ametembelea nchi chache huenda kuliko watangulizi wake wanne.
Magufuli ametembelea Kenya, Uganda, Rwanda na Ethiopia katika kipindi chote cha utawala wake huku akitimiza miaka miwili, miezi minne na siku saba tangu aapishwe kuwa Rais wa Tanzania Novemba 5, 2015.
Huenda hilo lilimfanya jana atoe siri na sababu zinazomfanya asipende kusafiri mara kwa mara nje ya nchi.
Akiwa mjini Singida jana alikozindua kiwanda cha mafuta ya kupikia cha Mount Meru Millers Group, Rais Magufuli alisema amekataa zaidi ya mialiko 70 ya kwenda nje ya nchi kwa sababu hakuchaguliwa na Watanzania kwenda huko bali kuwatumikia.
“Nataka Tanzania yote niizungukie ndiyo maana sitaki kwenda nje, maana huko si kwenye jimbo langu, jimbo langu mimi ni Tanzania. Nimekataa mialiko zaidi ya 70. Niende nje kufanya nini wakati sijamaliza kutatua kero za wananchi.”
“Nataka nizitatue kero za wananchi walionipigia kura kwanza, walipanga foleni wakati wa mvua na jua kunichagua mimi na waheshimiwa wabunge,” alisema Rais Magufuli.
“Bado sijaenda, Iringa, Mbeya, Rukwa na sehemu nyingine, lazima nizunguke nchi yote kutatua kero za wananchi..” alisema.
Julai 4, mwaka jana, alisema alipata mialiko zaidi ya 60 kwenda nje ya nchi baada ya kuwa Rais, lakini aliikataa kwa sababu anataka kuishughulikia Tanzania kwanza.
Alisema hayo akiwahutubia wakazi wa Sengerema katika uzinduzi wa mradi wa maji.
Alisisitiza kuwa hana haja ya kwenda nje ya nchi kwa sababu bado ana mzigo mkubwa wa kumaliza ufisadi. “Niende nje kufanya nini wakati nitaenda tu nikishastaafu, nataka nimalize kwanza haya ya hapa ndani,” alisema pia mwaka jana mjini Sengerema.
Alipozungumza na watendaji mbalimbali wa Serikali Ikulu jijini Dar es Salaam Novemba 7, 2015, Magufuli alifuta safari za nje kwa watendaji wote wa Serikali na kusisitiza kuwa kama kuna ulazima, mhusika atapaswa kupata kibali kutoka kwa Katiba Mkuu Kiongozi.
Baadaye akizindua bunge la 11, Novemba 20 mwaka 2015, Magufuli alisema kuanzia mwaka 2013 hadi 2015, safari za nje zilikuwa zimeigharimu Serikali Sh356.3 bilioni.
Ongezeko la kodi
Jana, Rais Magufuli katika uzinduzi huo wa kiwanda cha mafuta, aliagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kupandisha kodi kwa waingizaji wa mafuta ghafi ya chakula kutoka nje ya nchi.
Alisema hatua hiyo itawezesha wawekezaji wa ndani wa viwanda vya mafuta ya chakula kupata soko.
Rais Magufuli alitoa agizo hilo wakati ambao Serikali inafanya maandalizi kwa ajili ya bajeti ya mwaka wa fedha wa 2018/19.
Alisema anafahamu mchezo mchafu unaofanywa na waagizaji wa mafuta kutoka nje ya nchi ikiwa ni pamoja na kuua soko la ndani la mafuta ya chakula.
“Ninafahamu mchezo mchafu unaofanywa na waagizaji wa mafuta, wanapofanya hivyo lengo lao si kutengeneza soko la ajira bali ni kuua soko la mafuta,” alisema.
Rais Magufuli alisema, “wanachofanya wanaagiza mafuta kwa kisingizio kuwa ni crude oil (mafuta ghafi) yanayohesabika kama ni malighafi,” alisema.
Aliongeza kuwa, kwa kisingizio hicho, TRA na watu wengine hawawatozi kodi na wanapoyafikisha nchini waagizaji hao huyaweka kwenye madebe na kuyauza hivyo kutengeneza faida kubwa.
“Nataka mwaka huu... wabunge mko hapa na waziri uko hapa... na waziri wangu najua mnanisikia nataka mafuta hayo yanayoagizwa kutoka nje yatandikwe charge (gharama) kubwa sana,” aliagiza.
Alisema anafahamu waagizaji hao huwa wanajikusanya na kwenda bungeni kuzitembelea kamati za Bunge.
“Naomba wabunge na mawaziri msikubali lobbing (ushawishi) za namna hiyo, mnawaumiza wananchi,” alisema.
Rais Magufuli alisema mahitaji halisi ya mafuta ya chakula kwa mwaka ni tani 450,000 na nchi inazalisha tani 135,000 sawa na asilimia 30, huku asilimia 70 ya mafuta ikiagizwa kutoka nje.
Alisema wanapoagiza mafuta hayo wanatumia dola za Marekani, fedha ambazo zingeweza kutumika katika shughuli zingine.
Rais alisema mafuta ya chakula yanachukua nafasi ya pili ya bidhaa zinazoingizwa nchini kutoka nje.
“Lakini mtu wa kawaida angeweza kutuuliza kweli Tanzania tuna wajibu wa kuagiza mafuta, tutumie fedha yetu ya kigeni kununulia mafuta ya chakula?” alihoji.
“Mtu yeyote mwenye akili timamu atakushangaa, mimi ndugu zangu ni mtaalamu wa kutengeneza mafuta nimewahi kukaa viwandani ninafahamu mchezo mchafu wanaoucheza hawa waagizaji.”
Pia, alimuagiza Waziri wa Viwanda, Charles Mwijage akamweleze mwenzake wa Wizara ya Fedha, Dk Philip Mpango kuangalia namna wanavyoweza kuwapunguzia gharama za kodi wawekezaji wa viwanda vya ndani.
“Haiingii akilini kutoza Vat (Kodi ya Ongezeko la Thamani) na kutoza kodi zingine kwa mtu ambaye ana kiwanda hapa; anatumia umeme wa hapa, anatumia maji ya hapa, anatumia malighafi za hapa, ametengeneza mnyororo wa ajira mkubwa wa watu wa hapa,” alisema.
Aliongeza kuwa kiwanda kama hicho kitanunua umeme, hivyo Tanesco watachukua fedha na Wizara ya Maji pia itapeleka maji kwenye kiwanda.
“Yale maji yatalipiwa kodi na wakulima wataweza kuuza mazao yao na wafanyabiashara nao watapunguza gharama za kusafirisha bidhaa zao sababu kiwanda kipo karibu.”
Utekaji na mauaji
Akiwasalimia wananchi katika uzinduzi huo, Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk Mwigulu Nchemba alizungumzia utekaji na mauaji ya watu yanayoendelea nchini.
“Kasi hii unayoifanya na vitu vinaonekana ndio inayowasumbua wapinzani wa kisiasa, maana kama ni gari upepo umetoa matairi yote ndiyo maana ajenda za kisiasa zimekwisha,” alisema.
Dk Nchemba, ambaye ni mbunge wa Iramba Magharibi alisema kwa wale ambao ni adui wa Taifa na historia anayotaka kuiweka Rais wanapokosa ajenda huhamia kwenye zingine za kuchafua taswira ya Taifa.
“Kinachotafutwa katika mambo mengi yanayoonekana ni namna gani ya kuchafua taswira ya nchi yetu. Ndiyo maana yanapangwa maandamano,” alisema.
“Kinachotafutwa si kuwa na mabango, kinachotafutwa ni watu kukusanyika na ikitokea namna yoyote ya kutawanya watu, wafyatue risasi ili waseme Serikali imeua watu.
“Njama hiyo tumeiona na mimi nimemwelekeza IGP kwamba hata kupanga njama ya kuua ni kosa wachukue hatua kwa wale wanaopanga njama hizo na kuchafua taswira ya Taifa letu.”
Alisema kuna watu wanatumia mikusanyiko kwa lengo la kufanya mauaji ya watu ili kuichafua Serikali na kwamba, mifano ya maeneo ambayo matukio ya aina hiyo yalishatokea ipo.
“Mheshimiwa Rais ndio maana unaona vinyago vinyago vingi, kama hivi juzi ametokea kijana anasema ametekwa, eti ametekwa akapata na muda wa kutafuta pafyumu na nguo za kubadilisha ...utapata wapi muda wa kujiandaa,” alisema Dk Mwigulu.
Alisema ni vitu vya ajabu ambavyo watu wanatafuta namna ya kuichafua Serikali na jambo hilo sio la kucheza nalo.
“Hakuna sababu ya maandamano na hakuna sehemu ya kuandamania na wala hakuna ruhusa ya kuandamana,” alisisitiza.

Bavicha watoa neno kujiuzulu kigogo wake


Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha)  limezungumzia kujiuzulu kwa Naibu Katibu Mkuu wake, Gertrude Ndibalema huku likimtakia kila la heri.
Naibu Katibu mkuu huyo aliyeshika wadhifa huo tangu mwaka 2014 ametangaza kujiuzulu akisema atabaki kuwa mwanachama ili kutimiza majukumu yake binafsi.
Akizungumza leo na Mwananchi Machi 12, 2018, Katibu Mkuu wa BavichaJulius Mwita amesema hajapata taarifa rasmi ya kujiuzulu huko zaidi ya kusoma kupitia vyombo vya habari.
Amesema iwapo kama kinachoonekana mitandaoni na kuelezwa kuwa ni taarifa kwa umma ni kweli wanamtakia kila la heri huko aendako.
“Ninachofahamu Ndibalema ni mwandishi wa habari na alianzisha programu ya kufanya mahojiano na viongozi mbalimbali. Nafikiri ameona nafasi ya uongozi aliyopo katika chama ni ya juu huku programu aliyoianzisha inahusisha kuzungumza na viongozi kutoka pande nyingine, ameona haitakuwa sawa,” amesema Mwita.
Mwita alimtaka Ndibalema kufuata kanuni za Baraza kwa kuandika barua rasmi ya kufanya hivyo ili kuruhusu taratibu nyingine ziweze kuendelea.
Gertrude ni kiongozi wa pili wa ngazi ya juu Bavicha kujizulu akitanguliwa na aliyekuwa mwenyekiti wa baraza hilo, Patrobas Katambi aliyejiunga na CCM.

Hatua 10 zitakazokuwezesha kupandishwa cheo kazini


Uaminifu ni kitu kizuri na cha maana kinachowashinda wengi wetu. Wakati wowote unapopata nafasi ya kuongea na bosi wako, kuwa mkweli katika kila neno litokalo kinywani mwako, liwe dogo au kubwa, liwe kuhusu wewe mwenyewe au kuhusu mtu mwingine, kuwa mkweli hata katika yale yanayoonekana kukuathiri wewe, amua kuwa mkweli bila kujali mazingira. Kuwa mkweli katika yale unayoyatamani na katika maswala mazima ya maendeleo ya kazi yako, sio tu unazungumza kile unachofikiri bosi wako angetamani ukiseme. Staili za kuongea zaweza kutofautiana mtu na mtu lakini ujumbe ubaki kuwa wa kweli.
Penda mazingira masafi
Wakati wowote penda kuyaweka mazingira yako ya kazi safi, hatakama ofisi sio ya kuvutia sana lakini bado unaweza kuvipanga vitu katika meza yako au pale unapofanyia kazi vikawa vema na vyenye mpangilio mzuri. Wengine wamekuwa wakijidanganya kuwa kama wakipoteza muda wao kufanyia usafi eneo lao la kazi basi mabosi wao wataona kuwa hawana kazi za kutosha za kufanya, hii ni kinyume kwa maana hali yako ya ndani ya kiutendaji yaweza kuonekana pale tunapotazama mazingira ya wewe unapofanyia kazi.
Fanya kazi saa sahihi
Mara nyingi wengi wetu tumejidanganya kuwa kwa kufanya kazi masaa mengi sana, kutoka usiku makazini na kuwahi kufika mapema sana asubuhi ndio tunaandaa mazingira ya kupanda vyeo, bado kuwaza hivi ni kosa. Ukiendelea hivi kwa muda wanaokuzunguka pamoja na bosi wako wanapata ujumbe kuwa unahangaika sana na majukumu yako yanayoonekana kukushinda na hivyo itakuwia ngumu sana kukabidhi kazi katika wakati muafaka.
Jitahidi kufanya majukumu ya zaidi
Kama unadhani unahitaji kufanya majukumu ya zaidi ili upate changamoto za ziada basi inakubidi ukubali kujitolea kutoa msaada katika baadhi ya majukumu ya wengine pale inapobidi. Waweza kuzungumza na bosi wako kuhusu hili pia, jitahidi kuwa halisi zaidi katika matazamio yako na usiweke malengo yaliyo juu ya uwezo wako ka unajua hutoweza kuyatimiza.
Mara uchukuapo jukumu fulani ili kulifanya basi jitahidi kuonyesha kuwa unalifurahia na wala haulijutii, fanya kila ulilosema kuwa utalifanya, na kwa hivyo utaonyesha heshima kubwa na kujionyesha mtu unayeweza kutegemewa. Ni muhimu sana kuwa na tabia hizi kwa maendeleo binafsi.
Uliza maswali
Kukaa kimya tu huku umeinamisha kichwa chini pasipo kusema kitu hakutakusaidia chochote katika kupanda cheo, Usihofu kuuliza swali lolote na kama una kitu au wazo juu ya jinsi gani hali fulani inaweza kuboreshwa basi iseme kwa wahusika. Yawezekana ukajiona kama unayepitiliza mipaka yako ya kazi, na yamkini wengine wasikuelewe, lakini usihofu maana taratibu itawaonyesha kuwa unaipenda kazi na uko tayari katika kuboresha biashara au mafanikio ya ofisi kwa ujumla.
Fanya utafiti
Kama unakiu ya kupanda ngazi katika masuala ya kikazi na ajira basi lazima ufanye tafiti, kama kuna kazi maalumu unataka kuiomba hakikisha unajua kilakitu kuhusu kazi hiyo na uweze kuelezea jinsi gani ujuzi wako unaendana na ule unaohitajika katika kazi husika.
Onyesha mafanikio yako kwa undani iwezekanavyo lakini pasipo kujikweza au kujisifia, mfano; kama umefanikiwa kuvuka malengo ya mauzo yako kwa kipindi fulani, basi acha mabosi wako walijue hilo.
Jifunze kutengeneza nafasi mpya
Kama unafikiri kuna njia rahisi zaidi au za mafanikio zaidi katika utendaji wako wa kazi au kama unaona umuhimu wa kuwepo kwa nafasi nyingine ya kazi ni bora uzungumze na bosi wako. Kwa sababu wewe ndiyo uliyeona umuhimu wa nafasi hiyo na kulitolea wazo, kuna uwezekano mkubwa kwamba wewe ndiyo utakayeonekana kufaa kuchukua nafasi hiyo, hii inamaanisha kwamba utakuwa tayari kubeba majukumu mapya.
Ongeza ujuzi wako
Kama unaona kuna umuhimu wa kuongezea kidogo ujuzi ulionao basi tafuta kozi zinazoendana na kile unachotaka kukifanya, jitahidi kuhudhuria semina, warsha na makongamano mbalimbali ya mlengo wa kazi yako, penda kujua zaidi ya vile wenzako wanavyovijua. Waweza kuwauliza waajiri wako kama kuna fungu kwa ajili ya kujiendeleza ili ulifaidi, onyesha kuwa una kiu ya kujiongezea ujuzi kwa manufaa ya kampuni au ofisi, hii itawafurahisha wakuu wako na kupanua wigo wa kukufikiria kwa majukumu makubwa zaidi

Mkutano wa Trump na Kim Jong-Un waanza kuandaliwa

Mkutano huo unatajwa kuwa na umuhimu mkubwa kwa dunia
Image captionMkutano huo unatajwa kuwa na umuhimu mkubwa kwa dunia
Ujumbe wa Korea Kusini upo katika jitihada za maandalizi ya mkutano kati ya Rais wa Marekani Donald Trump na Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-Un.
Viongozi hao wa Korea kusini wanatarajiwa kufika China na Japan kutoa maelezo juu ya mkutano huo.
Muda na mahali pa kufanyika mkutano huo bado haijajulikana.
Trump amesema anatarajia watafikia muafaka mzuri
Image captionTrump amesema anatarajia watafikia muafaka mzuri
Viongozi wa juu wa Korea Kusini wiki iliyopita walifikisha ujumbe kwa Rais wa Marekan Donald Trump juu ya kukutana na kufanya mazungumzo na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un, huku Trump akikubali mara moja kushiriki katika mkutano huo na kuwapa taarifa china na mshirika wake Japan mara baada ya kupokea taarifa hizo.
China imeonesha nia ya kuwa mwenyeji wa mkutano huo lakini mahala pengine pa kufanyika mkutano huo pametajwa kuwa huenda ikawa ni uswizi, Sweden ama Panmunjom.
Wakati huo huo viongozi wa usalama Nchini marekani wamesema kuwa wanajua hatari iliyoko katika mkutano huo lakini wamefurahishwa na hatua ya Trump kukubali kushiriki.
Suala la makombora ya nyuklia linatajwa kuwa ajenda muhimu ya mazungumzo
Image captionSuala la makombora ya nyuklia linatajwa kuwa ajenda muhimu ya mazungumzo
Mkurugenzi wa CIA Mike Pompeo amesema kuwa, anajua ugumu wa kujihusisha na Korea kaskazini, lakini ana amini kuwa Trump amekubali kushiriki mazungumzo hayo kwa ajili ya kuondoa matatizo na korea kaskazini na si vinginezvyo.
''Hiki ni kitu ambacho kimepiganiwa kwa miongo kadhaa sasa, na wakati huo huo amekubali kuzungumza juu ya mpango wa kusitisha Nuklia, mwisho itajulikana kuwa sio maneno tuu au nani amesema nini, uongozi huu uko makini na wakati wote wa mazungumzo shinikizo juu ya korea kaskazini liendelea , hakuna kumpuzika hadi rais ahakikishe kuwa amefikia malengo aliyoyaweka katika kipindi atakacho kua madarakani ''alisema Mike Pompeo.
Aidha Trump amesema kuwa mkutano huo utaleta matokeo makubwa kwa dunia.
Lakini wakosoaji wa siasa za marekani wanasema kuwa mazungumzo hayo yakienda vibaya basi nchi hizo mbili zitakua na uhusiano mbovu Zaidi.

Sababu za Moise Katumbi kuanzisha Chama akiwa Afrika Kusini

Katumbi
Mfanyabiashara maarufu kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Moise Katumbi ambaye sasa amejitosa kwenye ulingo wa siasa, anazindua chama chake akiwa Afrika Kusini.
Katumbi ni kiongozi wa upinzani ambaye yupo uhamishoni kutoka DR Congo baada ya kutengana na Rais Joseph Kabila.
Katumbi ambaye amewahi kuwa Gavana wa jimbo tajiri zaidi nchini humo ,Katanga alijiuzulu na kumshtumu rais Kabila kwa uongozi duni.
Moise Katumbi ni kiongozi wa pekee wa upinzani nchini Congo ambaye ana ushawishi mkubwa na ufuasi mkubwa miongoni mwa raia wa Congo na anayetarajiwa kumpa rais Kabila ushindani mkali endapo atawania tena.
Alitangaza kutaka kuwania urais mwaka 2016, kabla ya uchaguzi huo kuahirishwa.
Katumbi aliondoka DRC Mwezi Mei mwaka 2016 na kuelekea Afrika Kusini kwa ajili ya kupata matibabu punde tu aliposhutumiwa kuwaajiri wapiganaji. Baada ya hapo alihukumiwa bila yeye kuwepo kwa kuuza maeneo kinyume cha sheria na kupatiwa kifungo cha miaka 3 jela.
Anakanusha tuhuma hizo na amewahi kusema kuwa bado anataka kuwania urais katika uchaguzi utakaofuata. Bw Katumbi pia ni Rais wa klabu ya soka maarufu katika Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo ya TP Mazembe.
Bw Katumbi pia ni Rais wa klabu ya soka maarufu katika Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo ya TP Mazembe.
Image captionBw Katumbi pia ni Rais wa klabu ya soka maarufu katika Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo ya TP Mazembe.

Historia ya Katumbi

  • Jina lake la mwisho pia Tshapwe
  • Anajulikana kama Moses Katumbi nchini Zambia, ambapo aliishi kwa miaka mingi
  • Tarehe ya kuzaliwa 28 Disemba 1964
  • Eneo la kuzaliwa ni Kashobwe
  • Ni kabila la Babemba
  • Ni kaka wa kambo wa Katebe Katoto, maarufu kama Rafael Soriano, na mfuasi wa Laurent Nkunda
  • Baba yake ni Padre Nissim Soriano, Mitaliano Myahudi kutoka Rhodes
  • Mama yake ni Virginie Katumbi, kutoka familia ya kifalme ya Kazembe
  • Rais wa kalbu ya Soka TP Mazembe Football iliopo Lubumbashi
  • Anajullikana kwa mapenzi yake na kofia za mtindo 'Cowboy'
Mabingwa mara tano wa Afrika TP Mazembe wakishika kombe la ShirikishoHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMabingwa mara tano wa Afrika TP Mazembe wakishika kombe la Shirikisho

Unaweza kujikinga vipi dhidi ya radi?

London Eye struck by lightning, July 2013Haki miliki ya pichaPA
Wakati wa mvua, huwa ni kawaida kwa radi kutokea na kila mwaka watu huuawa katika maeneo mbalimbali duniani baada ya kupigwa na radi.
Jumamosi, watu 16 waliuawa radi ilipopiga kanisa moja la kidventista kusini mwa Rwanda.
Meya wa eneo hilo alsiema waumini 140 walijeruhiwa wakati wa kisa hicho katika kanisa la SDA.
Meya huyo alisema wanafunzi 18 walijeruhiwa baada ya kupigwa na radi eneo hilo Ijumaa. Mmoja wao alifariki.
Msimu wa mvua za masika unawadia na tayari idara za utabiri wa hali ya hewa zimeanza kutoa tahadhari.
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) tayari imetabiri kwamba kutatokea mvua kubwa mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Lindi na Mtwara wiki hii.
"Wakazi wa maeneo yaliyotajwa wanashauriwa kuchukua tahadhari stahiki na kuendelea kufuatilia taarifa pamoja na tahadhari zinazotolewa," TMA imesema kupitia taarifa.
Kando na uharibifu unaotokana na mafuriko, kupigwa na radi kunaweza kusababisha maafisa.
Utawezaje kujikinga?

Radi ni nini?

Radi hutokana na kuachiliwa kwa umeme tuli, tukio ambalo hutokea kutokana na tofauti ya nguvu za umeme kati ya mawingu na ardhi.
Huwa ni cheche kubwa ya umeme kutoka angani, ambayo huwa na nguvu sana. Inaweza kusababisha moyo wa binadamu kuzima na kuacha kupiga na pia kuunguza viungo muhimu mwilini.
Zaidi ya robo tatu ya wanaonusurika baada ya kupigwa na radi hupata ulemavu wa aina fulani ambao hudumu maishani.

Radi hutoka wapi?

Mara nyingi radi hutokea kwenye sehemu ya chini ya anga, ambayo kwa Kiingereza hufahamika kama 'troposphere'.
Huwa inaenea kutoka kwa wingu moja hadi jingine au kutoka kwa wingu hadi ardhini.
Radi inaweza pia kupatikana katika mawingu ya majivu kutoka kwa volkano.
Two photos of men with lightning injuries that look like flower or tree branchesHaki miliki ya pichaWINSTON KEMP; OTHER
Image captionWanaume wawili waliopigwa na radi

Wanaume hupigwa zaidi ya wanawake

Kwa mujibu wa Taasisi ya Serikali ya Kuzuia Ajali UIngereza (Rospa), wanaume wana uwezekano mara nne zaidi ya wanawake wa kupiwa na radi.
Hili inadhaniwa hutokana zaidi na aina ya shughuli ambazo wanaume hujihusisha nazo, ambapo uwezekano wao wa kuwa nje wakati wa mvua huwa juu mno.
Wachezaji gofu mara nyingi huwa kwenye hatari zaidi kwani ndio walio na uwezekano mkubwa wa kuwa maeneo ya wazi mbali na nyumba au eneo la kujikinga mvua.
Aina tatu za kupigwa na radi
Huwa kuna aina tatu za radi ambazo zinaweza kumpiga mtu.
Moja ni kupigwa moja kwa moja, ambapo radi hukupiga na nguvu za umeme kupitia ndani ya mwili wako hadi ardhini.
Pili ni kupigwa pembeni, ambapo huwa kitu kilichokaribu nawe kimepigwa na radi, nguvu zikaruka na kukufikia.
Tatu ni radi inapopiga ardhini na kisha kukufikia.

Utawezaje kujikinga?

  • Tafuta hifadhi pahali ambapo kuna jumbwa kubwa au ndani ya gari. Kukiwa na jumba ambalo lina kifaa cha kukinga dhidi ya radi, utakuwa salama zaidi.
  • Usiwe katika maeneo ya wazi, au kwenye mlima ulio wazi.
  • Iwapo utakosa pahala pa kujikinga mvua, punguza uwezekano wako wa kupigwa kwa kujikunyata na kujifanya mdogo zaidi. Unaweza kuchutama, kuweka mikono yako kwenye magoti na kufichwa kichwa chako ndani.
  • Usijikinge mvua chini ya miti.
  • Iwapo upo pahala ambapo kuna maji, ondoka na kukwepa maeneo ya ufukweni yaliyo wazi.
  • Utafiti umeonesha kwamba kuwa karibu na maji huongeza hatari ya mtu kupigwa na radi.
  • Kwa kuwa radi huwa nguvu za umeme, unafaa kujiepusha na vitu vya chuma vyenye ncha kali ukiwa kwenye mvua.
LightningHaki miliki ya pichaTHINKSTOCK
Kumbuka, hatari ya kupigwa na radi inaweza kuwepo kwa muda hata baada ya mvua kubwa kuacha kunyesha.

Jeshi la Myanmar latuhumiwa kutwaa maeneo ya Warohingya jimbo la Rakhine

Wanajeshi wa MyanmarHaki miliki ya pichaAFP
Image captionWanajeshi wa Myanmar
Utafiti mpya uliofanywa na Shirika la Haki za Binadamu la Amnesty International limedai kuwa jeshi la Myanmar limejenga kituo katika vijiji ambavyo watu wa Rohingya wamelazimishwa kuyakimbia makaazi yao.
Wanaharakati wa shirika hilo wamesema watu walioshuhudia na uchambuzi uliofanywa kupitia picha za Satellite umeonesha kuwa mwezi Januari wanajeshi wa Burma walikuwa wakisawazisha ardhi ya vijiji vya wa Rohingya kwa kuponda nyumba na hivi karibuni wamechoma moto eneo hilo.
Msemaji wa Amnesty International Tirana Hassan ameelezea hatua zillizochukuliwa katika jimbo la Rakhine kama ''Jeshi kujinyakulia ardhi''.
Serikali ya Myanmar bado haijatoa tamko lolote kuhusiana na ripoti hiyo ya Amnesty International.