Tuesday, December 5

Mhasibu wa Takukuru akwama mahakamani


Dar es Salaam. Mahakama imegoma kumfutia shtaka la utakatishaji fedha mhasibu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Godfrey Gugai.
Gugai anayedaiwa kuwa na utajiri wa kutisha usiolingana na kipato chake, aliiomba mahakama kumfutia shtaka hilo na kujikuta likitupiliwa mbali.
Gugai na wenzake watatu, George Makaranga, Leonard Aloys na Yasini Katera wanakabiliwa na mashtaka hayo ambayo hayana dhamana pamoja na mengine ya jinai katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Washtakiwa hao walipandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza Novemba 16, na kusomewa mashtaka 43 yakiwamo 20 ya kutakatisha fedha.
Baada ya kusomewa mashtaka hayo, kupitia kwa jopo la mawakili wao lilioongozwa na Alex Mgongolwa waliiomba mahakama kuwafutia mashtaka ya utakatishaji fedha, pamoja na mambo mengine wakidai hayajakidhi vigezo vya kisheria.
Maombi na hoja za mawakili wa washtakiwa hao, zilipingwa vikali na upande wa mashtaka ulioongozwa na Simon Wankyo baada ya kusikiliza hoja za pande zote aliiahirisha hadi jana kwa uamuzi wa ama kuyafuta mashtaka hayo au la.
Hata hivyo, hakimu mkazi mkuu, Thomas Simba anayesikiliza kesi hiyo katika uamuzi wake alitupilia mbali maombi na hoja za mawakili wa washtakiwa hao.
Akisoma uamuzi wake, Simba alitupilia mbali maombi na hoja hizo akisema hazina msingi wa kisheria na hati ya mashtaka ipo sawa haina kasoro za kisheria.
Baada ya kusoma uamuzi huo, wakili wa Serikali mkuu, Vitalis Peter aliieleza mahakama kuwa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika na akaomba ipangiwe tarehe nyingine ya kutajwa.
Hakimu Simba aliahirisha shauri hilo hadi Desemba 18, litakapotajwa kwa ajili ya upande wa mashtaka kueleza hatua ya upelelezi ulipofikia.
Awali, akiwasilisha maombi ya kufutwa kwa mashtaka hayo, Mgongolwa alidai mashtaka hayo hayakidhi vigezo vya kisheria vilivyotajwa katika sheria ya utakatishaji fedha.
Alidai maelezo ya makosa hayo hayaelezi kosa la utakatishaji fedha na kwamba, lazima makosa hayo yaonyeshe uhalisia ili kumwezesha mshtakiwa kutengeneza utetezi wake.
Aliendelea kuwa msingi wa mashtaka ya utakatishaji wa fedha ni fedha, lakini katika mashtaka yote hayo ya utakatishaji hakuna sehemu iliyotajwa fedha na kwamba kinachoonekana ni udanganyifu wa kiwango cha mali anazomiliki mshtakiwa.
Maombi hayo yalipingwa na upande wa mashtaka ambao waliiomba mahakama kutupilia mbali maombi hayo, kwa kuwa hayana msingi kisheria.
Gugai kwa upande wake anakabiliwa na shtaka la kumiliki mali ambazo hazina maelezo.
Anadaiwa kuwa kati ya Januari 2005 na Desemba 2015, katika mkoa wa Dar es Salaam, akiwa ofisa wa umma aliyeajiriwa na Takukuru, alikutwa anamiliki mali zenye thamani ya Sh. 3,634,961,105.02 ambazo haziendani na kipato chake cha sasa wala cha nyuma. 

Kumbusho aachiwa baada ya kuhojiwa polisi


Dar es Salaam. Mbunge wa serikali ya wanafunzi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Daruso), Kumbusho Dawson ameachiwa baada ya kuhojiwa na polisi wa kitengo cha makosa ya mtandao.
Kumbusho alipelekwa Kituo Kikuu cha Polisi leo Jumanne Desemba 5,2017 akitokea Oysterbay alikokwenda kuripoti asubuhi baada ya kuachiwa kwa dhamana jana usiku.
Wakili Alex Masaba anayewakilisha Kumbusho amesema polisi wamemuachia baada ya mahojiano na wanaendelea na upelelezi hivyo wakimuhitaji watamwita.
Masaba amesema mteja wake amekamatwa kwa kosa la kusambaza picha zinazoonyesha nyufa kwenye jengo la  mabweni ya chuo hicho. Hata hivyo, amesema anaamini kilichofanyika si jinai.
"Kosa la kusambaza picha zilizopigwa si jinai hata polisi nimewaeleza kwa kitendo kilichofanyika inabidi apongezwe," amesema Masaba.

Mtoto aliyezaliwa ubongo ukiwa nje afanyiwa upasuaji


Dar es Salaam. Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu (MOI) imefanya upasuaji mkubwa wa kurudisha ubongo wa mtoto mwenye umri wa miezi minne aliyezaliwa ukiwa kwenye mfuko nje ya kichwa.
Upasuaji huo uliofanyika kwa mafanikio ni wa kwanza nchini wa kurudisha ubongo uliokuwa kwenye mfuko nje ya kichwa (occipital encephalocele).
Imeelezwa upasuaji huo uliwahusisha madaktari bingwa kutoka nchini kwa gharama ya Sh4 milioni badala ya kati ya Sh25 milioni na Sh30 milioni kama ungefanika nje ya nchi.
Daktari bingwa wa upasuaji wa ubongo na uti wa mgongo wa Moi, Nicephorus Rutasibwa amesema leo Jumanne Desemba 5,2017 kuwa upasuaji huo umefanywa kwa zaidi ya saa nne.
Dk Rutasibwa amesema upasuaji umefanyika baada ya utafiti wa miezi miwili kujua namna bora ya kumsaidia mtoto huyo ili kuokoa maisha yake.
“Tathmini ya uchunguzi ilionyesha uvimbe au mfuko ulikuwa umefunika sehemu kubwa ya ubongo na mishipa ya damu inayolisha ubongo, hivyo kuhatarisha maisha yake. Upasuaji ulihitaji umakini wa hali ya juu na vifaa vya kisasa,” amesema.
Dk Rutasibwa amesema upasuaji huo ulifanywa bila kuathiri utendaji kazi wa ubongo ambao wakati wote wa upasuaji ulikuwa unafanya kazi.
Hata hivyo, amesema walikabiliana na changamoto wakati wa maandalizi ya upasuaji ya upatikanaji wa mishipa ya damu ya mtoto kwa kuwa ilikuwa midogo.
“Baada ya upasuaji mtoto aliendelea vizuri na aliweza kunyonya, tangu alipozaliwa ilikuwa vigumu kumbeba lakini sasa mama anaweza kumbeba mwanaye. Mtoto amepata nafasi ya kuendelea na maisha,” amesema.
Mama wa mtoto huyo ambaye hakupenda kutajwa jina amesema awali alikata tamaa ya mwanaye kupona kutokana na uvimbe uliokuwa ukimuelemea.
“Nawashukuru madaktari bingwa kwa kufanikishwa upasuaji huu, nilishakata tamaa na sikujua kama leo ningeweza kumnyonyesha mwanangu akiwa mzima,” amesema.

Wafanyabiashara wapandishwa kizimbani kwa uhujumu uchumi


Dar es Salaam. Wanandoa wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi.
Minda Mfamai na mkewe Fatuma Mpondi ambao ni wafanyabiashara wamepandishwa kizimbani pamoja na mwenzao Oswini Mango wakidaiwa kusafirisha gramu 375.20 za dawa za kulevya aina ya heroin.
Mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri; wakili wa Serikali, Adolf Mkini amedai Novemba 22,2017 katika maeneo ya Chamazi kwa Mkongo, Dar es Salaam washtakiwa walisafirisha dawa hizo.
Baada ya kusomewa shtaka leo Jumanne Desemba 5,2017 washtakiwa hawakuruhusiwa kujibu chochote kwa sababu Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu haina mamlaka ya kuisikiliza kesi hiyo isipokuwa Mahakama Kuu.
Hakimu Mashauri ameahirisha kesi hiyo hadi Desemba 19,2017.
Mahakama imeamuru mshtakiwa Minda akatibiwe baada ya kulalamika kuwa alipigwa akiwa polisi.

Mahakama kutoa uamuzi wa dhamana kesho


Morogoro. Wabunge Susan Kiwanga na Peter Lijualikali waliofikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro pamoja na washtakiwa wengine 36 wamerejeshwa rumande.
Mahakama iliyokuwa itoe uamuzi wa dhamana leo Jumanne Desemba 5,2017 imekwama kufanya hivyo kutokana na kuibuka hoja za kisheria.
Upande wa mashtaka na ule wa utetezi unavutana kuhusu hati ya kiapo ya kupinga dhamana iliyowasilishwa mahakamani hapo.
Kutokana na mvutano wa kisheria, hakimu Ivan Msack ameahirisha kesi hiyo hadi kesho Jumatano Desemba 6,2017 ili kutoa fursa kwa pande zote mbili kujibu hoja kuhusu hati hiyo.
Washtakiwa wanakabiliwa na mashtaka nane likiwamo la kuchoma moto ofisi ya Kata ya Sofi iliyopo wilayani Malinyi.
Washtakiwa wanatetewa na mawakili Peter Kibatala, Ignas Punge, Fredrick Kiwelo na Bartholomew Tarimo. 
Upande wa mashtaka unawakilishwa na mawakili wa Serikali, Edga Bantulaki na Sunday Hyera. 
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na mjumbe wa kamati kuu ya chama hicho, Frederick Sumaye walihudhuria mahakamani.
Wengine waliofika mahakamani ni mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche na wa Viti Maalumu, Devota Minja.

JWTZ yaandaa mazoezi ya kijeshi ya pamoja EAC



Dar es Salaam. Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limeandaa mazoezi ya pamoja ya kijeshi kwa maofisa kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).
Mazoezi hayo yaliyopewa jina ‘Ushirikiano imara’ yanawashirikisha wanajeshi na maofisa wa Serikali kutoka Tanzania, Uganda, Burundi, Kenya na Rwanda.
Mkuu wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi, Brigedia Jenerali Alfred Kapinga amesema leo Jumanne Desemba 5,2017 kuwa watu 300 wanashiriki wakiwamo makamanda wa jeshi na maofisa wa juu kutoka wizara zaidi ya tatu ikiwamo ya Katiba na Sheria.
Amesema kwa Tanzania wanaoshiriki ni makamanda na maofisa watendaji wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.
Brigedia Jenerali Kapinga amesema kwa upande wa Tanzania washiriki ni 107 na kwamba, mazoezi yameanza jana Desemba 4,2017 na yatazinduliwa Desemba 7,2017 na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Hussein Mwinyi.
“Mazoezi yanafanyika katika Kituo cha Mafunzo ya Ulinzi wa Amani cha Kunduchi, Dar es Salaam na yamejikita katika mambo makuu manne,” amesema.
Ameyataja mambo hayo kuwa ni operesheni katika ulinzi wa amani; kupamba na ugaidi; kupambana na uharamia wa aina yoyote ndani ya Bahari ya Hindi; na majanga na maafa.
Amesema lengo la mazoezi hayo ni kuwaandaa na kuwapa uwezo washiriki katika kupanga na kutekeleza majukumu ya operesheni za ulinzi wa amani katika kupambana na ugaidi, uharamia na kukabiliana na maafa.
Brigedia Jenerali Kapinga amesema mazoezi  hayo ni ya siku 17.

Kumbusho aachiwa baada ya kuhojiwa polisi


Dar es Salaam. Mbunge wa serikali ya wanafunzi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Daruso), Kumbusho Dawson ameachiwa baada ya kuhojiwa na polisi wa kitengo cha makosa ya mtandao.
Kumbusho alipelekwa Kituo Kikuu cha Polisi leo Jumanne Desemba 5,2017 akitokea Oysterbay alikokwenda kuripoti asubuhi baada ya kuachiwa kwa dhamana jana usiku.
Wakili Alex Masaba anayewakilisha Kumbusho amesema polisi wamemuachia baada ya mahojiano na wanaendelea na upelelezi hivyo wakimuhitaji watamwita.
Masaba amesema mteja wake amekamatwa kwa kosa la kusambaza picha zinazoonyesha nyufa kwenye jengo la  mabweni ya chuo hicho. Hata hivyo, amesema anaamini kilichofanyika si jinai.
"Kosa la kusambaza picha zilizopigwa si jinai hata polisi nimewaeleza kwa kitendo kilichofanyika inabidi apongezwe," amesema Masaba.

Mtanzania afa baada ya kuzidiwa akiwa ndani ya ndege.


Dar es Salaam. Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), Rogers Sianga amethibitisha kupokea taarifa ya Mtanzania kufariki dunia akisafirisha dawa za kulevya.
Amesema alikuwa akisafiri kuelekea nchini China kwa ndege ya Shirika la Ethiopia na alizidiwa kutokana na dawa alizokuwa amemeza.
“Ni kweli kuna Mtanzania amekutwa amekufa kwenye ndege ya Shirika la Ethiopia akiwa amemeza dawa za kulevya. Tunaendelea kufuatilia kujua jina lake na amezitoa wapi hizo dawa,” amesema.
Sianga akizungumza na MCL Digital leo Desemba 5,2017 amesema taarifa hizo walizipata jana na kwamba wanaendelea kufuatilia.
Amesema hivi sasa Watanzania wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya wengi wanatumika kupokea mizigo na kuisafirisha kunakohitajika.

Lukuvi amesema kodi inapaswa kulipwa kila mwezi


Dar es Salaam. Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amewaonya wamiliki wa nyumba wanaopangisha na kudai kodi ya mwaka mzima.
Akizungumza leo Jumanne Desemba 5,2017 akifungua jengo la makao makuu ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) jijini Dar es Salaam na sanamu ya Mwalimu Julius Nyerere, amesema kodi ya nyumba inatakiwa kutozwa kila mwezi.
"Mpangaji anatakiwa kulipa kodi kila mwezi labda atake mwenyewe kulipa kwa miezi zaidi ya mmoja," amesema.
Lukuvi amesema hata NHC inatoza kodi kwa wateja wake kwa mwezi. "Acheni tamaa wenye nyumba chukueni kodi kila mwezi," amesema.
Amesema kuna vijana wanaoajiriwa wanashindwa kukaa jirani na mjini kutokana na kutozwa kodi ya nyumba kwa mwaka.
Mbali ya kauli hiyo, Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula Novemba 17,2017 akijibu swali la nyongeza la mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Halima Bulembo bungeni alisema Serikali iko katika mchakato wa maandalizi ya muswada wa sheria ambayo itasimamia sekta ya nyumba, hivyo kuondoa changamoto ya wamiliki kudai kodi ya pango ya zaidi ya mwezi mmoja.
Halima katika swali lake alisema vijana ambao ni kati ya asilimia 56 na 60 nchini, wanashindwa kutimiza ndoto zao kutokana na gharama kubwa ya kodi ambayo hutakiwa kulipa kwa kipindi cha mwaka mmoja au miezi sita.
Akijibu swali hilo, Mabula alisema Serikali imeliona tatizo hilo na ipo katika mchakato wa kuandaa muswada wa sheria utakaosimamia sekta hiyo.
Mabula alisema baada ya kukamilika kwa sheria ambayo itaunda chombo cha kusimamia sekta hiyo, wapangaji hawatalipa kodi ya mwaka wala miezi sita tena bali watalipa kwa mwezi na kuweka amana ya miezi mitatu.

HESLB yatoa orodha ya waliopata mikopo


Dar es Salaam. Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetangaza orodha yenye wanafunzi  2,679 waliopata mikopo yenye thamani ya Sh9.6 bilioni baada ya kukamilika uchambuzi wa rufaa walizowasilisha.
Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Abdul-Razaq Badru amesema leo Jumanne Desemba 5,2017 kuwa wanafunzi 1,847 ni wa mwaka wa kwanza ambao mikopo yao ina thamani ya Sh6.84 bilioni na wengine 832 ni wanaoendelea na masomo lakini hawakuwa na mikopo katika miaka iliyopita.
Amesema wanafunzi wanaoendelea na masomo wamepata mikopo yenye thamani ya Sh2.76 bilioni na fedha zimeshatumwa vyuoni.
Badru amesema kutokana na kukamilika kwa rufani hizo, wanafunzi 33,200 wa mwaka wa kwanza wamepangiwa mikopo yenye thamani ya zaidi ya Sh108 bilioni kwa mwaka wa masomo 2017/18 hadi sasa.
Amesema bajeti ya jumla kwa wanafunzi wote kwa mwaka 2017/18 ni Sh427.54 bilioni. Badru amesema dirisha la rufaa lilifungwa Novemba 19,2017.
HESLB pia imeanza kuhamisha mikopo iliyokuwa imeelekezwa katika vyuo tofauti.
Badru amesema mikopo ya wanafunzi 590 wa mwaka wa kwanza yenye thamani ya Sh1.78 bilioni ambayo awali ilikuwa imepelekwa katika vyuo tofauti na walipo wanafunzi imehamishwa.

Tani tatu za sangara zanaswa zikisafirishwa kwa magendo


Ngara: Tani tatu za samaki aina ya sangara zenye thamani ya Sh20.8 milioni zimekamatwa zikisafirishwa kwa magendo wilayani Ngara mkoani Kagera.
Samaki hao waliovuliwa katika Ziwa Victoria wilayani Muleba wamekamatwa jana Jumatatu Desemba 4,2017 jioni katika Kijiji cha Murusagamba wilayani Ngara wakisafirishwa kwa gari kwenda nchini Burundi.
Mkuu wa Wilaya ya Ngara, Michael Mntenjele amesema leo Jumanne Desemba 5,2017 kuwa samaki hao walivuliwa kinyume cha sheria na walikuwa wakiwasafirisha bila vibali.
Mntenjele amesema samaki hao walikuwa kwenye gari aina ya Mitsubishi likiendeshwa na Ayubu Sanga mkazi wa Dar es Salaam    anayefanya shughuli zake Kata ya Izigo wilayani Muleba.
Amesema dereva huyo akiwa na bosi wake walikatwa wakisafirisha mzigo huo kwa magendo. Alisema bosi huyo alitoroshwa wakati wakihojiwa na polisi kwa msaada wa baadhi ya maofisa uvuvi.
Mkuu wa wilaya amesema dereva na ofisa uvuvi wa kata ya Murusagamba wanashikiliwa na vyombo vya dola kwa mahojiano.
Ofisa Uvuvi Mkoa wa Kagera, Efraz Mkama amesema samaki hao wana uzito wa kuanzia nusu kilo hadi kilo 30 na urefu wa kati ya sentimita 25 na sentimita 90 .
Amesema watuhumiwa wametenda kosa la kusafirisha samaki ambao hawajachakatwa kwa mujibu wa sheria ya uvuvi.
“Mzigo haukuwa na nyaraka, ulisafirishwa usiku na kukiuka utaratibu kuanzia maeneo ya mwaloni katika kata na vijiji mbalimbali wilayani Muleba. Tutafuatilia huko alikotokea,” amesema Mkama.

WAZIRI AAGIZA SONGAS KUWASHA UMEME LEO

WAZIRI wa Nishati, Dk.Medard Kalemani ameuagiza uongozi wa kampuni ya kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia wa Songas kuhakikisha kuanzia leo wanawasha umeme   kumaliza tatizo lililopo.
Aliyasema hayo jana alipokutana na viongozi wa kampuni hiyo   Dar es Salaam, baada ya kutokea hitilafu katika mitambo yao iliyosababisha watumiaji waliounganishwa na gridi ya taifa kukosa umeme.
Alihoji sababu za kampuni hiyo kuchukua muda mrefu kufanya marekebisho katika mitambo ya kuzalisha umeme  hitilafu inapotokea,ikilinganishwa na kampuni nyingine.
Akijibu swali hilo, Meneja wa Uzalishaji wa Kampuni hiyo, Tvsk Kao alisema kwa kawaida muda wa kurejesha   uzalishaji wa umeme ni saa nane, lakini kutokana itilafu isiyo ya kawaidia iliwachukua muda mrefu kufanya matengenezo hayo.
“Tatizo lililojitokeza halijawahi kutokea, ilikuwa changamoto kubwa, tunaamini ifikapo saa 11 jioni (leo), tatizo litakuwa limetatuliwa na kurudisha upatikanaji wa umeme katika hali ya kawaida.
Alisema kampuni hiyo  inaelewa umuhimu wa nishati katika kukuza uchumi hivyo ingependa mitambo yote ya kuzalisha umeme ifanye kazi.
“Tutahakikisha  kuwa na vifaa  vya ziada vya kufunga katika mitambo   tatizo linapotokea,” alisema Tvsk.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati,Dk. Hamisi Mwinyimvua, aliwataka wataalamu hao kuhakikisha tatizo linatafutiwa suluhisho mapema na ahadi walizotoa zinatekelezwa kwa wakati.

Zoezi la Marekani, Seoul laibua wasiwasi

Mazoezi ya kivita
Wakati Marekani na Korea Kusini wanaanza zoezi kubwa zaidi la pamoja la kijeshi Jumatatu, maswali yameibuka iwapo jaribio la hivi karibuni la kombora lililofanywa na Korea Kaskazini limevuka "mstari mwekundu".
Kuvuka huko mstari huo ni uwezo wa Korea Kaskazini wa kusafirisha bomu lenye kichwa cha nyuklia na hatua gani zichukuliwe kudhibiti hali hiyo.
Mazoezi hayo ya kila mwaka ambayo hudumu kwa siku tano yenye jina ACE yanahusisha zaidi ya ndege za kijeshi 230 pamoja na wanajeshi 12,000 wa Marekani wanaoungana na wanajeshi wa Korea Kusini.
Ingawa mazoezi kama hayo huwa yamepangwa siku nyingi, zoezi la safari hii limeanza chini ya kipindi cha wiki moja baada ya Korea Kaskazini kufanya jaribio la silaha ya masafa marefu yenye uwezo wa kubeba kichwa cha nyuklia, jambo ambalo marekani imesema halikubaliki.
Jesha la anaga la korea kusini limesema zoezi hilo litahusisha mashambulio yanayofanana na kushambulia vituo vya nuklia vya Korea Kaskazini na makombora yake. .

Sudan Kusini: Watu 50 wauawa Juba kufuatia mzozo wa mifugo

Watu 50 wameuawa katika mzozo wa kugombea mifugo katika jimbo la Jonglei, Sudan Kusini, miongoni mwao wakiwemo watoto saba. Wizi wa mifugo umekuwa ukifanyika kwa karne kadhaa Sudan Kusini.

Südsudan Bewaffneter Hirte 23.12.2013 (Reuters)
Watu 50 wameuawa katika mzozo wa kugombea mifugo katika jimbo la Jonglei, Sudan Kusini, miongoni mwao wakiwemo watoto saba. Waziri wa habari wa jimbo hilo, Akech Dengdit amesema wanawake 23 na wanaume 10 pia waliuawa jana asubuhi katika kile alichosema ni shambulizi la pamoja lililosababishwa na wezi wa mifugo na waasi wanaomtii Riek Machar.
Ameitaka serikali kuu ya Sudan Kusini kupeleka jeshi na polisi katika maeneo ya ndani kwenye jimbo la Jonglei ili kuimarisha usalama na kupambana na ghasia na wizi wa mifugo.
Wizi wa mifugo umekuwa ukifanyika kwa karne kadhaa Sudan Kusini na mara nyingine watoto wanatekwa nyara wakati wa wizi huo ili wafanye kazi za utumwa majumbani. Nchi hiyo pia iko katikati ya vita vya wenyewe kwa wenyewe ambapo maelfu ya watu wameuawa tangu mwaka 2013 baada ya kutokea mpasuko kati ya Rais Salva Kiir na Machar, aliyekuwa makamu wa rais.

Rais wa Iran Rouhani awaonya wanaoishambulia Yemen

Rais wa Iran Hassan Rouhani amesema Wayemeni watawafanya wale wanaoishambulia nchi yao wajutie vitendo vyao wakati  muungano wa kijeshi unaoongozwa na Saudi Arabia ukishambulia mji mkuu wa Yemen unaoshikiliwa na waasi.

Iran Rohani 100-Tage-Bilanz der Regierung (irna.ir)
Mtoto wa rais wa  zamani  wa  Yemen Ali Abdallah  Saleh , aliyeuwawa na wanamgambo  wa  kihuthi , alitoa wito  wa  kulipiza  kisasi  dhidi  ya makundi  yanayoungwa  mkono  na  Iran.
"Watu  wa  Yemen  wanawafanya  wachokozi wajutie hatua walizochukua," Rouhani  amesema  katika  hotuba  iliyotangazwa moa  kwa  moja  katika  televisheni. Matamshi  yake  yanakuja  siku moja  baada  ya  kuuwawa  rais  wa  zamani  Ali  Abdallah Saleh na Wahuthi  wanaoungwa  mkono  na  Iran na  kusababisha mashambulizi  makali  kutoka  kwa  majeshi  yanayoungwa  mkon  na Saudi  Arabia  dhidi  ya  mji  mkuu  wa  Yemen Sanaa.
Jemen Ali Abdullah Saleh 2005 (picture-alliance/dpa/Yahya Arhab)
Rais wa zamani Ali Abdullah Saleh
Kamanda  wa  vikosi  maalum  vya jeshi  la  Iran, Mohammad Ali Jafari , amesema  Saleh aliuwawa  kwasababu  alikuwa  akijaribu kuuondoa  uongozi  wa  Wahuthi  kutoka  madarakani.
Saleh  hivi  karibuni  alivunja  muungano  wake wa  mashaka uliodumu  kwa  muda  wa  mika  mitatu  na  Wahuthi  na  kusema yuko tayari kwa  mazungumzo  na  Saudia.
"Wasaliti  Saudi Arabia  wanataka  kuleta  hali  ya  wasi  wasi  wa kiusalama  katika  eneo hili chini  ya  amri  kutoka  Marekani wakifanyakazi  kwa  pamoja  na  Israel , tumeshuhudia juhudi  zao  za kuanzisha  mapinduzi  dhidi  ya  Wahuthi, ambayo yamekabwa mapema kabla  ya  kuzaliwa.
Jemen Ali Abdullah Saleh wurde ermordet (Reuters/K. Abdullah)
Wapiganaji wa Kihuthi mjini Sanaa
Ndege  za  majeshi  ya  muungano  unaoongozwa  na  Saudi Arabia zimeshambulia  maeneo  ya  mji  mkuu  yanayoshikiliwa  na  waasi alfajiri ya  leo  baada  ya  waasi  kumuua  rais  wa  zamani  Ali Abdullah Saleh wakati  akikimbia  kutoka   mji  huo  kufuatia kuvunjika  kwa  muungano  wao , wakaazi  wa  mji  huo  wamesema.
Wito wa kupambana  na  Wahuthi
Rais  anayeishi  uhamishoni Abedrabbo Mansour Hadi  ametoa wito kwa  Wayemeni  kujiunga  pamoja  dhidi  ya  wapiganaji wanaoungwa  mkono  na  Iran. Karibu  mashambulio  saba yameangukia  katika  jengo  la makao  makuu  ya  rais  katika  eneo linaloishi  watui  wengi   katikati  ya  mji  wa  Sanaa, wamesema watu  walioshuhudia.
Kumekuwa  na mapambano  madogo  madogo  kati  ya  Wahuthi  na waungaji  mkono  wa  Saleh  katika  wilaya  za  kusini  ambazo zimekuwa  ni  ngome  kuu  ya  waungaji  wake  mkono.
Nae  mtoto  wa  rais  wa  zamani  Ali Abdullah Saleh  aliyeuwawa ametoa  wito  wa  kulipiza  kisasa dhidi  ya  makundi  yanayounga mkono  Iran.
Jemen Ali Abdullah Saleh wurde ermordet (Reuters/K. Abdullah)
Wanamgambo wa Kihuthi wakishangilia mtaani baada ya kuuwawa kwa Ali Abdullah Saleh
"Nitaongoza  mapambano  hadi  Mhuthi  wa  mwisho atakapoondo9lewa  kutoka  Yemen, damu  ya  baba  yangu itasikika katika  masikio  ya  Iran, "  alinukuliwa  Ahmed Ali Saleh  akisema. Amewataka  waungaji  mkono wa  baba  yake , "kuirejesha  Yemen kutoka  mikono  ya  wanamgambo  wa  Kihuthi wanaoungwa  mkono na  Iran".
Mkuu wa Umoja  wa  nchi  ya  Kiarabu  Arab League  Ahmed  Abdul Gheit ameshutumu  leo  kuuwawa  kwa  rais  wa  zamani  wa  Yemen na  waasi  wa  Kihuthi, akisema  hali  hiyo  inaelezea  juu  ya  hali msingi  wa uhalifu wa  kundi  hilo. Mkuu  huyo  wa  jumuiya  ya mataifa  ya  Kiarabu  ameonya  kwamba  kuuwawa  kwa  Saleh  siku ya  Jumatatu  kunatishia  kuripuka kwa  hali  mbaya ya  usalama , katika  nchi  hiyo  iliyoharibiwa  kwa  vita.

Mahakama Zimbabwe yamkuta mwanaharakati bila hatia

Mahakama ya Zimbabwe imemfutia mashtaka ya uasi mchungaji Evan Mawarire baada ya kumkuta hana hatia

Simbabwe Pastor Evan Mawarire in Harare (Reuters/P. Bulawayo)
Mahakama ya Zimbabwe imemfutia mashtaka ya uasi mchungaji Evan Mawarire baada ya kumkuta hana hatia. Mawarire ambaye pia ni mwanaharakati, alifunguliwa mashtaka hayo na utawala uliopita wa Robert Mugabe.
Jaji wa Mahakama Kuu ya Zimbabwe, Priscilla Chigumba ametoa uamuzi huo leo, akisema upande wa serikali haukutoa ushahidi dhidi ya kesi ya mchungaji huyo.
Mawarire amesema amefurahishwa na uamuzi huo na kwamba kipindi chote cha kesi hiyo kilikuwa cha ajabu na hakupaswa kukamatwa.
Amemtaka rais mpya wa Zimbabwe, Emmerson Mnangagwa kuheshimu haki za binaadamu, akisema watu wataandamana tena iwapo wataona serikali mpya inakiuka uhuru wao. Mawarire alikuwa mkosoaji mkubwa wa Rais Mugabe.

Mahakama kusikiliza kesi ya wapenzi wa jinsia moja walionyimwa keki Marekani

David Mullins (left) and Charlie Craig. Photo: 28 November 2017Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionDavid Mullins (kushoto) and Charlie Craig walikuwa wanataka keki kwa harusi yao
Mahakama ya juu zaidi nchini Marekani itasikiliza kesi ambapo wapenzi wa jinsia moja walifukuzwa kutoka duka moja la kuoka mikate huko Colorado wakati walijaribu kununua keki ya harusi.
Mwaka 2012 muoka mikate Jack Phillips alikataa kuwaokea keki David Mullins and Charlie Craig akisema kuwa ilikuwa kinyume na imani yake kama mkiristo.
Wawili hao walipeleka kesi katika mahakama ya Colorado na mahakama kusema kuwa muoka mikate aliwabagua.
Muoka mikate anasema kuwa hiyo inakiuka haki yake ya uhuru wa dini na uhuru wa kuongea.
Wapenzi hao baadaye wakapeleka malalamishi yao kwa tume ya haki za raia huko Colorado.
Jack Phillips decorates a cake in his shop. Photo: 21 September 2017Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionJack Phillips anasema kuwa hastahili kulazimishwa kuoka keki yenye umbo na ujumbe ambao yeye mwenyewe anapinga.
Colorado imepiga biashara marufuku ya kuwabagua wataja kwa misingi ya rangi na jinsia.
Mwaka 2015 mahakama ya rufaa ya Colorado ilidumissha umuzi huu nayo mahakama ya juu ya jimbo hilo ikikataa kuisikiliza upya kesi hiyo.
Kisha Bw Phillips akaamua kupeleka kesi kwa mahakama ya juu zaidi nchini Marekani.
Anasema kuwa hastahili kulazimishwa kuoka keki yenye umbo na ujumbe ambao yeye mwenyewe anapinga.
Mawakili wake pia wanasema kuwa hakukiuka sheria zinazopiga marufuku ubaguzi kwa sababu hakuwafukuza wapenzi hao kutoka kwa duka lake na hakukataa kuwahudumia.

Mwigizaji nyota wa Bollywood Shashi Kapoor afariki dunia

Shashi Kapoor in his younger daysHaki miliki ya pichaBBC HINDI
Image captionShashi Kapoor aliigiza kwenye filamu zaidi ya 150
Mwigizaji mkongwe wa Bollywood Shashi Kapoor amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 79.
Kapoor, aliyeigiza katika filamu maarufu kutoka India kama vile Deewar na Kabhie Kabhie, amekuwa akiuguza kwa muda na alikuwa amelazwa hospitali.
Shashi anatoka familia ya Kapoor ambayo imetawala tasnia ya filamu za Kihindi kwa miongo mingi.
Alishinda tuzo nyingi za filamu za taifa na alitunukiwa tuzo kuu ya heshima inayopewa raia na serikali ya India mwaka 2011, tuzo ya Padma Bhushan.
Aliigiza pia katika filamu kadha za Uingereza na Marekani.
Kapoor amefariki akitibiwa katika hospitali ya Kokilaben Dhirubhai Ambani mjini Mumbai.
Mpwa wake Randhir Kapoor ameambia Press Trust of India kwamba Kapoor amekuwa akitatizwa na figo kwa miaka mingi.
Shashi Kapoor in his younger days
Image captionShashi Kapoor alipokuwa kijana bado
Mwili wake utazikwa kesho asubuhi.
Alikuwa amemuoa mwigizaji mwingereza Jennifer Kendal, ambaye kwa pamoja walianzisha ukumbi maarufu wa sanaa Mumbai wa Prithvi mwaka 1978.