Sunday, January 13

Zitto aingia matatani

 MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe ameingia matatani, baada ya kutakiwa kukanusha tuhuma alizozitoa bungeni katika Mkutano wa Tisa wa Bunge, kwamba mfanyabiashara wa kigeni, Moto Mabanga, alipewa vitalu vya mafuta kinyume na taratibu.

Mfanyabiashara huyo amesema kuwa iwapo Zitto atashindwa kukanusha tuhuma hizo, atafikishwa mahakamani.

Barua iliyoandikwa kwenda kwa mbunge huyo iliyosainiwa na Mwanasheria wa Mabanga, Lawley Shein wa Kampuni ya Uwakili ya Lawley Shein Attorneys, ambayo Mwananchi Jumapili limeiona, inaeleza kuwa hoja binafsi aliyoitoa Zitto, haikuwa na ukweli wowote.

Barua hiyo ya tarehe 28 Novemba, 2012 ilisema kuwa hoja hiyo ya Zitto ni ya uongo, imemkashifu mteja wao na kumshushia hadhi yake binafsi na biashara zake.

“Katika kuthibitisha kuwa tuhuma zako siyo za kweli katika hoja uliyotoa, umemtaja mteja wetu kama raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Mteja wetu ni raia wa Afrika Kusini, lakini, umeamua kumtaja kama raia wa Kongo bila kuangalia ukweli,” alisema Shein.

Katika barua hiyo, Shein pia amesema kuwa Zitto amemtuhumu mteja wake Mabanga kuwa aliwahonga baadhi ya vigogo serikalini na kuwapa rushwa wanasiasa katika mchakato wa kufanikisha upatikanaji wa vitalu hivyo.

“Tuhuma hizo siyo za kweli, mteja wetu alifuata taratibu zote kwa uwazi na mamlaka husika nchini na hakuwahi kutoa rushwa kwa mtu yeyote,” alisema mwanasheria huyo.

“Tuhuma hizi ni za uongo, zimemharibia jina mteja wetu na kumsababishia madhara. Kama hutazifuta kauli hizo, uongo huo utamsababishia mteja wetu madhara makubwa zaidi na tutalazimika kudai fidia,” Shein alionya kupitia barua hiyo.

Shein aliongeza kuwa pamoja na Zitto kuongea hoja hiyo akiwa bungeni hivyo kuwa na kinga ya kibunge, lakini kwa mazingira aliyotolea hoja hiyo alitumia vibaya kinga ya kibunge, anayopata mbunge yeyote anapotoa hoja akiwa bungeni.

Kupitia barua hiyo, Shein alimtaka Zitto kufuta kauli yake dhidi ya mteja wao na kwamba mteja wao ana haki zote za kushtaki dhidi ya hoja hiyo.

Zitto azungumza
Alipotakiwa kuzungumzia hoja hiyo na hatua atakazochukua, Zitto alisema kuwa amemwandikia barua Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah, kumjulisha hatua hiyo ya kutaka kushtakiwa.
“Nimemwandikia Katibu wa Bunge kumjulisha kwamba nimeletewa kusudio la kushtakiwa, maana hili ni suala la Kinga ya Bunge,” alisema Zitto na kuongeza:

“Mbunge ana kinga kwa masuala aliyozungumza ndani ya Bunge kwa mujibu wa Ibara ya 100 ya Katiba. Kwa hiyo Katibu (Dk Kashililah), atawajibu hao wanasheria.”

Ibara hiyo ya 100 (2) inaeleza kuwa; Bila ya kuathiri Katiba au masharti ya sheria nyingine yoyote inayohusika, mbunge yeyote hatashtakiwa au kufunguliwa shauri la madai mahakamani kutokana na jambo alilosema au kulifanya ndani ya Bunge, au alilolileta bungeni kwa njia ya maombi, muswada, hoja au vinginevyo.

Naibu Spika
Kwa upande wake Naibu Spika, Job Ndugai alisema kuwa hana taarifa za kusudio hilo la kutaka kushtakiwa kwa Zi tto, lakini akasema kwamba mbunge ana kinga ya Bunge pindi akitoa hoja au wazo lolote, akiwa ndani ya Bunge.

Ndugai alisema kuwa kutokana na mabadiliko madogo ya sheria yaliyofanyika, mwananchi anaweza kuandika barua kwa Spika wa Bunge kutokana na tuhuma alizotoa mbunge dhidi yake bungeni.
“Mtu anaweza kuandika barua kwa Spika na Spika ataona hatua zaidi za kuchukua za kibunge,” alisema Ndugai.

Uswisi imeiumbua serikali, sasa fedha zirejeshwe

   
NILIMSIKILIZA kwa makini Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Frederick Werema, alipokuwa akijibu bungeni hoja ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe aliyoiwasilisha bungeni Novemba mwaka jana kuhusu mabilioni ya fedha yaliyotoroshewa katika mabenki mbalimbali nchini Uswisi.

Werema alisema kuwa Serikali imeanza kuzifanyia uchunguzi tuhuma hizo na kwamba Serikali haijalala bali inaendelea na uchunguzi.

Alisema vyombo vya usalama ikiwamo Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (Takukuru), wanalifanyia kazi suala hilo. Akatoa wito kwa Zitto na wananchi wengine kama wana ushahidi zaidi wauwasilishe katika vyombo hivyo ili fedha hizo ziweze kurejeshwa.

Wakati akiwasilisha hoja hizo Zitto alikwenda mbali zaidi ya kuwaelezea watu walioficha fedha hizo nje ya nchi na miaka ambayo walifanya hivyo.

Bila ya kuwataja kwa majina, Zitto aliwataja watu hao kwa nyadhifa kuwa ni watu wote walioshika nyadhifa za uwaziri mkuu katika kipindi cha 2003 hadi 2010, walioshika nyadhifa za uwaziri wa nishati na madini katika kipindi hicho na waliokuwa makatibu wakuu Wizara ya Nishati na Madini.

Wengine ni mawaziri na makatibu wakuu wa Wizara ya Ulinzi, wakuu wa majeshi, wanasheria wa Serikali, makamishna wa nishati, walioshika wadhifa wa Ukurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Uenyekiti na Ujumbe wa Bodi wa TPDC katika kipindi cha mwaka 2003 hadi 2010.

Pia Zitto alitaka Serikali kuwasiliana na Benki ya Dunia kupitia kitengo cha ‘Assets Recovery Unit’ ili mabilioni ya fedha na mali ambazo zimetoroshwa nje ya nchi kwenda Uswisi, Dubai, Mauritus na maeneo mengine ziweze kurejeshwa.

Hoja hiyo ya Zitto iliungwa mkono na Wabunge mbalimbali wakiwamo wa CCM ambao walitaka serikali kuchukua hatua za haraka kurejesha fedha hizo na wahusika wachukuliwe hatua.
Wapo wabunge ambao walikwenda mbali zaidi ya kutaka watu hao waliotorosha fedha hizo wakipatikana wanyongwe kwa sababu hao ni wasaliti wan chi yetu.

Mwisho wa mjadala bunge likaazimio kuipa serikali muda hadi bunge lijalo kutoa taarifa ya utekelezaji wa azimio hilo la kurejesha fedha hizo nyumbani.

Baada ya hapo kila mmoja tukajua kweli sasa serikali huenda ikalifanyia kazi azimio la bunge la kuzirejesha fedha hizo, kwa sababu siku zote serikali imeonyesha kuwa nzito katika kuzirejesha fedha hizo.

Kauli ya serikali ya Uswisi kuwa Serikali Tanzania haijaonyesha nia ya dhati kutaka kuchunguza na kupata mabilioni ya fedha yaliyofichwa na Watanzania katika benki mbalimbali nchini humo, inashtua sana.

Balozi wa Uswisi nchini, Olivier Chave alisema Ijumaa ya wiki hii kuwa mpaka sasa hakuna jitihada zozote zilizofanywa na Serikali ya Tanzania kutaka ufumbuzi wa tuhuma hizo.

Chave alisema Uswisi iko tayari kushirikiana na Tanzania kujua uhalali wa fedha hizo na endapo zikigundulika ni fedha chafu basi tutazirejesha nchini.

Alisema Serikali yao haina tatizo, kwani wameshafanya hivyo kwa nchi za Ufilipino na Nigeria hivyo watafurahi na Tanzania kama watamaliza suala hilo.

Alisema habari zinazoandikwa kuhusu mabilioni hayo kuhifadhiwa katika Benki za Uswisi, yanaharibu picha ya nchi hiyo mbele ya mataifa mengine, hivyo angependa suala hilo kumalizwa na kwamba wao wako tayari.

Kwa hakika, kauli ya balozi huyu imeimbua serikali ambayo imekuwa ikitoa visingizio vya vingi kwamba inashindwa kuzirejesha fedha hizo kutokana na kukosa ushirikiano.

Naamini kama alivyosema Zitto na watu wengine nchini kwamba fedha hizo zinamilikiwa na vigogo ndani ya serikali au waliowahi kushika nyadhifa za juu serikalini ndiyo maana inakuwa vigumu kuchukua hatua.

Kama serikali ya Uswisi inasema iko tayari kutoa ushirikiano wa kurejeshwa kwa fedha hizo nyumbani, serikali inataka msaada gani tena zaidi ya huo?

Ni kitu cha kushangaza tunapomuona Werema na mawaziri wengine wa serikali Rais Jakaya Kikwete wakisimama kuwapaka mafuta Watanzania kwa maneno matamu kwamba wameanza uchunguzi kuhusu suala hilo, wakati hata hawajawasiliana na serikali ya Uswisi.

Kuonyesha kuwa hawana nia ya dhati hata Zitto mwenyewe hadi sasa anasema Serikali haijamfuata kutaka kutoa ushirikiano wa aina yeyote kuhusu tuhuma hizo.

Zitto alikaririwa Ijumaa ya wiki hii akisema kuwa ingawa Serikali ilitaka iachiwe tuhuma hizo ili iweze kuzifanyia kazi, lakini hadi sasa ukimya umetawala.

Sasa tunaitaka serikali kuacha kutumia visingizio ili kuwazunga Watanzania, tunahitaji fedha hizo zirejeshwe na wahusika wachukuliwe hatua.
0754 304336
juliusmagodi@yahoo.com

Palestinian Leader Yasser Arafat To Be Exhumed For Toxicology Tests


The body of the former Palestinian leader, Yasser Arafat, is to be exhumed next week amidst suspicions he may have been poisoned.

Arafat, who led the Palestine Liberation Organisation for 35 years, died eight years ago after becoming the first president of the Palestinian Authority in 1996.

He fell ill in October 2004 and in spite of treatment in a French military hospital in Paris died on 11 November 2004, aged 75.

Medical records for Arafat said he died after suffering a stroke because of blood disorders. However, a French court opened a murder inquiry after high levels of radioactive polonium were found by a Swiss Institute on his clothing, which had been provided by his widow, Suha.

Arafat is buried in Ramallah on the West Bank in a tomb that was sealed off earlier this month. Once the former PLO leader's body is removed, scientists from France, Switzerland and Russia will each take samples, former Palestinian intelligence chief Tawfik Tirawi told the BBC.

No autopsy was carried out on Arafat when he died at the request of his widow, but she has since agreed to this exhumation to enable the Palestine Authority to find the truth about her husband's death, according to reports. Many Palestinians have long suspected that he was murdered by Israel, which has rejected such claims.

The exhumation is scheduled to take place on Tuesday.

Saturday, January 12

UTATA KUHUSU MUONEKANO WA DARAJA LA MANZESE


Picha hii imekua ikisambaa kwenye mitandao ya kijamii wakidai kuwa huu ndiyo utakua muonekano wa daraja la Manzese. ....

Mdau wa tulonge amejaribu kufanya uchunguzi kugundua kuwa hii ni project ambayo ilipangwa kufanywa na wachina huko Thailand mwaka 2010.....

Mimi binafsi pia sijawahi sikia serikali ikisema kuwa huu ndiyo utakua muonekano wa daraja la Manzese na Morogoro road kwa ujumla.....

Kama kuna mdau anafahamu mengi kuhusu hili atujuze ili tusije tukawa tunadanganyana na kufarijiana.....





POLISI WATANO WATIWA MBARONI KWA UPOTEVU WA MILIONI 150 KATIKA TUKIO LA WIZI LILILOTOKEA KARIAKOO HIVI KARIBUI




Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam linashikilia askari Polisi watano kwa tuhuma za kuhusika na upotevu wa Sh milioni 150 zilizoporwa na watu wanaosadikiwa kuwa majambazi eneo la Kariakoo.

Sambamba na askari hao pia wamekamatwa watu wawili wanaodaiwa kuhusika na tukio hilo ambao ni Deogratias Kimaro (30), mkazi wa Kalakata na Kulwa Mwakabala (30) mkazi wa Kijiwesamli Ilala.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, Kamanda wa Kanda hiyo, Suleiman Kova alisema askari hao wanashikiliwa kutokana na uchunguzi wa kina uliofanywa na jopo la upelelezi likiongozwa na Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai wa Kanda hiyo, Ahmed Msangi.

Alisema baada ya tukio hilo zilipatikana taarifa kwamba fedha hizo zilipotea baada ya mtuhumiwa Augustino Kayula au Frank Mwangiba, kukamatwa akiwa na bastola aina ya Browning bila fedha zilizoporwa wakati inasemekana ndiye aliyepora fedha hizo akiwa na wenzake.

“Askari hawa tunawashikilia na tayari mashitaka ya kijeshi yameanza huku uchunguzi ukiendelea na utakapokamilika, tutapeleka jalada kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa hatua za kisheria ili kuleta uwazi na uwajibikaji ndani ya jamii yetu”.

Alisema Jeshi hilo limekuwa likionesha uwajibikaji ambapo mwaka jana pekee askari 20 walichukuliwa hatua mbalimbali za kinidhamu.

Aidha, alisema majina ya askari hao yanahifadhiwa kwa sasa, kwa ajili ya usalama na wakati ukifika yatawekwa wazi huku polisi wakiendelea na upelelezi na gwaride la utambulisho.

Alisema baada ya tukio hilo kulikuwa na taarifa zenye kutuhumu askari hao juu ya upotevu wa fedha hizo na ndipo uchunguzi ulipoendelea ili kubaini ukweli.

“Baada ya uchunguzi wa kina na ushahidi uliokusanywa, umefanya askari hao washikiliwe na kuhojiwa … pamoja na uchunguzi askari kwanza watajibu mashitaka ya kijeshi,” alisema.

Katika tukio hilo la uporaji Desemba mwaka jana, inadaiwa Kayula na wenzake wakiwa wamepanda pikipiki mtindo wa ‘mshikaki’, walivamia duka la Kampuni ya Artan Limited na kupora Sh milioni 150, zilizokuwa zikitolewa dukani Kariakoo kwenda benki, ambapo watu watatu walipoteza maisha.

Waliopoteza maisha ni pamoja na mtuhumiwa Kayula, Sadiki Juma (38) na Ahmed Issa (55) waliopigwa risasi na majambazi katika eneo la tukio.

Katika hatua nyingine, Kova alikanusha taarifa kwamba alisema ameunda tume ya kuchunguza tukio la kiongozi wa Jumuiya ya Madaktari, Dk Stephen Ulimboka badala yake akasema ameunda Jopo la Upelelezi.

MCHAKATO WA KATIBA:Mtikila aibua mapya



MAKUNDI maalumu jana yaliendelea kutoa maoni yao kwenye mchakato wa Katiba Mpya, huku DP kikipendekeza Rais aapishwe baada ya siku 90 tangu kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu.
Mbali na maoni hayo yaliyowasilishwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Mchungaji Christopher Mtikila, makundi mengine; wakulima, wafugaji, wanahabari na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) nayo yalijitokeza kutoa moyoni.
Mtikila alisema kipindi hicho cha siku 90 kitatoa fursa kwa watu wanaotaka kuwasilisha pingamizi dhidi ya ushindi wa Rais mteule kufanya hivyo, kabla ya kuapishwa.
Alisema pingamizi linaweza kufanyiwa kazi kwa kipindi hicho cha miezi mitatu ili kuhakikisha kuwa taifa linapata kiongozi halali mwenye ridhaa ya wananchi.
“Pia tunataka kinga ya Rais ikome pale anapomaliza muda wake wa uongozi, kama alifanya makosa yoyote ya jinai aweze kushtakiwa ili kujenga nidhamu ya uongozi katika ofisi ya umma. Utaratibu wa kumwondoa madarakani uimarishwe asisubiriwe hadi amalize muda wake wa uongozi.”
Alisema kuwa Katiba ya nchi inapaswa kuwa mali ya wananchi wenyewe ili watawala wasijihusishe katika kuwaundia wananchi Katiba kama ilivyo kwa mchakato unaoendelea sasa wa kupata Katiba Mpya.
“Kumekuwa na hoja ya kuwapo kwa Serikali ya Tanganyika, hilo ni jambo muhimu na watu kutoka Tanganyika ni lazima wawe na Serikali yao ndani ya mipaka ya ardhi yao kupitia Katiba Mpya,” alisisitiza Mchungaji Mtikila.
Aliongeza kuwa nafasi za wabunge wa viti maalumu bungeni ziondolewe ili viti hivyo vishindaniwe kidemokrasia. Alisema wanawake wanatakiwa waelimishwe na kupikwa ili wahimili ushindani katika medani za kisiasa. Alisema kuwa taifa linahitaji viongozi bora na siyo kustarehesha jinsia.
Jukwaa la Wahariri
Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) limependekeza Katiba ijayo kutambua uhuru wa vyombo vya habari, haki ya kupata habari na uhuru wa kutoa mawazo.
“Kwa Katiba hii na sheria nyingine yoyote isiyoendana na Katiba hii, milele haitaruhusiwa kudhibiti habari nchini Tanzania,” ilieleza taarifa hiyo.
TEF ilisema kuwa haitakiwi kuwe na vikwazo katika kuanzisha magazeti au vyombo vya habari binafsi, kwamba wahariri na wachapishaji wa magazeti na vyombo vingine vya habari hawatakiwi kudhibitiwa au kuingiliwa na Serikali.
“Chombo chochote cha habari chenye wajibu wa kusambaza taarifa kwa jamii ambacho kinachapisha taarifa kuhusu, au dhidi ya mtu yeyote kinawajibika kutoa fursa ya kuchapisha mawazo ya upande wa pili, ikiwa yapo, kutoka kwa mtu ambaye taarifa au chapisho linamhusu,” ilieleza taarifa hiyo.
Vilevile, wamependekeza kuwe na sheria ya Bunge ya kuanzisha Baraza la Habari la Taifa, ndani ya miezi sita tangu siku ya kuanza kutumika kwa Katiba Mpya, baraza ambalo litakuwa na wajumbe 15 kutoka katika taaluma mbalimbali.
“Wajibu wa Baraza la Habari la Taifa itakuwa ni kusimamia vyombo vya habari, kuweka viwango vya kitaaluma kwa vyombo vya habari, kufuatilia utekelezaji wa viwango vilivyowekwa, kukuza taaluma na weledi katika vyombo vya habari,” ilisema taarifa hiyo na kuongeza;
“Kusikiliza mashauri au malalamiko dhidi ya vyombo vya habari, gharama za uendeshaji wa baraza. Kwa mujibu wa Katiba hii, Baraza la Habari la Taifa ndicho kitakuwa chombo cha mwisho katika kusimamia tasnia ya habari nchini.”
Katika suala la haki ya kupata habari, TEF imesema kila mwananchi ana haki ya kupata taarifa zozote hata zile zilizopo mikononi mwa Serikali.
Katika suala la uhuru wa kutoa mawazo Jukwaa hilo limeeleza kwamba kila mtu ana uhuru wa mawazo unaohusisha uhuru wa kutafuta, kupokea au kutoa taarifa au mawazo.
Baraza hilo limesema kuwa uhuru huo hautahusisha propaganda kwa ajili ya vita, uchochezi wa kuanzisha vurugu, hotuba za chuki, utetezi wa chuki, ukabila, ubaguzi kwa watu wengine au kuchochea mapambano.
Mtandao wa Jinsia
Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) umetaka Katiba Mpya iwe na dira ya kitaifa inayosisitiza ustawi wa wananchi katika kujenga mazingira ya kuwezesha mihimili mitatu kufanya kazi zake.
Mwenyekiti wa TGNP, Mary Rusimbi alisema kuwa moja ya mambo muhimu ambayo Katiba kwa kupitia itikadi hiyo inapaswa kuyasimamia na kuyastawisha ni haki za wanawake.
“Mchango wa mwanamke ni lazima utambulike kikatiba. Wanawake wana mchango mkubwa katika suala zima la malezi na uzalishaji mali wa aina mbalimbali, hivyo rasilimali za nchi pamoja na bajeti ya nchi zinapaswa kuwanufaisha wanawake kama ilivyo kwa wanaume,” alisema Rusimbi.
Profesa Ruth Meena alisema ni wajibu wa Serikali kuhakikisha mwanamke hafi kwa matatizo ya uzazi kwa kuboresha huduma ya uzazi katika hospitali zote nchini.
“Pia tunataka kuwapo na uwajibikaji wa viongozi. Viongozi ambao hawatimizi wajibu wao wanapaswa kujiuzulu badala ya kusubiri hadi wamalize muda wao wa uongozi, uwe wa miaka mitano au zaidi. Katiba ya sasa haiwapi wananchi mamlaka ya kuwawajibisha viongozi wazembe,” alisema Prof Meena.
Kuhusu Viti Maalumu, Profesa Meena alisema vinapaswa kuboreshwa ili hata wanawake ambao hawana chama cha siasa waweze kuwa na fursa ya kuteuliwa au kuchaguliwa kushika nafasi za uongozi.
Alisema kuwa kwa mfumo wa sasa ni wanawake walio kwenye vyama tu ndiyo wenye haki ya kupata nafasi za viti maalumu.
Wakulima
Wakulima nchini wametaka Katiba Mpya iweke uwiano sawa katika ugawaji wa ardhi kati ya wakulima na wafugaji ili kuondoa migogoro ya mara kwa mara.
Mwenyekiti wa Chama cha Wakulima Taifa (Taso), Engelbert Moyo alisema hatua hiyo itasaidia kuondoa migogoro ya wakulima na wafugaji na kuimarisha uchumi wa nchi.
“Tunapozungumzia wakulima hata ufugaji unaingia hapo ndiyo maana tukaona kuna haja ya kupendekeza kuwe na maeneo maalumu ya kufanyia shughuli hizo. Katiba iwe chanzo cha kuondoa migogoro hiyo kwa kuweka uwiano sawa katika ugawaji ardhi,” alisema na kuongeza;
“Kama Katiba Mpya itasema hivyo kwamba kutakuwa na ugawaji sawa wa ardhi kwa wakulima na wafugaji itasaidia kuondoa migogoro ambayo inaibuka mara kwa mara kati ya wakulima na wafugaji kitu ambacho hakileti picha nzuri kwa taifa letu.”
Alisema zaidi ya asilimia 80 ya uchumi wa taifa unategemea kilimo, lakini bado maisha ya wakulima yapo chini kitu ambacho ni vyema Katiba Mpya ikaliona.
Wafugaji
Umoja wa Wafugaji, umependekeza Katiba Mpya ijayo ianzishe sheria mpya ya ardhi kwa jamii pamoja na kutambua na kulinda mila na tamaduni za jamii mbalimbali nchini.
“Katiba itambue miliki ya pamoja ya ardhi kwa wafugaji inayoratibiwa na taasisi za jadi kwa mujibu wa sheria za mila za jamii mbalimbali,” alisema William Olenasha.
Alisema kitendo cha hakimiliki ya ardhi kuwa mikononi mwa Rais ni kuwanyima haki wananchi hususan wafugaji.
Rehema Mkalata, mfugaji kutoka Morogoro alisema kwa muda mrefu jamii ya wafugaji imeonekana kuwa ni jamii ya watu duni ndiyo maana hata matatizo yao hayapewi kipaumbele.
Alisema kuwa ni matarajio yake kwamba Katiba Mpya itawatambua jamii ya wafugaji kuwa na thamani sawa na watu wengine.
Pia alisema kuwa Katiba Mpya inatakiwa kuzitambua dawa asilia kuwa zinafaa kwa ajili ya matumizi ya binadamu.

Imeandikwa na Fidelis Butahe, Aidan Mhando, Ibrahim Yamola na Matern Kayela.

Thursday, January 10

Tucta yataka haki ya migomo,maandamano katika katiba

SHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta), limependekeza kwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, migomo na maandamano viwe haki ya msingi ya raia.
Wakati Tucta likitoa pendekezo hilo, Chama cha UPDP kimeungana na CCM kutaka mgombea binafsi aruhusiwe, huku NCCR Mageuzi kikiungana na Chadema kutaka umri wa urais ushushwe na apunguziwe madaraka.
Tucta, mbali na kutaka maandamano na migomo viruhusiwe, limependekeza hayo yafanyike kisheria baada ya kufutwa sheria kandamizi zinazowabana wafanyakazi wanaodai haki na masilahi yao.
Katibu Mkuu wa Tucta, Nicholas Mgaya alisema jana baada ya kuwasilisha maoni ya shirikisho hilo kuwa Katiba Mpya lazima iwe mkombozi wa wafanyakazi.
Alisema wanataka Katiba itamke kwamba kila mfanyakazi atakuwa na haki ya kugoma na kufanya maandamano wakati wanapoona haki zao hazizingatiwi.
“Sheria zilizopo zinazoruhusu maandamano na migomo ni kandamizi. Tunataka Katiba Mpya izifute na ziwepo sheria ambazo si kandamaizi ili kuwapa nafasi wafanyakazi kudai haki zao kwa maandamano bila vikwazo.”
Mgaya alisema Katiba Mpya iwe na kifungu kitakachoeleza uhusiano kazini ili kuhakikisha wafanyakazi wananufaika na kazi wanazofanya.
“Tunataka Katiba Mpya itamke kila mfanyakazi atakuwa na haki ya kushiriki na kushirikishwa kupitia vyombo mbalimbali vya mashauriano na vinavyohusika katika uamuzi wa kazi. Hiyo itakuwa njia sahihi ya kutoa nafasi kwa wafanyakazi kueleza mambo ambayo wanaona hawanufaiki nayo katika sehemu zao za kazi,” alisema.
Pia alisema: “Tunataka Katiba Mpya itamke kwamba ndani ya Bunge kutakuwa na uwakilishi wa wafanyakazi ili kutatua matatizo ya wafanyakazi.”
UPDP na mgombea binafsi
Mkurungezi wa Sheria na Katiba wa UPDP, Juma Nassoro alisema pamoja na mambo mengine, wamependekeza mgombea binafsi aruhusiwe katika nafasi zote za uongozi isipokuwa urais.
Alisema mfumo wa sasa unaolazimisha mgombea kutokana na chama cha siasa ni kuwanyima wananchi wasio na vyama kushiriki katika uongozi wa nchi kwa kutumia haki yao ya kuchagua na kuchaguliwa.
Alisema mantiki ya kutaka mgombea wa urais atokane na vyama vya siasa ni kutoa nafasi kwa wananchi kufanya tathmini za sera za vyama husika... “Yawezekana mtu akajitokeza kuwa mgombea urais na akawa na sera inayopingana na Katiba na maadili ya nchi. Ili kuepuka hilo Katiba Mpya isiruhusu mgombea binafsi kwa nafasi ya urais.”
Pia alisema wamependekeza muundo wa Serikali uwe wa Serikali tatu; Tanganyika, Zanzibar na Muungano... “Katika uongozi kwenye Serikali hizo kutakuwa na marais watatu kutoka kila Serikali huku Serikali za Tanganyika na Zanzibar zikiwa na mawaziri viongozi na ya Muungano ikiwa na waziri mkuu atakayeteuliwa na Rais wa Muungano na kuthibitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano.”
NCCR na umri wa Rais
Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, James Mbatia kwa upande wake alisema wametaka Rais asirundikiwe madaraka makubwa na asiruhusiwe kuteua viongozi wa mihimili mingine ya dola.
“Umri wa mtu kupiga kura uwe miaka 18, ila tunataka mtu mwenye miaka 21 ndiye awe na uwezo wa Kikatiba kugombea ubunge na udiwani pamoja na uwakilishi Zanzibar,” alisema Mbatia na kuongeza: “Katika urais tumependekeza kuwa umri wa kugombea nafasi hiyo uwe miaka 35 badala ya 41 ya sasa.”
Pia NCCR-Mageuzi kimependekeza muundo wa Serikali tatu; Tanganyika, Zanzibar na Serikali Kuu Shirikisho yenye mamlaka ya kidola, ambayo itakuwa chini ya mkataba unaoeleweka kimataifa.
Chama hicho pia kimependekeza Katiba kukitambua Kiswahili kuwa lugha ya taifa na itumike kufundishia katika ngazi zote za elimu.
Kuhusu mgombea binafsi alisema chama hicho kimependekeza Katiba iruhusu kwa kuwa kila mwananchi anayo haki ya kuchagua na kuchaguliwa hata kama si mfuasi wa chama chochote cha siasa.
“Haki ya kuchagua na kuchaguliwa ni ya kila mtu na inalenga mtu mmojammoja na si chama cha siasa, taasisi au kikundi cha watu,” alisema Mbatia.
Kuhusu muundo wa Serikali alisema wamependekeza kwamba Baraza la Mawaziri lisiwe kubwa kama ilivyo sasa na Katiba iweke idadi ya wizara na majina yake na zisizidi 15.
Jukwaa la Katiba na jinsia
Jukwaa la Katiba Tanzania limetaka Katiba Mpya iguse maeneo yote muhimu ikiwa ni pamoja na wanawake, wazee na watu wenye ulemavu ili kuhakikisha haki zao zinatambulika kikatiba.
Pia linataka itamke raia wa nchi hii ni nani na haki anazopaswa kupewa ili kumtofautisha na wageni wanaoingia.Mwenyekiti wa Jukwaa hilo, Deus Kibamba alisema Katiba ya sasa haimtofautishi raia wa Tanzania na wa kigeni kwani haielezi ni nani na haionyeshi haki anazopaswa kupewa.
Kuhusu elimu, Kibamba alisema Katiba Mpya itamke kwamba elimu ya ngazi ya msingi iwe hadi kidato cha nne ili kuongeza uelewa wa wanafunzi na itamke pia kwamba elimu hiyo itakuwa ni haki ya msingi kwa kila raia.
Imeandikwa na Fidelis Butahe, Aidan Mhando na Daniel Mwingira

TAWALA ZA MAJIMBO NA SERIKALI ZA MITAA

1. Nchi ya Tanganyika itagawanywa katika maeneo kumi ya kikanda yatakayojulikana kama Majimbo kama ifuatavyo:

(a) Jimbo la Nyanza Magharibi ambalo litaundwa na mikoa ya sasa ya Kagera, Geita na Shinyanga;

(b) Jimbo la Nyanza Mashariki litakaloundwa na mikoa ya sasa ya Mara, Mwanza na Simiyu;

(c) Jimbo la Ziwa Tanganyika litakalojumuisha mikoa ya sasa ya Kigoma, Katavi na Rukwa;

(d) Jimbo la Kati litakaloundwa na mikoa ya sasa ya Tabora, Singida, Dodoma na Iringa;

(e) Jimbo la Kaskazini litakaloundwa na mikoa ya sasa ya Arusha, Kilimanjaro na Manyara;

(f) Jimbo la Pwani ya Kaskazini litakaloundwa na mikoa ya sasa ya Tanga, Wilaya za Bagamoyo, Chalinze, Kibaha, Kisarawe na Mkuranga katika Mkoa wa sasa wa Pwani na Wilaya za Gairo, Kilosa, Mvomero, Morogoro na Kilombero katika Mkoa wa sasa wa Morogoro;

(g) Jimbo la Mji Mkuu wa Dar es Salaam;

(h) Jimbo la Pwani ya Kusini litakaloundwa na mikoa ya sasa Lindi, Mtwara na Wilaya za Rufiji na Mafia katika Mkoa wa sasa wa Pwani, na Wilaya ya Ulanga katika Mkoa wa sasa wa Morogoro;

(i) Jimbo la Nyanda za Juu Kusini litakaloundwa na mikoa ya sasa ya Mbeya, Njombe na Ruvuma;

2. Majimbo yataongozwa na Gavana atakayechaguliwa moja kwa moja na wananchi katika Jimbo husika.

3. Miji, manispaa na jiji ndani ya majimbo itaongozwa na Meya atakayechaguliwa moja kwa moja na Wananchi katika Mji husika;