Saturday, December 24

Serikali yapiga marufuku shule binafsi kufanya mitihani ya kuchuja wanafunzi

Serikali imepiga marufuku utaratibu wa shule binafsi kuendesha mitihani ya mchujo kwa wanafunzi wanaotarajia kufanya mitihani ya kitaifa ili shule zao ziweze kuongoza kwa kubaki ma wanafunzi wazuri(walio na uwezo mzuri darasani)

Agizo hilo pia linapiga marufuku kuwafukuza shule wanafunzi wanaoshindwa mitihani ya mchujo,kuwasajili kama private candidate wale wanafunzi wanaofeli mitihani hiyo,kuwahamisha shule au kuwakaririsha madarasa.

========

Kibano kipya chaja kwa shule binafsi
Hiyo ni baada ya kutangaza kupiga marufuku utaratibu wa kuwachuja wanafunzi wanaotakiwa kufanya mitihani ya taifa uliokuwa unaofanywa na baadhi yao kwa lengo la kuonekana shule zao zinafaulisha vizuri.

Hivi karibuni, Nipashe iliripoti kuhusu hofu ya baadhi ya shule hizo; za msingi na sekondari ziko hatarini kubadilishwa matumizi kutokana na kukosa wanafunzi wa kutosha baada ya Serikali kuboresha shule zake na kutoa elimu bure, huku hali ya kiuchumi ikiwaumiza wananchi.

Huku udahili kwenye shule za serikali ukiongezeka na kuonekana kuwa tishio kwa ustawi wa shule za watu na taasisi binafsi, imewabana tena wamiliki wa shule binafsi kwa kuwazuia kufanya mchujo wa wanafunzi wanaoingia kwenye madarasa au vidato vyenye mitihani ya taifa.

Mmoja wa wazazi aliliambia Nipashe kuwa mwanawe anayesoma kidato cha tatu katika shule moja ya binafsi jijini Dar es Salaam, amepangiwa kuhamishiwa shule nyingine ya mmiliki huyo huyo kutokana na kufaulu kwa daraja la tatu.

Kwa mujibu wa mzazi huyo, kuna wanafunzi takribani 70 wa kidato cha tatu, wanatarajiwa kuhamishwa katika shule hiyo waliyosajiliwa tangu kidato cha kwanza, watahamishwa shule hiyo na kubaki wale waliofaulu kwa viwango vya madaraja ya kwanza na pili tu.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dk. Leonard Akwilapo, akizungumza na Nipashe jijini Dar es Salaam juzi, alisema ni marufuku shule kumkaririsha darasa, kumfukuza, kumhamishia shule nyingine au kumsajili kama mtahiniwa binafsi (PC) mwanafunzi kwa kigezo cha kutofanya vizuri katika mitihani ya shule husika.

"Ni marufuku kabisa kufanya hivyo. Mitihani tulionayo sisi (Wizara ya Elimu) ndiyo mchujo sahihi. Na mtihani ambao unamkaririsha mwanafunzi ni mtihani wa taifa wa kidato cha pili na mtihani wa darasa la nne tu," alisema.

"Wala siyo mtihani wa shule na madarasa mengine hayana mtihani wa kumkaririsha mtoto au kumfanya aondolewe shuleni au ahamishiwe shule nyingine, hatuna utaratibu huo na serikali haiwezi kukubaliana nao," aliongeza Dk. Akwilapo.

Katibu Mkuu wa Chama cha Wamiliki wa Shule na Vyuo Binafsi (Tamongosco), Benjamin Nkonye, aliiambia Nipashe jana kuwa utaratibu wanaoutumia ni kushauriana na wazazi wa wanafunzi wanaoshindwa kufanya vizuri shuleni ikiwamo kuwapeleka katika vyuo vya ufundi (Veta).

Alisema shule binafsi zinapaswa kupongezwa kwa kudahili hata wanafunzi hasa wa sekondari ambao shule za serikali huwa haziwachukui kutokana na kushindwa kufanya vizuri katika mitihani ya shule za msingi.

“Hakuna shule ambazo zinapaswa kupongezwa kama za binafsi, serikali yenyewe imekuwa ikichagua wanafunzi wote. Inatuachia ‘vilaza’, lakini sisi kwa kujitoa kuwasaidia watoto wa Kitanzania, tunakubali kuwachukua hao hao wanaoonekana wabaya, tunawafundisha na mwisho wa siku wanakuwa wazuri kuliko hata hao wanaokuwa wamethaminiwa na serikali,” alisema Nkonya.

“Na sisi hatuchuji wala kumfukuza mwanafunzi, isipokuwa kinachofanyika kwa kuwa tunapokea wakati mwingine wanafunzi ambao ni ‘vilaza’ kabisa, huwa tunawagawanya katika makundi kulingana na uelewa wao, wenye uelewa wa kwanza, wa kati na wa mwisho. Na mwisho na tunawafundisha kulingana na ‘speed’ (kasi) ya uelewa wao na wanajikuta wanafanya vizuri.

“Lakini kwa sababu sisi tunakuwa na wanafunzi ambao ni wagumu sana, inapoonekana wakatokea wachache hawawezi kabisa huwa tunashauriana na wazazi wao, kuwapeleka Veta ili kule wanapokuwa wanaendelea kujifunza, wengine wanafanya vizuri hadi wanafika vyuo vikuu, hatuwaachi kama ilivyo katika shule za serikali na vyuo vya serikali, haya maneno mengine yanayozungumzwa ni ya kisiasa tu."

HALI ILIVYO

Uchunguzi wa Nipashe uliofanyika hivi karibuni katika baadhi ya mikoa, ulibaini baadhi ya wamiliki wa shule binafsi wamekuwa na utaratibu wa kuchuja wanafunzi kila mwaka kwa lengo la kupata wenye uwezo mkubwa darasani.

Ilibainika kuwa utaratibu huo umekuwa ukifanywa kwa nia ya kuwa na wanafunzi wenye uwezo mkubwa ili shule hizo zifanye vizuri katika mitihani ya taifa, hivyo kuvutia wazazi wengi zaidi kupeleka watoto wao.

Gazeti hili lilibaini kuwa, baadhi ya shule binafsi zimekuwa zikiendesha utaratibu huo kipindi cha mitihani ya mwishoni mwa mwaka kwa kuwafukuza, kuwakaririsha darasa au kuwahamishia shule nyingine wanafunzi wanaoshindwa kufikia kiwango kinachowekwa na shule husika kwenye mitihani ya kufunga mwaka.

Nipashe pia ilibaini baadhi ya shule hizo zimekuwa na utaratibu wa kuwachuja kwa kuwasajili kama watahiniwa binafsi (Private Candidates) kwenye mitihani ya taifa wanafunzi wake wanaoshindwa kiwango kilichowekwa wanapofanya mitihani ya shule husika.

MTOTO WA PROFESA AKACHA KULA

Akizungumzia suala hilo katika mahojiano maalumu na gazeti hili jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Masomo ya Shahada ya Kwanza Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Prof. Allen Mushi, alisema haungi mkono utaratibu wa baadhi ya shule binafsi kuwafukuza wanafunzi wanaoshindwa kufikia kiwango cha alama zilizojiwekea.

Alisema: "Ni makosa kumfukuza shule mwanafunzi aliyekuwa amedahiliwa, anasoma halafu unamsitishia, unamwambia nenda katafute shule nyingine.

"Na ni kweli wana tabia hiyo. “Nina kijana wangu yuko ‘Form One’ (Kidato cha Kwanza) anasoma shule ... (anataja eneo ilipo shule hiyo), yaani anasoma kupindukia. Nilikuwa na wasiwasi hata akija likizo hawezi kula vizuri, anasoma tu."

Alisema kuwa katika shule hiyo ya jijini Dar es Salaam anayosoma mtoto wake, wameambiwa ni lazima awe na wastani wa kuanzia alama 50 katika mitihani ya shule ili aruhusiwe kuingia kidato kinachofuata, vinginevyo wakatafute shule nyingine.

"Katika utaratibu wa elimu, siyo sahihi kufanya hivyo, wewe kama wanafunzi wameshindwa, wewe siyo ndiyo mwalimu, ndiyo kazi yako ya kufanya wanafunzi waelewe," alisema na kufafanua zaidi:

“Sasa ukiwa unafanya hivyo, mwisho wa siku utakuwa unafelisha darasa zima na kujitamba kwamba unafaulisha kwa sababu umefukuza wengi na kubaki na wazuri wachache. Sasa hiyo ni biashara, siyo elimu tena. Wewe kama ni mwalimu, unatakiwa kufundisha wanafunzi wote.

“Kwa hiyo, wanasema shule za ‘private’ (binafsi) zinafaulisha wanafunzi wote, kumbe wengine mliowachuja. Mimi binafsi sikubaliani na hali hiyo kabisa."

Alisema ni muhimu wizara yenye dhamana ya elimu nchini iweke masharti kwamba ukishadahili wanafunzi, wasiondolewe shuleni kwa utaratibu wa viwango vya ufaulu katika mitihani ya shule husika isipokuwa kwa sababu za tabia mbaya na zisizofaa kwa mwanafunzi kwa mujibu wa sheria za nchi.

MAKUNDI YA UELEWA

Msomi huyo alisema wanafunzi wamegawanyika katika madaraja mawili kiuelewa darasani, la kwanza likiwa la wenye uelewa wa haraka (fast learners) na jingine likiwa la wenye uelewa hafifu (‘slow learners).

"Wote hao wanapaswa wazingatiwe katika elimu. Sasa hawa (shule binafsi) wenyewe wanaangalia 'fast learners' tu. Ni vema wote wakachukuliwa katika vigezo sawa, siyo unawachuja wengine halafu unasema unafaulisha wote," alisema Prof. Mushi.

BIASHARA

Aliyekuwa Rais wa Chama cha Walimu (CWT), Gratian Mukoba, akizungumza na Nipashe jana kuhusu changamoto hiyo, alisema si vyema kumfukuza, kumkaririsha darasa au kumhamisha mwanafunzi aliyefanya vibaya katika mitihani ya shule.

"Mtihani wa Kidato cha Pili ni mchujo sahihi tu. Shule binafsi wanakosea. Ufundishaji wa kawaida huwezi kuwa na wanafunzi wanaopata daraja la kwanza na la pili tu," alisema.

"Hao shule binafsi kuna muda wanateleza kidogo, kwa sababu hakuna mwanafunzi asiyefundishika labda kwa sababu wao wanataka suala la biashara. Ni kuonea wanafunzi, bahati mbaya akishaanza shule ya 'private' (binafsi) kidato cha kwanza, hawezi kurudi kwenye mfumo wa serikali, kwa hiyo wanafunzi wanahangaika," alisema zaidi Mukoba.

Tuesday, December 20

Trump aadhinishwa rasmi Rais wa Marekani


Washington, Marekani. Wajumbe wa Jopo la Kuamua Mshindi wa Urais nchini Marekani wamemuidhinisha Donald Trump kuwa mshindi wa uchaguzi wa urais uliofanyika Novemba. Wajumbe hao walikutana katika majimbo yao kupiga kura.
Awali, kulikuwa na juhudi za kutaka kumzuia bilionea huyo kuingia ikulu kwa madai amekuwa akiendesha siasa za kibaguzi.
Hata hivyo, Trump amesema atakuwa rais wa Marekani wote na atafanya kila liwezekanalo kuwaunganisha wananchi.
Wajumbe walikuwa wametumiwa ujumbe kupitia baruapepe na pia kupigiwa simu wakihimizwa kutomuunga mkono bilionea huyo kabla yao kukutana kupiga kura.
Shughuli yao ya kupiga kura kwa kawaida huwa kama shughuli ya kutimiza wajibu kwani mara zote  huwa wanamuidhinisha mshindi.
Kumekuwa na lawama kuwa uchaguzi wa mwaka huu ulitawaliwa na hila ikiwamo vitendo vya udukuzi kutoka Urusi. Madai hayo yamepuuzwa na Urusi iliyosema hayana msingi wowote.
Jimbo la Texas hatimaye lilimuwezesha kufikisha idadi ya kura 270 za wajumbe alizohitaji,, licha ya wajumbe wawili wake kugeuka na kupiga kura kumpinga.
Matokeo ya kura hiyo yatatangazwa rasmi 6 Januari 6 kwenye kikao maalum cha pamoja cha Bunge la Congress.
"Nawashukuru Wamarekani kwa kunipigia kura kwa wingi kuwa rais wa Marekani," alisema Trump kupitia taarifa baada ya matokeo kutangazwa.
"Kwa hatua hii ya kihistoria tunaweza sasa kutazama mbele na kutarajia maisha ya kufana siku za usoni. Nitafanya kazi kwa bidii kuunganisha nchi yetu na kuwa rais wa Wamarekani wote," alisema.

Baba wa msaidizi wa Mbowe kukagua maiti iliyowekwa kwenye kiroba


Moshi. Wakati polisi wakisema kuwa wanaufanyia mchakato wa vipimo vya vinasaba (DNA), mwili wa mtu anayedaiwa kuuawa nje kidogo ya mji wa Moshi na kuwekwa kwenye kiroba na kuchomwa moto, familia ya Ben Saanane, msaidizi wa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe ambaye hajulikani aliko imesema inaenda kuuangalia mwili huyo.
Hatua hiyo ya polisi kupima DNA ilielezwa na Kamanda wa Polisi Mkoa Kilimanjaro, Wilbroad Mutafungwa baada ya hadi jana, mwili huo kutotambuliwa.
Mauaji hayo yaligunduliwa Ijumaa iliyopita, baada ya watu waliokuwa na gari ndogo ambao hawajafahamika, kumchoma moto mtu huyo katika Kijiji cha Ongoma na kisha kutoweka kusikojulikana.
Kamanda Mutafungwa aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa mtu huyo hajafahamika na wala hakuna mtu aliyejitokeza kuutambua mwili huo hivyo kulilazimu jeshi kufanya uchunguzi huo wa kisayansi.

Wahifadhi wamwambia Majaliwa, hakuna kaburi la Faru John


Arusha. Sakata na kifo cha Faru John (38), limechukua sura mpya baada ya wahifadhi wa eneo la Sasakwa Singita Grumet kueleza kuwa hakuna kaburi lake kwa kuwa hakuzikwa.
Wamesema hayo siku moja baada ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kutangaza kuunda timu mpya kuchunguza mazingira ya kifo cha faru huyo huku akihoji mambo manne yaliyozua utata.
Mambo aliyohoji wakati akifanya majumuisho ya ziara yake mkoani Arusha ni juzi, Faru John aliumwa lini, aliumwa nini, daktari gani aliyemtibu na zilipo taarifa za matibabu yake.
Pia aliagiza mwili wa faru huyo kufukuliwa na kutazama kama vinasaba vyake vinaendana na watoto wake 26 ambao bado wapo katika Creta ya Ngorongoro.
Akizungumza na mwandishi wetu jana, mmoja wawahifadhi wa Sasakwa Grumet aliyeomba kutotajwa jina ili kutoathiri uchunguzi wa tukio hilo, alisema kitaalamu wanyama ambao wanakufa bila kuwa na magonjwa ya mlipuko katika maeneo ya hifadhi hawazikwi.
“Faru John baada ya kufa aliondolewa pembe zake na kutupwa ili kiwe chakula cha wanyama wengine wanaotegemea mizoga, lakini kuna mifupa yake,” alisema.
Alisema faru huyo aliombwa na Grumet kwenda kupanda faru waliopo katika eneo hilo, hasa baada ya dume aliyekuwapo huko kuuliwa na tembo.
“Baada ya kuonekana kuna haja ya kutafuta dume, ndipo tuliomba kupata faru dume na tukaletewa na baadaye alikufa,” alisema.
Eneo hilo la Sasakwa Singita Grumet ni mali ya mfanyabiashara mkubwa raia ya Marekani, bilionea Tudor Jones ambaye amewekeza katika maeneo kadhaa ya uhifadhi.
Akifafanua hatua zinazochukuliwa baada ya mnyama kufa katika hifadhi, mhifadhi Peter Isango alisema kwa kawaida huzikwa au kuchomwa moto pale tu wanapobainika kuwa na magonjwa kama kimeta.
“Kama mnyama ana magonjwa ambayo yanaweza kuambukiza, basi anachomwa moto au kufukiwa lakini kama anakufa kawaida na magonjwa ya kawaida huwa anatupwa ili fisi, bweha na wanyama wengine wanaokula mizoga wale na hii ndiyo ikolojia,” alisema.
Kauli hiyo iliungwa mkono na mkurugenzi mkazi wa shirika la uhifadhi la kimataifa la Frankfurt Zoological Society, Gerald Bigurube ambaye alisema kwa kawaida wanyama wanaokufa hifadhini huwa hawazikwi.
Bigurube ambaye aliwahi kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa) alisema kwenye kanuni za uhifadhi kitu chochote, kinachokufa ndani ya hifadhi huachwa kwa ajili ya kulinda ikolojia na bionuwai.
“Mnyama ambaye anakufa kwa kifo cha kawaida mzoga wake unapaswa kuachwa kuoza na kutumiwa na wanyama wengine,” alisema.
Alisema hata wanyama wa kawaida kama swala na wengine wanapoumwa huwa hawatibiwi tofauti na wanyama kama tembo, faru na wengine wakubwa ambao hutibiwa.
Hata hivyo, alipoulizwa kuhusu Faru John, Bigurube alisema taasisi yake haikuwahi kushiriki katika suala hilo.
Wapata dhamana
Katika hatua nyingine, Polisi imewaachia kwa dhamana maofisa watano wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) na Tanapa waliokuwa wanashikiliwa kwa tuhuma za kumhamisha Faru John kutoka Creta ya Ngorongoro na kumpeleka Sasakwa Grumet.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo alisema jana kuwa licha ya dhamana hiyo, uchunguzi unaendelea.
Watuhumiwa hao ni Israel Naman ambaye alikuwa kaimu mkuu wa idara ya hifadhi wakati faru huyo akiondolewa, Cuthbert Lemanya aliyekuwa mkuu kanda ya Creta, Dk Athanas Nyaki ambaye ni daktari wa mifugo wa mamlaka hiyo.
Wengine ni aliyekuwa kaimu mkuu idara ya maendeleo ya jamii, Kuya Sayaleli na kaimu mkuu idara ya ikolojia, Patrice Mattey.
Kabla ya kukamatwa, maofisa hawa walikiri kushiriki kumhamisha Faru John kutoka Creta ya Ngorongoro hadi Sasakwa kwa maelezo kuwa ilikuwa ni kuendeleza uhifadhi wa faru na pia kutokana na ukorofi wa Faru John kuhodhi majike yote ndani ya Creta kuua madume wengine waliozaliwa.
Akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Arusha, Waziri Mkuu alitoa taarifa za kifo cha faru John huku akiwatuhumu baadhi ya watendaji wa NCAA kuhusika na njama za kumuuza kwa Sh200 milioni ambazo alisema walishapokea malipo ya awali ya Sh100 milioni.
Baada ya maelezo hayo, Waziri Mkuu alitaka kupewa taarifa kamili za tukio hilo, pamoja na pembe za faru huyo, ambazo alikabidhiwa Desemba 8 na Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe na kaimu mkurugenzi wa msaidizi kitengo cha kupambana na ujangili, Robert Mande ambaye alimweleza kuwa taratibu zilifuatwa katika kumhamisha.

Aliyebadili dini afariki baada ya kubatizwa


Moshi. Mkazi wa Mailisita wilayani Hai, Paulo (35) amekufa maji baada ya kuzama katika mto Kikafu, dakika chache baada ya kubadili dini na kubatizwa na maji ya mto huo kwa imani ya dini ya Kikristo.
Paulo ambaye jina lake la awali lilikuwa Issa Juma kabla hajabadili dini, alifariki Jumapili iliyopita katika mto huo, wakati shamrashamra za kubatizwa kwake zikiendelea pembeni ya mto.
Hata hivyo, Jeshi la Polisi lililazimika kuwakamata wachungaji wawili wa kanisa la Efatha waliombatiza lakini waliachiliwa baada ya Polisi kujiridhisha kuwa Paulo alikufa maji baada ya kubatizwa.
Habari zilizothibitishwa na Polisi, zimeeleza baada ya kubatizwa saa 8:30 mchana na wakati waumini wakiimba kwa ajili ya kurudi kanisani, ndipo Paulo na mwenzake waliamua kurudi kuogelea.

Thursday, December 8

Kardinali Pengo akerwa na matanuzi


Pwani. Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo amewataka waumini wa madhehebu hayo kutotumia muda na mali zao kufanya sherehe kubwa, badala yake wajikite katika ujenzi wa makanisa.
Alitoa rai hiyo juzi alipokuwa mgeni rasmi kwenye harambee ya kuchangia Sh50 milioni kwa ajili ya ujenzi wa Kanisa Katoliki Tumbi, Kibaha mkoani hapa.
Kanisa hilo litakuwa na uwezo wa kuhudumia waumini 1,232 kwa wakati mmoja.
Kardinali Pengo alisema ili wanadamu waishi kwa furaha, upendo na amani wanapaswa kupewa ujumbe wa neno la Mungu wakiwa kwenye mazingira bora, hivyo ni vyema jitihada za dhati zikafanyika kujenga makanisa zaidi.
“Nakushukuru Padri Beno (Kikudo) wa kanisa hili ambaye uliona ni vyema utumie siku ya maadhimisho ya miaka yako 50 ya kuzaliwa kufanya harambee hii kukusanya fedha za kukamilisha ujenzi wa kanisa, kuliko wengine ambao wamekuwa wakitumia sherehe hizo maeneo ya fukwe za bahari,” alisema. Alisema makusudi ya Mungu siyo kufuja mali ambazo anawajalia wanadamu, bali kutumia mapato yao kwenye mambo ya maendeleo.
Padri Kikudo aliwashukuru waumini kwa kuonyesha juhudi na moyo wa michango ya hali na mali tangu ujenzi wa kanisa hilo ulipoanza.
Alisema ujenzi wa kanisa hilo umefanyika kwa njia tofauti, ikiwa ni pamoja na waumini kuuza kuku na kujitolea kwa nguvukazi kulingana na vipawa na ujuzi walionao ili kufanikisha ujenzi huo.

Serikali yaombwa kuisadia Dangote

Mtwara. Serikali imetakiwa kukaa na mmiliki wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote, Aliko Dangote kutafuta ufumbuzi wa changamoto zinazokikabili kiwanda hicho kwa kuwa anaweza kuwa balozi wa wawekezaji nchini.
Katibu wa CCM Mkoa wa Mtwara, Shaibu Akwilombe  ametoa ombi hilo jana akisema Dangote ana jina kubwa, iwapo kungekuwa na mazingira mazuri ya uwekezaji angesaidia kuwavutia wengine.
 “Siku za hivi karibuni kumekuwa na taarifa kadhaa katika vyombo mbalimbali vya habari zinazohusiana na kiwanda cha Dangote, kutozalisha kwa kile kinachoelezwa ni kutokana na hitilafu za ufundi.  Kwa kuwa tatizo la ufundi limejitokeza kipindi ambacho tayari kulikuwa na malalamiko kutoka kwa wamiliki juu ya gharama za uzalishaji, inasababisha kuwapo mkanganyiko kujua kiini cha tatizo,” amesema Akwilombe.

Sunday, November 20

Urefu wazuia matibabu yake MOI

KIJANA Baraka Elias (35), mwenye urefu wa futi 7.4 ambaye ameshindwa kufanyiwa matibabu ya kubadilishwa nyonga katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu (MOI), amevunja ukimya na kueleza changamoto zilizosababisha ashindwe kupatiwa matibabu kutokana na urefu wake usiokuwa wa kawaida.
Akizungumza na MTANZANIA nyumbani kwa wazazi wake Mtaa wa Bwela, Pugu Majohe, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam jana, Elias alisema madaktari wameshindwa kumtibu kwa sababu mashine za MOI hazilingani na urefu wake.
Alisema anatarajia kupewa rufaa ili akatibiwe nje ya nchi.
“Madaktari wamenieleza bado wanafanya mazungumzo na wenzao wanaoshirikiana nao kutoka nje ya nchi ili wajue ni nchi gani itakuwa tayari kunichukua kufanikisha matibabu yangu.
“Sielewi matibabu yatagharimu kiasi gani cha fedha, nitatumia muda gani na vifaa gani hadi kukamilika,” alisema.
Elias alisema alifikishwa katika taasisi hiyo, Aprili mwaka huu baada ya kupewa rufaa kutoka Hospitali ya Peramiho mkoani Ruvuma.
Akizungumzia chanzo cha tatizo lake, Elias alisema alipata hitilafu ya nyonga baada ya kuanguka kwenye ngazi za nyumbani kwake mkoani Ruvuma na tangu wakati huo hakuweza kuendelea kufanya shughuli zake za kiuchumi.
Alisema baada ya muda kidogo alipelekwa Hospitali ya Peramiho ambako alifanyiwa kipimo cha X-ray na kuonekana nyonga yake ilikuwa imevunjika.

ALIVYOPOKEA RIPOTI YA MOI
Elias ambaye muda wote anaonekana kuwa mchangamfu, alisema taarifa aliyopatiwa na madaktari wa MOI kwamba anapaswa kupewa rufaa kwenda kutibiwa nje ya nchi aliipokea kwa mtazamo chanya.
“Niliona ni hali ya kawaida kwa sababu kupewa rufaa ni mfumo wa kawaida wa kimatibabu, madaktari wana utendaji wao… wanapoona wameshindwa wanakupeleka kwingine ambako unaweza kupata msaada zaidi na ndiyo maana nilitolewa Peramiho kuja MOI.

HAWEZI KUPANDA DALADALA
Alisema kwa sasa hawezi kupanda daladala kutokana na urefu wake kwani kukaa kwenye kiti huwa ni changamoto kubwa kwake kwa sababu siti zake zimetengenezwa kwa kujibana.
“Zamani nilipokuwa mzima nilikuwa napanda daladala, nilikuwa napata shida kukaa, jinsi zilivyotengenezwa hazina nafasi ya kutosha tofauti na gari za wenzetu (wazungu) zimetengenezwa kwa kuachanishwa nafasi mtu yeyote anaweza kukaa bila usumbufu,” alisema.

UREFU KWENYE DNA
Elias alisema wazazi wake wamemweleza kuwa urefu alionao ni wa kurithi kutoka kwenye kizazi chao, kwani hata mababu zake wapo ambao walikuwa warefu.
“Wazee hao wanatoka katika pande zote mbili, yaani kwa baba na kwa mama, sijui watu wananichukuliaje jinsi nilivyo, binafsi najiona kawaida na wengine kwa sababu hata hapa nyumbani hakuna aliye mrefu zaidi yangu,” alisema.

CHANGAMOTO
Alisema changamoto kubwa anayokabiliana nayo hivi sasa ni usafiri wa kumtoa nyumbani hadi Muhimbili kupata matibabu.
“Huwa tunalazimika ama kukodi gari kutoka nyumbani hadi hospitalini au tunaazima la mtu tunaweka mafuta,” alisema.

KUPANDA NDEGE
Elias alisema iwapo rufaa itapatikana hahofii kama atashindwa kuingia ndani ya ndege kwa safari ya matibabu nje ya nchi.
“Kama nilivyoeleza awali, wazungu huwa wanafikiri mbali, wanafanya vitu vikubwa. Huko kwenye nchi zao wapo warefu zaidi yangu na wanapanda ndege kama watu wengine.
“Hata gari zao wanazotengeneza siku hizi ni za tofauti, hivi karibuni tu Japan ilitoa hizi gari ndogo ambazo zina uwezo wa kusogeza kiti nyuma na ukakaa vizuri, najua nitaweza kuingia ndani ya ndege,” alisema.

AOMBA MSAADA
Elias alisema ingawa kanisa analoabudu linashirikiana naye bega kwa bega, msaada mkubwa kwake umebaki kwa familia yake.
Kutokana na hali hiyo, anaomba msaada kutoka kwa mtu, mashirika au taasisi yoyote itakayoguswa na mkasa wake.
“Siwezi kufanya kazi, kila siku nahitaji fedha za matumizi, nahitaji msaada, naamini wapo watakaoguswa, nipo tayari kwa msaada wowote kwa sababu nina changamoto nyingi, naumwa sijui lini nitapata matibabu, nategemea majibu ya madaktari,” alisema.

Wasira agoma kustaafu siasa

MWANASIASA mkongwe, Steven Wasira, amesema hana mpango wa kustaafu siasa baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza kuhalalisha ushindi wa Mbunge  wa Bunda Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Ester Bulaya.
Wasira ambaye kwa sasa ana umri wa miaka 71, aliyasema hayo jana wakati alipozungumza na MTANZANIA Jumapili lililotaka kufahamu msimamo wake kuhusu hukumu hiyo iliyotolewa juzi na mustakabali wake kisiasa.
Baadhi ya wafuatiliaji wa siasa nchini, wamekuwa na mtazamo kuwa huweda hukumu hiyo ingemfanya Wasira astaafu siasa kutokana na umri wake, lakini pia kulishikilia jimbo hilo kwa awamu tofauti tangu alipojiengua Chama cha NCCR-Mageuzi na kushinda ubunge mwaka 2005 kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
“Nistaafu siasa kwa hukumu? Kukosa ubunge haihusiani kabisa na kustaafu, na kwanini hilo swali hamkuniuliza tangu mwaka jana baada ya uchaguzi?” alihoji Wasira wakati akizungumza na gazeti hili jana.
Akijibu swali la mwandishi ambaye alitaka kujua iwapo atakata rufaa, Wasira alimtaja wakili wake Constantino Mtalemwa kuwa ndiye anayepaswa kulizungumzia hilo.
Kuhusu kutokuwapo wakati wa hukumu hiyo juzi, Wasira alisema yeye alikwenda mahakamani hapo kama shahidi na kwamba wapigakura wake ndio walifungua kesi hiyo.
Hata hivyo, katika hatua nyingine, Wasira alishindwa kumzungumzia mshindi wa hukumu hiyo, Bulaya na kuishia kusema kuwa ni mwanasiasa aliyekuwapo tangu Bunge lililopita.
Wasira alihamia upinzani kupitia chama cha NCCR-Mageuzi baada ya kutoridhishwa na ushindi wa Jaji Joseph Warioba (Waziri Mkuu na Makamu wa Rais mstaafu) katika jimbo la Bunda na baadaye mwaka 1999 alirudi tena CCM.
Mwanasiasa huyo mwaka jana alikuwa miongoni mwa makada 42 wa CCM waliojitokeza kuomba ridhaa ya kuteuliwa kupeperusha bendera ya urais, lakini hata hivyo aliikosa.
Wafuatiliaji wa siasa hapa nchini wanamtambua Wasira kama mwanasiasa mkongwe aliyeanza kuwa mbunge tangu akiwa na miaka 25 baada ya kushinda kiti hicho katika Jimbo la Mwibara mwaka 1970.
Katika nafasi za utumishi wa umma, Wasira alianza kuwa Naibu Waziri wa Kilimo chini ya utawala wa Rais wa Kwanza wa Tanzania, Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere.
Tangu enzi hizo za Mwalimu Nyerere, Wasira aliendelea kushika nafasi mbalimbali za uongozi serikalini, huku akiwa mbunge katika tawala zilizofuata hadi utawala huu wa Rais Dk. John Magufuli alipoanguka ubunge.
Itakumbukwa katika kesi iliyotolewa hukumu juzi, kwa mara ya kwanza ilifunguliwa na wapigakura wanne wa Wasira baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka jana wakipinga matokeo yaliyompa ushindi Bulaya.
Wapigakura hao ni Magambo Masatu, Matwiga Matwiga, Janes Ezekiel na Asetic Malagila.
Maombi hayo ya kutaka kesi isikilizwe, yaliwasilishwa kwa mara ya kwanza kwa Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Sumbawanga, Mohamed Gwae, ambaye Januari 25, mwaka huu aliitupilia mbali kwa hoja kuwa wapigakura hawana haki ya kupinga matokeo hayo.
Baada ya kukataliwa maombi hayo, walikata rufaa kwenda kwa Jaji Sirilius Matupa wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, Kitengo cha Biashara, ambaye hata hivyo aliwarudisha walalamikaji hao kurekebisha baadhi ya vifungu, kisha ilipelekwa kwa Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, Rosemary Ebrahim ambaye aliisikiliza na kuiondoa tena baada ya kubaini kasoro katika kiapo kuwa wakili aliyesaini siye aliyekuwa ameapa.
Makosa hayo yaliondolewa na baadaye kesi hiyo kupelekwa kusikilizwa na Jaji wa Mahakama Kuu Kanda hiyo, Jackilene Dimelo, ambaye aliiruhusu iende kwa jopo la majaji watatu ambao waliipiga tarehe ili iweze kusikilizwa na majaji watano ambao waliamuru irejeshwe kwa Jaji Lameck Mlacha.
Novemba 18, mwaka huu, Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza ilikohamishiwa kesi hiyo namba moja ya mwaka huu, katika Mahakama ya Mkoa wa Mara mjini Musoma, chini ya Jaji Noel Chocha, iliitupilia mbali na kumthibitisha Bulaya kuwa ni mbunge halali wa jimbo hilo.
Wakati huo huo, walalamikaji wa shauri hilo wamesema hawajaridhika na uamuzi huo, hivyo wanajiandaa kukata rufaa katika Mahakama ya Rufaa.
Akizungumza jana na gazeti hili kwa ujumbe mfupi wa simu, mmoja wa walalamikaji, Asetic Malagila, alisema baada ya kusikiliza hukumu hiyo walikubaliana na mwanasheria wao kuwa wakate rufaa kwa kile alichokiita walishindwa kwa sababu ya uonevu.
“Tumeshindwa kwa uonevu tutatafuta haki yetu katika mahakama ya rufaa, tuko katika hatua ya kukata rufaa Court of Appeal,” unasomeka ujumbe huo wa Malagila.

Mabilioni ya fedha Kagera yaiibua Serikali


*Ni baada ya watu kuhoji ujenzi wa miundombinu
* Ofisi ya Waziri Mkuu yasisitiza msimamo uko palepale
Na VERONICA ROMWALD – DAR ES SALAAM
SIKU chache baada ya kuenea taarifa za kuyeyuka mabilioni ya fedha yaliyochangwa na wasamaria wema kwa ajili ya kusaidia waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera, Serikali imeibuka na kutoa taarifa juu ya sakata hilo.
Wiki iliyopita, Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Jenerali Salum Kijuu, aliwaambia waandishi wa habari kuwa hadi sasa Serikali imetumia Sh bilioni 1.13 kukarabati miundombinu na si kuwajengea au kukarabati nyumba wananchi ambao wanaishi kwenye mahema.
Aidha, Meja Jenerali Kijuu aliendelea kushikilia msimamo wa Serikali kuwa kila mwananchi aliyeathirika na tukio hilo, ajihudumie na kukarabati nyumba yake mwenyewe.
mkuu-wa-mkoa-mhe-kijuu-akiongoza-zoezi-la-kugawa-mahitaji-kwa-wahanga-laeo-jioniAlisema Serikali tayari imekusanya Sh bilioni 5.428 kutoka kwa watu, taasisi na mashirika mbalimbali, waliotikia wito wa kusaidia waathiria wa tetemeko hilo lililotokea Septemba 10, mwaka huu.
Kijuu alisema fedha hizo zilivunwa kupitia akaunti maalumu ya maafa iitwayo ‘Kamati Maafa Kagera’ na michango mingine kupitia mihamala ya fedha ya simu za mkononi.
Baada ya taarifa ya Kijuu kutoka, iliibua maswali na mjadala mkali, hasa katika mitandao ya kijamii, ambako wachangiaji wengi walihoji kwanini fedha hizo hazijawafikia walengwa hadi sasa, huku wakibaki kutaabika.
Kutokana na mjadala huo kushika kasi kila kukicha, jana Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera,Uratibu na  Bunge), Uledi Mussa, alilazimika kutoa ufafanuzi wa Serikali namna ambavyo imeshirikina na wadau kuchukua hatua kubwa za kuwasaidia waathirika na kwamba bado inaendelea kufanya hivyo.
Alisema hadi kufikia Novemba 13, mwaka huu, Serikali ilikuwa imepokea misaada ya vifaa, vyakula, fedha na ahadi mbalimbali zenye thamani ya Sh bilioni 15.19.
Mussa alisema pamoja na misaada hiyo, tayari Serikali imetoa matibabu bure kwa majeruhi wote 560, imeandaa na kugharamia mazishi ya watu 17 waliofariki dunia katika tetemeko hilo, huku Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alihudhuria.
“Serikali kwa kushirikiana na wadau ilitoa mkono wa pole wa Sh milioni 1.8 kwa kila familia iliyopatwa na msiba. Imeendelea kutoa misaada mbalimbali ya kibinadamu ikiwamo chakula, dawa, nguo, makazi ya muda, huduma za tiba, vifaa vya shule na huduma ya ushauri wa kisaikolojia kwa waathirika katika wilaya zote za Mkoa wa Kagera zilizopata athari,” alisema.
Alisema Serikali imeendelea kufanya tathmini ya pamoja ya mahitaji ya haraka ya athari za tetemeko hilo ili kubaini maeneo zaidi ya kuwasaidia wananchi kwa kushirikiana na ofisi ya Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa na wadau mbalimbali, wakiwamo Msalaba Mwekundu, Plan International (T), BRAC(T), World Vision, CARITAS, Save the Children, JH Piego na Benki ya Dunia.
“Tathmini za wataalamu, makadirio ya awali yanaainisha Sh bilioni 104 zinahitajika kukabiliana na kurejesha hali katika Mkoa wa Kagera. Gharama hizo zinajumuisha ujenzi wa makazi ya muda kwa waathirika wa nyumba zipatazo 16,667 zilizoharibika katika viwango tofauti, ambapo kiasi cha Sh bilioni 41.7 zinahitajika.
“Sh bilioni 1.92 kwa ajili ya kodi ya miezi sita kwa wapangaji waliokuwa wakiishi kwenye nyumba zilizoharibika, ukarabati wa shule za msingi 163 kwa gharama ya sh bilioni 12.7, sekondari 57 kwa gharama ya Sh bilioni 45.65, vituo vya afya na zahanati 32 kwa gharama ya Sh milioni 772 na majengo ya taasisi nyingine 20 kwa Sh bilioni 1.3,” alisema.
Alisema hadi kufikia Novemba 13, mwaka huu, Serikali imepokea misaada ya vifaa, vyakula, fedha na ahadi mbalimbali zenye thamani ya Sh bilioni 15.19 kutoka kwa wadau mbalimbali, washirika wa maendeleo, balozi na nchi marafiki. Tayari misaada hiyo imeshagawiwa na inaendelea kusambazwa kwa walengwa.
“Mchanganuo wa misaada hiyo iliyopelekwa ipo kama ifuatavyo: Fedha taslimu kiasi cha Sh 5,412,984,934.82 kimeshapokelewa kupitia benki. Kiasi cha Sh 17,579,427.00 kupitia mitandao ya simu, ahadi za Sh 6,703,000,000. Hivyo jumla ya ahadi na fedha taslimu hadi sasa ni Sh 12,133,564,361.82,” alisema.
Alisema Serikali pia imepokea misaada mingine yenye thamani ya Sh bilioni 2.25, ikiwamo unga tani 58.12, sukari mifuko 1,150, mchele tani 133.96, maharage tani 19,666, mahindi tani 70.1, majani ya chai tani 3, maji katoni 1,570, mafuta lita 6,022, sabuni katoni 443, shuka 495, blanketi 6,125, magodoro 1,146, mahema 367 na turubai 6,237.
Aliongeza: “Serikali imepokea pia vifaa vya ujenzi vikiwamo saruji mifuko 24,233, bati 20,933, misumari kilo 145, nondo vipande 725, kofia za bati 150 na mbao 250.
“Ifahamike baadhi ya waliotoa ahadi kama Serikali ya Uingereza, wameahidi kutekeleza ahadi zao kwa kujikita moja kwa moja katika ujenzi wa shule, baada ya Wakala wa Majengo kuainisha viwango na gharama. Aidha Serikali inaendelea kupokea michango kutoka kwa wananchi na wadau mbalimbali kwa lengo la kusaidia waathirika hawa.”

HATUA ZA KUREJESHA HALI
Mussa alisema tangu kutokea kwa maafa hayo, Serikali imeendelea kufanyia kazi masuala muhimu yaliyoainishwa katika tathmini ya tetemeko.
Alisema hadi kufikia Novemba 13, mwaka huu, licha ya kuendelea kuwapatia wananchi mahitaji muhimu kama chakula, dawa na misaada ya kujikimu katika makazi ya muda, kiasi cha Sh 969,238,326.35, mifuko ya saruji 17,423, bati 5,348 na misumari kilo 1,107 vilitumika kwa kufanya ukarabati mkubwa na mdogo wa shule za msingi na sekondari.
“Juhudi hizi ziliwezesha wanafunzi wa shule hizo waliokuwa katika hatari ya kukosa masomo kuendelea na masomo yao. Gharama hizo pia zimejumuisha ukarabati wa zahanati katika halmashauri za Mkoa wa Kagera, na kuanza kwa ujenzi wa kituo kipya cha afya (Ishozi/Kabyaile) kitakachojumuisha chumba cha upasuaji na wodi ya kinamama na watoto kwa faida ya wananchi wote wa maeneo hayo.
“Pia Serikali imegharamia urejeshwaji wa miundombinu ya barabara, maji, na umeme katika maeneo kadhaa yaliyoathiriwa na tetemeko,” alisema.
Alisema Shirika la Word Vision kwa kushirikiana na Serikali tayari limetoa mifuko ya saruji 2,300 yenye thamani ya Sh 39,000,000 kwa kaya 460 zilizobomokewa nyumba na zilizoonekana kuwa na uhitaji zaidi. Katika awamu ya kwanza kila kaya ilipata mifuko mitano ya saruji.
“Na kwa sasa utekelezaji wa awamu ya pili umeanza, inatarajiwa kugawiwa mifuko ya saruji 10,645 yenye thamani ya Sh milioni 164.9 kwa kaya 2,129. Tumeainisha pia kaya nyingine zilizoathirika zaidi zipatazo 370 za watu waliomo kwenye makundi maalumu (wazee, wajane na walemavu), ambao watapatiwa vifaa vya ujenzi (mabati 20 na mifuko mitano ya saruji kwa kila kaya) kukarabati nyumba zao,” alisema.
Aliongeza: “Serikali inapenda kusisitiza tena kwa wananchi, maafa ya tetemeko hayakupangwa wala kutokea kwa nguvu za mwanadamu bali majanga ya asili, hivyo wakati juhudi zikiendelea kusaidia zaidi pale panapowezekana, wananchi wanaendelea kuombwa kufanya jitihada zao binafsi za kurejesha makazi yao katika hali yake ya awali.
“Serikali inawapongeza wananchi wengi ambao tayari wameitikia wito wa Rais Dk. John Magufuli aliyewaasa kuanza ujenzi wa nyumba zao kwa kuwa Serikali isingeweza kumjengea nyumba kila mwathirika.
“Kwa sababu ingawa michango na misaada hii japo haijafikia lengo la Sh bilioni 104.9 zinazohitajika kurejesha hali nzima ya Kagera, itaendelea kutumika kwa uadilifu na uwazi kwa faida ya waathiria wenyewe,” alisema.
Tetemeko la ardhi lilitokea Septemba 10, mwaka huu na kusababisha vifo vya watu 17, watu 252 walijeruhiwa, nyumba 840 zilianguka na nyingine 1,264 zilipata nyufa.

JK azuiwa uwanja wa ndege

RAIS mstaafu, Jakaya Kikwete, jana amezuiwa na maofisa wa Serikali kusafiri nje ya nchi kutokana na miongoni mwa wajumbe wanne aliokuwa ameongozana nao kutokuwa na viza.
Taarifa zilizofika chumba cha habari jana jioni, zilidai kuwa Kikwete ambaye pia alikuwa ameongozana na mke wake, Salma alizuiwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, tukio hilo lilitokea saa 10:00 jioni na hivyo Kikwete pamoja na ujumbe wake huo kukwama kusafiri.
Chanzo kimoja kilichopo uwanjani hapo, kililidokeza gazeti hili kuwa Kikwete pamoja na ujumbe wake huo, walikuwa wakielekea nchini Dubai na ilikuwa wasafiri kwa ndege ya Shirika la Ndege la Emirates.
“Kikwete kama Kikwete yeye hakuwa na shida kwa sababu ana Diplomatic Passport, watu wengine ndio hawakuwa na viza.
“Kwa kawaida International flight (ndege za kimataifa) kaunta zinafungwa saa moja kabla ya ndege kuruka, na ndege waliyokuwa waondoke nayo ilikuwa inaondoka saa 10:30 jioni, viza za hao watu zilikuja saa 10:00 wakati kaunta zikiwa zimefungwa,” kilisema chanzo hicho.
Kilisema kwa kiongozi kama Kikwete, linapotokea tatizo kama hilo, wakati mwingine unaweza kupiga simu kwa watu wa Uhamiaji huko anakoelekea, lakini hilo halikuwezekana kwa sababu tayari ndege ilikuwa imeondoka.
Haijajulikana mara moja kilichosababisha kutotumiwa utaratibu wa kupiga simu kama inavyoelezwa, ikitokea kiongozi mkubwa kama Kikwete au wasaidizi wamekwama kukamilisha taratibu fulani fulani za kusafiri nje ya nchi.
Kwa mujibu wa chanzo hicho, huenda Kikwete na ujumbe wake wakasafiri leo baada ya kuwa wamekamilisha taratibu zote.
Taarifa kutoka kwa wasaidizi wa Kikwete, zilidai kuwa wakati tukio hilo linatokea uwanjani hapo, rais huyo mstaafu hakuwa amefika bali wasaidizi wake ingawa tayari mizigo ilikuwa imekwishapandishwa ndani ya ndege.
Inaelezwa kuwa baada ya safari hiyo kukwama mizigo hiyo ilishushwa.
Taarifa nyingine zilidai kuwa wakati tukio hilo likitokea, Kikwete alikuwa uwanjani hapo na kwamba  kwa kawaida mizigo isingepandishwa kama muhusika hayupo.
Akizungumza na gazeti hili, mmoja wa wasaidizi wa Kikwete, alisema wajumbe ambao hati zao ama zilikuwa na kasoro au hazijakamilika ni wasaidizi wake.
Alisema Kikwete, mke wake pamoja na wasaidizi wake, walikuwa wanaelekea Abudhabi na walikuwa wapande ndege hiyo ya Emirates Dubai na kisha kuendelea na usafiri mwingine.
Msaidizi wake huyo alisema taratibu zote zilikamilika ingawa walikiri kuwa walikuwa wamechelewa.
MTANZANIA Jumapili lilimtafuta ndugu wa karibu na Kikwete ambaye alithibitisha kuwa alikuwa anasafiri, lakini hakuwa na habari za kukwama kwake.
Zipo taarifa ambazo hazijathibitishwa zinazodai kuwa imekuwa ni kawaida kwa wasaidizi wa Kikwete kusafiri nje ya nchi bila viza, na kwamba tukio la safari ya jana kukwama lisingetokea kama utaratibu huo haungekuwapo.
MTANZANIA Jumapili lilipomtafuta Msemaji wa JNIA, Nuru Nyoni azungumzie sababu za Kikwete na ujumbe wake kukwama, alisema suala hilo lipo chini ya Uhamiaji.
“Siwezi kuzungumzia mimi, hili suala lipo chini ya Uhamiaji, labda uwapigie Uhamiaji, pia hata uthibitisho siwezi kutoa maana leo ni weekend sijafika ofisini,” alisema Nuru.
Alipotafutwa Ofisa Uhusiano wa Idara ya Uhamiaji, Abasi Ilovia, kupitia simu yake ya kiganjani, aliomba apigiwe baada ya dakika kumi ili aweze kuwasiliana na watu waliopo JNIA kwa taarifa zaidi.
Ilovia alipopigiwa tena baada ya muda huo, alisema anasubiri majibu kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Uhamiaji cha Uwanja wa Ndege.

Saturday, November 12

top footballers in the world by goal.com


GOAL 50 - POSITIONS 10-1

The Goal 50 counts down the world’s 50 best football players of 2016, featuring the likes of Cristiano Ronaldo, Lionel Messi and Zlatan Ibrahimovic. Below you can find the stars who were selected from positions 10 to 1.

Chief editors and correspondents from Goal‘s 38 editions across the globe all cast their votes. Players were judged on their level of consistency over the past year, their big-game performances, footballing legacy and the success of their team at both club and international level.

#10 ZLATAN IBRAHIMOVIC | MANCHESTER UNITED & SWEDEN

The Swede has a wonderful sense of humour and a tremendous flair for hyperbole but it is hard to dispute his claim that he is ageing like a fine wine. Last season was the most prolific of his career, with Ibra racking up 50 goals in PSG's treble-winning campaign, while he wasted little time in winning over United fans by scoring four times in his first three games for his new club.

#09 GONZALO HIGUAIN | JUVENTUS & ARGENTINA

The striker's detractors believe that he misses big chances in big games yet this is a man who hit a hat-trick on the final day of last season to break the record for goals in a single Serie A season. Furthermore, when his critics piled on the pressure after he'd piled on the pounds following his €90m summer switch from Napoli to Juventus, he responded with seven goals in his first nine outings in all competitions for the Bianconeri.

#08 ROBERT LEWANDOWSKI | BAYERN MUNICH & POLAND

Any doubts over the striker's suitability to Pep Guardiola's tactics were blown away last season, with the 28-year-old becoming the first foreign player ever to score 30 goals in one Bundesliga campaign. Though a marked man at Euro 2016 - he suffered more fouls than any other player despite exiting at the quarter-final stage - he still managed a goal in his country's shootout loss to Portugal. 

#07 RIYAD MAHREZ | LEICESTER CITY & ALGERIA

A player signed from Le Havre for €500,000 in 2014 was described as "priceless" by Foxes boss Claudio Ranieri last December and it's easy to understand why. With 17 Premier League goals and 10 assists, Mahrez was not only a worthy recipient of the 2015-16 PFA Players' Player of the Year award in April but also a most deserving Premier League title winner just a few days later. The highest ranked midfielder in the Goal 50.


#06 NEYMAR | BARCELONA & BRAZIL

One leg of arguably the greatest ever front three, Neymar netted the winner in the Blaugrana's double-clinching victory over Sevilla in the Copa del Rey final in May. After being forced to miss the Copa America by his club, the 24-year-old then led his country to victory in the one international tournament that had eluded them by claiming Olympic gold in Rio in August. What’s more, he scored the winning penalty in the final shootout success over Germany.

#05 GARETH BALE | REAL MADRID & WALES

The winger has his injury issues but when fully fit, he rarely fails to step up to the mark for both club and country. One of Madrid's best players in the Champions League final win over Atletico, the 27-year-old Cardiff native then carried Wales through the group stage of Euro 2016 with three goals in three games, laying the foundation for the Dragons' surprise run to the semi-finals.

#04 LIONEL MESSI | BARCELONA & ARGENTINA

It says something about the staggering standards of excellence that the diminutive No.10 has set for himself that a year in which he inspired his club side to a domestic double and his country to a third final in three years can be considered slightly below par. Indeed, at regular intervals over the past 12 months, Messi reminded everyone just why he is not competing for the title of the best player in the world but the greatest of all time, with his performance in Argentina's Copa America semi-final demolition of USA a particular highlight.

#03 ANTOINE GRIEZMANN | ATLETICO MADRID & FRANCE

The finals of both the Champions League and Euro 2016 ended in heartbreak for the Frenchman but even those desperately disappointing defeats couldn’t overshadow the attacker's illuminating displays for club and country this year. It was Griezmann's goals that knocked both Barcelona and Bayern Munich out of Europe, while his fantastic form for France – including a match-winning double versus Germany in the semis - saw him claim both the Golden Boot and the Golden Ball at Euro 2016.


#02 LUIS SUAREZ | BARCELONA & URUGUAY

After being forced to share the Golden Shoe with Cristiano Ronaldo last year, the former Liverpool ace made no mistake this time around, blowing the Portuguese superstar and several other illustrious rivals out of the water with 40 Liga goals in just 35 games. Suarez's brilliance was only further emphasised by the fact that he also created 16 goals - a tally only matched by Messi - to become the first player to top both the goalscoring and assists charts in Liga history.

#01 CRISTIANO RONALDO | REAL MADRID & PORTUGAL

Reports of the 31-year-old's decline proved greatly exaggerated, with the Madeira native enjoying the most successful season of his career - at least trophy-wise. Ronaldo struck a whopping 51 club goals in all competitions last term – and top-scored once again with 16 strikes as Real won the Champions League in May. Just over six weeks later, he cemented his status as an all-time great by claiming the first major title of his international career thanks to Portugal's stunning triumph at Euro 2016. Congratulations to Cristiano Ronaldo – the winner of the 2016 Goal 50!