Saturday, November 18

Mwanajeshi wa Korea Kaskazini aliyetorokea K Kusini apatikana na minyoo mingi

Minyoo yapatikana ndani ya mwili wa mwanbajeshi wa Korea Kaskazini aliyetorokea Korea KusiniHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMinyoo yapatikana ndani ya mwili wa mwanbajeshi wa Korea Kaskazini aliyetorokea Korea Kusini
Mwanajeshi wa Korea Kusini aliyepigwa risasi alipokuwa akitorokea Korea Kusini katika mpaka wa mataifa hayo mawili amepatikana na vimelea vingi katika matumbo yake , kulingana na daktari wake.
Mtoro huyo alivuka eneo linalolindwa sana mpakani siku ya Jumatatu , lakini akapigwa risasi kadhaa na walinzi wa Korea Kaskazini.
Madaktari wanasema mwanajeshi huyo kwa sasa yuko katika hali nzuri , lakini idadi kubwa ya minyoo katika mwili wake unafanya hali yake kuwa mbaya.
Hali yake inaonyesha hali ya maisha yalivyo nchini Korea Kaskazini.
''Sijawahi kuona kitu kama hiki katika miaka yangu 20 kama daktari , daktari wa Korea Kusini Lee Cook-jong aliwaambia waandishi wa habari, akielezea kwamba kimelea mrefu katika tumbo lake alikuwa na urefu wa sentimita 27.
Mwanajeshi wa Korea Kaskazini akikimbizwa hospitalini Korea KusiniHaki miliki ya pichaEPA
Image captionMwanajeshi wa Korea Kaskazini akikimbizwa hospitalini Korea Kusini
Mwanadamu anaweza kupata vimelea kupitia kula chakula kichafu kwa kuumwa na wadudu ama vimela waliongia kupitia katika ngozi.
Kwa upande wa mwanajeshi huyo huenda vimelea hao waliingia kupitia chakula kichafu.
Korea Kaskazini inatumia kinyesi kama mbolea. Iwapo vinyesi hivyo havitibiwi na kutumiwa kama mbolea katika mboga ambayo haijapikwa ,vimelea hivyo vinaingia mdomoni hadi katika matumbo ya mwanadamu.

Pentagon yamtaka Trump kujiuzulu kimakosa

Ujumbe huo ambao pia uliwataka wanasiasa wengine wawili wa Marekani kujiuzulu kufuatia madai ya unyanyasaji wa kijinsia ulitumwa kutoka kwa akaunti ya @ProudResisterHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionUjumbe huo ambao pia uliwataka wanasiasa wengine wawili wa Marekani kujiuzulu kufuatia madai ya unyanyasaji wa kijinsia ulitumwa kutoka kwa akaunti ya @ProudResister
Ndio idara inayosimamia nambari za siri makombora, Idara inayosimamia usalama wa Marekani na mkuu wake ni rais wa Marekani ambaye hupendelea sana kutumia mtandao wa Twitter.
Lakini inapofikia wakati wa kusimamia akaunti yake ya mtandao huo, the Pentagon inafaa kuimarisha uwezo wake.
Siku ya Alhamisi idara hiyo ya ulinzi ilituma ujumbe kimakosa katika mtandao wake wa Twitter ukimtaka rais Trump kujiuzulu.
Ujumbe huo ambao pia uliwataka wanasiasa wengine wawili wa Marekani kujiuzulu kufuatia madai ya unyanyasaji wa kijinsia ulitumwa kutoka kwa akaunti ya @ProudResister, mwanaharakti ambaye ni mkosaji mkuu wa Trump.
Akaunti hiyo ilisema: Suluhu ni rahisi. Roy More jiuzulu katika kinyanganyiro. AI: Jiuzulu katika bunge la Congres, Donald Trump Jiuzulu katika urais. GOP: Wacha kulifanya swala la unyanyasaji wa kijinsia kuwa la kibinafsi.Ni uhalifu kama unafiki wao.
Ujumbe wa Trump uliosambazwa na akaunti ya idara ya ulinzi ya marekani kimakosaHaki miliki ya pichaTWITTER
Image captionUjumbe wa Trump uliosambazwa na akaunti ya idara ya ulinzi ya marekani kimakosa
Akaunti ya Idara hiyo ya ulinzi iliusambaza ujumbe huo kimakosa kwa takriban wafuasi wake milioni 5.2 kabla ya kuufuta.
Lakini makosa hayo yalionekana.
Picha ya ujumbe huo wa Pentagon lisambazwa na majibu yake pia yakawa ya haraka sana.

Rambo akana kumnyanyasa kingono shabiki wake mwenye umri wa miaka 16

Nyota wa filamu Sylvester StalloneHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionNyota wa filamu Sylvester Stallone
Nyota wa filamu Sylvester Stallone amekana ripoti kwamba yeye na mlinzi wake walimnyanyasa kingono shabiki wake wa miaka 16 mjini Las Vegas mapema miaka ya themanini.
Gazeti la mtandao la The Mail limechapisha kile linasema ni ripoti ya polisi kutoka 1986 ambayo ilielezea madai hayo.
Mwanamke huyo hakuwasilisha mashtaka dhidi ya Stallone kwa sababu alinyanyaswa na kuaibishwa mbali na kuwa na hofu.
Hakuna hatua iliochukuliwa.
Msemaji wa nyota huyo wa filamu ya Rocky alisema kuwa taarifa hiyo ilikuwa ya uwongo.
Michelle Bega aliyaelezea madai hayo kuwa ya uwongo, akiongezea : hakuna mtu aliyekuwa akijua kuhusu habari hiyo hadi ilipochapishwa leo, akiwemo bwana Stallone.
''Bwana Stallone hakuwasiliana na mtu yeyyote ama malaka ama mtu yeyote yule kuhusu swala hilo''.

Muswada kuwabana wenye nyumba waandaliwa


Dodoma. Serikali iko katika mchakato wa maandalizi ya muswada wa sheria ambayo itasimamia sekta ya nyumba, hivyo kuondoa changamoto ya wamiliki kudai kodi ya pango ya zaidi ya mwezi mmoja.
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula amesema hayo bungeni leo Ijumaa Novemba 17,2017 akijibu swali la nyongeza la mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Halima Bulembo.
Halima katika swali lake amesema vijana ambao ni kati ya asilimia 56 na 60 nchini, wanashindwa kutimiza ndoto zao kutokana na gharama kubwa ya kodi ambayo hutakiwa kulipa kwa kipindi cha mwaka mmoja au miezi sita.
"Serikali inasemaje kuhusu kuleta sheria itakayofuta tabia ya wenye nyumba kulazimisha kulipwa kodi ya mwaka?" amehoji mbunge huyo.
Akijibu swali hilo, Mabula amesema Serikali imeliona tatizo hilo na ipo katika mchakato wa kuandaa muswada wa sheria utakaosimamia sekta hiyo.
Mabula amesema baada ya kukamilika kwa sheria ambayo itaunda chombo cha kusimamia sekta hiyo, wapangaji hawatalipa kodi ya mwaka wala miezi sita tena bali watalipa kwa mwezi na kuweka amana ya miezi mitatu.
Katika swali la msingi, Halima amesema kumekuwa na upandaji holela wa gharama za pango kwa nyumba za Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).
"Je Serikali haioni kuna haja ya kudhibiti upandaji holela ambao unaathiri wananchi wengi kutokana na kipato chao?" amehoji.
Akijibu, Mabula amesema utaratibu wa urekebishaji wa viwango vya kodi za shirika hilo husimamiwa na bodi ya wakurugenzi ambayo imepewa mamlaka ya kisheria ya kusimamia kodi ya pango na kuidhinisha viwango vya kodi vinavyotozwa kwa wapangaji wa nyumba za shirika.
"Kwa mara ya mwisho bodi ya wakurugenzi ya Shirika la Nyumba la Taifa iliidhinisha viwango vipya vya kutoza kodi kwenye nyumba za shirika mwaka 2011 ambavyo ndivyo vinavyotumika mpaka sasa," amesema.

Nuzulack Dausen apeta tuzo za mwandishi bora Afrika


Addis Ababa-Ethiopia. Mwandishi mwandamizi wa kampuni ya Mwananchi Communications Ltd (MCL), Nuzulack Dausen ameshinda tuzo ya mwandishi bora Afrika wa masuala ya nishati na miundombinu katika tuzo za umahiri wa habari Afrika za Zimeo zilizotolewa jana Alhamisi usiku jijini hapa.
Zimeo ambazo zimetolewa kwa mara ya tatu sasa ni tuzo maarufu katika tasnia ya habari barani Afrika sambamba na tuzo za CNNMultichoice ambazo zimekuwa zikitolewa kila mwaka.
Tuzo hizo za Zimeo hutolewa na shirika linaloshughulikia ukuaji wa tasnia ya habari Afrika ya African Media Initiative (AMI) yenye makazi yake jijini Nairobi, Kenya na kudhaminiwa na mashirika mbalimbali ya kimataifa yakiwemo Unesco, Kamisheni ya Uchumi ya Afrika ya Umoja wa Mataifa (ECA) na Shirika la Habari la Al-Jazeera.
Katika kipengele cha nishati na mazingira, Dausen alikuwa akichuana na wanahabari Jeffrey Moyo ambaye huandikia Shirika la Habari la Thomson Reuters na The New York Times na Femi Asu wa gazeti la The Punch la nchini Nigeria.
"Kwanza namshukuru Mungu kwa tuzo hii ya heshima katika maisha yangu ya uandishi wa habari na nawashukuru viongozi na wafanyakazi wenzangu wa MCL kwa kunijenga kitaaluma na kunitia moyo kwa kila nachojaribu kukifanya.
"Pia nawashukuru familia yangu kwa kunipa moyo wa kufanya kazi kwa bidii na kukubali kunikosa kwa muda napokuwa katika majukumu ya kazi nje ya Dar es Salaam na wasomaji ambao maoni yao hunijenga zaidi," amesema Dausen.
Dausen, ambaye ni mhariri wa habari za takwimu wa MCL, amesema uhuru wa habari na uandishi mahiri wa habari unaochambua masuala kwa kina utasaidia kuchochea maendeleo Tanzania na duniani kwa ujumla kwa kuainisha fursa na kutoa majibu ya changamoto zinazoikabili jamii.
Habari iliyompa ushindi Dausen inahusu namna wakazi wa vijiji vya Namikango A na B wilayani Nachingwea mkoani Lindi Tanzania walivyotumia fursa ya umemejua kupata mwanga na kukabiliana na umaskini. Habari hiyo ilichapwa katika gazeti dada la The Citizen zaidi ya miezi miwili iliyopita.
Akizungumzia vigezo vya utoaji tuzo hizo, Jaji Mwandamizi katika tuzo hizo Dk George Nyabuga wa Chuo Kikuu cha Nairobi (UoN) amesema walizingatia vigezo vingi vya kihabari vikiwemo uhalisia wa wazo la habari, mpangilio wa hoja na umahiri wa kueleza habari hiyo ikaeleweka na wananchi wa kawaida.
Vigezo vingine ni namna mada husika inavyowagusa wananchi, matumizi ya takwimu na uzingatiaji misingi ya habari ya usawa, weledi, na ukweli.
"Haikuwa kazi rahisi kuchambua mamia ya kazi za wanahabari Afrika nzima hadi kupata washindi wetu leo, " amesema Dk Nyabuka.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa AMI, Erick Chinje amesema ili vyombo vya habari viwe na msaada kwa watu wa Afrika ni lazima tasnia ya habari iboreshe utendaji wake kwa kuripoti na kuchambua masuala yanayogusa wananchi.
"Mchango wa AMI umekuwa katika kuandaa mipango ambayo itawasaidia wanahabari kuongeza uwezo wao kitaaluma na mbinu nyingine zitakazofanya wawe bora zaidi. Tuzo za Zimeo zitawatambua wanahabari waliofanya vyema katika kuripoti sekta muhimu katika maisha ya watu," amesema Chinje.
Baadhi ya wanahabari walioshinda tuzo hizo jana usiku ni Dorcas Wangira kutoka Kenya, Ridwan Dini-Osman kutoka Ghana na Jay Caboz wa Afrika Kusini aliyeibuka mshindi wa jumla wa tuzo hizo.

TRA yapeleka elimu ya kodi kwa wachimbaji

Mkurugenzi wa huduma na elimu ya mlipa kodi
Mkurugenzi wa huduma na elimu ya mlipa kodi (TRA) Richard Kayombo 

Geita. Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wametoa elimu ya mlipa kodi kwa wachimbaji wadogo mkoani Geita ili watekeleze agizo la Serikali la kulipa asilimia tano wanapouza madini kwa mujibu wa sheria.
Mkuu wa idara ya huduma na elimu wa TRA mikoa ya Kanda ya Ziwa, Lutufyo Mtafya alisema wameamua kuwafuata wachimbaji hao maeneo yao ili kuwaelimisha watimize matakwa ya kisheria ya kulipa kodi.
Baadhi ya wachimbaji hao eneo la Rwamgasa wilayani Geita, walisema uelewa duni kuhusu sheria ya ulipaji kodi ndiyo sababu inayowafanya kutolipa kodi.
Emmanuel Samson alisema ni vyema elimu ikatolewa zaidi kwa kuwa sasa wanashindwa kuelewa, kwani awali walijua kodi ya halmashauri na ya mmiliki wa kiwanja lakini nyongeza ya asilimia tano nyingine ni mzigo kwa wachimbaji.

Serikali zatakiwa kuwajengea uwezo wataalamu wa afya


Taasisi ya magonjwa yasiyoambukizwa, usalama wa chakula na lishe kupitia Shirika la Kikanda la Afya (ECSA) limetaka Kenya, Tanzania na Uganda kuweka umuhimu wa kuwajengea uwezo wataalamu wa afya wa ngazi za chini ili waweze kutoa elimu stahiki kwa jamii.
Akizungumza leo Ijumaa Novemba 17,2017 wakati wa mkutano wa siku mbili uliohusisha nchi hizo tatu, meneja wa taasisi hiyo, Rosemary Mwaisaka amesema ili kutokomeza udumavu na magonjwa yasiyoambukizwa ni muhimu kuwekeza kwa watumishi wa afya wanaotoa huduma za kila siku kwenye vituo vya afya.
“Kwa kutambua hilo, tumetengeneza vitini kwa ajili ya watenda kazi katika ngazi ya vituo vya afya na jamii ili kutoa ujuzi katika masuala ya lishe, usalama wa chakula na kuepukana na magonjwa yasiyoambukizwa,” amesema Rosemary.
Amesema kwa muda mrefu wamekuwa wakifanya kazi peke yao lakini lishe ni suala mtambuka.
Mwakilishi wa Wizara ya Afya nchini Kenya,  Peter Cherotich amesema wamepokea vitini na kwamba, suala linalofanyiwa kazi sasa ni kuhakikisha usalama wa chakula na lishe unatiliwa mkazo.

Zitto ataka Serikali kununua tumbaku ya wakulima


Urambo. Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe ametaka Serikali kununua tumbaku yote ya wakulima iliyoshindikana kununuliwa.
Akihutubia wananchi leo Ijumaa katika mkutano wa kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani katika Kijiji cha Kalemela A, Kata ya Muungano wilayani Urambo Zitto ameishangaa Serikali kutumia fedha nyingi kununua ndege aina ya bombardier zinazopakia watu wachache badala ya kuwekeza kwenye kilimo kinachoajiri wananchi wengi.
Zitto amesema katika ziara yake amezunguka vijijini na kushuhudia nyuso za huzuni, huku wananchi wakimwambia tumbaku ya mwaka jana haijauzwa na msimu mpya umeanza.
“Serikali makini ingefanya nini kwenye kadhia hii ya tumbaku? Sisi ACT- Wazalendo tungekuwa madarakani tungenunua tumbaku yote ya ziada ya wakulima kwa kutumia kasma ya fedha za dharura kwenye Fungu la 50 Wizara ya Fedha,” amesema.
Amesema Serikali iliwahimiza wananchi kufanya kazi kwa bidii, lakini baada ya kuzalisha kwa wingi wanaadhibiwa kwa kukosa masoko.
Zitto ameshauri Serikali kutafuta soko kwa mfumo uliosema ni wa G to G (Government to Government) na kuuza tumbaku hiyo na kurejesha fedha hizo kwenye mfuko wa dharura.
Amesema wakati asilimia 65 ya Watanzania wanategemea kilimo kama ajira, kilimo kimekuwa kikishuka na kusababisha wakulima kuendelea kuwa masikini na kukosa chakula.
“Tunazalisha watu zaidi kuliko chakula, ni dhahiri tunaelekea kubaya,” amesema Zitto.
Amesema katika hali hiyo ya kudumaa kwa kilimo bado wakulima wa Tabora hawajafutwa machozi na zao lao la tumbaku wakati ndilo linaloingiza fedha za kigeni kuliko korosho.
“Serikali ipo tayari kutumia Sh1 trilioni kulipia ndege ambazo ni Watanzania asilimia tano wanapanda kuliko kuokoa wakulima 1.4 milioni wa tumbaku nchi nzima kwa Sh150 bilioni tu, tena ikiwa fedha hizo zinarudi ndani ya muda mfupi,” amesema Zitto.
Amewataka wananchi wa kijiji hicho kuchagua mgombea udiwani wa chama hicho ili apambane kuhakikisha tumbaku ya mwaka jana inanunuliwa.
Amesema Ilani ya Uchaguzi ya ACT -Wazalendo ilitangazwa na Taasisi ya Mviwata (Muungano wa vikundi vya wakulima) kuwa ilani bora zaidi kuhusu masuala ya kilimo kuliko ilani za vyama vyote katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 kwa kuwa ilipendekeza kuwapo kwa Hifadhi ya Jamii kwa Wakulima.

Mabomu yatikisa Nairobi


Nairobi, Kenya. Umati mkubwa wa wafuasi wa muungano wa Nasa umejitokea kumpokea kiongozi wao, Raila Odinga katika sherehe zilizogeuka kuwa za vurugu, mabomu ya machozi na mapambano ya kukimbizana na polisi.
Watu wawili wanadaiwa kufariki dunia baada ya kupigwa na kinachosadikiwa kuwa ni risasi wakati polisi wakiwatawanya watu waliokuwa wanatembea kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA) walipokuwa wakitembea sambamba na msafara wa kiongozi huyo wa Nasa aliyerejea mchana leo akitokea Marekani alikofanya ziara ya siku 10.
Mapema, polisi na wafuasi wa Raila walipambana katika barabara ya kuelekea uwanja wa ndege kabla ya Raila kuwasili.
Licha ya ulinzi huo na moshi wa mabomu ya machozi wafuasi wa Nasa wapatao 200 wakiwemo wanawake walifanikiwa kupita utepe uliowekwa na vyombo vya usalama na wakaingia hadi ndani ya uwanja.
Helikopta ya polisi ilikuwa ikizunguka juu ya uwanja huo huku magari ya maji ya kuwasha na magari ya maalumu ya kusafisha njia yalikuwepo uwanjani hapo na yalitumika kuzima moto wa matairi.
Lakini wakati Raila akiondoka katika msafara wenye makumi ya magari yakiwemo ya viongozi wa Nasa na mamia ya wafuasi, yalizuka mapambano huku polisi wakitumia magari ya kurusha maji ya kuwasha, mabomu ya machozi huku waandamanaji wakirusha mawe na fimbo.

Jeshi la Polisi lasaidiwa vifaa tiba


Dar es Salaam. Jeshi la Polisi limepokea vifaa tiba kutoka shirika la Project Cure la nchini Marekani vyenye thamani ya Sh2 bilioni.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Simon Siro akizungumza alipopokea vifaa hivyo katika Hospitali Kuu ya Polisi Kilwa Road leo Ijumaa Novemba 17,2017, amesema vitasambazwa katika vituo vya tiba vya polisi 20.
IGP Siro amesema wanalenga kuhakikisha askari wanapata huduma bora na kuwafanya wawe imara katika kutekeleza majukumu yao.
“Tutajitahidi kuwasomesha wataalamu wetu wa afya ili waweze kufanya kazi kwa weledi. Hospitali kuu ya polisi ipo vizuri, hivyo tunawakaribisha kwa yeyote atakayehitaji kutibiwa hapa kwa kuwa ina vifaa bora,” amesema IGP Siro.
Pia, amezindua majengo matatu katika hospitali hiyo ambayo ni kwa ajili ya  wagonjwa mahututi, stoo kuu ya dawa na jengo la kuhifadhia maiti.
Kamanda wa Afya, Paul Kasabago amesema wanakabiliwa na changamoto ya vifaa tiba katika wodi ya wagonjwa mahututi itakayofunguliwa.
Kasabago amesema wanahitaji mashine za CT- scan na MRI ili kuendelea kuboresha hospitali hiyo iweze kutimiza vigezo vya kuwa hospitali ya rufaa.
Ameishukuru Serikali ya watu wa Marekani kupitia shirika la misaada la USAID kwa kufadhili juhudi za Serikali ya Tanzania katika kupambana na Ukimwi kupitia shirika lisilo la kiserikali la JSI na AIDSfree Tanzania linalofanya kazi na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi katika majeshi ya Polisi na Magereza.
Mkurugenzi mkuu wa Shirika la JSI, Peter Maro amesema mradi wa AIDSFree umetoa mafunzo kwa watumishi wa afya katika nyanja mbalimbali za utoaji wa huduma za Ukimwi na Kifua Kikuu.

Mgombea udiwani kizimbani kwa kujeruhi


Mwanza. Mgombea udiwani kata ya  Mhandu (Chadema), Godfrey Misana na kampeni meneja wake, Charles Chinjibela, wamepandishwa kizimbani kujibu shtaka la kujeruhi.
Misana (46) na Chinjibela (37) wanadaiwa kumjeruhi meneja wa kampeni za CCM katika kata hiyo, Thomas Warioba.
Katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mwanza, mbele ya hakimu Ainawe Moshi wanadaiwa kutenda kosa hilo Novemba 14,2017.
Akisoma mashtaka katika shauri hilo namba 540/2017, mwendesha mashtaka wa Jamhuri, Elizaberth Barabara amedai leo Ijumaa Novemba 17,2017 kuwa washtakiwa walitumia visu na mawe kumjeruhi Warioba.
Kabla ya kuhamia CCM, Warioba alikuwa mwanachama wa Chadema.
Upande wa Jamhuri umeiomba Mahakama kuzuia dhamana ya washtakiwa kwa kile ilichoeleza ni kwa usalama wao.
Ombi hilo la Jamhuri limepingwa na wakili wa utetezi, Gasper Mwanaliela.
Wakili Mwanaliela amesema dhamana ni haki ya wateja wake na kwamba, kuwanyima kutawazuia kushiriki kikamilifu katika kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani unaotarajiwa kufanyika Novemba 26,2017.
Baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili, Hakimu Moshi amesema Mahakama itatoa uamuzi kuhusu dhamana Novemba 21,2017.
Washtakiwa wamepelekwa mahabusu hadi siku huyo.

Vurugu, mabomu vyatawala mapokezi ya Raila


Nairobi, Kenya. Vurugu, mabomu ya machozi, na mapambano ya kukimbizana ni baadhi ya matukio yaliyogubika mapokezi ya kiongozi wa muungano wa Nasa Raila Odinga katikati ya jiji la Nairobi aliporejea jana akitokea Marekani alikofanya ziara ya siku 10.
Polisi walitumia mabomu ya machozi na maji ya kuwasha kuwatawanya wafuasi wa Nasa ambao walijitokeza kwa mamia kumpokea Raila. Kuna madai kwamba risasi zilitumika na pia inadaiwa watu wawili walikufa katika makabiliano huo
Kioo cha mbele cha gari alilopanda Raila kiliharibiwa wakati polisi wakifukuzana na wafuasi wa kiongozi huyo. Hata hivyo, haikuweza kufahamika mara moja ikiwa kiliharibiwa kwa risasi au jiwe.
Kioo hicho kiliharibiwa katika Barabara ya Jogoo. Raila hakudhuriwa na msafara wake uliongoza moja kwa moja hadi Kibra ambako alihutubia mkutano mkubwa wa wafuasi wake.
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani Mwenda Njoka alitupilia mbali madai ya kuwepo jaribio la kutoa uhai wa Raila. "Madai kwamba lilikuwepo jaribio la kutoa uhai wa Raila ambayo yanasambazwa kwenye mitandao ya kijamii ni ya uongo na hayana msingi,” alimsema katika ujumbe wa Twitter.
Njoka alisema madai hayo yanayosambazwa kupitia akunti iliyothibitika kuwa ni ya muungano wa Nasa ina lengo la kuomba huruma. “Madai hayo yapuuzwe na yadharauliwe,” alisema.
 Msafara wa Raila
Raila aliondoka kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA) katika msafara wa makumi ya magari yaliyoongozana nay a viongozi wa Nasa pamoja na mamia ya wafuasi wao.
Wafuasi wake walijimwaga mitaani tangu alipotua. Baadhi walilazimisha kufika na kuingia kwenye uwanja wa ndege ambako walizuiwa na polisi walikuwa wamejihami kwa silaha, mabomu ya kutoa machozi, magari ya kurusha maji ya kuwasha na helikopta.
Baadaye hali ilibadilika kuwa ya vurugu na mapambano kati ya polisi na wafuasi wa Nasa ambao walikuwa wakichoma matairi barabarani, wakiweka vizuizi, wakiwakejeli polisi na kuwarushia mawe, vijinga vya moto huku wakiimba.
Vurugu zilianza baada ya msafara wa Raila kuondoka JKIA lakini ukaingia kimakosa katika barabara ya Mombasa. Hii ni kwa sababu barabara hiyo ilikuwa na msafara mrefu umbali wa kilomita kadhaa kutokana na mapambano ya polisi na wafuasi wa Raila.
Wafuasi wa Nasa walitaka kulazimisha kuingia kwenye uwanja wa ndege lakini polisi waliwarushia mabomu ya kutoa machozi eneo la City Cabanas na maeneo mengine ili kuwazuia.
Baadaye msafara huyo uliacha barabara ya Mombasa na kuingia Barabara ya Jogoo lakini vurugu ziliufuata msafara wa Raila na wafuasi wake baada ya polisi kupambana na vijana walikuwa wakirusha mawe.
Lengo lao lilikuwa kutembea kwa miguu katika Barabara ya Jogoo kisha Haile Sellasie halafu waende viwanja vya Uhuru Park, lakini ilishindikana kutokana na mkabiliano wa ghasia.
 Hasara
Mapambano kati ya polisi na wafuasi wa Nasa yalisababisha biashara kusimama katika barabara hiyo ya kibiashara upande wa mashariki mwa jiji.
Mzunguko katika Uwanja wa Jiji ulitulia baada ya polisi kuziba barabara katika juhudi za kuzuia vurugu kuenea katika maeneo mengine ya jiji. Kwa kipindi kirefu magari yalitulia huku vibanda vya biashara vikifungwa na wauzaji wakikimbia kwa usalama wao.
Basi dogo linalomikiwa na kampuni ya Forward Travellers sacco, lori la polisi na mikokoteni miwili vyote vilichomwa moto nje ya soko la Burma. Barabarani kulikuwa na moshi wa matairi yaliyochomwa moto uliochanganyika na hewa ya machozi iliyopigwa kwa mabomu ya polisi.

Spika aunda kamati mbili kuchunguza sekta ya uvuvi, gesi


Dodoma. Spika wa Bunge, Job Ndugai ameunda kamati mbili zitakazoshughulikia sekta ya uvuvi wa bahari kuu na gesi akisema lazima wajue ni kwa nini hazichangii pato la Taifa.
Ndugai ameunda kamati hizo baada ya zingine mbili za kutathmini mfumo wa uchimbaji, usimamizi, umiliki na udhibiti wa madini ya Tanzanite na almasi kuwasilisha taarifa kwa Rais John Magufuli Septemba,2017 na kusababisha baadhi ya mawaziri kujiuzulu.
Akitangaza kamati za sekta ya uvuvi na gesi bungeni mjini Dodoma leo Ijumaa Novemba 17,2017, Spika Ndugai amemrejesha Dotto Biteko aliyeongoza kamati iliyochunguza Tanzanite kuwa mwenyekiti wa kamati itakayochunguza sekta ya gesi.
Mussa Zungu alikuwa mwenyekiti wa kamati iliyochunguza almasi na sasa ni mjumbe katika kamati ya uvuvi.
Ndugai akitangaza kamati hizo amesema anatumia kanuni ya 5(1) ya Kanuni za Bunge toleo la 2016 ambayo inampa madaraka ya kuziunda kwa kadri atakavyoona inafaa.
Amesema kumekuwa na hali ya kusuasua kwa sekta hizo, ukiwemo uvuvi wa bahari kuu. Amesema sekta hiyo inachangia pato la Taifa kwa asilimia 1.4 ambayo ni sawa na Sh3.2 bilioni wakati kuna zaidi ya Sh400 bilioni ambazo zinapotea bure.
Spika Ndugai amewataja wajumbe wa kamati ya sekta ya uvuvi itakayoongozwa na Anastazia Wambura kuwa ni Zungu, Salum Mwinyi Rehani, Masoud Salim Abdalla, Tauhida Nyimbo, Mbaraka Dau, Dk Immaculate Semesi, Dk Christina Ishengoma, Stanslaus Mabula, Mussa Mbarouk na Cosato Chumi.
Kamati ya sekta ya gesi itaundwa na Innocent Bashungwa, Dastan Kitandula, Dk Seleman Yusufu, Wanu Hafidhi Ameir, Oscar Mukasa, Ruth Mollel, Richard Mbogo, Omari Kigua, Abdallah Mtolea na Sebastian Kapufi.
Spika Ndugai amemwagiza Katibu wa Bunge kuwawezesha wabunge hao ili waanze kazi na kamati zimetakiwa kufanya kazi ndani ya siku 30 tangu siku watakayokabidhiwa majukumu yao.

Abiria mmoja anusurika ajali ya ndege iliyoua 11 Ngorongoro


Arusha. Mfanyakazi wa hoteli za kitalii za andBeyond Serengeti, Moses Muhina aliyetajwa kuwa ni miongoni mwa abiria waliofariki dunia katika ajali ya ndege ya shirika la Coastal Aviation, imebainika alibadili ndege muda mfupi kabla ya safari ili kuwahi kazini.
Muhina ambaye ni mwongozaji watalii katika hoteli hiyo, alikuwa aondoke na ndege ya Coastal Aviation saa nne asubuhi lakini viongozi wa hoteli walimbadilishia ndege, hivyo aliondoka na Air Exel iliyofika salama Serengeti.
Akizungumza na Mwananchi leo Ijumaa Novemba 17,2017 Meneja Uendeshaji wa hoteli ya andBeyond Serengeti UnderCanvas, Mussa Matala amesema Muhina ambaye anasomeka kwenye orodha ya ndege kama Maina alikuwa apande ndege hiyo lakini waliamua kumbadilishia ili awahi kazini.
Amesema waliomba aondolewe kwenye orodha ya wasafiri wa ndege hiyo lakini kwa bahati mbaya hadi ndege ilipoondoka jina lake lilikuwepo.
Wakati huohuo, raia watano wa kigeni ambao walifariki dunia katika ajali ya ndege ya Coastal Aviation, akiwemo rubani, Dewald Raubenheimer raia wa Afrika Kusini, ambaye kwenye orodha ya awali ya waliofariki jina lake halikuwepo inatarajiwa kusafirishwa Jumapili Novemba 19,2017.
Mhudumu wa chumba cha kuhifadhi maiti  katika Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru, Francis Costa amesema miili mitatu kati ya 11 imechukuliwa na ndugu.
Amesema miili iliyochukuliwa ni ya ndugu wawili waliokuwa wakurugenzi wa Masai Wondering, Nasibu na Shatri Mfinanga. Mwingine ni wa Joyce Mkama ambaye alikuwa mfanyakazi wa hoteli ya Serena.
"Uchunguzi wa miili ya wageni kutoka nje ya nchi unaendelea na ukikamilika itasafirishwa kwa mazishi katika nchi za Afrika Kusini, Ujerumani na Italia," amesema.
Ndege hiyo namba 5H-EGG aina ya Cessna Grand Caravan ilianguka baada ya kugonga kingo za creta ya Empakai, umbali wa mita 3,250 kutoka usawa wa bahari ikitoka Kilimanjaro kwenda Hifadhi ya Serengeti.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo amesema uchunguzi unaendelea kuhusu ajali hiyo.

Friday, November 17

USAID funded projects in Iringa voiced how keen their, in transforming people live

 The Chief of Party of the Sauti Project a Jhpiego’s lead program Dr. Albert Komba elaborating a point to the USAID Mission Director in Tanzanian Andy Karas when he visited projects interventions conducted to reduce HIV/Aids prevalence to the vulnerable groups in Iringa. The program is conducting Behavior Change Communication Sessions, Screening for Gender Based Violence and cancelling on usage of Alcohol and Drugs to the Vulnerable groups including young girls.
 Scholina Charles (22) a young girl from umoja groups in iringa giving her testimony to the USAID Mission Director in Tanzanian Andy Karas and his delegation on the risk she went through before joining the Sauti project to fight HIV/ AIDS. Looking center is the Sauti Project Chief of Party Dr. Albert Komba .
 The USAID Mission Director in Tanzanian Andy Karas,  Deputy Mission Director Helen Pataki (second right), Jhpiego Country Director (right) and Sauti Project Chief of Party Dr. Albert Komba (left) following a Behavior Change Communication Sessions conducted by Zera Mingo (23) to the young adolescences girls as part of HIV/ AIDS intervention to reduce HIV/Aids prevalence to the vulnerable groups in Iringa.
 The USAID Mission Director in Tanzanian Andy Karas and his Deputy Mission Director Helen Pataki looks at the clothes made by Mwanahamisi Mketo (23) during his field visit in Iringa to assess the implementation of USAID funded Project activities. Mwanahamisi Mketo she is a member of Behavior Change Communication group conducted by Jhpiego at kihesa ward in Iringa who are also economically empowered. 

The United State Agency for International Development (USAID) funded projects in iringa has demostrated how their bringing impacts to the lives of the people in Iringa. This expression was made by USAID funded NGO’s and local CSO’s to the newly USAID Mission Director in Tanzanian Andy Karas who conducted a field visit in Iringa to assess the implementation of USAID funded Project activities.

Andy who was accompanied by his deputy Mission Director Helen Pataki and other USAID staff expressed his appreciation to the regional administration and local authorities for the support their giving to all implementing partners funded by USAID in the region and thanks them for their work their doing for the people of Iringa.    

Explaining on how they engage the local authorities and the entire community to fight the spread of the HIV/AIDS in Iringa, the Chief of Party with Sauti Project a Jhpiego’s lead program Dr. Albert Komba said despite the fact that the project works in 14 region countrywide, in Iringa Municipal they targets all Vulnerable groups including young girls by  linking them into services like Behavior Change Communication Sessions, Economic Empowerment groups, Screening for Gender Based Violence and cancelling on usage of Alcohol and Drugs.

“we are working to ensure we reduce the spread of HIV/AIDS because the groups we are targeting like these adolescence girls and female sex workers are more vulnerable and engaging them in the fight against HIV will lead to an HIV/AIDS free generation in Iringa” said Dr. Komba

As part of their interventions to reduce HIV/Aids prevalence, the project also has mobilized girls to form WORTH+ groups which is the voluntary money saving groups for income generating activities, and train them on economic empowerment, gender issues and how to protect themselves against high risk behaviors of which most girls from these groups have managed to change their lives by living a decent life.

Reaching a testimonie delivered by Scholina Charles (22) a young girls from umoja groups on the risk she went through before joining the sauti project, she said the situation was devastating and because of her economic status from her family she got engaged into sex business as part of income generating.

“The situation was bad, I remember men used to bribe me even for two hundred shilling to have sex with them and I had no option. But now that I have joined this group, I am empowered with self-awareness on the risk of HIV/AIDS, gender violence, and through this group I have also managed to raise money and now I am engaging into agricultural activities and employ men in my maize farm”. Said Scholina.

Earlier speaking with USAID delegation and other USAID funded implementing partners, the Iringa Regional Administration Secretary Wamoja Ayubu thanks the delegation for the support they are giving to the region level by complimenting government effort in the health sector agriculture sector and other sectors especially by emphasizing the inclusion and empowerment of youth and woman. 

“The government has policy and laws which advocates for the inclusion of gender especially youth and woman in all activities, I am happy that USAID is also advocating that and we promise to collaborate with all partners to empower them especially locals so that they bring up new ideas for development and at the regional level. In our side we will chip in to address all challenges that might be faced by our implementing partners” she insisted.

Sauti is implemented by Jhpiego in partnership with Pact, Engenderhealth and NIMR/ Mwanza with support from the American people through USAID under the United States President’s Emergency Plan for AIDS Relief (PEPFAR) and DREAMS Initiatives.