Monday, October 30

Wanawake kuruhusiwa kuingia viwanja vya michezo Saudi Arabia

Saudi women sit in a stadium to attend an event in the capital Riyadh on 23 SeptemberHaki miliki ya pichaAFP
Image captionWanawake wa Saudi Arabia kuruhusiwa kuingia viwanja vya michezo
Saudi Arabia itawaruhusu wanawake kuhudhuria michezo katika viwanga vya michezo kwa mara ya kwanza kuanzia mwaka ujao.
Familia zitaweza kuingia kwenye viwanja vitatu vya michezo vya - Riyadh, Jeddah na Dammam.
Ni hatua nyingine ya kuwapa wanawaka wa Saudi Arabia uhuru zaidi, ambao kawaida hukumbwa na ubaguzi wa kijinsia na baada ya kuendolewa marufuku ya kuendesha magari.
Mfalme Mohammed bin Salman yuko katika harakati kubwa kuifanya Saudi Arabia kuwa nchi ya kisasa na kuboresha uchumi.
Mabadiliko hayo yanaambatana na mipango mikubwa ya mabadiliko yaliyotangazwa na mfalme huyo wa umri wa miaka 32 kuleta mabadiliko ya kijamii na kiuchumi kwa taifa hilo linalotegemea mafuta, yanayojulikana kama maoni ya mwaka 2030.
Women walk on Tahlia street in the Saudi capital Riyadh on 24 SeptemberHaki miliki ya pichaAFP
Image captionWanawake wa Saudi Arabia kuruhusiwa kuingia viwanja vya michezo
Mwezi uliopita amri ya kifalme ilisema kuwa wanawake wanaweza kuendesha magari kwa mara ya kwanza kuanzia mwezi Juni mwaka ujao. Warsha zinafanywa na sinema zinatarajiwa kurejeshwa tena.
Siku ya Jumatano Prince Mohammed alisema kurejeshwa kwa uislamu wa wastani ni kiungo muhimu cha kuifanya nchi kuwa ya kisasa.
Alisema kuwa asilimia 70 ya watu nchini Saudi Arabia wana umri wa chini ya miaka 30 na alisema kuwa wanahitaji maisha ambayo yanastahili dini.
Lakini wadadisi wanasema mipango haitakosa pingamiza.
Wanawake nchini Saudi Arabia bado ni lazima wafuate mitindo ya mavazi na wasikuwe na mahusiano na wanaume wasiostahili.

Iran: Tutaunda silaha yoyote kujilinda

Rais Hassan RouhaniHaki miliki ya pichaAFP
Image captionRais Hassan Rouhani
Rais wa Iran amesema kuwa nchi yake itaunda silaha zozote inazohitaji kujilinda dhidi ya uvamizi.
Wakati akihubia bunge Rais Hassan Rouhani, alisema kuwa Iran haitakuwa ikikiuka makubaliano yoyote ya kimataifa kwa kuunda silaha yakiwemo makombora ya masafa marefu.
Aliionya Marekani kuwa ukiukaji wa mkataba wa nyuklia uliotiwa sahihi kati ya Iran na mataifa sita yenye nguvu ni kwa manufaa yake.
Rais wa Marekani Donald Trump hivi karibuni alikataa kuidhinisha mkataba huo akiitaja Iran kama nchi kaidi inayounga mkono ugaidi.

Ndege ya Urusi iliyotoweka yapatikana chini ya bahari Norway

A 2011 photo of the Russian Mi-8 helicopter at BarentsburgHaki miliki ya pichaAFP
Image captionPicha ya mwaka 2011 ya ndege ya Mi-8 helicopter ikiwa Barentsburg
Norway inasema kuwa kundi la watafutaji limepata mabaki ya ndege ya Urusi aina ya helikopta, ambayo ilianguka baharini ikiwa na watu 8 ndani yake.
Ndege hiyo ambayo haikuwa haijulikani iliko tangu Alhamisi, kwa sasa iko chini ya bahari karibu na eneo la Barentsburg, kwa mujibu wa maafisa.
Polisi nchini Norway sasa wanaweza kuwatafuta wale waliokuwa ndani ya ndege hiyo, taarifa hiyo ilisema.
map
Image captionRamani
Ofisi ya Urusi huko Barentsburg inasema kuwa wahudumu watano na wanasayansi watatu, walikuwa ndani ya ndege hiyo wote raia wa Urusi na kuna hofu kuwa wamefariki.
Ilikuwa katika safari fupi kutoka Pyramiden kwenda Barentsburg eneo la madini la Urusi.
Pyramiden, 19 Jul 15Haki miliki ya pichaAFP
Image captionEneo la madini la Urusi la Pyramiden

Aliyekuwa kiongozi wa Catalonia anaweza kugombea tena

Carles Puigdemont, 28 OctoberHaki miliki ya pichaEVN
Image captionKiongozi wa Catalonia aliyefutwa anaweza kugombea tena
Serikali ya Uhispania inasema kuwa inakaribisha kushiriki kwa kiongozi aliyefuwa wa Catalonia Carles Puigdemont kwenye uchaguzi mpya.
Serikali ya Madrid imeamrisha kuwa uchaguzi mpya kwa bunge la eneo la Catlonia utafanyika mwezi Disemba.
Madrid ililivua eneo la Catalonia utawala wake baada ya bunge la Catalonia kupiga kura ya kujitangazia uhuru,
Bwana Puigdemont amewashauri watu kukataa udhibiti kamili kutoka Madrid.
Alilaani kufutwa kwa utawala wa Catalonia na kuahidi kuendelea kufanya kazi ya kujenga nchi ili huru.
Wakati huo huo mamia ya raia wa Uhispania wamekusanyika katika mji mkuu Barcerlona kuunga mkono umoja wa Uhispania.
Aidha Uhispania inaendelea kushinikiza kuchukua udhibiti wa nguvu dhidi ya serikali ya jimbo la Catalonia, iliyofutiliwa mbali.

Mamia ya wafuasi wa IS wakamatwa Uturuki

Polisi wa Uturuki wakiwa katika mazishi ya mmoja wa polisi mwenzo aliyeuawa na IS mwezi Agosti
Image captionPolisi wa Uturuki wakiwa katika mazishi ya mmoja wa polisi mwenzo aliyeuawa na IS mwezi Agosti
Polisi nchini Uturuki imewakamata mamia ya watu wanaodhaniwa kuwa wafuasi wa kikundi cha wanamgambo wa IS.
Raia wawili wa Azerbaijan na wengine 28 wa Syria, ni miongoni mwa waliokamatwa katika mji wa Mashariki wa Erzurum na mji wa Bursa uliopo Kaskazini Magharibi.
Wengine walikamatwa katika mji mkuu Ankara siku ya Jumamosi.
Mpiganaji wa IS aliwaua watu 39 katika ukumbu mmoja wa usiku uitwao Reina mjini Istanbul, na tukio hilo bado limeacha simanzi kubwa.

Polisi yadhibiti shambulizi la al-Shabab lilouwa 23

Askari akipita karibu na mabaki ya gari lililolipuka mjini Mogadishu, Somalia Jumamosi, Octoba 28, 2017.
Polisi nchini Somalia wamesema Jumapili kuwa wameweza kudhibiti shambulizi la waasi wa kikundi cha Kiislam kilichokuwa  kimeizingira hoteli moja katika mji mkuu Mogadishu.
Maafisa wa polisi wamesema kuwa watu wasiopungua 23 wameuawa katika shambulizi hilo katika hoteli mbili maarufu za Nasa Hablod Mogadishu. Dozeni ya watu wengine walijeruhiwa kutokana na mlipuko huo.
Waasi hao walivamia hoteli Jumamosi, baada ya gari lilokuwa na bomu kulipuka wakati likiwa katika lango la kuingia katika hoteli hiyo.
Polisi wanasema wamefanikiwa kuwakamata washambuliaji wawili na wamewaua wengine wawili.
Kikundi cha waasi wa al-Shabab kimedai kuhusika na shambulizi hilo katika hoteli hiyo.
Kadhalika kulikuwa na mlipuko wa pili Jumamosi karibu na jengo la zamani la bunge. Hata hivyo kiasi cha uharibifu uliotokea katika mlipuko huo hakikuweza kujulikana mara moja.
Milipuko hiyo miwili imetokea wiki mbili baada ya gari kubwa kulipuka na kuuwa watu wasiopungua 358 katika makutano ya barabara mjini Mogadishu kwenye harakati nyingi.
Serikali ya Somalia imekilaumu kikundi cha waasi wa al-Shabab kwa shambulizi lililotokea Octoba, ingawaje kikundi hicho hakijadai kuhusika na shambulizi hilo.

Wakenya milioni 7.5 walipiga kura Alhamisi - IEBC

Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati
Tume ya uchaguzi na mipaka ya Kenya, IEBC, ilitangaza Jumapili jioni kwamba Wakenya 7.4 walipiga kura kwenye uchaguzi wa marudio uliofanyika siku ya Alhamisi.
Mwenyekiti wa tume hiyo, Wafula Chebukati, alisema kuwa kufikia saa moja jioni siku ya Jumapili, tume hiyo ilikuwa imepokea fomu 259 kati ya fomu 290 za 34B, ambazo zinahitajika kusafirishwa hadi kwenye kituo cha kitaifa cha kujumlisha kura ya urais, kwenye ukumbi wa Bomas of Kenya, mjini Nairobi.
Aidha Chebukati alisema kuwa licha ya kunukuliwa kabla ya uchaguzi kuanza akisema kuwa hakuwa na uhakika kama zoezi hilo lingekuwa la haki na kweli, sasa ana uhakika kuwa uchaguzi uliofanyika Alhamisi ulikuwa wa haki na ukweli.
Chebukati alisema maafisa wa tume hiyo walikuwa wanaendelea kuhakiki na kuthibitisha uhalisi wa fomu hizo kabla ya kutangaza matokeo ya urais.
Rais Kenyatta alikuwa anaongoza kwa Zaidi ya kura milioni 7.2. Uchaguzi huo wa urais, ambao umezua utata, ulifanyika siku ya Alhamisi licha ya mgombea wa upinzani, Raila Odinga, kujitoa kwenye kinyang’anyiro hicho, kwa madai kwamba haungekuwa wa haki na wa kweli.
Tume ya IEBC inahitajika kikatiba kutangaza mshindi wa uchaguzi huo katika kipindi cha siku 7 tangu zoezi hilo lilipofanyika.
Wakati huo huo kiongozi wa upinzani Raila Odinga, siku ya Jumapili aliwashutumu wale wanaosema kuwa ni mzee mno kuendelea na siasa, na kusema kwamba hana nia ya kustaafu kutoka kwa siasa katika siku za karibuni.
"Mimi nitastaafu wakati niatataka na sihitaji kuambiwa na mtu nistaafu," alisema Odinga.
Odinga, mwenye umri wa miaka 72, ameahidi kutoa mwelekeo mpya kwa wafuasi wake siku kesho Jumatatu.

Mawakili wa Afrika Kusini wadai kutotendewa haki Tanzania

Sibongile Ndashe
Mawakili watatu wa Afrika Kusini waliokuwa wamekamatwa nchini Tanzania wakituhumiwa kwa kukuza mapenzi ya jinsia moja wamesema hawakuwa na hatia.
Mawakili hao wa utetezi wa haki za binadamu (LHR) wenye makao yao makuu Afrika Kusini walikamatwa wakiwa pamoja na watu wengine katika hoteli moja mjini Dar es Salaam. Serikali ya Tanzania imewaondoa mawakili hao nchini.
Sibongile Ndashe, mmoja wa mawakili hao ameviambia vyombo vya habari Jumamosi kuwa polisi nchini Tanzania walikuwa hawana haki ya kuwakamata na ameishtumu mamlaka ya Dar es Salaam kwa kutowatendea haki.
Sanja Bornman wa LHR- Progamu ya Usawa wa Kijinsia amesema, “ Hakuna msingi wa sheria yoyote uliotumika katika kuwakamata watu hawa, na pia kuwapa dhamana na baadae kuifuta.
Ameongeza, "Hili linaonyesha ni jaribio la kuwadhibiti na kuwatishia watu na mawakili wanaotetea haki za binadamu, ambao kisheria walikuwa wanapata maelekezo kutoka kwa wateja wao kwa ajili ya kuchukua hatua za kisheria."
"Jambo hili halikubaliki na ni kinyume na majukumu ya kulinda haki za kibinadamu katika nchi ya Tanzania na kimataifa. Hivyo tunataka vyombo vya serikali kuwaachia huru wale wote waliokamatwa wakiwemo wanaharakati wenzetu wa Afrika Kusini," amesisitiza Bornman.
Kwa mujibu wa vyanzo vya habari nchini Tanzania waandalizi wa mkutano huo wamesema kuwa mkutano ulikuwa kwa ajili ya kujadili maamuzi ya serikali ya Tanzania unaohusu kuzuia utoaji wa baadhi ya huduma za afya.
Serikali mwaka huu ilisimamisha huduma za kliniki kibinafsi zinazotoa huduma za ugonjwa wa HIV na ukimwi ikidai zinajihusisha na kukuza mapenzi ya jinsia moja ambayo ni ukiukaji wa sheria za Tanzania.
Mawakili wa utetezi wa haki za binadamu (LHR) wenye makao yao makuu Afrika Kusini, walishtushwa na kitendo cha kukamatwa kwa wanaharakati wa haki za binadamu 13 wakiwemo raia wawili wa Afrika Kusini, nchini Tanzania kwa tuhuma za kufagilia mapenzi ya jinsia moja.
Kwa mujibu wa Shirika la Haki za Binadamu Amesty International, ushoga ni kinyume cha sheria katika nchi 38 kati ya nchi za Kiafrika 54 na adhabu yake ni kifo huko Mauritania, Somalia na Sudan.
Uganda in 2014 tried to impose the death penalty on those found guilty of being homosexual, however the controversial law was later repealed.
Uganda mwaka 2014 ilijaribu kuweka adhabu ya kifo kwa wale watakao kutinakana na kosa la kujihusisha na ushoga , lakini sheria hiyo tata iliondolewa kabisa siku za usoni.

PITIA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO OKTOBA 30,2017