Sunday, November 20

Urefu wazuia matibabu yake MOI

KIJANA Baraka Elias (35), mwenye urefu wa futi 7.4 ambaye ameshindwa kufanyiwa matibabu ya kubadilishwa nyonga katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu (MOI), amevunja ukimya na kueleza changamoto zilizosababisha ashindwe kupatiwa matibabu kutokana na urefu wake usiokuwa wa kawaida.
Akizungumza na MTANZANIA nyumbani kwa wazazi wake Mtaa wa Bwela, Pugu Majohe, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam jana, Elias alisema madaktari wameshindwa kumtibu kwa sababu mashine za MOI hazilingani na urefu wake.
Alisema anatarajia kupewa rufaa ili akatibiwe nje ya nchi.
“Madaktari wamenieleza bado wanafanya mazungumzo na wenzao wanaoshirikiana nao kutoka nje ya nchi ili wajue ni nchi gani itakuwa tayari kunichukua kufanikisha matibabu yangu.
“Sielewi matibabu yatagharimu kiasi gani cha fedha, nitatumia muda gani na vifaa gani hadi kukamilika,” alisema.
Elias alisema alifikishwa katika taasisi hiyo, Aprili mwaka huu baada ya kupewa rufaa kutoka Hospitali ya Peramiho mkoani Ruvuma.
Akizungumzia chanzo cha tatizo lake, Elias alisema alipata hitilafu ya nyonga baada ya kuanguka kwenye ngazi za nyumbani kwake mkoani Ruvuma na tangu wakati huo hakuweza kuendelea kufanya shughuli zake za kiuchumi.
Alisema baada ya muda kidogo alipelekwa Hospitali ya Peramiho ambako alifanyiwa kipimo cha X-ray na kuonekana nyonga yake ilikuwa imevunjika.

ALIVYOPOKEA RIPOTI YA MOI
Elias ambaye muda wote anaonekana kuwa mchangamfu, alisema taarifa aliyopatiwa na madaktari wa MOI kwamba anapaswa kupewa rufaa kwenda kutibiwa nje ya nchi aliipokea kwa mtazamo chanya.
“Niliona ni hali ya kawaida kwa sababu kupewa rufaa ni mfumo wa kawaida wa kimatibabu, madaktari wana utendaji wao… wanapoona wameshindwa wanakupeleka kwingine ambako unaweza kupata msaada zaidi na ndiyo maana nilitolewa Peramiho kuja MOI.

HAWEZI KUPANDA DALADALA
Alisema kwa sasa hawezi kupanda daladala kutokana na urefu wake kwani kukaa kwenye kiti huwa ni changamoto kubwa kwake kwa sababu siti zake zimetengenezwa kwa kujibana.
“Zamani nilipokuwa mzima nilikuwa napanda daladala, nilikuwa napata shida kukaa, jinsi zilivyotengenezwa hazina nafasi ya kutosha tofauti na gari za wenzetu (wazungu) zimetengenezwa kwa kuachanishwa nafasi mtu yeyote anaweza kukaa bila usumbufu,” alisema.

UREFU KWENYE DNA
Elias alisema wazazi wake wamemweleza kuwa urefu alionao ni wa kurithi kutoka kwenye kizazi chao, kwani hata mababu zake wapo ambao walikuwa warefu.
“Wazee hao wanatoka katika pande zote mbili, yaani kwa baba na kwa mama, sijui watu wananichukuliaje jinsi nilivyo, binafsi najiona kawaida na wengine kwa sababu hata hapa nyumbani hakuna aliye mrefu zaidi yangu,” alisema.

CHANGAMOTO
Alisema changamoto kubwa anayokabiliana nayo hivi sasa ni usafiri wa kumtoa nyumbani hadi Muhimbili kupata matibabu.
“Huwa tunalazimika ama kukodi gari kutoka nyumbani hadi hospitalini au tunaazima la mtu tunaweka mafuta,” alisema.

KUPANDA NDEGE
Elias alisema iwapo rufaa itapatikana hahofii kama atashindwa kuingia ndani ya ndege kwa safari ya matibabu nje ya nchi.
“Kama nilivyoeleza awali, wazungu huwa wanafikiri mbali, wanafanya vitu vikubwa. Huko kwenye nchi zao wapo warefu zaidi yangu na wanapanda ndege kama watu wengine.
“Hata gari zao wanazotengeneza siku hizi ni za tofauti, hivi karibuni tu Japan ilitoa hizi gari ndogo ambazo zina uwezo wa kusogeza kiti nyuma na ukakaa vizuri, najua nitaweza kuingia ndani ya ndege,” alisema.

AOMBA MSAADA
Elias alisema ingawa kanisa analoabudu linashirikiana naye bega kwa bega, msaada mkubwa kwake umebaki kwa familia yake.
Kutokana na hali hiyo, anaomba msaada kutoka kwa mtu, mashirika au taasisi yoyote itakayoguswa na mkasa wake.
“Siwezi kufanya kazi, kila siku nahitaji fedha za matumizi, nahitaji msaada, naamini wapo watakaoguswa, nipo tayari kwa msaada wowote kwa sababu nina changamoto nyingi, naumwa sijui lini nitapata matibabu, nategemea majibu ya madaktari,” alisema.

Wasira agoma kustaafu siasa

MWANASIASA mkongwe, Steven Wasira, amesema hana mpango wa kustaafu siasa baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza kuhalalisha ushindi wa Mbunge  wa Bunda Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Ester Bulaya.
Wasira ambaye kwa sasa ana umri wa miaka 71, aliyasema hayo jana wakati alipozungumza na MTANZANIA Jumapili lililotaka kufahamu msimamo wake kuhusu hukumu hiyo iliyotolewa juzi na mustakabali wake kisiasa.
Baadhi ya wafuatiliaji wa siasa nchini, wamekuwa na mtazamo kuwa huweda hukumu hiyo ingemfanya Wasira astaafu siasa kutokana na umri wake, lakini pia kulishikilia jimbo hilo kwa awamu tofauti tangu alipojiengua Chama cha NCCR-Mageuzi na kushinda ubunge mwaka 2005 kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
“Nistaafu siasa kwa hukumu? Kukosa ubunge haihusiani kabisa na kustaafu, na kwanini hilo swali hamkuniuliza tangu mwaka jana baada ya uchaguzi?” alihoji Wasira wakati akizungumza na gazeti hili jana.
Akijibu swali la mwandishi ambaye alitaka kujua iwapo atakata rufaa, Wasira alimtaja wakili wake Constantino Mtalemwa kuwa ndiye anayepaswa kulizungumzia hilo.
Kuhusu kutokuwapo wakati wa hukumu hiyo juzi, Wasira alisema yeye alikwenda mahakamani hapo kama shahidi na kwamba wapigakura wake ndio walifungua kesi hiyo.
Hata hivyo, katika hatua nyingine, Wasira alishindwa kumzungumzia mshindi wa hukumu hiyo, Bulaya na kuishia kusema kuwa ni mwanasiasa aliyekuwapo tangu Bunge lililopita.
Wasira alihamia upinzani kupitia chama cha NCCR-Mageuzi baada ya kutoridhishwa na ushindi wa Jaji Joseph Warioba (Waziri Mkuu na Makamu wa Rais mstaafu) katika jimbo la Bunda na baadaye mwaka 1999 alirudi tena CCM.
Mwanasiasa huyo mwaka jana alikuwa miongoni mwa makada 42 wa CCM waliojitokeza kuomba ridhaa ya kuteuliwa kupeperusha bendera ya urais, lakini hata hivyo aliikosa.
Wafuatiliaji wa siasa hapa nchini wanamtambua Wasira kama mwanasiasa mkongwe aliyeanza kuwa mbunge tangu akiwa na miaka 25 baada ya kushinda kiti hicho katika Jimbo la Mwibara mwaka 1970.
Katika nafasi za utumishi wa umma, Wasira alianza kuwa Naibu Waziri wa Kilimo chini ya utawala wa Rais wa Kwanza wa Tanzania, Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere.
Tangu enzi hizo za Mwalimu Nyerere, Wasira aliendelea kushika nafasi mbalimbali za uongozi serikalini, huku akiwa mbunge katika tawala zilizofuata hadi utawala huu wa Rais Dk. John Magufuli alipoanguka ubunge.
Itakumbukwa katika kesi iliyotolewa hukumu juzi, kwa mara ya kwanza ilifunguliwa na wapigakura wanne wa Wasira baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka jana wakipinga matokeo yaliyompa ushindi Bulaya.
Wapigakura hao ni Magambo Masatu, Matwiga Matwiga, Janes Ezekiel na Asetic Malagila.
Maombi hayo ya kutaka kesi isikilizwe, yaliwasilishwa kwa mara ya kwanza kwa Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga, Mohamed Gwae, ambaye Januari 25, mwaka huu aliitupilia mbali kwa hoja kuwa wapigakura hawana haki ya kupinga matokeo hayo.
Baada ya kukataliwa maombi hayo, walikata rufaa kwenda kwa Jaji Sirilius Matupa wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, Kitengo cha Biashara, ambaye hata hivyo aliwarudisha walalamikaji hao kurekebisha baadhi ya vifungu, kisha ilipelekwa kwa Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, Rosemary Ebrahim ambaye aliisikiliza na kuiondoa tena baada ya kubaini kasoro katika kiapo kuwa wakili aliyesaini siye aliyekuwa ameapa.
Makosa hayo yaliondolewa na baadaye kesi hiyo kupelekwa kusikilizwa na Jaji wa Mahakama Kuu Kanda hiyo, Jackilene Dimelo, ambaye aliiruhusu iende kwa jopo la majaji watatu ambao waliipiga tarehe ili iweze kusikilizwa na majaji watano ambao waliamuru irejeshwe kwa Jaji Lameck Mlacha.
Novemba 18, mwaka huu, Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza ilikohamishiwa kesi hiyo namba moja ya mwaka huu, katika Mahakama ya Mkoa wa Mara mjini Musoma, chini ya Jaji Noel Chocha, iliitupilia mbali na kumthibitisha Bulaya kuwa ni mbunge halali wa jimbo hilo.
Wakati huo huo, walalamikaji wa shauri hilo wamesema hawajaridhika na uamuzi huo, hivyo wanajiandaa kukata rufaa katika Mahakama ya Rufaa.
Akizungumza jana na gazeti hili kwa ujumbe mfupi wa simu, mmoja wa walalamikaji, Asetic Malagila, alisema baada ya kusikiliza hukumu hiyo walikubaliana na mwanasheria wao kuwa wakate rufaa kwa kile alichokiita walishindwa kwa sababu ya uonevu.
“Tumeshindwa kwa uonevu tutatafuta haki yetu katika mahakama ya rufaa, tuko katika hatua ya kukata rufaa Court of Appeal,” unasomeka ujumbe huo wa Malagila.

Mabilioni ya fedha Kagera yaiibua Serikali


*Ni baada ya watu kuhoji ujenzi wa miundombinu
* Ofisi ya Waziri Mkuu yasisitiza msimamo uko palepale
Na VERONICA ROMWALD – DAR ES SALAAM
SIKU chache baada ya kuenea taarifa za kuyeyuka mabilioni ya fedha yaliyochangwa na wasamaria wema kwa ajili ya kusaidia waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera, Serikali imeibuka na kutoa taarifa juu ya sakata hilo.
Wiki iliyopita, Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Jenerali Salum Kijuu, aliwaambia waandishi wa habari kuwa hadi sasa Serikali imetumia Sh bilioni 1.13 kukarabati miundombinu na si kuwajengea au kukarabati nyumba wananchi ambao wanaishi kwenye mahema.
Aidha, Meja Jenerali Kijuu aliendelea kushikilia msimamo wa Serikali kuwa kila mwananchi aliyeathirika na tukio hilo, ajihudumie na kukarabati nyumba yake mwenyewe.
mkuu-wa-mkoa-mhe-kijuu-akiongoza-zoezi-la-kugawa-mahitaji-kwa-wahanga-laeo-jioniAlisema Serikali tayari imekusanya Sh bilioni 5.428 kutoka kwa watu, taasisi na mashirika mbalimbali, waliotikia wito wa kusaidia waathiria wa tetemeko hilo lililotokea Septemba 10, mwaka huu.
Kijuu alisema fedha hizo zilivunwa kupitia akaunti maalumu ya maafa iitwayo ‘Kamati Maafa Kagera’ na michango mingine kupitia mihamala ya fedha ya simu za mkononi.
Baada ya taarifa ya Kijuu kutoka, iliibua maswali na mjadala mkali, hasa katika mitandao ya kijamii, ambako wachangiaji wengi walihoji kwanini fedha hizo hazijawafikia walengwa hadi sasa, huku wakibaki kutaabika.
Kutokana na mjadala huo kushika kasi kila kukicha, jana Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera,Uratibu na  Bunge), Uledi Mussa, alilazimika kutoa ufafanuzi wa Serikali namna ambavyo imeshirikina na wadau kuchukua hatua kubwa za kuwasaidia waathirika na kwamba bado inaendelea kufanya hivyo.
Alisema hadi kufikia Novemba 13, mwaka huu, Serikali ilikuwa imepokea misaada ya vifaa, vyakula, fedha na ahadi mbalimbali zenye thamani ya Sh bilioni 15.19.
Mussa alisema pamoja na misaada hiyo, tayari Serikali imetoa matibabu bure kwa majeruhi wote 560, imeandaa na kugharamia mazishi ya watu 17 waliofariki dunia katika tetemeko hilo, huku Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alihudhuria.
“Serikali kwa kushirikiana na wadau ilitoa mkono wa pole wa Sh milioni 1.8 kwa kila familia iliyopatwa na msiba. Imeendelea kutoa misaada mbalimbali ya kibinadamu ikiwamo chakula, dawa, nguo, makazi ya muda, huduma za tiba, vifaa vya shule na huduma ya ushauri wa kisaikolojia kwa waathirika katika wilaya zote za Mkoa wa Kagera zilizopata athari,” alisema.
Alisema Serikali imeendelea kufanya tathmini ya pamoja ya mahitaji ya haraka ya athari za tetemeko hilo ili kubaini maeneo zaidi ya kuwasaidia wananchi kwa kushirikiana na ofisi ya Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa na wadau mbalimbali, wakiwamo Msalaba Mwekundu, Plan International (T), BRAC(T), World Vision, CARITAS, Save the Children, JH Piego na Benki ya Dunia.
“Tathmini za wataalamu, makadirio ya awali yanaainisha Sh bilioni 104 zinahitajika kukabiliana na kurejesha hali katika Mkoa wa Kagera. Gharama hizo zinajumuisha ujenzi wa makazi ya muda kwa waathirika wa nyumba zipatazo 16,667 zilizoharibika katika viwango tofauti, ambapo kiasi cha Sh bilioni 41.7 zinahitajika.
“Sh bilioni 1.92 kwa ajili ya kodi ya miezi sita kwa wapangaji waliokuwa wakiishi kwenye nyumba zilizoharibika, ukarabati wa shule za msingi 163 kwa gharama ya sh bilioni 12.7, sekondari 57 kwa gharama ya Sh bilioni 45.65, vituo vya afya na zahanati 32 kwa gharama ya Sh milioni 772 na majengo ya taasisi nyingine 20 kwa Sh bilioni 1.3,” alisema.
Alisema hadi kufikia Novemba 13, mwaka huu, Serikali imepokea misaada ya vifaa, vyakula, fedha na ahadi mbalimbali zenye thamani ya Sh bilioni 15.19 kutoka kwa wadau mbalimbali, washirika wa maendeleo, balozi na nchi marafiki. Tayari misaada hiyo imeshagawiwa na inaendelea kusambazwa kwa walengwa.
“Mchanganuo wa misaada hiyo iliyopelekwa ipo kama ifuatavyo: Fedha taslimu kiasi cha Sh 5,412,984,934.82 kimeshapokelewa kupitia benki. Kiasi cha Sh 17,579,427.00 kupitia mitandao ya simu, ahadi za Sh 6,703,000,000. Hivyo jumla ya ahadi na fedha taslimu hadi sasa ni Sh 12,133,564,361.82,” alisema.
Alisema Serikali pia imepokea misaada mingine yenye thamani ya Sh bilioni 2.25, ikiwamo unga tani 58.12, sukari mifuko 1,150, mchele tani 133.96, maharage tani 19,666, mahindi tani 70.1, majani ya chai tani 3, maji katoni 1,570, mafuta lita 6,022, sabuni katoni 443, shuka 495, blanketi 6,125, magodoro 1,146, mahema 367 na turubai 6,237.
Aliongeza: “Serikali imepokea pia vifaa vya ujenzi vikiwamo saruji mifuko 24,233, bati 20,933, misumari kilo 145, nondo vipande 725, kofia za bati 150 na mbao 250.
“Ifahamike baadhi ya waliotoa ahadi kama Serikali ya Uingereza, wameahidi kutekeleza ahadi zao kwa kujikita moja kwa moja katika ujenzi wa shule, baada ya Wakala wa Majengo kuainisha viwango na gharama. Aidha Serikali inaendelea kupokea michango kutoka kwa wananchi na wadau mbalimbali kwa lengo la kusaidia waathirika hawa.”

HATUA ZA KUREJESHA HALI
Mussa alisema tangu kutokea kwa maafa hayo, Serikali imeendelea kufanyia kazi masuala muhimu yaliyoainishwa katika tathmini ya tetemeko.
Alisema hadi kufikia Novemba 13, mwaka huu, licha ya kuendelea kuwapatia wananchi mahitaji muhimu kama chakula, dawa na misaada ya kujikimu katika makazi ya muda, kiasi cha Sh 969,238,326.35, mifuko ya saruji 17,423, bati 5,348 na misumari kilo 1,107 vilitumika kwa kufanya ukarabati mkubwa na mdogo wa shule za msingi na sekondari.
“Juhudi hizi ziliwezesha wanafunzi wa shule hizo waliokuwa katika hatari ya kukosa masomo kuendelea na masomo yao. Gharama hizo pia zimejumuisha ukarabati wa zahanati katika halmashauri za Mkoa wa Kagera, na kuanza kwa ujenzi wa kituo kipya cha afya (Ishozi/Kabyaile) kitakachojumuisha chumba cha upasuaji na wodi ya kinamama na watoto kwa faida ya wananchi wote wa maeneo hayo.
“Pia Serikali imegharamia urejeshwaji wa miundombinu ya barabara, maji, na umeme katika maeneo kadhaa yaliyoathiriwa na tetemeko,” alisema.
Alisema Shirika la Word Vision kwa kushirikiana na Serikali tayari limetoa mifuko ya saruji 2,300 yenye thamani ya Sh 39,000,000 kwa kaya 460 zilizobomokewa nyumba na zilizoonekana kuwa na uhitaji zaidi. Katika awamu ya kwanza kila kaya ilipata mifuko mitano ya saruji.
“Na kwa sasa utekelezaji wa awamu ya pili umeanza, inatarajiwa kugawiwa mifuko ya saruji 10,645 yenye thamani ya Sh milioni 164.9 kwa kaya 2,129. Tumeainisha pia kaya nyingine zilizoathirika zaidi zipatazo 370 za watu waliomo kwenye makundi maalumu (wazee, wajane na walemavu), ambao watapatiwa vifaa vya ujenzi (mabati 20 na mifuko mitano ya saruji kwa kila kaya) kukarabati nyumba zao,” alisema.
Aliongeza: “Serikali inapenda kusisitiza tena kwa wananchi, maafa ya tetemeko hayakupangwa wala kutokea kwa nguvu za mwanadamu bali majanga ya asili, hivyo wakati juhudi zikiendelea kusaidia zaidi pale panapowezekana, wananchi wanaendelea kuombwa kufanya jitihada zao binafsi za kurejesha makazi yao katika hali yake ya awali.
“Serikali inawapongeza wananchi wengi ambao tayari wameitikia wito wa Rais Dk. John Magufuli aliyewaasa kuanza ujenzi wa nyumba zao kwa kuwa Serikali isingeweza kumjengea nyumba kila mwathirika.
“Kwa sababu ingawa michango na misaada hii japo haijafikia lengo la Sh bilioni 104.9 zinazohitajika kurejesha hali nzima ya Kagera, itaendelea kutumika kwa uadilifu na uwazi kwa faida ya waathiria wenyewe,” alisema.
Tetemeko la ardhi lilitokea Septemba 10, mwaka huu na kusababisha vifo vya watu 17, watu 252 walijeruhiwa, nyumba 840 zilianguka na nyingine 1,264 zilipata nyufa.

JK azuiwa uwanja wa ndege

RAIS mstaafu, Jakaya Kikwete, jana amezuiwa na maofisa wa Serikali kusafiri nje ya nchi kutokana na miongoni mwa wajumbe wanne aliokuwa ameongozana nao kutokuwa na viza.
Taarifa zilizofika chumba cha habari jana jioni, zilidai kuwa Kikwete ambaye pia alikuwa ameongozana na mke wake, Salma alizuiwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, tukio hilo lilitokea saa 10:00 jioni na hivyo Kikwete pamoja na ujumbe wake huo kukwama kusafiri.
Chanzo kimoja kilichopo uwanjani hapo, kililidokeza gazeti hili kuwa Kikwete pamoja na ujumbe wake huo, walikuwa wakielekea nchini Dubai na ilikuwa wasafiri kwa ndege ya Shirika la Ndege la Emirates.
“Kikwete kama Kikwete yeye hakuwa na shida kwa sababu ana Diplomatic Passport, watu wengine ndio hawakuwa na viza.
“Kwa kawaida International flight (ndege za kimataifa) kaunta zinafungwa saa moja kabla ya ndege kuruka, na ndege waliyokuwa waondoke nayo ilikuwa inaondoka saa 10:30 jioni, viza za hao watu zilikuja saa 10:00 wakati kaunta zikiwa zimefungwa,” kilisema chanzo hicho.
Kilisema kwa kiongozi kama Kikwete, linapotokea tatizo kama hilo, wakati mwingine unaweza kupiga simu kwa watu wa Uhamiaji huko anakoelekea, lakini hilo halikuwezekana kwa sababu tayari ndege ilikuwa imeondoka.
Haijajulikana mara moja kilichosababisha kutotumiwa utaratibu wa kupiga simu kama inavyoelezwa, ikitokea kiongozi mkubwa kama Kikwete au wasaidizi wamekwama kukamilisha taratibu fulani fulani za kusafiri nje ya nchi.
Kwa mujibu wa chanzo hicho, huenda Kikwete na ujumbe wake wakasafiri leo baada ya kuwa wamekamilisha taratibu zote.
Taarifa kutoka kwa wasaidizi wa Kikwete, zilidai kuwa wakati tukio hilo linatokea uwanjani hapo, rais huyo mstaafu hakuwa amefika bali wasaidizi wake ingawa tayari mizigo ilikuwa imekwishapandishwa ndani ya ndege.
Inaelezwa kuwa baada ya safari hiyo kukwama mizigo hiyo ilishushwa.
Taarifa nyingine zilidai kuwa wakati tukio hilo likitokea, Kikwete alikuwa uwanjani hapo na kwamba  kwa kawaida mizigo isingepandishwa kama muhusika hayupo.
Akizungumza na gazeti hili, mmoja wa wasaidizi wa Kikwete, alisema wajumbe ambao hati zao ama zilikuwa na kasoro au hazijakamilika ni wasaidizi wake.
Alisema Kikwete, mke wake pamoja na wasaidizi wake, walikuwa wanaelekea Abudhabi na walikuwa wapande ndege hiyo ya Emirates Dubai na kisha kuendelea na usafiri mwingine.
Msaidizi wake huyo alisema taratibu zote zilikamilika ingawa walikiri kuwa walikuwa wamechelewa.
MTANZANIA Jumapili lilimtafuta ndugu wa karibu na Kikwete ambaye alithibitisha kuwa alikuwa anasafiri, lakini hakuwa na habari za kukwama kwake.
Zipo taarifa ambazo hazijathibitishwa zinazodai kuwa imekuwa ni kawaida kwa wasaidizi wa Kikwete kusafiri nje ya nchi bila viza, na kwamba tukio la safari ya jana kukwama lisingetokea kama utaratibu huo haungekuwapo.
MTANZANIA Jumapili lilipomtafuta Msemaji wa JNIA, Nuru Nyoni azungumzie sababu za Kikwete na ujumbe wake kukwama, alisema suala hilo lipo chini ya Uhamiaji.
“Siwezi kuzungumzia mimi, hili suala lipo chini ya Uhamiaji, labda uwapigie Uhamiaji, pia hata uthibitisho siwezi kutoa maana leo ni weekend sijafika ofisini,” alisema Nuru.
Alipotafutwa Ofisa Uhusiano wa Idara ya Uhamiaji, Abasi Ilovia, kupitia simu yake ya kiganjani, aliomba apigiwe baada ya dakika kumi ili aweze kuwasiliana na watu waliopo JNIA kwa taarifa zaidi.
Ilovia alipopigiwa tena baada ya muda huo, alisema anasubiri majibu kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Uhamiaji cha Uwanja wa Ndege.

Saturday, November 12

top footballers in the world by goal.com


GOAL 50 - POSITIONS 10-1

The Goal 50 counts down the world’s 50 best football players of 2016, featuring the likes of Cristiano Ronaldo, Lionel Messi and Zlatan Ibrahimovic. Below you can find the stars who were selected from positions 10 to 1.

Chief editors and correspondents from Goal‘s 38 editions across the globe all cast their votes. Players were judged on their level of consistency over the past year, their big-game performances, footballing legacy and the success of their team at both club and international level.

#10 ZLATAN IBRAHIMOVIC | MANCHESTER UNITED & SWEDEN

The Swede has a wonderful sense of humour and a tremendous flair for hyperbole but it is hard to dispute his claim that he is ageing like a fine wine. Last season was the most prolific of his career, with Ibra racking up 50 goals in PSG's treble-winning campaign, while he wasted little time in winning over United fans by scoring four times in his first three games for his new club.

#09 GONZALO HIGUAIN | JUVENTUS & ARGENTINA

The striker's detractors believe that he misses big chances in big games yet this is a man who hit a hat-trick on the final day of last season to break the record for goals in a single Serie A season. Furthermore, when his critics piled on the pressure after he'd piled on the pounds following his €90m summer switch from Napoli to Juventus, he responded with seven goals in his first nine outings in all competitions for the Bianconeri.

#08 ROBERT LEWANDOWSKI | BAYERN MUNICH & POLAND

Any doubts over the striker's suitability to Pep Guardiola's tactics were blown away last season, with the 28-year-old becoming the first foreign player ever to score 30 goals in one Bundesliga campaign. Though a marked man at Euro 2016 - he suffered more fouls than any other player despite exiting at the quarter-final stage - he still managed a goal in his country's shootout loss to Portugal. 

#07 RIYAD MAHREZ | LEICESTER CITY & ALGERIA

A player signed from Le Havre for €500,000 in 2014 was described as "priceless" by Foxes boss Claudio Ranieri last December and it's easy to understand why. With 17 Premier League goals and 10 assists, Mahrez was not only a worthy recipient of the 2015-16 PFA Players' Player of the Year award in April but also a most deserving Premier League title winner just a few days later. The highest ranked midfielder in the Goal 50.


#06 NEYMAR | BARCELONA & BRAZIL

One leg of arguably the greatest ever front three, Neymar netted the winner in the Blaugrana's double-clinching victory over Sevilla in the Copa del Rey final in May. After being forced to miss the Copa America by his club, the 24-year-old then led his country to victory in the one international tournament that had eluded them by claiming Olympic gold in Rio in August. What’s more, he scored the winning penalty in the final shootout success over Germany.

#05 GARETH BALE | REAL MADRID & WALES

The winger has his injury issues but when fully fit, he rarely fails to step up to the mark for both club and country. One of Madrid's best players in the Champions League final win over Atletico, the 27-year-old Cardiff native then carried Wales through the group stage of Euro 2016 with three goals in three games, laying the foundation for the Dragons' surprise run to the semi-finals.

#04 LIONEL MESSI | BARCELONA & ARGENTINA

It says something about the staggering standards of excellence that the diminutive No.10 has set for himself that a year in which he inspired his club side to a domestic double and his country to a third final in three years can be considered slightly below par. Indeed, at regular intervals over the past 12 months, Messi reminded everyone just why he is not competing for the title of the best player in the world but the greatest of all time, with his performance in Argentina's Copa America semi-final demolition of USA a particular highlight.

#03 ANTOINE GRIEZMANN | ATLETICO MADRID & FRANCE

The finals of both the Champions League and Euro 2016 ended in heartbreak for the Frenchman but even those desperately disappointing defeats couldn’t overshadow the attacker's illuminating displays for club and country this year. It was Griezmann's goals that knocked both Barcelona and Bayern Munich out of Europe, while his fantastic form for France – including a match-winning double versus Germany in the semis - saw him claim both the Golden Boot and the Golden Ball at Euro 2016.


#02 LUIS SUAREZ | BARCELONA & URUGUAY

After being forced to share the Golden Shoe with Cristiano Ronaldo last year, the former Liverpool ace made no mistake this time around, blowing the Portuguese superstar and several other illustrious rivals out of the water with 40 Liga goals in just 35 games. Suarez's brilliance was only further emphasised by the fact that he also created 16 goals - a tally only matched by Messi - to become the first player to top both the goalscoring and assists charts in Liga history.

#01 CRISTIANO RONALDO | REAL MADRID & PORTUGAL

Reports of the 31-year-old's decline proved greatly exaggerated, with the Madeira native enjoying the most successful season of his career - at least trophy-wise. Ronaldo struck a whopping 51 club goals in all competitions last term – and top-scored once again with 16 strikes as Real won the Champions League in May. Just over six weeks later, he cemented his status as an all-time great by claiming the first major title of his international career thanks to Portugal's stunning triumph at Euro 2016. Congratulations to Cristiano Ronaldo – the winner of the 2016 Goal 50!